Sunday, October 31, 2010

Best Blogger Tips
Upigaji kura wamalizika Tanzania

Via BBC

Mamilioni ya Watanzania wamejitokeza kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, uchaguzi ambao kwa jumla umekwenda kwa hali ya utulivu licha ya matatizo na vurugu za hapa na pale.

 Wapiga kura kadha hawakuweza kupiga kura kutokana na majina yao kutokuwemo katika daftari la wapigaji kura, kwingineko karatasi za kupigia kura zilichelewa kufika au hazikufika kabisa.

Katika visiwa vya Zanzibar, karatasi za kupigia kura katika uchaguzi wa rais na wabunge wa muungano zilikosekana katika vituo mbalimbali.

Uchaguzi wa madiwani umelazimika kuahirishwa hadi siku zijazo kwa sababu hizo hizo.

Vituo vya uchaguzi vimefungwa rasmi saa kumi jioni, huku kazi ya kuhesabu kura ikianza katika vituo hivyo.

Wapiga kura milioni 19.6 walitarajiwa kushiriki katika upigaji wa kura.

Wakati huo huo Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini Tanzania imetangaza imeahirisha Uchaguzi katika baadhi ya Majimbo na Kata kutokana na upungufu uliojitokeza hususan katika karatasi za kura.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Rajabu Kiravu, Kata na Majimbo ambayo uchaguzi wake umeahirishwa ni kama ifuatavyo:-

1. Uchaguzi wa Wabunge katika majimbo ya Nkenge, Mpanda Mjini na Mpanda vijijini. Kwa upande wa Zanzibar (Unguja) Majimbo ya Mwanakwerekwe, Mtoni na Magogoni, na Wete (Pemba)
2. Uchaguzi wa Madiwani katika kata zifuatazo:


HALMASHAURI KATA

1. Newala DC Mtonya

2. Mbulu DC Endegikot

3. Manyoni DC Kitaraka

4. Same DC Kisiwani

5. Kibaha DC Janga

6. Rufiji (a)Kibiti

(b) Chemchem

(c) Ngorongo

(d) Kipugira

(e) Mjawa

7. Uyui DC (a)KIgwa

(b)Ibelamilundi

8. Sikonge Kisanga

9. Njombe Mji Mwema

10. Ulanga DC Msogezi

11. Karagwe DC (a) Kimuli

(b) Kamuli

12. Kasulu Kitagata

13. Chato DC Buseresere

14. Mwanza (Jiji) (a) Mkuyuni

(b) Mirongo

Hata hivyo katika majimbo hayo matatu ambapo Uchaguzi wa Wabunge umeahirishwa, uchaguzi wa Rais na Madiwani umefanyika kama ilivyopangwa.

Vile vile, katika Kata ambazo Uchaguzi wa Madiwani umeahirishwa, Uchaguzi wa Rais na Wabunge umefanyika kama ilivyopangwa.

Tume hiyo ya Taifa ya Uchaguzi imesema tarehe za kufanyika uchaguzi huo itatangazwa hapo baadaye.
Best Blogger Tips

Jina langu lilikatwa nisigombee ubunge - Dk. Mwakyembe

Via Ippmedia

  Mgombea Ubunge Jimbo la Kyela kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Dk.Harrison Mwakyembe, amevunja ukimya kwa kutoboa siri kwamba Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Mbeya ilikata jina lake ili asiwe mgombea.

Lakini akasema pamoja na mbinu hiyo, Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete, ndiye aliyeokoa jahazi kwa kuamuru jina lake lirejeshwe ili kulinda heshima na maamuzi ya wananchi wa Kyela waliompa kura nyingi wakati wa mchakato wa kura za maoni.

Dk. Mwakyembe alitoa madai hayo mazito wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kijiji cha Mpunguti, kata ya Makwale, alipokuwa akieleza sababu zinazomfanya aendelee kumnadi mgombea urais kupitia CCM, Dk. Kikwete, licha ya mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk.Wilbroad Slaa, kumtaka asimnadi mgombea huyo ili chama chake kisiweke mgombea ubunge wa kupambana naye jimbo la Kyela.

“Nawajibika na nalazimika kumpigia debe Rais Kikwete kwa sababu bila ya JK nisingesimama kuongea nanyi hapa, Kamati ya Siasa Wilaya walinipa alama A kwa maana ya kwamba nafaa kugombea kwa tiketi ya CCM, lakini jina lilipopelekwa kwenye kikao cha Kamati ya Siasa ya Mkoa ambayo miongoni mwa wajumbe wake ni Mkuu wa Mkoa walikata jina langu,” alisema.

Dk. Mwakyembe ambaye alipata kura 15,336 wakati wa mchakato wa kura za maoni, alidai kuwa wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Mbeya walichukua uamuzi wa kukata jina lake na kumpa mgombea aliyeshika nafasi ya pili katika kura za maoni kwa madai kuwa “yeye ni mkorofi, amewaumiza wenzake hasa katika suala la mkataba tata wa kampuni ya Richmond”.

"Kamati ya siasa ya Mkoa imekata jina langu, wengine tunapenda kutoa hoja za msingi na siyo hadithi, walikata jina langu na leo nalazimika kusema hivyo, kisa eti mimi ni mkorofi nilishawaumiza wenzangu, mimi nashangaa watu wanaozungumzia mambo hayo, unajua tunaanza kuwa taifa linalokosa maadili, umeumiza nini, mwizi umwangalie umchekee chekee?" alihoji.

Hata hivyo, alisema baada ya matokeo ya maamuzi hayo kupelekwa Dodoma kwenye kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichoketi chini ya Mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete, kiongozi huyo wa CCM aliamuru jina lake lirejeshwe haraka ili kuzingatia demokrasia ya wananchi wa wilaya ya Kyela ambao walimpa kura nyingi wakati wa mchakato wa kura za maoni.

Alisema kutokana na upendo alionao Rais Kikwete kwa wananchi wenzake, kuna kila sababu kwa wana- Kyela kuhakikisha leo wanamchagua mgombea huyo wa urais wa CCM ili aweze kuendeleza mipango ya maendeleo katika jimbo hilo.

Saturday, October 30, 2010

Best Blogger Tips
R.I.P Syllesaid Mziray


Kocha aliyechangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya soka nchini Tanzania, Syllesaid Mziray "Mwanangu", amefariki dunia asubuhi ya leo katika hospitali ya Agakhan, jijini Dar-es-salaam. 

Coach Mziray, aliyekuwa mwajiriwa wa Chuo kikuu huria kama Mhadhiri, atakumbukwa kwa umahiri katika ufundishaji soka katika vilabu mbalimbali hadi timu ya Taifa iliyoshinda ubingwa wa Nchi za Afrika Mashariki.

Alifundisha pia Pilsner, Simba, Yanga, Pan African na kabla mauti kumkuta alikuwa mwalimu wa viuongo na saikolojia wa klabu ya Simba.


Mwenye-ezi Mungu Umuweke Mahala Pema Peponi Super Coach Syllesaid Mziray.

Friday, October 29, 2010

Best Blogger Tips

Leo ni funga kazi ya kampeni 2010
 
HATIMAYE mbio za kampeni kwa ajili ya uchaguzi mkuu zinahitimishwa leo kwa wagombea kufunga pazia kwenye maeneo mbalimbali kabla ya Watanzania kuamua mustakabali wa nchi yao kesho.
Kampeni hizo zilizinduliwa rasmi Agosti 20 na vyama kuanza kujinadi siku iliyofuata wakati CCM ilipofanya mkutano wake kwenye viwanja vya Jangwani na kufuatiwa na CUF iliyoendesha mkutano wake Agosti 27 kwenye Uwanja wa Kidongo Chekundu na baadaye Chadema ilizindua kampeni zake Agosti 28 kwenye viwanja vya Jangwani.

Vyama hivyo vitatu, ambavyo vinachuana vikali kwenye kinyang'anyiro cha urais, vilifungua pazia kwa vyama vingine kuzindua kampeni zake kwa staili tofauti na viwanja tofauti na leo vitakuwa vikitupa karata ya mwisho baada ya safari ndefu zaa kujaribu kuwafikia wananchi kwenye mikoa tofauti ya Bara na Visiwani.

Wakati vyama hivyo vilitegeana wakati wa uzinduzi, leo vyote vitakuwa majukwaani kuhitimisha kampeni hizo ili kuwaweka sawa wapigakura kabla ya kufanya maamuzi yao kwa siri kesho.
CCM, ambayo inawania kubakia madarakani ili kuendeleza ubabe wake wa takriban miaka 49, itahitimisha kampeni zake kwenye viwanja vya Jangwani ambako mgombea wake wa urais, Jakaya Kikwete atahutubia wafuasi na wanachama wa chama hicho kikongwe.

Chadema, ambayo bila ya kutarajiwa imeonekana kutoa upinzani mkali kwenye kinyang'anyiro cha urais ambacho katika chaguzi zilizopita kilikuwa kati ya CCM na CUF, itahitimisha kampeni zake mkoani Mbeya ambako mgombea wake wa urais, Dk Willibrod Slaa atahutubia.
CUF, ambayo mgombea wake wa urais, Prof Ibrahim Lipumba anawania kwa mara ya nne kuingia Ikulu, itahitimisha kampeni zake kwenye Uwanja wa Kidongo Chekundu jijini Dar es salaam ambako watapokonyana mashabiki na CCM.

Monday, October 25, 2010

Best Blogger Tips
Mauaji Maswa: Shibuda aachiwa huru



 JESHI la Polisi limemwachia huru mgombea ubunge wa Jimbo la Maswa Magharibi kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Shibuda, kwa madai hakuhusika na mauaji yaliyosababishwa na vurugu zilizotokea katika Kijiji cha Kizungu, wilayani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Maswa jana, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini, Robert Manumba, alisema wameamua kumwachia huru mgombea huyo kutokana na upelelezi wa awali kuonyesha kuwa hakuhusika na tukio hilo.

Alisema upelelezi huo umeonyesha wazi kuwa hakuwepo katika eneo la tukio ambapo mauaji hayo yalipotokea baada ya wafuasi wa vyama vya CHADEMA na CCM waliposhambuliana na kusababisha kifo cha Stephen Kwilasa.

“Unajua linapotokea tukio kama hilo la mauaji ni lazima tufanye upelelezi kwa makini, ili kuweza kutenda haki kwa pande zote na sisi kama polisi tupo hapa kwa ajili ya kulinda usalama wa raia, hasa katika matukio haya ya kampeni za kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu, ni lazima tufanye kazi kwa umakini mkubwa,” alisema.

Alisema bado wanaendelea na upelelezi na iwapo itabainika kwa namna moja au nyingine alihusika na tukio hilo, atafikishwa mahakamani na kuongeza kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria.

Aidha, alisema Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM wa Kata ya Nyalikungu, Abel Jombo, amelalamika katika Kituo cha Polisi Maswa dhidi ya Shibuda akidai kuwa alimpiga mateke alipopelekwa katika eneo la mkutano, ambapo alikuwa akihutubia mgombea huyo na kusisitiza kuwa upelelezi wa tukio hilo haujakamilika.
Endelea kusoma habari hii..............
Best Blogger Tips
Gregory Isaac Dead - Reggae Star dies of cancer

Reggae legend Gregory Isaacs has died after a battle with cancer.
Isaacs, who was 59 years old, died on Monday morning at his home in London where he spent part of his time.

He leaves behind a wife and children.

Close friends told BBC Caribbean that he had originally been diagnosed with cancer of the liver which had then spread.

The Jamaican reggae singer, who was nicknamed the Cool Ruler, was best known for the song 'Night Nurse'.








 

Saturday, October 23, 2010

Best Blogger Tips
Mugabe hands Munya US$300,000



BIG Brother Africa star Munyaradzi Chidzonga has received US$300,000 from President Robert Mugabe following his disappointment of controversially missing out on winning the reality TV show last Sunday.

The money was raised overnight after businessmen Phillip Chiyangwa and David Chapfika set up a Chidzonga Trust Fund and opened a bank account on Tuesday to marshal donations.

Wednesday’s gift, received by Munya at State House, means he has now received MORE MONEY than the show’s winner Uti Nwanchukwu of Nigeria who took home US$200,000.

Munya received a hero’s welcome as he emerged from the arrivals terminal at the Harare International Airport, coming from South Africa where the show is filmed.
 
But fans were left high and dry after the Big Brother star was bundled into a maroon Chevrolet and driven to State House.
   
Best Blogger Tips
CCM, Chadema walumbana mauaji Maswa

Via Mwananchi

WAKATI Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba akikitupia makombora Chadema kwamba kinahusika na mauaji yaliyotokea katika mkutano wa kampeni, Jimbo la Maswa Magharibi, Chadema kimesema chama hicho tawala ndicho kitabeba lawama kwa kuvamia mkutano wao.

Mgombea urais wa Chadema, Dk Willibrod Slaa akiwa katika mkutano wa kampeni mkoani Tanga jana alisema maafa hayo yamesababishwa na CCM kwa kuwafundisha na kuhamasisha vijana wake kuvamia mikutano ya vyama vingine vya siasa.

Alisema muda sasa umefika kwa serikali kuonyesha kwa vitendo kwa kuwashughulikia wote wanaohusika kuvunja amani ya nchi bila kujali itikadi zao za kisiasa kwa kuwakamata na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria kwani kuvunja amani ni kosa la jinai.

Dk Slaa alitaja baadhi ya maeneo nchini ambako umwagaji damu umetokea mpaka sasa kutokana na sababu za kisiasa kuwa ni pamoja na Hai, Kagera, Tarime, Mwanza, Mpanda na Maswa na kuhoji sereikali inasubiri watu wangapi wajeruhiwe au kupoteza maisha ndipo ichukue hatua.

"Tangu nimeanza mikutano yangu inayokaribia zaidi ya mikutano 460 hadi sasa nimesisitiza amani na kueleza wazi kuwa siko tayari kwenda Ikulu kwa wananchi wangu kuvamiwa, kupigwa na kujeruhiwa na wengine kupata ulemavu au kupoteza maisha. Nimekuwa nikimuomba Kikwete ajitokeze hadharani kukemea vitendo vya vijana wa CCM kuanzisha vurugu na avunje na kupiga marufuku makambi ya vijana hao lakini hata siku moja hajafanya hivyo ikiwa ni dalili ya kuunga mkono vitendo hivyo," alisema Dk Slaa.

Wakati Slaa akisema hayo, kwa upande wa CCM Katibu Mkuu wa chama hicho, Yusufu Makamba amesema kuna ushahidi wa kimazingira unaoonyesha kuwa mgombea wa Chadema jimbo la Maswa Magharibi, John Shibuda amehusika katika mauaji yaliyotokea juzi wilayani humo na kusababisha kifo cha mtu mmoja

Makamba ambaye alikuwa wilayani Maswa jana ambapo mbali na kufanya shughuli za chama pia alikwenda kutoa salamu za rambirambi kwa ndugu wa merehemu Steven Kwilasa, ambaye alikuwa dereva wa mgombea ubunge wa jimbo la Maswa Magharibi kupitia CCM, Robert Kisena.
Endelea kusoma habari hii..............

Monday, October 18, 2010

Best Blogger Tips

Alicia Keys Calls Motherhood ‘Bliss’


Alicia Keys is “Fallin’” for motherhood!
The gorgeous Grammy-winner, who gave birth to her son, Egypt, on Thursday, took to her Twitter page to share her maternal joy.

“There is no word to properly describe LOVE, to describe BLISS, to express a FEELING like this!!!” Alicia Tweeted on Sunday.

“Thank U 4 your love, support & prayers! ;-),” she added.

As previously reported on AccessHollywood.com, a representative for Alicia said the star gave birth on Thursday night in New York. Alicia and her husband, rapper-producer Swizz Beatz, have named their son Egypt Dean.

Egypt is the first child for the 29-year-old superstar and the fourth child for Swizz, whose real name is Kaseem Dean. The couple married on July 31.

Swizz, 31, took time to Tweet about his son’s arrival on Friday, calling the arrival another blessing.

“I’m so thankful for everything I been blessed with in my life wowwwwww!” he wrote.
Source: Access Hollywod

Thursday, October 14, 2010

Best Blogger Tips
Gari la Chenge lagonga tena, laua


MGOMBEA ubunge wa Jimbo la Bariadi Magharibi mkoani Shinyanga (CCM), Andrew Chenge ameingia matatani tena baada ya gari lake kudaiwa kumgonga mwendesha pikipiki na kusababisha kifo wakati akitoka kwenye kampeni.

Tukio hilo limetokea wakati mwanasheria huyo wa zamani akiendelea na kesi ya mashtaka mawili ya kuendesha kizembe na kugonga pikipiki ya matairi matatu na kusababisha vifo vya watu wawili na jingine la kuendesha gari ambalo bima yake ilishaisha.

Hata hivyo, imeelezwa kuwa katika ajali ya jana waziri huyo wa zamani wa Miundombini hakuwa akiendesha gari hilo, bali alikuwa ndani.

Habari zilizopatikana jana kutoka wilayani Bariadi zimeeleza kuwa Chenge akiwa anatokea Kijiji cha Namisagusa na Kilalo alikokuwa na mkutano wa kampeni kuelekea mjini Bariadi, alipata ajali hiyo katika Kijiji cha Mbiti kilicho Kata ya Mhango, Tarafa ya Ntunzu.

“Hii ajali imetokea majira ya saa 1:00 usiku, Chenge baada ya kuona gari lake limegonga alishuka na kuhamia katika gari jingine na kuondoka eneo hilo. Wananchi walipofika hapo walilizuia gari hilo, lakini baadaye wakatimuliwa na polisi ambao waliliondoa gari hilo,” alieleza Patrick Liyuba mmoja wa wananchi wanaodai kushuhudia ajali hiyo.
Source: Mwananchi
Best Blogger Tips
'The View': Joy and Whoopi walk out on Bill O'Reilly


What you see here is the “Before” moment. Bill O’Reilly appeared on The View today to argue against Park51, the Muslim community center slated to be built two blocks from the World Trade Center.

 First he spoke to Joy Behar like a child: “Hold it, hold it. Listen to me because you’ll learn.” She responded in the only practical way: bunny ears. O’Reilly kept at it, insisting that 70 percent of Americans don’t want this mosque.

 “Where’s that poll?” Joy wondered. The eruption occurred after O’Reilly blamed Muslims for the WTC attacks: “Muslims didn’t kill us on 9/11? That’s what you’re saying?” O’Reilly wanted to make sure. And Whoopi and Joy stormed off the set! “I don’t want to sit here anymore,” Joy said, to clarify.

Barbara Walters took the reins.”You have just seen what should not happen. We should be able to have discussions without washing our hands and screaming and walking offstage. I love my colleagues, but that should not have happened.
Source: EW.com

Best Blogger Tips

Mgodi Chile: Miujiza yasherehekewa


Rais wa Chile amesema kamwe nchi yake haitarejea hali iliyokuwa nayo awali baada ya kukamilika kwa shughuli ya uokoaji wa wachimba migodi 33 waliokuwa wamenaswa chini ya ardhi kwa siku 69.

Sebastian Pinera amesema anahisi wananchi wa Chile sasa "wana umoja zaidi na imara kuliko wakati mwingine wowote" na wanaothaminika kote duniani.

Kulikuwa na kila hali ya ushangiliaji wakati Luis Urzua, mwenye umri wa miaka 54, mchimbaji wa mwisho alipotolewa nje ya mgodi huo.

Shughuli hiyo iliyofanyika kwa saa 22, ilitekelezwa kwa kila mmoja wao kutolewa kwa kutumia chombo maalum. Wote sasa wamepelekwa hospitalini.

Baadhi yao wamebainika kuwa na matatizo ya meno, na wengine wanasumbuliwa na macho kutokana na kuishi katika vumbi na giza mgodini humo. Mmoja wao amegundulika kuwa na kichomi, ingawa hali yake inaelezewa kuwa si mbaya sana.
Endelea kusoma habari hii...................
Best Blogger Tips

Inside Story: T.I. Knew in His Heart He Needed to Save Suicidal Atlanta Man


What started off as any other day for T.I. ended with an emotional rescue as the rapper helped coax a suicidal Atlanta man off a ledge Wednesday.

After hearing about the man, who was contemplating jumping off the V103 radio station building, the rapper decided he needed to stop listening and do something.

"People were trying to talk to him and tell him to get down," the rapper, 30, whose real name is Clifford Harris Jr., tells PEOPLE in a phone interview from the set of his new music video. "Something in my heart just said, 'You need to help.' At that point, I started calling people at the radio station."

But the radio station said the man was unresponsive to their pleas not to jump – so T.I. drove himself to the scene.

"I went down there and talked to a police officer and he sent me to the negotiator," the rapper says. "They told him I was there and he started responding a little bit."
Access the full story....................
Best Blogger Tips
Ndoto za Nyerere zimewekwa kando


WASOMI, wanasiasa na viongozi wa dini wamesema ndoto za Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere zimemezwa na watu wachache wenye uchu wa madaraka na wasiojali wala kuitakia mema Tanzania.

Wakitoa maoni yao jana kwa nyakati kuhusiana na maadhimisho ya miaka 11 tangu Mwalimu Nyerere alipofariki dunia inayofanyika leo, wanazuoni na viongozi hao waliwataka Watanzania mwaka huu kumwenzi muasisi huyo taifa kwa kutowachagua watu wabaya na kuwahimiza wagombea wa nafasi mbalimbali kuheshimu matokeo ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Okotba 31.

Walisema maadili ya uongozi yaliyoachwa na Nyerere yamesahauliwa na viongozo hivyo kuna haja kwa taifa kurejesha maadili hayo ili kuinusuru nchi.
Mwalimu Nyerere alifariki dunia kwa ugonjwa wa saratani ya damu Oktoba 14, 1999 katika Hospitali ya Mtakatifu Thomas nchini Uingereza alikoenda kutibiwa.

''Moja ya mambo ya msingi ambayo tunapaswa kumuenzi Mwalimu Nyerere, ni kuheshimu maamuzi ya wananchi katika kuchagua mgombea wa urais, ubunge na udiwani. Kuchakachua matokeo, itakuwa ni jambo la hatari,'' alisema aliyewahi kuwa Waziri katika Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Arcado Ntagazwa.

Ntagazwa alisema kuheshimu maamuzi ya wananchi ni sehemu ya kumuenzi Mwalimu Nyerere katika kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu.
Endelea kusoma habari hii..............

Wednesday, October 6, 2010

Best Blogger Tips

Sunday, October 3, 2010

Best Blogger Tips
Helkopta ya Dr Slaa ikitua Iringa

Helkopta ya Dr Slaa ikitua katika moja ya mikutano yake ya kampeni Mkoani Iringa. Picha kwa hisani ya francisgodwin.blogspot.com
Best Blogger Tips

 

Best Blogger Tips

Nigeria: Mshukiwa wa bomu akamatwa SA


Kiongozi wa zamani wa kundi la waasi nchini Nigeria ametiwa nguvuni kuhusiana na mashambulio ya bomu nchini Nigeria ya Ijumaa iliyopita.

Henry Okah alikamatwa na maafisa wa polisi wa Afrika Kuisni katika nyumba yake mjini Johannesburg. Okah aliwahi kuwa kiongozi wa kundi la MEND kundi la waasi lililofanya mashambulio mengi dhidi ya maeneo ya mafuta.

Kundi hilo limedaiwa kuhusika katika mashambulio hayo japo lilikuwa linastahili kutekeleza usitishwaji wa vita chini ya makubaliano kati yake na serikali.
Source: BBC

Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits