Wednesday, July 13, 2011

Rostam Aziz: Hotuba ya kujivua Gamba

Best Blogger Tips
UTANGULIZI

WAZEE wangu, kwanza kabisa kabla ya kueleza kile ambacho kimenisukuma kuzungumza nanyi leo, napenda kuanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kutuwezesha kufikia siku hii ambayo inatukutanisha waja wake.

Wazee wangu wa Igunga, baada ya kufanya hivyo napenda pia kutumia fursa hii kuwashukuru ninyi nyote mmoja mmoja na katika umoja wenu kwa kuitikia wito wangu, kijana wenu, niliyewaomba nije nizungumze nanyi siku hii ya leo.

Nafanya hivyo nikitambua vyema kwamba, kama si nyinyi wazee wangu na wengine wengi ambao hatuko nao hapa leo kwa sababu mbalimbali, ambao mmekuwa na imani kubwa nami nisingeweza kufikia hapa nilipofika sasa.

Wazee wangu, waasisi wa taifa letu walitufundisha kutambua na kuheshimu ukweli kwamba; ‘Uongozi ni Dhamana’ dhana ambayo kila ninapokaa na kutafakari huwa inanirejesha nyuma na kukumbuka jinsi nyinyi mlivyokaa katika umoja wenu na kuniteua mimi, miongoni mwa vijana wenu wengi, kuwa mwakilishi wa Jimbo la Igunga tangu mwaka 1994.

Katika kipindi hicho chote cha utumishi wangu, nyinyi wazee wangu mmekuwa mhimili muhimu ambao umeniwezesha kutimiza wajibu wangu kwa bidii kubwa, maarifa na nidhamu ya hali ya juu nikitambua namna ambavyo mmekuwa na imani kubwa juu yangu.

Ari na moyo wa imani, ushirikiano na mshikamano ambao wazee wangu mmekuwa nao kwangu ndiyo ambao kwa kiwango kikubwa umetuwezesha kufanya kazi kwa pamoja, tukishinda changamoto mbalimbali ambazo zimekuwa zikilikabili jimbo letu katika kipindi chote ambacho mmeendelea kuniamini kuwa mbunge wenu kwa miaka 18 sasa.

Wakati nikitambua na kuheshimu ukweli kwamba katika kipindi chote cha ubunge wangu mmekuwa na imani kubwa nami na kuniunga mkono kwa dhati, naamini kwamba kwa upande wangu pia nimejitahidi kwa kadiri nilivyoweza, kutimiza matarajio ya wananchi wa Igunga.

Miongoni mwa mafanikio makubwa tuliyoyafikia kupitia ushirikiano wetu na uongozi wa pamoja ni kwamba, mwaka 1994 Igunga ilikuwa ni wilaya ya mwisho kwa maendeleo mkoani Tabora lakini leo ndiyo ya kwanza, taa za barabarani, bima ya afya kwa kila kaya, zahanati kila kijiji na shule nyingi kuliko idadi ya kata zilizomo kwenye wilaya.

Wazee wangu, nayasema haya nikitambua kwamba, kama ilivyo katika maeneo mbalimbali hapa nchini, mafanikio makubwa tuliyoyapata katika nyanja za elimu, afya, makaazi bora na kilimo katika kipindi chote ambacho mmendelea kuniamini kuwa mbunge wenu kwa miaka 18 sasa.

Wakati nikitambua na kuheshimu ukweli kwamba katika kipindi chote cha ubunge wangu mmekuwa na imani kubwa nami na kuniunga mkono kwa dhati, naamini kwamba kwa upande wangu pia nimejitahidi kwa kadiri nilivyoweza, kutimiza matarajio ya wananchi wa Igunga.

Wazee wangu, nayasema haya nikitambua kwamba, kama ilivyo katika maeneo mbalimbali hapa nchini, mafanikio makubwa tuliyoyapata katika nyanja za elimu, afya, makaazi bora na kilimo katika kipindi hicho chote hayajaweza kumaliza changamoto zote za maendeleo ambazo zinatukabili.

Wazee wangu, ingawa nimekuwa na kawaida ya kukutana na kuzungumza nanyi mara kwa mara, mmoja mmoja na wakati mwingine katika umoja wenu, wito wangu wa leo una makusudi ambayo kwa kiwango kikubwa ni tofauti na yale ambayo tumeyazoea.

Japokuwa ujumbe ninaotaka kuzungumza nanyi wazee wangu, si mgeni sana masikioni mwenu, tofauti ya leo na mikutano yetu mingine iliyopita ni uamuzi ambao nimekusudia kuufanya na ambao nitayatangaza muda mfupi ujao.

YATOKANAYO

Wazee wangu, naamini mmekuwa mkifuatilia kwa karibu hali ya siasa nchini na hususani afya ya kisiasa na matukio mengine ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho mimi ni mwanachama wake na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) nikiuwakilisha Mkoa wetu wa Tabora.

Naamini kwamba katika kufuatilia kwenu mtakuwa mmebaini kuwapo kwa matukio ambayo kwa namna moja au nyingine yamekuwa yakitokea huku yakiligusa jina langu na wakati fulani nafasi yangu kama kiongozi wa chama hicho.

Wazee wangu, nayasema hayo kwa sababu mara kwa mara ninapokutana nanyi nikiwa katika ziara zangu jimboni na wakati mwingine mnapowasiliana nami kwa njia mbalimbali mmekuwa mkionesha kuguswa kushitushwa na kutaka kujua kulikoni kuhusu mambo hayo yanayotokea.

Mimi, kama mnavyonijua nyote, ni mtu muwazi na mkweli. Siku zote nimekuwa mwepesi sana wa kuwaeleza kuhusu kila kinachotokea ili kuwaondoa hofu na wakati huo huo kuwahakikishia kwamba masuala yasiyo na msingi hususani yale yanayogusa siasa za kitaifa hayawezi kutuondoa katika mstari sahihi wa kuwahudumia wananchi wa Igunga, mkiwamo nyinyi wazee wangu ambao mmeniamini na kunituma kuwawakilisha.

Nyinyi wenyewe ni mashahidi wazuri kwamba tangu matukio yanayogusa jina langu yaanze kutokea miezi michache tu baada ya Serikali ya Awamu ya Nne inayoongozwa na Rais Jakaya Kikweti kuingia madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 2005, tumekuwa tukiyapuuza na tukaendelea kufanya kazi pamoja kwa bidii.

Bado naamini na nitaendelea kuamini kwamba tulifanya uamuzi sahihi wa kuyapuuza matukio hayo kwani mbali ya kuendelea kutimiza malengo mbalimbali yaliyokuwamo katika Ilani yetu ya Uchaguzi ya CCM, pia mliendelea kuniamini kwa nafasi yangu ya kuwa mwakilishi wenu bungeni na hata mkaniruhusu nibebe jukumu jingine kubwa la kuwa Mjumbe wa NEC ninayewakilisha mkoa wetu wa kihistoria wa Tabora.

Wazee wangu, nyinyi ndiyo watu mnaolifahamu vyema jimbo letu la Igunga na hakika nyinyi ni sehemu muhimu ya watu wanaojua historia ya kisiasa ya Mkoa wa Tabora kwa miaka mingi hata kabla ya kuja kwa mfumo wa vyama vingi hapa nchini.

Hakuna shaka hata kidogo kwamba, Tabora ni kitovu hasa cha uasisi wa siasa za vyama vingi hapa nchini. Ni wazi kwamba huwezi ukazungumzia chimbuko la vyama vya upinzani tunavyoviona hapa nchini leo pasipo kugusa mkoa huu ambao umekuwa chimbuko la wanasiasa wenye mizizi hapa na nchini kwa ujumla.

Majina ya wanasiasa wa aina ya wazee wetu, hayati Chifu Said Abdallah Fundikira na Christopher Kassanga Tumbo, Kasela Bantu (Mungu awalaze mahala pema peponi), James Mapalala, Profesa Ibrahim Lipumba na mengi mengine yana mizizi yao katika Mkoa wetu wa Tabora.

Kutokana na ukweli huo basi ni wazi kwamba, nikiwa Mbunge wa Igunga kwa vipindi vinne mfululizo na wakati huo huo nikiwa Mjumbe wa NEC kwa vipindi vitatu mfululizo, moja ya kazi ambazo nimezifanya kwa uaminifu na kwa bidii kubwa huku nikiungwa mkono na kushirikiana nanyi ni ile ya kuhakikisha kwamba mkoa huu pamoja na kuwa kitovu cha upinzani unaendelea kubakia kuwa ngome muhimu ya kisiasa ya CCM.

Si vibaya tukakumbushana kwamba, wakati nachaguliwa kuwa mjumbe wa NEC wa Mkoa mwaka 1997, jimbo moja katika mkoa wetu lilikuwa likishikiliwa na upinzani. Leo hii Tabora ni mkoa pekee miongoni mwa mikoa iliyotuzunguka ambao haukupoteza jimbo hata moja kwenda upinzani katika Uchaguzi Mkuu wa 2010. Mafanikio haya tuliyafikia kwa pamoja kutokana na ushirikiano wenu wazee wangu.

Wazee wangu, Waswahili wanasema usione vyaelea, vimeundwa. Kazi ya kuijenga CCM katika mazingira yenye mizizi hasa ya upinzani nikiwa mbunge na hususani M-NEC kutoka Mkoa wa Tabora haijapata kuwa rahisi na itaendelea kuwa ngumu na ambayo mapambano yake ni makali sana.

Wazee wangu, kwa namna ya pekee kabisa napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru nyinyi wazee wangu wa Igunga na wananchi wenzangu wote wa Mkoa wa Tabora kwa kushikamana na kuifanya kazi hiyo kwa bidii, uaminifu na mafanikio makubwa.

Matunda ya kazi hiyo kubwa yanaonekana. Pamoja na kuwa kitovu cha kihistoria cha siasa za upinzani, Tabora ndiyo mkoa pekee katika eneo hili ambao unaongozwa na wabunge wote kutoka CCM baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na hata kabla ya hapo.

Kwa sababu hiyo basi, wazee wangu, sote katika umoja wetu ukiacha mafanikio makubwa tuliyopata katika jimbo na Wilaya yetu ya Igunga, tunayo mambo mengine ya msingi ya kujivunia. Kwa moyo wa dhati na kwa unyenyekevu mkubwa napenda kuwapongeza kwa namna mlivyojitoa kukipigania na kukitetea chama chetu kwa ari na nguvu ya kipekee.

KUJIVUA GAMBA

Wazee wangu, chama chetu chini ya uongozi wa Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete kimeamua kwa kauli na nia moja kujitathmini na kufanya mabadiliko makubwa ya kimfumo yenye lengo la kukiwezesha kiendelee kubakia chama kinachoaminiwa na kuungwa mkono na Watanzania walio wengi.

Dhamira ya mwelekeo huo wa kufanya mabadiliko ya ndani ya chama chetu ilitangazwa rasmi na Mwenyekiti wetu Rais Kikwete wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa kwa CCM, mjini Dodoma.

Katika hotuba yake hiyo, Rais Kikwete aliyafananisha mabadiliko hayo na tabia ya kawaida na ya asili ya nyoka na wanyama wengine kadhaa ya ‘Kujivua Gamba’.

Wazee wangu hatua ya kwanza ya utekelezaji wa azimio hilo na mwelekeo huo sahihi ilifanyika mjini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati Kuu ya Taifa ya CCM ambacho mimi nilikuwa mjumbe wake.

Wakati wa kikao hicho, wajumbe wote wa Kamati Kuu na wale wa Sekretarieti ya chama chetu wa wakati huo kwa kauli moja tulikubaliana kujiuzulu, lengo likiwa ni kumpa Mwenyekiti wetu fursa nzuri ya kufanya mabadiliko ya uongozi yatakayotoa nafasi ya kupata mwelekeo mpya wa Chama.

Wazee wangu, tulifanya hivyo tukionesha kuunga mkono kwa asilimia 100 kile ambacho bado naendelea kuamini kuwa ni mawazo sahihi na yenye mwelekeo thabiti ya Mwenyekiti wetu ambayo kwa kiwango kikubwa yalikuwa yakiakisi matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa urais, ubunge na udiwani wa Oktoba mwaka jana.

Niliseme kwa maneno machache tu hili. Ingawa ni kweli kwamba Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana umekirudisha madarakani chama chetu kwa kukipa ushindi mkubwa katika uchaguzi wa urais, ubunge na udiwani kwa Tanzania Bara na Zanzibar, kiwango cha ushindi tulichopata kimeonyesha waziwazi dalili za wananchi kupunguza imani yao kwetu kuilinganisha na ilivyokuwa mwaka 2005.

Tungekuwa ni chama cha siasa cha ovyo iwapo tungepuuza kupungua kwa kura za rais kutoka zaidi ya asilimia 80 tulizopata mwaka 2005 hadi kufikia aislimia 61 mwaka jana kiwango ambacho ni pungufu kwa asilimia 20 ya kura katika kipindi cha miaka mitano tu, hasa ikizingatia ukweli kwamba mgombea urais ni mtu yule yule.

Tungekuwa ni chama cha siasa kilichokosa umakini iwapo tungekaa pasipo kuchukua hatua zozote za kujiimarisha baada ya matokeo ya Uchaguzi Mkuu kuonesha wazi kukua kwa upinzani ambao umeongeza idadi ya wabunge na madiwani katika pande zote mbili za muungano.

Matokeo hayo ya uchaguzi ambayo hapana shaka yamekitikisa chama chetu yalitukumbusha wasia ambao tuliachiwa na Baba wa Taifa aliyesema; ‘Bila ya CCM Madhubuti Nchi Yetu Itayumba’.

Wazee wangu, kwa sababu ya kutambua ukweli kwamba hakuna haki isiyo na wajibu kama nilivyosema awali, mimi na wenzangu tuliokuwa katika Kamati Kuu tuliona ulazima, haja na umuhimu wa kukubali kwa kauli moja wito wa kututaka tujiuzulu ikiwa ni hatua moja ya kujipanga na kukijenga upya chama chetu.

KUJIVUA GAMBA KWAPOTOSHWA

Wazee wangu, kilichotokea baada ya kujiuzulu kwetu kila aliye ndani na nje ya chama chetu amekisikia na anakifahamu. Chama kilipata safu mpya ya uongozi iliyotokana na kuundwa kwa Sekretarieti inayoongozwa na Katibu Mkuu wetu mpya, Mhe. Wilson Mukama, na Kamati Kuu iliyokuwa na sura tofauti na ile ya awali.

Wakati tukitafakari na kuangalia mustakabali mpya wa kisiasa ndani ya chama chetu, ghafla yalianza kutokea mambo ambayo chokochoko zake zilianza kusikika tangu tukiwa ndani ya Kamati Kuu ambayo ilijiuzulu baadaye.

Mara tu baada ya kumalizika kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ambacho kilichagua wajumbe wapya wa Kamati Kuu na kuidhinisha uundwaji wa Sekretarieti mpya, dhana ya kujivua gamba ambayo naamini Mwenyekiti wetu aliianzisha kwa nia njema ilianza kuenezwa ikichukua tafsiri na mwelekeo tofauti na ule wa awali.

Wajumbe wawili wa Sekretarieti, Naibu Katibu Mkuu (Tanzania Bara), Mhe. John Chiligati, na Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi, Mhe. Nape Nnauye, walisikika wakitangaza kwamba Halmashauri Kuu ya Taifa ilikuwa imefikia uamuzi wa kuwapa siku tisini wale walioitwa watuhumiwa wanaokabiliwa na tuhuma za ufisadi ndani ya chama kujitoa katika nafasi zao za uongozi vinginevyo watafukuzwa na chama.

Wazee wangu, baada ya kushinikizwa sana na vyombo vya habari wawataje kwa majina wanasiasa waliokuwa wakituhumiwa kwa ufisadi ambao ni wajumbe wa NEC na ambao wanapaswa kujiuzulu nyadhifa zao, wajumbe hao wa Sekretarieti walikwenda mbele zaidi.

Baada ya awali kuwaeleza waandishi wa habari kwamba majina ya watuhumiwa hao yalikuwa yakifahamika kutokana na kuhusishwa katika kashfa tofauti kama zile za Richmond, EPA na ununuzi wa rada, mwishoni viongozi hao walikaririwa wakiyataja majina ya wanasiasa watatu kuwa ndiyo ambao walikuwa wakilengwa na maamuzi hayo.

Wazee wangu, nilishangazwa na kushitushwa na namna porojo na fitina za kisiasa zilivyofinyangwa kwa mara nyingine tena baada ya kusikia jina la mbunge wenu ambaye ni mimi, likitajwa kuwa miongoni mwa yale matatu ya viongozi waliokuwa wakitakiwa eti kupima wenyewe na kisha kuchukua uamuzi wa kujiuzulu nafasi zao za uongozi ndani ya NEC katika kipindi cha siku tisini.

Niliseme hili mapema. Mshangao na mshituko wangu haukusababishwa na kutajwa kwa jina langu, la hasha, bali namna uamuzi halisi wa NEC na hususani dhana nzima ya ‘kujivua gamba’ ilivyoweza kupindishwa na wajanja wachache na kisha kuendeshwa kwa maslahi binafsi ya kikundi fulani cha watu.

Pili, nilishangazwa na kushitushwa na hatua ya viongozi wa chama changu ambacho nimekitumikia kwa bidii na uaminifu mkubwa kufanya juhudi kubwa hata kukivisha kikao kitukufu cha NEC uamuzi ambao msingi wa hoja zake ni vita vya kimakundi ya kisiasa yaliyo ndani ya CCM kwa upande mmoja na propaganda za vyama vya siasa vya upinzani na vyombo vya habari kwa upande mwingine.

Tatu, nilishangazwa na kushitushwa na ujasiri ambao umekuwa ukioneshwa na baadhi ya viongozi wetu wapya wa Sekretarieti wanaolitaja jina langu na kulihusisha na kile wanachokiita ufisadi ambao hata ukweli wa kimazingira na kihistoria ukiachilia mbali ushahidi wa wazi umeshathibitisha kwamba ni porojo za kisiasa zilizotokana na makovu na matarajio ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 na ule ujao wa 2015.

Wazee wangu, nyinyi ni mashahidi kwamba, mbali ya mimi mwenyewe kujitokeza kupitia vyombo vya habari na kueleza wazi kwamba sijapata kujihusisha katika vitendo vyovyote vya ukiukwaji wa maadili ya uongozi au vya rushwa, hakuna ushahidi wowote uliotolewa unaonihusisha na kashfa yoyote miongoni mwa zile zilizotajwa.

Wazee wangu, ni wazi kwamba kama chama chenye siasa chenye dhamana ya kuwaoongoza Watanzania kutoka katika lindi la ufukara, maradhi, matatizo ya makaazi na mengineyo siku zote tunapaswa kuwa makini katika kuhakikisha kwamba changamoto za kuwaongoza na kuwakomboa wananchi waliotupa dhamana hazitikiswi na mawimbi ya matakwa ya nyakati ama ya vyombo vya habari au wapinzani wetu wa kisiasa walio nje ya CCM.

Ni kwa sababu ya kulitambua hilo na hasa kuyatambua madhara yanayoweza kukipata chama chetu na nchi yetu iwapo tutaendekeza siasa za kupakana matope pasipo na sababu za msingi, kuchafuana kusikokoma na kulipizana kisasi ndiyo maana nimeona nitumie fursa hii kuzungumza nanyi wazee wangu ili kuweka kumbukumbu sahihi.

MAAMUZI YANGU

Wazee wangu, nimetafakari sana na kimsingi nimefikia hatua ya kupima yale ambayo yamekuwa yakisemwa na kuandikwa juu yangu na ambayo kwa mtazamo wangu unaoungwa mkono na wanafamilia yangu, marafiki zangu na washirika wangu wa kibiashara walio ndani na nje ya nchi, naona umefika wakati muafaka wa kuchukua hatua.

Kwa sababu ya kutambua uzito wa hatua ninazokusudia kuzichukua, niliona halitakuwa jambo la hekima hata kidogo iwapo ningefanya hivyo pahala pengine popote bali hapa Igunga mbele ya nyie wazee wangu.

Baada ya kukaa na wanafamilia yangu, marafiki na washirika wangu wa kibiashara niliona halitakuwa jambo la busara hata kidogo kuendelea kuvutana na viongozi wa chama changu na wanachama wenzangu wa CCM katika mambo ambayo yanaweza kumalizwa kwa njia muafaka.

Wazee wangu, sina budi niwaeleze kwamba, mbali ya athari za kisiasa na kifamilia, vita vya ovyo vya kisiasa kama hivi tunavyoviendesha na kuviendeleza ndani ya CCM na ndani ya nchi yetu huwa vina athari kubwa katika ulimwengu wa kibiashara. Athari kama hizo za kibiashara huingia ndani zaidi kuliko vichwa vya habari vya magazeti vinavyolenga kuchafuana, na athari hizo huwa kubwa zaidi kwa mtu kama mimi kwa sababu tofauti na wengine wengi hapa nchini, mimi ni mfanyabiashara wa kimataifa.

Katika ulimwengu wa kibiashara wa leo, vita hivi ambavyo vinaweza kuonekana kuwa ni vidogo tu vyenye malengo ya kuchafuana kisiasa, vinakuwa na athari kubwa katika uhusiano wa kibiashara kuliko hata wale wasioelewa wanavyoweza kukadiria. Ndiyo maana nimeona ni afadhali sasa niwape nafasi wale wanaoendesha siasa hizi uchwara na zisizo na tija waendelee na siasa zao hizo ambazo kwa bahati mbaya kwao, mimi sina muda nazo na siwezi kuwa sehemu yake. Na mimi kwa upande wangu niendelee na maisha yangu.

Kutokana na ukweli huo na sababu zote hizo basi, kwa moyo wa dhati na kwa nia thabiti, hatua ya kwanza niliyoiona kuwa ninapaswa kuichukua ilikuwa ni hii ya kuitikia wito unaotokana na msukumo wa ndani ya nafsi yangu wa kuamua kukomesha kabisa malumbano na mivutano isiyo na manufaa kwangu binafsi, kwa viongozi wa chama changu na chama chenyewe.

Msukumo huo si mwingine bali ni ule wa kuamua kuachia nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama, nikianzia na ile ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa nikiuwakilisha Mkoa wa Tabora na hii ya ubunge wa Igunga ambazo kama si kwa baraka za chama changu nisingelikuwa nazo.

Napenda kuliweka hili sawa sawa. Uamuzi wangu wa kuachia nafasi zangu zote za uongozi nilizopata kwa tiketi ya CCM haukutokana na wala haumaanishi kukubaliana na shinikizo lililopotoshwa kuhusu azma ya utekelezaji wa dhana ya kujivua gamba, la hasha, bali dhamira ya dhati ya kuachana na siasa hizi uchwara (gutter politics) na kutumia muda wangu kushughulika na biashara zangu.

Aidha, nimefikia uamuzi huo lengo likiwa ni kuwajengea heshima na imani machoni mwa wanachama na wananchi wengine, viongozi wangu ambao naamini baada ya mimi kujitoa watapata fursa ya kutafakari upya changamoto nyingine mbadala zinazowakabili ambazo msingi wake ni dhamana kubwa walizo nazo za kukiongoza chama chetu na nchi yetu kupitia Serikali yake.

Wakati nachukua uamuzi huu, natambua vyema kwamba, watatokea watu ndani ya chama chetu na nje ambao watafanya kila juhudi kupotosha au kupindisha ukweli kuhusu hatima yangu ya kisiasa baada ya kujiweka kando na kujipa mimi mwenyewe na chama changu fursa ya kutafakari kwa kina majaaliwa yangu na ya nchi yangu katika siku zijazo.

Nafanya hivyo nikiwa na imani thabiti kwamba, uamuzi wangu huu, hususani ule wa kuachia nafasi yangu ya ubunge, yatakipa fursa nyingine CCM ya kuendelea kuliongoza jimbo letu la Igunga katika kipindi cha miaka minne ijayo kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Kwa upande mwingine, uamuzi wangu huu naona ni fursa kwa viongozi wa Chama changu cha CCM kutafakari na kuamua njia wanayoiona wao ni sahihi kuichukua kwa hatima na mustakabali wa chama chetu na ambayo wanaamini itakipa nguvu mpya ya kisiasa dhidi ya vyama vya upinzani.

Sambamba na hilo, ninayo imani thabiti kwamba, uamuzi wangu wa kubakia kuwa mwanachama wa kawaida na mtiifu wa CCM utakuwa chachu kwa chama changu na kwa Serikali yake kuwatumikia wananchi kwa Ari Zaidi, Kasi Zaidi na Nguvu Zaidi.

Mwisho kabisa, nikimalizia naomba nitumie fursa hii kutoa heshima za pekee kwa Rais Jakaya Kikwete kwa kazi kubwa aliyoifanyia na anayoendelea kuifanyia nchi yetu. Amefanya mengi na makubwa kuiendeleza nchi yetu na watu wake kuliko inavyothaminiwa na kufahamika. Kazi yake kubwa inashindwa kuthaminiwa na kufahamika kutokana na siasa chafu tunazoziendesha Tanzania. Wasia wangu kwa wanasiasa wenzangu, waandishi wa habari na Watanzania wenzangu kwa ujumla ni kuwa tunahitaji kuisaidia nchi yetu kwa kufanya siasa zenye mwelekeo wa kujenga ambazo ndiyo hasa zinapaswa kuwa siasa kwa maana halisi ya neno hilo.

Wazee wangu, baada ya maelezo hayo, nawashukuru sana kwa kunisikiliza na kunielewa.

Ahsanteni sana.
 

Tuesday, July 12, 2011

Ludacris ndani ya Serengeti Fiesta 2011

Best Blogger Tips
Via Tanzania Daima

MWANAMUZIKI mahiri wa miondoko ya hip hop ambaye pia ni mwigizaji wa filamu kutoka nchini Marekani, Christopher Brian Bridges ‘Ludacris’ anatarajiwa kutoa shoo ya aina yake kwenye kilele cha tamasha la Serengeti Fiesta 2011, kitakachofanyika viwanja vya Leaders Club, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na kusainiwa na Mkurugenzi wa Maendeleo na Utafiti wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, taratibu zote za kumleta Ludacriss zimekamilika, hivyo Watanzania wakae mkao wa kupata raha wakati wowote kuanzia sasa.

Aidha, aliongeza kuwa, mwanamuziki mwingine wa kimataifa kutoka nje, atatajwa baadaye ambako wote kwa pamoja wanatarajiwa kutumbuiza kwenye tamasha la miaka 10 ya msimu wa dhahabu unaoendelea na Serengeti Fiesta 2011 kwenye viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Julai 30.

Ruge alisema kwamba shamrashamra za kufikia kilele cha miaka 10 ya Serengeti Fiesta 2011 zitakuwa tofauti na zenye msisimko mkubwa, ikilinganishwa na miaka mingine yote iliyowahi kufanyika tamasha hilo, ambalo ni kubwa katika anga ya burudani ndani na nje ya Tanzania ikiwamo Afrika Mashariki kwa ujumla.

Wakati huo huo, Mutahaba ametoa shukurani kwa wakazi wa Mkoa wa Iringa na Mbeya kwa namna walivyojitokeza kwa wingi na kulikubali tamasha hilo ambalo hufanyika mara moja tu kila mwaka.

Wikiendi hii tamasha la Serengeti Fiesta 2011 litakuwa ndani ya mji wa Moshi kwenye uwanja wa Chuo cha Ushirika huku jijini Arusha litafanyika Namatongee.

Wachezaji wa Eritrea waingia mitini Tanzania

Best Blogger Tips
Via Tanzania

Wachezaji kumi na watatu wa timu ya mpira wa miguu ya Eritrea ya Red Sea mpaka sasa hawajarejea nchini kwao baada ya michuano ya kanda Tanzania, maafisa wamesema.

Baada ya Klabu hiyo ya Red Sea kupoteza ushindi wake katika michuano ya CECAFA ya nusu fainali siku ya Jumamosi, ni nusu tu ya wachezaji wote waliingia kwenye ndege kurejea Eritrea.

Inaripotiwa kuwa hii ni mara ya nne wa wachezaji wa mpira wa miguu kutoka Eritrea wanatoweka.

Vijana wa Eritrea mara kadhaa wanajaribu kukimbia umaskini, seikali ya kibabe na jeshi kujenga taifa.

Katibu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Tanzania Angetile Osiah ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa suala hilo limeripotiwa kwenye vyombo vya sheria kwa ajili ya Uchunguzi.

"Baadhi ya wachezaji waligongana katika tukio la kujaribu kugonga muhuri pasi za kusafiria za wachezaji ambao hawakuwepo wakati wa ukaguzi katika ofisi uhamiaji uwanja wa ndege lakini walipohesabiwa mmoja mmoja iligunduliwa kuwa wachezaji 13," alisema.

Timu ya Tanzania ya Yanga iliwashinda mahasimu wake wa muda mrefu Simba 1-0 katika fainali ya CECAFA Jumapili.

Monday, July 11, 2011

Dini yaibuka ikizuia kutibiwa hospitalini

Best Blogger Tips
Via Majira

MADHAHEBU ya dini yanayozuia waumini wake kwenda hospitali wala kutumia dawa ya aina yoyote wanapougua yameibuka Kibaha mkaoni Pwani na tayari watu
wawili wameripotiwa kupoteza maisha kwa kuzingatia masharti.

Mchungaji wa kanisa hilo kwa sasa jina tunalihifadhi kwa sababu hatujampata kuzungumzia madai dhidi yake, anadaiwa kuwazuia waumini wake kwenda hospitali wala kutumia dawa ya aina yoyote kwa madai kuwa kufanya hivyo ni kumkufuru Mungu wao mwenye kutibu kila aina ya ugonjwa.

Mchungaji huyo anadaiwa kuwakataza waumini wake kushirikiana na mtu yeyote asiyekubaliana na imani yao, hata kama ni wazazi wao.

Muumini wa kanisa hilo akiugua na ndugu wakaonekana kutaka kumhudumia, mahitaji ya kawaida na tiba, mchungaji huyo anamhamisha nyumbani.

Kutokana na imani hiyo, watu wawili, Bw. Tumainieli Mfinanga aliyefariki Oktoba mwaka jana na mkewe Bi. Jane Mathayo aliyefariki mwishoni mwa wiki iliyopita, Julai 9, 2011 kutokana na kukataa kwenda hospitali kutokana na imani hiyo.

Wakazi wa Kibaha na ndugu wa marehemu hao wameiomba serikali ifunge huduma hiyo na kumchukulia hatua mchungaji husika.

Akizungumza na Majira juzi katika mazishi ya Jane ambaye mara baada ya kujiunga na dini hiyo alibadili jina na kuitwa Sarah, ndugu wa marehemu huyo, Bi. Rebeka Mfinanga aliyetengwa na familia baada ya kukataa imani hiyo, alimfananisha mchungaji huyo na Joseph Kibwetere wa Uganda aliyewafungia kanisani waumini wake ili wasubiri siku mwisho kisha kuwateketeza kwa moto.

Alisema ndugu yake alianza kuugua Machi, 2011 na mchungaji huyo akamhamishia nyumbani kwake kumficha ili ndugu wasije wakampa dawa au kumpeleka hospitali hadi ndugu walipochukuwa hatua za kumshtaki polisi ambapo Julai 9, 2011 alimbeba mgonjwa akiwa ajitambui na kumtelekeza jirani na nyumbani kwa Bw. Bright Mfangavo ambaye ni binamu yake.

Alisema akiwa hajitambui alibebwa na kupelekwa katika hospitali ya Tumbi ambapo daktari aliyewapokea aligomba kumchelewesha mgonjwa kumpeleka hospitalini hadi kuzidiwa kiasi hicho.

Pamoja na mgonjwa huyo kupatiwa tiba hospitalini ya Tumbi, haikufaa kitu kwa kuwa ugonjwa ulikuwa umekwishafikia hatua mbaya na akaaga dunia.

Baada ya kifo hicho mchungaji alijulishwa lakini akadai hayamhusu kwa kuwa imani yake inaagiza kuwaacha wafu wazikane wenyewe na kuwataka ndugu wa marehemu watawanyike kila mmoja arudi katika makazi yake kabla hayajawakuta makubwa.

Bw. Mfangavo alisema, kauli hiyo ya mchungaji iliikera familia na kujiandaa kwa vita dhidi yake lakini wakalazimika kutoa taarifa polisi kuhusu vitisho vya mchungaji huyo na hatua walizokusudia kuzichukua dhidi yake.

Alisema mchungaji huyo aliwazuia baadhi ya ndugu wa marehemu ambao ni waumini wake kushiriki katika msiba, akiwamo mama mkwe wa marehemu, Bi. Christina Eliatosha, wifi yake Bi. Justa Mfinanga na mtoto wa marehemu, hadi juzi familia ilipokwenda kuwachukua kwa nguvu nyumbani kwa mchungaji, pamoja na mali za marehemu zilizokuwa zimebaki kwa mchungaji.

Bw. Mfangavo alisema mchungaji huyo alichoma moto baadhi ya mali za marehemu ikiwemo televisheni kwa madai kwamba ni mali haramu kwa kuwa marehemu alizipata kabla hajamjua Mungu.

Katika hatua nyingine, Bw. Mfangavo alililalamikia jeshi la polisi kwa kushindwa kutoa ushirikiano wa aina yoyote katika tukio hilo linalohusisha uhalibifu wa mali.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Bw. Ernest Mangu alisema hajapata taarifa yoyote kuhusu tukio hilo na kuahidi kuchukua hatua pale taarifa zitakapomfikia.

Jitihada za gazeti hili kumpata mchungaji huyo ziligonga mwamba kwani alipofuatwa nyumbani kwake hakupatikana na simu yake ya mkononi ilikuwa haipatikani hewani.

Wanafunzi wa kike watelekezwa gesti

Best Blogger Tips
Via HabariLeo

WANAFUNZI wawili wa kike wa kidato cha pili katika sekondari ya Enyeitu mkoani Arusha, wametelekezwa katika nyumba ya kulala wageni Dar es Salaam kwa mwezi mmoja sasa.

Wasichana hao wakazi wa Mianziani, Arusha, walifika Dar es Salaam Juni 4 wakifuatana na mwanamume anayejulikana kwa jina la Rwaka au Swai.

Mwanamume huyo aliwafikisha katika nyumba hiyo ya Flamingo iliyopo Nzasa A Mbagala katika wilayani Temeke.

Wanafunzi hao Neema Abel (17) anayedai anaishi na mjomba wake, Amos Michael na Tatu Salim (16) aanayeishi na dada yake Aisha Salim, walifika katika nyumba hiyo siku hiyo saa nane usiku na kupokewa na mhudumu Zainabu Abdallah.

Mwandishi wa habari hizi alifika katika nyumba hiyo ya kulala wageni juzi na kuwakuta wanafunzi hao wamekaa nje kama wapo nyumbani tena wakicheza bao na baadaye akazungumza nao.

Awali, mhudumu huyo alidai kuwa mwanamume huyo aliwaandika katika daftari la wageni wanafunzi hao kuwa ni Aisha Salim (Tatu) na Angela Amos (Neema) ambaye alidai mwanamume huyo ni baba yao mdogo na walifika naye jijini Dar es Salaam kwa lengo la kutembea.

Alisema, baba huyo alikuwa akifika kila siku katika nyumba hiyo na kuwapa fedha za chakula na kulipia gharama ya chumba namba nane walichokuwa wakiishi kwa wiki tatu.

Zainabu alisema, baadaye walishangaa kutomwona huyo mtu na hivyo wasichana hao wakashindwa kulipia chumba na chakula ndipo wakafichua kuwa hakuwa baba yao na amewatelekeza na wanadaiwa Sh 35,000 za chumba.

Mabinti hao wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili, walidai kuwa, mwanamume huyo ambaye ni mtu wa makamo, alikutana nao Arusha na kuwa marafiki wa kawaida.

Tatu alisema, baada ya kufunga shule, baba huyo aliwaambia waje Dar es Salaam kuona mji, ndipo naye akamtafuta rafiki yake, Neema, ambaye wanasoma wote shule moja na kutorokea Dar es Salaam.

Alisema, walipofika jijini, mwanamume huyo aliwaambia waseme kuwa ni baba yao mdogo na kuwaacha kwenye nyumba hiyo naye akaenda kwa mkewe, na akawa akifika mara kwa mara akiwa na rafiki yake na kuwaachia matumizi.

Alisema, siku moja alifika na kumtaka kimapenzi alipokataa, ndipo alikawaambia kuanzia siku hiyo watajua wenyewe watalala wapi, kula wapi na hata nauli ya kurudi Arusha.

Alisema, kuanzia siku hiyo wamekuwa wakipika chakula pamoja na wahudumu wa nyumba hiyo, huku bado wakiwa na deni la Sh 35,000 na bila kusema fedha wanazochanga kwa ajili ya chakula wanazipata wapi.

Angela alisema, wanachohitaji sasa ni nauli ya kuwarudisha Arusha, ili kuendelea na masomo, kwa kuwa shule wanayosoma ilifunguliwa jana na wamejifunza kutokana na makosa waliyofanya.

Baadhi ya wafanyakazi wa nyumba hiyo, walidai wasichana hao walisitishiwa huduma baada ya mwanamume huyo kuwakuta wakiwa na vijana wadogo na baada ya kusitishiwa huduma, wamekuwa wakitoka usiku na kwenda kwenye kumbi za starehe ili kupata fedha za kujikimu.

Kikwete amjenga Zitto

Best Blogger Tips
Via Tanzania Daima

SHEREHE za kuzaliwa upya kwa taifa la Sudan Kusini zilizofanyika juzi mjini Juba, ziliibua hisia mpya katika siasa za Tanzania baada ya Rais Jakaya Kikwete na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe, kuandamana kuhudhuria tukio hilo la kihistoria.

Ziara hiyo ilifanyika baada ya Rais Kikwete kumaliza safari ya kikazi mkoani Kigoma wiki iliyopita, ambako alizindua miradi kadhaa, ikiwamo ya Barabara ya Mwandiga – Manyovu inayopita katika Jimbo la Kigoma Kaskazini linalowakilishwa na Zitto.

Wakiwa Sudan, Kikwete na Zitto walipata fursa ya kusalimiana na kuzungumza na viongozi mbalimbali waliohudhuria sherehe hizo, akiwamo Rais wa nchi hiyo, Salva Kiir.

Safari hiyo ya Zitto na Kikwete imezua maswali miongoni mwa wadadisi wa siasa wanaofuatilia mwenendo wa rais anayekaribia kuondoka madarakani na mwanasiasa kijana katika harakati za mageuzi nchini.

Ingawa inajulikana kuwa Kikwete na Zitto wamekuwa na uhusiano mzuri kikazi, licha ya kupingana kiitikadi, ziara yao ya juzi iliongeza minong’ono, hasa baada ya Zitto kuvujisha sehemu ya mazungumzo kati ya rais na yeye (Zitto) na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, walipokuwa kwenye hafla ya uzinduzi wa barabara mkoani Kigoma.

Kwa mujibu taarifa zilizobandikwa na Zitto katika ukurasa wake wa facebook siku chache zilizopita, Rais Kikwete aliwanong’oneza yeye na Kafulila kwamba asingependa baada ya kustaafu kwake nchi iongozwe na rais ‘mzee’ kama yeye.

Rais Kikwete, ambaye aliingia madarakani kwa kampeni ya “ujana” huku akiwa na umri wa miaka 55 mwaka 2005, aliwaambia kina Zitto:
“Msikubali atakayenirithi awe wa rika langu, sasa kizazi chenu kijiandae.”

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema kauli hiyo, kama ilitolewa na Rais Kikwete kweli, ililenga kuhamisha mjadala wa kisiasa kuhusu mrithi wa Kikwete nje na ndani ya CCM.

Inafahamika kwamba wanasiasa “wakali” ambao Rais Kikwete anawaogopa, na ambao wameonyesha nia ya kuutaka urais baada yake, ni watu wa makamo kama yeye.

Vile vile, wananchi wanapokuwa wanajadili mustakabali wa nchi, suala la umri, dini, jinsia na eneo analotoka mtu, havijawahi kuwa vigezo vinavyotumika kumuunga mkono mgombea.

Lakini kwa taifa lililoshuhudia siasa zenye mrengo wa kijinsia katika kumpata Spika wa Bunge, na kauli za udini kwenye kampeni mara baada ya Uchaguzi Mkuu, haliwezi kupuuza kauli hizi za kigezo cha umri.

Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wamekuwa wakisisitiza kuwa ujana au uzee si hoja.
Wapo pia wanaosema kwa msisitizo mkubwa kwamba mgombea yeyote wa CCM atakayebebwa na Rais Kikwete ataanguka. Wanatoa sababu kadhaa.

Kwanza, wanasema nguvu yake ndani ya mfumo inalegalega kiasi cha kumnyima uwezo wa kushinikiza wanachama wakubaliane naye katika chaguo atakalowaletea.

Na kwa msingi wa makundi ndani ya CCM, kuna watu wamejipanga kwamba yeyote atakayeonekana kubebwa na JK lazima “apigwe chini.”

Pili, wachunguzi wanasema historia inaonyesha kuwa hakuna aliyebebwa na rais anayeondoka madarakani, akashinda.

Wanatoa mifano ya jinsi Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1985, alivyomtaka Dk. Salim Ahmed Salim, lakini akazidiwa kete na wajumbe waliomtaka mzee Ali Hassan Mwinyi. Hata mwaka 1995 alimtaka Dk. Salim, ikashindikana baada ya Dk. Salim mwenyewe kukataa kwa kutazama upepo wa kisiasa wa wakati huo.
Endelea kusoma habari hii...........................

Sunday, July 10, 2011

Kakobe, Mtikila wapambana ubalozi wa Marekani

Best Blogger Tips
Via Mwananchi

MCHUNGAJI Christopher Mtikila andaiwa kwamba amevuruga mpango wa kwenda nchini Marekani wa Askofu Zachary Kakobe wa Kanisa la Full Gaspel Bible Fellowship (FGBF).

Mtikila anadaiwa kuuomba Ubalozi wa Marekani nchini kumnyima viza kiongozi huyo mkuu wa FGBF kwa maelezo kwamba ana kesi ya kujibu mahakamani.

Kupitia taasisi ya Liberty International Foundation, Mchungaji Mtikila ameuandikia barua ubalozi wa Marekani nchini, akiutaka usimruhusu Kakobe kwenda nchini humo, kwa kuwa ana kesi ya kujibu.

Akiwa ameorodhesha tuhuma mbalimbali anazoeleza kuwa zinamkabili Askofu Kakobe katika kesi hiyo, Mtikila amesema, mpango wake wa kwenda Marekani, umelenga kuikimbia kesi hiyo.

"Tunaomba Askofu Kakobe asiruhusiwe kwenda Marekani hadi hapo kesi yake Namba 78 ya mwaka 2011 iliyofunguliwa kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania itakapomalizika," alisema Mtikila katika barua hiyo ya Julai 5 mwaka huu.

Mtikila ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji wa taasisi hiyo ya haki za binadamu, amefafanua kuwa Askofu Kakobe ameshtakiwa na wachungaji watatu wa kanisa lake la FGBF ambao ni Dezedelius Patrick, Angelo Mutasingwa na Benedict Kaduma.

"Anahusishwa na matumizi mabaya ya fedha za kanisa hilo zinazofikia Sh14 bilioni," alisema Mtikila katika barua hiyo na  kuongeza:
“Tunakuandikia kuomba mamlaka zako husika kumnyima Zacharia (Zachary) Kakobe kibali cha kuingia nchini kwako hadi hapo kesi dhidi yake iliyofunguliwa Mahakama Kuu itakapoamuliwa.”

Katika barua hiyo, Mtikila ameueleza ubalozi wa Marekani kuwa Askofu Kakobe anataka kuimbikia kesi hiyo na kuhamia katika mji wa Boston, ambako ataishi na kuendesha taasisi yake inayojulikana kama Bishop Zachariah Kakobe International Ministry.

Mwananchi lilimtafuta Askofu Kakobe juzi na jana ili kufahamu undani wa safari yake ya kwenda nchini Marekani, lakini simu yake ilikuwa ikiita muda wote bila kupata majibu.

Baadaye gazeti hili lilimpata msadizi wake ambaye alisema kwamba askofu huyo asingeweza kuzungumza kutokana na kwamba alikuwa kwenye huduma.
Endelea kusoma habari hii...............

Thursday, July 7, 2011

Biashara zafungwa Uganda siku ya pili

Best Blogger Tips
Via BBC

Wafanya biashara katika mji mkuu wa Uganda, Kampala wamefunga maduka yao kwa siku ya pili mfululizo kulalamikia kiwango cha sarafu ya nchi hiyo kinachoshuka kila kukicha pamoja na idadi kubwa ya wachuuzi wenye asili ya Kichina.

Wauza maduka wanadai kuwa sarafu dhaifu inapandisha bei za bidhaa kutoka nje.

Wakati huo huo wanasema hawawezi kushindana na wafanya biashara wa Kichina waliomimina bidhaa zao kwa wingi na kwa bei rahisi.

Mgomo wao wa siku mbili ni tukio la hivi sasa katika mfululizo wa maandamano ya kupinga kupanda kwa gharama za maisha nchini Uganda.

Polisi wa kuzuia fujo walikuwa mitaani kulinda doria katika mji wa Kampala, kuzuia uwezekano wa kuzuka ghasia.

Msemaji wa shirika la wafanyabiashara la jiji la Kampala, Issa Sekito amesema kua wamefunga maduka yao kuishinikiza serikali ishughulikie masaibu yao.

Bw.Sekito amesema kua shirika lake limeitaka serikali ushughikie biashara za Wachina ambao wamezidsha kujiimarisha nchini Uganda.

Bw.Sekito aliliambia gazeti moja la nchini Uganda kuwa ''Kwa mda sasa,tumekua tukiilalamikia serikali juu ya hawa wageni wanaoshiriki biashara ndogo ndogo,hususan Wachina, wanaokuja wakidai eti ni wawekezaji'.

Shilingi ya Uganda ilidondoka kufikia kiwango cha chini dhidi ya dola ya Marekani mwezi uliopita hadi Benki kuu ilipoingilia kati kujaribu kuiimarisha.

Shirika la habari la Reuters limearifu kuwa 'Mgomo huo umesababisha bei ya bidhaa kama sukari na chumvi kupanda nchini humo''.

Mkaazi mmoja wa mji wa Kampala aliyehojiwa na shirika hilo, Linda Sempijja alisema kuwa maisha yamekuwa magumu kwa sababu bei ya bidhaa zote imepanda.

Mkaazi huyo aliongezea kusema kuwa hawezi kuwalaumu wafanyabiashara, kwa sababu wao pia wanakabiliwa na hali ngumu. Nailaumu serikali, alisema.

Gazeti la kiserikali la New Vision limearifu kuwa Waziri wa Biashara na viwanda,Bi.Amelia Kyambadde alikutana na wafanyabiashara kwa mda wa saa sita.

Waziri huyo aliwasilisha ujumbe kutoka kwa Rais Museveni akiwahimiza wasimamishe mgomo wao, kwa mujibu wa gazeti hilo.

Wafanyabiashara, hata hivyo walisema hawatofungua maduka yao na kwamba mgomo wao utaendelea hata siku ya leo alhamisi.

Wadadisi wanasema kuwa mgomo wao ni ishara ya hivi karibuni inayoonyesha hali ya ongezeko la kutoridhia kwa wananchi kwa serikali ya nchi.

Mnamo mwezi Aprili, vyama vya upinzani vilianzisha maandamano ya kususia usafiri wa umma na kutembea kwenda kazini, kama ishara ya kuitaka serikali itambue ukweli wa kupanda kwa gharama za maisha.

Makundi ya kutetea haki za binadamu yanasema kuwa vikosi vya usalama viliua watu tisa walioshiriki maandamanao hayo.

Serikali ilivilaumu vikundi vya upinzani kwa kujaribu kuteka madaraka kupitia ghasia baada ya kushindwa katika Uchaguzi mkuu uliofanywa mwezi Febuari.

Andrew Chenge kikaangoni

Best Blogger Tips
Via Majira

SAKATA la ununuzi wa rada ya ulioingizia serikali hasara, limechukua sura mpya baada timu ya wabunge iliyotumwa Uingereza kufuatilia malipo ya
fedha hizo kutoka Kampuni ya BAE kupendekeza kuangaliwa uwezekano wa kuwafikisha wahusika hao mahakamani.

Pendekezo la timu hiyo iliyokuwa chini ya Naibu Spika, Bw. Job Ndugai na wenzake Bw. Azan Zungu, Bi. Angela Kairuki na Bw. John Cheyo yamefanana na yaliyotolewa na Kambi ya upinzani bungeni juzi, kuwa wahusika katika kesi hiyo washtakiwe.

Kamati ya Ndugai ilisema kuwa pamoja na kesi hiyo kufungwa au kumalizika nchini Uingereza lakini Tanzania inayo nafasi ya kuwaburuta mahakamani watuhumiwa wa kashfa hiyo.

Ingawa timu hiyo haikutaja majina ya wahusika, miongoni mwa waliokuwa wanachunguzwa na Taasisi ya Makosa ya Jinai ya Uingereza (SFO), ni aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakati wa sakata hilo, Bw. Andrew Chenge, aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt. Idris Rashid na mfanyabiashara Sailesh Vithlan.

Lakini baadaye jioni, akijibu hoja za wabunge kwenye kuhitimisha mjadala wa Bajeti ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma jana, Waziri wa Utawala Bora, Bw. Mathias Chikawe alimkingia kifua Bw. Chenge akisema Uingereza ilikwishamsafisha na hivyo hastahili kushtakiwa.

Mbali na wabunge hao kuitaka serikali kuchukua hatua za haraka kwa watuhumiwa hao zikiwemo za kuwafikisha mahakamani, pia wamelitaka bunge kutenga muda wa kujadili suala hilo ili wajue undani wake.

Akikabidhi taarifa ya safari hiyo kwa Spika wa Bunge, Bi. Anne Makinda jana, Bw. Ndugai alisema kuwa baada ya kamati hiyo kujadiliana na SFO, wameona bado kuna uwezekano wa kuchukua hatua zaidi kwa wahusika wote.

“Wakati tukiwa huko, moja ya changamoto ambayo tulikumbana nayo ni pale tulipohojiwa ni hatua gani tulizochukua kama nchi kuhusiana na suala hilo,” alisema Bw. Ndugai.

Alisema kuwa wao walijibu kwamba wamekwenda kwa nia ya kushinikiza kulipwa fedha zilizoamuriwa na Mahakama ya Uingereza kama chenji ya rada iliyouzwa kwa Tanzania kwa bei ya kuruka, kupitia serikalini badala ya asasi za kiraia za nchi hiyo, kwa kuwa ni za wananchi na wao ni wawakilishi wao, hivyo suala la kufungua kesi ni suala la serikali.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye pia alikuwa miongoni mwa timu hiyo, Bw. Mussa Zungu, alisema kuwa mafanikio yaliyopatikana katika ziara hiyo, ni pamoja na bunge la Uingereza na Serikali kutambua mchezo mchafu uliofanywa na Kampuni ya kuuza zana za kijeshi iliyouza rada hiyo, BAE Sustem, kwa kuiba na kuidhalilisha Tanzania kwa kutaka kulipa fedha hizo kupitia asasi za kiraia.

Hata hivyo alisema kuwa Julai 19 mwaka huu, timu hiyo imekaribishwa kwenye mjadala wa wazi ambao utakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo SFO, BAE, Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Kimataifa, Wizara ya Sheria ya Uingereza kwa lengo la kuweka mambo wazi kuhusiana na kitendo kilichofanywa na BAE, pia hiyo itakuwa ni fursa kubwa kwa timu ya bunge la Tanzania kuhoji maswali mbalimbali kuhusiana na mchakato huo.

Timu hiyo inataka fedha hizo zilipwe kwa riba inayoendelea kupatikana kutokana na fedha hizo kuwa katika akaunti ya BAE ambako zimehifadhiwa.

Kutokana na hali hiyo, wameitaka serikali kushirikiana na bunge kuhakikisha fedha hizo zinarudi na kuwa endapo hazitarudi mpaka Septemba 2011 hatua zaidi zichukuliwe kwa kampuni ya BAE.

Bw. Musa Zungu alisema kuwa hata baada ya kukutana na wahusika wa kampuni ya BAE, bado wamebaki na msimamo wao kuwa fedha hizo si tozo bali ni msaada.

Aidha timu hiyo pia ilikutana na Mkurugenzi wa SFO ambaye aliomba radhi kwa Serikali ya Tanzania kutokana na kushindwa kuishirikisha katika kesi hiyo wakati ikiendeshwa.

Mara kadhaa, Chenge amekuwa akikana kuhusika kwa namna yoyote na ufisadi huo wa rada na mara ya mwisho alijitokeza hadharani na kutangaza usafi wake baada ya SFO kuitimisha kesi hiyo bila kutaja chochote juu yake.

Utetezi wa Chikawe

Waziri Chikawe jana aliweka msimamo kwa niaba ya serikali kuwa
haiko tayari kumchukulia hatua yoyote Bw. Chenge kwa tuhuma za ununuzi wa rada hiyo.

Ilisema kuwa haina ushahidi wowote dhidi ya Bw. Chenge kuhusiana na tuhuma zinazoelekezwa kwake hasa kwenye sakata la ununuzi wa Rada ambao unadaiwa ulighubikwa na rushwa.

Hata hivyo, Bw. Chikawe alisema kuwa kama kuna mbunge yoyote au mtu yoyote mwenye ushahidi dhidi ya Bw. Chenge autoe na serikali itafanyia kazi siku hiyo hiyo.

“Suala la Rada limezungumzwa sana na limepotoshwa kwa kiasi kikubwa, SFO kwa kushirikiana na TAKUKURU walifanya uchunguzi wa kashfa hiyo na kubaini kuwa kwa hapa Tanzania hakuna mtu hata mmoja aliyehusika bali waliobainika katika makosa hayo ni watuhumiwa watatu kutoka nchini Uingereza,” alisema Bw. Chikawe.

Alisema kuwa waliohusika na kashfa hiyo, ni Bw. Sailesh Vithlan ambaye alikuwa dalali wa rada hiyo, Meneja Biashara wa Kampuni ya BAE, Bw. Jonathan Calman na mwingine aliyetajwa kama Bw. Christopher.

“Tutafanya kama kanisani kuwa mwenye ushahidi alete na asipoleta  hatutakwenda mahakamani kwa kuwa hatuna ushahidi, mahakamani huwezi ukaenda mikono mitupu ni lazima uwe na ushahidi wa kutosha...Chenge hatuna ushahidi naye na hili suala sasa nadhani mngeliacha,” alisema Bw. Chikawe.

Msimamo wa Upinzani

Juzi, Kambi ya Upinzania ilipinga fedha za rada kulipwa kupitia serikalini kwa madai kuwa haiaminiki na hasa ikizingatiwa kuwa fedha hizo zilipotelea mikononi mwake.

Msemaji wa Kambi ya Upinzani, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bi. Sazan Lyimo alisema, "Kambi ya upinzani tunaona kuwa bila watuhumiwa hao kuchukuliwa hatua, ni dhahiri kuwa taifa haliwezi kuwa na uhakika wa kuzilinda vizuri fedha hizo za rada pindi zikilipwa pamoja na fedha zingine za umma ambazo zinaendelea kupotea kwa kuwa umekuwa ni utamaduni wa serikali kutochukua hatua.

“Tunataka Bunge lako tukufu lijadili na liazimie kuanzishwa kwa akaunti ya muda ya fedha za rada, itakayosimamiwa kwa pamoja na wawakilishi wa Asasi zisizo za kiserikali za Tanzania, wawakilishi wa sekta binafsi na mwakilishi wa serikali na tunataka fedha hizi zilipwe haraka iwezekanavyo kupitia akaunti hiyo,” alisema Bi. Lyimo.
Endelea kusoma habari hii.........................

Tuesday, July 5, 2011

Serikali yamsafisha rasmi Chenge

Best Blogger Tips
Via Tanzania daima

WAKATI Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikiwa kimewaweka pabaya makada wake watatu kinaotaka kuwafukuza uongozi katika vikao vikuu vya chama katika dhana ya kukjivua gamba, serikali imemsafisha rasmi mmoja wao, Andrew Chenge, ikidai hauhusiki na kashfa anazotuhumiwa.

Chenge, ambaye amekuwa akihusishwa na ufisadi katika ununuzi wa rada nchini Uingereza, alisafishwa na serikali jana bungeni kwa kauli ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Mathias Chikawe, wakati akijibu hoja za wabunge kuhusu makadirio ya matumizi na mapato ya ofisi yake kwa mwaka wa fedha 2011/2012.

Alisema Chenge hahusiki na kashfa ya ununuzi wa rada. Badala yake, serikali imewataja waliohusika katika tuhuma hizo kuwa ni dalali Sailesh Vithlani na vigogo wawili wa Kampuni ya BAE System ya Uingereza, inayotengeneza zana za kivita.

Alisema kwa mujibu wa Shirika la Uchunguzi wa Makosa Makubwa la Uingereza (SFO) na Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa nchini (TAKUKURU), Chenge hakuonekana sehemu yoyote kuhusika katika sakata hilo.

“Hakuna ushahidi kuhusu Chenge kuhusika na mchakato huo wa rada, hivyo hatuwezi kwenda mahakamani kwa hisia, ndiyo maana hadi leo tulikaa kimya,” alisema Chikawe.

Alisema suala la rada limekuwa likizungumzwa kwa muda mrefu na kwa namna mbalimbali, ikiwamo kupotoshwa, hivyo ikiwa kuna mtu ana ushahidi dhidi ya Chenge aupeleke kwa serikali ili wamshitaki haraka iwezekavyo.

“Kama hakuna ushahidi, ndiyo maana tunatangaza kama kanisani kuwa kama kuna mtu ana ushahidi na yanayosemwa alete, tutaushughulikia hata leo,” alisema Chikawe kwa kujiamini.

Hatua hiyo inachukuliwa wakati zikiwa zimebaki siku chache kwa Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM kukaa kujadili, pamoja na mambo mengine, kuwafukuza uongozi makada walioamuliwa kujiondoa wenyewe kwa tuhuma za ubadhirifu, ambao hadi sasa hawajajiondoa.

Katika hatua nyingine, Kamati ya Bunge iliyotumwa kufuatilia fedha za rada imewasilisha ripoti yake kwa Spika jana mchana huku ikipendekeza waliohusika katika kashfa hiyo ya ununuzi wa rada wa Tanzania na Uingereza wachukuliwe hatua.

Mapendekezo hayo yalitolewa jana na mjumbe wa kamati iliyoundwa kufuatilia fedha hizo, Mussa Azzan Zungu, kwa niaba ya wenzake. Kwa niaba ya kamati, Naibu Spika Job Ndugai ndiye aliyemkabidhi Spika Anne Makinda ripoti hiyo.

Katika ziara ya Uingereza, mbali na Ndugai na Zungu, wajumbe wengine walikuwa Mbunge wa Viti Maalumu, Angela Kairuki (CCM) na Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Cheyo (UDP).

Kamati ilipendekeza pia kwamba ifikapo Septemba, kama BAE Systems itakuwa haijatekeleza matakwa ya kukabidhi pesa hizo serikalini, ishitakiwe.

Zungu alisema walipokuwa Uingereza walisisitiza kwamba pesa hizo si msaada bali ni haki ya Watanzania.

Alisema kwa sasa Bunge la Uingereza na serikali wanatambua mchezo mchafu uliofanywa na BAE kwa kutaka kulipa fedha zetu kwa kutumia asasi za kiraia. Alisema Serikali ya Uingreza imeona uonevu huo wa BAE Systems.

Awali Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Job Ndugai, alikiri kwamba walipokuwa Uingereza walikuwa wakihojiwa kama serikali imekwisha kuchukua hatua zozote dhidi ya watuhumiwa waliosababisha pesa hizo kuibwa. Alisema hii ndiyo ilikuwa changamoto kubwa waliyokumbana nayo.

Hata hivyo, alisema kuna ugumu katika kuwashughulikia wahusika, kwani BAE walikwisha kujiondoa katika kashfa hiyo na kesi ilikwishafungwa, wakajisafisha.

Kwa mujibu wa Ndugai, kamati za Kampuni ya BAE na SFO zinatarajiwa kubanwa na Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza kujibu tuhuma za sakata hilo la rada.

Ndugai alisema kikao hicho cha wazi cha pamoja kinatarajiwa kufanyika Julai 19 mwaka huu kwa kushirikiana na Wizara ya Sheria, Taasisi ya Rushwa ya Uingereza na wengine.

Kamati hiyo ilikwenda Uingereza Juni 17, 2011 na kurejea Juni 28, 2011 kushawishi BAE ilipe pauni milioni 29.9 na riba yake kupitia katika akaunti ya BAE zilikohifadhiwa.

Saturday, July 2, 2011

Strauss-Khan aachiwa bila dhamana

Best Blogger Tips
Via BBC

Aliyekuwa mkuu wa shirika la fedha duniani, IMF Dominique Strauss-Khan ameachiwa huru baada ya kupewa kifungo cha nyumbani na kurejeshewa dhamana yake ya dola za kimarekani milioni 3.7.

Imeripotiwa waendesha mashtaka wamekubaliana kuwa Bw Strauss-Khan aachiliwe huru "kwa udhamini wake mwenyewe," ikimaanisha aahidi kufika mahakamani.

Anatuhumiwa kumdhalilisha kijinsia mhudumu kwenye hoteli moja mjini New York mwezi Mei 14.

Lakini kesi hiyo inakaribia kufutwa baada ya kuibuka mashaka makubwa juu ya uaminifu wa aliyemshtaki.

Mwanasiasa huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 62 - aliyeonekana kuwa miongoni mwa wagombea wa urais wanaoongoza- alifika mahakamani siku ya Ijumaa.

Baada ya kutathmini taarifa za mwendesha mashtaka kutoka kwenye ofisi ya mahakama ya wilaya ya Manhattan, jaji ametangua masharti makali ya dhamana aliyopewa na Bw Staruss-Khan, lakini aliamuru kushikiliwa kwa hati yake ya kusafiria ili asiweze kusafiri nje ya Marekani.

Miongoni mwa yaliyowasilishwa ni taarifa kuwa mhudumu huyo alitoa ushahidi usio wa kweli kwa wazee wa baraza, bila kusema alisafisha chumba chengine kabla ya kumwambia msimamizi wake juu ya madai ya kudhalilishwa kijinsia.

Friday, July 1, 2011

Profesa Mwandosya, Prof. Lipumba walazwa

Best Blogger Tips
Via New Habari

VIONGOZI wawili, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba; na Waziri wa Maji, Profesa Mark Mwandosya, wanaumwa.

Wamelazwa katika Hospitali ya Apollo iliyopo katika mji wa Hyderabad, nchini India.

Profesa Lipumba alifika hospitalini hapo siku tano zilizopita kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.

Kwenye uchunguzi huo, kwa mujibu wa watu walio karibu naye, ilibainika kuwa anasumbuliwa na maradhi ya figo.

Juzi, Profesa huyo wa uchumi alifanyiwa upasuaji. Alipoombwa azungumzie maendeleo ya afya yake, hakuwa tayari kufanya hivyo kwa maelezo kwamba bado alikuwa akikabiliwa na ‘ulevi’ wa dawa.

Aliahidi kuzungumza leo au kesho kadri afya yake itakavyoruhusu. Baadhi ya watu walio karibu na mwanasiasa huyo walisema maendeleo yake kiafya yanaridhisha.

Kwa upande wake, Profesa Mwandosya amelazwa hospitalini hapo kwa zaidi ya wiki mbili sasa.

Imeelezwa kwamba waziri huyo aliugua ghafla wakati akishiriki Mkutano wa Bajeti mjini Dodoma. Alikodishiwa ndege kwa dharura na kupelekwa Muhimbili. Hata hivyo, hali yake iliendelea kuwa mbaya na kulazimika kupelekwa nchini India.

Watu walio karibu na Profesa Mwandosya walisema kwamba anasumbuliwa na maradhi ya uti wa mgongo.

“Mheshimiwa Waziri anasumbuliwa na uti wa mgongo, kuna pingili imelika,” kilisema chanzo chetu.
Ilielezwa kwamba Waziri Mwandosya ilikuwa arejee nchini jana ili awahi kusoma bajeti ya wizara yake, lakini hali yake ilibadilika ghafla kabla hajaondoka.

Kubadilika kwa hali yake kuliwalazimu madaktari wamshauri aendelee na matibabu.
“Hali ilibadilika ghafla, ikalazimu apelekwe katika chumba cha x-rays, ana maumivu makali, lakini wananchi wasiwe na wasiwasi,” kilisema chanzo chetu.

Watanzania wengi wamekuwa wakienda kutibiwa nchini India. Hatua hiyo inatokana na upungufu wa vifaa uliopo nchini. Serikali imekuwa ikijitahidi kuhakikisha vifaa na wataalamu wanapatikana ili kupunguza mzigo kwa Serikali wa kugharimia matibabu ya raia wake.

Tayari mipango madhubuti imeshakamilika kwa ajili ya kufanya upasuaji wa moyo na usafishaji figo hapa hapa nchini.

Zito alianika Baraza la Mawaziri

Best Blogger Tips
Via Mwananchi

WAKATI Ofisi ya Bunge ikigoma kumsaidia Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kupata nyaraka za Kikao cha Baraza la Mawaziri kwa ajili ya kuthibitisha madai yake kuwa Baraza hilo limerubuniwa, mbunge huyo amewasilisha kurasa nne za ushahidi huo akitumia dokezo la kikao hicho cha siri.

Habari zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel zilisema kuwa Zitto aliwasilisha ushahidi huo kwenye Ofisi ya Bunge jana mchana, huku taarifa zaidi zikionyesha kuwa aliwasilisha ushahidi huo ukiwa na hoja tatu kuthibitisha madai yake.

Kwa mujibu wa habari hizo, mbunge huyo aliwasilisha ushahidi wake uliosomeka “Tofauti kati ya mapendekezo ya Waraka wa Barazaa la Mawaziri na Pendekezo la Azimio la Bunge lililoletwa bungeni kuhusu kuongeza muda wa Shirika Hodhi la Mali za Mashnirika ya Umma, yaani Consolidated Holding Corporation (CHC)" .

"Amewasilisha ushahidi wake leo, uko hapa unafanyiwa kazi," alisema Joel alipoulizwa na gazeti hili.

Juzi, Spika Anne Makinda alimwongezea muda Zitto hadi Jumatatu Juni 4 mwaka huu, kuthibitisha madai yake hayo baada ya kueleza kuwa alishindwa kufanya hivyo juzi, Juni 29 kutokana na ofisi ya Spika kugoma kumsaidia kupata nyaraka za Kikao cha Baraza la Mawaziri kwa kuwa ni siri.

Akithibitisha hoja zake katika ushahidi huo ambao gazeti hili umefanikiwa kuuona, Zitto alisema, Azimio la Bunge lililowasilishwa bungeni na Serikali kabla ya marekebisho lilitaka CHC iongezewe muda wa mpito wa miaka mitatu na baadaye kazi zitakazokuwa zimebaki zipelekwe kwenye Ofisi ya Msajili wa Hazina ni tofauti na mapendekezo ya kitaalamu yaliyofikishwa mbele ya Baraza la Mawaziri.

Kwa mujibu wa maelezo ya Zitto, waraka wa wataalamu ulikuwa na mapendekezo ya aina mbili na kwamba hakuna hata pendekezo moja katika mapendekezo hayo lililozungumzia CHC kuongezewa muda wa miaka mitatu.

"Pendekezo la kwanza linalopatikana katika Aya ya 11.0 ya waraka huo, lilitaka CHC ifanywe kuwa taasisi ya kudumu. Pendekezo la pili linalopatikana katika Aya ya 12.0 ya waraka huo, liligusia mpango mbadala wa kuiongezea CHC muda wa miaka 5," ilisema sehemu ya ushahidi huo.

Katika ushahidi huo, Zitto alisema Aya ya sita ya Azimio la Bunge ilianza kujenga hoja ya kutaka CHC iongezewe muda wa mpito na baadaye majukumu yake yahamishiwe kwenye Ofisi ya Msajili wa Hazina. Alisema aya hiyo ilisomeka hivi:

"Na kwa kuwa Serikali inatambua umuhimu wa kuiongeza muda wa mpito wa shirika na Serikali inaandaa na kukamilisha utaratibu wa kuhamishia majukumu ya CHC kwenye Ofisi ya Hazina.

"Wakati Azimio lililoletwa bungeni lilijenga hoja hiyo ya kutaka majukumu ya CHC yaje kuhamishiwa kwenye ofisi ya Msajili wa Hazina, Waraka wa Baraza la Mawaziri katika pendekezo lake la pili, umetahadharisha kuwa mpango wa kuhamishia kazi za CHC kwenye ofisi ya Msajili wa Hazina, utakabiliwa na changamoto kubwa,"ilisema sehemu ya ushahidi huo.

Ushahidi wake huo kwenye hoja ya tatu ulisema kuwa, wakati Azimio hilo lililoletwa bungeni (kabla ya kurekebishwa) lilijikita katika kutaka CHC iongezewe miaka mitatu na baadaye majukumu yake yahamishiwe kwenye ofisi ya Msajili wa Hazina, hitimisho la waraka uliowasilishwa kwa Baraza la Mawaziri katika Aya ya 13 linasomeka:

"Waheshimiwa mawaziri, mnombwa kutafakari mapendekezo yaliyomo kwenye Aya ya 11 ya waraka huu na kumshauri Mheshimiwa Rais ayakubali na aagize utekelezaji wake

"Hivi ni dhahiri kuwa Baraza lamawaziri lilikiuka maoni na ushauri wa wadau na watalaamu wote waliotaka CHC ifanywe kuwa taasisi ya kudumu; na dhahiri kuwa Seriakli ilikiuka mapendekezo na sababu zake zote za msingi zilizowasilishwa katika kikao hicho ambazo zilitaka CHC ifanywe kuwa taasisi ya kudumu" inahitimisha taarifa hiyo.

Juni 23 mwaka huu wakati anachangia Azimio hilo, Zitto alisisitiza mara tatu kwamba Baraza la Mawaziri limerubuniwa kufikia hatua hiyo na akawataka wabunge kwa umoja wao kutokubali kupitisha azimio hilo kwa kuwa lipo kwa maslahi ya watu.

"Waheshimiwa wabunge, nawaombeni kwa umoja wetu tulikatae azimio hilo, hicho sicho tulichokubaliana kufanya. Tayari tumeiagiza CHC kufuatilia madeni yetu kwenye kampuni za umma halafu leo, tunataka kuliua shirika hili? alihoji Zitto kabla Spika Makinda hajamtaka athibitishe kauli hiyo.

Kadhalika, wakati Makinda akimwongezea Zitto muda wa kuthibitisha madai yake alisema “Waheshimiwa wabunge itakumbukwa kuwa tarehe 23 mwezi huu Mheshimiwa Zitto wakati akichangia Azimio la Serikali kutaka kuliongezea uhai Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma (CHC), alitoa tuhuma bungeni kwamba Baraza la Mawaziri, limerubuniwa kufikia maamuzi hayo."

Aliongeza: "Itakumbwa pia kuwa baada ya kauli hiyo, nilimtaka (Zitto) alete ushahidi ifikapo tarehe 29 Juni yaani leo. Sasa kwa kuwa siku yenyewe ya kuleta ushahidi ni leo, naona bora nitoe taarifa rasmi kwenu."

"Kwamba siku ileile ya tarehe 23, Mheshimiwa Zitto aliniandikia barua kuniomba nimsaidie kumpatia nyaraka za Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichopitisha uamuzi huo. Amefanya hivyo kwa kutumia Kanuni ya Haki, Sura na Madaraka ya Bunge zinazompa haki mbunge kuiomba ofisi ya umma kumpa nyaraka anazozihitaji.

Hata hivyo, Makinda alisema, ofisi yake haikuweza kumpatia Zitto nyaraka hizo kwa kuwa vikao vya Baraza la Mawaziri ni siri na nyaraka zake zote hazitolewi kwa umma.

Thursday, June 30, 2011

Urusi: Wafaransa wamekiuka maadili Libya

Best Blogger Tips
Via BBC

Waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov amelaani hatua ya Ufaransa kuwapa silaha waasi wanaopinga utawala wa kanali Muammar Gaddafi.

Bw Lavrov anasema hatua hiyo ikiwa imedhibitshwa ni kosa kubwa kwani imekiuka azimio 1970 la umoja wa mataifa ambalo linazuia silaha kuingizwa nchini humo na pande zote husika kwenye mzozo huo.

Wanajeshi wa Ufaransa walikiri kuwaangushia silaha wapiganaji wa kabila la Berber wanaoishi kwenye maeneo ya milima kusini mwa mji mkuu wa Tripoli.

Umoja wa Afrika pia umelaani uaamuzi wa Ufaransa wa kuimarisha nguvu za kijeshi za waasi hao.

Mwenyekiti wa tume ya Umoja huo Jean Ping amesema kitendo hicho kinaweka eneo zima hatarini.

Waziri wa mambo ya nje wa urusi amepanga kukutana na mwenzake kutoka Ufaransa Alain Juppe mjini Moscow kudhibitisha suala hilo tete.

Serikali ya urusi ilisusia kupigia kura mswada uliowasilishwa kwenye baraza la usalama la umoja wa mataifa kuruhusu harakati za kijeshi nchini Libya.

Mzozo unaoendelea mjini Libya ndio umepewa kipa umbele katika mkutano wa viongozi wa Afrika unaoendelea nchini Equatorial Guinea.

Bw Ping amesema kuna uwezekano mkubwa vita vya wenyewe kwa wenyewe vikazuka nchini humo sawa na hali iliyoko nchini Somalia.

Mwenyekiti wa tume hiyo ya Umoja wa Afrika amefahamisha BBC kuwa mpango wa amani uliyobuniwa mnamo mwezi March bado unazingatiwa.

Mpango huo unataka pande zote zisitishe mapigano ili mazungumzo ya amani yaweze kuanza.
Habari kwamba Ufaransa imedondosha silaha nchini Libya zilijitokeza kupitia gazeti la Ufaransa, Le Figaro la jumatano.

Gazeti hilo lilisema kuwa Ufaransa, nchi inayoongoza operesheni ya NATO nchini Libya haikufahamisha nchi wanachama wenzake kuhusu operesheni hio.

Uwamuzi huo ulifikiwa baada ya mkutano uliofanyika mwezi April kati ya Rais Nicolas Sarkozy na Mkuu wa vikosi vya waasi wa Libya Gen Abdelfatah Younis.

Slaa afufua upya ufisadi

Best Blogger Tips
Via Raia Mwema

WAKATI wafadhili wakikabidhiwa ripoti inayoonyesha bado Tanzania kuna ufisadi, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, ameibuka na kusema hatorudi nyuma katika mapambano dhidi ya rushwa kutokana na serikali kuwaogopa wala rushwa na mafisadi wakubwa.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na Raia Mwema, jana, Jumanne, Dk. Slaa amesema wakati wote ambao yeye na wenzake katika Upinzani wakipigania hatua kuchukuliwa dhidi ya mafisadi na wala rushwa wakubwa, serikali imekuwa na kigugumizi katika kuchukua hatua; huku ikitumia mbinu za kuwafunga midomo.

Akitoa mfano wa kesi mbalimbali zikiwamo za wizi katika akaunti ya madeni ya nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (EPA) kupitia kampuni ya Kagoda Agricultural Limited na kashfa ya rushwa katika ununuzi wa rada ya kijeshi, Dk. Slaa amesema serikali inawalinda wahusika wakuu.

 “Kampuni kama Kagoda wahusika wanajulikana lakini hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi ya wahusika. Hii si dalili nzuri maana inaashiria kwamba wakubwa wanahusika ama wanawaogopa wahusika. Hatudanganyiki na hatunyamazishwi, tutaendelea kusema na kutaka hatua zichukuliwe,” anasema na kuendelea;

“Kashfa ya rada ni aibu kusikia serikali inadai fedha za rada wakati ilikuwa na kigugumizi wakati Uingereza wakichunguza wahusika wa rada na walishindwa kutoa ushirikiano kwa wachunguzi, lakini sasa eti wanasikia kuna fedha ndio wanazitaka. Kwa nini walikataa kushughulikia wahusika kwa sheria zetu za Tanzania na kuachia Waingereza kila kitu?” alihoji Dk. Slaa.
Endelea kusoma habari hii....................

Aibiwa gari baada ya kuleweshwa

Best Blogger Tips
Via habariLeo

DEREVA teksi Minaji Omary (39), ameibiwa gari baada ya abiria aliyempakia
kumnywesha soda inayodhaniwa kuwa na dawa za kulevya.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Adolfina Chialo alisema, tukio hilo limetokea jana saa 6 usiku kwenye baa ya Uhuru, mjini Morogoro.

Gari iliyoibwa ni yenye namba za usajili T321 BCU aina ya Toyota Corola ambayo dereva wake, baada ya kunywa soda hiyo alipoteza fahamu.

Kamanda Chialo alisema, alfajiri dereva huyo alipoamka hakuiona gari wala
abiria huyo na ndipo alipofika katika Kituo Kikuu cha Polisi na kutoa taarifa hizo. Polisi wanaendelea na uchunguzi.

Katika hatua nyingine, Kamanda Chialo alisema, mkazi wa Kihonda, Amina Maulid amefariki dunia baada ya kunywa vidonge ambavyo havifahamiki. Chanzo cha kujiua hakijajulikana.

Mtoto wa mwanamke huyo ambaye polisi haikutaja jina lake, ndiye aliyetoa taarifa Polisi kuwa mama yake alifariki dunia Juni 28 mwaka huu saa 5:30 usiku eneo la Kihonda, mjini Morogoro.

Alisema, baada ya polisi kufika nyumbani kwao, walikuta dawa za aina mbalimbali kwenye meza ndani ya chumba alichokuwa amelala mwanamke huyo.

Polisi inaendelea na uchunguzi wakati mwili ukiwa umehifadhiwa katika hospitali ya mkoa.

Posho kumfukuza Shibuda Chadema

Best Blogger Tips
Via Mwananchi

KITENDO cha Mbunge wa Maswa Mashariki, John Shibuda kupingana na sera ya chama chake kuhusu suala la posho za vikao (sitting allowance), kimeichefua Chadema ambayo imemuita msaliti ikisema, "adhabu yake ni kufukuzwa.

"Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe aliliambia Mwananchi mjini Dodoma jana kuwa, alikerwa na kauli iliyotolewa na Shibuda ya kwenda kinyume na msimamo kambi hiyo kupinga posho za vikao kwa wabunge na wafanyakazi wengine wa umma.

Mbowe alisema kwamba kwa kauli yake ya juzi ya kuunga mkono posho ilidhihirisha kwamba mbunge huyo ni msaliti wa kambi hiyo, hivyo sheria zitafuata mkondo wake.

"Kutokana na tukio la jana (juzi) bungeni, Shibuda kutusaliti katika suala la posho za vikao, taratibu za kisheria zitafuata mkondo wake kwani utovu wa nidhamu haukubaliki katika kambi yetu, hata katika chama chetu,"alisema Mbowe na kuongeza:

"Suala la posho si la mtu binafsi, lipo kwenye Ilani ya Uchaguzi wa 2010 ya chama chetu na kama kuna kiongozi hafahamu hili basi hakustahili kugombea ubunge kwa sababu naamini Ilani ya Uchaguzi, Shibuda anayo."

"Posho zilijadiliwa na kupitishwa katika vikao maalumu vya chama, kwa hiyo kama Katiba yetu ya chama inavyotuongoza, Shibuda alitakiwa kulipinga katika vikao hivyo sio kutoka nje ya kikao na kuanza kupingana na maamuzi yake,"alisema Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema.


Akinukuu kifungu katika Katiba ya chama chake kinachoeleza maadili ya viongozi, Mbowe alisema, "Kiongozi anatakiwa kutii na kutimiza maagizo anayopewa na viongozi wa ngazi ya juu au vikao halali na kama hakubaliani na maagizo hayo aeleze hivyo kwa kupitia taratibu na ngazi zilizowekwa kwenye kanuni."

Kauli ya Zitto
Kwa upande wake, Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe, aliliambia gazeti hili jana kuwa mbunge kupingana na sera ya chama chake, ni kutokiamini chama hicho.

"Maana yake hakiamini chama, hivyo hafai kuendelea kuwa mwanachama na mbunge wa chama hicho,"alisema Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema.

Aliendelea, "Hapa kuna mambo mawili; masuala ya kisera na masuala ya utaratibu. Mbunge anayepingana na taratibu adhabu yake ni kumwita na kumpa onyo, lakini mbunge anayepingana na sera, huyo hakiamini chama na dhabu yake ni kufukuzwa."

Kwa mujibu wa Zitto, suala la kupinga posho kwa Chadema ni sera kwa kuwa limo kwenye Ilani yake ya Uchaguzi ya mwaka 2010.

"Hili (suala la posho), lipo kisera. Kwenye Ilani yetu ya uchaguzi tulisema, tutapunguza mishahara ya wabunge na posho zao. Sasa kama mbunge anachaguliwa kwa sera hiyo halafu anaipinga haradhani, huyo hakiamini chama na chama hakipaswi kumwamini."

Aliendelea,"Sasa, adhabu ya juu kabisa ya mbunge asiyekiamini chama, ni kufukuzwa. Huu ni usaliti. Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni na mwenyekiti wa chama ameshalitolea tamko suala hilo halafu mbunge anakuja kumpinga hadharani maana yake nini,?" alihoji.

Tundu Lissu je?
Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake jana, Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu alisema kitendo cha Shibuda kupingana na sera ya chama chake, "ni uasi usiovumilika".

"Sasa nikiwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni nadhani ninahitaji kukaa naye. Nitamwita anieleze kulikoni. Aseme kulikoni ameamua kukiasi chama na upinzani kwa ujumla?"

Aliendelea, "Lakini kwa bahati mbaya sana, adhabu kubwa inayoweza kutolewa na kambi ya upinzani ni kumtenga na kambi. Lakini kwa mtu kama Shibuda ambaye tayari anaijua adhabu hiyo na kuitafuta kwa makusudi, inaonekana haitamtosha."

"Kwa sababu hiyo basi, kambi ya upinzani itaenda mbali zaidi baada ya kumtenga. Tutakiandikia chama barua kukijulisha usaliti huo wa mbunge wake halafu chenyewe kina taratibu zake za kinidhamu."
Endelea kusoma habari hii...........................

Wednesday, June 29, 2011

Mwanamke wa kwanza kuongoza IMF

Best Blogger Tips
Via BBC

Waziri wa Fedha wa Ufaransa Christine Lagarde ameteuliwa kuwa mkurugenzi mkuu wa shirika la fedha duniani IMF.

Kufuatia uteuzi huo Ufaransa itakuwa imeshikilia kiti hicho kwa miaka 26 kati ya miaka 33 iliyopita.

Christine Lagarde mwenye umri wa miaka 55, alikuwa mwanamke wa kwanza kuteuliwa waziri wa fedha katika muugano wa nchi saba zilizostawi maarufu kama G-7.

Lagade anatarajiwa kujiuzulu kutoka serikali ya Ufaransa ili kuandikisha historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwahi kuongoza shirika la fedha duniani IMF.

Uteuzi wake umefuatia kujiuzulu wa mfaransa mwenzake Dominique Strauss Kahn, baada ya kukabiliwa na kashfa ya ubakaji.

Sio wengi walioshangazwa na uteuzi wa wakili huyo wa zamani ambaye ana sifa nzuri kote duniani.
Amekuwa msuluhishi wa matatizo mengi ya kiuchumi yanayokumba mataifa kadhaa barani ulaya katika miaka ya hivi karibuni.

Kabla ya kuteuliwa kwake alikuwa ameungwa mkono na China na India na hivyo kuteuliwa kwake kama mkurugenzi mkuu wa shirika hilo la fedha duniani ilikuwa jambo lililotarajiwa.

Kuna maelewano ambayo hayajanakiliwa kuwa raia wa mataifa ya bara ulaya pekee ndio wanaopaswa kuteuliwa kuhudumu kama mkurugenzi mkuu wa IMF huku raia wa marekani wakipewa nafasi za kuongoza benki kuu ya dunia.

Mataifa yaliostawi yanataka kupewa nafasi kuu katika siasa za dunia, lakini huu ni wakati mgumu kwa mataifa ya ulaya huku mzozo wa kiuchumi wa Ugiriki ukitishia kuathiri mataifa mengine katika kanda hiyo.

Muungano wa ulaya na IMF zimeishurutisha serikali ya Ugiriki kupunguza matumizi yake ili kuendelea kupata msaada kutoka kwao.

Lagarde amekuwa katika mstari wa mbele kujaribu kutatua matatizo hayo ya nchi wanachama wa EU.

Tuesday, June 28, 2011

Hawara amuua mwenye mume

Best Blogger Tips
Via HabariLeo

MWANAMKE mkazi wa Ronsoti mjini Tarime mkoani Mara, Debora James (30), anatuhumiwa kumuua mwenzake, Teresia Nago, kwa kumchoma kisu katika mauaji yanayohusisha kugombea mwanamume.

Kwa mujibu wa Polisi, Teresia aliuawa jana saa 4.30 asubuhi Bomani mjini Tarime, baada ya kuchomwa visu viwili tumboni na kifuani na mgomvi wake huyo.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rorya/Tarime, Sebastian Zakaria, alisema Debora alikuwa akituhumiwa kuwa na uhusiano na mume wa Teresia, John Nago ambaye ni mtumishi wa Idara ya Ujenzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Kaimu Kamanda alisema, wanawake hao wawili walikuwa na ugomvi wa muda mrefu na vurugu wakigombea mwanamume huyo.

Alisema, jana Teresia na Debora walikwenda kusuluhishwa na mzee wa Kanisa ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja eneo la Bomani.

Lakini wakiwa Bomani, kulitokea vurugu na Debora ambaye alikuwa na kisu alimshambulia Teresia kwa kumchoma kisu kifuani karibu na moyo na tumboni na kusababisha kifo chake papo hapo, baada ya kutokwa damu nyingi naye akajichoma visu sehemu mbalimbali za mwili wake kwa lengo la kujimaliza.

Kamanda Zakaria alisema Debora amelazwa katika hospitali ya wilaya mjini hapa chini ya ulinzi wa Polisi baada ya kujijeruhi.

Monday, June 27, 2011

Best Blogger Tips
Libya yapuuza hati dhidi ya Gaddafi

Via BBC

Waziri wa sheria nchini Libya Mohammed al Qamoodi amesema hati za mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita za kutaka Kanali Muammar Gaddafi akamatwe zimelenga kuficha uhalifu wa Nato.

Akizungumuza mjini Tripoli, Bw Qamoodi amesema operesheni za Nato zinazoendelea nchini humo ni uhalifu wa kivita dhidi ya raia wa Libya lakini ICC imezifungia jicho.

Waziri huyo ameongeza kuwa wanajeshi wa Nato sasa wamepata kisingizio cha kumuua kiongozi wao Kanali Gaddafi.

Hata hivyo ametangaza kuwa Libya imepata fursa ya kufungulia Nato mashtaka ya uhalifu wanaoendeleza nchini Libya.

Mahakama hiyo imemtuhumu Gaddafi kwa uhalifu dhidi ya binadamu na kuamuru mashambulio kwa raia baada ya machafuko dhidi yake kuanza kati kati ya mwezi Februari.

Mahakama hiyo iliyopo the Hague pia imetoa hati ya kukamatwa kwa mtoto wake wa kiume Saif al-Islam na mkuu wa idara ya ujasusi Abdullah al-Sanussi.

Hatua hio imeendelea kuzua hisia tofauti.

Mwenyekiti wa kamati ya bunge ya mashauri ya nchi za kigeni nchini Urusi, Konstatin Kosachev amesema kuwa uamuzi wa jaji hao sasa utavuruga juhudi za kutafuta suluhu ya mzozo huo.

Bw Kosachev amesema nia kuu ya jumuiya ya kimtaifa ni kuwa Kanali Gaddafi ajiuzulu na atoke nchini humo lakini sasa hilo huenda lisifanyike.

Badala yake, Kosachev amesema huenda kiongozi huyo atafanya kila juhudi kushinda vita hivyo na hii sio habari njema kwa Libya.

Lakini kwa upande wao, wapinzani wamekaribisha uamuzi huo.

Msemaji wao Ibrahim Dabbashi amesema sasa jukumu lipo kwa washirika wa Gaddafi kuelewa kuwa wanafanya kazi na mhalifu na wamshauri aondoke madarakani.

Maelfu ya watu wanaaminiwa kufariki dunia kwenye ghasia hizo.

Saturday, June 25, 2011

Best Blogger Tips
Katiba mpya 2014

Via Tanzania Daima

SERIKALI imetangaza rasmi kuwa Katiba mpya itazinduliwa Aprili 26 mwaka 2014, siku ambayo itakuwa ni maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Kauli hiyo ilitolewa jana mjini Dodoma na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipokuwa akifungua Semina Elekezi kwa wakuu wa mikoa na wa wilaya kuhusu mchakato wa Katiba Mpya.

Semina hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya St. Gasper, Pinda alisema mchakato wa uundwaji wa katiba hiyo umeshaanza ambapo wananchi wamepewa fursa ya kutoa maoni yao.

Alisema matarajio ya serikali ni kuwa mpaka ifikapo mwaka 2014 mchakato wa Katiba mpya utakuwa umekamilika na Aprili 26 Katiba mpya itazinduliwa.

“Ni matarajio ya serikali kuwa Katiba mpya itakuwa imekamilika na kuzinduliwa ifikapo Aprili 26, 2014 katika maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,” alisema.

Pinda alisema kama mambo yote yatakwenda kama yalivyopangwa, Muswada wa Sheria kuhusu Mapitio ya Marekebisho ya Katiba utawasilisha bungeni mwishoni mwa Mkutano wa Nne wa Bunge unaoendelea hivi sasa.

Alisema iwapo muswada huo hautawasilishwa katika mkutano wa nne basi utawasilishwa mwanzoni mwa mkutano wa tano unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Waziri Mkuu, aliwataka wakuu wa mikoa na wa wilaya kutoa ushirikiano kwa Tume ya Kuratibu na Kukusanya Maoni itakayoundwa ili kuwezesha mikutano ya hadhara ya kukusanya maoni kufanyika kama ilivyokusudiwa kwa kuhamasisha wananchi kuhudhuria na kutoa maoni yao.“Suala hili ni kubwa na la kitaifa, ni vyema viongozi wasiingize siasa na wajiepushe kuwashawishi wananchi katika kutoa maoni yao, bali wawaache watoe maoni kwa uhuru au pasipo shinikizo lolote,” alisema.

Waziri Mkuu alisisitiza kuwa hatua ya sasa si ya kutunga Katiba Mpya bali ni kuunda Tume ya Kuratibu na Kukusanya Maoni ya Wananchi kuelekea kutungwa kwa Katiba Mpya.

Mchakato huo wa kuelekea uundwaji wa Katiba Mpya, umekwishaanza na katika hatua ya awali, serikali imeandaa rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Marekebisho ya Katiba (The Constitutional Review Act) ya mwaka 2011.

Hata hivyo mchakato huo ulipata upinzani mkali kutoka kwa wadau mbalimbali wakipinga vipengele kadhaa vilivyomo kwenye muswada huo uliopelekwa bungeni kwa hati ya dharura katika Mkutano wa Tatu wa Bunge uliofanyika Aprili mwaka huu.

Miongoni mwa mambo yaliyolalamikiwa na wadau ni kuwa muswada huo uliandikwa kwa lugha ya Kiingereza ambayo ni watu wachache wanaoizungumza na kuielewa.

Wadau walipinga pia vituo vya kutolea maoni kuwa vitatu, ambavyo ni Zanzibar, Dar es Salaam na Zanzibar.

Hata hivyo serikali ililazimika kuuondoa muswada huo katika mkutano wa tatu wa Bunge na kuahidi kuwa utaandikwa kwa lugha ya Kiswahili na kuufanyia marekebisho kulingana na maoni ya wadau.

Wednesday, June 22, 2011

Best Blogger Tips
Pinda aacha kutumia Mercedes Benz

Via HabariLeo

KATIKA kile kinachotafsiriwa kuwa ni kuwatega mawaziri na viongozi wa Serikali wanaotumia magari ya kifahari na yenye gharama kubwa, Waziri Mkuu,Mizengo Pinda ameanza kuachana na matumizi ya magari yenye gharama kubwa.

Hatua hiyo inadaiwa kuwa inalenga kuwafanya mawaziri na viongozi wengine wa juu
wa Serikali, kupima, kutafakari na kuchukua hatua juu ya matumizi ya magari
ya gharama kubwa wanayotumia sasa ambayo yamekuwa yakipigiwa kelele na
baadhi ya wabunge na wananchi.

Uchunguzi wa gazeti hili ambao ulithibitishwa pia jana jioni na Katibu Mkuu wa
Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhan Khijjah, ulibaini kuwa Waziri Mkuu,
ameacha kutumia magari ya kifahari aina ya Mercedes Benz na Toyota
Land Cruiser VX na kuanza kutumia Toyota Land Cruiser GX.

Katika mahojiano maalumu na HABARILEO, Khijjah amethibitisha Pinda kuanza
kutumia aina hiyo ya magari katika misafara yake ambayo alisema ni ya gharama ya
chini ikilinganishwa na Benz na VX ambayo gharama yao ni kubwa sana.

“Ni kweli Mheshimiwa Pinda sasa ameamua kutumia magari haya ya GX, hajatangaza
popote juu ya uamuzi wake huu, lakini nahisi ni kama ujumbe kwa viongozi wengine
wa juu wa Serikali wanaotumia magari ya gharama kubwa ili kuwafanya nao wapime
na kuchukua hatua,” amesema Khijjah.

Katibu Mkuu huyo wa Hazina, alisema ipo mikakati kabambe iliyowekwa na Serikali
ili kudhibiti matumizi holela ya fedha za umma, lakini akasema si kila kitu lazima kisemwe bungeni, kwani mambo mengine yanahitaji utekelezaji wa moja kwa
moja.

“Mfano hatua hii ya magari ya msafara wa Waziri Mkuu kuwa ya gharama ya chini
unaonesha dhamira ya dhati ya kuanza kuokoa fedha za umma kwa matumizi yasiyo na sababu. Kama Waziri Mkuu anatumia gari kama hili kuna haja gani kwa kiongozi wa
chini kuagiza gari la thamani zaidi, haiwezekani,” alisema Khijjah.

Tuesday, June 21, 2011

Best Blogger Tips
Michelle Obama akutana na Nelson Mandela


Michelle Obama mke wa Rais wa Marekani amekutana na kiongozi wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake katika nchi mbili za kusini mwa Africa.

Wakfu wa Mandela umesema kuwa Bi Michelle Obama, mama yake na binti zake wawili wamemtembelea Bw. Mandela na kuzungumza nae kwa muda mfupi.

Mwandishi wa BBC Karen Allen ambaye yuko Johannesburg anasema kuwa shujah huyo wa ukombozi dhidi ya ubaguzi wa rangi mwenye umri wa miaka 92 anaonekana hafifu na ni nadra yeye kuwapokea wageni.

Ziara hii ya Michelle Obama inanuiwa kupigia debe umuhimu wa vijana uwongozini.

Ziara hii ni ya pili rasmi ambayo Michelle Obama amefanya peke yake tangu mumewe achukuwe hatamu za uwongozi mwaka 2009.Anatarajiwa kukutana na kiongozi wa sasa wa Afrika Kusini Jacob Zuma kabla ya kuelekea Bostwana.

Bi Michelle Obama pia anatarajiwa kuyatembelea makumbusho ya enzi za utawala wa ubaguzi wa rangi na mji wa mabanda wa Soweto ambao ulikuwa katikati ya harakati za kukabiliana na utawala wa wazungu waliochache katika enzi hizo za ubaguzi wa rangi.

Ziara hii pia itajumuisha kutembelea kisiwa cha Robin ambako Bw. Mandela alihudumu 18 kati ya miaka 27 aliyokuwa gerezani.

Bi Obama alikaribishwa Afrika Kusini jumanne jioni baada ya kutua katika uwanja wa ndege wa kijeshi mjini Pretoria ambako binti zake wawili Malia na Sasha walipewa blanketi kubwa zilizokuwa na rangi ya bendera ya Afrika Kusini kujikinga baridi.

Jumatano Michelle atakutana na viongozi vijana wa kike atakapotoa hotuba yake.
Source: BBC

Sunday, June 19, 2011

Best Blogger Tips
Familia ya Kawawa yagombea nyumba

FAMILIA ya aliyekuwa Waziri Mkuu mstaafu hayati Rashidi Kawawa, imesema itapigania kulinda heshima ya mwanasiasa huyo baada ya kuwapo tishio la nyumba yao iliyopo Kilimani mjini Dodoma inauzwa na kupangishwa na mama yao wa kambo.

Mama huyo, Asina Kawawa, anadai kuwa nyumba hiyo ni mali yake.

Kwa mujibu wa familia hiyo, nyumba hiyo inataka kupangishwa na mama huyo anayedai kwamba alirithishwa na Kawawa, licha ya familia kueleza kutotambua hilo, lakini pia ni makumbusho na moja ya maeneo ya kihistoria ya mwanasiasa huyo aliyepigania Uhuru wa Tanganyika.

Ingawa mama huyo anadaiwa kuwa mbioni kupangisha nyumba hiyo iliyopo kiwanja namba 34 eneo la Uzunguni mjini hapa, lakini ipo hatarini kuuzwa na benki ya CRDB baada ya kutumika kama dhamana ya mkopo wa Sh milioni 350 kwa ajili ya kujenga nyumba nyingine pembeni mwa hiyo, mali ya Asina.

Mmoja wa wanafamilia ya Kawawa, Zainab Kawawa ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), aliwaeleza waandishi wa habari akiwa katika nyumba hiyo, kwamba familia inataka kulinda na kutunza heshima ya Mzee Kawawa, kwa sababu hakuwa mtu wa kukopakopa ovyo.
“Tunataka kulinda heshima ya Mzee Kawawa, tumemweleza mama kuwa tuko tayari kulipa deni hilo, lakini hayuko tayari, kwa sababu anaamini tukilipa deni nyumba hii itakuwa yetu, lakini zaidi ni kwamba tayari kuna notisi ya CRDB ya kuuza nyumba kutokana na deni,” alisema Zainab.
Alisema licha ya kuomba mkopo wa Sh milioni 350, ambao ulikuwa ukitolewa kwa awamu, mama huyo alipewa Sh milioni 74 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa nyumba hiyo ya ghorofa moja nyuma ya nyumba ya Mzee Kawawa, lakini sasa deni hilo limefikia Sh milioni 102.

“Kama familia, tulikaa na kuzungumzia deni hili na kukubaliana kuwa linatuhusu, hivyo baadaye lilisimamishwa na sasa limefikia Sh milioni 102, na tayari CRDB wanataka kuja kuuza nyumba hii kwa sababu ya deni,” alisema Zainab ambaye alizungumza na wanahabari baada ya mkutano kati yake na mama yake na mwanasheria Ngonyani kutoka makao makuu ya CCM.

Alisema kwa mujibu wa maelezo ya mama yao, nyumba hiyo aliyokuwa akiishi Mzee Kawawa kwa muda mrefu, aliinunua kwa ubia mwaka 2007 kutoka serikalini na inadaiwa kuwa ilikuwa na kipengele cha kuwa mmojawapo akifariki dunia, basi anayebaki atairithi. 
Endelea kusoma habari hii.....................

Thursday, June 16, 2011

Best Blogger Tips
Zawahir sasa ni mkuu wa Al-Qaeda


Ayman al-Zawahiri, ambaye kwa muda mrefu mno amekuwa msaidizi wa Osama Bin Laden katika kuiongoza Al-Qaeda, na akishikilia nafasi ya pili katika kutoa amri, sasa ataliongoza kundi hilo.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa katika wavuti ya kundi hilo.

Bin Laden aliuawa nchini Pakistan alipopigwa risasi na kikosi maalum kutoka nchini Marekani mwezi Mei.
Kundi la Al-Qaeda limeonya kwamba litaendelea na vita vyake dhidi ya Marekani na Israel chini ya uongozi wa Zawahiri.

Wadadisi wa masuala ya Al-Qaeda wanaelezea kwamba Zawahiri, mwenye umri wa miaka 59, na aliyezaliwa nchini Misri, ni mtu mwerevu sana, lakini hana uwezo wa kuwavutia wafuasi wengi kama alivyofanya Osama.

Baadhi ya wadadisi wanasema yeye ndiye aliyepanga na kuendesha shughuli nyingi zilizohusiana na shambulio la Marekani la 9/11.

Kwa muda wa miaka mingi, msaidizi wa Bin Laden, ambaye atakayefanikiwa kumpata atapokea dola milioni 25 (pauni milioni 15), alitazamiwa kurithi madaraka hayo.

Taarifa iliyotangaza madaraka hayo ilichapishwa katika wavuti ya Al-Qaeda, na kusemekana imetolewa na uongozi wa juu unaotoa amri katika kundi hilo.

"Sheikh Dk Ayman al-Awahiri, Mungu amsaidie, katika kuendelea na uongozi wa kundi", taarifa ilielezea.
Endelea kusoma habari hii..............

Monday, June 13, 2011

Best Blogger Tips
Mavs know Dirk is the primary reason they won an NBA title

Dirk Nowitzki had taken 12 shots, missed 11. He was -- for a shooter, for a scorer, for a leader -- having a nightmarish offensive game.

And since he and his Dallas Mavericks had mentally framed Game 6 as their Game 7, with a championship on the line not across 72 hours but right now, right then, Nowitzki could not have picked a worse time to suffer through a horrible, potentially crushing half of basketball.

OK, OK, Dallas actually was in front at that point, 53-51. So it wasn't a worst-case scenario, just a bad-case scenario. Especially if Nowitzki's just-off-the-mark shots kept missing, if the Miami Heat found their rhythm or (yikes) both.

His pal, Steve Nash, had Tweeted in the afternoon that he sensed a "monster" game from Nowitzki, and he wasn't far off. His many misfires were scaring small children.

"It was weird," Nowitzki said. "I had so many good looks. I can't even explain it. I had some threes, top of the key. I had a wide-open three in the corner. I had some pull-ups. I had some one-leg fadeaways that I normally make.

"The team always told me, 'Stay with it. Stay with it. You're too good of a shooter, too good of a player to keep missing.' "

Ya think?

Nowitzki isn't LeBron James, a player versatile enough or self-conscious enough -- you be the judge -- to turn away from his duties as a scorer. He did what shooters do and kept shooting.

He drained a 17-footer 12 seconds after halftime. He hit a pull-up bank shot on the break minutes later. He splashed a 3-pointer that made it 71-65 with 5:08 left in the third.
 Access the full story..................

Saturday, June 11, 2011

Best Blogger Tips
Marekani yathibitisha kifo cha Fazul

Via BBC

Waziri wa mashauri ya nje wa Marekani Bi Hillary Clinton, amesema kifo cha Fazul Abdullah Mohammed, aliyeshukiwa kuwa mkuu wa Al Qaeda Afrika Mashariki, "ni pigo kubwa" kwa kundi hilo na washirika wake.

Jumamosi serikali ya Marekani imethibitisha kifo cha Fazul Abdullah Mohammed, katika tukio la kufyatuliana risasi na vikosi vya Somalia mjini Mogadishu.

"Kifo cha Harun Fazul ni pigo kubwa kwa Al Qaeda, washirika wake wa siasa kali, na shughuli zake Afrika Mashariki," Clinton aliwaeleza waandishi wa habari akiwa mjini Dar es Salaam, Tanzania.

"Ni mwisho unaostahili kwa gaidi aliyewaletea wengi kifo na huzuni watu wasiokuwa na hatia Nairobi, Dar es Salaam na kwingineko; Watanzania, Wakenya, Wasomali na wafanyakazi wetu wa ubalozi".

Awali afisa mmoja wa cheo cha juu katika serikali ya Marekani alithibitisha kifo cha kiongozi huyo wa Al Qaeda Afrika Mashariki, na kuipongeza serikali ya muda nchini Somalia.

Kiongozi huyo wa Al Qaeda katika kanda ya Afrika ya Mashariki Fazul Abdullah Mohammed, alishukiwa kuhusika na shambulio dhidi ya balozi za Marekani katika Kenya na Tanzania mnamo mwaka 1998.

Fazul Abdullah amekuwa mtu anayetafutwa sana barani Afrika baada ya zaidi ya watu 220 kuuawa na zaidi ya 5000 kujeruhiwa katika mashambuliio ya mwaka 1998.

FBI iliahidi dola milioni 5 kwa kichwa chake.
Endelea kusoma habari hii......................

Friday, June 10, 2011

Best Blogger Tips
Tetemeko latikisa Dar

Via Majira

WAKAZI wa jiji la Dar es Salaam jana walikumbwa na taharuki baada ya kutokea kwa tetemeko la ardhi lililodumu kwa sekunde kadhaa.

Tetemeko hilo lililotokea majira ya saa 5:28 asubuhi ambapo kwa mujibu wa wataalamu wa hali ya hewa lilitokea kilometa 52 kusini mashariki mwa jiji hilo.

Baadhi ya watu waliokuwa kwenye majengo marefu waliamua kuzikimbia ofisi zao kwa lengo la kujiokoa licha ya tetemeko hilo kutoleta uharibifu wa mali.

Vikundi vya wananchi vilionekana kujazana katikati ya mitaa mbalimbali nje ya majengo vikijadili tukio hilo.

Abdul Juma, mfanyabiashara aliyepanga katika jengo la PPF, alisema waliamua kutoka katika ofisi hizo kwa hofu kuwa huenda tetemeko hilo lingetokea tena.

“Ndugu yangu maisha ni matamu, mimi sijui nimeshukaje kutoka ghorofa ya tano, nilijawa na hofu baada ya kusikia tetemeko hilo.

Katika jengo la PPF House, askari polisi walionekana kurandaranda huku na huku kwa lengo la kuhakikisha kuna usalama wa raia na mali zao.

Taarifa za mtandao wa Geolojia zilisema kuwa tukio hilo lilikuwa na nguvu ya 4.8 upana kilometa 10.

“Tetemeko hilo limeonekana katika latitudo kusini mwa mstari wa greenwhich limekuwa kwa 7 na mashariki ni longitudo 39,” ilifafanua.

Taarifa hiyo iliyataja maeneo ambayo tetemeko hilo lilipita kuwa ni Zanzibar, Tanga na Nairobi nchini Kenya.

Tuesday, June 7, 2011

Best Blogger Tips
Rais Saleh wa Yemen 'aliumia' sana

Rais wa Yemen, Ali Abdullah Saleh, alijeruhiwa zaidi katika shambulio la makombora katika boma lake juma lililopita kuliko ilivyodhaniwa, maafisa wa Serikali wameambia vyombo vya Habari vya Marekani.

Maafisa wa Serikali waliambia shirika la Habari la AP kuwa Bwana Saleh alichomeka asilimia 40 ya mwili wake na anavuja damu katika fuvu lake kutokana na shambulio hilo la Ijumaa.

Rais anaendelea kupata matibabu nchini Saudi Arabia baada ya kushambuliwa katika Ikulu yake katika Mji Mkuu wa Yemen, Sanaa.

Afisa wa cheo cha juu Serikalini aliambia BBC kuwa hawatasema lolote kuhusiana na afya ya Rais Saleh.

"Sisi si madaktari. Na kama Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani, Bi Hillary Clinton alivyosema jana, sisi tuko hapa na Sanaa na tunafanya kila juhudi kuhakikisha kuwa tunaleta mabadiliko kwa utaratibu, amani na bila ghasia, kama inavyosema Katiba ya Yemen," afisa huyo alisema.
Endelea kusoma habari hii....................

Sunday, June 5, 2011

Best Blogger Tips
Binti mbaroni kwa 'kubaka kavulana'

Via Majira

MSICHANA mwenye umri wa miaka 16 (jina linahifadhiwa), mkazi wa Kigogo, Luhanga, Dar es Salaam anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za 'kumbaka' mtoto wa
kiume mwenye umri wa miaka mitatu.

Msichana huyo anadaiwa kumbaka mtoto huyo mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo alimuiba nyumbani kwao na kumpeleka kwenye pagale, nyuma ya Shule ya Msingi Kawawa.

Mama mzazi wa mtoto aliyefanyiwa unyama huo, ambaye hakutaka kutajwa jina lake alisema, wakati akifanya usafi ndani ya nyumba yake siku ya tukio saa 4 asubuhi, mtoto wake alikuwa nje akicheza na wenzake.

Alisema alipomaliza ndani alitoka nje kumchukua mwanaye huyo ili ampe kifungua kinywa, lakini hakumwona ndipo, akaanza kumtafuta zaidi ya saa nzima bila mafanikio.

Mama huyo alisema, baada ya kuhangaika kumtafuta mwanaye, akili ilimtuma kuchungulia ndani ya nyumba hiyo inayojengwa na alipofanya hivyo alikuta mwanaye amelaliwa na msichana huyo.

Alisema kuona hivyo alikwenda mbio kuita mama mwingine jirani yake ili ashuhudie kitendo anachofanyiwa mwanaye.

"Nikiwa na jirani yangu tulishuhudia msichana huyo akifanya kitendo hicho kwa mtoto wangu," alisema.

Baada ya kushuhudia yote hayo, walipiga kelele na kumkamata akiwa uchi na kumpeleka Kituo Kidogo cha Polisi Kigogo- Luhanga.

Msichana huyo alishikiliwa kwa muda katika kituo hicho kidogo cha polisi kisha akahamishiwa Kituo cha Urafiki kwa hatua zaidi za kisheria ambapo mtoto aliyebakwa akilipelekwa katika Hospitali ya Amana kupatiwa matibabu.
Best Blogger Tips
UKIMWI uliginduliwa mwaka 1981

Mwaka wa 1981, daktari mmoja wa California Marekani aliona vijana wa kiume watano, walioshiriki katika mapenzi ya jinsia moja, wakiwa na ugonjwa usiokuwa wa kawaida.

Walikuwa na homa ya pneumonia na saratani ya ngozi.

Dakta Gottlieb hakujua kuwa ripoti zake, ndio zitakuwa historia ya kwanza kuandikwa juu ya ugonjwa ambao baadae utakuja kuwa janga kubwa la AIDS, au UKIMWI.

Virusi vya HIV viligundulikana miaka miwili baada ya ugunduzi huo wa Dakta Gottlieb.

Tena damu ikaweza kupimwa kama ina virusi vya HIV, na baadae zikapatikana dawa kadha za kudhibiti ugonjwa huo.

Umoja wa Mataifa unakisia kuwa tangu mwaka wa 1981, UKIMWI umeuwa watu milioni 30, na idadi kama hiyo hivi sasa wanaishi na virusi vya HIV.

Lakini juma lilopita, umoja huo uliripoti kuwa idadi ya watu wanaoambukizwa inapungua katika nchi kadha, lakini mamilioni ya wagonjwa bado hawapati dawa wanazohitaji.

Matabibu wanasema virusi vya HIV sasa wanavifahamu sawasawa, na wagonjwa wanaofululiza kula dawa kwa wakati, wanaweza kuishi karibu maisha ya kawaida.
Source: BBC

Saturday, June 4, 2011

Best Blogger Tips
NY-born twin friars die on same day at age 92

BUFFALO, N.Y. – Identical twins Julian and Adrian Riester were born seconds apart 92 years ago. They died hours apart this week. The Buffalo-born brothers were also brothers in the Roman Catholic Order of Friars Minor. Professed friars for 65 years, they spent much of that time working together at St. Bonaventure University, doing carpentry work, gardening and driving visitors to and from the airport and around town.

"It was fun to see them, just quiet, gentle souls," Yvonne Peace, who worked at the St. Bonaventure Friary for nearly 21 years, said Friday.

They died Wednesday at St. Anthony Hospital in St. Petersburg, Fla., Brother Julian in the morning and Brother Adrian in the evening.

Both died of heart failure, said Father James Toal, guardian of St. Anthony Friary in St. Petersburg, where the inseparable twins lived since moving from western New York in 2008.

"It really is almost a poetic ending to the remarkable story of their lives," St. Bonaventure spokesman Tom Missel said. "Stunning when you hear it, but hardly surprising given that they did almost everything together."

Julian and Adrian Riester were born Jerome and Irving on March 27, 1919, to a couple who already had five daughters. They took the names of saints upon their ordination in the Catholic church.
"Dad was a doctor and he said a prayer for a boy," Adrian once said, according to St. Bonaventure. "The Lord fooled him and sent two."

After attending St. Joseph's Collegiate Institute, the brothers were turned away by the military because of their eyesight, the university said. One had a bad left eye, the other a bad right eye.

Eventually they joined the friars of Holy Name Province in New York City. They received separate assignments before reuniting at the seminary at St. Bonaventure from 1951 to 1956. After serving parishes in Buffalo for 17 years, they returned to St. Bonaventure in 1973 and spent the next 35 years there.

They had separate rooms in the friary but one telephone extension that rang into both, Peace recalled. It was usually the more talkative Adrian who answered, though Julian possessed a quiet authority. They never said who was born first.

"Brother Julian was like the big brother. Brother Adrian would defer to him," Peace said. "They picked up one of our friars at the airport one time and the friar said, `Can I take you to dinner?'
"Brother Adrian looked at Brother Julian and said, `We aren't going to dinner?' `No, we'll go home,'" Peace said. "So that was it. No discussion, no contradicting. `No, we aren't going today.'"

Funeral services are scheduled for Monday at St. Mary Our Lady of Grace Church in St. Petersburg. Afterward, the brothers' bodies will be flown to Buffalo and buried Wednesday at St. Bonaventure Cemetery, across the street from the university.
Source: Associate Press

Friday, June 3, 2011

Best Blogger Tips
Mjane wa Sisulu A Kusini afariki dunia

Afrika Kusini inaomboleza kifo cha mmoja wa watu walioongoza harakati za kupambana na ubaguzi wa rangi, Albertina Sisulu, aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 92.

Bi Sisulu alikuwa mjane wa Walter Sisulu, rafiki na mshauri wa aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela.

Mwanasiasa mashuhuri wa aina yake, alikuwa mpambanaji katika shirikisho la wanawake wa African National Congress (ANC).

Msemaji wa ANC Brian Sokutu alisema Bi Sisulu alikuwa wakati wote wa maisha yake akiwa katika harakati za kuleta demokrasia nchini Afrika Kusini.

Gazeti la Afrika Kusini la South Africa Times limemnukuu akisema, " Komredi Sisulu ametumia muda wake wote kuitumikia ANC na kuikomboa Afrika Kusini. Tunatoa heshima zetu kwa kiongozi huyu na mama wa harakati hizi."
Endelea kusoma habari hii...................

Thursday, June 2, 2011

Best Blogger Tips
Hillary Clinton kutembelea Afrika

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Hillary Clinton, atasafiri wiki ijayo kuelekea nchi tatu barani Afrika, kuzungumzia biashara, maendeleo  na masuala ya usalama wa kieneo.

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani inasema Clinton atatembelea Zambia, Tanzania na Ethiopia, kisha ataelekea Umoja wa falme za  kiarabu, ambapo atalenga mgogoro wa Libya.

Clinton amepangiwa kuhudhuria mkutano wa biashara nchini Zambia, utakaofanyika Ijumaa ya Juni 10 na kukutana na Rais wa Zambia, Rupiah Banda. Akiwa nchini Tanzania, wizara ya mambo ya nchi za nje ya Marekani inasema Clinton, ataelezea mafanikio ya nchi mbili  ikiwa ni pamoja na program kadhaa zilizopo huko.

Clinton anatarajiwa kutembelea Umoja wa Afrika wakati akiwa Ethiopia na kukutana na mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, Jean Ping. Wakati wa safari yake, Clinton pia atakutana na Waziri Mkuu wa Ethiopia,  Meles Zenawi na Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete.
Source: VOANews

Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits