Wednesday, November 30, 2011

Wahusika wa kashfa ya BAE TZ kushtakiwa

Best Blogger Tips
Kampuni ya BAE Systems ya Uingereza
 Kundi la wabunge kutoka vyama mbali mbali vya siasa nchini Uingereza limetoa wito wa kufunguliwa mashtaka dhidi ya mtu yeyote aliyehusika katika kashfa ya ufisadi na rushwa kuhusiana na mauzo ya rada yaliyofanywa na kampuni ya vifaa vya ulinzi ya BAE Systems ya Uingereza.

Kampuni ya BAE Systems tayari imekubali kulipa takriban dola millioni 46 kama fidia kwa Tanzania kwa kukosa kuweka kumbukumbu zake za mahesabu kuhusiana na mauzo hayo yenye utata.

Lakini kamati ya maendeleo ya kimataifa ya bunge la Uingereza imeishutumu kampuni hiyo kwa kuchukua muda mrefu kurejesha kiasi cha fedha ilichozidisha katika mauzo ya rada hiyo.

Kiasi kikubwa cha fedha kilichotozwa na kampuni ya BAE system ya Uingereza iliyoiuzia Tanzania rada ya kijeshi kilichochea kufanyika kwa uchunguzi dhidi ya kampuni hiyo.

uchunguzi

Uchunguzi huo ulifanywa na Shirika la Kupambana na Ufisadi la Uingereza, Serious Fraud Office.

Mwaka jana, baada ya BAE kukiri kushindwa kutunza kumbukumbu zake kuhusu mauzo hayo, kampuni hiyo ilikubali kulipa kiasi cha dola milioni 46 kwa Tanzania kama fidia ya mauzo kutokana na ulaghai uliofanyika.

Fedha hizo zilikubalika zitumike kununulia vitabu vya shule na vifaa vingine.

Lakini bunge la Uingereza limesikitishwa kuwa fedha hizo bado hazijalipwa.

BAE systems inasema kwa sasa inawasiliana na shirika la misaada la kimataifa la Uingereza kuona namna fedha hizo zitakavyotumika.

Japokuwa BAE systems haikupatikana na hatia ya rushwa, lakini watu binafsi waliohusika na kashfa hiyo wanaweza kushitakiwa.

Wabunge wa Uingereza wamesema wako tayari kushirikiana na serikali ya Tanzania katika mahakama zake kuendesha mashtaka dhidi ya watu wanaohusika na ulaghai huo.
Chanzo: BBC

Saturday, November 19, 2011

Orodha ya watu matajiri Afrika yatolewa

Best Blogger Tips
Jarida la Forbes limechapisha orodha ya kwanza ya watu matajiri barani Afrika.

Wa kwanza ni mfanyabiashara kutoka Nigeria Aliko Dangote mwenye kumiliki kampuni za saruji ambao utajiri wake unazidi dola za kimarekani bilioni 10.

Nicky Oppenheimer mwenyekiti wa kampuni ya madini ya almasi nchini Afrika Kusini, De Beers ni wa pili.

Orodha hiyo ya Forbes ina majina ya watu 40 matajiri zaidi barani Afrika ambapo utajiri wa hao wote kwa pamoja unafikia zaidi ya dola bilioni 65.


40

Paul Harris

25061
39

Markus Jooste

26050
38

Mohamed Bensalah

27041
36

Cyril Ramaphosa

27559
36

Giovanni Ravazzotti

27568
34

Adrian Gore

28047
34

Strive Masiyiwa

28051
33

Michiel Le Roux

29062
31

Chris Kirubi

30070
31

Jannie Mouton

30064
30

Mohammed Indimi

33063
29

Abdulsamad Rabiu

400NA
28

Hakeem Belo-Osagie

45056
27

Gerrit Thomas (GT) Ferreira

46063
26

Uhuru Kenyatta

50050
25

Raymond Ackerman

54580
24

Oba Otudeko

55067
23

Samih Sawiris

56054
22

Alami Lazraq

57561
21

Theophilus Danjuma

60072
20

Stephen Saad

64047
19

Shafik Gabr

73059
18

Lauritz (Laurie) Dippenaar

75063
17

Jim Ovia

77557
16

Mohamed Al Fayed

1,30078
14

Yasseen Mansour

1,55050
14

Youssef Mansour

1,55066
13

Mohamed Mansour

1,70063
12

Anas Sefrioui

1,75054
11

Othman Benjelloun

2,40079
10

Patrice Motsepe

2,50049
9

Onsi Sawiris

2,60081
8

Christoffel Wiese

2,70070
7

Naguib Sawiris

2,90057
6

Miloud Chaabi

3,00082
5

Mike Adenuga

4,30058
4

Johann Rupert & family

4,70061
3

Nassef Sawiris

4,75050
2

Nicky Oppenheimer & family

6,50066
1

Aliko Dangote

10,10054

Monday, November 14, 2011

Mapigano ya kikabila nchini Libya

Best Blogger Tips
Mapigano Libya
Kumekuwepo na mapambano ya siku kadhaa kati ya makundi yanayokinzana katika mji wa mwambao wa Zawiya nchini Libya ambapo takriban watu 7 waliuawa.

Mwandishi wa BBC Karen Allen akiwa Libya anasema jamii zinazopingana zimekua zikipigania eneo ambalo zamani lilidhibitiwa na wafuasi wa kanali Gaddafi.

Hatahivyo serikali ya mpito imesema kwamba mapigano hayo yalisuluhishwa.

Wachambuzi wanasema mapigano hayo yanazusha masuala kadhaa kuhusu hali ya utulivu baada ya kuondoka kwa Gaddaffi nchini Libya.

Libya bado inakabiliwa na changamoto za kuenea silaha na vikundi vya watu wenye silaha baada ya uasi uliosababisha kuporomoka kwa utawala wa Kanali l Muammar Gaddafi.

Kiongozi wa utawala wa mpito Mustafa Abdul-Jalil alisema baraza la taifa la mpito limewakutanisha wazee kutoka maeneo yanayogombaniwa ya Zawiya na maeneo ya karibu ya makabila ya Warshefana - na kwamba mzozo huo umesuluhishwa mwishoni mwa wiki.

Hatahivyo baadhi ya watu wamearifu kuwa mapigano bado yalikuwa yanaendelea wakati akiongea.
Taarifa zaeleza kuwa mapigano yalianza pale wapiganaji kutoka Warshefana walipoweka kizuizi cha barabarani katika njia panda karibu na Zawiya, na kuwatambia wapiganaji kutoka mjini humo.

Wapiganaji kutoka Zawiya waliwashutumu wale kutoka Warshefana kuwa na ufungamano na utawala wa zamani.
Chanzo: BBC

Wednesday, November 9, 2011

Mke (60) amshitaki mume mwenye miaka 30

Best Blogger Tips
MWANAMKE mwenye umri wa miaka 60, mkazi wa Kibaoni mjini hapa, amewavunja mbavu wasikilizaji wa kesi katika Mahakama ya Mwanzo Ipembe, baada ya kumjibu Hakimu kuwa kijana aliyemfikisha mahakamani hapo si mwanawe bali mumewe.

Katika kesi hiyo, mwanamke huyo Asha Abdallah anamshitaki mumewe, Kiemi Itambu (30), kwa kumwibia Sh 30,000 alizokuwa ameficha chini ya godoro.

Wawili hao wakiwa kizimbani jana, Hakimu Hosea Mkude alimwuliza mke: “Kwa nini wewe bibi unaolewa na kijana ambaye ana umri wa mwanao, huoni aibu?

Asha alijibu: “Mheshimiwa, huyu ni mtoto kwa mama yake aliyemzaa, kwangu ni mume wangu halali ambaye ananitimizia mahitaji yangu yote muhimu.”

Kama vile jibu hilo halikutosha, Asha aliendelea ‘kumpasha’ hakimu: “Kwanza kwa taarifa yako, wako wanawake wengi tu hapa mjini walioolewa na vijana, tena wengine wana vijana wenye umri unaofanana na wa wajukuu zao. Sembuse miye?”

Majibu hayo yalisababisha watu waliojazana kwenye chumba hicho cha Mahakama, washindwe kujizuia na kuangua vicheko.

Ilidaiwa mahakamani hapo, kuwa mshitakiwa Kiemi alitenda kosa hilo Novemba 3, saa mbili asubuhi Kibaoni mjini hapa.

Asha alidai mahakamani hapo kuwa mumewe amekuwa na tabia ya kumwibia Sh 100, 200 na 500, lakini safari hii alivuka mpaka kwa kuiba Sh 30,000 ndiyo maana akaamua kumfikisha mahakamani.

Mshitakiwa alikana mashitaka na yuko nje baada ya kujidhamini mwenyewe kwa ahadi ya kutoa Sh 50,000 hadi Novemba 15 kesi hiyo itakapotajwa.
Chanzo: BBC

Monday, November 7, 2011

Daktari wa Michael Jackson hatiani

Best Blogger Tips
Daktari binafsi wa Michael Jakson, Dk Conrad Murray amekutwa na hatia ya kosa la mauaji bila kukusudia na mahakama moja mjini Los Angeles, Marekani.

 Baraza la wazee wa mahakama - wanaume saba na wanawake watano - walichukua siku mbili kujadili kesi na kufikia hukumu hiyo.

Michael Jackson alifariki Juni 25 mwaka 2009 kutokana na kuzidisha kipimo cha dawa ya usingizi.

Adhabu 

Murray, 58, anaweza kukabiliwa na adhabu kamili ya kwenda gerezani kwa miaka minne na kupoteza leseni yake ya uganga.

 Wanasheria wa Dk Murray walihoji kuwa Michael Jackson alijidunga mwenyewe dawa hiyo wakati daktari wake akiwa nje ya chumba.

Dk Murray alipelekwa rumande baada ya kukutwa na hatia na atasalia huko hadi wakati atakaposomewa adhabu yake, inayotarajiwa kutolewa Novemba 29.

Akielezea uamuzi wake, jaji alisema Dk Murray kwa sasa ni mhalifu aliyekutwa na hatia na kwa kuwa anafahamiana na watu nje ya jimbo la California, inamaanisha hakuna uhakika kuwa daktari huyo ataweza kubakia bila kutoka katika jimbo hilo.

Rumande  

Dk Murray alibaki kimya mahakamani hapo, akijisogeza kidogo katika kiti chake wakati hukumu ikisomwa.

Maafisa wa mahakama walianza kumfunga pingu daktari huyo wakati jaji akikamilisha kusoma hukumu, na baadaye kupelekwa rumande.

Baraza la wazee - lililoundwa na wazungu weupe sita, Mmarekani mweusi mmoja na Wamarekani watano wenye asili ya Hispania - walijadili shauri hilo kuanzia Ijumaa hadi Jumatatu asubuhi.

Nje ya mahakama, mashabiki wa Michael Jackson walikuwa wakishangilia na kuimba "Hatia! Hatia!" muda mfupi kabla ya hukumu kusomwa.

Wakati wa wiki sita za kusikilizwa kwa kesi hiyo, mashahidi 49 na zaidi ya vipande 300 vya ushahidi viliwasilishwa mahakamani hapo.

Michael Jackson ambaye alikuwa kimya katika ulimwengu wa sanaa kwa miaka kadhaa, alikufa mwaka 2009 wakati akijiandaa kufanya mfululizo wa maonesho katika ukumbi wa 02 jijini London.

Kuwa na baba

Katika hoja za mwisho mahakamani siku ya Alhamisi, upande wa mashtaka ulisema Dk Murray alisababisha kifo cha nyota huyo kutokana na uzembe, na hivyo kuwanyima watoto wa Jackson haki ya kuwa na baba.

Upande wa utetezi ulihoji kuwa Jackson alikuwa amejizoesha kutumia dawa, kitu ambacho kilisababisha kifo chake kutokana na kujipa kiwango kikubwa cha dawa ya kulevya huku daktari wake akiwa nje ya chumba katika jumba alilokuwa amekodi nyota huyo mjini Los Angeles.
Chanzo: BBC


Joe Frazier aumwa saratani ya ini

Best Blogger Tips
Joe Frazier
 Bingwa zamani wa ndondi za uzito wa juu duniani Joe Frazier yupo katika nyumba wanayouguzwa wagonjwa mahututi akiwa anaumwa saratani ya ini, meneja wake amesema.

Amesema Frazier - anayejulikana pia kwa jina la Smokin' Joe - aligunduliwa anaumwa saratani wiki kadha zilizopita.

"Nitakuwa muongo iwapo sitawaeleza kwamba hali yake si nzuri," Leslie Wolf alilieleza shirika la habari la Uingereza la Reuters.

Frazier mwenye umri wa miaka 67 alishikilia mkanda wa ubingwa wa dunia miaka kati ya 1970 na 1973. Alikuwa ndiye mtu wa kwanza kumchapa Muhammad Ali mwaka 1971. Baadae akachapwa na Ali katika mapambano mawili yaliyofuatia.

Bw Wolf amesema Frazier aligunduliwa na maradhi ya saratani ya ini mwezi uliopita na kwa sasa anatibiwa katika nyumba maalum inayotunza wagonjwa mahututi huko Philadelphia.

"Joe ni mpiganaji. Joe kamwe hashindwi," meneja huyo alisema, akaongeza madaktari na watu wa karibu wa Frazier "tunafanya kila jitahada".

Frazier alishinda taji la ubingwa wa dunia kwa uzito wa juu mwaka 1970 baada ya kumtwanga Jimmy Ellis mjini New York. Aliendelea kushikilia taji hilo hadi mwaka 1973, ambapo alipigwa na George Foreman.

Lakini mwanamasumbwi huyo huenda anafahamika zaidi kwa mapambano makubwa na Ali, likiwemo lile la kukata na shoka la Phillipines lililopewa jina la Thriller in Manila mwaka 1975.

Friday, November 4, 2011

Ferguson asherehekea miaka 25 Man U

Best Blogger Tips
Sir Alex Ferguson

Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson anasherehekea miaka 25 na timu hiyo.

Ferguson ameeleza miaka hiyo 25 akiwa na mashetani wekundu ni kama hadithi nzuri.

Katika miaka hiyo yote mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 70 ameisaidia Man U kushinda kombe la Premier mara 12, kombe la FA mara tano na Ligi ya mabingwa bara Ulaya mara mbili
.
Licha ya mafanikio hayo, Ferguson amekuwa hapendelei sana kuzungumzia sifa hizo.

Na hata anapoulizwa kuhusu mafanikio yake Man United , Meneja huyo huanza na usemi wake wa kawaida " Sitazungumzia swala hilo".

Lakini mwaka jana akiwa na umri wa miaka 69 alizungumzia kwa muda enzi zake na mafanikio yake tangu alipochukuo uongozi wa Man U Novemba 6 mwaka 1986 kutoka kwa Ron Atkinson.

Kutoka mwaka huo Ferguson amenyakuwa mataji 27 na kushuhudia miamba wengi wakikuza vipaji vyao wakiwa klabu cha Man United.

Kwa wakati huu litakaloangaliwa ni muda gani Fergerson atabakia kuwa kileleni mwa timu hiyo, swali ambalo amenukuliwa akijibu kwa kusema " ataendelea ilimradi afya yake inamruhusu kufanya hivyo"
Chanzo: BBC

Thursday, November 3, 2011

Serikali yakataa ushoga

Best Blogger Tips
TANZANIA imesema ipo tayari kukosa  misaada yote kutoka Serikali ya Uingereza  na kamwe haiwezi kuruhusu sheria inayotambua mashoga na kuhalalisha ndoa za jinsia moja.Msimamo huo mzito wa serikali umekuja siku chache baada ya Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, kutamka kwamba nchi yake ina mpango wa kusitisha misaada yake kwa nchi ambazo sheria na katiba zao, hazitambui mashoga na ndoa za jinsia moja.

Cameron alikaririwa akithibitisha kuwa tayari amewajulisha juu ya suala hilo Wakuu  wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola waliokuwa wakihudhuria mkutano wa Jumuiya hiyo uliomalizika siku nne zilizopita,  mjini Perth , Austaralia ambao pia ulihudhuriwa na Rais Jakaya Kikwete.

Waziri Mkuu huyo kutoka chama cha Conservative ambacho kilishinda uchaguzi Mei mwaka jana, alisema  suala hilo la mashoga na ndoa za jinsi moja ni moja ya mambo yanayoongoza sera ya serikali yake kuhusu misaada kwa mataifa mbalimbali na kwamba tayari imeanza kutekelezwa katika maeneo kadhaa duniani.

Kauli ya Cameron imechukuliwa kama kielelezo cha ukoloni mamboleo ambao Uingereza inajaribu kuupandisha daraja  kwa mataifa yanayoendelea kwa kigezo cha misaada  

Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe,  alisema pamoja na umasikini wake, Tanzania kamwe haitaruhusu upuuzi huo kwa kigezo cha misaada.

“ Tanzania ni nchi maskini lakini hatutakubali kuruhusu upuuzi huo eti kwa sababu ya misaada yake na fedha zao, lakini ushoga si utamaduni wetu, hata sheria zetu zinakataa,” alisema Membe.

Alifafanua kuwa katika kuonesha msimamo wa kutokukubaliana na masharti hayo, Tanzania imeshikilia msimamo thabiti kupinga  upuuzi huo ambapo  Januari mwaka huu,  ilimkataa balozi shoga ambaye aliteuliwa na nchi yake kuja kuiwakilisha hapa  nchini. Hata hivyo Waziri Membe hakutaja jina la balozi huyo wala nchi  anayotoka.

“Niwape siri moja ambayo tuliificha lakini leo ngoja niwaambie, mwanzoni mwa mwaka jana nililetewa barua  kunijulisha ujio wa balozi mmoja anayekuja kuiwakilisha nchi yake, mwanamume mwenye ndoa ya jinsia moja. Nilikwenda kumweleza Rais Jakaya Kikwete kuhusu wasifu wa balozi huyo mtarajiwa naye akajibu kwa maneno matatu, yarabi toba! Mkatae!” 

Waziri Membe alifafanua kuwa serikali ilimkataa balozi huyo kwa kuwa ni kinyume cha utamaduni wetu na sheria za nchi kuwa na watu wenye tabia hizo.

Alisema alimjulisha waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo kwamba balozi huyo haruhusiwi kuja kufanya kazi nchini kwa kuwa ni kinyume na utamaduni wetu.  “ Waliendelea kuniomba kwamba balozi huyo akija hatatoka kwenye makazi yake akiwa na mwenza wake hivyo watu hawatamuona lakini tulimkataa kabisa, wakatuelewa,” alisema Membe.

 Alieleza kuwa  tamko hilo la Waziri Mkuu Cameron linaweza kusababisha hatari ya kuvunjika kwa uhusiano miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola na koloni mama  Uingereza na waziri huyo atabeba lawama hizo

 Akisisitiza msimamo huo wa serikali, Membe,  alisema  Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 kifungu cha tisa, kinatambua ndoa ya jinsia mbili tofauti,  yaani mume na mke.  “ Sheria hizi tunazozitumia hivi sasa tumezirithi kutoka Uingereza ambako leo wanatukuza ndoa za jinsia moja na ushoga,” alisema Membe.

Suala la kile kinachoitwa haki za binadamu kuhusu ushoga ilikuwa moja ya ajenda ambazo viongozi kadhaa walishindwa kuafikiana katika mkutano  Perth .

Hoja ya  kukomesha vizuizi dhidi ya ushoga na ndoa za jinsi moja lilikuwa moja ya mapendekezo yaliyokuwamo katika ripoti ya ndani kuhusu matarajio ya baadaye ya Jumuiya hiyo ya Madola.
  
Itakumbukwa kwamba, Malawi tayari imeathirika na mpango huo wa Uingereza kwa sehemu ya misaada yake kusitishwa kutokana na msimamo wa nchi hiyo kuhusu kile Uingereza na nchi za Magharibi zinazokiita haki za mashoga. Ikumbukwe pia kuwa, mjadala mzito ulioibuka katika Bunge la Uganda mwaka 2009 kuhusu ndoa za jinsi moja ilikuwa sehemu ya utekelezaji wa sera hiyo ya Uingereza na washirika wake.

  Ajenda zingine Mkutano wa Perth   Waziri Membe alisema viongozi wa Jumuiya ya Madola walikubaliana suala la mabadiliko ya tabia nchi kuwa ajenda kuu katika nchi hizo.

Alisema ajenda hiyo sasa inakuwa muhimu kutokana na nchi nyingi wanachama wa jumuiya hiyo kuwa katika tishio kubwa la uharibifu wa mazingira.

Aidha, Membe alisema nchi hizo zimekubaliana kuandaa kanuni na mwongozo ambao utatakiwa kufuatwa na nchi za jumuiya hiyo.

“ Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Jumuiya ya Madola tutakutana Aprili mwakani kuandaa miongozo na kanuni hizo,” alisema Membe.
Source: Mwanachi

Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits