RAIS Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa jana alipanda kizimbani
kumtetea Balozi wa zamani wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa
Mahalu katika kesi ya uhujumu uchumi yanayomkabili, huku akimmwagia sifa
kemkem za utumishi mwema.
Profesa Mahalu na mwenzake, Grace
Martin aliyekuwa Ofisa Utawala wa Ubalozi huo, wanakabiliwa na kesi hiyo
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakidaiwa kuisababishia
Serikali hasara ya Euro 2,065,827.60, kupitia mchakato wa ununuzi wa
jengo la Ubalozi wa Tanzania Italia.
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Tanzania kwa Rais Mstaafu kupanda kizimbani kwa sababu yoyote ile.
Mkapa
ambaye wakati wa ununuzi wa jengo hilo alikuwa Rais, aliieleza Mahakama
kuwa anatambua mchakato wa ununuzi huo na kwa kuwa yeye ndiye aliyetoa
idhini ya ununuzi, mchakato wote ulikwenda vizuri.
Mkapa na
msafara wake ulioongozwa na maofisa wa itifaki aliwasili mahakamani hapo
saa 3:45 asubuhi. Akiwa amevalia suti ya rangi ya kijivu alielekea
ndani ya Mahakama hiyo akiwa amezungukwa na wapambe wake akitabasamu
baada ya kuwaona wanahabari.
Aliingia katika chumba maalumu cha mapumziko hadi saa 5:32 asubuhi muda ambao aliitwa kizimbani kutoa ushahidi wake.
Kabla
hajaanza kutoa ushahidi, alikula kiapo maalumu cha kutoa ushahidi wa
ukweli na baadaye kuendelea hadi saa 7:31 mchana alipomaliza na
kuondoka.
Mkapa alianza kutoa ushahidi katika kesi hiyo
inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Ilvin Mugeta, akiongozwa na
mmoja wa mawakili wa Profesa Mahalu, Alex Mgongolwa kwa kueleza historia
ya utumishi wake katika nafasi za kidiplomasia.
Mkapa alijibu
maswali kwa kujiamini na kwa umakini mkubwa huku mara kadhaa akiwavunja
mbavu wasikilizaji kwa jinsi alivyokuwa akiwajibu mawakili wa Serikali
wakati mwingine mwenyewe alishindwa kujizuia kucheka.
Akielezea
mchakato mzima wa ununuzi wa jengo hilo. Mkapa alidai kuwa Serikali yake
ilifahamu ununuzi wake na taratibu za malipo baada ya kufahamishwa na
Profesa Mahalu na kwamba lilinunuliwa kwa maagizo ya Serikali yake.
“Nilitambua
muuzaji alipaswa alipwe malipo kwa kutumia akaunti mbili tofauti na
Serikali ilitoa baraka. Mimi nilitaarifiwa na sikuzuia,” alidai Mkapa.
Kuhusu
kuwepo kwa mikataba miwili katika ununuzi wa jengo hilo Mkapa alijibu:
“Ninachoweza kukumbuka kwa hakika mimi ni kwamba niliambiwa kuwa kuna
malipo katika akaunti mbili ‘separate’ (tofauti).
Alieleza
kushangazwa na taarifa kwamba aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Martin
Lumbanga katika ushahidi wake alidai kuwa alikuwa hajui mchakato wa
ununuzi wa jengo hilo.
Wakili Mgongolwa: Shahidi, alikuja hapa
Shahidi wa kwanza wa mashtaka (PW1), Martin Lumbanga akasema kuwa hakuwa
na taarifa za idhini ya Serikali katika ununuzi wa jengo hilo. Je, wewe
unasemaje?
Mkapa: Ninashangaa ni kwa nini alisema hivyo.
Mgongolwa: Lakini wewe ukiwa Rais ulijua na ukabariki, inawezekana yeye asingeweza kujua?
Mkapa: Ndiyo.
Mkapa
alidai kuwa katika mchakato wa ununuzi wa jengo hilo, mbali na Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kupitia kwa Balozi Mahalu,
wizara nyingine ambazo zilihusika ni Ujenzi na Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi akidai kuwa zote zilituma wataalamu wake kufanya
tathmini ya jengo hilo kabla ya ununuzi.
Akielezea maelezo
yaliyoko katika kielelezo cha 6 cha ushahidi wa upande wa utetezi
ambacho ni taarifa ya aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa bungeni wakati huo Jakaya Kikwete (sasa Rais) juu ya mchakato
wa ununuzi wa jengo hilo Mkapa alisisitiza:
“Maneno hayo ni sahihi. Hayo ndiyo ninayoyajua mimi kuwa ndiyo yaliyotokea.”
Taarifa
hiyo pamoja na mambo mengine, inaeleza kuwa jengo hilo lilinunuliwa kwa
jumla ya Sh.2.9 bilioni na kwamba hati za umiliki wake
zilishawasilishwa wizarani na kupelekwa kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
Hesabu za Serikali (CAG).
Mkapa alieleza kuwa hajawahi kupata
malalamiko yoyote kutoka Italia kuhusu ukiukwaji wa sheria katika
mchakato wa ununuzi wa jengo hilo na wala kwa mmiliki wa jengo hilo
kudai kuwa alilipwa pungufu ya kiasi walichokubaliana.
Wakili
Mgongolwa: Kikatiba Rais hukabidhiwa ripoti ya CAG. Je, una taarifa
yoyote ya CAG kuhusu malalamiko juu ya ununuzi wa jengo hilo?
Mkapa: Sikuwahi kupata malalamiko hayo.
Wakili: Nini ufahamu wako kama Rais Mstaafu juu ya utumishi wa mshtakiwa ambaye ulimteua kuwa Balozi Italia?
Mkapa: Ninamfahamu kama ni msomi mzuri, mwadilifu na mfanyakazi mwaminifu na kiongozi wa haki.
Akizungumzia
mawasiliano yake na Profesa Mahalu wakati akiwa Balozi, Mkapa alidai
kuwa walikuwa wakiwasiliana ama kwa maandishi au kwa mdomo na kwamba
hiyo ilitegemea usiri wa jambo husika, lakini akasisitiza kuwa wakati wa
mchakato wa ununuzi wa jengo hilo waliwasiliana.
Baada ya kumaliza
kutoa ushahidi wake, Mkapa aliulizwa maswali mbalimbali na mawakili wa
Serikali, Vicent Haule na Ponsiano Lukosi kuhusu ununuzi wa jengo hilo,
sehemu ya mahojiano hayo ilikuwa kama ifuatavyo:
Wakili Haule:
Mheshimiwa katika Hansard (kielelezo namba 6 cha upande wa utetezi)
uliyosoma imeandikwa jumla ya pesa zilizopelekwa kununua jengo hilo ni
kiasi gani?
Mkapa: Sh.2.9bilioni.
Haule: Na zilizoandikwa kwenye hii risiti ambazo ulisema ulikuwa unazifahamu ni kiasi gani?
Mkapa:
Nilichosema ni Euro 3milioni, mimi sijui exchange rate (gharama za
ubadilishaji wa fedha) wakati huo ilikuwa ni kiasi gani hiyo si kazi
yangu.
Haule: Nani aliagiza upelelezi wa ununuzi wa jengo hilo?
Mkapa: Mimi Sijui.
Haule: Uchunguzi wa malipo hayo ulifanyika lini ukiwa bado madarakani au baada ya kutoka madarakani?
Mkapa: Mimi sijui, nilikuja kusikia tu kuwa Balozi wako anashtakiwa.
Haule: Ulijua lini kuwa Balozi wako uliyekuwa umemteua wewe anashtakiwa?
Mkapa: Siku alipofikishwa mahakamani ndipo nilipoambiwa na kesho yake kweli nikamuona kwenye magazeti.
Haule: Ulisema ulipotaarifiwa kuhusu ununuzi huo ulibariki na hukuzuia, kwani ulipaswa kuzuia?
Mkapa:
Ningeweza kuzuia na kuamuru hizo pesa zipelekwe kwingine kwa kuwa
wakati huo tulikuwa na crisis (tatizo) ya fedha, lakini kwa kuwa niliona
umuhimu wa ununuzi wa jengo hilo nikaagiza linunuliwe.
Haule: Umuhimu upi wa kulipa kupitia akaunti mbili?
Mkapa: Kupata Chancellery (ofisi ya ubalozi)
Haule:
Baada ya kutoa maagizo hayo (kwa Profesa Mahalu) ni nani mwingine
wizarani (Mambo ya Nje) uliyemwarifu kuhusu malipo hayo kwa akaunti
mbili?
Mkapa: Kwani hiyo inahusiana na nini? Maagizo yangu mimi
nilishatoa kwa balozi jengo linunuliwe, kama Rais nilikuwa ninaagiza tu.
Haule:
Mheshimiwa, nakuuliza tena na nisingependa nawe uniulize swali. Ni
kweli au si kweli kwamba hakuna mtu mwingine wizarani ambaye ulimpa
taarifa hizo?
Mkapa: Sikumbuki mimi.
Lukosi: Mheshimiwa, Lumbanga akiwa Katibu Kiongozi ulikuwa ukimwamini?
Mkapa: Ndiyo.
Lukosi: Ni kwa kiasi gani ulimshirikisha katika ununuzi wa jengo hilo?
Mkapa:
Specifically katika hilo sikumbuki lakini ki-principle nilishatoa
maagizo kuwa kupata chancellery nunueni na yeye alikuwa akijua.
Tulifanya hivyo India, Marekani na Uingereza.
Lukosi: Sasa Lumbanga alisema hajui ununuzi wa hili. Je, wewe unaona ni kitu cha kawaida?
Mkapa:
Ndiyo maana nimesema nashangaa, maana haingewezekana kwamba mimi
nika-communicate (nikafanya mawasiliano) na wizara moja tu na Lumbanga
asijue.
Lukosi: Ulipata kujua au kuuliza ni kwa nini muuzaji alitaka alipwe kupitia akaunti mbili tofauti?
Mkapa: Sikuuliza, mimi nilichokuwa nataka ni Chancellery.
Lukosi:
Unakumbuka kuna jengo jingine la ubalozi ambalo muuzaji alitaka alipwe
kwa utaratibu huu wa kupitia akaunti mbili tofauti?
Mkapa: Siwezi
kusema, nakumbuka lakini siwezi kusema kwa sababu mambo mengine
ukiyasema, yanaweza kuharibu uhusiano na nchi husika.
Hakimu Mugeta: Kwa hiyo hayo mazingira huwa yapo?
Mkapa: Ndiyo.
Lukosi: Unawakumbuka watu wengine uliowahi kuwateua ambao wako mahakamani na yuko mwingine alishakuja kukuomba umtetee?
Mkapa: Ni lazima nilijibu hili? Alihoji Mkapa huku akicheka na kuwafanya wasikilizaji nao wacheke.
Lukosi: Kwa hiyo hii ni kesi ya kwanza kwako kuombwa kuja kutoa ushahidi?
Mkapa: Ndiyo.
Wakili:
Nikiwaambia lengo la mwenye jengo kutaka mchakato wa uuzwaji kuwepo na
mikataba miwili lilikuwa ni kukwepa kodi kwa Serikali yake utasemaje?
Mkapa:
Hilo ni tatizo lake na nchi yake, mimi nilikuwa nataka nyumba na
nimepata nyumba, nasema Al Hamdulillah, alisema Mkapa huku akicheka tena
na kuwafanya wasikilizaji nao wavunjike mbavu.
Lukosi: Nikikwambia
kuwa hizo pesa kulipwa kwa instalment (awamu), Profesa Mahalu alikuwa
anataka azitumie kwa maslahi yake utasemaje?
Mkapa: Mimi nitashangaa sana, hasa nitakushangaa wewe, maana Profesa mimi namuamini. Alisema Mkapa na kuwachekesha wasikilizaji.
Mahojiano
kati ya Mkapa na Wakili wa Profesa Mahalu, Mabere Marando katika
kusawazisha maswali aliyoulizwa na mawakili wa Serikali yalikuwa kama
ifuatavyo:
Wakili Marando: Shahidi, Umewahi kupata malalamiko yoyote
kutoka wizarani kuwa kuliwapo makosa katika ununuzi wa jengo la Ubalozi
Italia?
Mkapa: Sijawahi.
Wakili: Ama kutoka kwa Katibu Mkuu
Kiongozi, Martin Lumbanga au Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje au wa
Wizara ya Fedha au Hazna kwamba Balozi alifanya kosa kwenda kufanya
malipo katika akaunti mbili za muuzaji?
Mkapa: Yeyote kati ya hao hakuna.
Marando:
Mpaka unaalikwa kwenda kuzindua jengo hilo uliwahi kupata ushauri
kutoka Ofisi ya DPP (Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma) au kwa AG
(Mwanasheria Mkuu wa Serikali) kwamba usiende katika uzinduzi wa jengo
hilo kwa kuwa kuna uchafu?
Mkapa: Sikuwahi kushauriwa.
Awali,
Profesa Mahalu akijibu maswali ya Wakili Mgongolwa, alisema kuwa
Februari 19, 2006 alipigiwa simu na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya
Nje na kumwarifu kuwa kesho yake anatakiwa afike Dar es Salaam kwa
ajili ya mashauriano.
Alidai kuwa alimwambia kuwa kesho yake
isingewezekana kwa sababu ilibidi ajiandae, ndipo akaambiwa kuwa
Februari 21, awe amefika.
Alidai kuwa majira ya alasiri kama saa
10:30 ya Februari 21 alikuwa ameshafika ofisini kwa Kaimu Katibu Mkuu,
Balozi Patrick Mombo ambaye alimpa barua ya utenguzi wa uteuzi wake kama
Balozi nchini Italia iliyokuwa imeandikwa siku hiyohiyo ya Februari 21,
2006.
Profesa Mahalu alisema kuwa alishangaa maana hakuwahi kuwa
na jambo la kusababisha uteuzi wake kutenguliwa na kwamba alipomuuliza
Mombo alimjibu tu kuwa ni agizo ya Rais.
“Kabla ya kutenguliwa kwa uteuzi huo sikuwahi kuwa na tuhuma yoyote juu ya jambo lolote,” alisisitiza Profesa Mahalu.
Katika
kiapo chake alichokiwasilisha mahakamani mwaka jana Mkapa alisema: “Kwa
kipindi chote ambacho nimefanya kazi na Balozi Mahalu katika nafasi
mbalimbali za utumishi wa Serikali ameonyesha tabia thabiti na za dhati,
uaminifu, utiifu, uchapakazi na ubora.”
Alisema kuwa sifa hizo
zilimfanya atunukiwe na Rais wa Italia, Tuzo ya Heshima ya Juu wakati wa
kuadhimisha siku ya taifa hilo, muda mrefu baada ya kuwa ameondoka
nchini humo.
Mahalu na mwenzake wanadaiwa kula njama na kutenda
makosa hayo katika tarehe tofauti na katika maeneo tofauti huko Italia,
likiwamo la kumpotosha mwajiri wao katika hati ya matumizi.
Wanadaiwa
kuwa Septemba 23, 2002 jijini Rome, wakiwa waajiriwa wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, walisaini vocha yenye namba
D2/9/23/9/02 ikionyesha kuwa bei ya ununuzi wa jengo la ubalozi ni Euro
3,098,741.58, maelezo ambayo yalikuwa ni ya uongo na yenye nia ya
kumdanganya mwajiri wao.
Chanzo: Mwananchi
Monday, May 7, 2012
Monday, April 30, 2012
Jenerali Ntaganda ateka miji miwili DRC
Vikosi vinavyomtii Bosco Ntaganda, anayetafutwa na ICC vimeteka miji miwili ya mashariki mwa DRC.
Mwandishi wa BBC katika eneo hilo anasema maelfu ya watu wanakimbia mapigano makali na kuelekea karibu na mjini Goma.Mamia ya askari wenye silaha nzito wanaomtii Jenerali Ntaganda hivi karibuni walijitenga kutoka jeshi la nchi hiyo.
Akiwa anafahamika kama‘Terminator,’ Jenerali Ntaganda amekanusha tuhuma za ICC kuwa aliwasajili watoto kuwa askari.
'majibu ya chuki'
Mwandishi wa BBC Thomas Hubert akiwa Sake, kilometa 30 (18 maili) magharibi mwa Goma, anasema wakazi wamemwambia wamesikia mapigano kati ya vikosi vya Jenerali Ntaganda na vikosi vya serikali yakiendelea Jumapili usiku.Askari wa serikali walirudishwa nyuma na kuondolewa katika miji ya Mushake na Karuba, mwandishi wetu anasema, na wamerudi nyuma kwa kilometa 12 mashariki mwa mji wa Sake, ambako wanajikusanya kupambana naye.
Askari hao waasi walikimbia jeshi la Congo lenye ngome yake Goma mapema mwezi huu, idadi kati ya 400-500, kwa mujibu wa vyanzo vya UN na Majeshi ya DRC.
‘Terminator kwa ufupi’
- Alizaliwa mwaka 1973 nchini Rwanda
- Alikimbilia DR Congo akiwa kijana baada ya mashambulizi dhidi ya kabila la Watutsi
- Akiwa na miaka 17, anaanza siku za mapigano –akibadilisha kati ya waasi na askari, kote Rwanda na DR Congo
- Akawachezaji wa kujitoa wa tennis
- Mwaka 2006, alishtakiwa ICC kwa tuhuma za kusajili watoto kuwa askari.
- Ni kiongozi wa vikosi vilivyofanya mauaji ya Kiwanji mwaka 2008
- Mwaka 2009, anaujiunga na jeshi la Taifa la DRC na kuwa jenerali.
- Mwaka 2012, anaasi jeshi na kujitenga.
Kati ya mwaka 2002-2005, Jenerali Ntaganda alikuwa mkuu wa harakai za kijeshi wa waasi wa UCP wakiongozwa na mbabe wa kivita Thomas Lubanga – ambaye mwezi Machi alikuwa wa kwanza kukutwa na hatia na mahakama ya ICC baada ya kukutwa na hatia ya kusajili watoto kuwa aksari.
Jen Ntaganda mtuhumiwa mwenza – lakini Rais Joseph Kabila awali alikataa kukamatwa kwake kwa ajili ya amani ya DRC.
Rais mapema mwezi huu alitoa wito wa kukamatwa kwake lakini anasema hatampeleka ICC.
Licha ya kumalizika kwa vita vya DRC mwaka 2003, makundi kadhaa yenye silaha bado yanazunguka katika eneo lenye utajiri mkubwa wa madini mashariki mwa nchi lichaya UN na jeshi la nchi hiyo kuwanyang’anya silaha.
Source: BBC
Monday, April 23, 2012
Hakimu ambembeleza Lulu mahakamani
MSANII wa filamu, Elizabeth Michael Kimemeta maarufu kama Lulu, jana
alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu huku akibubujikwa
machozi kiasi cha kumfanya Hakimu Ritha Tarimo ambembeleze ili
kumnyamazisha.
Lulu anashtakiwa mahakamani hapo kwa kutuhuma za kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba na alifikishwa jana kwa mara ya pili akiwa chini ya ulinzi mkali wa askari Magereza na Polisi.
Lulu alifikishwa mahakamani hapo saa 3:06 asubuhi akiwa katika basi dogo la Magereza pamoja na mahabusu wengine wanawake ambalo lilikuwa likisindikizwa na magari mengine mawili na alikuwa chini ya ulinzi wa askari sita wa kike wa Magereza na askari mmoja wa kike wa Polisi wakishirikiana na askari wa kiume wa Magereza zaidi ya sita.
Mara baada kuingia katika chumba cha Mahakama, Lulu ambaye alikuwa amevalia dira jekundu alianza kulia kwa uchungu hali ambayo ilimlazimu Hakimu Tarimo pamoja na baadhi ya askari kumnyamazisha.
Kutokana na kujaa kwa watu mahakamani hapo, askari wa Kikosi Maalumu cha Magereza walilazimika kuufunga mlango wa Mahakama hiyo ili kesi hiyo isikilizwe.
Baada ya kesi hiyo kutajwa, Wakili Mwandamizi wa Serikali Elizabeth Kaganda aliiomba Mahakama iamuru watu wote watoke nje kwa sababu walikuwa wamefunga njia ili mtuhumiwa huyo aweze kupitishwa.
Hakimu Tarimo alikubaliana na ombi hilo na kuwaamuru askari kusafisha njia ili waweze kumpitisha msanii huyo kwa kile alichosema kuwa Lulu bado ni mtuhumiwa na anaweza kuumizwa.
“Askari safisheni njia ili mtuhumiwa aweze kupita kwa sababu yeye bado ni mtuhumiwa anaweza kuumizwa,"alisema Hakimu Tarimo.
Baada ya kutolewa kwa amri hiyo, askari walitimiza wajibu wao na muda mfupi njia ilipatikana na msanii huyo kutolewa mahakamani hapo.
Jopo la mawakili
Katika kesi hiyo, Lulu anatetewa na jopo hilo la mawakili akiwemo Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRAGG), Joaquine De- Melo, Kenedy Fungamtama, Peter Kibatala na Fulgence Massawe.
De- Melo pia aliwahi kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) na mshindi wa Tuzo ya Mwanamke Jasiri Tanzania ya Martin Luther King.
Fungamtama ambaye ndiye kiongozi wa jopo la mawakili hao wanaomtetea Lulu, anakumbukwa kwa kuitetea kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans, katika kesi dhidi ya Tanesco, ambayo alishinda na shirika hilo kuamriwa kuilipa kampuni hiyo zaidi ya Sh94 bilioni kwa kuvunja mkataba.
Kibatala ambaye pia anamtetea kada wa Chadema, Fred Mpendazoe katika kesi ya uchaguzi Jimbo la Segerea, pia ni Makamu wa Rais wa TLS, wakati Massawe anatoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).
Mawakili hao walijitokeza jana mbele ya Hakimu Tarimo tayari kumtetea Lulu na baada ya mawakili hao kujitambulisha, Wakili Kaganda alisema upelelezi wa kesi bado haujakamilika na kuiomba Mahakama iipangie tarehe nyingine.
Hakimu Tarimo aliiahirisha kesi hiyo hadi Mei 7, mwaka huu itakapofikishwa mbele ya Mahakama hiyo kwa ajili ya kutajwa.
Kwa mara ya kwanza Lulu alifikishwa mahakamani hapo Aprili 10, mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando akikabiliwa na la shtaka hilo la mauaji.
Wakili Kaganda alimsomea hati ya mashtaka alidai kuwa Aprili 7, mwaka huu katika maeneo ya Sinza Vatican, Wilaya ya Kinondoni, mtuhumiwa alimuua Kanumba. Kanumba alifariki dunia siku hiyo saa 9:00 usiku kwa kile kilichodaiwa kuwa ni baada ya ugomvi baina yake na Lulu.
Chanzo: Mwananchi
Lulu anashtakiwa mahakamani hapo kwa kutuhuma za kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba na alifikishwa jana kwa mara ya pili akiwa chini ya ulinzi mkali wa askari Magereza na Polisi.
Lulu alifikishwa mahakamani hapo saa 3:06 asubuhi akiwa katika basi dogo la Magereza pamoja na mahabusu wengine wanawake ambalo lilikuwa likisindikizwa na magari mengine mawili na alikuwa chini ya ulinzi wa askari sita wa kike wa Magereza na askari mmoja wa kike wa Polisi wakishirikiana na askari wa kiume wa Magereza zaidi ya sita.
Mara baada kuingia katika chumba cha Mahakama, Lulu ambaye alikuwa amevalia dira jekundu alianza kulia kwa uchungu hali ambayo ilimlazimu Hakimu Tarimo pamoja na baadhi ya askari kumnyamazisha.
Kutokana na kujaa kwa watu mahakamani hapo, askari wa Kikosi Maalumu cha Magereza walilazimika kuufunga mlango wa Mahakama hiyo ili kesi hiyo isikilizwe.
Baada ya kesi hiyo kutajwa, Wakili Mwandamizi wa Serikali Elizabeth Kaganda aliiomba Mahakama iamuru watu wote watoke nje kwa sababu walikuwa wamefunga njia ili mtuhumiwa huyo aweze kupitishwa.
Hakimu Tarimo alikubaliana na ombi hilo na kuwaamuru askari kusafisha njia ili waweze kumpitisha msanii huyo kwa kile alichosema kuwa Lulu bado ni mtuhumiwa na anaweza kuumizwa.
“Askari safisheni njia ili mtuhumiwa aweze kupita kwa sababu yeye bado ni mtuhumiwa anaweza kuumizwa,"alisema Hakimu Tarimo.
Baada ya kutolewa kwa amri hiyo, askari walitimiza wajibu wao na muda mfupi njia ilipatikana na msanii huyo kutolewa mahakamani hapo.
Jopo la mawakili
Katika kesi hiyo, Lulu anatetewa na jopo hilo la mawakili akiwemo Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRAGG), Joaquine De- Melo, Kenedy Fungamtama, Peter Kibatala na Fulgence Massawe.
De- Melo pia aliwahi kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) na mshindi wa Tuzo ya Mwanamke Jasiri Tanzania ya Martin Luther King.
Fungamtama ambaye ndiye kiongozi wa jopo la mawakili hao wanaomtetea Lulu, anakumbukwa kwa kuitetea kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans, katika kesi dhidi ya Tanesco, ambayo alishinda na shirika hilo kuamriwa kuilipa kampuni hiyo zaidi ya Sh94 bilioni kwa kuvunja mkataba.
Kibatala ambaye pia anamtetea kada wa Chadema, Fred Mpendazoe katika kesi ya uchaguzi Jimbo la Segerea, pia ni Makamu wa Rais wa TLS, wakati Massawe anatoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).
Mawakili hao walijitokeza jana mbele ya Hakimu Tarimo tayari kumtetea Lulu na baada ya mawakili hao kujitambulisha, Wakili Kaganda alisema upelelezi wa kesi bado haujakamilika na kuiomba Mahakama iipangie tarehe nyingine.
Hakimu Tarimo aliiahirisha kesi hiyo hadi Mei 7, mwaka huu itakapofikishwa mbele ya Mahakama hiyo kwa ajili ya kutajwa.
Kwa mara ya kwanza Lulu alifikishwa mahakamani hapo Aprili 10, mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando akikabiliwa na la shtaka hilo la mauaji.
Wakili Kaganda alimsomea hati ya mashtaka alidai kuwa Aprili 7, mwaka huu katika maeneo ya Sinza Vatican, Wilaya ya Kinondoni, mtuhumiwa alimuua Kanumba. Kanumba alifariki dunia siku hiyo saa 9:00 usiku kwa kile kilichodaiwa kuwa ni baada ya ugomvi baina yake na Lulu.
Chanzo: Mwananchi
Kortini kwa kumbaka mtoto wa kaka yake
MKAZI wa Kiluvya, wilaya ya Kinondni jijini Dar es Salaam,
Mustafa Wachega (39), amefikishwa katika mahakama ya Kinondoni
akikabiliwa na mashtaka ya kumbaka mtoto wa kaka yake.
Akisomewa shtaka hilo mbele ya Hakimu Mkazi, Athuman Nyamlani, mwendesha mashtaka wa polisi, Magina Magoma, alidai kuwa Aprili 17 mwaka huu katika maeneo ya Manzese Tip top mshtakiwa anadaiwa kumbaka mtoto wa miaka 16 (jina linafadhiwa).
Mshtakiwa alikana shtaka hilo na yuko nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti na kesi hiyo na itatajwa tena Mei 7.
Chanzo: Tanzania Daima
Akisomewa shtaka hilo mbele ya Hakimu Mkazi, Athuman Nyamlani, mwendesha mashtaka wa polisi, Magina Magoma, alidai kuwa Aprili 17 mwaka huu katika maeneo ya Manzese Tip top mshtakiwa anadaiwa kumbaka mtoto wa miaka 16 (jina linafadhiwa).
Mshtakiwa alikana shtaka hilo na yuko nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti na kesi hiyo na itatajwa tena Mei 7.
Chanzo: Tanzania Daima
Friday, April 20, 2012
Wabunge kumng’oa Waziri Mkuu?
BAADA ya wabunge kuwasulubu mawaziri wakiwatuhumu baadhi yao kuhusika na
ubadhirifu wa fedha za Serikali, lakini kutokuwa na mamlaka ya
kuwafukuza katika nyadhifa zao, wametangaza azma ya kumng’oa Waizri Mkuu
Mizengo Pinda.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mashirika ya Umma (POAC), alitoa hoja hiyo jana usiku wakati akihitimisha hoja ya taarifa ya Kamati yake aliyoiwasilisha bungeni juzi.
Zitto alisema bunge halina mamlaka na mawaziri hao isipokuwa wana mamlaka na Waziri Mkuu ambaye kuanzia kesho, watakaa mlango wa Bunge kwa ajili ya kukusanya saini hizo.
"Mawaziri kwa njia moja au nyingine wamekuwa wagumu sana kuwajibika wanampa
kazi rais kuwafukuza. Sisi hatuwezi kuwafukuza, tuna mamlaka na mtu mmoja, Waziri
Mkuu wa Jamhuri; bila kumwajibisha Waziri Mkuu hawa mawaziri waliotajwa hawatatoka.
Na wasipotoka madudu haya yatarudia," alisema. "Mbunge yeyote anayekereka...kuanzia
kesho tunakusanya saini ili Jumatatu tutoe hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu," alisema na kuwataka mawaziri waliotajwa kujipima.
Hata hivyo, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema suala la kumwajibisha Waziri
Mkuu ni lazima lifuate Kanuni za Bunge.
Kuhusu hoja nyingine, Zitto alikubaliana na mapendekezo ya wabunge kuboresha pendekezo
namba saba kwamba Bunge liunde kamati teule kuchunguza mazingira ya ukodishaji wa ndege ya ATCL.
Wajumbe watatu wameteuliwa ambao ni Ester Bulaya, Mustafa Mangungu, Kibona Aidha, kuhusu CHC wamekubaliana kuwa taarifa ya CAG ifanyiwe kazi na kamati.
Zitto pia aliwashauri mawaziri wasiingilie mashirika ya umma. Kuhusu Bodi ya Pamba na majibu aliyoyatoa Waziri Maghembe kwamba anasubiriwa Rais ateue Mwenyekiti, Zitto aliwaonya mawaziri kumsingizia Rais kwa baadhi ya maamuzi yaliyo ndani ya uwezo wao kwa
kuwa wanao uwezo wa kuvunja bodi.
“Tabia ya kumsingizia Rais ikome…” alisema. Alisema tatizo lililopo ni ukosefu wa uwajibikaji
ambalo alisema linapaswa liwekwe katika Katiba mpya. Alisema bila kuhakikisha serikali inawajibika katika hayo, mwaka kesho watarudia.
Awali, juzi na jana, Bunge lilitawaliwa na mjadala mzito wakati wa kujadili taarifa za Kamati za Kudumu za Bunge za Usimamizi wa Fedha za Umma ambazo ziliwasilisha taarifa zake juzi.
Hizo ni Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Mashirika ya Umma (POAC) na Serikali za Mitaa (LAAC).
Wabunge bila kujali itikadi za vyama vyao, walidai wapo baadhi ya mawaziri ambao
‘wanaitafuna’ nchi wakiwatuhumu kwa kuhusika katika ubadhirifu wa fedha za Serikali.
Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe (CCM), alikwenda mbali zaidi akisema ana ushahidi unaoonesha kuwa wengi wa viongozi hao wa wizara ‘wanaitafuna’ nchi.
Tuhuma hizo, zilisababisha Mnadhimu Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni, William Lukuvi kusimama na kutaka ushahidi huo na orodha ya majina ya mawaziri husika viwasilishwe kwa Spika.
Hata hivyo, baadhi ya mawaziri jana walijibu hoja mbalimbali zilizoibuliwa katika taarifa hizo pamoja na michango ya wabunge pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu kuagiza kuanzia sasa kwamba Serikali nayo itakuwa inatoa taarifa za utekelezaji.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Mkuchika alisema wakurugenzi 35 na wakuu wa idara mbalimbali 197 wamechukuliwa hatua kutokana na kuhusika na ubadhirifu wa fedha za umma.
Alisema kati ya hao, wapo waliofikishwa kwenye Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na wengine kufikishwa mahakamani.
Mkuchika aliyekuwa na orodha ya watumishi hao ambayo hata hivyo hakuisoma bungeni
kutokana na muda, aliwaambia wabunge siyo kwamba Serikali haichukui hatua.
Hata hivyo, alisema Baraza la Madiwani linalohusisha pia wabunge, ndilo ndiyo serikali ya wilaya ambalo linapaswa liwe mlinzi namba moja wa mali ya umma.
Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia alisema Takukuru imepelekewa majina ya watu walio nje ya utumishi wa umma walioshiriki katika malipo hewa.
Aidha, walio katika utumishi wa umma, wametakiwa warejeshe fedha.
Zaidi ya Sh milioni 800 zimesharejeshwa na ziko katika akaunti ya Benki Kuu (BoT) kwa
mishahara iliyochukuliwa kama hewa.
Pia wafanyakazi waliostaafu waliendelea kupewa mshahara, walikatwa kwenye pensheni yao.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) akizungumza kwa niaba ya
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alisema Serikali ilikuwa ikitekeleza maagizo ya CAG, lakini tatizo
lilikuwa ni kwamba hapakuwa na utaratibu wa kutoa taarifa.
“Kuanzia sasa Waziri Mkuu amesema kwamba kwa taarifa ya Serikali za Mitaa kwa kuwa inatolewa Machi, watazirudisha taarifa na kuielekeza mikoa kati ya Mei na Julai halmashauri zijibu zote na hatua ziwe zimechukuliwa. Taarifa zote za CAG zijadiliwa na vikao vya RCC.
Zitarudishwa kwenye halmashauri kama hazikujibiwa vizuri,” alisema Lukuvi. Kwa mujibu wa Lukuvi, pamoja na utekelezaji uliokuwa ukifanyika bila kuwa na taarifa kwa umma, safari hii lazima kitabu kichapishwe na wabunge wapate, wajue fedha za wananchi zinatumikaje.
Aidha, Waziri Mkuu ameagiza mashirika yote yaliyotajwa kwenye taarifa za kamati, yahakikishe kwamba ifikapo Septemba mwaka huu ziwe zimejibiwa kwa uhakika ili pia
zichapishwe kwenye kitabu na kiwasilishwe kwa wabunge.
“Mwakani tutakuwa na mapinduzi juu ya taarifa za serikali,” alisema Lukuvi.
Awali, Filikunjombe alisema anayo orodha ya mawaziri wabadhirifu baada ya kuomba Mwongozo wa Naibu Spika, juu ya mchango wa Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami aliyefafanua juu ya sakata la Shirika la ViwangoTanzania (TBS) kwa kusisitiza kuwa Wizara yake haimkingii kifua Mkurugenzi, Charles Ekelege, kama wanavyosema wabunge.
“Waziri anapolidanganya Bunge, achukuliwe hatua gani? Waziri Chami anasema alitekeleza maelekezo yote ya PAC, kwamba uchunguzi unapofanyika Mkurugenzi wa TBS akae pembeni.
Uchunguzi umefanyika Mkurugenzi akiwa kazini…tuna ushahidi wa kutosha, kwamba wanaoongoza ‘kutafuna’ nchi hii ni mawaziri wenyewe na nitataja mmoja mmoja kwa majina na ushahidi tunao,” alisema Filikunjombe.
Waziri Lukuvi alisimama na kusema: “Ningeelewa kama angejenga hoja kuona kama Waziri Chami alidanganya…kuhitimisha kwamba mawaziri wote ni wezi, athibitishe.
Naomba akukabidhi (Naibu Spika) wizi uliofanywa wa kila waziri aliye katika Bunge.”
Hata hivyo, Filikunjombe alisimama tena na kusema ni mawaziri wengi na akasisitiza kutoa
ushahidi.
Dk. Chami katika kuchangia mjadala, alisema ikibainika kuwapo mtu, ndugu au rafiki mwenye kampuni hewa au maslahi binafsi katika ukaguzi wa magari nje ya nchi, ataweka uwaziri wake rehani kwa kujiuzulu.
“Haina maana, nitaamua kumfukuza kazi mteule wa Rais bila kufuata utaratibu? Nimekosea wapi? Kwamba mimi namlinda Mkurugenzi?” Alihoji na kusisitiza kwamba hakuna mtu atakayelindwa au kukingiwa kifua asichunguzwe.
Mbunge wa Singida Magharibi, Tundu Lissu (Chadema), aliwataka wabunge kuanzisha mjadala wa kutokuwa na imani na Serikali.
Alisema kila mwaka taarifa ya CAG imekuwa ikionesha wizi mkubwa uliofanyika, lakini hakuna waziri anayewajibika kwa wizi unaofanyika katika wizara.
“Hatujawahi kuona mtendaji akichukuliwa hatua. Hatujaona Waziri akiwajibika kwa sababu ya wizi katika wizara yake au sababu ya kuhusishwa na uvundo wa wizi wa fedha za umma,” alisema Lisu na kuongeza kuwa wapo wanaotaka ubunge ili wawe mawaziri kwa lengo la kupora.
Hata hivyo, Lisu alisema hoja yake ya kutaka mjadala wa kutokuwa na imani ya Serikali na Waziri Mkuu, si kwamba ana hila na Mizengo Pinda, isipokuwa ni kwa sababu ya mfumo wa utawala uliopo.
“Tuna uwezo kusema Waziri Mkuu wajibika kwa madudu ya Serikali yako,” alisisitiza.
Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed aliwataka wabunge watumie mamlaka waliyopewa na Katiba, kuhakikisha wanawajibisha wasiotaka kuwajibika.
Alisema Katiba inawapa mamlaka ya kutumia asilimia 30 kuishauri Serikali na iliyobaki ni kuidhibiti.
“Asilimia 70 tumeshafanya muda mrefu, sasa tutumie kudhibiti madhambi yasiyopatiwa ufumbuzi,” alisema.
Akizungumzia taarifa ya CAG iliyoonesha kuwapo mishahara hewa iliyolipwa katika baadhi ya vyuo vikuu, Mbunge wa Viti Maalumu, Christowaja Mtinda (Chadema) aliitaka Serikali itoe maelezo ni nani anapokea fedha hizo.
Mtinda ambaye alipinga makatibu wakuu kupewa nyumba Dodoma na kuzitumia kipindi cha mikutano ya Bunge pekee, alisema katika kupitia taarifa za mwaka za Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) alikuta jina lake kwenye orodha ya watumishi wa chuo hicho, licha ya kwamba hajawahi kufanya kazi katika taasisi hiyo.
Mbunge wa Viti Maalumu, Aina Mohamed Mwidau (CUF), aliendelea kuhoji mkataba wa ukodishaji ndege kwa kuhoji Menejimenti ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) iliyokuwapo ilipata wapi kiburi cha kuchukua uamuzi huo wakati timu ya wataalamu ilisema si busara kufanya hivyo.
Mbunge wa Lulindi, Jerome Bwanausi (CCM) alitaka halmashauri zinazotuhumiwa na ubadhirifu wa fedha za umma, wakurugenzi na watendaji wasimamishwe mara moja.
Hata hivyo, Mbunge wa Shinyanga Mjini, Steven Masele (CCM) licha ya kueleza kusikitishwa na ripoti za CAG kutofanyiwa kazi, alisema wapo mawaziri na wakurugenzi wanaofanya kazi nzuri isipokuwa wanaangushwa na Wizara ya Fedha kwa kuwapa fedha kidogo tofauti na bajeti.
Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Aggrey Mwanri, akichangia mjadala alitangaza ‘vita’ kwenye halmashauri na kusema itakapoanza, Serikali haitataka suluhu.
“Tuachieni, msitushike mkono. Tutaandaa vita katika jambo hili ili kutatua tatizo la msingi,”
alisema na kusisitiza kwamba wataingia pia kwenye halmashauri zenye hati safi kuangalia thamani ya fedha na kwamba kwa wenye hati chafu, Katibu Mkuu ameshaagizwa wakurugenzi watendaji wawajibishwe.
Naibu Waziri wa Fedha, Pereira Ame Silima akichangia mjadala, alisema imeundwa timu kwenda halmashauri zote kufuatilia mishahara hewa.
Alikiri kuwepo tatizo hilo na watendaji wanaojihusisha huku akisema baada ya taarifa, hatua zitachukuliwa kwa wahusika.
Chanzo: HabariLeo
Mbunge wa Kigoma Kaskazini ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mashirika ya Umma (POAC), alitoa hoja hiyo jana usiku wakati akihitimisha hoja ya taarifa ya Kamati yake aliyoiwasilisha bungeni juzi.
Zitto alisema bunge halina mamlaka na mawaziri hao isipokuwa wana mamlaka na Waziri Mkuu ambaye kuanzia kesho, watakaa mlango wa Bunge kwa ajili ya kukusanya saini hizo.
"Mawaziri kwa njia moja au nyingine wamekuwa wagumu sana kuwajibika wanampa
kazi rais kuwafukuza. Sisi hatuwezi kuwafukuza, tuna mamlaka na mtu mmoja, Waziri
Mkuu wa Jamhuri; bila kumwajibisha Waziri Mkuu hawa mawaziri waliotajwa hawatatoka.
Na wasipotoka madudu haya yatarudia," alisema. "Mbunge yeyote anayekereka...kuanzia
kesho tunakusanya saini ili Jumatatu tutoe hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu," alisema na kuwataka mawaziri waliotajwa kujipima.
Hata hivyo, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema suala la kumwajibisha Waziri
Mkuu ni lazima lifuate Kanuni za Bunge.
Kuhusu hoja nyingine, Zitto alikubaliana na mapendekezo ya wabunge kuboresha pendekezo
namba saba kwamba Bunge liunde kamati teule kuchunguza mazingira ya ukodishaji wa ndege ya ATCL.
Wajumbe watatu wameteuliwa ambao ni Ester Bulaya, Mustafa Mangungu, Kibona Aidha, kuhusu CHC wamekubaliana kuwa taarifa ya CAG ifanyiwe kazi na kamati.
Zitto pia aliwashauri mawaziri wasiingilie mashirika ya umma. Kuhusu Bodi ya Pamba na majibu aliyoyatoa Waziri Maghembe kwamba anasubiriwa Rais ateue Mwenyekiti, Zitto aliwaonya mawaziri kumsingizia Rais kwa baadhi ya maamuzi yaliyo ndani ya uwezo wao kwa
kuwa wanao uwezo wa kuvunja bodi.
“Tabia ya kumsingizia Rais ikome…” alisema. Alisema tatizo lililopo ni ukosefu wa uwajibikaji
ambalo alisema linapaswa liwekwe katika Katiba mpya. Alisema bila kuhakikisha serikali inawajibika katika hayo, mwaka kesho watarudia.
Awali, juzi na jana, Bunge lilitawaliwa na mjadala mzito wakati wa kujadili taarifa za Kamati za Kudumu za Bunge za Usimamizi wa Fedha za Umma ambazo ziliwasilisha taarifa zake juzi.
Hizo ni Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Mashirika ya Umma (POAC) na Serikali za Mitaa (LAAC).
Wabunge bila kujali itikadi za vyama vyao, walidai wapo baadhi ya mawaziri ambao
‘wanaitafuna’ nchi wakiwatuhumu kwa kuhusika katika ubadhirifu wa fedha za Serikali.
Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe (CCM), alikwenda mbali zaidi akisema ana ushahidi unaoonesha kuwa wengi wa viongozi hao wa wizara ‘wanaitafuna’ nchi.
Tuhuma hizo, zilisababisha Mnadhimu Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni, William Lukuvi kusimama na kutaka ushahidi huo na orodha ya majina ya mawaziri husika viwasilishwe kwa Spika.
Hata hivyo, baadhi ya mawaziri jana walijibu hoja mbalimbali zilizoibuliwa katika taarifa hizo pamoja na michango ya wabunge pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu kuagiza kuanzia sasa kwamba Serikali nayo itakuwa inatoa taarifa za utekelezaji.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Mkuchika alisema wakurugenzi 35 na wakuu wa idara mbalimbali 197 wamechukuliwa hatua kutokana na kuhusika na ubadhirifu wa fedha za umma.
Alisema kati ya hao, wapo waliofikishwa kwenye Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na wengine kufikishwa mahakamani.
Mkuchika aliyekuwa na orodha ya watumishi hao ambayo hata hivyo hakuisoma bungeni
kutokana na muda, aliwaambia wabunge siyo kwamba Serikali haichukui hatua.
Hata hivyo, alisema Baraza la Madiwani linalohusisha pia wabunge, ndilo ndiyo serikali ya wilaya ambalo linapaswa liwe mlinzi namba moja wa mali ya umma.
Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia alisema Takukuru imepelekewa majina ya watu walio nje ya utumishi wa umma walioshiriki katika malipo hewa.
Aidha, walio katika utumishi wa umma, wametakiwa warejeshe fedha.
Zaidi ya Sh milioni 800 zimesharejeshwa na ziko katika akaunti ya Benki Kuu (BoT) kwa
mishahara iliyochukuliwa kama hewa.
Pia wafanyakazi waliostaafu waliendelea kupewa mshahara, walikatwa kwenye pensheni yao.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) akizungumza kwa niaba ya
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alisema Serikali ilikuwa ikitekeleza maagizo ya CAG, lakini tatizo
lilikuwa ni kwamba hapakuwa na utaratibu wa kutoa taarifa.
“Kuanzia sasa Waziri Mkuu amesema kwamba kwa taarifa ya Serikali za Mitaa kwa kuwa inatolewa Machi, watazirudisha taarifa na kuielekeza mikoa kati ya Mei na Julai halmashauri zijibu zote na hatua ziwe zimechukuliwa. Taarifa zote za CAG zijadiliwa na vikao vya RCC.
Zitarudishwa kwenye halmashauri kama hazikujibiwa vizuri,” alisema Lukuvi. Kwa mujibu wa Lukuvi, pamoja na utekelezaji uliokuwa ukifanyika bila kuwa na taarifa kwa umma, safari hii lazima kitabu kichapishwe na wabunge wapate, wajue fedha za wananchi zinatumikaje.
Aidha, Waziri Mkuu ameagiza mashirika yote yaliyotajwa kwenye taarifa za kamati, yahakikishe kwamba ifikapo Septemba mwaka huu ziwe zimejibiwa kwa uhakika ili pia
zichapishwe kwenye kitabu na kiwasilishwe kwa wabunge.
“Mwakani tutakuwa na mapinduzi juu ya taarifa za serikali,” alisema Lukuvi.
Awali, Filikunjombe alisema anayo orodha ya mawaziri wabadhirifu baada ya kuomba Mwongozo wa Naibu Spika, juu ya mchango wa Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami aliyefafanua juu ya sakata la Shirika la ViwangoTanzania (TBS) kwa kusisitiza kuwa Wizara yake haimkingii kifua Mkurugenzi, Charles Ekelege, kama wanavyosema wabunge.
“Waziri anapolidanganya Bunge, achukuliwe hatua gani? Waziri Chami anasema alitekeleza maelekezo yote ya PAC, kwamba uchunguzi unapofanyika Mkurugenzi wa TBS akae pembeni.
Uchunguzi umefanyika Mkurugenzi akiwa kazini…tuna ushahidi wa kutosha, kwamba wanaoongoza ‘kutafuna’ nchi hii ni mawaziri wenyewe na nitataja mmoja mmoja kwa majina na ushahidi tunao,” alisema Filikunjombe.
Waziri Lukuvi alisimama na kusema: “Ningeelewa kama angejenga hoja kuona kama Waziri Chami alidanganya…kuhitimisha kwamba mawaziri wote ni wezi, athibitishe.
Naomba akukabidhi (Naibu Spika) wizi uliofanywa wa kila waziri aliye katika Bunge.”
Hata hivyo, Filikunjombe alisimama tena na kusema ni mawaziri wengi na akasisitiza kutoa
ushahidi.
Dk. Chami katika kuchangia mjadala, alisema ikibainika kuwapo mtu, ndugu au rafiki mwenye kampuni hewa au maslahi binafsi katika ukaguzi wa magari nje ya nchi, ataweka uwaziri wake rehani kwa kujiuzulu.
“Haina maana, nitaamua kumfukuza kazi mteule wa Rais bila kufuata utaratibu? Nimekosea wapi? Kwamba mimi namlinda Mkurugenzi?” Alihoji na kusisitiza kwamba hakuna mtu atakayelindwa au kukingiwa kifua asichunguzwe.
Mbunge wa Singida Magharibi, Tundu Lissu (Chadema), aliwataka wabunge kuanzisha mjadala wa kutokuwa na imani na Serikali.
Alisema kila mwaka taarifa ya CAG imekuwa ikionesha wizi mkubwa uliofanyika, lakini hakuna waziri anayewajibika kwa wizi unaofanyika katika wizara.
“Hatujawahi kuona mtendaji akichukuliwa hatua. Hatujaona Waziri akiwajibika kwa sababu ya wizi katika wizara yake au sababu ya kuhusishwa na uvundo wa wizi wa fedha za umma,” alisema Lisu na kuongeza kuwa wapo wanaotaka ubunge ili wawe mawaziri kwa lengo la kupora.
Hata hivyo, Lisu alisema hoja yake ya kutaka mjadala wa kutokuwa na imani ya Serikali na Waziri Mkuu, si kwamba ana hila na Mizengo Pinda, isipokuwa ni kwa sababu ya mfumo wa utawala uliopo.
“Tuna uwezo kusema Waziri Mkuu wajibika kwa madudu ya Serikali yako,” alisisitiza.
Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed aliwataka wabunge watumie mamlaka waliyopewa na Katiba, kuhakikisha wanawajibisha wasiotaka kuwajibika.
Alisema Katiba inawapa mamlaka ya kutumia asilimia 30 kuishauri Serikali na iliyobaki ni kuidhibiti.
“Asilimia 70 tumeshafanya muda mrefu, sasa tutumie kudhibiti madhambi yasiyopatiwa ufumbuzi,” alisema.
Akizungumzia taarifa ya CAG iliyoonesha kuwapo mishahara hewa iliyolipwa katika baadhi ya vyuo vikuu, Mbunge wa Viti Maalumu, Christowaja Mtinda (Chadema) aliitaka Serikali itoe maelezo ni nani anapokea fedha hizo.
Mtinda ambaye alipinga makatibu wakuu kupewa nyumba Dodoma na kuzitumia kipindi cha mikutano ya Bunge pekee, alisema katika kupitia taarifa za mwaka za Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) alikuta jina lake kwenye orodha ya watumishi wa chuo hicho, licha ya kwamba hajawahi kufanya kazi katika taasisi hiyo.
Mbunge wa Viti Maalumu, Aina Mohamed Mwidau (CUF), aliendelea kuhoji mkataba wa ukodishaji ndege kwa kuhoji Menejimenti ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) iliyokuwapo ilipata wapi kiburi cha kuchukua uamuzi huo wakati timu ya wataalamu ilisema si busara kufanya hivyo.
Mbunge wa Lulindi, Jerome Bwanausi (CCM) alitaka halmashauri zinazotuhumiwa na ubadhirifu wa fedha za umma, wakurugenzi na watendaji wasimamishwe mara moja.
Hata hivyo, Mbunge wa Shinyanga Mjini, Steven Masele (CCM) licha ya kueleza kusikitishwa na ripoti za CAG kutofanyiwa kazi, alisema wapo mawaziri na wakurugenzi wanaofanya kazi nzuri isipokuwa wanaangushwa na Wizara ya Fedha kwa kuwapa fedha kidogo tofauti na bajeti.
Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Aggrey Mwanri, akichangia mjadala alitangaza ‘vita’ kwenye halmashauri na kusema itakapoanza, Serikali haitataka suluhu.
“Tuachieni, msitushike mkono. Tutaandaa vita katika jambo hili ili kutatua tatizo la msingi,”
alisema na kusisitiza kwamba wataingia pia kwenye halmashauri zenye hati safi kuangalia thamani ya fedha na kwamba kwa wenye hati chafu, Katibu Mkuu ameshaagizwa wakurugenzi watendaji wawajibishwe.
Naibu Waziri wa Fedha, Pereira Ame Silima akichangia mjadala, alisema imeundwa timu kwenda halmashauri zote kufuatilia mishahara hewa.
Alikiri kuwepo tatizo hilo na watendaji wanaojihusisha huku akisema baada ya taarifa, hatua zitachukuliwa kwa wahusika.
Chanzo: HabariLeo
Sunday, April 15, 2012
Msani Lulu atendewe haki na haki ionekane inatendeka
Lula wa Ndali Mwananzela
Msiba wa Msanii maarufu zaidi wa filamu Tanzania Stephen Kanumba umekuja na kutuachia mshtuko kupita kiasi. Kutokea kwake katikati ya Ijumaa Kuu na Pasaka kwa kweli umefanya sikuu ya Pasaka (yenye kuadhimisha ufufuko) kuwa na maana ya pekee kwa baadhi yetu. Sisi wengine tayari tulikuwa tunaomboleza kuondokewa kwa aliyekuwa Inspekta Generali wa Polisi Mzee Harun G. Mahundi hatukutarajia mioyo yetu kuchomwa na msiba mwingine ndani ya muda huo. Lakini Mungu ni Mungu kwani nina uhakika wapo watu wengine wengi tu ambao walikuwa kwenye misiba mingine wakati huo huo na msiba wa Kanumba ukaja kama kidonda kingine.
Kilichoshtua wengi zaidi na hasa tuliopata habari mapema zaidi ni nini kilitokea. Taarifa za mwanzo kama ilivyotarajiwa zilikuwa na utata sana maana wengine walianza kusema ilikuwa ni ajali ya gari huko Mbagala wakati wengine wakitaja vyanzo mbalimbali. Lakini baada ya muda taarifa zikawa wazi zaidi kwamba kifo cha Kanumba kimesababishwa kwa namna moja au nyingine katika mazingira ya ugomvi wa kwenye nyumba (domestic conflict) ambao matokeo yake ni mmoja kufariki. Na kilichokuwa wazi mapema hiyo ni kuwa msanii mwingine maarufu Elizabeth Michael a.k.a Lulu alikuwa anahusika.
Mara moja hata hivyo baadhi ya watu walianza kueneza habari kuwa “Lulu kamuua Kanumba” na wengine kwenda mbali na kumuita “muuaji”. Niliwasoma wengine wakielezea kifo cha Kanumba kama “mauaji” bila ya shaka wengine wakishindwa kujua kuwa baadhi ya lugha wanayotumia ina maana ya kisheria zaidi. Kwamba Kanumba ametutoka hilo halina ubishi lakini ni mazingira gani yalisababisha hilo hilo ni suala la kitaalamu na la kisheria. Hapa ndio hoja ya Lulu kutendewa haki inapokuja kwa sababu tusipoangalia kutokana na maumivu tuliyonayo ya kupotelewa na mtu tuliyempenda mno basi tunapoteza macho yetu ya haki na tunajenda macho ya kisasi ambayo hayataki kuutafuta wala kuujali ukweli.
Niwashirikishe maneno yenye hisia hizo yaliyoandikwa na mmoja wa wanaForum wa JamiiForums.com akijaribu kuturudisha kwenye fikra za kujali haki bila kumuangalia nani atanufaika na haki hiyo. Yaani, badala ya kuangalia ni “Lulu” anahusika basi tumweke huyo “Lulu” kama ni mdogo wetu, binti yetu, rafiki yetu n.k na amefanya kitu ambacho pia kimemsababishia mauti ndugu, rafiki au jamaa yetu mwingine; je tungependa atendewe vipi? Ni wazi wengi tungependa atendewe haki; asionewe, asidhulumiwe au kupendelewa. Yaani, isije kuwa watu ambao walikuwa na chuki na Lulu kabla ya tukio hili ndio wanakuwa wa kwanza kupiga debe la “muuaji muuaji” kumbe wanathibitisha tu midomoni mwao kile wanachokiamini moyoni kutokana na chuki.
Mwanachama huyo aitwaye WomanofSubstance aliandika hivi katika mtandao huo na nimebandika hapa ili kutupa fikra na sisi wengine:
Naanza na kutoa Pole kwa watanzania wote, hasa ndugu jamaa na marafiki wa karibu wa Kanumba The Great (R.I.P) kabla sijatoa mchango wangu kuhusu hili jambo zito na nyeti ambalo limetawala maongezi katika kipindi hiki cha Sikukuu ya Pasaka. Mengi yamesemwa na pia kuna mengi pia hayajasemwa, moja wapo likiwa "ujinai" wa Lulu katika kifo cha Kanumba.
Katika mukatadha wa sheria, tunaona kwamba Tanzania ni moja ya nchi zenye kuuweka uwajibikaji kijinai kuwa chini ya UMRI wa miaka 18 kwa kuweka miaka 10 kama umri ambapo mtu anaweza kushtakiwa kwa kosa la jinai. (Linganisha na Kenya miaka 8, Zimbabwe -7,Zambia 8,Africa Kusini 10) n.k. Ina maana kwamba mtu (mtoto) aliye chini ya umri huu hawezi kushtakiwa labda ithibitishwe kuwa alikua anajua kabisa anachokifanya. Lulu hafit kwenye kundi hili hata kama ana umri wa miaka 17 kama ambavyo Mh Halima Mdee ame tweet leo baada ya kumtembelea LuLU Oysterbay Polisi.
Tukiacha sheria na matakwa yake, kwa kuzingatia yale yanayosemwa kuhusu mkasa huu wa kifo cha Kanumba (R.I.P), inatupasa tuone kuwa kila hadithi ina pande mbili. Hadithi ya Kanumba ambaye kwa sasa hayupo kuelezea, na hadithi ya Lulu aliye mahabusu. Inasikitisha sana kwamba kifo kimetokea katika mazingira ya kutatanisha. Kifo hiki kimesikitisha watu wengi na kufanya udadisi wa kutaka kujua ukweli ulio objective iwe vigumu. Watu wamebakia kushusha lawama ZOTE kwa Lulu tu bila kutaka kujua haswa ilitokea nini hadi kifo hicho kikatokea.
Endelea kusoma habari hii..............
Msiba wa Msanii maarufu zaidi wa filamu Tanzania Stephen Kanumba umekuja na kutuachia mshtuko kupita kiasi. Kutokea kwake katikati ya Ijumaa Kuu na Pasaka kwa kweli umefanya sikuu ya Pasaka (yenye kuadhimisha ufufuko) kuwa na maana ya pekee kwa baadhi yetu. Sisi wengine tayari tulikuwa tunaomboleza kuondokewa kwa aliyekuwa Inspekta Generali wa Polisi Mzee Harun G. Mahundi hatukutarajia mioyo yetu kuchomwa na msiba mwingine ndani ya muda huo. Lakini Mungu ni Mungu kwani nina uhakika wapo watu wengine wengi tu ambao walikuwa kwenye misiba mingine wakati huo huo na msiba wa Kanumba ukaja kama kidonda kingine.
Kilichoshtua wengi zaidi na hasa tuliopata habari mapema zaidi ni nini kilitokea. Taarifa za mwanzo kama ilivyotarajiwa zilikuwa na utata sana maana wengine walianza kusema ilikuwa ni ajali ya gari huko Mbagala wakati wengine wakitaja vyanzo mbalimbali. Lakini baada ya muda taarifa zikawa wazi zaidi kwamba kifo cha Kanumba kimesababishwa kwa namna moja au nyingine katika mazingira ya ugomvi wa kwenye nyumba (domestic conflict) ambao matokeo yake ni mmoja kufariki. Na kilichokuwa wazi mapema hiyo ni kuwa msanii mwingine maarufu Elizabeth Michael a.k.a Lulu alikuwa anahusika.
Mara moja hata hivyo baadhi ya watu walianza kueneza habari kuwa “Lulu kamuua Kanumba” na wengine kwenda mbali na kumuita “muuaji”. Niliwasoma wengine wakielezea kifo cha Kanumba kama “mauaji” bila ya shaka wengine wakishindwa kujua kuwa baadhi ya lugha wanayotumia ina maana ya kisheria zaidi. Kwamba Kanumba ametutoka hilo halina ubishi lakini ni mazingira gani yalisababisha hilo hilo ni suala la kitaalamu na la kisheria. Hapa ndio hoja ya Lulu kutendewa haki inapokuja kwa sababu tusipoangalia kutokana na maumivu tuliyonayo ya kupotelewa na mtu tuliyempenda mno basi tunapoteza macho yetu ya haki na tunajenda macho ya kisasi ambayo hayataki kuutafuta wala kuujali ukweli.
Niwashirikishe maneno yenye hisia hizo yaliyoandikwa na mmoja wa wanaForum wa JamiiForums.com akijaribu kuturudisha kwenye fikra za kujali haki bila kumuangalia nani atanufaika na haki hiyo. Yaani, badala ya kuangalia ni “Lulu” anahusika basi tumweke huyo “Lulu” kama ni mdogo wetu, binti yetu, rafiki yetu n.k na amefanya kitu ambacho pia kimemsababishia mauti ndugu, rafiki au jamaa yetu mwingine; je tungependa atendewe vipi? Ni wazi wengi tungependa atendewe haki; asionewe, asidhulumiwe au kupendelewa. Yaani, isije kuwa watu ambao walikuwa na chuki na Lulu kabla ya tukio hili ndio wanakuwa wa kwanza kupiga debe la “muuaji muuaji” kumbe wanathibitisha tu midomoni mwao kile wanachokiamini moyoni kutokana na chuki.
Mwanachama huyo aitwaye WomanofSubstance aliandika hivi katika mtandao huo na nimebandika hapa ili kutupa fikra na sisi wengine:
Naanza na kutoa Pole kwa watanzania wote, hasa ndugu jamaa na marafiki wa karibu wa Kanumba The Great (R.I.P) kabla sijatoa mchango wangu kuhusu hili jambo zito na nyeti ambalo limetawala maongezi katika kipindi hiki cha Sikukuu ya Pasaka. Mengi yamesemwa na pia kuna mengi pia hayajasemwa, moja wapo likiwa "ujinai" wa Lulu katika kifo cha Kanumba.
Katika mukatadha wa sheria, tunaona kwamba Tanzania ni moja ya nchi zenye kuuweka uwajibikaji kijinai kuwa chini ya UMRI wa miaka 18 kwa kuweka miaka 10 kama umri ambapo mtu anaweza kushtakiwa kwa kosa la jinai. (Linganisha na Kenya miaka 8, Zimbabwe -7,Zambia 8,Africa Kusini 10) n.k. Ina maana kwamba mtu (mtoto) aliye chini ya umri huu hawezi kushtakiwa labda ithibitishwe kuwa alikua anajua kabisa anachokifanya. Lulu hafit kwenye kundi hili hata kama ana umri wa miaka 17 kama ambavyo Mh Halima Mdee ame tweet leo baada ya kumtembelea LuLU Oysterbay Polisi.
Tukiacha sheria na matakwa yake, kwa kuzingatia yale yanayosemwa kuhusu mkasa huu wa kifo cha Kanumba (R.I.P), inatupasa tuone kuwa kila hadithi ina pande mbili. Hadithi ya Kanumba ambaye kwa sasa hayupo kuelezea, na hadithi ya Lulu aliye mahabusu. Inasikitisha sana kwamba kifo kimetokea katika mazingira ya kutatanisha. Kifo hiki kimesikitisha watu wengi na kufanya udadisi wa kutaka kujua ukweli ulio objective iwe vigumu. Watu wamebakia kushusha lawama ZOTE kwa Lulu tu bila kutaka kujua haswa ilitokea nini hadi kifo hicho kikatokea.
Endelea kusoma habari hii..............
Saturday, April 14, 2012
Mkapa awa mbogo
RAIS mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa jana alijikuta katika
wakati mgumu baada ya kubanwa na wasomi waliokosoa hadharani sera zake
za ubinafsishaji kwa maelezo kwamba hazijaonesha mafanikio, badala yake
zimechangia kudorora kwa uchumi wa nchi.
Sakata la Mkapa na wasomi hao lilibuka jana katika Kongamano la Kigoda cha Mwalimu Nyerere lililofanyika kwenye ukumbi wa Nkrumah katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuibua msisimko wa aina yake kwa watu waliohudhuria.
Katika mjadala huo uliochukua takribani saa mbili, washiriki hao wengi wao wakiwa wasomi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), walihoji sababu za Rais huyo mstaafu kupigia debe sera zake za uwekezaji kwamba zingekuwa suluhisho lakini hadi sasa hali ya uchumi wan chi imezidi kudorora.
Hata hivyo, Mkapa alipinga vikali hoja za wasomi hao na kuwahoji akitaka wamtajie, tangu mwaka 2005 alipoondoka madarakani, ni viwanda vingapi vipya vimejengwa?
'Mnanilaumu kwa sera ya ubinafsishaji lakini niambieni viwanda vingapi vipya vimejengwa tangu mwaka 2005?" Alihoji Mkapa ambaye aliongoza Tanzania kuanzia mwaka 1995 hadi 2005.
Mkapa alitetea sera za ubinafsishaji na kueleza kwamba kimsingi hazikushindwa lakini zimeonekana kuwa na kasoro kwenye utekelezaji wake kutokana na matatizo ya uongozi na kwamba aliamua kubinafsisha baadhi ya vitega uchumi kwani vilifilisika.
“Ili uendesha kiwanda unahitaji mitaji, uongozi bora na soko pamoja na ujuzi, sisi tulibinafisha baada ya kukosa mitaji na uwezo wa kuviendesha, tulishindwa kuviendesha, tulikuwa na viwanda vitano vya nguo… vyote vilikwenda hovyo hovyo,”alisema Mkapa.
Aliilaumu mamlaka iliyohusika na uwekezaji wakati wa utawala wake, kwa kile alichodai, kushindwa kuueleza umma ukweli uliosababisha Serikali yake kuchukua uamuzi wa kubinafisha mashirika na viwanda mbalimbali.
“Tulibinafsisha mashirika na viwanda 330, kati yake 180 walikabidhiwa Watanzania na 23 wageni, vilivyobaki vilimilikiwa kwa ubia kati ya Watanzania na wageni, kwanini watu hawahoji sababu za hata wenyeji kushindwa kuviendeleza? Twende tufanye utafiti tupate sababu za kushindwa,”alisizitiza Mkapa.
Aliongeza kuwa mbali ya kuwapo matatizo katika sekta ya uchumi wa nchi, baadhi ya viwanda vilivyobinafisishwa vinafanya vizuri huku akitolea mfano kile cha Sukari cha Kilombero mkoani Morogoro.
Mkapa alitoa wito kwa watanzania kujituma kwa bidii kutafuata maendelea badala ya kuendelea kujadili masuala yasiyo na tija kwa maendeleo ya taifa.
Akizungumza kwenye mjadala huo, Profesa Issa Shivji, alisema ubinafsishaji uliofanywa nchini uliuza njia kuu za uchumi zikiwemo benki na Shirika la Bima na kuifanya Serikali kushindwa kusimamia na kulinda uchumi wa nchi.
Shivji alitofautiana na mtazamo wa Mkapa aliyedai kuwa ubinafishaji ulifanywa kwenye viwanda vilivyoshindwa kujiendesha kwa kukosa mitaji akisema:
“Viwanda tulivyobinafisha ni vile vilivyokuwa vinatoa faida, tatizo tulilofanya tulibinafisha njia kuu zote za uchumi hali iliyosababisha Serikali kushindwa kusimamia uchumi wa nchi.”
Msomi huyo alibainisha kuwa hata nchi zilizoendelea, ikiwamo China, ziko kwenye ubinafishaji lakini zinatenga maeneo ya kubinafisha.
Kwa upande wake Dk Ng'wanza Kamata ambaye ndiye aliyechokoza mada katika mdahalo huo, alihoji kama Afrika inaweza kutimiza ndoto ya kuwa kitovu cha uchumi duniani kwa kutumia sera na mfumo uliopo ambao unatoka mataifa ya Ulaya.
“Katika hotuba yako uliyoitoa Afrika ya Kusini umesema Afrika inaweza kuwa kitovu cha uchumi wa dunia kutokana na wingi wa raslimali zilipo, je ni kweli tunaweza kufika huko kwa kutumia mifumo na sera zilizopo? Alihoji Dk Kamata na kuongeza:
“Wazungu wanajua kuwa Afrika ina utajiri wa rasilimali tangu mkutano wa Berlin”.
Dk Kamata alisema mfumo wa utandawazi unaonekana kama umejileta wenyewe ambao ndani yake watu wa Ulaya wanatafuta mahali pa kupeleka mitaji yao ili waweze kupata faida.
“Zipo kampuni 600 zinazoshika uchumi wa dunia, lengo lao siyo kusadia wananchi katika nchi husika bali kutengeneza faida kwa maslahi yao,”alisema.
Kuhusu udhaifu wa Serikali wadau hao walisema mikakati mingi ya maendeleo inashindwa kutekelezeka kutokana na tatizo la viongozi kutowashirikisha wananchi katika kuandaa miradi ya maendeleo.
“Kama viongozi serikalini wangewashirikisha wananchi katika kujadili miradi ya maendeleo mikakati mingi ingefanikiwa,”alisema Maselina Charles kutoka Morogoro.
Historia ya ubinafsishaji
Ubinafsishaji wa Mashirika ya umma hapa nchini ulianza tangu mwaka 1993 na ulikuwa unaratibiwa na Tume ya Rais ya Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC) iliyopewa mamlaka ya kusimamia
na kuongoza shughuli zote za ubinafsishaji.
Hata hivyo shughuli za tume hiyo zilisitishwa Desemba 2007 baada ya kukamilisha ubinafsishaji wa mashirika mengi ambayo yalikuwa yametengwa.
Mashirika ya Umma 34 ambayo yalikuwa kwenye hatua za ubinafsishwaji yalihamishiwa katika Shirika Hodhi la Mali za Makampuni yaliyobinafsishwa kutoka PSRC kuanzia kuanzia Januari 2008.
Januari 2008 Shirika Hodhi la Mali za
Makampuni Yaliyobinafsishwa lilipewa majukumu ya kuendesha shughuli za kampuni zilizokuwa kwenye makakati wa kubinafsishwa.
Matatizo kwenye Ubinafsishaji
Kwa mujibu wa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (SAG)mashirika yaliyotengwa kawa ajili ya kubinafsishwa, yalikuwa yamezuiwa kupanuka zaidi kwa sababu hayawezi kuandaa na kutekeleza mipango mikakati au kuwekeza.
Pia wafanyakazi wa mashirika hayo wanakuwa hawana morali wa kufanya kazi au kutimiza wajibu wao kwa sababu ya kutokujua hatima ya ajira yao na ya mwajiri wao.
Uchakavu wa mali na raslimali za mashirika yaliyotengwa unakuwa ni wa kiasi cha juu kutokana na kukosa fedha kwa ajili ya ukarabati au urudishwaji wa mali zilizoharibika unakuwa mgumu.
Chanzo: Mwananchi
Sakata la Mkapa na wasomi hao lilibuka jana katika Kongamano la Kigoda cha Mwalimu Nyerere lililofanyika kwenye ukumbi wa Nkrumah katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuibua msisimko wa aina yake kwa watu waliohudhuria.
Katika mjadala huo uliochukua takribani saa mbili, washiriki hao wengi wao wakiwa wasomi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), walihoji sababu za Rais huyo mstaafu kupigia debe sera zake za uwekezaji kwamba zingekuwa suluhisho lakini hadi sasa hali ya uchumi wan chi imezidi kudorora.
Hata hivyo, Mkapa alipinga vikali hoja za wasomi hao na kuwahoji akitaka wamtajie, tangu mwaka 2005 alipoondoka madarakani, ni viwanda vingapi vipya vimejengwa?
'Mnanilaumu kwa sera ya ubinafsishaji lakini niambieni viwanda vingapi vipya vimejengwa tangu mwaka 2005?" Alihoji Mkapa ambaye aliongoza Tanzania kuanzia mwaka 1995 hadi 2005.
Mkapa alitetea sera za ubinafsishaji na kueleza kwamba kimsingi hazikushindwa lakini zimeonekana kuwa na kasoro kwenye utekelezaji wake kutokana na matatizo ya uongozi na kwamba aliamua kubinafsisha baadhi ya vitega uchumi kwani vilifilisika.
“Ili uendesha kiwanda unahitaji mitaji, uongozi bora na soko pamoja na ujuzi, sisi tulibinafisha baada ya kukosa mitaji na uwezo wa kuviendesha, tulishindwa kuviendesha, tulikuwa na viwanda vitano vya nguo… vyote vilikwenda hovyo hovyo,”alisema Mkapa.
Aliilaumu mamlaka iliyohusika na uwekezaji wakati wa utawala wake, kwa kile alichodai, kushindwa kuueleza umma ukweli uliosababisha Serikali yake kuchukua uamuzi wa kubinafisha mashirika na viwanda mbalimbali.
“Tulibinafsisha mashirika na viwanda 330, kati yake 180 walikabidhiwa Watanzania na 23 wageni, vilivyobaki vilimilikiwa kwa ubia kati ya Watanzania na wageni, kwanini watu hawahoji sababu za hata wenyeji kushindwa kuviendeleza? Twende tufanye utafiti tupate sababu za kushindwa,”alisizitiza Mkapa.
Aliongeza kuwa mbali ya kuwapo matatizo katika sekta ya uchumi wa nchi, baadhi ya viwanda vilivyobinafisishwa vinafanya vizuri huku akitolea mfano kile cha Sukari cha Kilombero mkoani Morogoro.
Mkapa alitoa wito kwa watanzania kujituma kwa bidii kutafuata maendelea badala ya kuendelea kujadili masuala yasiyo na tija kwa maendeleo ya taifa.
Akizungumza kwenye mjadala huo, Profesa Issa Shivji, alisema ubinafsishaji uliofanywa nchini uliuza njia kuu za uchumi zikiwemo benki na Shirika la Bima na kuifanya Serikali kushindwa kusimamia na kulinda uchumi wa nchi.
Shivji alitofautiana na mtazamo wa Mkapa aliyedai kuwa ubinafishaji ulifanywa kwenye viwanda vilivyoshindwa kujiendesha kwa kukosa mitaji akisema:
“Viwanda tulivyobinafisha ni vile vilivyokuwa vinatoa faida, tatizo tulilofanya tulibinafisha njia kuu zote za uchumi hali iliyosababisha Serikali kushindwa kusimamia uchumi wa nchi.”
Msomi huyo alibainisha kuwa hata nchi zilizoendelea, ikiwamo China, ziko kwenye ubinafishaji lakini zinatenga maeneo ya kubinafisha.
Kwa upande wake Dk Ng'wanza Kamata ambaye ndiye aliyechokoza mada katika mdahalo huo, alihoji kama Afrika inaweza kutimiza ndoto ya kuwa kitovu cha uchumi duniani kwa kutumia sera na mfumo uliopo ambao unatoka mataifa ya Ulaya.
“Katika hotuba yako uliyoitoa Afrika ya Kusini umesema Afrika inaweza kuwa kitovu cha uchumi wa dunia kutokana na wingi wa raslimali zilipo, je ni kweli tunaweza kufika huko kwa kutumia mifumo na sera zilizopo? Alihoji Dk Kamata na kuongeza:
“Wazungu wanajua kuwa Afrika ina utajiri wa rasilimali tangu mkutano wa Berlin”.
Dk Kamata alisema mfumo wa utandawazi unaonekana kama umejileta wenyewe ambao ndani yake watu wa Ulaya wanatafuta mahali pa kupeleka mitaji yao ili waweze kupata faida.
“Zipo kampuni 600 zinazoshika uchumi wa dunia, lengo lao siyo kusadia wananchi katika nchi husika bali kutengeneza faida kwa maslahi yao,”alisema.
Kuhusu udhaifu wa Serikali wadau hao walisema mikakati mingi ya maendeleo inashindwa kutekelezeka kutokana na tatizo la viongozi kutowashirikisha wananchi katika kuandaa miradi ya maendeleo.
“Kama viongozi serikalini wangewashirikisha wananchi katika kujadili miradi ya maendeleo mikakati mingi ingefanikiwa,”alisema Maselina Charles kutoka Morogoro.
Historia ya ubinafsishaji
Ubinafsishaji wa Mashirika ya umma hapa nchini ulianza tangu mwaka 1993 na ulikuwa unaratibiwa na Tume ya Rais ya Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC) iliyopewa mamlaka ya kusimamia
na kuongoza shughuli zote za ubinafsishaji.
Hata hivyo shughuli za tume hiyo zilisitishwa Desemba 2007 baada ya kukamilisha ubinafsishaji wa mashirika mengi ambayo yalikuwa yametengwa.
Mashirika ya Umma 34 ambayo yalikuwa kwenye hatua za ubinafsishwaji yalihamishiwa katika Shirika Hodhi la Mali za Makampuni yaliyobinafsishwa kutoka PSRC kuanzia kuanzia Januari 2008.
Januari 2008 Shirika Hodhi la Mali za
Makampuni Yaliyobinafsishwa lilipewa majukumu ya kuendesha shughuli za kampuni zilizokuwa kwenye makakati wa kubinafsishwa.
Matatizo kwenye Ubinafsishaji
Kwa mujibu wa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (SAG)mashirika yaliyotengwa kawa ajili ya kubinafsishwa, yalikuwa yamezuiwa kupanuka zaidi kwa sababu hayawezi kuandaa na kutekeleza mipango mikakati au kuwekeza.
Pia wafanyakazi wa mashirika hayo wanakuwa hawana morali wa kufanya kazi au kutimiza wajibu wao kwa sababu ya kutokujua hatima ya ajira yao na ya mwajiri wao.
Uchakavu wa mali na raslimali za mashirika yaliyotengwa unakuwa ni wa kiasi cha juu kutokana na kukosa fedha kwa ajili ya ukarabati au urudishwaji wa mali zilizoharibika unakuwa mgumu.
Chanzo: Mwananchi
Tuesday, April 10, 2012
Mamia wamzika Steven Kanumba Tanzania
Mazishi ya aliyekuwa msanii maarufu wa filamu nchini
Tanzania Steven Kanumba yamefanyika katika makaburi ya Kinondoni mjini
Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Tanzania Dr Ghalib Bilal aliwaongoza maelfu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wanaokadiriwa kufikia elfu arobaini, kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa msanii huyo kabla ya mwili wake kwenda kuzikwa.
Shughuli hiyo ya mazishi ilisitishwa kwa muda baada ya umati huo wa watu kusongamana na kukosekana udhibiti na utaratibu wa kuuga mwili huo.
Msanii Kanumba alijipatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya Tanzania kutokana na fani ya uigizaji wa filamu za Kiswahili maarufu kama Bongo Movies.
Akizungumza kwa niaba ya Serikali Waziri wa Habari,utamaduni,vijana na Michezo Dr Emmanuel John Nchimbi amesema, ‘Tanzania imempoteza kijana shupavu aliyetumia vema kipaji chake kujitafutia maendeleo na pia kuitangaza nchi yake.’
Kanumba alikuwa mbunifu katika Fani ya Filamu. Juhudi zake zilimefikisha hadi Afrika Magharibi ambako aliweza kuwashirikisha wasanii kadhaa maarufu kutoka Nigeria katika Filamu zake.
Wakati huo huo Jeshi la Polisi nchini Tanzania, linaendelea kumshikilia binti mmoja ambaye jeshi hilo limemweleza kuwa alikuwa na Uhusiano wa Kimapenzi na Marehemu Steven Kanumba, kwa maelezo kuwa alikuwa mtu wa mwisho kuwa na marehemu muda mfupi kabla ya kifo chake.
Aidha uchunguzi wa Daktari katika mwili wa marehemu bado unasubiriwa ili kujua chanzo cha kifo cha msanii huyo. Polisi inasema uamuzi wa kumfungulia mashtaka Binti huyo utafuta baada ya taarifa za daktari.
Kifo cha Msanii huyo Steven Kanumba kimegusa hisia za wengi nchini Tanzania kiasi cha kuufanya msiba wake kuwa na sura ya Kitaifa ambako hii leo barabara kadhaa jijini Dar es Salaam zilifungwa kwa muda ili kupisha msafara wa mwili wa marehemu wakati ukielekea kwenye viwanja vya Leader Club Kinondoni.
Mamia ya wananchi kutoka pande mbali za jiji la Dar es Salaam walilazimika kutembea umbali mrefu kwa miguu kwenda kutoa heshma zao za mwisho kwa msanii huyo aliyejizolea sifa nyingi katika sanaa hiyo na wengi kuipenda na kuiheshimu kazi yake.
Chanzo: BBC
Saturday, April 7, 2012
Rais Kikwete Amlilia Msanii Kanumba
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Rais
wa Shirikisho la Filamu Tanzania –TAFF- kuomboleza kifo cha msanii maarufu
nchini Steven Charles Kanumba, aliyeaga dunia usiku wa kuamkia leo, Jumamosi,
Aprili 7, 2012.
Katika salamu hizo, Rais
Kikwete amemwomba kiongozi huyo wa TAFF kufikisha salamu za rambirambi za dhati
ya moyo wake kwa wana-familia ya Kanumba na kwa wasaani wote nchini ambao
wamepotelewa na mdau na mwenzi wao.
Rais
Kikwete amesema kuwa ameshtushwa na kuzunishwa na kifo cha msanii huyo ambaye
amemwelezea kuwa msanii mahiri na mwenye kipaji kikubwa ambaye katika uhai wa
maisha yake mafupi na akiwa bado kijana sana amechangia kwa kiwango kikubwa
maendeleo ya sanaa ya filamu nchini na kupitia sanaa hiyo kuitangaza Tanzania
kimataifa.
Amesema
Rais: ”Nimepokea kwa mshtuko na huzuni nyingi taarifa za kifo cha Ndugu Steven
Charles Kanumba. Kupitia filamu zake, ameburudisha na kuelimisha jamii yetu kwa
namna ambayo haiwezi kupimika. Alikuwa msanii mahiri na mwenye kipaji kikubwa
ambaye mchango wake mkubwa katika kuanzisha, kukuza na kuimarisha sanaa ya
filamu nchini hautasahaulika.”
Ameongeza
Rais Kikwete: “Ndugu Kanumba pia ametoa mchango mkubwa katika kuitangaza nchi
yetu ya Tanzania mbele ya mataifa mengine kupitia sanaa ya filamu na uwezo
mkubwa wa kisanii. Tutaendelea kumkumbuka kwa mchango wake huo kwa nchi yetu.”
“Nakutumia
wewe Rais wa TAFF salamu zangu za rambirambi na kupitia kwako kwa wasanii wote
wa filamu na sanaa nyingine kufuatia msiba huu mkubwa kwa fani yetu ya sanaa.
Aidha, naomba unifikishie
salamu za dhati ya moyo wangu kwa wanafamilia wote. Wajulishe kuwa niko nao
katika msiba huu mkubwa. Waambie naelewa machungu yao katika kipindi hiki
kigumu cha msiba,” amesema
Rais Kikwete na kuongeza:
“Namwomba
Mwenyezi Mungu awape subira na nguvu za kuweza kuhimili kipindi hiki kigumu kwa
sababu yote mapenzi yake. Aidha, naungana na wana-familia na wasanii wote
nchini kuwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, aiweke pema peponi roho ya
Marehemu Steven Charles Kanumba. Amen.”
Mwisho.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
07 Aprili, 2012
Friday, April 6, 2012
Rest In Peace Kanumba, Gone Too Soon
Kanumba, ni mchezaji wa filamu ambaye ametoa filamu nyingi sana na ambazo zinavutia sana ukiziangalia. Watanzania, hasa wapenzi wa filamu wamepata pigo kubwa sana kwa kuondekewa na mmoja wa watu ambao wameleta mchango mkubwa katika tasnia ya filamu nchini Tanzania.
Mungu Umeweke Mahala Pema Peponi Steven Kanumba, Amina.
Thursday, April 5, 2012
New Couple Alert?
Look who was hanging out again today!
After seeing The Hunger Games together last night, Kanye West and his new muse, Kim Kardashian, were seen in Manhattan together again this afternoon, first lunching at Serafina with four other people and then going shopping at Jeffrey and FAO Schwarz, E! News has confirmed.
Read on for more on how the pair spent their day together...
MORE: Bikini Shot of the Day: Kim Kardashian Doubles Our Pleasure
Kardashian was photographed getting into a chauffeured car outside of West's apartment building this morning, seemingly the one time he hasn't been by her side in the last 24 hours.
A source tells E! News that the duo are "very close" and that Kardashian, who is divorcing Kris Humphries, is "trying to move on with her life and have fun."
The fashionable pair go way back together and hanging out is certainly nothing new. West was at Kardashian's 30th birthday party in New York City and attended the opening of the NYC branch of Dash back in 2010. More recently, they were photographed together during Paris Fashion Week.
"We've been friends for years," Kardashian told Ryan Seacrest just a couple weeks ago. "We just support each other, that's what friends do."
MORE: Kim Kardashian Plays Rumor Roulette: Is She Adopting? Marrying Kanye? Plus, Latest on Jon Hamm Slam
But as for today's lunch...
"Kim loves Serafina, she's been coming here for years," Alexa McBride, the restaurant's director of public relations, tells E! News. "She came today with Kanye West and they were with some friends...The restaurant was packed so they were sitting among customers who were excited to see them."
And perhaps some fans who fondly remembered Kanye's appearance on Kourtney & Kim Take New York.
McBride tells us that the pair showed "signs of affection," noting that West helped Kardashian adjust her jacket at one point and also toyed with her shoe.
"They were talking, leaning in really close, talking in each other ears—but keep in mind it was very loud in the restaurant," McBride said. "It seemed they were happy and at ease with other."
But, she admitted, there were "no huge outward signs of PDA."
Well, it's nice to have something to look forward to.
Source: E! Online
After seeing The Hunger Games together last night, Kanye West and his new muse, Kim Kardashian, were seen in Manhattan together again this afternoon, first lunching at Serafina with four other people and then going shopping at Jeffrey and FAO Schwarz, E! News has confirmed.
Read on for more on how the pair spent their day together...
MORE: Bikini Shot of the Day: Kim Kardashian Doubles Our Pleasure
Kardashian was photographed getting into a chauffeured car outside of West's apartment building this morning, seemingly the one time he hasn't been by her side in the last 24 hours.
A source tells E! News that the duo are "very close" and that Kardashian, who is divorcing Kris Humphries, is "trying to move on with her life and have fun."
The fashionable pair go way back together and hanging out is certainly nothing new. West was at Kardashian's 30th birthday party in New York City and attended the opening of the NYC branch of Dash back in 2010. More recently, they were photographed together during Paris Fashion Week.
"We've been friends for years," Kardashian told Ryan Seacrest just a couple weeks ago. "We just support each other, that's what friends do."
MORE: Kim Kardashian Plays Rumor Roulette: Is She Adopting? Marrying Kanye? Plus, Latest on Jon Hamm Slam
But as for today's lunch...
"Kim loves Serafina, she's been coming here for years," Alexa McBride, the restaurant's director of public relations, tells E! News. "She came today with Kanye West and they were with some friends...The restaurant was packed so they were sitting among customers who were excited to see them."
And perhaps some fans who fondly remembered Kanye's appearance on Kourtney & Kim Take New York.
McBride tells us that the pair showed "signs of affection," noting that West helped Kardashian adjust her jacket at one point and also toyed with her shoe.
"They were talking, leaning in really close, talking in each other ears—but keep in mind it was very loud in the restaurant," McBride said. "It seemed they were happy and at ease with other."
But, she admitted, there were "no huge outward signs of PDA."
Well, it's nice to have something to look forward to.
Source: E! Online
Tuesday, April 3, 2012
Waasi wa Tuareg wasonga kati ya Mali
![]() |
| Mpiganaji wa Tuareg |
Waasi wanaoongozwa na
Watuareg-wamesonga mbele katika maeneo ya Kaskazini ya Mali,
eneo kubwa wanalodai liwe huru.
Hali ya wasiwasi inazidi kuongezeka
kuhusu harakati za makundi ya wapiganaji wa Kiislamu Kaskazini ya Mali
baada ya waasi wanaoongozwa na Watuareg kuyateka maeneo makuu ya eneo
hilo mnamo wiki iliyopita.
Awali walisema mji wa Homboni hauko katika eneo la Azawad wanalodai liwe huru. Hakuna ishara yoyote kama watasonga mbele kuelekea kusini. Wapiganaji wa kundi la Waislamu la Ansar Eddine wameanza kutekeleza kanuni za sheria za kiislamu katika miji mikuu mitatu iliyotekwa na waasi mwishoni mwa wiki iliyopita.
Taarifa kutoka Kidal Gao na Timbuktu zaeleza kua wapiganji wa Ansar Edinne walishambulia baa zinazouza pombe na kupiga marufuku kucheza muziki wa nchi za Magharibi katika vituo vya redio. Shirika la Utamaduni la umoja wa mataifa limeelezea wasiwasi wao kua maeneo ya kale katika Timbuktu huenda yakaharibiwa na uasi huo.
Waasi Wanaongozwa na kundi kuu la Watuareg la MNLA,wamekanusha kua na fungamano zozote na Ansar Edine licha ya kwamba makundi yote mawili yameshawahi kushirikiana mara kadhaa katika mapigano.
Makundi haya yanatofautiana katika malengo yao. Kundi la MNLA likidai kupigania uhuru wa kaskazini bila ya fungamano zozote za kidini huku Ansar Edine likitaka kuweka mfumo wa sheria za kiislamu nchini kote na hii kuzusha khofu ya kuzuka.
Chanzo: BBC
Subscribe to:
Posts (Atom)








