Wednesday, October 19, 2011

Hotuba ya Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa kwa Waandishi wa habari Monduli, Octoba 19, 2011

Best Blogger Tips

NDUGU wana habari nimewaita katika mkutano huu leo kwa sababu moja kubwa, kutoa ufafanuzi kuhusu matukio ambayo yamekuwa yakitokea huku yakinihusisha mimi binafsi kwa namna ambayo sasa yanatishia ustawi na mshikamano wa kimaadili, kihistoria na kikazi miongoni mwa viongozi na baina ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

"Ndugu wana habari, naamini mmekuwa mkifuatilia kwa karibu habari zinazoripotiwa katika baadhi ya vyombo vya habari zinazolihusisha jina langu na harakati kadha wa kadha chafu ambazo hata mimi mwenyewe ninayehusishwa nazo huwa nazisikia na kuzijua baada ya kuwa zimesharipotiwa katika vyombo hivyo vya habari," alisema.

Alisisitiza kwamba uamuzi wake wa kukutana wanahabari haukuwa na nia ya kuzozana na vyombo vya habari wala kwenda kinyume cha utamaduni wa kimaadili wa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unaotaka viongozi kujadili masuala yanayokihusu chama chao ndani ya vikao rasmi vya kimaamuzi, bali kutoa ufafanuzi na angalizo kwa pande zote hizo mbili ambazo zinaguswa na matukio yanayoendelea kutokea.

Moja ya mambo ambayo yameligusa jina langu kwa namna hiyo ni lile linalonihusisha eti na kundi moja la wanasiasa ambao wamekuwa na mikakati ya kumhujumu mwenyekiti wetu wa chama, Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete. Hakuna shaka ni madai ya kipuuzi, kizushi na yenye malengo machafu.
Hawakuishia hapo sasa wamefikia hatua ya kuvitumia vyombo hivyo hivyo vya habari na kufikia hatua ya kudai kwamba nimeanza kuandaa orodha ya kile wanachokiita madhambi ya Rais Kikwete ambayo wanadai nimepanga kuyasoma wakati wa kikao kijacho cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (CCM).

Ninaamini kwa dhati kabisa kwamba, waandishi wa habari wanaofuatilia kwa karibu na kwa umakini mwenendo wa masuala ya kisiasa nchini wanatambua kwamba, watu wanaopenyeza taarifa hizi katika vyombo vya habari wanafanya hivyo kwa malengo ya kufikirika ya kujisafishia njia kisiasa.

Ni jambo lisiloingia akilini kunihusisha na kile kinachoitwa mikakati ya kumhujumu rais au chama ambacho mimi ni kada wake wa muda mrefu, mbunge anayetokana na chama hicho hicho na mtu ninayeiongoza Kamati nyeti ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na zaidi ya yote kiongozi wa ngazi mbalimbali za kisiasa na kiserikali nilizowahi kushikilia.

Kuhusu hili napenda kusema kwa uwazi kwamba, mbali ya ukweli kuwa sijapata kufikiria hata mara moja kuhusu hicho wanachokiiita mabaya au madhambi ya rais, sina na wala siijui hiyo wanayoitaja kuwa ni orodha ya mabaya ya namna yoyote dhidi ya Rais Kikwete.

Saturday, October 15, 2011

Man United yalazimisha sare na Liverpool

Best Blogger Tips
Steven Gerrard akishangilia bao na wenzake
Javier Hernandez aliisawazishia Manchester United zikiwa zimesalia dakika tisa kabla mchezo haujamalizika na kuisaidia timu yake kuambulia angalao pointi moja katika pambano kali dhidi ya Liverpool.

Mshambuliaji huyo anayechezea pia timu ya taifa ya Mexico, aliingizwa mchezaji wa akiba kipindi cha pili, alitumia akili ya haraka baada ya mpira uliochongwa na Danny Welbeck na kufanikiwa kuisawazishia kwa kichwa timu yake ya Manchester United na kuinyima ushindi Liverpool kutokana na bao lililofungwa awali na Steven Gerrard.

Nahodha huyo wa Liverpool alifunga bao katika dakika ya 68 kwa aina ya mikwaju anayofunga sana ya adhabu ndogo na mpira ukaingia langoni na kumuacha mlinda mlango wa Manchester United David De Gea asijue la kufanya.

Jordan Henderson alikosa nafasi nzuri mbili za kuipatia ushindi Liverpool katika dakika za nyongeza kabla mpira haujamalizika, lakini walinzi wa Manchester United walikaa imara na kuokoa hatari zote na hasa mlinda mlango David De Gea.

Kwa matokeo hayo Liverpool wamefikisha pointi 14 wakijikita nafasi ya tano ya msimamo wa ligi ya soka ya England.
Chanzo: BBC

Friday, October 14, 2011

Watanzania tunamkumbuka Mwalimu Nyerere

Best Blogger Tips


Matatizo kwa wateja wa Blackberry

Best Blogger Tips
Simu ya Blackberry
Mwanzilishi wa kampuni ya Blackberry Mike Lazaridis amesema huduma zake zitarejea kama kawaida baada ya kukumbwa na matatizo makubwa kwa kipindi cha siku tatu duniani kote.

Mamillioni ya wateja duniani kote walikuta mawasiliano yao ya ujumbe mfupi na barua pepe yakikatizwa nawengi wao walielezea hasira zao kupitia mtandao wa Twitter.

Katika ujumbe wake kwa njia ya video kwenye tovuti ya kampuni hiyo, Bw Lazaridis hakutangaza tarehe yoyote kuhusu ni lini huduma kamili zitarudishwa.

Pia alionya kwamba huenda kukazuka matatizo zaidi baadae.

"Hivi sasa tunafikia viwango vya kawaida katika Ulaya, Mashariki ya Kati, India na Afrika" alisema ,ingawa huenda kukazuka "matatizo" wakati kampuni inaendelea kutanzua malimbikizo ya ujumbe mfupi na barua pepe.

Wakuu wa shirika la RIM ambalo ndilo linalomiliki Blackberry limekua likijibu kwa haraka zaidi manun'guniko ya wateja baada ya malalamiko kwamba hawakuwa na mawasiliano mazuri baada ya kujitokeza kwa matatizo haya.

"Tunajua tumewavunja moyo wateja wetu wengi. Mulitraji mengi kutoka kwetu.Nataraji mengi kutoka kwetu "alisema.

Wateja walianza kuarifu kupoteza huduma kuanzia Octoba 10 na matatizo yakaanza kusambaa duniani kote.

Kampuni ya Blackberry ina hamu kubwa kutaka ionekane inalitatua tatizo hili kwa haraka baada ya matatizo ya mapema wiki hii ambapo ilisema huduma zilirejea kama kawaida kauli iliyopingwa vikali na wateja walioghadhibika.
Chanzo: BBC

Wednesday, October 12, 2011

Mwinyi-Viongozi wa dini mnanuka

Best Blogger Tips
RAIS mstaafu Ali Hassan Mwinyi, amesema viongozi wa dini kutoka Tanzania wanatia aibu na kuchangia Watanzania kunuka nje ya nchi kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya.

Mzee Mwinyi alitoa kauli hiyo jana mbele ya viongozi hao na kusimulia mkasa uliomkuta yeye binafsi wa kupekuliwa kupita kiasi katika kiwanja cha ndege nje ya nchi, akishukiwa kuwa kiongozi wa dini kutoka Tanzania anayesafirisha dawa za kulevya.

Alikuwa akizindua Baraza la Viongozi wa Dini la Kupambana na Athari za Dawa za Kulevya jana Dar es Salaam katika hafla iliyoandaliwa na asasi ya kiraia ya American International Health Alliance (AIHA).

“Ninachokisema kuna maneno mengi ya aibu yanasemwa kuhusu Watanzania, aibu zaidi hata kwa wacha Mungu wa Tanzania sasa hawaaminiki, wanatumia fursa walizonazo kuficha na kusafirisha dawa za kulevya.

“Nilikuwa naenda Ujerumani hivyo nililazimika kubadili ndege katika moja ya nchi huko ughaibuni, wakati wa kupanda ndege ya pili tukaanza kukaguliwa. Ilipofika zamu yangu, nilikaguliwa sana, lakini hawakutosheka, nikaingizwa kwenye chumba cha pembeni, nikavuliwa viatu na koti wakanikagua kwa mashine na mwisho wakanipapasa mwili mzima,” alisema Mzee Mwinyi.

Alisema alikumbana na kadhia hiyo pamoja na hadhi yake ya kidiplomasia kwa vile tu alikuwa ameshikilia tasbihi (rozari) mkononi, jambo lililofanya ahisiwe kuwa ni kiongozi wa dini anayesafirisha dawa za kulevya.

“Yule aliyenikagua alikuwa akifanya kazi yake, amenifundisha, lakini nataka mjue Watanzania wenzangu kuwa tunanuka huko nje,” alisema Mwinyi maarufu kama Mzee Ruksa wakati wa utawala wake.

Mzee Mwinyi alilazimika kutoa mkasa huo uliompata miaka mingi iliyopita bila kutaja mwaka wala uwanja husika mbele ya viongozi hao wa dini mbalimbali ili kufikisha ujumbe kwao kuwa Tanzania inanuka kwa kuhusishwa na dawa za kulevya.

Alisema mmoja wa wasaidizi wake alijaribu kumnusuru katika hali hiyo kwa kumtahadharisha ofisa wa uwanja huo wa ndege kuwa huyo anayemkagua ni mwanadiplomasia.

“Lakini bwana yule alimjibu tena kwa ukali ‘I don’t care’ (sijali), wakaendelea kunikagua wanavyotaka baadaye nikajiuliza kwani imekuaje wakanikagua vile, nikagundua kuwa ni kwa vile nimebeba tasbihi,” alisimulia Mzee Mwinyi.

Alisema alionekana kama mwanadini anayetumia alama ya tasbihi ili apitishe dawa za kulevya kirahisi, jambo ambalo lilimsikitisha na wakati anaondoka uwanjani hapo, alilazimika kumkabidhi yule ofisa aliyemkagua tasbihi yake kama zawadi.

Kauli hiyo ya Mzee Mwinyi, imetolewa baada ya Rais Jakaya Kikwete kuwataka viongozi wa dini kukemea uhalifu huo na kutahadharisha kuwa sasa biashara hiyo imeaanza kuvutia viongozi wa dini.

Rais Kikwete alitoa kauli hiyo alipokuwa akiwahutubia waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbinga, kwenye ibada maalumu ya kupewa kuwekwa wakfu Mhashamu Askofu John Ndimbo wa Jimbo hilo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, alisema Serikali imejipanga kuhakikisha kunakuwa na sheria moja yenye nguvu itakayoziba mianya yote inayojitokeza katika sheria za dawa za kulevya.

Alisema kwa sasa sheria zilizopo zina mianya mikubwa ambayo inasababisha mapapa wa biashara hiyo na vipapa vidogo vinavyokamatwa kuishia kulipishwa faini ya Sh. milioni moja na kutoka.

“Sheria inasema wazi ukikamatwa na dawa za kulevya unalipishwa mara tatu ya gharama ya mzigo wa dawa hizo, kifungo cha miaka 30 au maisha lakini hivi kweli mmeshawaona watu wakifungwa kwa kosa hilo, lazima kuwe na marekebisho katika sheria hizi,” alisema

Kamishna wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya, Christopher Shekiondo, alisema kikosi kazi maalumu kilichopo chini ya Tume hiyo kimekamata watu wengi wanaotuhumiwa kufanya biashara hiyo.

Takwimu zinaonesha mwaka 2008 hadi mwaka huu, watuhumiwa 22,814 walikamatwa nchini na 67 nje ya nchi huku idadi ya dawa zilizokamatwa ikiongezeka.

Kwa mujibu wa Shekiondo, dawa zilizokamatwa zimeongezeka kutoka heroine kilo 100 kutoka mwaka 2000 hadi 2009 hadi kilo 154 mwaka jana na mwaka huu; na cocaine kilo 57 mwaka 2000 hadi 2009 hadi kufikia kilo 191 mwaka 2010 hadi mwaka huu.

Baraza hilo la Viongozi wa Dini kazi yake ni kuhamasisha vijana kuepuka biashara na matumizi ya dawa za kulevya na linaongozwa na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum.
Chanzo: HabariLeo

Monday, October 10, 2011

Mwakyembe apelekwa India

Best Blogger Tips
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe amepelekwa katika Hospitali ya Apollo nchini India kwa matibabu baada ya hali ya afya yake kuwa tete kwa kuugua ugonjwa unaomsababishia kuvimba mwili wake.

Akizungumza na gazeti hili, Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa (CCM), alikiri kuwa Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Kyela, anasumbuliwa na maradhi hayo na amesafirishwa jana kwenda India kwa matibabu zaidi.

“Ni kweli Mheshimiwa Waziri ameondoka leo (jana) mchana na ndege ya Qatar Airline kwenda India kwa matibabu zaidi,” alisema Mwambalaswa ambaye kama Dk. Mwakyembe anatoka mkoani Mbeya.

Kwa mujibu wa Mwambalaswa, hali ya Dk. Mwakyembe si mbaya sana kwa kuwa anaweza kula na kutembea vizuri ingawa bado amevimba baadhi ya sehemu mwilini.

Dk. Mwakyembe anadaiwa kusumbuliwa na ugonjwa wa ngozi unaojulikana kitaalamu kama Exfoliative Dermatitis na alianza kusumbuliwa na ugonjwa huo zaidi ya miezi mitatu iliyopita, lakini kwa sasa hali ya ugonjwa huo imezidi kuwa mbaya.

Kwa upande wake, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Haji Mponda alisema hana taarifa za kuugua kwa Dk. Mwakyembe kwa kuwa alikuwa safarini, lakini aliahidi kuzungumzia suala hilo baada ya kupata ripoti zaidi.

Mwakyembe alizungumza juzi na gazeti moja la kila siku na kukiri kuwa anaumwa na kwamba hata sura yake imebadilika huku akikanusha madai ya kulishwa sumu.

Ugonjwa unaomsumbua Dk. Mwakyembe unadaiwa huathiri wanaume na wanawake wenye umri kuanzia miaka 55 na dalili zake ni kuwashwa, mwili kuishiwa nguvu na sehemu ya juu ya ngozi kupukutika.

Chanzo cha ugonjwa huo hakijajulikana, lakini kinahusishwa na magonjwa ya ngozi na madhara ya matumizi ya dawa mbalimbali. Hospitali ya Apollo aliyopelekwa Dk. Mwakyembe, ndiko alikolazwa Waziri wa Maji, Profesa Mark Mwandosya kwa muda mrefu sasa, baada ya kufanyiwa upasuaji wa mgongo, ambaye kwa sasa hali yake imeelezwa kuendelea vizuri.

Juzi, Rais Jakaya Kikwete alikwenda kumjulia hali Dk. Mwakyembe nyumbani kwake Kunduchi jijini Dar es Salaam.
Chanzo: HabariLeo

Pires wa Cape Verde ashinda Mo Ibrahim

Best Blogger Tips
Bw Pedro Veroan Pires wa Cape Verde
Aliyekuwa rais wa Cape Verde Pedro Verona Pires ametunukiwa dola za kimarekani milioni tano inayotolewa na wakfu wa Mo Ibrahim kwa ajili ya utawala bora barani Afrika.

Kamati inayoshughulikia zawadi hiyo ilisema Bw Pires, aliyeachia madaraka mwezi Agosti, amesaidia kuifanya nchi hiyo kuwa " yenye demokrasia, utulivu na kustawi zaidi".

Tuzo hiyo intakaiwa kutolewa kila mwaka kwa kiongozi anayechaguliwa kidemokrasia na kuondoka madarakani kwa hiari.

Hapajakuwa na mshindi kwa miaka miwili iliyopita.

Kamati hiyo ilisema hakukuwa na mgombea anayestahili.

Tuzo hiyo ya dola za kimarekani milioni tano, inayotolewa kwa zaidi ya miaka 10, ni zawadi yenye thamani kubwa duniani inayotolewa kwa mtu binafsi.

Washindi wa awali ni aliyekuwa rais wa Botswana Festus Mogae na wa Msumbiji Joaquim Chissano.
Chanzo: BBC

Sunday, October 9, 2011

Dk Mwakyembe mgonjwa

Best Blogger Tips
Rais Kikwete alipomtembelea Dr Mwakyembe
AFYA ya Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe, ni tete baada ya kuugua ugonjwa uliomsababisha kuvimba mwili wote.Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na yeye mwenyewe zinaeleza kuwa, alianza kuwashwa ngozi miezi mitatu iliyopita kabla ya hali kubadilika siku za karibuni na hatimaye kuvimba sehemu kubwa ya mwili wake.

Mwakyembe alilieleza gazeti hili jana kuwa, baada ya  hali yake kubadilika alianza kupata matibabu katika hospitali mbalimbali jijini Dar es Salaam akiwa nyumbani kwake Kunduchi Beach.Akizungumza na gazeti hili kwa shida, Dk Mwakyembe alisema hajui chanzo cha ugonjwa huo wa ngozi, daktari wake ndiye anaweza kuelezea kwa usahihi.

“Ni kweli naumwa nipo nyumbani, hata sura yangu imebadilika. Sasa hivi namsubiri daktari wangu, nilisikia natakiwa kupelekwa India kwa matibabu, nasubiri kauli yake si mimi niamue,” alisema na kuongeza;
“Siwezi kusema nimelishwa sumu, ninachosema mimi nimevimba kweli mwili mzima naumwa kweli hapa nimelala na sijui umenipataje kwa simu kwa sababu huwa siiwashi muda huu una bahati kweli”.

Mke wa Dk Mwakyembe  Mkewe Linah Mwakyembe alipozungumza kwa njia ya simu na Mwananchi Jumapili, alisema kwa mujibu wa daktari wake, Dk mumewe  anasumbuliwa na ugonjwa wa ngozi unaojulikana kitaalamu kama Exfoliative Dermatitis.
 “Alianza kuugua muda mrefu kidogo, kama miezi mitatu iliyopita, hali hiyo ilikuwa inatokea na kupotea hadi sasa ambapo hali imekuwa mbaya zaidi,” alisema.

Alisema madaktari waliomfanyia uchunguzi kwa nyakati tofauti katika kipindi hicho walitoa majibu tofauti na kuongeza kuwa wapo waliosema hali hiyo ilisababishwa na kisukari na mwingine ambaye hakutaka kutaja jina lake, alisema kulikuwa na chembechembe za sumu katika damu yake.

“Baada ya ngozi yake kubadilika sana na hali kuwa mbaya, tulienda hospitali na madaktari walitupa majibu tofauti, wapo waliosema ni kisukari na kuna mwingine alisema kuna chembechembe za sumu,” alisema Linah na kufafanua  kuwa daktari aliyedai hivyo hakuwapa maelezo zaidi.
Kwa mujibu wa Linah, ngozi ya Dk Mwakyembe inawasha na inakuwa kama inatoa mba mwili mzima hadi kichwani.

Aliongeza kuwa daktari wake ameshauri ufanyike uchunguzi wa kina zaidi ili kujua kama atahitajika kupatiwa matibabu nje ya nchi.
“Walipendekeza afanyiwe uchunguzi zaidi, hivyo kama kutakuwa na ulazima wa kupatiwa matibabu zaidi nje ya nchi basi watatueleza,” alisema Linah.
Alisema kuwa leo ndio watapata  jibu kama atahitajika kwenda nje au kuendelea  na matibabu hapa nchini.

Alisema kumekuwa na uvumi mwingi juu ya ugonjwa wa Dk Mwakyembe na kusisitiza kuwa wao kama familia wanasikiliza kinachosemwa na madaktari na kile watakachoshauri.
“Sisi tunaendelea kusubiri kile kitakachogundulika baada ya uchunguzi huo na kama kutakuwa na mengine tutajulishwa na kujua hatua itakayofuata,” alisema Linah.

Exfoliative Dermatitis Kwa mujibu wa maelezo ya kitabibu, ugonjwa huu huweza kusababisha madhara makubwa ya mwili na matatizo mengine hivyo kuhitaji uangalizi wa karibu wa kitabibu.
Ugonjwa huu ukikomaa husababisha ngozi ‘kuwaka moto’ na huathiri wanawake na wanaume  lakini zaidi wanaume wenye umri kuanzia miaka 55.
Dalili  Dalili za ugonjwa huu ni kuwashwa, mwili kuishiwa nguvu pia sehemu ya juu ya ngozi hupukutika.

Chanzo  kwa mujibu wa maelezo ya kitabibu, sababu za ugonjwa huo bado hajizulikani, hata hivyo matukio ya ugonjwa huu mara nyingi yanahusishwa na magonjwa mbalimbali ya ngozi, madhara ya dawa kama penicillin, sulfonamides, isoniazid na phenytion.

Rais Kikwete amtembelea Baadaye mchana Rais Jakaya Kikwete alifika nyumbani kwa Dk Mwakyembe Kunduchi Beach kumjulia hali.
Mwakyembe ambaye ni Mbunge wa Kyela mwaka 2008, aliongoza Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza kashfa ya Mkataba wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Richmond.

Katika baraza jipya la mawaziri ambalo Rais Kikwete aliliunda mwaka jana, alimteua Dk Mwakyembe kuwa Naibu waziri wa Ujenzi akimsaidia Dk John Magufuli.

Mikasa ya Mwakyembe

Mei 21 mwaka 2009  Dk Mwakyembe alinusurika kufa katika  ajali mbaya ya gari eneo la Ihemi kilomita 40 kutoka Iringa mjini akiwa safari kutokea Mbeya kwenda Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa za Polisi, gari alilokuwa akisafiria Toyota Landcruiser T362ACH,   liliacha njia  saa moja asubuhi baada ya kukanyaga shimo na tairi ya upande wa kulia kuchomoka na dereva wake, Joseph Msuya (30), kupoteza mwelekeo kabla ya gari hilo kutoka nje ya barabara upande wa kushoto na kuparamia mti kisha kupinduka.

Ajali hiyo ilitokea wakati dereva wa Dk Mwakyembe akijaribu kulipita lori kabla ya kukanyaga shimo hilo.

Dk Mwakyembe na abiria wengine waliokolewa na Wasamaria wema pamoja na trafiki wawili  waliokuwa kwenye basi dogo wakisafiri kutoka Iringa kwenda Njombe.

Baada ya ajali hiyo alilazwa  katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa. Ilifahamika kuwa aliumia taya kisha alihamishiwa Dar es Salaam kwa matibabu.

Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP)  aliunda tume iliyoongozwa na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani wakati huo, Kamanda James Kombe,  kuchunguza chanzo cha ajali hiyo. Matokeo yalionesha kwamba ilisababishwa na uzembe wa dereva wake, Msuya.
Chanzo: Mwananchi

Saturday, October 8, 2011

Wabrazil waahidi kuitoa nchi gizani

Best Blogger Tips
MATUMAINI ya Watanzania kuwa na umeme wa uhakika, yameanza kuonesha nuru, baada ya Ijumaa, kampuni ya Odebreicht ya hapa kukubali kuwekeza katika umeme wa maji kwenye maporomoko ya maji ya Stiglers Gorge yaliyopo ndani ya Bonde la mto Rufiji, umbali wa kilomita 374 kutoka jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo ilifikiwa Ijumaa katika mazungumzo kati ya wawakilishi wa kampuni hiyo kubwa ya uwekezaji katika sekta hiyo duniani kufanya mazungumzo na ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano huo jijini hapa, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja alisema mradi huo utakaoanzishwa katika Bonde la Rufiji, ukikamilika utakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme wa megawati 2,100.

Mahitaji ya nchi hayazidi megawati 1,000 ingawa kwa sasa umeme unaozalishwa kutoka
mitambo ya vyanzo vya maji na mafuta unafikia megawati 500, hivyo kufanya upungufu wa kati ya megawati 300 na 500 ambazo zikipatikana zitaiondoa kabisa nchi gizani.

Hivyo, kupatikana kwa umeme wa Brazil kutakuwa kumeandika historia mpya, kwani tatizo la umeme linaweza lisionekane kwa miaka mingi ijayo.

Alisema kampuni hiyo ilisema imeridhishwa na mradi huo baada ya kutembelea Tanzania
Agosti 17, mwaka huu na kuthibitisha kuwa mradi huo unawezekana.

"Hawa watu wana uwezo mkubwa, kwani huu hautakuwa mradi wao wa kwanza, walishakuwa na mradi kama huo nchini mwao hapa ambao unazalisha megawati 3,150...tunaamini watafanya vizuri," alisema Ngeleja.

Alisema mradi huo ambao umekuwa ukipigiwa kelele muda mrefu na wananchi, ukikamilika utaiwezesha Tanzania kujitosheleza kwa nishati hiyo na kuuza mwingine nje ya nchi na kuipatia nchi fedha za kigeni.

Aliongeza kuwa mbali na kuuza nje, lakini pia utakuwa wa bei nafuu kwa wananchi. Hata hivyo Ngeleja alisema Serikali haitakaa na kubweteka ila itaendelea kutafuta vyanzo zaidi vya umeme ili kuhakikisha kuwa tatizo linalojitokeza hivi sasa la umeme halijirudii.

Aliongeza kuwa licha ya hivyo bado Tanzania haitategemea vyanzo vya umeme wa maji pekee bali itaendelea kutafuta vingine jinsi itakavyowezekana.

Kabla ya kujitokeza kwa mwekezaji huyo wa Kibrazil, serikali ilikuwa katika juhudi za kuendeleza mradi wa Stigler’s Gorge tangu miaka ya 1970, kwa kufanya upembuzi yakinifu kwa msaada wa serikali ya Norway, lakini hakuna uendelezaji wowote uliokuwa umefanyika katika mradi huo wa kufua umeme.

Kuhusu mafuta, alisema Kampuni ya Petrobras ya hapa ambayo ilitoa meli kubwa ya
kutafuta mafuta Tanzania inaendelea na juhudi zake katika mwambao wa Bahari ya Hindi
na mpaka sasa haijapata mafuta wala gesi lakini matarajio ni makubwa.

Alisema Petrobras ambayo pia ni kampuni kubwa ya mafuta nchini hapa inatarajia kutoa taarifa ya awali ifikapo Desemba.

Kuhusu juhudi za Serikali kutafuta wabia wa miradi hii, Ngeleja alisema Serikali inafanya hivyo kwa kuwa haina fedha za kutosha yenyewe kuiendeleza na ndiyo sababu inashirikisha sekta binafsi.
Chanzo: HabariLeo

Friday, October 7, 2011

Wanawake watatu washinda tuzo ya Nobel

Best Blogger Tips
Bi Tawakul Karman, Rais Ellen Johnson Sirleaf na Bi Leymah Gbowee
Tuzo ya amani ya Nobel ya mwaka huu imewatunuku kwa pamoja wanawake watatu- Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf, Leymah Gbowee wa Liberia na Tawakul Karman wa Yemen. 

Wametambulika kutokana na "harakati zao bila kutumia vurugu kwa usalama wa wanawake na haki za wanawake katika kushiriki kikamilifu kwenye kujenga amani".

Bi Sirleaf ni rais wa kwanza mwanamke barani Afrika, Bi Gbowee mwanaharakati wa amani Liberia na Bi Karman kiongozi wa harakati za kidemokrasia Yemen.

Tuzo hiyo ikitangazwa Oslo, mwenyekiti wa kamati ya Nobel Thorbjorn Jagland alisema: " Hatuwezi kufanikiwa kupata demokrasia na amani ya kudumu katika dunia hii mpaka wanawake wafanikiwe kupata fursa sawa na wanaume ili kuweza kuchochea maendeleo katika viwango vyote vya jamii."

Taarifa hiyo ilisema "ni matumaini ya kamati ya Nobel ya Norway kuwa tuzo hiyo itasaidia kumaliza ukandamizaji wa wanawake ambao bado unaendelea katika nchi nyingi, na kutambua uwezo mkubwa wa demokrasia na amani ambao wanawake wanaweza kuwakilisha."

'Mwanamke Ngangari'

Bi Karman anaongoza shirika la Yemen la Women Journalists without Chains, yaani waandishi wa habari wa kike wasio na mipaka na amefungwa jela mara nyingi kutokana na kampeni zake za kutaka uhuru wa habari na upinzani wake kwa rais wa serikali ya Ali Abdullah Saleh.

Alitambuliwa kwa kuchukua nafasi kubwa kwenye harakati za haki za wanawake katika machafuko ya kuunga mkono demokrasia huko Yemen "katika hali ngumu sana".

Bi Karman, mama mwenye watoto watatu, ameiambia idhaa ya Kiarabu ya BBC kuwa anatunukia tuzo yake kwa "wote waliojitoa mhanga na kujeruhiwa na machafuko ya nchi za kiarabu"- wimbi la ghasia lililoenea Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita na kwa " watu wote wanaopigania haki zao na uhuru wao".

Ni mwanamke wa kwanza wa kiarabu kushinda tuzo ya amani ya Nobel.
Bw Jagland amesema ukandamizwaji wa wanawake ndilo "jambo muhimu sana" katika dunia ya kiarabu na kumtunukia Bi Karman ni "kutoa ishara kwamba kama itafanikiwa katika jitihada za kuleta demokrasia, lazima iwahusishe wanawake".

Bi Sirleaf, mwenye umri wa miaka 72, ambaye tetesi kwa kiasi kikubwa zilikuwa zikimwelekeza yeye, alisema tuzo hiyo ni " kwa Waliberia wote" na kutambuliwa kwa " miaka mingi ya harakati za kupata haki".

Alichaguliwa mwaka 2005, kufuatia kumalizika kwa miaka 14 ya vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyosababisha vifo vya watu 250,000, na kusababisha wengi kukimbilia nchi za nje na kuvuruga uchumi wa nchi hiyo.

Alipoingia madarakani, mchumi aliyepata elimu yake Marekani na aliyekuwa waziri wa fedha- anayejulikana kama "mwanamke Ngagari" wa Liberia aliahidi kupambana na rushwa na kuleta "hisia za kimama kwenye urais" kama njia ya kuponyesha majeraha yaliyotokana na vita.

Ni maarufu sana miongoni mwa wanawake na wasomi wachache nchini humo, lakini anachukiwa na jamii za kimila zinazoongozwa zaidi na wanaume.

Bi Sirleaf anagombea tena urais wiki ijayo, licha ya kusema kuwa atashikilia nafasi hiyo ya urais kwa mhula mmoja tu.

Bi Gbowee alikuwa kinara wa kupinga vurugu wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe Liberia, akiwashawishi wanawake wa makabila na dini zote katika harakati za amani- wakati fulani hata "kugoma kufanya ngono"- na kuwahimiza kushiriki kwenye uchaguzi.

Taarifa kuhusu tuzo hiyo ilisema, " Tangu wakati huo amaefanya kazi ya kuwashawishi wanawake Afrika Magharibi wakati na baada ya vita."

Wanawake hao watagawana zawadi yenye thamani ya dola za kimarekani milioni 1.5.
Chanzo: BBC

Thursday, October 6, 2011

Steve Jobs wa Apple afariki dunia

Best Blogger Tips
Steve Jobs
Steve Jobs, mwanzilishi msaidizi na aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa kampuni kubwa ya kimarekani ya Apple, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 56. 

Apple imesema "uhodari wake, hisia zake na uwezo wake ulikuwa chanzo cha ubunifu usiohesabika uliostawisha na kuimarisha maisha yetu sote.

Joba alitangaza kuugua saratani ya kongosho mwaka 2004.

Rais wa Marekani Barack Obama alisema kutokana na kifo chake, dunia "imempoteza mtu mwenye upeo"
Bw Obama alisema, " Steve alikuwa miongoni mwa wabunifu muhimu Marekani- mwenye ujasiri wa kutosha wa kufikiri tofauti, shujaa wa kutosha wa kuamini anaweza kubadili dunia, na mwenye kipaji cha kutosha cha kuweza kufanya hivyo.

Taarifa kutoka kwenye familia ya Bw Job imesema walikuwa naye alipofariki dunia kwa amani siku ya Jumatano.

"Katika maisha yake ya kikazi, Steve alijulikana mwenye upeo; katika maisha yake ya binafsi, aliipenda familia yake," walisema, wakiomba faragha na kuwashukuru wale "waliomwombea" katika mwaka wake wa mwisho.

Tim Cook, aliyerithi nafasi yake katika kampuni ya Apple baada ya Bw Job kuachia madaraka mwezi Agosti, amesema aliyemtangulia aliacha "kampuni ambayo yeye pekee ndiye angeweza kuijenga, na nafsi yake maisha itakuwa msingi wa Apple".

Bendera zimeshushwa nusu mlingoti nje ya makao makuu ya Apple huko Cupertino, California, huku mashabiki wa kampuni hiyo wakiacha rambirambi nje ya maduka ya Apple duniani kote.

Cory Moll, mfanyakazi wa Apple wa San Fransisco alisema, "Alichotufanyia ni kama utamaduni, inauma kwa namna ya kipekee kwa kila mtu".
Chanzo: BBC

Sunday, October 2, 2011

Shoga 'Anti Suzy' afichua siri nzito

Best Blogger Tips
SHOGA maarufu jijini Dar es Salaam, Ibrahim Mohamed ‘Anti Suzy’ (25) ameibuka na kutoa siri nzito kuhusu mambo yanayofanywa na mashoga kwa kushirikiana na baadhi ya vigogo
nchini kuwaharibu watoto wadogo wa kiume.

Ametoa tahadhari huku akidai kuwa kama Serikali kwa kushirikiana na watu wengine
haitachukua hatua, kizazi cha kiume cha Watanzania siku zijazo kitapotea katika dunia hii kutokana na ukweli kwamba wimbi la uwepo wa mashoga linazidi kuongezeka kwa kasi.

Anti Suzy ambaye ni mkazi wa Jangwani, pia amejitangaza kuwa ni muathirika anayeishi na Virusi vya Ukimwi kwa zaidi ya miaka 10 sasa na akasema mashoga wengi wameshaambukizwa virusi vya Ukimwi kama yeye na wanaishi kwa matumaini, hivyo kwa kuwa nao ni binadamu, wasingependa kuona watoto wadogo wa kiume wakiharibiwa kama walivyofanyiwa wao.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hizi katika ofisi za gazeti hili zilizopo Mtaa wa Samora, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Anti Suzy alisema hivi sasa wanaume wenye fedha akiwataja kwa jina maarufu la ‘mapedejee’ wanatumia fedha zao kuharibu watoto wadogo huku wengi wao wakijijua kuwa ni waathirika wa Ukimwi.

“Najua kuwa na Ukimwi si mwisho wa maisha lakini si vizuri mtu ukijijua kuwa umeathirika,
ukamwambukiza mwenzako kwa makusudi, kwa kweli sasa hivi hali ni mbaya, wanaume wenye pesa ‘mapedejee’ wanapenda sana watoto wadogo wa kiume,” alisema na kuongeza:

“Wazazi wawe macho sana, sasa hivi mashoga wa rika langu ukienda ukumbi wa starehe au baa, wakijua wewe ni shoga, anakutafuta mtu anakuomba simu ili umtafutie mtoto
mdogo kwa gharama yoyote.

“Mashoga watu wazima hivi sasa hawana soko, wanasakwa watoto wadogo walioko mitaani na hata shuleni,kama Mwalimu hana utu anaweza hata kuuza mtoto wako kwa sababu ya fedha, mtu yuko radhi kukupa pesa yoyote umtafutie mtoto mdogo wa kiume.

“Wanawapenda pia watoto wa kiume wanaochipukia kwenye ushoga ambao siku hizi ndiyo wapo kibao (wengi), watoto wanaharibika sana, wanaowatafuta wanapewa mpaka laki mbili hata zaidi kwa mtoto mmoja”.

Huku akiwataja kwa majina (yanahifadhiwa), Anti Suzy alisema mapedejee hao wana fedha nyingi hivyo wana ushawishi mkubwa, lakini alitoa angalizo kuwa si watu wote wanaoitwa pedejee wana mchezo huo, ingawa alikiri kuwa wengi wao hujitangaza kwa jina hilo wanapotaka kutafutiwa watoto au mashoga wapya kutoka nje ya mkoa kwa wanaoishi Dar es Salaam.

Akizungumzia ongezeko hilo sambamba na maambukizi ya Ukimwi, Anti Suzy aliyezaliwa
Bugando mkoa Mwanza mwaka 1986 akiwa kitinda mimba kwenye familia yao ya watoto watano, alisema hivi sasa mashoga wengi wameambukizwa ugonjwa huo na wengi wao wanafanya biashara ya kujiuza hivyo wanaendelea kuambukiza watu wengine.

Alisema mwanaume akimkuta shoga baa au katika ukumbi wa starehe kwenye Casino, na pembeni ikiwa kuna mwanamke anayejiuza, humchukua shoga jambo linalofanya
kuendelea kuathirika na kuharibiwa vibaya viungo vyao vya siri.

Alidai yeye alizaliwa akiwa na homoni nyingi za kike na wazazi wake walihangaika hospitali bila mafanikio na alipofika darasa la tatu alianza mchezo huo na mfanyabiashara wa kiarabu (jina tunalo) aliyekuwa akifanya kazi za ndani nyumbani kwake akitoka shule ili apate
fedha za mahitaji ya shule, ikiwemo sare.

Anti Suzy alidai mfanyabiashara  huyo alimtorosha kutoka nyumbani kwao Mwanza na kumpeleka Zanzibar ambako alikaa naye nyumba ya wageni (jina tunalo) kwa zaidi ya mwezi mmoja usiku na mchana akimwingilia jambo alilokuja kubaini baadaye kuwa ameharibu maumbile yake ya kiume.

Alisema pamoja na kuwa na wanaume wengine, alihisi ndiye aliyemuambukiza Ukimwi. “Siwezi kusema ni nani kaniambukiza Ukimwi lakini nahisi ni yule mwarabu, maana mashoga wengi nawafahamu wenye Ukimwi amewachezea sana yeye na pia ameharibu watoto wengi sana, sijui hivi
sasa yuko wapi lakini kweli ameharibu watoto sana na kama yupo hai basi huenda anaendelea kuwaharibu,” alibainisha Anti Suzy.

Siri nyingine aliyoitoboa Anti Suzy alidai, akiwa Dar es Salaam alifanya biashara ya kujiuza na kutembea na waume za watu wakiwemo vigogo nchini wanaopenda kutembea na mashoga kuliko wanawake na alikuwa na uwezo wa kutembea na wanaume watano hadi sita kwa siku wakati mwingine bila kinga, kutegemea na uwezo na matakwa ya wanaume hao na mara nyingine aliwalisha
dawa za kulevya na kuwaibia.

“Kweli nilikuwa naiba sana, kuna jamaa nilimlisha dawa, nikaiba na kugeuza mkono wa simu ya chumbani, simu zikapigwa hazipatikani, wakaja kabla sijatoka, wakamkuta jamaa amelala anakoroma mimi nimeshika baadhi ya vitu na pesa, jamani nilipigwaaa! nilipigwaaa! Lakini sikujali maana aibu ilikuwa kwake, ameshachukua malaya (shoga) watu walimjalia mpaka waandishi wa habari walimpiga picha,” alisema.

Aliwataka wanawake wafuatilie mienendo ya waume zao kwa kuwa japo baadhi yao wamejitangaza kuwa na Ukimwi, lakini wanaume wamekuwa wakiwataka na wengine wanawakimbia wake zao na kuwalazimisha mashoga wawalelee watoto wao kama alivyoletewa yeye mtoto wa mwaka mmoja na nusu na mwanaume aliyekuwa akiishi naye kama mume wake ingawa sheria za nchi haziruhusu.
Source: HabariLeo

Saturday, October 1, 2011

Hukumu ya Igunga leo

Best Blogger Tips
MACHO na masikio ya Watanzania, leo yanaelekezwa Jimbo la Igunga mkoani Tabora, ambako wananchi watapiga kura kumchagua mgombea mmoja kati ya wanane wanaoshiriki uchaguzi mdogo wa ubunge, kuwa mbunge wao.Mgombea atakayechaguliwa atamrithi Rostam Aziz, aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, ambaye alijiuzulu katika tukio lililohusishwa na mchakato wa kujivua gamba ndani ya chama hicho.

Rostam alikuwa mbunge wa jimbo hilo kwa miaka 15 mfululizo kuanzia mwaka 1994 hadi alipojiuzulu Julai 13, mwaka huu.Wagombea wanaowania nafasi hiyo ni Leonard Mahoma wa CUF Joseph, Dk Dalaly Kafumu wa CCM na Kashindye wa Chadema.

Wagombea wengine wanaoshiriki uchaguzi huo na vyama vyao kwenye mabano ni Said Cheni (DP), Heme Dedu (UPDP), Hassan Rutegama (Chausta), John Maguma (Sau), na Steven Mahuyi (AFP).
 
Wagombea wote mbali na kujinadi kwa sera za kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo hilo tangu kampeni hizo zilipoanza Septemba 7, mwaka huu walikuwa wakipigana vijembe wakati wote wa kampeni.

Kazi ya wagombea hao na vyama vyao kunadi sera imekamilika jana na leo wakazi wa Igunga, wataamua nani awawakilishe bungeni kama mbunge wao.

Polisi waimarisha ulinzi Igunga

Msemaji wa Jeshi la Polisi katika uchaguzi huo, Isaya Mngulu aliliambia gazeti hili kuwa, jeshi hilo limejiandaa kikamilifu kuhakikisha kuwa uchaguzi huo unakamilika katika mazingira ya amani.

“Hadi leo (jana) tunapozungumza hakuna tukio lolote la uvunjifu wa amani na tunaamini hali itaendelea kuwa shwari na tunavitaka vyama viwaelimishe wanachama na mashabiki wao umuhimu wa amani,” alisema.

Mngulu alisema wapo polisi wa kutosha Igunga, kikiwamo Kikosi Maalumu cha Kutuliza ghasia (FFU) na kuonya watu kujaribu kuvuruga akisema watapambana na mkono wa dola.

“Nataka niwahakikishie wapiga kura kuwa wajitokeze kwa wingi na waende kupiga kura, ulinzi ni imara hakuna mtu atakayeletewa vurugu au kuzuiwa kupiga kura… kwa kweli tuko kamili,” alisisitiza Mngulu.

Alisema katika kuimarisha ulinzi huo, polisi wamefungua komandi ndogo nane, maeneo yenye wananchi wengi ya Simbo, Mwisi, Nkinga, Sungwisi, Ziba, Mwanshimba, Igurubi na Itumba ambazo zitakuwa katika utayari wa kukabiliana na chokochoko yeyote.

Polisi wapeperusha  bendera nyekundu
Magari ya polisi yanayotumika kusimamia ulinzi na usalama katika uchaguzi mdogo Jimbo la Igunga, yameonekana yakirandaranda mitaani usiku na mchana huku yakipeperusha bendera nyekundu.

Mengi ya magari hayo aina ya Toyota Land Cruicer rangi ya bluu yameonekana yakizunguka mitaani na askari wa FFU, hali inayotafsiriwa kuwa ni kudhihirisha kuwa, atakayeleta chokochoko atakiona cha moto.

Juzi gari lililosheheni lita 80,000 za maji ya kuwasha, nalo lilionekana likitoka mafichoni katika kituo cha polisi Igunga na kuzunguka mitaani, katika kile kinachotafsiriwa kuwa ni kutoa ujumbe wa kuzatiti kwa jeshi hilo.

Msimamizi wa uchaguzi anena
Kwa upande wake Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Igunga, Protas Magayane, alilsema jana kuwa vifaa vyote vya kupigia kura vilianza kusambazwa jana asubuhi.

Magayane alisema jimbo hilo lina kata 26 na wapigakura waliojiandikisha 170,077 na kwamba ili kuharakisha usambazaji wa vifaa unaenda vizuri, wamekodi malori 52 yatakayokwenda kila kata mawili kusambaza vifaa hivyo.

Magayane aliwataka wapigakura wafike mapema vituoni wakiwa na vitambulisho halali vya kupigia kura na si fotokopi na kwamba, watakapomaliza kupiga kura waondoke maeneo hayo wakisubiri matokeo.

“Kuna wapigakura wali-scan vitambulisho vyao au kutengeneza fotokopi, Hivyo havitaruhusiwa bali waje na vitambulisho 'original' (halisi) na waepuke kuvaa sare yoyote ya chama au kufanya kampeni vituoni,” alisema.

Hekaheka zatawala Igunga
Kumekuwa na hekaheka katika Jimbo la Igunga kwa siku mbili mfululizo sasa huku magari makubwa na madogo, baiskeli, bajaji, pikipiki na hata mikokoteni, ikipeperusha bendera za vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo.

Lakini kubwa ni magari ya viongozi na wafuasi wa vyama vikubwa vitatu vinavyoonekana kukabana koo vya CUF, Chadema na CCM ambayo yamekuwa yakiporomosha muziki unaosifu vyama na wagombea wao.

Tambo za hapa na pale baina ya wafuasi wa vyama vya Chadema CCM na CUF zinaonekana wazi kwenye vijiwe, nyumba za burudani na makazi ya watu.

Mbali pilikapilika hizo, helikopta za vyama hivyo nazo zilipasua anga kuanzia asubuhi jana kuelekea maeneo ya mikutano ya hadhara ya kuhitimisha kampeni hizo zilizodumu takribani siku 25.

Igunga yaelemewa na wageni
MJI wa Igunga unaelekea kulemewa na wageni wengi wakiwa ni viongozi na makada wa vyama vya siasa vinavyoshiriki katika uchaguzi huo mdogo wa ubunge.

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa nafa za kulala katika nyumba za kulala wageni sasa hivi zimekuwa adimu kutokana na wingi wa wageni hao huku baadhi ya wamiliki wakipandisha gharama za malazi kwa siku.

Kila nyumba ya wageni utakayopita sasa utakutana na kibao chenye maandishi “hakuna nafasi” kutokana na vyumba kujaa kunakochangiwa na kuwapo kwa nyumba hizo chache ikilinganishwa na idadi ya wageni waliopo.

Inakadiriwa kuwa wageni kati ya 3,000 na 6,000 wako Jimboni Igunga hivi sasa. Wengi wao ni viongozi wa kisiasa wakiwamo viongozi wa kitaifa, wabunge, makada, wapiga debe wa vyama na wanahabari.

Ujio huo wa wageni unaonekana kuwanufaisha zaidi wamiliki wa nyumba hizo ambao baadhi wamelazimika kupandisha gharama za malazi kwa kati ya asilimia 10 na 20 ikilinganishwa na bei za awali.

Baadhi ya madereva na wapiga debe wa vyama vya siasa hivi sasa wanalazimika kulala kwenye magari na wengine wa jinsia moja kulala wawili kwenye chumba kimoja kutokana na upungufu wa vyumba.

Lakini ujio huo wa wageni umeongeza mzunguko wa fedha katika jimbo hilo ambapo mama lishe mmoja alisema: “Kimsingi, uchaguzi huu ni neema kwetu, tunatamani ufanyike kila mwezi.”

Wafanyabiashara wote, awe mama lishe, mmachinga, maduka ya nguo, migahawa na nyumba za starehe kama baa na kumbi za muziki wanaonekana kunufaishwa na ongezeko hilo la mzunguko wa fedha wilaya humo hivi sasa.
Source: Mwananchi

Wednesday, September 28, 2011

Helkopta Chadema yavuruga Igunga

Best Blogger Tips
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana kilianza kutumia helkopta katika mikutano yake ya
kampeni za ubunge katika Jimbo la Igunga na kusababisha baadhi ya mikutano ya vyama vingine vinavyoshiriki kampeni hizo kuvunjika.

Helkopta hiyo inayoendeshwa na Kapteni Paul Denge iliwasili saa 6:00 mchana katika kiwanja cha Shule ya Msingi Choma cha Nkola na kusababisha walimu na wanafunzi kuvunja vipindi vya masomo kushuhudia chopa, pia wananchi waliikimbilia kwa baiskeli na pikipiki, kitendo kilicholazimisha walinzi wa Chadema kufanya kazi ya ziada kuzuia wananchi walionekana kutaka kuishika na kupiga picha.

Wakati Chadema kikianza kutumia helkopita hiyo na kupata wananchi wengi kwenye mikutano yao, Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana kilikuwa kimesimamisha kampeni kusubiri helkopita zake mbili ambazo zilitarajiwa kuwasili muda wowote, zikitokea Dar es Salaam.

Nacho Chama cha Wananchi  (CUF), kilikutana na waandishi wa habari na kuwaeleza nia ya kuleta chopa kama hiyo, ili kuwafikia wananchi katika maeneo ya jimbo hilo ambalo kijiografia limekuwa na miundombinu isiyopitika kirahisi.

Mara baada ya helkopita hiyo kuwasili, iliwachukua viongozi wa Chadema, akiwemo Mwenyekiti, Bw. Freeman Mbowe, mgombea ubunge Bw. Joseph Kashindye na mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Morogoro, Bi. Susan Kiwanga pamoja na waandishi wa habari na kuelekea katika kijiji cha Chabiso.

Katika Kijiji cha Chabiso, CUF walikuwa wafanye mkutano eneo hilo lakini baada ya kukimbiwa na wananchi wote waliamua kuvunja mkutano na kuondoka.

Akizungumza katika mkutano kijijini hapo, Bw. Mbowe alisema CCM imekabwa kila kona na safari hii haitatoka, kisha akawataka wananchi kufumbua macho kwa kuwa saa ya ukombozi imefika kwani wameteseka ndani ya miaka 50 bila mafanikio.

“Nawaambia ndugu zangu Chadema imeikamata CCM kweli kweli hadi kufikia hatua ya kutuogopa, safari hii tutabanana na ninawahakikishia hawatoki, tumejipanga kupambana nao. CCM inaogopa sana Chadema ndiyo maana mnasikia kila siku kwamba wanasema chama chetu ni cha fujo, siyo kweli wameona tunakubarika kwa Watanzania roho imeanza kuwadunda,” alisema.

Aliwataka wananchi hao kuwa wanakabiliwa na mtihani mkubwa ambao hivi sasa Watanzania wote wameelekeza macho na masikio yao kwao, kusikia wataamua nini juu ya hatma ya kupata kiongozi atakayewasaidia matatizo yanayowakabili.

“Nimepata taarifa kwamba kuna matatatizo makubwa yakiwemo maji, zahanati na barabara, lazima mfanye maamuzi mazuri, CCM hii ni ya matajiri ambao wanawakumbuka kila uchaguzi unapofika lazima muonyesha miaka 50 ya uhuru wa Tanzania wameshindwa kumaliza kero zenu.

…Lakini pia nimesikia hapa kuna chakula cha msaada kinagawiwa, hizi ni fedha zenu si za CCM, kama wanavyopita humo wanawadanganya…kama kuna mwanachama wetu yeyote atakayenyimwa atoe taarifa kwa viongozi wetu haraka, kwa sababu ni haki yenu kupata chakula,” alisema.
Endelea kusoma habari hii.................

Monday, September 26, 2011

Prof Wangari Maathai afariki dunia

Best Blogger Tips
Mtunukiwa wa tuzo ya Amani ya Nobel Prof Wangari Maathai ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 71.

Mwanaharakati huyo mashuhuri wa mazingira na haki za binadamu wa Kenya Profesa Wangari Maathai amefariki dunia mjini Nairobi usiku wa kuamkia , Jumatatu kutokana na maradhi ya saratani.

Prof Karanja Njoroge ambaye ni mkurugenzi wa Green Belt Movement, shirika ambalo Prof Maathai alilianzisha amethibitisha kifo hicho.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari Prof Njoroge amesema wakati wa kifo chake Wangari alikuwa na wanafamilia na marafiki.

Marehemu ameacha watoto watatu, wawili wakiume na mmoja wa kike.

Profesa Wangari Maathai alipata tuzo la amani ya Nobel mwaka 2004, kufuatia juhudi za kupigania uhifadhi wa mazingira nchini Kenya.

Mbali ya kuwa Mwanaharakati wa Maswala ya Mazingira na haki za binadamu , Wangari Maathai pia alikuwa mwanasiasa shupavu.

Amewahi kuhudumu kama Mbunge na Naibu waziri wa Mazingira nchini Kenya.

Prof Maathai pia katika uhai wake alipata tuzo mbalimbali za kimataifa kwa kutambua mchango wake.

Prof. Wangari Muta Maathai alianzisha vuguvugu la Green Belt mnamo mwaka 1977, ambapo alifanya kazi na wanawake kote nchini kuboresha maslahi yao na kuhifadhi mazingira.

Alikuwa mtetezi mashuhuri wa matumizi bora ya mali asili .Shughuli zake zilitambuliwa mara kwa mara kote duniani.
Chanzo: BBC

Saturday, September 24, 2011

Liyumba atoka jela

Best Blogger Tips
Hatimaye aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Amatus Liyumba (63), jana aliachiwa huru na Jeshi la Magereza, baada ya kumaliza kifungo chake cha miaka miwili kwa kosa la matumizi mabaya ya ofisi.

Liyumba aliachiwa jana asubuhi baada ya kutumikia kifungo cha miaka miwili alichohukumiwa na jopo la mahakimu wawili kati ya watatu waliosikiliza kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na NIPASHE jana majira ya saa 4:42 asubuhi, kwa njia ya simu, msemaji wa jeshi hilo, Kamishna Mwandamizi, Omary Mtiga, alisema kuwa Liyumba aliachiwa baada ya kumaliza kifungo chake mapema saa 3:00 asubuhi na kuongeza kuwa alikuwa huru rasmi nje ya gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam. 

“Ndiyo Liyumba ameachiwa leo (jana) asubuhi kwa sababu ameshamaliza kutumikia adhabu ya kutumikia kifungo cha miaka miwili katika gereza la Ukonga, jijini Dar es Salaam,” alisema Kamishna Mtiga.

Mei 24, mwaka jana, mahakimu wawili, Lameck Mlacha na Benedict Mwingwa kati ya watatu walitoa hukumu iliyomtia hatiani bosi huyo wa zamani wa BoT, ambaye alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela.

Liyumba alituhumiwa kutumia madaraka yake vibaya na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Sh. bilioni 221 kupitia kwenye mradi wa ujenzi wa majengo pacha ya benki hiyo.

Hukumu ya Hakimu Edson Mkasimongwa ilimuona Liyumba ana hatia katika kosa hilo.

Mbali na kuachiwa huru, Liyumba yuko nje kwa dhamana kwa shtaka la kukutwa na simu gerezani kinyume na kifungu namba 86 kidogo cha kwanza na cha pili cha Sheria ya Jeshi la Magereza.

Ilidaiwa kuwa Julai 27, mwaka huu kinyume cha sheria hiyo ya magereza, Mkurugenzi huyo wa zamani, alikutwa na simu ya mkononi aina ya Nokia 1280 ya rangi nyeusi iliyokuwa inatumia laini namba 0653-004662 pamoja na namba ya utambulisho ya simu (IMEI) 356273/04/276170/3.

Ilidaiwa kuwa mshtakiwa alikutwa na simu hiyo katika chumba chake cha magereza bila kuwa na kibali cha kufanya hivyo huku akijua ni kosa.

Mshtakiwa alikana shtaka hilo na mahakama ilimtaka kujidhamini kwa hati ya dhamana ya Sh. 50,000 na mdhamini mmoja ambaye ni mtumishi wa serikali au kutoka kwenye taasisi inayotambulika.

Mshtakiwa alitimiza masharti hayo na mahakama ilimuachia kwa dhamana hadi Septemba 29, mwaka huu.

Friday, September 23, 2011

Waziri amuumbua daktari

Best Blogger Tips
NAIBU Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Lucy Nkya, ameelezea udhaifu wa utoaji huduma za afya kwa baadhi ya hospitali nchini, baada ya kwenda katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru na kuandikiwa dawa bila kujieleza kwa daktari.

Dk. Nkya alisema hayo wakati akizungumza na menejimenti, wafanyakazi na wanafunzi wa uuguzi na udaktari katika Hospitali Teule ya Halmashauri ya Wilaya ya Hai, baada ya kupata hati rasmi ya kutambua kupanda hadhi kwa hospitali hiyo.

Huku akiitaja hospitali hiyo, Naibu Waziri alisema alifika hapo bila kujitambulisha huku amejifunika nguo hadi usoni akaingia kwa daktari ambaye hakumtaja jina, lakini daktari huyo alimwandikia dawa bila kumwuliza tatizo lake.

“Niliingia kwa daktari na kabla sijakaa, akaanza kuniandikia vipimo huku akinihoji kama nina homa na shinikizo la damu (BP), nilimjibu nitajuaje wewe ndiye mtaalamu, akanieleza tena natakiwa kupigwa picha za mionzi (X-ray), nilishangaa sana,” alisema.

Alisema kutokana na hali ile, alimweleza daktari husika kwamba anatakiwa amsikilize kabla ya vipimo, lakini katika hali ya kushangaza, alisisitiza kuwa anatakiwa kwenda kupigwa picha za X-ray.

“Niligundua kuwa daktari yule alikuwa amedhamiria na analosema nilijitambulisha kwamba mimi ni Dk. Lucy Nkya, Naibu Waziri … alipatwa mshtuko, nikamhoji kama ndivyo anavyotoa huduma kwa wananchi wa kawaida, nilimwonya nikaondoka,” alisema.

Alisema aliondoka na kuahidi kurejea wakati mwingine bila kutambulika, ili kuangalia mwenendo wa mtumishi huyo kama anatekeleza wajibu wake kulingana na sheria, kanuni na taratibu za utoaji tiba.

Akizungumza na watumishi wa hospitali hiyo teule, alisema imekuwa miongoni mwa hospitali teule 34 nchini na kuwataka watumishi wake kuzingatia kanuni na taratibu za afya kwa kutoa huduma kulingana na viapo vya taaluma yao.

“Ninyi leo mmepata hati rasmi ya utambuzi kuwa Hospitali Teule ya Wilaya ya Hai, hakikisheni mnatimiza wajibu wenu … hii sasa ni hospitali ambayo inatoa huduma kwa vigezo vya Serikali, nisingependa kusikia malalamiko dhidi yenu,” alionya.

Aliitaka Halmashauri ya Hai kutohamisha watumishi wa hospitali hiyo kwa namna yoyote na badala yake wajitahidi kukabili changamoto zilizopo ili iweze kutekeleza wajibu wake.

“Sasa Serikali itakuwa ikilipa mishahara na marupurupu kwa watumishi wa hospitali hii, tukisikia halmashauri mnahamisha watumishi au kutumia fedha zinazotumwa ili kufanyia vikao, safari za namna yoyote … tutawachukulia hatua kisheria,” alisema.

Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Dk . Saitore Laizer, aliiomba Serikali ianze kutoa ruzuku ya mishahara, dawa, vifaa tiba na vitendanishi kwa hospitali hiyo, ili wananchi wapate huduma kwa gharama nafuu kama ilivyo kwa hospitali zingine za umma.

Alisema changamoto nyingine ni uhaba wa watumishi unaosababishwa na kuhama kwa watumishi kutoka mashirika ya dini na ya binafsi kwenda serikalini, jambo ambalo limeiathiri hospitali hiyo hususani idara za meno na macho.
Chanzo ; HabariLeo

Thursday, September 22, 2011

Michael Sata ashinda uchaguzi Zambia

Best Blogger Tips
Mshindi wa uchaguzi wa Zambia Michael Sata
Kiongozi wa chama cha Patriotic Front, Micheal Sata ametangazwa kwa mshindi wa uchaguzi wa urais nchini Zambia

Bw Sata alipata asilimia 43 ya kura zilizopigwa na kumshinda Rais Rupiah Banda wa chama tawala cha MMD ambacho kimekuwa mamlakani kwa muda wa miaka 20.

Tangazo hilo lilitolewa na Jaji Mkuu wa Zambia Ernest Sakala.

Awali watu wawili waliuawa kufuatia ghasia katika maeneo ambayo ni ngome ya upinzani.

Mkuu wa Polisi wa jimbo hilo maafuru kwa uzalishaji Shaba ameliambia shirika la habari la Reuters watu wamejitokeza katika barabara za mji wa Kitwe na Ndola wakivurumisha mawe.

Mwandishi wa BBC anasema ghadhabu hizi zimechochewa na agizo la serikali kupiga marufuku vyombo vya habari kutangaza matokeo bila ya idhini ya tume ya uchaguzi ya nchi hiyo.

Mwandishi wa BBC Mutuna Chanda akiwa Lusaka kilomita 300 kusini mwa Kitwe, anasema huko Kitwe, waandamanaji waliteketeza soko moja usiku na Polisi wameweka vizuwizi katika mji wa Wusaikile.

Rais Banda alimshinda Bw Sata kwa kura 35,000 katika uchaguzi wa mwaka 2008, matokeo yaliozusha ghasia kutoka upande wa upinzani katika ngome zao za mijini.

Tangu uchaguzi wa mwaka 2008, watu wengine milioni moja wamejiandikisha kuwa wapiga kura,wengi wao vijana wasio na ajira.
Chanzo: BBC

Upinzani waelekea kushinda Zambia

Best Blogger Tips
Bwana Michael Sata
 KIONGOZI wa upinzani nchini Zambia, Michael Sata, anaelekea kushinda katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo, uliofanyika Jumanne wiki hii katika nchi hiyo yenye utajiri mkubwa wa madini ya shaba.

Hata hivyo, ghasia kubwa ziliripotiwa kuibuka katika Jimbo la Kaskazini mwa Zambia la Ukanda wa Shaba, kwenye ngome kuu ya Sata, kufuatia kusitishwa kwa matokeo ya awali ya uchaguzi, yaliyokuwa yakionyesha kwamba kiongozi huyo anaongoza dhidi ya Rais anayemaliza muda wake, Rupiah Banda.

Matokeo ya awali ya uchaguzi huo uliofanyika Jumanne wiki hii, yalitangazwa jana jioni na Tume ya Uchaguzi ya nchi hiyo, yakionyesha kuwa Sata alikuwa akiongoza kwa kura 639,787 dhidi ya 542,362 za Banda, ambaye ni kiongozi wa Chama cha The Movement for Multi-party Democracy (MMD) kilichotawala taifa hilo tangu 1991.
Matokeo yaliyotangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zambia, Irene Mambilima yalikuwa ni yale yaliyokusanywa katika majimbo 85 kati ya 150.

Hatua ya kusitishwa kwa matokeo yaliyokuwa yakimpa matumaini Sata (74) maarufu kwa jina la "King Cobra" kutokana na kauli zake kali, kumezusha ghasia kubwa kutokana na kuwapo kwa hisia za wizi wa kura.
Wakati matokeo ya uchaguzi huo yakisubiriwa kwa hamu, Mahakama Kuu ya nchi hiyo imevizuia vyombo vya habari kutangaza matokeo kabla ya kutolewa na Tume ya Uchaguzi.

Amri ya Mahakama Kuu ilitolewa kufuatia ombi lililowasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Zambia. Jaji wa Mahakama Kuu, Jane Kabuka, alisema wanavizuia vyombo vya habari kutangaza au kuchapisha matokeo yasiyo rasmi hadi yapate idhini ya Tume ya Uchaguzi.

Katika toleo lake la juzi, gazeti binafsi la The Post lilikuwa na kichwa cha habari kuwa Satta ameshinda uchaguzi huo. Na hata baada ya pingamizi hilo la Mahakama Kuu, jana tena gazeti hilo liliandika kuwa kiongozi huyo wa upinzani anaongoza kwa 59%.

Hatua hiyo ya Mahakama Kuu  imekuja huku Tume ya Uchaguzi  ikisema kuwa wezi wa mitandao wameingilia mtandao wao na kuweka matokeo ya uongo yanayoonyesha kuwa kiongozi wa chama cha upinzani cha Patriotic Front, Satta, anaongoza.

Msemaji wa Tume hiyo, Cris Akufuna, alisema kutokana na hitilafu hiyo maofisa wake wanafanya kazi kuhakiki zaidi ya mara mbili matokeo kutoka maeneo mbalimbali.Alisema mchakato huo umesababisha kuchelewa kutolewa kwa matokeo, hali ambayo imeanza kuzua hofu ya kwamba matokeo ya uchaguzi huo yamefanyiwa hila.

Katika maeneo kadhaa tayari washabiki wa kiongozi huyo wa upinzani wameanza kusherehekea wakiamiani kuwa kiongozi wao ameshinda.Rais Banda anatarajiwa kupata kura nyingi katika maeneo ya mikoani, ambako kuna uwezekano wa matokeo kutolewa taratibu, kuliko maeneo ambayo ni ngome ya  upinzani, ambayo ni mji mkuu Lusaka na maeneo ya Ukanda wa Shaba, ambako ndiko kitovu cha uchumi wa Zambia.

Hata hivyo, kwa mujibu wa duru za habari ni mapema mno kusema iwapo Satta, yuko katika nafasi nzuri ya kushinda na kukiondoa madaraka chama tawala kwa mara ya kwanza tokea kumalizika kwa mfumo wa chama kimoja mwaka 1991.Akufuna alisema bado wanaendelea kupokea matokeo kutoka maeneo mbalimbali na kwamba mpaka itakapofika leo jioni watatangaza matokeo rasmi.

Vurugu mpaka Mbeya
Mpaka wa Zambia na Tanzania katika eneo la Tunduma mkoani Mbeya umefungwa upande wa Zambia kutokana na vurugu zinazoendelea maeneo mbalimbali ya nchi hiyo. Maeneo hayo ni pamoja na mji wa Nakonde  katika mpaka huo upande wa Zambia, ambako  magari yanadaiwa kupigwa mawe.

 Habari kutoka ndani ya  vyombo vya usalama Mkoa wa Mbeya zinadai kuwa katika mji huo unaopakana na Tunduma,  kumezuka vurugu ambapo wananchi wa Nakonde wamekuwa wakifanya vurugu kwa kupiga mawe magari, huku polisi nao wakituliza vurugu hizo kwa kurusha mabomu ya machozi.

 "Vurugu hizi zipo mpakani  upande wa Zambia kwani hata  wenzetu Zambia wameamua kufunga mpaka, lakini siyo kiofisi ni kienyeji kwa ajili ya kuzuia vurugu zisiweze kuvuka upande wetu wa Tanzania na  kuepusha mali, yakiwamo magari kuharibiwa na vurugu hizo,"inadai taarifa hiyo.

 Taarifa hizo zilisema kuwa, magari yaliyopigwa mawe ni pamoja na basi aina ya Taqwa linalofanya safari zake kutoka Tanzania kwenda Zambia na lori la mkoani Iringa  la kampuni ya Asasi ambapo yalipigwa mawe yakiwa  mpakani upande wa Zambia.

 Aidha, kwa upande wa Tanzania katika mji wa Tunduma hakuna kinachoendelea, kwani malori yote yaliyopo Tunduma yamezuiwa kuvuka mpaka hadi hapo vurugu hizo zitakapotulia.
Chanzo: Mwananchi

Wednesday, September 21, 2011

Msuya aonya Serikali isicheze na mgawo umeme

Best Blogger Tips
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Cleopa Msuya ameitahadharisha Serikali kuwa makini na suala la mgawo wa umeme ambao amesema unaongeza ugumu wa maisha kwa wananchi, kwani unaweza kusababisha matatizo makubwa kiasi cha nchi kushindwa kutawalika.“Hali ikiendelea hivi tusishangae kutokea kwa mambo kama yaliyotokea kwa nchi za Kiarabu ambazo wananchi wake wameshindwa kuvumilia ugumu wa maisha na kuamua kuandamana.”  Msuya alitoa tahadhari hiyo, Dar es Salaam jana wakati wa mjadala wa kitaifa  kuhusu miundombinu, nishati na madini kwenye Wiki ya Maonyesho ya Miaka 50 ya Uhuru yaliyoandaliwa na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).

Angalizo la Msuya inakuja kipindi ambacho nchi ipo katika mgawo wa umeme kutokana na uhaba mkubwa wa nishati hiyo hali ambayo inaathiri sekta mbalimbali za uzalishaji na watumiaji wa kawaida.

Msuya alikuwa Waziri Mkuu kati ya Novemba 7, 1980 hadi Februari 24, 1983 na kushika tena wadhifa huo Desemba, 1994. Pia aliwahi kuwa Waziri wa Fedha, Viwanda katika vipindi tofauti.

Ili kukabiliana na tatizo hilo, Serikali kupitia kwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja ilitangaza mpango wa dharura wa Sh1.2 trilioni kukabiliana na mgawo, lakini hadi sasa hakuna mabadiliko yoyote yanayoonekana tangu ulipoasisiwa Agosti, mwaka huu.

Kauli ya Msuya
Msuya alisema Tanzania inahitaji uchumi unaokua na kwamba Serikali isipoangalia, tatizo la kushindwa kukua kwa uchumi, maendeleo ya nchi hayatafanikiwa.  “Kabla ya uhuru idadi ya watu ilikuwa milioni nane na sasa tuko zaidi ya watu 53 milioni, kuna haja ya kuwa na uchumi unaokua badala ya kuzalisha bila mafanikio, Serikali iwe makini katika kuimarisha mambo muhimu kama nishati,” alisema na kuongeza:

“Serikali inatakiwa kufikiri juu ya kuimarisha masuala ya umeme nchini wakati wawekezaji wanapoingia ili kusaidia uchumi kukua haraka na kuepusha kutokea kwa mambo yaliyozikumba nchi za Kiarabu.”  Ingawa hakuzitaja nchi hizo, lakini Misri, Tunisia, na Yemen ndizo zilikumbwa na maandamano kupinga hali ngumu ya kiuchumi na kusababisha viongozi wa Misri na Tunisia na kung’olewa madarakani.

Msuya alisema Serikali ina jukumu la kuimarisha mazingira yatakayoendeleza uchumi na kwamba ipo changamoto kubwa ya kuziunganisha sekta binafsi ili kuinua uchumi.  “Tatizo ni namna Serikali itakavyokubaliana na sekta binafsi katika kuimarisha uchumi wake na kuwainua wananchi kibiashara kwa sababu miundombinu ya uzalishaji hasa umeme bado haijasambaa katika mikoa yote,” alisema.

Alisema Serikali itakapoiunganisha mikoa 26 katika kuzalisha biashara na kuipatia nguvu ya umeme, itakuwa njia mojawapo ya kuimarisha mafanikio ya kila mwananchi na kuondokana na umaskini. “Sasa hivi tunaambiwa kuwa kuna fungu la fedha la kutekeleza kilimo, lakini bado kuna maswali mengi ya kujiuliza juu ya uwezeshwaji wa kilimo, kwa sababu maeneo ya vijijini ambayo ndiyo yanayojishughulisha na kilimo hayana umeme, Kilimo Kwanza kitatekelezwaje?,” alihoji Msuya.  Msuya alisema, ipo haja kwa Serikali kuangalia namna ya kuboresha mazingira ya kiutendaji ya halmashauri mikoani ili kila mkoa uunganishiwe umeme kirahisi.
 
Kauli ya Ngeleja

Ngeleja akizungumza kwenye hafla hiyo alisema, Serikali imetoa fursa kwa sekta binafsi kuwekeza hasa katika masuala ya nishati ili kuzalisha, kusambaza na kusafirisha.Alisema sekta binafsi imepewa jukumu hilo ili kuzalisha zaidi na kuimarisha uchumi wa nchi kwa kiwango kinachotakiwa na kuboresha miundombinu yake.

“Tangu Serikali ilipofanya mageuzi ya kisera katika uendeshaji uchumi wa nchi, sekta binafsi imekuwa ikiongezewa nguvu ya biashara hivyo ni vyema sekta hiyo ikatumia fursa ya kuwekeza zaidi katika sekta muhimu na kuzingatia sera ya nishati ya mwaka 2008,” alisema.

Alisema matatizo ya umeme yaliyopo yanatokana na mfumo wa kuunganisha umeme na kiwango kikubwa kinachopotea kutokana na usambazaji kuanzia katika chanzo cha umeme.

“Uwekezaji mdogo katika umeme unaochukua muda mrefu pia ni chanzo kikubwa katika kuchangia umeme, tozo zinazotozwa hazikidhi mahitaji yaliyopo na gharama kubwa za mafuta katika soko la dunia zinaongeza gharama za uzalishaji,” alisema.  Akizungumzia tatizo la mgawo wa umeme, Ngeleja alisema uchumi wa nchi umeporomoka kwa asilimia 6.9 na kuwa megawati 236 za mgawo huo kwa siku moja zinagharimu Dola za Marekani 400 milioni (takriban Sh500 bilioni).

 Mgawo wa umeme umekuwa ukiitikisa nchi zaidi tangu mwaka 2006 na hadi sasa Serikali imekuwa na mipango mingi ukiwamo ule uliopitishwa na Bunge hivi karibuni, kuonekana kukosa tija.  Katika mpango huo wa dharura, Serikali ilitangaza kuwa itatumia kiasi hicho cha Sh1.2 trilioni kwa ajili ya  mpango huo wa ili kunusuru uchumi wa nchi kuanzia Agosti hadi Desemba mwaka huu na Januari hadi Desemba mwakani. 

 Wiki moja iliyopita, Waziri Ngeleja alitoa ahadi ya kupungua makali ya mgawo huo lakini hadi sasa, hakuna nafuu iliyojitokeza.
Chanzo: Mwananchi

Wednesday, September 14, 2011

Rais Kikwete ateua wakuu wapya wa mikoa 15

Best Blogger Tips
RAIS Jakaya Kikwete amewateua wakuu wa mikoa wapya 15, kuwabadilisha vituo vya kazi wakuu wa mikoa watano huku wengine saba wakielezwa kwamba wamestaafu kwa mujibu wa taratibu. Katika uteuzi huo, wa wakuu wa mikoa 21, kati yao 11 walikuwa wakuu wa wilaya na ni Perseko Ole Kone pekee aliyebaki katika kituo chake cha kazi cha Mkoa wa Singida.

Mbali ya idadi kubwa ya wakuu wa wilaya waliopandishwa vyeo, katika uteuzi huo, Rais Kikwete pia amewateua waliokuwa Manaibu Waziri watatu, Mwantumu Mahiza, Ludovick Mwananzila na Joel Bendera, kuwa wakuu wapya wa mikoa.

Taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu iliyotolewa Dar es Salaam jana iliwataja wakuu hao wa wilaya waliopandishwa vyeo na mikoa yao katika mabano kuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, John Tupa (Mara), DC wa Morogoro, Saidi Mwambungu (Ruvuma), Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Chiku Gallawa (Tanga), DC wa Ilala, Leonidas Gama (Kilimanjaro), DC wa Newala, Dk Rehema Nchimbi (Dodoma), Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Elaston Mbwillo (Manyara).

Wengine ni DC wa Karagwe, Kanali Fabian Massawe (Kagera), DC wa Mvomero, Fatma Mwassa (Tabora), DC wa Manyoni, Ali  Rufunga (Lindi), DC wa Kilombero, Mhandisi Ernest Ndikillo (Mwanza), DC wa Bagamoyo, Magesa Mulongo (Arusha). Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Stella Manyanya ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
Katika uteuzi huo, Mahiza anakwenda Mkoa wa Pwani, Bendera ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na Mwananzila Shinyanga. Kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, Mahiza alikuwa ni Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi pamoja na Mwananzila huku Bendera akiwa ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo.

Waliobadilishwa vituo vya kazi ni Abbas Kandoro anayekwenda Mbeya akitokea Mwanza, Said Mecky Sadiki anayehamia Dar es Salaam akitokea Lindi, Christine Ishengoma anayekwenda Iringa akitokea Ruvuma, Luteni Kanali Issa Machibya kutoka Morogoro kwenda Kigoma na Kanali Joseph Simbakalia anakwenda Mtwara akitokea Kigoma.

Wakuu wa mikoa waliostaafu ni Mohammed Babu aliyekuwa Kagera; Isidore Shirima (Arusha), Kanali Anatory Tarimo (Mtwara), John Mwakipesile (Mbeya), Kanali Enos Mfuru (Mara), Brigedia Jenerali Dk Johanes Balele (Shinyanga) na Meja Jenerali   Said Kalembo (Tanga).

Wakuu wa wanne wa mikoa waliostaafu ambao watapangiwa vituo vingine vya kazi ni Amina Mrisho aliyekuwa Pwani, Dk James Msekela aliyekuwa Dodoma, Abeid Mwinyimusa aliyekuwa Tabora na Daniel Ole Njoolay wa Rukwa.

Taarifa hiyo ya Ofisi ya Waziri Mkuu imesema: “Wakuu wa mikoa mipya minne ya Simiyu, Geita, Katavi na Njombe itakayoundwa baada ya taratibu kukamilika watatangazwa baadaye.”

Taarifa hiyo iliongeza: "Wakuu wote wa mikoa waliopo sasa wameagizwa kuandaa hati za makabidhiano katika muda wa siku 14 kuanzia siku ya kuapishwa kwa wakuu wapya wa mikoa. Aidha, wakuu wa wilaya ambao wamepandishwa vyeo kuwa wakuu wa mikoa nao wanapaswa kufanya hivyohivyo kwa ajili ya wakuu wa wilaya watakaopangiwa vituo vitakavyokuwa vimeachwa wazi kutokana na uteuzi wao.”

"Makabidhiano hayo lazima yahusishe pia kutembelea kwa pamoja baadhi ya maeneo na miradi ambayo ni muhimu kama sehemu ya makabidhiano yao," ilisisitiza taarifa hiyo na kuongeza:

"Wakuu wote wa mikoa walioteuliwa na wakuu wa mikoa minne mipya watakaoteuliwa pamoja na wakuu wote wa wilaya watakaoteuliwa baada ya zoezi kukamilika watatakiwa kuhudhuria mafunzo ya wiki tatu kwenye Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo zaidi wa kiuongozi na kiutendaji.”

Wakuu hao wapya wa mikoa wataapishwa na Rais Kikwete kesho saa 4.00 asubuhi kwenye Viwanja vya Ikulu, Dar es Salaam.
Chanzo: Mwananchi

Monday, September 12, 2011

Miss Universe 2011 ni Leila Lopes Kutoka Angola

Best Blogger Tips
Miss Universe 2011 Leila Lopes
Miss Angola Leila Lopes amevishwa taji la Miss Universe 2011 katika mchuano uliofanyika siku ya jumanne katika jiji la Sao Paulo nchini Brazil.

Lopez, alikuwa katika la watu watano walioweza kufika katika fainali za mashindano hayo. Wengine walikuwa ni kutoka China, Brazil, Philippines, Ukraine na Panama.

Nchi zilizoingia katika kumi bora ni Australia, Costa Rica, France, Ukraine, Portugal, Panama, Philippines, Angola, China na Brazil.

Lopez ameweza kuwashinda washiriki wengine 88 kutoka nchi mbambali duniani zilizoshiriki mashindano hayo ikiwamo Tanzania.

Mashindano hayo yalikuwa ni ya 60 kufanyika tangu yaanzishwe 1952.




Boma la mafuta lalipuka Kenya na kuua zaidi ya 100

Best Blogger Tips
Waokozi wakisaidia watu baada ya Bomba kulipuka mjini Nairobi
 Zaidi ya watu mia moja wamekufa baada ya bomba la mafuta kupasuka na kulipuka katika katika mji mkuu wa Kenya Nairobi, polisi wamesema.

Mlipuko huo umetokea katika eneo la viwandani la Lunga Lunga na askari wa zima moto walipambana na moto mkali ambao ulikuwa ukitishia makazi ya watu mjini humo.

Bomba hilo la mafuta limepita katika makazi ya watu wengi kwenye mitaa ya mabanda katikati ya mji wa Nairobi na Uwanja wa ndege.

Zaidi ya majeruhi 100 wamepelekwa hospitali, maafisa wanasema.

Msemaji wa magari ya huduma za dharura alisema waathirika wengi waliungua kiasi cha kutokufatambulika.

Taarifa zinasema mlipuko huo huenda umesababishwa na kishungi cha sigara kilichotupwa katika mtaro wa maji ambao ulikuwa ukielea mafuta.

Mafuta hayo yalivuja kutoka kwenye tangi moja katika ghala linalomilikiwa na Kampuni ya Mafuta ya Kenya, msemaji wa polisi Charles Owino ameliambia shirika la habari la Reuters.

‘Miili yaelea

Polisi na jeshi wameweka vizuizi katika eneo hilo, ambapo wakazi walisema kuvuja kwa mafuta kwenye bomba hilo na kusababisha watu wengi kukimbilia kuchota mafuta yaliyovuja.

"Kulikuwa na sauti kubwa ya mlipuko, mlipuko mkubwa, na moshi na moto ukiwaka juu angani," mkazi mmoja Joseph Mwego aliliambia shirika la habari la AFP.

Sehemu ya miili ilionekana ikiungua kiasi cha mita 300 (futi 1,000) karibu na eneo la tukio, wenyeji walisema.

Miili mingine likuwa inaelea katika mto karibu na eneo hilo ambapo watu walioungua iliripotiwa waliruka baada ya kushika moto.

Vibanda vilivyoezekwa kwa mabati vimejengwa karibu kabisa na bomba hilo, wakazi walisema.

Kumekuwa na vifo vingine ambavyo vimetokana na watu kuchota mafuta yanayovuja: Zaidi ya watu mia moja walikufa eneo la Molo, magharibi mwa Kenya mwaka 2009 baada ya lori la mafuta kupinduka na moto kulipuka.
Chanzo: BBC

Saturday, September 10, 2011

Ajali ya meli Zanzibar: Mamia wafariki

Best Blogger Tips
Watu wasiopungua 187 wamekufa baada ya meli iliyokuwa imezidisha mizigo kuzama katika pwani ya kisiwa cha Zanzibar ikiwa na watu takriban 800.

Msemaji wa serikali amesema watu 620 walionusurika wameokolewa. Serikali imetangaza siku tatu za maombolezo.

Inadhaniwa kuwa meli hiyo ilizama baada ya injini yake kukosa nguvu.

Shughuli za uokoaji zilikwazwa kwa kuwa meli hiyo ilizama usiku.

Zaidi ya watu 100 bado hawajulikani walipo, lakini watu 325 walionusurika wameokolewa, kwa mujibu wa waziri wa masuala ya dharura wa Zanzibar.

Meli hiyo, MV Spice Islander ilikuwa ikisafiri kati ya Kisiwa kikuu cha Unguja kuelekea Pemba.
Meli hiyo ilikuwa ikirejesha watu baada ya kumalizika kwa mfungo wa Ramadhani.

Msaada

Mamlaka za huko zimezidiwa na tukio hilo na zimeomba msaada kutoka nje.

Serikali ya Zanzibar imeunda kituo cha uokoaji na kutoa wito kwa taasisi zote kusaidia katika shughuli za uokozi. Serikali hiyo pia imeomba msaada kutoka nchi nyingine za nje, kama vile Kenya na Afrika Kusini.

Walionusurika walichukuliwa na boti za kibinafsi na kupelekwa katika bandari ya Zanzibar, amekaririwa kamishna wa polisi wa Zanzibar Mussa Hamis.

Miili ya watu imekuwa ikisukumwa katika pwani ya Zanzibar na mawimbi. Mpaka sasa miili ya watu 100 wamepatikana, amesema mwandishi wa BBC Ali Saleh akiwa Zanzibar.

Maelfu ya ndugu na jamaa wanasubiri kusikia taarifa za ndugu zao ambao walikuwa ndani ya meli hiyo, anasema mwandishi wetu.

Mohhamed Aboud, waziri wa masuala ya dharura wa Zanzibar anasema watu 259 walionusurika wameokolewa lakini 40 kati yao wamejeruhiwa sana.

Catherine Purvis, mtalii kutoka Uingereza aliyepo Zanzibar, akisubiri boti ya kwenda Dar es Salaam amesema ameshuhudia miili ya watu wengi ikitolewa ndani ya maji.

"Nimesimama katika bandari ya Zanzibar nikiwa na watalii wengine kama 10 wa Marekani na Uingereza.

"Boti yetu imechelewa kwa sababu wanatumia vyombo vyote vya baharini kuokoa watu".

Rubani mmoja wa helikopta Kapteni Neels van Eijk alipita juu ya eneo la tukio.

"Tuliona walionusurika wakiwa wameshikilia magodoro na majokofu au chochote kile kinachoweza kuelea. Ni vigumu kusema idadi kamili, lakini naweza kusema walikuwepo zaidi ya watu 200 walionusurika ndani ya maji na miili ya watu pia," ameiambia BBC.

"Wakati huo, kulikuwa na boti chache zilizofika katika eneo hilo. Walikuwa wakitafuta walionusurika, ingawa bahari haikuwa imechafuka sana, mawimbi walikuwa makubwa, kwa hiyo ilikuwa vugumu kuona walionusurika.

"Tulirusha ndege yetu na kuziongoza boti hadi kwa watu walionusurika ili waweze kuwachukua. Kulikuwa na miili kadhaa ndaniya maji."

Meli hiyo iliondoka Unguja takriban saa tatu usiku saa za Afrika Mashariki na inadhaniwa kuwa ilizama majira ya saa saba usiku.

Ilikuwa imebeba abiria wengi kiasi kwamba baadhi ya abiria waligoma kupanda, amekaririwa abiria mmoja aliyenusurika Abdullah daid, akizungumza na shirika la habari la AP.
Chanzo: BBC



Friday, September 9, 2011

Hatimaye BAE yakubali kuilipa Tanzania fedha za Rada

Best Blogger Tips
Kampuni ya kutengeneza silaha za kijeshi ya Uingereza BAE Systems, hatimaye imekubali kuilipa moja kwa moja serikali ya Tanzania dola milioni 47.

Fedha hizo ni malipo ya ziada yaliyotokana na mauzo ya Rada ambayo yalikuwa ni zaidi ya fedha halisi ya ununuzi wa rada hiyo .

Uamuzi huo unahitimisha mvutano wa muda mrefu kuhusu ununuzi wa rada hiyo ambao ulifanyika katika mazingira ya rushwa na kusababisha mahakama nchini Uingereza kuamuru fedha hizo zirejeshwe Tanzania
Kampuni ya BAE Systems ilishutumiwa na wabunge wa Uingereza kwa kujivuta kutekeleza amri ya mahakama iliyotolewa zaidi ya mwaka mmoja uliopita .

Serikali ya Uingereza ilisema imeiambia BAE kuwa hawana budi kulipa malipo hayo na kutarajia kuwa suala hilo lingefikiwa muafaka kwa faida ya watanzania.

Awali katika taarifa yake rasmi BAE ilisema inafanya kazi na serikali ya Uingereza kupitia wizara yake ya Maendeleo ya Kimataifa (DFID) kutoa malipo hayo kulingana na utaratibu wao.

BAE haikuwa tayari kuilipa serikali ya Tanzania fedha hizo na ilitaka ilipe kupitia misaada yake kwa mashirika ya hisani ya Uingereza yanayofanya kazi nchini Tanzania.

Akizungumza na BBC Idhaa ya Kiswahili kutoka Kongwa Dodoma, Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai alisema ‘huku Tanzania tumeupokea uamuzi huo kwa furaha kubwa sana sana sana, kwa sababu ni jambo ambalo kwa upande wetu tukuwa tunaona kuwa si haki na kwa kuwa sasa fedha hizo zinarudi Tanzania,
‘Ni matumaini yetu kuwa fedha hizi zitatumika vizuri, kupitia serikali yetu kwa manufaa ya watanzania wote kama ilivyokusudiwa.’ Aliongeza Bw Ndugai.

Naibu Spika Job Ndugai miezi michache iliyopita aliongoza ujumbe wa wabunge wa Tanzania mjini London kufuatilia malipo hayo, baada ya kutokea mvutano wa muda mrefu kati ya serikali Tanzania na kampuni hiyo ya BAE.
Chanzo: BBC

Thursday, September 8, 2011

Chadema yazindua kampeni, Mkapa atua Igunga

Best Blogger Tips
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimezindua kampeni zake za kuwania Jimbo la Igunga huku Katibu Mkuu wake, Dk. Willibrod Slaa, akiwataka wananchi kumchagua mgombea wa chama hicho, Joseph Kashindye ili alinde rasilimali za wana Igunga.

Wakati Chadema wakizindua kampeni hizo kwa mtindo wa kumwaga tuhuma na kashfa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mwenyekiti mstaafu wa CCM, Rais wa Awamu ya Tatu, alitua Igunga tayari kwa uzinduzi wa kampeni za chama hicho na kuelezea furaha aliyonayo ya kusafiri kwa lami kutoka Dar es Salaam hadi Igunga.

Katika uzinduzi wa Chadema, Dk. Slaa aliwataka wananchi waliokuwa wamefurika katika Uwanja wa Sokoine mjini hapa, kumchagua Kashindye ili alinde rasilimali hizo na kupunguza aliowaita panya wanaozitafuna.

Alidai kuwa mgombea wa CCM, Dk. Peter Kafumu, hawezi kuleta mabadiliko yoyote Igunga na kwa Taifa kutokana na alichoita kuwepo kwa mfumo mbovu wa CCM katika kusimamia maslahi ya wananchi.

Dk. Slaa alisema kuwa nchi inahitaji kutetewa na makamanda, ili ifanikiwe kwa kuwa CCM imeshindwa kazi ya kuwasaidia wananchi.

Aliwaambia polisi aliowaita wanaoagizwa kuwapiga mabomu wananchi, wasifanye hivyo kwa kuwa kazi ya Chadema, ni kuwatetea polisi wa vyeo vya chini ambao alidai wanapewa posho ndogo isiyokidhi mahitaji yao.

Naye Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema kuwa Serikali ya CCM imeshindwa kazi hivyo haifai kuwa madarakani wala kuongezewa wabunge kwa kuwa itazidi kuwadidimiza wananchi.

Kwa upande wake Kashindye alijinadi mbele ya wananchi hao kuwa wakiona mwalimu anaachia chaki na kwenda kwenye siasa, basi wajue hali ni mbaya kwa kuwa Taifa linahitaji ukombozi.

“Hata Mwalimu Nyerere (Baba wa Taifa Mwalimu Julius), aliachia chaki alipoona hali ni mbaya na akaamua kuingia kwenye siasa na kuikomboa Tanzania tunayoishi leo,” alisema.

Alidai kuwa CCM wanadhani kuwa watumishi wa Serikali ni mali yao kitu ambacho si kweli na ameamua kuingia Chadema ili awatetee wananchi wa Igunga na Taifa kwa ujumla.

“CCM ni chama kinachokufa nisingeweza kuondoka na kuingia CCM kuwa mbunge wa kusinzia kwa kuwa hawana hoja,” alidai.

Alidai kuwa fedha nyingi za kujenga barabara zimeliwa kitu ambacho kimesababisha wananchi kuteseka kutokana na mfumo mbovu wa CCM.

“Nawaombeni mnitume niende huko bungeni niende nikawe Spika ya Igunga; nikaseme yote na tupate mafanikio wote,” alisema.

Mbunge wa Viti Maalumu Chadema, Susan Kiwanga alisema ni lazima Igunga wahakikishe chama hicho kinashinda kwa kumchagua Kashindye ili awatetee bungeni.

Alisema, ataweka kambi Igunga na kuhakikisha chama hicho kinashinda kwa kuwa Chadema ni chama cha kutetea wanyonge ambao wamekuwa wakinyonywa na CCM kwa miaka nenda rudi.

Mkapa atua Igunga Lakini Mkapa baada ya kutua Igunga, aliweka bayana kuwa amefika kupambana na kumnadi mgombea wa CCM kwa kuwa anajisikia faraja na matunda ya CCM yakiwemo kutembelea barabara ya lami kutoka Dar es Salaam mpaka Mwanza.

Akiwahutubia wananchi katika Kitongoji cha Makomero alisema kuwa ni muhimu kwa wana Igunga kupuuza vyama vingine kwa kuwa CCM ikitoa ahadi, inatimiza na viongozi wake ni makini.

“Kazi yetu ni moja tu, kila mtu ahakikishe Dk. Kafumu anashinda na kila mtu ambaye amejiandikisha aende kupiga kura ili mambo yawe poa,” alisema Mkapa.
Chanzo: HabariLeo

Mbuzi mwenye miguu nane azaliwa Bunda

Best Blogger Tips
KATIKA  hali isiyokuwa ya kawaida mbuzi mmoja katika Kijiji cha Nafuba kilichoko Kata ya Nansimo wilayani hapa, amezaa mapacha  huku mmojawao akiwa na miguu minane, mikia miwili na kichwa kimoja.

Habari zilizopatikana kutoka kijijini hapo na kuthibitishwa na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kilomo, kulikotokea tukio hilo, Fabian Kamanyi zinasema tukio hilo la kustaajabisha lilitokea jana mnamo  saa 1:45 asubuhi wakati mbuzi huyo aliyekuwa ametimiza miezi tisa ya ujauzito wake kuzaa mapacha hao kikiwamo kiumbe hicho ambacho hata hivyo kilikufa saa mbili baadaye.

Fabian alisema kabla ya kuzaa mbuzi huyo ambaye hiyo ni mara yake ya tatu kuzaa usiku, alikuwa akilia kama ishara ya kutaka kuzaa  hali iliyomfanya mmiliki wake Silvanus Bernado, asubuhi yake  kumtenganisha na wenzake kwa kumfunga jirani na nyumbani ili ampatie uangalizi wa pekee.

Alisema hatimaye ulipotimia muda wake wa kuzaa (usiku), mbuzi huyo alizaa mapacha hao akiwamo huyo mmoja wa ajabu ambaye alikuwa wa kwanza kuzaliwa akiwa haonyeshi jinsi  ya aina yoyote tofauti  na mwenzake ambaye alikuwa ana jinsi ya kiume.

Ingawa mwenye mbuzi huyo (Bernado), alilielezea tukio hilo kama kitu cha kawaida, lakini baadhi ya wakazi wa kijiji hicho ambacho ni moja ya Visiwa ndani ya Ziwa Victoria eneo la Wilaya ya Bunda wanaliona kama moja ya matendo ya ushirikina hali iliyosababisha wazee wa kisiwa hicho kulikemea kwa kumtaka aliyefanya hivyo aache mara moja.

Kwa upande wake daktari wa mifugo wa wilaya hiyo, Dk Ndyanabo Tibaijuka alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo licha ya kusema hakuwa hajapata taarifa rasmi, lakini alisema kama limetokea ni jambo la kawaida katika maisha ya viumbe linalojitokeza wakati wa hatua za awali za uchanga wa mimba pindi viungo mbalimbali vya mwili vinapogawanyika ili kujiumba katika umbo linalotakiwa.

“Sijapata taarifa rasmi za tukio hilo; lakini kama limetokea hilo ni jambo la kawaida linalotokea katika hatua za awali za uchanga wa mimba viungo vinapojigawanyisha,”alisema Dk Ndyanabo.
Chanzo: Mwananchi

Wednesday, September 7, 2011

Wakutwa na heroine za bilioni 4/-

Best Blogger Tips
JESHI la Polisi Kitengo cha Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini, limewakamata watu watano akiwemo raia wa Iran, Ali Mirzael Pirbaksh, kwa tuhuma za kukutwa na kilo 97 za dawa hizo aina ya heroine zenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 4.4.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkuu wa Kitengo hicho Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Godfrey Nzowa, alisema kukamatwa kwa watuhumiwa hao kumetokana na taarifa walizopewa na raia wema.

Aliwataja watuhumiwa wengine kuwa ni Said Mrisho (31) wa Tandale, Aziz Kizingiti (32) wa Magomeni Mapipa, Abdul Lukongo (36) wa Kariakoo na Hamidu Karimu (43), wa Tandale.

Nzowa alisema watuhumiwa hao waliokuwa wamepakia dawa hizo ndani ya magari mawili, Toyota Carina namba T 954 BGT na Caldina namba T 107 BAS, walikamatwa jana saa 9.30 alifajiri eneo la Afrikana Mbuyuni, Kinondoni.

“Baada ya mimi kupewa taarifa za watu hao, nilichukua vijana wangu na kuwafuatilia taratibu katika maeneo waliyokuwa wakienda na hatimaye kuwakamata eneo hilo,” alisema Nzowa.

Alisema baada ya kuwahoji watuhumiwa hao, isipokuwa raia huyo wa Iran, ambaye ndiye anadaiwa kuingiza dawa hizo nchini, walidai kuwa zilikuwa mali ya Pirbaksh, ambaye hata hivyo hakuhojiwa baada ya kukosekana mkalimani.

Nzowa alisema watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani wakati wowote upelelezi wa tukio hilo utakapokamilika, huku akiwataka wananchi wanaojihusisha au kutumiwa kufanya biashara hiyo kuacha, ili kuepuka mkono wa sheria.

Aidha, aliwashukuru wananchi kwa ushirikiano wanaolipa Jeshi hilo katika kupambana na biashara hiyo haramu, huku akiwataka kuendelea kudumisha uhusiano huo hadi mapambano hayo yatakapofanikiwa.
Chanzo: HabariLeo

 

Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits