Saturday, July 30, 2011

Iringa inaongoza kwa VVU

Best Blogger Tips
Sehemu ya mji wa Iringa
WAZIRI wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hadji Mponda, ameutaja mkoa wa Iringa kuongoza nchini kwa maambukizi ya virusi vya ukimwi.

Kauli hiyo aliitoa jana bungeni alipokuwa akijibu swali la mbunge wa Masasi, Mariam Kasembe (CCM), aliyetaka kujua ni mashirika mangapi kutoka nje ambayo yanatoa misaada nchini kwa ajili ya kupambana na janga la ukimwi.

Aidha mbunge huyo alitaka kujua hali ya maambukizi ya virusi vya ukimwi nchini ikoje kwa sasa na takwimu za mikoa ambayo inaongoza na ambayo ina hali nzuri.

Dk. Mponda alisema kuwa kwa sasa mashirika ya nje 16 ndiyo yanayotoa msaada dhiti ya vita ya ukimwi nchini na kwamba mashirika hayo hutoa misaada ya kifedha na kiufundi katika kutekeleza afua mbalimbali zinazolenga kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU) na kutoa huduma kwa wale wanaoishi na VVU.

Alisema baadhi ya afua zinazotolewa ni pamoja na uzuiaji wa maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT), huduma ya ushauri nasaha na upimaji wa VVU, kuelimisha jamii katika masuala mbalimbali ya ukimwi.

Alizitaja huduma nyingine kuwa ni pamoja na huduma za kimaabara, matibabu ya magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya ngono, kusambaza kondom na kutoa huduma ya tohara kwa wanaume.

Aidha alisema kuwa ripoti ya tafiti ya viashiria vya VVU na malaria ya mwaka 2008 inaonyesha hali ya maabukizi ya VVU kwa ujumla ni asilimia 5.7 hali ya maambukizi inatofautiana miongoni mwa watu na katika makundi tofauti.

Dk. Mponda alisema kuwa maambukizi yapo zaidi kwa wanawake ambayo ni asilimia 6.8 tofauti na wanaume ambao ni asilimia 4.7, wakati mjini maambukizi ni asilimia 8.7 na vijiji ni asilimia 4.7.

Alisema katika suala la kijiografia mkoa wa Iringa ndio wenye maambukizi ya juu ukiwa na asilimia 14.7 na mikoa yenye maambukizi ya chini ni Kigoma, Arusha, Kilimajaro na Manayara ikiwa na asilimia 2.
Source: Tanzania Daima

Mbunge aliyeghushi saini ya Pinda abainika

Best Blogger Tips
Jengo la Bunge, Dodoma
Sakata la kughushi saini limeingia katika sura mpya baada Ofisi ya Bunge kumpata Mbunge aliyefanya kitendo hicho na jina lake kukabidhiwa kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Akizungumza na NIPASHE jana, Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel, alisema mbunge huyo alipatikana juzi jioni na jina lake lilikabidhiwa kwa Waziri Mkuu siku hiyo hiyo.

Alisema walilikabidhi jina hilo kwa Waziri Mkuu ili aamue kama atamchukulia hatua ama la na kwamba wamefanya hivyo kwa sababu hakuna mtu aliyelalamikia tukio hilo.

“Hakuna hatua tutakayomchukulia kwa sababu hakuna mtu aliyekuja kulalamikia kwetu na jina la mbunge aliyegushi tumekabidhi kwa Waziri Mkuu ataamua yeye mwenyewe hatua gani atamchukulia,” alisema Joel.

Hata hivyo, alikataa kutaja jina la mbunge huyo wala chama chake. “Siwezi kukuambia jina wala chama anachotoka," alisema Joel.

Hata hivyo, chanzo kimeidokeza NIPASHE kuwa mbunge huyo ni wa jimbo moja la Mkoa wa Rukwa.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mmoja wa baadhi ya wabunge ambao mbunge huyo hukaa nao jirani ndani ya ukumbi wa Bunge, alishauriwa kutokufanya hivyo, lakini alibisha.

“Tulimuona wakati akiandika barua ile na kuweka sahihi na tukamshauri tukamwambia Waziri Mkuu ana mamlaka ya juu sana huwezi kumfanyia mchezo halafu Selasini (Joseph Mbunge wa Rombo Chadema) si mtani wake, lakini yeye aliendelea na msimamo wake ndiyo yakampata haya,” alisema mbunge huyo. 

Jumatano iliyopita, muda mfupi kabla ya kuahirishwa kikao cha Bunge cha jioni, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, alisimama na kuomba mwongozo wa Mwenyekiti wa Bunge kuhusu baadhi ya wabunge kuwaandikia wenzao barua wakitumia jina la WaziriMkuu Pinda.

”Mheshimiwa Mwenyekiti, umeibuka mtindo kwa baadhi ya waheshimiwa wabunge kuandika vimemo kwenda kwa wenzao wakiwahadaa kuwa wanaitwa na Waziri Mkuu kwa majadiliano muhimu. Vimemo hivyo hughushiwa jina na sahihi ya Waziri Mkuu. Hii si tabia nzuri hata kidogo.

Mfano wa sasa hivi Mheshimiwa Selesini aliandikiwa kimemo kama hicho na alipoinukana kumfuata Waziri Mkuu, alimkuta anafuatilia kwa makini hoja za Waziri wa Kilimo,” alisema Lukuvi na kuongeza:
“Ilibidi Mheshimiwa Selasini aendelee kusimama pale kwa adabu na kwa muda mrefu hadi Waziri Mkuu alipomwambia kuwa memo hiyo hakuandika yeye. Naomba mwongozo wako Mheshimiwa Mwenyekiti kwa suala hili.”

Bajeti ya Marekani yakwama

Best Blogger Tips
Mjadala kati ya wanasiasa, kuhusu bajeti, na jinsi ya kuzidisha kiwango cha mkopo wa serikali ya Marekani umekwama.

Ufumbuzi unatakiwa ufikiwe kabla ya Jumanne, ambapo Wizara ya Fedha itaanza kupungukiwa na fedha za kulipia matumizi ya serikali.

Ijumaa usiku, baraza la wawakilishi, ambalo wabunge wake wengi ni kutoka chama cha Republican, lilipitisha mswada kuzidisha kiwango cha mkopo na kupunguza matumizi ya serikali, lakini mswada huo ulikataliwa na baraza la Senate, lenye wajumbe wengi wa chama cha Democrat.

Hali ya uhasama na mashindano imetanda Washington huku Jumaane inakaribia.

Wanasiasa bado wanavutana wakati wanahitaji kupatana ili kuepuka wasi-wasi na pengine matafaruku katika uchumi wa Marekani, ikiwa muafaka haukufikiwa kabla ya tarehe ya mwisho, yaani tarehe mbili Agosti.

Mswada uliopendekezwa na wabunge wa chama cha upinzani cha Republican Ijumaa, katika baraza la wawakilishi, ulizimwa katika baraza la Senate, ambako wajumbe wa chama cha Democrat sasa wanashindana na upinzani, na wanajaribu kusukuma mbele pendekezo lao wenyewe.

Lakini mswada huo piya, uliopendekezwa na kiranja wa chama cha Democrat, Harry Reid, unafanyiwa kazi ili ukubalike kwa wengi.

Vikao kati ya wanasiasa vitaendelea weekendi nzima na huenda makubaliano yakafikiwa dakika ya mwisho, na hatimaye kuwatuliza raia na masoko.

Friday, July 29, 2011

Soulja Boy's 21st Birthday Gift To Self -- $55 Million G5 Jet

Best Blogger Tips
Soulja Boy
 Most young adults would be content celebrating their 21st birthday with a trip to Las Vegas, but rap superstar Soulja Boy had a grander idea.

For his 21st birthday Thursday, the Atlanta rapper bought himself a $35 million dollar private jet, a rep from his management team reportedly told TMZ.

But apparently, the G5 jet needed some "Pretty Boy Swag" upgrades. According to reports, Soulja will be spending an additional $20 million dollars to add flat screen TVs, 4 liquor bars, a dozen Italian leather seats, Brazilian hardwood cabinets, and travertine tiled flooring.

The restroom will be remolded and enlarged, and the aircraft will get a new custom paint job featuring his logo.

A spokesperson for Soulja Boy had not responded to our request to confirm the jet purchase by press time.

On Friday, the "Crank That" rapper, will host a birthday extravaganza in Miami believed to cost $300,000. Sean Kingston, Bow Wow, and Dwight Howard are expected to attend. The event will be streamed live from SouljaBoyBirthdayBash.com at 11 p.m. eastern.

In April, Soulja Boy told Hip Hop Media Training that he was planning to team up with MTV for a Las Vegas-based bash. "MTV [is going to] be doing my birthday party. It's going to be in Vegas. I'm going to be in Vegas," Soulja Boy said. "MTV is going to be doing it just like I did my swag eighteenth party. I don't know. It's going to be my first time being 21. So I'm just gonna do me."

Tuesday, July 26, 2011

Cocain ya mil. 700 yabambwa Tanga

Best Blogger Tips
POLISI Mkoa wa Tanga kwa kushirikiana na Kikosi Maalumu cha Kupambana na Dawa za Kulevya, kimekamata dawa za kulevya aina ya Cocaine zenye thamani ya sh. milioni 700 ndani ya basi Raha leo na Tawaqal.

Dawa hizo zilikamatwa katika matukio mawili tofauti baada ya Kikosi cha Kupamba na Dawa za Kulenya kuwatilia shaka watuhumiwa hao.

Kwa mujibu wa Mkuu Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga, Bw. Jafary Mohamed, watu saba wanashikiliwa katika matikio hayo.

Alisema kuwa tukio la kwanza lilitokea Jumamosi ndani ya basi la Raha Leo katika eneo la Kabuku ambapo polisi iliwakamata watuhumiwa watatu wakiwa na kilo 12 za Cocain.

Kukamatwa kwa dawa hizo kutokana na mtego uliowekwa na kikosi hicho kwa kuwatilia shaka baadhi ya watu akiwemo mfanyabiashara mwenye asili ya Kiasia mkazi wa Magomeni, Dar es Salaam.

Mkuu huyo wa upelelezi alisema mfanyabiashara huyo alikamatwa Jumamosi saa 5:30 asubuhi, katika kizuizi cha Polisi Tanga baada ya kupekuliwa na kukutwa na baadhi ya dawa kwenye mfuko.

Alisema kuwa kikosi hicho, kilifuatilia nyendo za mfanyabiashara huyo ambaye alionekana katika Kituo Kikuu cha cha Mabasi Tanga na akimkabidhi mkazi mmoja wa Pongwe begi lililokuwa na dawa na kupanda basi la Raha Leo lililokuwa likitoka Mombasa kwenda Dar es Salaam.

Mfanyabiashara huyo alianza safari akiwa nyuma ya basi hilo akiwa kwenye gari ndogo aina ya Baloon.

Hata hivyo, basi hilo lilikamatwa baada ya kufika kwenye mizani ya Tanga na katika upekuzi walibaini kuwepo kwa dawa hizo kwenye begi.

Alisema mfanyabiashara huyo alikamatwa akiwa na mifuko mikubwa 12 ya dawa za kulevya.

"Ni mapema kuwataja majina yao kwa kuwa bado kuna watuhumiwa wengine tunaendelea kuwatafuta kutokana na kushiriki kwenye uuzaji na usambazaji wa dawa hizo," alisema Bw. Mohamed.

Alisema katika tukio la pili, jeshi hilo linawashikilia watuhumiwa wanne wakisafirisha dawa za kulevya kwenye basi la Tawaqal kutoka Dar es Salaam kwenda Mombasa.

Alisema watuhumiwa hao walikamatwa na kilo tatu na mara baada ya kukamilika kwa upelelezi watafikishwa mahakamani.
Source: Majira

Monday, July 25, 2011

Kikwete apunguza maofisa anaosafiri nao nje

Best Blogger Tips
RAIS Jakaya Kikwete ameridhia idadi ya maofisa katika ziara zake za nje ipunguzwe ikiwa ni hatua ya kupunguza gharama.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe aliliambia Bunge mwishoni mwa wiki wakati akijibu hoja ya kambi ya upinzani iliyoendelea kutaka safari za nje kwa viongozi zipunguzwe.

Membe alisema katika safari ya hivi karibuni ya Rais Kikwete nchini Shelisheli, idadi ya maofisa alioongozana nao ilikuwa 34 na kwa safari ya Afrika Kusini ilikuwa 34.

Hata hivyo, Waziri Membe alisema wakati mwingine, wingi wa maofisa huzingatia na aina ya ziara na nchi anakokwenda.

Alitoa mfano kwamba, endapo anakwenda nchi ambayo ulinzi wake upo shakani, idadi inaweza kuongezeka.

Alisema, zipo ziara nyingine kama vile za kibiashara inawezekana akalazimika kuongozana na ujumbe wa wafanyabiashara.

Awali, katika kuchangia hotuba ya makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara yaliyopitishwa, kambi hiyo ya Upinzani kupitia kwa Waziri Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Ezekia Wenje ilisema safari za viongozi wa juu zinatakiwa ziendane na hali ya uchumi.

Wenje alisema katika dhana ya kupunguza matumizi, baadhi ya safari za nje ambazo siyo lazima mkuu wa nchi kwenda, awaachie viongozi wengine washiriki kwa kuwa msafara wa Rais nje ya nchi una gharama kubwa ikilinganishwa na mawaziri au maofisa wengine wa Serikali.

“Kambi ya Upinzani inaitaka wizara ikishirikiana na ofisi ya Rais kuweka utaratibu wa safari za viongozi nje ya nchi, ili kupunguza matumizi makubwa ya Serikali na hatimaye fedha hizo zielekezwe katika miradi mbalimbali ya maendeleo,” alisema Wenje.

Hata hivyo, Serikali imekuwa ikisisitiza kwamba safari za Rais Kikwete nje ya nchi ni zenye manufaa na imekuwa ikitoa mafanikio ya ziara hizo katika nchi mbalimbali duniani.

Kwa mfano, Marekani ambako Rais Kikwete amekuwa na ziara tangu wakati wa utawala wa Rais George W. Bush na sasa Rais Barack Obama, Tanzania imenufaika kwa kupatiwa fedha nyingi katika miradi ya barabara, umeme, afya na maji.
Chanzo: HabariLeo

Gamba laivuruga CCM

Best Blogger Tips
 Nape Nnauye

MPANGO mkakati wa kujivua gamba kwa lengo la kurejesha uhai ndani ya CCM unaelekea kuwa bomu la maangamizo kwa chama hicho, baada ya baadhi ya wenyeviti wa mikoa kuupinga huku wakiagiza wafuasi wao kuwashusha majukwaani makada wanaoupigia debe.Wakati wenyeviti hao wakiupinga, Baraza Kuu la Umoja wa Vijana CCM (UVCCM), jana limetoa tamko rasmi la kuunga mkono ziara hizo zinazofanywa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa chama hicho, Nape Nnauye za kutekeleza mkakati huo.

Mpango huo wa kujivua gamba ulitangazwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete katika maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa chama hicho kikongwe barani Afrika, lakini jana baadhi ya wenyeviti wake wa mikoa akiwamo, John Guninita wa Dar es Salaam na Hamis Mgeja wa Shinyanga, waliupinga wakisema unamwaga sumu kali dhidi ya chama.

Msimamo wa UVCCM

Baraza Kuu la UVCCM limetoa msimamo wake kuunga mkono ziara za mikoani zinazoongozwa na Nnauye za kujivua gamba huku likiweka bayana kuwa huo ni msimamo wa Halmashauri Kuu (Nec) ya chama na si wa Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi.

Mbali na Nape, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka wamekuwa wakifanya ziara mikoani hasa katika mwisho wa wiki ambazo pamoja na mambo mengine, wamekuwa wakifanya mikutano ya kukipa uhai chama huku wakitangaza uvuaji gamba.

Kaimu Mwenyekiti wa UVCCM, Benno Malisa alisema UVCCM ilipongeza uamuzi wote wa NEC: "Kila kinachofanyika ni sahihi na sisi tunaunga mkono kabisa."
Endelea kusoma habari hii.................

Mwakiteleko taa iliyozimika ghafla - Lowassa

Best Blogger Tips
Via Majira

WAZIRI Mkuu wa zamani, Bw. Edward Lowassa jana alikuwa miongoni mwa mamia ya watu waliofika nyumbani kwa Naibu Mhariri Mtendaji wa New Habari 2006, Marehemu
Danny Mwakiteleko aliyefariki dunia juzi na kusema kuwa waandishi wa habari nchini wamepoteza kiungo mahimu katika tasnia ya habari nchini.

Bw. Lowassa aliyeongozana na mkewe, Regina Lowassa, alisema Bw. Mwakiteleko ni taa yenye mwanga iliyozimika ghafla.

Akizungumza na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nyumbani kwa Marehemu, Tabata Chang'ombe, Dar es Salam jana, Bw. Lowassa alisema Marehemu Mwakiteleko alikuwa mwandishi makini aliyefanya kazi yake kwa ajili ya maslahi ya Taifa.

Alisema wahariri, jamii na Taifa kwa ujumla wamepoteza mwandishi mahili aliyesimama imara kutetea jamii kupitia kalamu yake.

"Mimi binafsi na familia yangu, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo langu la Monduli, tunaipa familia yake pole nyingi. Naomba Mwenyezi Mungu awape nguvu na faraja ya kweli hasa katika kipindi hiki cha majonzi," alisema.

Aliwataka waandishi wa habari nchini kuiga mfano wa uandishi wa marehemu Mwakiteleko.


Kibanda kuwakilisha wahariri

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanazania (TEF), Bw. Absalom Kibanda atawakilisha wahariri wenzake katika msafara wa mazishi ya Marehemu Mwakiteleko mkoani Mbeya.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Katibu wa TEF, Bw. Neville Meena ilisema kuwa katika msafara huo, Bw. Kibanda ataambatana na mwakilishi wa jukwaa hilo kutoka Zanzibar ambaye jina lake halikutajwa.

Bw. Mwakiteleko alifariki dunia saa 10 alfajiri, Jumamosi Julai 23, 2011 kufuatia majeraha aliyoyapata kichwani kwenye ajali ya gari Julai 20, 2011 katika eneo la Tabata TIOT saa nne usiku alipokuwa akirejea kutoka kazini.
Endelea kusoma habari hii.......................

Saturday, July 23, 2011

Gaidi wa Norway

Best Blogger Tips
Anders Behring Brevik
Polisi wa Norway wamemshtaki Anders Behring Brevik akituhumiwa kuhusika na mashambulio mawili yaliyotokea Ijumaa.

Yale yanayojulikana kuhusu Brevik ni yale yaliyochapishwa katika tovuti za mawasiliano kama Twitter na Facebook - na haya yanaonesha yaliandikwa siku chache tu zilizopita.

Polisi wanasema maandishi yake kwenye mtandao wa internet, yanaonesha alikuwa na msimamo wa mrengo wa kulia na alikuwa dhidi ya Waislamu.

Kwenye Facebook alijielezea mwenyewe kuwa Mkristo na wa mrengo wa kulia.

Picha yake kwenye Facebook inaonesha mwanamme mwenye nywele za "blond" na macho ya buluu.
Inafikiriwa Bwana Brevik alikulia mjini Oslo.

Baadae alihama mjini na kuanzisha kampuni yake, iitwayo Brevik Geofarm.

Taarifa zinasema kampuni hiyo ilianzishwa ili kulima mboga.

Vyombo vya habari vya Norway vinafikiri alitumia kampuni hiyo kununua mbolea, ambayo inaweza kutumiwa kutengeneza mabomu.

Gazeti la Norway la Verdens Gang, linamnukuu rafiki yake akisema kuwa mshukiwa alipokuwa anakaribia mika 30, alibadilisha msimamo wake na kuwa na mawazo makali ya mrengo wa kulia.

Piya alishiriki katika tovuti zinazohusu msimamo mkali wa kizalendo.

Pumzika Kwa Amani Danny Mwakiteleko

Best Blogger Tips

Naibu Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Habari Corporation inayochapisha magazeti ya Mtanzania, Bingwa, Dimba, The African na Rai, Danny Mwakiteleko amefariki dunia.

Mwakiteleko amefariki dunia saa moja asubuhi ya leo (Jumamosi Julai 23) katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kufuatia ajali mbaya ya gari aliyoipata Julai 19, mwaka huu saa 5 usiku wa maeneo ya Tabata ya TIOT, jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoka kazini kurudi nyumbani kwake, Tabata ya Baracuda.

Marehemu, akiwa kwenye gari lake aina ya Nadia, aliingia nyuma ya lori lililokuwa limeegeshwa kando ya barabara.

Baada ya ajali hiyo, marehemu alipelekwa  Hospitali ya Wilaya ya Ilala, Amana ambako madaktari waliamua kumkimbiza Muhimbili kwa sababu hali yake ilikuwa mbaya.

Jana Ijumaa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Kikwete alimtembelea marehemu wodini Muhimbili alikolazwa kwa lengo la kumjulia hali.

Msiba upo nyumbani kwa marehemu, Tabata Baracuda ambako pia mipango ya mazishi inafanywa.

Marehemu ni mwenyeji wa Mkoa wa Mbeya, ameacha mke na watoto wawii, mmoja anasoma kidato cha pili, mwingine darasa la tano.

Watu 92 wameuwawa Norway

Best Blogger Tips
Polisi nchini Norway sasa wanasema kuwa mtu aliyekuwa na bunduki aliyefyatua risasi katika mkusanyiko wa vijana katika kisiwa chenye kambi ya vijana nje ya mji mkuu, Oslo, Ijumaa jioni, alisababisha vifo vya watu 85.

Awali mlipuko wa bomu ulikuwa umesababisha vifo vya watu saba.

Polisi wamemfungulia mashtaka raia mmoja wa Norway, mwenye umri wa miaka 32, kwa kutekeleza mashambulio yote mawili.

Mtu huyo aliyekuwa amevaa mavazi ya afisa wa polisi wakati wa kufanya mashambulio hayo, alikamatwa katika kisiwa kidogo cha Utoeya, baada ya kufyatua risasi ovyo kwa kipindi cha saa nzima.

Waziri mkuu Jens Stoltenberg amesema watu wengi bado wanaendelea kuwatafuta watoto wao kufuatia mashambulio hayo.

Waziri mkuu alisema hayo kufuatia kuwatembelea walioathiriwa na vile vile jamaa zao.

Kiongozi huyo alikuwa ameandamana na Mfalme wa Norway, Harald na Malkia Sonja, na vile vile mwanamfalme Haakon, walipoutembelea mji wa Sundvollen, karibu na kisiwa cha Utoeya.

Mtu aliyekamatwa amehusishwa na makundi yenye itikadi za siasa kali.

Anders katika Facebook anasema yeye ni Mkristo
Jina lake ni Anders Behring Breivik.

Polisi usiku mzima wamekuwa wakiikagua nyumba anayoishi mjini Oslo, na bado wanaendelea kumhoji.

Mwandishi wa BBC Richard Galpin, anasema Norway imekuwa na matatizo ya kisasa yanayotokana na makundi yanayounga mkono siasa za ki-Nazi, lakini raia wengi wamekuwa wakiamini kwamba makundi mengi ya aina hiyo yamekomeshwa.

Polisi wanaendelea kuchunguza iwapo alitekeleza mashambulio hayo kama mtu binafsi, au alisaidiwa na makundi fulani.
Source: BBC

Amy Whinehouse amefariki

Best Blogger Tips
Amy Winehouse
Mwimbaji maarufu mwanamke wa Uingereza, Amy Winehouse, amekutwa amekufa katika fleti yake mjini London.

Alikuwa na umri wa mika 27 tu.

Amy Winehouse alishinda tuzo kadha kwa albamu yake ya pili, Back to Black, ambayo ilitolewa mwaka wa 2006.

Sababu ya kifo haijulikani bado.

Lakini mwimbaji huyo amekuwa akipambana na uraibu wa ulevi na mihadarati kwa muda.
Mara nyingi alitokeza kwenye tamasha huku amelewa.

Friday, July 22, 2011

Hosea: Chenge ana kesi ya kujibu

Best Blogger Tips
Andrew Chenge
Via Mwananchi

SAKATA la kumiliki dola 1.2 milioni za Kimarekani (zaidi ya Sh1.2bilioni) katika kisiwa cha Jersey, Uingereza, linalomkabili mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, limeingia katika hatua mpya baada ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kutangaza kukamilisha uchunguzi na kukabidhi jalada kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), kwa hatua zaidi za kisheria.

Chenge alikutwa na kiasi hicho cha fedha mwaka 2008, kufuatia uchunguzi wa kashfa ya ununuzi wa  rada uliofanywa na Taasisi ya Makosa Makubwa ya Jinai ya Uingereza (SFO).

Chenge ambaye wakati wa ununuzi huo alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) anatuhumiwa kuwa kiungo muhimu katika ununuzi wa rada kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya BAE Systems.

Hata hivyo, kufuatia Chenge kukutwa na kiasi hicho kikubwa cha fedha zenye utata ambacho alikiita vijisenti, kumekuwa na shinikizo kubwa kutoka kwa watu wa kada tofauti nchini wakitaka ashitakiwe, na jana Mkurugenzi wa Takukuru Dk Edward Hoseah, alitangaza hadharani mjini Arusha kwamba mtuhumiwa huyo wa ufisadi atashtakiwa chini ya kifungu cha 27 Sheria ya Takukuru ya mwaka 2007.

Sehemu yakifungu hicho cha sheria, kinaainisha kuwa mtu akiwa na mali ambazo hazilingani na kipato chake alichokipata akiwa madarakani au baada ya kuondoka, ni kosa kisheria.


“Mtu ambaye atafanya kosa akiwa au akishikilia madaraka ya umma, kwa kuishi kwa kipato ambacho hakilingani na kipato cha sasa au kile alichopata…Au anayemiliki mali ambazo hazilingani na kipato chake kisheria, atakuwa akitenda kosa.” Kifungu hicho kinaeleza.

Dk Hoseah alifafanua zaidi kwamba,  kama DPP atalipitisha jalada hilo la Chenge, mbunge huyo atafikishwa mahakamani wakati wowote.

Kashfa ya kuwa na fedha hizo katika akaunti ya nje, ndiyo ilimwondoa Chenge katika wadhifa wa Uwaziri wa Miundombinu mwaka 2008, baada ya gazeti la Guardian la Uingereza kufichua kuwa Mwanasheria Mkuu huyo wa Serikali wa zamani, alikuwa akimiliki kiasi hicho cha fedha.

Hata hivyo, alipoulizwa na waandishi Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere baada ya kuachana na msafara wa Rais Jakaya Kikwete, aliyekuwa akitoka naye ziarani nchini China, Chenge alikiri kumiliki akiba hiyo ya fedha, lakini akiziita ni vijisenti, jambo ambalo liliwashangaza watu wengi nchini na kuibua hasira zaidi.

Lakini, Dk Hoseah akifafanua zaidi mchakato huo mzito wa kisheria, alisema ni Watanzania wachache mno wanaoweza kuwa na akiba ya fedha kiasi kama hicho nje ya nchi au mahali kokote, jambo ambalo aliongeza kuwa ndilo lililowasukuma kufanya uchunguzi kuhusu fedha hizo za Chenge.
Endelea kusoma habari hii.............................

Thursday, July 21, 2011

Jairo asimamishwa kazi

Best Blogger Tips
Via Uhuru

SERIKALI imemsimamisha kazi Katibu Mkuu  wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo.  Hatua hiyo inalenga kutoa nafasi ya   ufanyika uchunguzi dhidi ya tuhuma  zinazomkabili zilizoibuliwa bungeni.

Jairo anadaiwa kuziandikia barua idara na  taasisi zilizo chini ya wizara ili kila moja itoe  sh. milioni 50 kwa ajili ya kufanikisha  uwasilishaji wa makadirio ya matumizi ya  wizara kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012. Anadaiwa pia kuwalipa posho za safari  watumishi wa wizara waliofuatana na  viongozi wa juu licha ya kuwa walishalipwa  na idara na taasisi zao.

Wabunge Beatrice Shellukindo (Kilindi-CCM)  na Christopher Ole Sendeka (Simanjiro  -CCM), ndio walioibua tuhuma hizo  walipojadili makadirio ya wizara, kabla ya  serikali kuyaondoa bungeni.  Serikali iliyaondoa makadirio hayo bungeni  kutokana na hoja za wabunge kuwa  haijajipanga kukabiliana na tatizo la umeme.  Bunge limetoa wiki tatu kwa serikali  kujipanga na kuyarejesha.

Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo,  akizungumza na waandishi wa habari jana  mjini hapa, alisema amemwagiza Mdhibiti  na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  (CAG), kufanya uchunguzi wa kina, ambao  anatakiwa kuukamilisha ndani ya siku 10  kuanzia alipopewa kazi hiyo. "Wakati uchunguzi ukiendelea, Jairo   mesimamishwa kazi.

Hatua nyingine  zitafanyika baadaye kulingana na matokeo  ya uchunguzi," alisema. Luhanjo alisema anatarajia kufanya uteuzi  wa mtu atakayekaimu nafasi hiyo katika  kipindi kisichozidi siku tatu. Luhanjo alisema baada ya uchunguzi  kukamilika na endapo tuhuma dhidi ya Jairo  zitathibitika, uamuzi dhidi yake utachukuliwa  na rais kwa kuwa ndiye mamlaka yake ya  uteuzi.

Alisema amachukua uamuzi huo dhidi ya  Jairo kwa kuwa sheria ya  tumishi wa  umma inampa uwezo wa kushughulikia  nidhamu serikalini. "Kwa sababu suala hili ni zito nimeamua  aende likizo, lakini baada ya uchunguzi na  nikipata matokeo ya uchunguzi huo nitampa  taarifa itakayoambatana na hati ya  mashitaka," alisema. Akizungumzia utaratibu alisema baada ya  matokeo ya uchunguzi kupatikana, Jairo  atapatiwa taarifa itakayoambatana na hati  ya mashitaka, itakayoeleza kwa kifupi kosa  alilotenda na namna alivyolitenda ili atoe  majibu.

Luhanjo alisema katika kipindi hicho,  atakuwa amesimamishwa kazi na kuanza  kulipwa nusu mshahara.  Kwa mujibu wa Luhanjo, katika majibu,  anaweza kukubali au kukana tuhuma dhidi  yake, ambapo mamlaka ya nidhamu  itaendelea kutoa adhabu kulingana na uzito  na kwamba, kwa kuwa Jairo ni mteule wa  rais, ndiye atakayeamua hatima dhidi yake.
Endelea kusoma habari hii...............

Maumau ruksa Uingereza

Best Blogger Tips
Via BBC

Mahakama kuu ya Uingereza imetoa ruhusa kwa watu wanne raia wa Kenya kuishtaki serikali ya Uingereza kwa tuhuma za ukatili uliofanywa wakati wa ukoloni.

Wizara ya mambo ya nje pamoja na ofisi ya Jumuiya ya Madola zilisema haziwezi kubeba jukumu hilo kisheria, lakini jaji anayesikiliza shuri hilo alitupilia mbali hoja hiyo.

Jaji huyo amesema hajaona kama kulikuwa na utesaji wowote, lakini kama ulikuwepo, serikali ya Uingereza ndio ilikuwa na mamlaka.

Shauri hilo litaruhusu kufunguliwa kwa kesi ya tuhuma za ukatili uliofanywa dhidi ya vuguvugu la Maumau kati ya mwaka 1952 hadi 1961.

Waliowasilisha shauri hilo ni Ndiku Mutwiwa Mutua, Paulo Muoka Nzili, Wambugu Wa Nyingi na Jane Muthoni Mara, ambao umri wao ni kati ya miaka 70 hadi 80.

Wanne hao hata hivyo hawakuwepo mahakamani.

Katika shauri hilo, awali, jaji aliambiwa kuwa Bw Mutua na Bw Nzili walihasiwa, Bw Nyingi alipigwa hadi kupoteza fahamu katika tukio ambalo watu 11 walipigwa hadi kufa, huku Bibi Mara akinyanyaswa kijinsia. Lakini ofisi ya mambo ya nje ilisema jukumu la kisheria lilikabidhiwa kwa jamhuri ya Kenya baada ya kupata uhuru wake mwaka 1963.

Wednesday, July 20, 2011

JK asubiriwa hatima ya Jairo

Best Blogger Tips
Via Uhuru

UAMUZI kuhusu hatima ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, utajulikana baada ya Rais Jakaya Kikwete kurejea nchini kutoka Afrika Kusini. Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari, baada ya kuzindua meza ya maabara inayohamishika katika viwanja vya Bunge mjini hapa.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa awali kuhusu safari ya Rais Kikwete nchini Afrika Kusini, atarejea nchini leo.  Pinda alisema ameshawasiliana na Rais Kikwete aliye nchini Afrika Kusini kikazi, ambaye ameahidi kutoa uamuzi atakaporejea nchini. "Nimeshawasiliana na rais, ameniambia atakuja kutoa uamuzi akifika nchini.

Mheshimiwa rais ameona si busara kutoa uamuzi wa jambo kama hilo akiwa kwenye mkutano, hivyo ameahidi kulitolea uamuzi akirejea," alisema. Akizungumzia tetesi zilizozagaa kuwa Jairo amejiuzulu wadhifa wake, Waziri Mkuu Pinda alisema hana taarifa rasmi. Waziri mkuu alisema endapo kungekuwa na taarifa hizo angezipata lakini kwa wakati huo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari hakuwa na taarifa yoyote.

"Mwenyewe nimesikia imeandikwa katika gazeti moja lakini kwangu sina taarifa, labda kama aliandika barua na kuipeleka huko sijui," alisema Waziri Mkuu Pinda. Gazeti moja nchini (si Uhuru) liliandika habari jana kuwa Jairo amejizulu.

Jairo aliingia matatani baada ya kudaiwa kuandika barua ya kuzichangisha fedha taasisi na idara zilizo chini ya wizara, ambapo kila moja ilitakiwa kuchangia sh. milioni 50 kufanikisha upitishwaji wa makadirio ya matumizi ya fedha ya wizara hiyo kwa mwaka 2011/2012.

Akizungumzia suala hilo bungeni juzi, Waziri mkuu alisema ameshindwa kutoa uamuzi wa kumtimua kazi kwa kuwa kufanya hivyo ni kuingilia madaraka ya rais.

BAE yashutumiwa na Wabunge wa UK

Best Blogger Tips
Via BBC

Kampuni ya Uingereza inayotengeneza silaha na ndege za kijeshi, BAE Systems imeshutumiwa vikali na tume iliyoundwa na Bunge la Uingereza kuchunguza kesi ya rushwa kuhusu Radar ambayo shirika hilo liliiuzia Tanzania.

Wabunge wameituhumu BAE kwa mpango wake wa malipo kwa Tanzania na kuutaja kama ''unafiki mtupu''.

BAE imekiri kuwa haina kumbukumbu ya maandishi kuhusu malipo ya pauni milioni 8 sawa na dola milioni 12 za Marekani kwa wakala aliyesimamia biashara hiyo.

Hata hivyo, baada ya kujitetea, kampuni haikupatikana na hatia nyingine zaidi kuwa ilishiriki rushwa.
Mvutano huu unahusu Radar ya kuongoza safari za ndege iliyouziwa Tanzania mwaka 1999.

Hata hivyo hili huenda kikawa kigezo kwa wakereketwa wanaopinga rushwa wanaodai kuwa hongo na rushwa ni kizuizi cha maendeleo ya uchumi.

Katika kujitetea mbele ya mamlaka yaliyoendesha kesi hiyo, afisi inayosikiliza kesi za ufisadi wa kupindukia(Serious Fraud Office) BAE imekubali kuwalipa raia wa Tanzania pauni milioni 30.

Kiwango cha pauni hizo milioni 30 ni fidia kwa Tanzania kwa sababu ya kufedheheshwa kwa malipo ya pauni milioni 8 pamoja na madai ya kuwauzia Tanzania mtambo wa matumizi ya kijeshi wasiouhitaji na kwa gharama kubwa.

Hata hivyo Shirika la BAE pamoja na mamlaka ya kuchunguza ufisadi hayakuweza kusema kama pesa hizo milioni 8 zilitumiwa kama hongo ya kuficha mauzo ya radar hiyo.

Wakili mkuu wa BAE, Philip Bramwell, alisema kuwa kampuni hiyo imesikitishwa na matukio yote na kuomba radhi. Wakili huyo alikiri kuwa kampuni hiyo kamwe haitorudia kutoa malipo ya aina hiyo.

Wabunge wa Kamati nyingine ya Maendeleo ya Kimataifa wamepuuza msimamo wa kampuni hiyo na kuutaja kama usioridhisha.

Walirudia matamshi ya Jaji mmoja aliyesema kuwa mradi mzima ulikuwa ni aibu tupu, na ukitizama malipo ya pauni milioni 8 lazima ushuku na kuna uwezekano mkubwa kuwa kitita hicho kilitumiwa wakati wa majadiliano ya kutaka kampuni ya BAE ipendelewe katika kuuza radar hiyo.

Wabunge hao wakauliza kwanini hadi wakati huu kampuni hiyo imeshindwa kulipa angalau sehemu ya pauni hizo milioni 30.

Vilevile walihoji jinsi gani kampuni hiyo ilivyoweza kuunda bodi yake binafsi iliyofikia uwamuzi wa jinsi fedha hizo zingetumiwa badala ya kuzikabidhi moja kwa moja kwa serikali ya Tanzania, kama lilivyotaka kundi la wabunge kutoka Tanzania.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Malcolm Bruce MP akauliza kama si dharau na matusi kwa kampuni hiyo kutoa mapendekezo ya namna pesa hizo zitakavyotumiwa na kujifanya kuwa inaelewa zaidi kuliko serikali ya Tanzania jinsi ya kutumia pesa zake.

Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka inayochunguza rushwa, Richard Alderman, aliyekuepo mbele ya Kamati hiyo alisema kuwa ameshangazwa kuona kuwa malipo hayo yamechelewa.

Alijitolea kuiandikia BAE kuuliza sababu za kuchelewa na kuongezea kuwa wakizidi kuchelewesha malipo hayo huenda wakakabiliwa na adhabu nyingine.
Endelea kusoma habari hii........................

Tuesday, July 19, 2011

Baba adaiwa kumbaka mtoto wake Muheza

Best Blogger Tips
Via Mwananchi

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, mkazi  wa Muheza, mkoani Tanga, (Jina limehifadhiwa), anadaiwa kumbaka mwanaye wa kumzaa mwenye umri wa miaka minne.Tukio hilo la kusikitisha linadaiwa kufanyika miezi kadhaa iliyopita na kuripotiwa katika vyombo vya dola.Pamoja na kuripoti taarifa hiyo polisi  ilielezwa kwamba vyombo vya dola vimekuwa vikisuasua kufuatilia na kuchunguza ukweli juu ya tuhuma hizo.

Shemeji wa mlalamikiwa aliyejitambulisha kwa jina la Mbaruku Mwaita alisema taarifa za udhalilishaji watoto ziliripotiwa katika kituo cha polisi Chumbageni wilayani Muheza  siku nyingi, lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea.Alisema  tatizo hilo lina  jalada namba MUH/IR/205/2011,  lakini tangu ilipofunguliwa hakuna dalili za kuendelea kwa kesi.

Mwaita, alisema  shemeji yake amekuwa na tuhuma za kufanya vitendo hivyo viovu mara kadhaa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe, alipoulizwa jana kwa njia ya simu alikiri kupokea  jalada hilo  Julai 16 , mwaka huu.Massawe alisema  faili hilo litapelekwa kwa  Mwanasheria wa Serikali ili kuangaliwa na kuanza kwa kesi kama linajitosheleza.

Aliwataka wahusika kuwa na  subira  kutokana na ukweli kwamba polisi wanaendelea kushguhulikia na kwamba kesi itasikilizwa  kabla ya mwaka huu kuisha.Lakini, shemeji huyo wa mtuhumiwa akifafanua zaidi, alisema  mtuhumiwa mara ya kwanza alishafanya kitendo kama hicho kwa mdogo wake wa kike aliyekuwa anaishi naye awali jambo ambalo lilisababisha dada yake aombe talaka na shemeji huyo kuoa mke mwingine.

Mbaruku alisema  baada ya wawili hao kupeana talaka, mwanaume aling’ang’ania kukaa na mtoto wake akitaka akalelewe na mama wa kambo jambo ambalo lilizua mtafaruku, lakini alifanikiwa kuondoka na mtoto huyo.

 ‘’Baada ya mwezi mmoja kupita mtuhumiwa alimpiga simu mama ambaye ni bibi yake aende akamchukue mtoto stendi ya basi ,lakini mtoto yule alionyesha kudhoofu kwa kiasi kikubwa kiafya akawa akijisaidia haja ndogo anatoa damu jambo lilisababisha wampeleke hospitali."

Katika ripoti iliyotolewa na hospitali teule ya Muheza, inaoonyesha sehemu za siri za zimetanuka na kuathirika vibaya  kuliko umri wake na ikithibitishwa ni kweli ameingiliwa kimaumbile zaidi ya maramoja.

‘’Sikufichi hii kesi hata inavyoendeshwa kama familia hatujaafiki na tulishaandika barua ya malalamiko yaliyojibiwa kuna upungufu katika ushahidi uliotolewa , mshtakiwa alipokamatwa kwa mara ya kwanza alikaa polisi kwa  muda wa siku sita tu siku tuliyoenda tukaambiwa amepelekwa mahakama ya Tanga chumbageni lakini tulipofika tuliambiwa huyo mtuhumiwa hakufikishwa mahakamani turudi Muheza” alifafanua  Mbaruku.

Alifafanua kwamba,  huenda kesi hii haitendewi haki na wamekuwa wakizungushwa kila wanapofatilia mahakamani wanaambiwa kesi imeenda jambo ambalo si la kweli na kuongeza, wakati mwingine huambiwa ipo mahakamani hivyo si swala lao tena kwani kesi hiyo iko chini ya wakili wa serikali.

Mbaruku alisema kinachomsikitisha zaidi muhalifu anayekabiliwa kesi ya kubaka ametoka polisi kwa dhamana na akiendelea na shughuli zake kama kawaida.Tukio kama hili liliripotiwa mwishoni mwa  wiki iliyopita kutokea maeneo ya Kimara Suka ,ambapo  Hamisi Elia Minja  anadaiwa  kumuingilia kinyume na maumbile binti yake wa kuzaa mwenye umri wa miaka 10  huku akimtishia kumchoma na kisu wakati akimfanya kitendo hicho cha kinyama.

Monday, July 18, 2011

Shellukindo ailipua Wizara ya Ngeleja

Best Blogger Tips
Via Mwananchi

MBUNGE wa Kilindi (CCM), Beatrice Shellukindo amelipua bomu Bungeni akimtuhumu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, kwa kutumia zaidi ya Sh 1 bilioni kwa ajili ya kutoa rushwa kwa watu mbalimbali ili bajeti ya wizara hiyo iweze kupitishwa na Bunge.Tuhuma hizo nzito zinakuja kipindi ambacho tayari Wabunge wa Kamati ya Nishati na Madini wakiwa wameibua tuhuma kama hizo za baadhi ya wajumbe kutaka kuhongwa na maofisa wa wizara hiyo, ili kurahisisha upitishaji wa bajeti ndani ya kamati.

Takriban wiki tatu tangu wabunge wa kamati hiyo kuibua tuhuma hizo ambazo zilifika hadi kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, jana Shellukindo alikoleza moto huo wakati akichangia bajeti ya wizara.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda jana alikubaliana na tuhuma hizo. Akitoa hoja ya kuondoa bungeni hotuba ya makadirio ya matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini, Pinda alisema alikuwa akisubiri Rais Jakaya Kikwete afike Afrika ya Kusini alikokwenda katika ziara ya kiserikali ili aweze "kumshtaki" Katibu Mkuu huyo kutokana na tuhuma zilizotolewa dhidi yake. Pinda alisema hawezi kuchukua hatua dhidi ya Jairo kwani kwa mujibu wa sheria, mamlaka ya uteuzi ndiyo inayoweza kuchukulia hatua dhidi yake.

"Kwa jinsi jambo hili lilivyokaa, hakuna jinsi mtu unavyoweza kulitetea hata kidogo, nilitamani sana kwamba nije hapa niseme kwamba uamuzi wangu mimi ni huu, lakini haikuwezekana," alisema Pinda na kuongeza: "Kwa dhati kabisa naomba wabunge tuwe na subira, mara tu mheshimiwa Rais atakapotua South Africa (Afrika Kusini) jioni ya leo  (jana), nitamuarifu na ninaamini tutaelewana kuhusu hatua za kuchukua."

Shinikizo la kutaka Jairo kuondolewa katika nafasi yake lilitolewa ndani ya kikao cha wabunge wa CCM waliokutana jana mchana wakitaka Katibu huyo wa zamani wa Rais Kikwete afukuzwe kazi, huku wakiitaka Serikali iiamuru Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (Takukuru) imchunguze.

Awali, akichangia bajeti hiyo bungeni jana huku akianza kwa kumwomba Mungu msaidie katika kauli zake, alisema alifanikiwa kuipata barua iliyoandikwa na Jairo kwenda kwa taasisi na idara zaidi ya 20, ikiagiza zitoe Sh50 milioni kila moja.

Shellukindo alisema barua hiyo inaonyesha idara na taasisi hizo ziliagizwa fedha hizo ziwekwe kwenye akaunti namba 5051000068 inayomilikiwa na Geological Survey of Tanzania (GST) kwenye Benki ya NMB, Tawi la Dodoma."Tena inaagiza kwamba fedha hizo zikishatumwa kwenye akaunti hiyo, wizara ipewe taarifa kupitia Ofisi ya DP kwa ajili ya utaratibu," alisema.

Alisema barua hiyo yenye kichwa cha habari: "Yahusu kuchangia gharama za kukamilisha maandalizi na uwasilishaji wa hotuba ya bajeti ya wizara ya 2011/12 bungeni Dodoma, Jairo alisema wizara imefanikisha maandalizi ya mpango wa bajeti kwa mwaka 2011/12 na imekwishapitishwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini na hivyo aliinukuu barua hiyo: "Katika kukamilisha mchakato huo, hotuba ya bajeti inatarajiwa kuwasilishwa Bungeni tarehe 15 na 18, Julai 2011."

"Kama ilivyo kawaida wakati wa kuwasilisha hotuba ya Bajeti Dodoma, maofisa mbalimbali wa wizara na taasisi zilizo chini yake huambatana na viongozi waandamizi kwa ajili ya kutoa ufafanuzi wa masuala yanayojitokeza wakati wa mjadala wa hotuba hiyo. Ili kufanikisha mawasilisho ya hotuba hiyo ya bajeti, unaombwa kuchangia jumla ya Sh50 milioni.

Katika uchunguzi wake, Shellukindo alisema amebaini fedha hizo tayari zimetolewa na Jairo kwenye benki hiyo hivyo akahoji; "Naomba kufahamu fedha hizo zimekwenda wapi?"

Kutokana na hali hiyo, Shellukindo alishauri bajeti hiyo isiendelee kujadiliwa Bungeni na badala yake Ngeleja arejeshewe ili akaifanyie marekebisho na aiwasilishe upya Bungeni baada ya wiki mbili... "Nakusudia kutoa hoja kwamba bajeti hii irudishwe na baada ya wiki mbili irudishwe hapa.”

Habari kutoka ndani ya Kikao cha Kamati ya Wabunge wa CCM zinasema kuwa wabunge hao walikuwa wametoa muda kwa Serikali kwamba hadi saa 11:00 jioni jana Jairo awe amefukuzwa kazi. Kwa mujibu wa habari hizo, wabunge hao pia waliitaka Serikali kuielekeza Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (Takukuru) kuanza uchunguzi wa jinsi fedha hizo zilivyotolewa na matumizi yake, ili ikibainika vinginevyo wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.

Chanzo chetu ndani ya kikao hicho cha wabunge wa CCM kiliwataja waliotaka Jairo afukuzwe kazi kuwa ni pamoja na Christopher Ole Sendeka (Simanjiro), Esther Bulaya (Viti Maalumu), George Simbachawene (Kibakwe), Godfrey Zambi (Mbozi Mashariki), Henry Shekifu (Lushoto), Murtaza Mangungu (Kilwa Kaskazini), Alphaxard Lugora (Mwibara), Shellukindo (Kilindi) na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, January Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli.

"Wabunge wamegeuka wamekuwa wakali sana na hawataki kusikia cha mtu, wamesema lazima leo (jana) ikifika saa 11 Jairo awe amefukuzwa kazi, hawataki kumuona kabisa," alisema mmoja wa wabunge waliohudhuria kikao hicho.Mbunge huyo alisema Waziri Ngeleja na Naibu wake, Adam Malima pia walitakiwa wajiuzulu kwa maelezo kwamba: "Haiwezekani wasiwe wanafahamu chochote kuhusu mkakati huo wa katibu wao mkuu katika wizara wanayoiongoza."

"Hawawezi kujivua lawama, hata hao tumewataka wajiuzulu, ina maana gani kama barua nzito namna hiyo Waziri na Naibu wake hawazifahamu, haiingii akilini kabisa," alisema mbunge huyo.
Endelea kusoma habari hii.........................

Sunday, July 17, 2011

Mandela atimiza miaka 93 ya kuzaliwa

Best Blogger Tips
Via BBC

 Nelson mandela ambaye kwa sasa ni myonge kiafya amekuwa chini ya uanagilizi wa karibu kutoka kwa madakatari kwa muda wa saa 24 tangu atoke hospitali mwezi januari pale alipolazwa baada ya kuugua.

Lakini hali hii haijawazuia raia wa Afrika Kusini na watu wengi duniani kumtakia kheri njema anavyo sheherekea miaka 93 tangu azaliwe.

Kuadhimisha siku hii, nyimbo maalum imetungwa kwa heshima yake.
Raia wa Afrika kusini wanatarajia kuweka historia ambapo yamkini watu milioni 12 wataimba wimbo huo kwa wakati mmoja.

Shirika la utangazaji nchini humo (SABC) pamoja na idara ya elimu wamefanya mapango kuwa ifikiapo saa mbili na dakika tangu asubuhi hii, wanafaunzi katika shule zote nchini watauimba wimbo huo maalum uliotungwa kwa heshima ya Madiba.

Siku hii ya kuzaliwa kwa Nelson Mandela, rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini ni siku ya kimataifa iliorodheshwa na Umoja wa Mataifa.

Nchini Afrika Kusini kila mtu atajitolea dakika 67 za muda wake leo kufanya huduma za kijamii.
Viongozi mbali mbali duniani wamemtumia salamu za kheri njema mzee Mandela wakiongozwa na Rais Barack Obama wa Marekani.

Rais Obama amesema Mandela ni nembo ya demokrasia na haki duniani na amemshukuru kwa kujitolea maisha yake kwa huduma ya jamii.

Kiongozi huyo wa marekani amesema Mandela ataacha urithi wa busara, nguvu na fadhila nyingi.

Sita amkaba koo Ngeleja

Best Blogger Tips
Via Mwananchi

SUALA la mgawo wa umeme unaoendelea nchini kote linazidi kuchukua sura mpya baada ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta kutaka wote waliofikisha nchi kwenye mgawo huo wawajibishwe.
Sitta alisema haitoshi kwa watu hao kuomba msamaha pekee kwa kulingiza taifa katika makali na kadhia ya mgawo huo unaoendelea kuporomosha uchumi wa nchi.


Kauli ya Sitta imekuja wakati wabunge mjini Dodoma wakiwa wamebana Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja wakitaka aeleze jinsi atakavyomaliza mgawo huo nchini baada ya kuwasilisha bajeti ya wizara yake juzi, vinginevyo hawataipitisha.

Sitta akizungumza na Vijana wa CCM kutoka vyuo vikuu mkoani Mbeya jana  alisema: “Ni lazima tuwaombe radhi Watanzania kwa kuwapo kwa mgawo wa umeme kwani hii siyo nchi ya kupata mgawo.”

“Tunazo rasilimali nyingi ambazo zinaifanya Tanzania kuwa na umeme wa kuuza na siyo mgawo,” aliongeza Sitta.

“Haitoshi kuwaomba radhi Watanzania lazima waliotufikisha kwenye mgawo wawajibishwe, hili lazima tutalishughulikia tunawaahidi lazima nchi yetu ibaki kuwa na heshima aliyoiacha Baba wa Taifa (Mwalimu Julius Nyerere), ”alisema Sitta.

Sitta ambaye ameongozana na Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe (ambaye ni Mbunge wa Kyela), Mbunge wa Simanjiro, Christopher ole Sendeka, Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela, alisema ili nchi iweze kurejea katika hadhi yake iliyokuwa nayo lazima utaratibu wa kuwajibishana urejewe.

Wengine waliohudhuria kongamano hilo ni Naibu Waziri wa Viwanda Biashara na Masoko ambaye pia ni Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mary Mwanjelwa, Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi na Mbunge wa Mbarali, Dickson Kilufi.

Katika kongamano hilo pia, Sitta ambaye alikuwa Spika wa Bunge la Tisa alizungumzia jaribio la kutaka kuvuliwa uanachama wa CCM mwaka 2009, akisema kuwa kundi la watu wachache wenye fedha walitaka kutumia fedha zao kumng’oa na kumvua uanachama.

“Nataka kuwaeleza haya matukio yapo ya kutaka kufukuzwa kwenye chama, kwani hata mimi nilitaka kufukuzwa na watu wenye fedha, lakini walishindwa, tunamshukuru Rais Jakaya Kikwete aligundua kuwa kuna ulazima wa kuvua gamba katika chama chetu,”alisema.

“Nawapa matumaini katika chama chetu kuwa sisi mnaotuona hapa ndio tunaotumia akili siyo tumbo katika kufikiri, hivyo chama chetu kitakwenda vizuri,”aliongeza Sitta.

Alisema kuna baadhi ya viongozi wa Serikali na wanachama wa CCM wanatanguliza ubinafsi, kwani hivi karibuni walidiriki hata kusafirisha wanyama na kuwapeleka nje ya nchi.

“Hivi karibuni kuna wenzetu walisafirisha wanyama wetu aina ya twiga wapatao130 kuwapeleka Uarabuni, hii hali hatutaweza kukubaliana nayo, lazima tupambane,” alisema.

Akijibu maswali ya wanafunzi hao, Sitta alisema kuhusu soko la ajira katika Jumuia ya Afrika Mashariki, vijana wategemee kuwapo kwa ajira hizo na kwamba watapimwa uwezo huku akiwahakikishia kuwa wapo watakaoajiriwa na kufanya kazi Kenya.
Endelea kusoma habari hii.........................

Friday, July 15, 2011

Jennifer Lopez & Mac Anthony split!

Best Blogger Tips
Via Access Hollywood

“It is a painful time for all involved,” the statement continued, “and we appreciate the respect of our privacy at this time.”
After seven years of marriage, Jennifer Lopez and Marc Anthony have split, the couple confirmed on Friday.

“We have decided to end our marriage,” the pair said in a joint statement to Access Hollywood. “This was a very difficult decision. We have come to amicable conclusions on all matters.”

The split will come as a shock to many who saw Jennifer and Marc appearing happy and in love as the reality TV show judge and singer joined her husband on stage as she danced during his performance on the “American Idol” season finale.

Jennifer and Marc have two children – twins Emme and Max, now 3.

Back in January, Jennifer stopped by Access Hollywood Live, where she hinted she wasn’t ready to expand their family because she was concentrating on work.

“I don’t know, we’ll see,” she told Billy Bush and Kit Hoover.

“I would love it, if I got pregnant, if that happened right now, I’d be like, ‘Oh my God, I’m pregnant everybody!’ I’d be so happy,” the 41-year-old continued.

“I don’t know if it’s going to happen for us,” she added. “Or if, you know, I would plan it… because right now I’m just getting back into the groove of working again and I missed it.”

The “Idol” judge went on to explain that navigating career and family life is a challenge.
”[My career] was such a huge part of my life for so long… it’s so much a part of who I am,” she continued. “You lose that for a while when you have the babies, its all about them and it’s just like, you know, miracle time.”

The pair had announced in April that they were teaming up on “Q’Viva! The Chosen.”
The show was originally set to feature the pair as they traveled 21 countries to find the best performers in Latin music, dance and other arts with the goal of creating a live extravaganza. No word yet on how their split will impact plans for the show.

Jennifer and Marc married in June 2004.

Marc was previously married to former Miss Universe Dayanara Tores. They married in 2000 and split in 2002.

Jennifer was previously married to dancer Cris Judd (2001-2002) and waiter Ojani Noa (1997-1998).

Kijana amuua mama yake kwa panga

Best Blogger Tips
Via Tanzania Daima

KIJANA mmoja mkazi wa kijiji cha Mgori, mkoani Singida, Miraji Joseph (22), anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumuua mama yake kwa kumchinja kwa kutumia panga na kisha kutenganisha kichwa na kiwiliwili.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa katika vyombo vya habari na kamanda wa polisi wa mkoa huo, Celina Kaluba, ilimtaja aliyeuawa kuwa ni Juliana Hango (57).

Taarifa hiyo iliongeza kuwa tukio hilo la kusikitisha lilitokea Julai 12, mwaka huu, majira ya saa 10.45 jioni katika kitongoji cha Mwamba.

Taarifa hiyo ilisema kuwa polisi walipata taarifa juu ya mauaji hayo kupitia kwa mtoto mwingine wa marehemu Adam Joseph anayefanya kazi ya ualimu katika Shule ya Msingi Mbusuruangiri, mkoani Shinyanga.

Joseph ambaye alikuwa katika mapumziko ya likizo mkoani Singida alishangaa kumkosa mama yake aliporejea katika shughuli zake.

Hata hivyo kamanda huyo alisema baada ya mwalimu huyo kumwuliza mtuhumiwa wa tukio hilo alikokwenda mama yao…alijibu kuwa hafahamu.

Taarifa hiyo ilisema kuwa Joseph aliamua kuzunguka nyuma ya nyumba na kugundua michirizi ya damu huku mwili wa mama yake ukiwa umechinjwa na kichwa chake kikiwa ndani ya boksi.

Katika eneo hilo walikuta panga likiwa na damu ambalo linasadikiwa kutumika katika tukio hilo.

Jeshi la polisi limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo na atafikishwa mahakamani wakati wo wote kujibu tuhuma hizo.

Taarifa ya awali ilidai kuwa inawezekana mtuhumiwa huyo alirudiwa na ugonjwa wake kutokana na siku za nyuma kuwahi kuugua ugonjwa wa akili (kichaa).


Lowassa: Nimeshtushwa

Best Blogger Tips
Via Mwananchi

WAKATI uamuzi wa Rostam Aziz kung'atuka ubunge wa Igunga na ujumbe wa Halmashauri Kuu (Nec) ndani ya chama chake cha CCM ukiibua gumzo kubwa karibu kila kona nchini, mshirika wake mkubwa kisiasa, Edward Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli ameeleza kushtushwa na tukio hilo.Juzi, Rostam, mmoja wa watu muhimu ndani ya CCM aliyeshiriki vyema katika mtandao uliomwingiza madarakani Rais Jakaya Kikwete mwaka 2005, alitangaza uamuzi mzito wa kung'atuka siasa akipinga kile alichokiita siasa uchwara za baadhi ya viongozi wake.

Uamuzi huo mzito wa Rostam uliibua kwikwi na vilio kutoka kwa wapigakura jimboni kwake Igunga, wakiwamo wale waliomchagua kwa vipindi vitatu mfululizo tangu mwaka 1994 ulipofanyika uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Charles Kabeho. Jana, Lowassa alisema: "Kwa kweli nimeshtushwa, nimesikitishwa...kilichonishtua zaidi ni vilio. Namna wananchi wa Igunga walivyokuwa wanalia na kusikitika."

Hata hivyo, Lowassa ambaye naye amekuwa akitajwa katika orodha ya watu watatu wanaopaswa kuachia nafasi zao za uongozi CCM katika kile kinachoitwa chama kujivua gamba, alipoulizwa kuhusu taarifa za yeye kufuata njia ya mshirika wake huyo alijibu: "Siku ikifika nitatoa uamuzi na nitajibu wakati ukifika."

Lowassa alikuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma, kuhusu alivyopokea uamuzi huo wa Rostam na kama yuko tayari kufuata mfano na njia hiyo ya kujiuzulu nyadhifa zote ndani ya CCM.
Lakini, juzi Rostam aliweka bayana kwamba uamuzi wake wa kujiuzulu hautokani na shinikizo lolote ikiwamo kile kinachoitwa mpango wa kujivua gamba, bali aliufanya uamuzi huo kuepuka kuathiri biashara zake kutokana na kuchafuliwa na siasa uchwara akieleza kuwa yeye ni mfanyabiashara wa kimataifa, lakini akaahidi kuendelea kuwa mwanachama mtiifu wa CCM.

Hata hivyo, Lowassa jana hakutaka kufafanua kuhusu kauli yake hiyo ya "Nitajibu wakati ukifika," ingawa alionyesha tabasamu wakati akiulizwa na kujibu swali hilo  la iwapo atafuata nyayo za Rostam au la.
Mshirika wao mwingine, Andrew Chenge, jana alivumishiwa kuandaa mkutano na waandishi wa habari  ili naye atangaze uamuzi wa kujiuzulu nafasi zake zote kama hatua ya kutekeleza azimio la Nec la kujivua gamba.

Lakini, alipotafutwa kwa simu na kuulizwa kuhusu taarifa za yeye kutaka kujiuzulu, Chenge alijibu kwa kifupi kuwa alikuwa Uingereza, kitu kilichothibitisha kuwa hakukuwa na mpango huo wa kujiuzulu huku akisisitiza: "Mimi niko nje ya nchi, nipo Uingereza."

Hivi karibuni, Chenge, Mbunge wa Bariadi Magharibi, maarufu kama Mzee wa Vijisenti, aliwahi kuliambia gazeti hili: "Sijui kama mimi ni gamba CCM," huku akisisitiza kwamba anaheshimu taratibu za chama na asingeweza kukurupuka na kuanza kuzungumza mambo ya chama nje ya utaratibu.
Chenge alisema chama kina utaratibu wake wa kufanya maamuzi, hivyo kuanza kutoka nje ya taratibu na kuzungumzia mambo ya ndani ya chama isingekuwa rahisi kwake kwani anaheshimu taratibu zilizopo.
Endelea kusoma habari hii.....................

Wednesday, July 13, 2011

Igunga yazizima, Rostam kujiuzulu

Best Blogger Tips
Via Mwananchi

MJI wa Igunga na vitongoji vyake jana ulizizima, Mbunge wa Igunga Rostam Aziz alipotangaza kuachia ubunge wa jimbo hilo.Tukio hilo liliambatana na matukio kadhaa ya wananchi kuonyesha mabango yaliyokuwa na ujumbe tofauti, wengine kuzirai na mara kadhaa kumvamia ili asiendelee na uamuzi wake huo.

Mbunge huyo aliwasili Igunga saa saba mchana na baada ya kufika akaingia katika ofisi za CCM wilaya na kuzungumza na Baraza la Vijana la Wilaya. Aliwambia vijana hao kwamba, halikuwa lengo lake kuingilia mkutano wao bali alitaka kuzungumza na wazee.

Wakati akiingia katika mkutano huo, alipokewa na mabango yaliyokuwa na ujumbe uliosomeka kwamba "Kama wakikufukuza na sisi tutaondoka CCM”,  “Igunga bila Rostam hakuna maendeleo”, “Rostam umeboresha huduma za kijamii Igunga”, “Mbunge wetu tunakupenda sana” na “Tuna imani na wewe”.

Alitumia dakika saba kuzungumza na vijana kabla ya kukutana na viongozi wa CCM wa wilaya hiyo, akiwamo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazee, Kassim Ally.  Akiwa na viongozi hao alizungumza nao kwa dakika 49.

Saa nane mchana aliondoka kwenda kwenye Ukumbi wa Sakao uliopo kilomita moja kutoka jengo la CCM wilaya hiyo.

Akiwa huko alipokewa na kisha kuanza kusoma hotuba yake ndefu ya kurasa takribani 10, lakini mara baada ya kutangaza kuachia nafasi zake ndani ya CCM huku akilengwa na machozi, baadhi ya wanachama walianza kulia huku wengine wakivamia meza kuu kumtaka mbunge huyo abadili uamuzi yake.

Wananchi hao walikuwa wamebeba mabango yenye maneno “ wao CCJ, sisi CCM”,  huku wakilitaja jina la Nape Nnauye, ambaye ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho.

Kufuatia tukio hilo Rostam alilazimika kuacha kuendelea kuisoma hotuba hiyo kwa dakika 15 baada ya kuvamiwa na kundi la baadhi ya vijana waliomtaka kusitisha uamuzi wake huo na kuwasihi wasimzuie, ili amalizie hotuba hiyo na baadaye watoe maoni yao.

Baada ya wanachama hao kutulia walipewa nafasi ya kutoa maoni yao wakasema kwamba akiendelea na uamuzi huo watarudisha kadi za CCM.

"Hatukubali wewe kwetu ni muhimu sana umetufanyia mengi, yanayosemwa yavumulie nakuomba ubadili msimamo wako na kama hautabadili msimamo huo hatuoni haja wa kubakia ndani ya chama cha CCM," alisema Hamis Kanama.

Watu wazirai


Baada ya Rostam kumaliza kusoma hotuba, Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Nzega, Daudi Ngutu, na Katibu wa Uchumi Kata ya Igoweko, Athuman Kanyama, walizirai na kupandishwa katika gari la Halmashauri ya kupelekwa hospitalini wakiwa katika hali mbaya.

Mjumbe wa Barala la Utekelezaji la UVCCM, Hussein Bashe, alikuwa miongoni mwa mashuhuda wa tukio la Rostam kutangaza kung’atuka. Bashe ambaye alikuwa sambamba na Rostam tangu akiwa katika ofisi za wilaya aliliambia Mwananchi kuwa uamuzi wa Rostam ni mwiba mchungu kwa wananchi wa jimo hilo.

"Alichokifanya Rostam ni haki yake, lakini pamoja na hayo hawatendei haki wananchi wa Igunga, ila kwa kuwa ni maamuzi yake hakuna jinsi,"alisema Bashe na kusisitiza kwamba, CCM isipokuwa makini uchaguzi wa mwaka 2015 ukimalizika, utakiacha kikiwa chama cha upinzani na si chama tawala.

"Sekretarieti ya CCM itakabidhi chama kikiwa cha upinzani Watanzania wana matatizo mengi , lakini viongozi badala ya kuangalia hayo wanaendekeza siasa za chuki na kinafiki," alisema Bashe.
Endelea kusoma habari hii............................

Rostam Aziz: Hotuba ya kujivua Gamba

Best Blogger Tips
UTANGULIZI

WAZEE wangu, kwanza kabisa kabla ya kueleza kile ambacho kimenisukuma kuzungumza nanyi leo, napenda kuanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kutuwezesha kufikia siku hii ambayo inatukutanisha waja wake.

Wazee wangu wa Igunga, baada ya kufanya hivyo napenda pia kutumia fursa hii kuwashukuru ninyi nyote mmoja mmoja na katika umoja wenu kwa kuitikia wito wangu, kijana wenu, niliyewaomba nije nizungumze nanyi siku hii ya leo.

Nafanya hivyo nikitambua vyema kwamba, kama si nyinyi wazee wangu na wengine wengi ambao hatuko nao hapa leo kwa sababu mbalimbali, ambao mmekuwa na imani kubwa nami nisingeweza kufikia hapa nilipofika sasa.

Wazee wangu, waasisi wa taifa letu walitufundisha kutambua na kuheshimu ukweli kwamba; ‘Uongozi ni Dhamana’ dhana ambayo kila ninapokaa na kutafakari huwa inanirejesha nyuma na kukumbuka jinsi nyinyi mlivyokaa katika umoja wenu na kuniteua mimi, miongoni mwa vijana wenu wengi, kuwa mwakilishi wa Jimbo la Igunga tangu mwaka 1994.

Katika kipindi hicho chote cha utumishi wangu, nyinyi wazee wangu mmekuwa mhimili muhimu ambao umeniwezesha kutimiza wajibu wangu kwa bidii kubwa, maarifa na nidhamu ya hali ya juu nikitambua namna ambavyo mmekuwa na imani kubwa juu yangu.

Ari na moyo wa imani, ushirikiano na mshikamano ambao wazee wangu mmekuwa nao kwangu ndiyo ambao kwa kiwango kikubwa umetuwezesha kufanya kazi kwa pamoja, tukishinda changamoto mbalimbali ambazo zimekuwa zikilikabili jimbo letu katika kipindi chote ambacho mmeendelea kuniamini kuwa mbunge wenu kwa miaka 18 sasa.

Wakati nikitambua na kuheshimu ukweli kwamba katika kipindi chote cha ubunge wangu mmekuwa na imani kubwa nami na kuniunga mkono kwa dhati, naamini kwamba kwa upande wangu pia nimejitahidi kwa kadiri nilivyoweza, kutimiza matarajio ya wananchi wa Igunga.

Miongoni mwa mafanikio makubwa tuliyoyafikia kupitia ushirikiano wetu na uongozi wa pamoja ni kwamba, mwaka 1994 Igunga ilikuwa ni wilaya ya mwisho kwa maendeleo mkoani Tabora lakini leo ndiyo ya kwanza, taa za barabarani, bima ya afya kwa kila kaya, zahanati kila kijiji na shule nyingi kuliko idadi ya kata zilizomo kwenye wilaya.

Wazee wangu, nayasema haya nikitambua kwamba, kama ilivyo katika maeneo mbalimbali hapa nchini, mafanikio makubwa tuliyoyapata katika nyanja za elimu, afya, makaazi bora na kilimo katika kipindi chote ambacho mmendelea kuniamini kuwa mbunge wenu kwa miaka 18 sasa.

Wakati nikitambua na kuheshimu ukweli kwamba katika kipindi chote cha ubunge wangu mmekuwa na imani kubwa nami na kuniunga mkono kwa dhati, naamini kwamba kwa upande wangu pia nimejitahidi kwa kadiri nilivyoweza, kutimiza matarajio ya wananchi wa Igunga.

Wazee wangu, nayasema haya nikitambua kwamba, kama ilivyo katika maeneo mbalimbali hapa nchini, mafanikio makubwa tuliyoyapata katika nyanja za elimu, afya, makaazi bora na kilimo katika kipindi hicho chote hayajaweza kumaliza changamoto zote za maendeleo ambazo zinatukabili.

Wazee wangu, ingawa nimekuwa na kawaida ya kukutana na kuzungumza nanyi mara kwa mara, mmoja mmoja na wakati mwingine katika umoja wenu, wito wangu wa leo una makusudi ambayo kwa kiwango kikubwa ni tofauti na yale ambayo tumeyazoea.

Japokuwa ujumbe ninaotaka kuzungumza nanyi wazee wangu, si mgeni sana masikioni mwenu, tofauti ya leo na mikutano yetu mingine iliyopita ni uamuzi ambao nimekusudia kuufanya na ambao nitayatangaza muda mfupi ujao.

YATOKANAYO

Wazee wangu, naamini mmekuwa mkifuatilia kwa karibu hali ya siasa nchini na hususani afya ya kisiasa na matukio mengine ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho mimi ni mwanachama wake na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) nikiuwakilisha Mkoa wetu wa Tabora.

Naamini kwamba katika kufuatilia kwenu mtakuwa mmebaini kuwapo kwa matukio ambayo kwa namna moja au nyingine yamekuwa yakitokea huku yakiligusa jina langu na wakati fulani nafasi yangu kama kiongozi wa chama hicho.

Wazee wangu, nayasema hayo kwa sababu mara kwa mara ninapokutana nanyi nikiwa katika ziara zangu jimboni na wakati mwingine mnapowasiliana nami kwa njia mbalimbali mmekuwa mkionesha kuguswa kushitushwa na kutaka kujua kulikoni kuhusu mambo hayo yanayotokea.

Mimi, kama mnavyonijua nyote, ni mtu muwazi na mkweli. Siku zote nimekuwa mwepesi sana wa kuwaeleza kuhusu kila kinachotokea ili kuwaondoa hofu na wakati huo huo kuwahakikishia kwamba masuala yasiyo na msingi hususani yale yanayogusa siasa za kitaifa hayawezi kutuondoa katika mstari sahihi wa kuwahudumia wananchi wa Igunga, mkiwamo nyinyi wazee wangu ambao mmeniamini na kunituma kuwawakilisha.

Nyinyi wenyewe ni mashahidi wazuri kwamba tangu matukio yanayogusa jina langu yaanze kutokea miezi michache tu baada ya Serikali ya Awamu ya Nne inayoongozwa na Rais Jakaya Kikweti kuingia madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 2005, tumekuwa tukiyapuuza na tukaendelea kufanya kazi pamoja kwa bidii.

Bado naamini na nitaendelea kuamini kwamba tulifanya uamuzi sahihi wa kuyapuuza matukio hayo kwani mbali ya kuendelea kutimiza malengo mbalimbali yaliyokuwamo katika Ilani yetu ya Uchaguzi ya CCM, pia mliendelea kuniamini kwa nafasi yangu ya kuwa mwakilishi wenu bungeni na hata mkaniruhusu nibebe jukumu jingine kubwa la kuwa Mjumbe wa NEC ninayewakilisha mkoa wetu wa kihistoria wa Tabora.

Wazee wangu, nyinyi ndiyo watu mnaolifahamu vyema jimbo letu la Igunga na hakika nyinyi ni sehemu muhimu ya watu wanaojua historia ya kisiasa ya Mkoa wa Tabora kwa miaka mingi hata kabla ya kuja kwa mfumo wa vyama vingi hapa nchini.

Hakuna shaka hata kidogo kwamba, Tabora ni kitovu hasa cha uasisi wa siasa za vyama vingi hapa nchini. Ni wazi kwamba huwezi ukazungumzia chimbuko la vyama vya upinzani tunavyoviona hapa nchini leo pasipo kugusa mkoa huu ambao umekuwa chimbuko la wanasiasa wenye mizizi hapa na nchini kwa ujumla.

Majina ya wanasiasa wa aina ya wazee wetu, hayati Chifu Said Abdallah Fundikira na Christopher Kassanga Tumbo, Kasela Bantu (Mungu awalaze mahala pema peponi), James Mapalala, Profesa Ibrahim Lipumba na mengi mengine yana mizizi yao katika Mkoa wetu wa Tabora.

Kutokana na ukweli huo basi ni wazi kwamba, nikiwa Mbunge wa Igunga kwa vipindi vinne mfululizo na wakati huo huo nikiwa Mjumbe wa NEC kwa vipindi vitatu mfululizo, moja ya kazi ambazo nimezifanya kwa uaminifu na kwa bidii kubwa huku nikiungwa mkono na kushirikiana nanyi ni ile ya kuhakikisha kwamba mkoa huu pamoja na kuwa kitovu cha upinzani unaendelea kubakia kuwa ngome muhimu ya kisiasa ya CCM.

Si vibaya tukakumbushana kwamba, wakati nachaguliwa kuwa mjumbe wa NEC wa Mkoa mwaka 1997, jimbo moja katika mkoa wetu lilikuwa likishikiliwa na upinzani. Leo hii Tabora ni mkoa pekee miongoni mwa mikoa iliyotuzunguka ambao haukupoteza jimbo hata moja kwenda upinzani katika Uchaguzi Mkuu wa 2010. Mafanikio haya tuliyafikia kwa pamoja kutokana na ushirikiano wenu wazee wangu.

Wazee wangu, Waswahili wanasema usione vyaelea, vimeundwa. Kazi ya kuijenga CCM katika mazingira yenye mizizi hasa ya upinzani nikiwa mbunge na hususani M-NEC kutoka Mkoa wa Tabora haijapata kuwa rahisi na itaendelea kuwa ngumu na ambayo mapambano yake ni makali sana.

Wazee wangu, kwa namna ya pekee kabisa napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru nyinyi wazee wangu wa Igunga na wananchi wenzangu wote wa Mkoa wa Tabora kwa kushikamana na kuifanya kazi hiyo kwa bidii, uaminifu na mafanikio makubwa.

Matunda ya kazi hiyo kubwa yanaonekana. Pamoja na kuwa kitovu cha kihistoria cha siasa za upinzani, Tabora ndiyo mkoa pekee katika eneo hili ambao unaongozwa na wabunge wote kutoka CCM baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na hata kabla ya hapo.

Kwa sababu hiyo basi, wazee wangu, sote katika umoja wetu ukiacha mafanikio makubwa tuliyopata katika jimbo na Wilaya yetu ya Igunga, tunayo mambo mengine ya msingi ya kujivunia. Kwa moyo wa dhati na kwa unyenyekevu mkubwa napenda kuwapongeza kwa namna mlivyojitoa kukipigania na kukitetea chama chetu kwa ari na nguvu ya kipekee.

KUJIVUA GAMBA

Wazee wangu, chama chetu chini ya uongozi wa Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete kimeamua kwa kauli na nia moja kujitathmini na kufanya mabadiliko makubwa ya kimfumo yenye lengo la kukiwezesha kiendelee kubakia chama kinachoaminiwa na kuungwa mkono na Watanzania walio wengi.

Dhamira ya mwelekeo huo wa kufanya mabadiliko ya ndani ya chama chetu ilitangazwa rasmi na Mwenyekiti wetu Rais Kikwete wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa kwa CCM, mjini Dodoma.

Katika hotuba yake hiyo, Rais Kikwete aliyafananisha mabadiliko hayo na tabia ya kawaida na ya asili ya nyoka na wanyama wengine kadhaa ya ‘Kujivua Gamba’.

Wazee wangu hatua ya kwanza ya utekelezaji wa azimio hilo na mwelekeo huo sahihi ilifanyika mjini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati Kuu ya Taifa ya CCM ambacho mimi nilikuwa mjumbe wake.

Wakati wa kikao hicho, wajumbe wote wa Kamati Kuu na wale wa Sekretarieti ya chama chetu wa wakati huo kwa kauli moja tulikubaliana kujiuzulu, lengo likiwa ni kumpa Mwenyekiti wetu fursa nzuri ya kufanya mabadiliko ya uongozi yatakayotoa nafasi ya kupata mwelekeo mpya wa Chama.

Wazee wangu, tulifanya hivyo tukionesha kuunga mkono kwa asilimia 100 kile ambacho bado naendelea kuamini kuwa ni mawazo sahihi na yenye mwelekeo thabiti ya Mwenyekiti wetu ambayo kwa kiwango kikubwa yalikuwa yakiakisi matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa urais, ubunge na udiwani wa Oktoba mwaka jana.

Niliseme kwa maneno machache tu hili. Ingawa ni kweli kwamba Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana umekirudisha madarakani chama chetu kwa kukipa ushindi mkubwa katika uchaguzi wa urais, ubunge na udiwani kwa Tanzania Bara na Zanzibar, kiwango cha ushindi tulichopata kimeonyesha waziwazi dalili za wananchi kupunguza imani yao kwetu kuilinganisha na ilivyokuwa mwaka 2005.

Tungekuwa ni chama cha siasa cha ovyo iwapo tungepuuza kupungua kwa kura za rais kutoka zaidi ya asilimia 80 tulizopata mwaka 2005 hadi kufikia aislimia 61 mwaka jana kiwango ambacho ni pungufu kwa asilimia 20 ya kura katika kipindi cha miaka mitano tu, hasa ikizingatia ukweli kwamba mgombea urais ni mtu yule yule.

Tungekuwa ni chama cha siasa kilichokosa umakini iwapo tungekaa pasipo kuchukua hatua zozote za kujiimarisha baada ya matokeo ya Uchaguzi Mkuu kuonesha wazi kukua kwa upinzani ambao umeongeza idadi ya wabunge na madiwani katika pande zote mbili za muungano.

Matokeo hayo ya uchaguzi ambayo hapana shaka yamekitikisa chama chetu yalitukumbusha wasia ambao tuliachiwa na Baba wa Taifa aliyesema; ‘Bila ya CCM Madhubuti Nchi Yetu Itayumba’.

Wazee wangu, kwa sababu ya kutambua ukweli kwamba hakuna haki isiyo na wajibu kama nilivyosema awali, mimi na wenzangu tuliokuwa katika Kamati Kuu tuliona ulazima, haja na umuhimu wa kukubali kwa kauli moja wito wa kututaka tujiuzulu ikiwa ni hatua moja ya kujipanga na kukijenga upya chama chetu.

KUJIVUA GAMBA KWAPOTOSHWA

Wazee wangu, kilichotokea baada ya kujiuzulu kwetu kila aliye ndani na nje ya chama chetu amekisikia na anakifahamu. Chama kilipata safu mpya ya uongozi iliyotokana na kuundwa kwa Sekretarieti inayoongozwa na Katibu Mkuu wetu mpya, Mhe. Wilson Mukama, na Kamati Kuu iliyokuwa na sura tofauti na ile ya awali.

Wakati tukitafakari na kuangalia mustakabali mpya wa kisiasa ndani ya chama chetu, ghafla yalianza kutokea mambo ambayo chokochoko zake zilianza kusikika tangu tukiwa ndani ya Kamati Kuu ambayo ilijiuzulu baadaye.

Mara tu baada ya kumalizika kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ambacho kilichagua wajumbe wapya wa Kamati Kuu na kuidhinisha uundwaji wa Sekretarieti mpya, dhana ya kujivua gamba ambayo naamini Mwenyekiti wetu aliianzisha kwa nia njema ilianza kuenezwa ikichukua tafsiri na mwelekeo tofauti na ule wa awali.

Wajumbe wawili wa Sekretarieti, Naibu Katibu Mkuu (Tanzania Bara), Mhe. John Chiligati, na Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi, Mhe. Nape Nnauye, walisikika wakitangaza kwamba Halmashauri Kuu ya Taifa ilikuwa imefikia uamuzi wa kuwapa siku tisini wale walioitwa watuhumiwa wanaokabiliwa na tuhuma za ufisadi ndani ya chama kujitoa katika nafasi zao za uongozi vinginevyo watafukuzwa na chama.

Wazee wangu, baada ya kushinikizwa sana na vyombo vya habari wawataje kwa majina wanasiasa waliokuwa wakituhumiwa kwa ufisadi ambao ni wajumbe wa NEC na ambao wanapaswa kujiuzulu nyadhifa zao, wajumbe hao wa Sekretarieti walikwenda mbele zaidi.

Baada ya awali kuwaeleza waandishi wa habari kwamba majina ya watuhumiwa hao yalikuwa yakifahamika kutokana na kuhusishwa katika kashfa tofauti kama zile za Richmond, EPA na ununuzi wa rada, mwishoni viongozi hao walikaririwa wakiyataja majina ya wanasiasa watatu kuwa ndiyo ambao walikuwa wakilengwa na maamuzi hayo.

Wazee wangu, nilishangazwa na kushitushwa na namna porojo na fitina za kisiasa zilivyofinyangwa kwa mara nyingine tena baada ya kusikia jina la mbunge wenu ambaye ni mimi, likitajwa kuwa miongoni mwa yale matatu ya viongozi waliokuwa wakitakiwa eti kupima wenyewe na kisha kuchukua uamuzi wa kujiuzulu nafasi zao za uongozi ndani ya NEC katika kipindi cha siku tisini.

Niliseme hili mapema. Mshangao na mshituko wangu haukusababishwa na kutajwa kwa jina langu, la hasha, bali namna uamuzi halisi wa NEC na hususani dhana nzima ya ‘kujivua gamba’ ilivyoweza kupindishwa na wajanja wachache na kisha kuendeshwa kwa maslahi binafsi ya kikundi fulani cha watu.

Pili, nilishangazwa na kushitushwa na hatua ya viongozi wa chama changu ambacho nimekitumikia kwa bidii na uaminifu mkubwa kufanya juhudi kubwa hata kukivisha kikao kitukufu cha NEC uamuzi ambao msingi wa hoja zake ni vita vya kimakundi ya kisiasa yaliyo ndani ya CCM kwa upande mmoja na propaganda za vyama vya siasa vya upinzani na vyombo vya habari kwa upande mwingine.

Tatu, nilishangazwa na kushitushwa na ujasiri ambao umekuwa ukioneshwa na baadhi ya viongozi wetu wapya wa Sekretarieti wanaolitaja jina langu na kulihusisha na kile wanachokiita ufisadi ambao hata ukweli wa kimazingira na kihistoria ukiachilia mbali ushahidi wa wazi umeshathibitisha kwamba ni porojo za kisiasa zilizotokana na makovu na matarajio ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 na ule ujao wa 2015.

Wazee wangu, nyinyi ni mashahidi kwamba, mbali ya mimi mwenyewe kujitokeza kupitia vyombo vya habari na kueleza wazi kwamba sijapata kujihusisha katika vitendo vyovyote vya ukiukwaji wa maadili ya uongozi au vya rushwa, hakuna ushahidi wowote uliotolewa unaonihusisha na kashfa yoyote miongoni mwa zile zilizotajwa.

Wazee wangu, ni wazi kwamba kama chama chenye siasa chenye dhamana ya kuwaoongoza Watanzania kutoka katika lindi la ufukara, maradhi, matatizo ya makaazi na mengineyo siku zote tunapaswa kuwa makini katika kuhakikisha kwamba changamoto za kuwaongoza na kuwakomboa wananchi waliotupa dhamana hazitikiswi na mawimbi ya matakwa ya nyakati ama ya vyombo vya habari au wapinzani wetu wa kisiasa walio nje ya CCM.

Ni kwa sababu ya kulitambua hilo na hasa kuyatambua madhara yanayoweza kukipata chama chetu na nchi yetu iwapo tutaendekeza siasa za kupakana matope pasipo na sababu za msingi, kuchafuana kusikokoma na kulipizana kisasi ndiyo maana nimeona nitumie fursa hii kuzungumza nanyi wazee wangu ili kuweka kumbukumbu sahihi.

MAAMUZI YANGU

Wazee wangu, nimetafakari sana na kimsingi nimefikia hatua ya kupima yale ambayo yamekuwa yakisemwa na kuandikwa juu yangu na ambayo kwa mtazamo wangu unaoungwa mkono na wanafamilia yangu, marafiki zangu na washirika wangu wa kibiashara walio ndani na nje ya nchi, naona umefika wakati muafaka wa kuchukua hatua.

Kwa sababu ya kutambua uzito wa hatua ninazokusudia kuzichukua, niliona halitakuwa jambo la hekima hata kidogo iwapo ningefanya hivyo pahala pengine popote bali hapa Igunga mbele ya nyie wazee wangu.

Baada ya kukaa na wanafamilia yangu, marafiki na washirika wangu wa kibiashara niliona halitakuwa jambo la busara hata kidogo kuendelea kuvutana na viongozi wa chama changu na wanachama wenzangu wa CCM katika mambo ambayo yanaweza kumalizwa kwa njia muafaka.

Wazee wangu, sina budi niwaeleze kwamba, mbali ya athari za kisiasa na kifamilia, vita vya ovyo vya kisiasa kama hivi tunavyoviendesha na kuviendeleza ndani ya CCM na ndani ya nchi yetu huwa vina athari kubwa katika ulimwengu wa kibiashara. Athari kama hizo za kibiashara huingia ndani zaidi kuliko vichwa vya habari vya magazeti vinavyolenga kuchafuana, na athari hizo huwa kubwa zaidi kwa mtu kama mimi kwa sababu tofauti na wengine wengi hapa nchini, mimi ni mfanyabiashara wa kimataifa.

Katika ulimwengu wa kibiashara wa leo, vita hivi ambavyo vinaweza kuonekana kuwa ni vidogo tu vyenye malengo ya kuchafuana kisiasa, vinakuwa na athari kubwa katika uhusiano wa kibiashara kuliko hata wale wasioelewa wanavyoweza kukadiria. Ndiyo maana nimeona ni afadhali sasa niwape nafasi wale wanaoendesha siasa hizi uchwara na zisizo na tija waendelee na siasa zao hizo ambazo kwa bahati mbaya kwao, mimi sina muda nazo na siwezi kuwa sehemu yake. Na mimi kwa upande wangu niendelee na maisha yangu.

Kutokana na ukweli huo na sababu zote hizo basi, kwa moyo wa dhati na kwa nia thabiti, hatua ya kwanza niliyoiona kuwa ninapaswa kuichukua ilikuwa ni hii ya kuitikia wito unaotokana na msukumo wa ndani ya nafsi yangu wa kuamua kukomesha kabisa malumbano na mivutano isiyo na manufaa kwangu binafsi, kwa viongozi wa chama changu na chama chenyewe.

Msukumo huo si mwingine bali ni ule wa kuamua kuachia nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama, nikianzia na ile ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa nikiuwakilisha Mkoa wa Tabora na hii ya ubunge wa Igunga ambazo kama si kwa baraka za chama changu nisingelikuwa nazo.

Napenda kuliweka hili sawa sawa. Uamuzi wangu wa kuachia nafasi zangu zote za uongozi nilizopata kwa tiketi ya CCM haukutokana na wala haumaanishi kukubaliana na shinikizo lililopotoshwa kuhusu azma ya utekelezaji wa dhana ya kujivua gamba, la hasha, bali dhamira ya dhati ya kuachana na siasa hizi uchwara (gutter politics) na kutumia muda wangu kushughulika na biashara zangu.

Aidha, nimefikia uamuzi huo lengo likiwa ni kuwajengea heshima na imani machoni mwa wanachama na wananchi wengine, viongozi wangu ambao naamini baada ya mimi kujitoa watapata fursa ya kutafakari upya changamoto nyingine mbadala zinazowakabili ambazo msingi wake ni dhamana kubwa walizo nazo za kukiongoza chama chetu na nchi yetu kupitia Serikali yake.

Wakati nachukua uamuzi huu, natambua vyema kwamba, watatokea watu ndani ya chama chetu na nje ambao watafanya kila juhudi kupotosha au kupindisha ukweli kuhusu hatima yangu ya kisiasa baada ya kujiweka kando na kujipa mimi mwenyewe na chama changu fursa ya kutafakari kwa kina majaaliwa yangu na ya nchi yangu katika siku zijazo.

Nafanya hivyo nikiwa na imani thabiti kwamba, uamuzi wangu huu, hususani ule wa kuachia nafasi yangu ya ubunge, yatakipa fursa nyingine CCM ya kuendelea kuliongoza jimbo letu la Igunga katika kipindi cha miaka minne ijayo kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Kwa upande mwingine, uamuzi wangu huu naona ni fursa kwa viongozi wa Chama changu cha CCM kutafakari na kuamua njia wanayoiona wao ni sahihi kuichukua kwa hatima na mustakabali wa chama chetu na ambayo wanaamini itakipa nguvu mpya ya kisiasa dhidi ya vyama vya upinzani.

Sambamba na hilo, ninayo imani thabiti kwamba, uamuzi wangu wa kubakia kuwa mwanachama wa kawaida na mtiifu wa CCM utakuwa chachu kwa chama changu na kwa Serikali yake kuwatumikia wananchi kwa Ari Zaidi, Kasi Zaidi na Nguvu Zaidi.

Mwisho kabisa, nikimalizia naomba nitumie fursa hii kutoa heshima za pekee kwa Rais Jakaya Kikwete kwa kazi kubwa aliyoifanyia na anayoendelea kuifanyia nchi yetu. Amefanya mengi na makubwa kuiendeleza nchi yetu na watu wake kuliko inavyothaminiwa na kufahamika. Kazi yake kubwa inashindwa kuthaminiwa na kufahamika kutokana na siasa chafu tunazoziendesha Tanzania. Wasia wangu kwa wanasiasa wenzangu, waandishi wa habari na Watanzania wenzangu kwa ujumla ni kuwa tunahitaji kuisaidia nchi yetu kwa kufanya siasa zenye mwelekeo wa kujenga ambazo ndiyo hasa zinapaswa kuwa siasa kwa maana halisi ya neno hilo.

Wazee wangu, baada ya maelezo hayo, nawashukuru sana kwa kunisikiliza na kunielewa.

Ahsanteni sana.
 

Tuesday, July 12, 2011

Ludacris ndani ya Serengeti Fiesta 2011

Best Blogger Tips
Via Tanzania Daima

MWANAMUZIKI mahiri wa miondoko ya hip hop ambaye pia ni mwigizaji wa filamu kutoka nchini Marekani, Christopher Brian Bridges ‘Ludacris’ anatarajiwa kutoa shoo ya aina yake kwenye kilele cha tamasha la Serengeti Fiesta 2011, kitakachofanyika viwanja vya Leaders Club, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na kusainiwa na Mkurugenzi wa Maendeleo na Utafiti wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, taratibu zote za kumleta Ludacriss zimekamilika, hivyo Watanzania wakae mkao wa kupata raha wakati wowote kuanzia sasa.

Aidha, aliongeza kuwa, mwanamuziki mwingine wa kimataifa kutoka nje, atatajwa baadaye ambako wote kwa pamoja wanatarajiwa kutumbuiza kwenye tamasha la miaka 10 ya msimu wa dhahabu unaoendelea na Serengeti Fiesta 2011 kwenye viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Julai 30.

Ruge alisema kwamba shamrashamra za kufikia kilele cha miaka 10 ya Serengeti Fiesta 2011 zitakuwa tofauti na zenye msisimko mkubwa, ikilinganishwa na miaka mingine yote iliyowahi kufanyika tamasha hilo, ambalo ni kubwa katika anga ya burudani ndani na nje ya Tanzania ikiwamo Afrika Mashariki kwa ujumla.

Wakati huo huo, Mutahaba ametoa shukurani kwa wakazi wa Mkoa wa Iringa na Mbeya kwa namna walivyojitokeza kwa wingi na kulikubali tamasha hilo ambalo hufanyika mara moja tu kila mwaka.

Wikiendi hii tamasha la Serengeti Fiesta 2011 litakuwa ndani ya mji wa Moshi kwenye uwanja wa Chuo cha Ushirika huku jijini Arusha litafanyika Namatongee.

Wachezaji wa Eritrea waingia mitini Tanzania

Best Blogger Tips
Via Tanzania

Wachezaji kumi na watatu wa timu ya mpira wa miguu ya Eritrea ya Red Sea mpaka sasa hawajarejea nchini kwao baada ya michuano ya kanda Tanzania, maafisa wamesema.

Baada ya Klabu hiyo ya Red Sea kupoteza ushindi wake katika michuano ya CECAFA ya nusu fainali siku ya Jumamosi, ni nusu tu ya wachezaji wote waliingia kwenye ndege kurejea Eritrea.

Inaripotiwa kuwa hii ni mara ya nne wa wachezaji wa mpira wa miguu kutoka Eritrea wanatoweka.

Vijana wa Eritrea mara kadhaa wanajaribu kukimbia umaskini, seikali ya kibabe na jeshi kujenga taifa.

Katibu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Tanzania Angetile Osiah ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa suala hilo limeripotiwa kwenye vyombo vya sheria kwa ajili ya Uchunguzi.

"Baadhi ya wachezaji waligongana katika tukio la kujaribu kugonga muhuri pasi za kusafiria za wachezaji ambao hawakuwepo wakati wa ukaguzi katika ofisi uhamiaji uwanja wa ndege lakini walipohesabiwa mmoja mmoja iligunduliwa kuwa wachezaji 13," alisema.

Timu ya Tanzania ya Yanga iliwashinda mahasimu wake wa muda mrefu Simba 1-0 katika fainali ya CECAFA Jumapili.

Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits