Tuesday, January 31, 2012

Mama yake Drogba awapikia mashabiki

Best Blogger Tips
Wakati mshambuliaji wa Ivory Coast Didier Drogba akiwa uwanjani, mama yake anawapikia chakula mashabiki wa nchi yake katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika. 

Clotilde Drogba amefungua mgahawa karibu na uwanja wa mpira katika viunga vya mji mkuu wa Equatorial Guinea, Malabo, limeripoti shirika la habari la AP.

Mama huyo anapika kuku na samaki na wali, ndizi na vyakula vingine kwa ajili ya mashabiki, wakati mwanaye akila chakula cha hoteli aliyofikia pamoja na wachezaji wenzake.

Mama yake Drogba pia alipika chakula kwa ajili ya mashabki wakati wa Kombe la Dunia mwaka 2006 nchini Ujerumani.

Drogba ni mmoja wa watu maarufu sana nchini Ivory Coast, na mwaka jana alijumuishwa katika Tume ya Ukweli na Maridhiano iliyoundwa ili kupunguza mvutano uliotokana na utata wa matokeo ya uchaguzi na miaka mingi ya mgawanyiko.

Kundi la mashabiki wapatao 60 limesafiri kwenda Equatorial Guinea, ambapo Ivory Coast inacheza mechi zake za awali, na kila siku mashabiki hao wanapata chakula chao cha asili kilichopikwa na mama wa mshambuliaji wao mashuhuri.

"Kila mtu anafanya anachopenda kukifanya," Amesema mama yake Drogba, huku akiwa amevalia nguo za rangi ya chungwa ambayo huvaliwa na Ivory Coast.

"Hii sio kwa sababu ya mwanangu, ni kwa sababu ya kuunga mkono taifa langu."

Mama yake Drogba aliiambia AP kuwa alitazama mechi za ufunguzi kupitia televisheni huku akiwa anakata nyanya na vitunguu na kupika kuku.

Amesema ana imani ya kutazama mechi ya nusu fainali kwenye uwanja wa Bata - iwapo Drogba na timu yake watafuzu.

Amesema anaheshimu sheria, na hiyo ina maana kuwa mwanaye hawezi kula chakula chake wakati huu - anatakiwa kula chakula cha hotelini tu kwa mujibu wa utararibu.

Mama yake Drogba ameiambia AP kuwa ana uhakika atamuona mwanaye akilibeba Kombe la Mataifa ya Afrika.
Chanzo: BBC

Monday, January 30, 2012

Mahojiano kati ya Jennifer Lopez na Matt Lauer

Best Blogger Tips

Saturday, January 28, 2012

Romney would rank among richest presidents ever

Best Blogger Tips
 Just how rich is Mitt Romney? Add up the wealth of the last eight presidents, from Richard Nixon to Barack Obama. Then double that number. Now you're in Romney territory.

He would be among the richest presidents in American history if elected — probably in the top four.
He couldn't top George Washington who, with nearly 60,000 acres (24,000 hectares) and more than 300 slaves, is considered the big daddy of presidential wealth. After that, it gets complicated, depending on how you rate Thomas Jefferson's plantation, Herbert Hoover's millions from mining or John F. Kennedy's share of the vast family fortune, as well as the finer points of factors like inflation adjustment.

But it's safe to say the Roosevelts had nothing on Romney, and the Bushes are nowhere close.

The former Massachusetts governor has disclosed only the broad outlines of his wealth, putting it somewhere from $190 million to $250 million. That easily could make him 50 times richer than Obama, who falls in the still-impressive-to-most-of-us range of $2.2 million to $7.5 million.

"I think it's almost hard to conceptualize what $250 million means," said Shamus Khan, a Columbia University sociologist who studies the wealthy. "People say Romney made $50,000 a day while not working last year. What do you do with all that money? I can't even imagine spending it. Well, maybe ..."
Of course, an unbelievable boatload of bucks is just one way to think of Romney's net worth, and the 44 U.S. presidents make up a pretty small pond for him to swim in. Put alongside America's 400 or so billionaires, Romney wouldn't make a ripple.
Access the full story!

Friday, January 27, 2012

Madaktari - Pinda njoo tuzungumze

Best Blogger Tips
KAMATI ya Muda ya Jumuiya ya Madaktari wanaoendelea na mgomo nchi nzima imesema hawajafunga milango ya mazungumzo na ujumbe wowote kutoka kwa Waziri Mkuu.

Wameshangaa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, kutowafuata walipo madaktari wote kama alivyofanya Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, mwaka 2005 na badala yake juzi kuzungumza na waandishi wa habari.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dk. Stephen Ulimboka alisema hayo jana katika kikao cha madaktari hao walichokihamishia katika ukumbi wa Starlight baada ya ukumbi wa Don Bosco kushindwa kuchukua madaktari wote waliojitokeza jana.

Juzi Pinda, alisema haoni sababu ya kukwama kwa mazungumzo kati ya Serikali na madaktari hao na kwamba yupo tayari kukutana na wawakilishi wao na kutuma salamu popote walipo na wakisikia ujumbe wake, wafike wamwone kabla hajaenda bungeni Dodoma, Jumamosi.

Awali walielezwa kuwa Jumanne, Pinda angefika kuonana nao, lakini iliishia kuonana na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Peniel Lyimo na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Lucy Nkya, katika kikao walichokaa hadi saa tatu usiku bila mwafaka.

Kutokana na hatua hiyo, walimtaka Pinda afike na kuonana nao, kwani wao wapo tayari kumsikiliza pamoja na ujumbe wake, ili kufikia muafaka wa malalamiko yao na kuendelea kutoa huduma.

Wakati madaktari hao wakiendelea na kikao chao ambacho jana kilifurika zaidi, huduma katika hospitali za Serikali zimezidi kudorora na wagonjwa kurudishwa nyumbani huku wakitakiwa kurudi watakaposikia tangazo kwenye vyombo vya habari.

Katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Kitengo cha Watoto hali ilizidi kuwa mbaya baada ya watoto wenye ugonjwa wa upungufu wa damu - selimundu, kutakiwa kurejea nyumbani na kurudi Alhamisi ijayo.

Pia watoto wenye matatizo ya moyo walitakiwa kurudi wiki ijayo jambo ambalo ni hatari, kutokana na kuwa watoto hao walitakiwa kusafiri wiki ijayo, kwenda India kwa matibabu.

Muhonewa Mfaume, mama wa Hamida mwenye umri wa miaka miwili na nusu, mwenye matatizo ya moyo na mkazi wa Kigoma aliyefikia Mwananyamala kwa ajili ya matibabu ya mtoto wake, alisema aliishakamilisha tararibu zote za Wizara ya Afya na alichobakiza ni kuonana na daktari ili ajaziwe fomu itakayomwezesha kwenda kuchukua viza kwa ajili ya kwenda India.

Alisema cha kushangaza ni kuwa jana alifika kumwona daktari, lakini akaambiwa arudi wiki ijayo, kutokana na maelezo kwamba madaktari wa kumwandikia hawapo.

“Acha nirudi nyumbani nikaendelee kumwomba Mungu tufike hiyo Ijumaa na Mungu ajalie wawe wamemaliza mgomo wao, kwani huyu mtoto kufika umri huu ni neema ya Mungu, hawezi kukakaa wala kusimama, hata kuongea anaongea kwa shida akizungumza sana anashindwa kupumua,“ alilalamika mama huyo.

Katika kitengo hicho, mmoja wa madaktari wanafunzi wa mwaka wa nne, alisema hali ni mbaya, kwani huduma zote za wagonjwa wa nje zimesitishwa, labda kwa wenye hali mbaya sana na waliolazwa.

Alisema wanaofanya kazi sasa ni wao, walio katika mafunzo na wahadhiri wanaofundisha Chuo Kikuu cha Muhimbili, ambao ni wataalamu wa watoto, lakini hutoa huduma mara chache sana.

Katika Kitengo cha Wagonjwa wa Nje, ilionekana misururu mirefu ya wagonjwa wakisubiri madaktari, huku ikionekana kuwapo madaktari katika vyumba lakini wakidaiwa kuwa wanafunzi.

“Mimi ni daktari wa Kitengo hiki cha Wagonjwa wa Nje na wote tupo kwenye mgomo, ninachoshangaa hao wanaotoa huduma wametoka wapi, kwani siwatambui, hebu jaribuni kuwauliza,” alisema mmoja wa madaktari wa hospitali hiyo aliyekataa kutaja jina.
Baadaye ilionekana wagonjwa hao wakirejeshewa fedha walizotoa kwa ajili ya vipimo na kumwona daktari.

Ramadhani Makuka wa Kimara anayesumbuliwa na tumbo, aliandikiwa na daktari afike jana lakini alipofika aliandikiwa arudi Machi 22.

Hali mbaya zaidi, ilionekana katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa ya Muhimbili (MOI) ambapo wagonjwa waliondolewa na kutakiwa kurejea mara watakaposikia tangazo katika vyombo vya habari.

Mgonjwa wa mgongo, Rukia Hamis, mkazi wa Ununio alisema amesikitishwa kwa baadhi ya maofisa kuwasumbua na kutumia gharama kufika hospitali baada ya kuelezwa kuwa hakuna mgomo lakini kumbe upo.

Bryceson Sauli, aliyepata ajali ya mguu, alisema ifike mahali wagonjwa nao waandamane kuhakikisha Serikali inawasikiliza madaktari, ili waweze kupata haki zao za matibabu.

Huduma katika Hospitali za Amana na Temeke pia zilikuwa za kusuasua, huku wakionekana idadi kubwa ya wagonjwa wa nje wakirejeshwa nyumbani.

Dk. Ayub Kibao, akizungumza kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Amana alisema wameamua kusitisha huduma za wagonjwa wa nje, baada ya madaktari wanafunzi kuendesha mgomo.
Mgomo wa madaktari ulianza rasmi Jumanne na umeendelea kadri siku zinavyosonga mbele.
Chanzo: HabariLeo

Thursday, January 26, 2012

Mheshimiwa Galinoma Amefariki Dunia

Best Blogger Tips
 Aliyekua mbuge wa Jimbo la Kalenga,Iringa miaka ya nyuma.mheshimiwa Galinoma amefariki Dunia leo asubuhi mjini Iringa wakati akiwa garini akipelekwa hospitalini kutoka kijijini kwake Kalenga,ambako alikokuwa anaishi.

Mheshimiwa Galinoma ,alikuwa mtumishi wa serikali mstaafu aliyeshika nafasi mbali mbali katika uhai wake zikiwa Katibu mkuu idara ya ulinzi na jeshi la kujenga taifa,mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa mbuga za wanyama poli,mwenyekiti wa bodi ya mashirika ya Umma(SCOPO),Katibu wa tume ya uchunguzi wa viongozi,pia amewahi kuwa mbunge wa jimbo la Kalenga ,Iringa.

Marehemu Mhe. Galinoma alikuwa anaugua kwa muda mrefu pia aliwahi kuenda India kwa matibabu alikua huko wiki 6, na alipata nafuu kwa kiasi fulani lakini baadae alizidiwa tena.

Marehemu ameacha wajukuu na watoto ,miongoni mwa watoto wa wake ni wanamuziki Innocent na Buti Jiwe aka Henry Galinoma. Taaritibu za mazishi zitatolewa si muda mrefu.

Mungu amlaze mahala pema peponi.

Kwa habari zaidi za msiba wasiliana na Joseph Galinoma kwa namba hii 00255716492048 au Denis Galinoma namba hii 00255784769945
Chanzo: Globu ya Jamii

Wednesday, January 25, 2012

Marekani yaokoa Mateka Somalia

Best Blogger Tips

 Vikosi maalum vya Marekani viliingia nchini Somalia usiku wa manane na kufanikiwa kuwaokoa wafanyakazi wawili wa mashairika ya misaada kutoka mikononi mwa watekaji nyara wao nchini Somalia.

Mateka hao, Mmarekani mmoja na raia mmoja wa Denmark walitekwa nyara na kikundi cha Wasomalia mwaka uliopita na kwa mujibu wa tume ya Baraza la Denmark linalosika na wakimbizi limethibitisha kua Mmarekani Jessica Buchanan na Poul Hagen kutoka Denmark wameachiliwa na wako njiani kujiunga na familia zao.

Operesheni hii ilikua ya kipekee na ilibidi kua kivutio kikubwa kwa sababu kadhaa. Kwanza, ni namna ya ujasiri uliotumiwa kuifanikisha. Ni bayana kwamba ufanisi wake utamfaidi Rais Obama mwenyewe na utawala wake na pia vikosi vya Marekani.

Pia ni kumbusho kua vikosi vya Marekani havijathubutu kuweka guu nchini Somalia tangu kisa cha mjini Mogadishu cha mwaka 1993, ambapo askari 28 waliuawa.

Hata hivyo kumekuepo matukio ya kutumia makombora ya mbali kuweza kufikia malengo ya vikosi hivyo pamoja na ndege zinazopaa bila rubani kutimiza mashambulizi yanayohitajika.

Na Somalia imezidi kutazamwa kwa mashaka na Marekani pamoja na Mataifa mengine ya Dunia.
Jinsi Operesheni hii ilivyoendeshwa kuwaokoa mateka kutoka mikononi mwa kikundi cha wahalifu ni ishara ya wasiwasi unaozidi kuongezeka juu ya hali ya mambo nchini Somalia na kiwango cha uhalifu kinachozidi kupanda, ikizingatiwa kua kuna utekaji nyara wa Meli baharini na vilevile raia wa nchi za magharibi.

Pamoja na hayo, Marekani imezidisha ukaguzi wa anga ya nchi hio pamoaja na kua na ushirikiano wa karibu na Mataifa jirani kutokana na hofu kubwa juu ya uwezekano wa shughuli zinazokisiwa kua za kigaidi nchini humo.

Hisia mbalimbali zimejitokeza kuhusu shambulio la hivi sasa. Lakini huenda limefanyika kwa sababu Marekani ina uwezo wa kufanya hivyo au kwa sababu uchunguzi wa jasasusi wao umewapa taarifa za kutosha kutimiza operesheni hio.

Huenda likawa tukio la mara moja. Lakini kwa hali yoyote ile, linatimiza haja ya Rais Obama ya kutuma vikosi vyenye uwezo wa kuzima tukio kama hili mara moja badala ya vita vya mda mrefu na kuhitaji askari wengi na gharama kubwa.

Makamu wa Rais wa Marekani, Joe Biden akizungumza kuhusu Operesheni hii amesema,Nathibitisha kua Rais mwenyewe ndiye aliyeamuru lifanyike hili. Hakutaka kutoa maelezo zaidi ila tu kusema anazidi kushangazwa na jinsi vikosi vyao vinavyotekeleza operesheni ngumu kama hizo kwa mda mfupi.
Chanzo: BBC

The Message of Islam (Full Movie)

Best Blogger Tips

Tuesday, January 24, 2012

Ocampo asema hakati rufaa kuhusu Kenya

Best Blogger Tips
Louis Moreno Ocampo
 Kiongozi wa mashtaka katika mahakama ya kimataifa ua Jinai,ICC, iliyoko mjini The Hague Louis Moreno Ocampo anasema atawasilisha ushahidi zaidi kutaka mashtaka yathibitishwe dhidi ya wakenya wawili mashuhuri, ambao majaji katika mahakama hiyo walikataa kuthibitisha mashtaka dhidi yao kuhusiana na ghasia za baada ya uchagzui wa mwaka 2007 nchini Kenya.

Siku ya jumatatu mahakama ya ICC ilithibitisha mashtaka dhidi ya washukiwa wanne akiwemo naibu waziri mkuu Uhuru Kenyatta, lakini majaji wakasema hawakuridhishwa na ushahidi ulitoloewa na kiongozi wa mashtaka dhidi ya aliyekuwa mkuu wa Polisi Major Generali Hussein Ali na waziri wa zamani Bwana Henry Kosgey, na kwa hivyo wakakataa kuthibitisha mashtaka dhidi yao.

Wengine ambao mashtaka yao yalithibitishwa ni mkuu wa utumishi wa umma Francis Muthaura, aliyekuwa waziri wa elimu ya juu William Ruto na mtangazaji wa redio Joshua Arap Sang.

Akihutubia waandishi wa habari katika mahakama ya ICC, Bwana Ocampo amesema hatakata rufaa dhidi ya uamuzi wa majaji, lakini ataendelea kukusanya ushahidi zaidi kutoka waathirika na kuuwasilisha tena mbele ya jopo la majaji watatu walioshughulikia kesi hiyo ya washukiwa wa ghasia za Kenya.

Amesema atafanya uchunguzi zaidi juu ya Bwana Ali na Bwana Kosgey wakati kesi dhidi ya watuhumiwa wanne ambao mashtaka dhidi yao yalithibitishwa itakapoanza.

Wakati wa kutoa uamuzi siku ya Jumatatu, jaji kiongozi Ekaterina Trendafilova alisema hawakushawishika na ushahidi uliotolewa wa kumhusisha Bwana Kosgey na ghasia dhidi ya wafuasi wa chama cha PNU katika maeneo kadhaa mkoani Rift Valley.

Alielezea kwamba kiongozi wa mashtaka alitegemea shahidi mmoja tu dhidi ya Bwana Kosgey, na ambaye hakuthibitishwa.

Pia aliongeza kwamba upande wa mashtaka ulibana tarehe ambazo inadaiwa Bwana Kosgey alihudhuria mikutano ya kupanga ghasia, na hivyo kumkosesha fursa ya kuandaa utetezi.

Jaji huyo pia alisema ushahidi uliowasilishwa haukuwa na misingi ya kutosha kuonyesha kwamba Polisi walishiriki kwenye ghasia katika maeneo ya Nakuru na Naivasha.

Kuhusu uamuzi huo, Bwana Ocampo amesema atafanya uchunguzi zaidi katika sehemu za Kisumu na Kibera mjini Nairobi, ambako anadai Polisi walishiriki kwenye ghasia.

Amesema atatafuta ushahidi zaidi kuthibitisha kwamba Bwana Kosgey alihusika kwenye ghasia pamoja na Bwana Ruto na Bwana Sang.
Chanzo: BBC

Monday, January 23, 2012

Best Blogger Tips
 
Uamuzi huu metolewa  leo katika mfulilizo wa Mikutano waliyoianza toka jumatano ya wiki iliyopita (18/01/2012) katika  kujaribu kutafuta suluhu ya matatizo yao na ya Sekta ya Afya kwa Ujumla,Juhudi hizo hazikuzaa matunda kutoka kwa Serikali kuanzia ngazi ya Wizara ya Afya mpaka ofisi ya Waziri Mkuu ambapo kutozaa matunda.

Madaktari/watumishi wa afya hao wana madai kadhaa ikiwemo

*Kuboresha Huduma za Afya nchini (hospitali na vitanda kwa kila mgonjwa inawezekana)

*Maslahi Duni kwa watumishi wa sekta ya afya

*Malipo kwa kazi za ziada kwani   Madktari wanalipwa shilingi 10,000/=  kwa kukesha na kufanya kazi masaa 36 tofauti na taratibu za serikali ambapo ilitakiwa walipwe  shilingi 40,000(half pediem) kama taratibu za serikali zinavyoonesha lakini viongozi wa Wizara hasa Mama Blandina Nyoni wamekuwa wakikwamisha hili.

*Haki ya kupewa nyumba  au posho ya Nyumbai kama muongozo wa utumishi wa umma  wa serikali ya Tanzania unavyoelekeza ule wa mwka 1994 na wa mwaka 2009..

*Kulipwa posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi(Risk allowance)

*Lingine ni Kuondolewa kwa Katibu mkuu wa wizara ya afya Bi.Blandina Nyoni ambaye anaonekana kuwa ni kikwazo katika juhudi za msingi katika kuboresha sekta ya afya Tanzania.


*Bi Blandina Nyoni anatuhumiwa kutoa kauli ya kejeli  kwa watumishi wa afya kuwa anamshukuru baba yake kwa kumkataza kusomea mambo ya afya kwani sekta ya ya afya haifai na ndio maana licha ya kufaulu masomo ya sayansi baba yake alimshauri asomee uhasibu.

Maamuzi hayo magumu yamefikiwa katika Mkutano wa leo uliofanyika Don Bosco Upanga DSM ikiwa ni mwendelezo wa Mikutano isiyokoma iliyoanza Toka jumatano ya Wiki iliyopita.



Mwandishi wa habari wa Mwananchi afariki dunia

Best Blogger Tips
Beatus Kagashe
 MWANDISHI wa habari wa Kampuni Mwananchi Communications Limited (MCL), Beatus Kagashe (31), amefariki dunia juzi usiku.Kifo cha mwandishi huyo aliyekuwa akiandikia gazeti la The Citizen, kilitokea katika Hospitali ya Ocean Road, Dar es Salaam ambako alikuwa amelazwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa saratani ya damu baada ya kutibiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Aga Khan kwa miezi miwili.

Msemaji wa familia ya marehemu Gasper Mikimba alisema, Kagashe alifariki mnamo saa 2:45 usiku na kwamba familia iko katika mipango ya mazishi ambayo yatafanyika Bukoba mkoani Kagera. Alisema mwili wa marehemu unatarajiwa kusafirishwa kwenda huko Jumanne na mazishi kufanyika Jumatano.

“Bado tunaendelea na mipango ya mazishi... lakini nadhani tutasafirisha mwili wa marehemu kwenda nyumbani Bukoba siku ya Jumanne kwa ajili ya mazishi,” alisema Mikimba.

Alisema kifo cha Kagashe kimeacha mshtuko mkubwa katika familia,jamii pamoja na taifa kwa ujumla hasa ikizingatiwa kwamba alikuwa bado kijana aliyetarajiwa kulijenga taifa lake.

Marehemu Kagashe alizaliwa Februari 23, 1981 mkoani Kagera na alipata elimu ya msingi katika Shule ya Bilele iliyoko Bukoba Mjini kati ya mwaka 1990 na 1996, alijiunga na Shule ya Sekondari Ihungo kuanzia mwaka 1997 mpaka 2000 kabla ya kujiunga na Shule Sekondari Mpwapwa kwa masomo ya kidato cha tano na sita.

Mwaka 2004, alichaguliwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kusoma kozi ya uandishi wa habari (Bachelor ofn Arts Journalism) katika Taasisi ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano kwa Umma (IJMC) alipohitimu mwaka 2007. Alijiunga na masomo ya shahada ya uzamili katika masuala ya utawala (Masters in Public Administration) katika Chuo Kikuu cha Mzumbe mwaka 2010 na kuhitimu Novemba mwaka jana.

Mhariri Mtendaji wa Gazeti la The Citizen, Bakari Machumu alisema amepokea kifo cha marehemu Kagashe kwa masikitiko makubwa. Alimwelezea kama kijana aliyekuwa mpenda watu na mwenye kusimamia alichokiamini.

“Tulidhani alikuwa anaendelea vizuri na matibabu... nimepata mshtuko kusikia kwamba Kagashe ameaga dunia. Nilikutana naye hospitali wiki moja iliyopita alionekana kuwa na nguvu ya kupambana na ugonjwa wake,” alisema Machumu.

Alisema idara yake imepoteza hazina ambayo Mwananchi Communications Limited ilikuwa imewekeza kwa manufaa ya kampuni pamoja na gazeti.

Alisema marehemu Kagashe alikuwa ni zao la utaratibu wa kusaka vipaji kutoka vyuo vya elimu ya juu, programu iliyoanzishwa na Kampuni ya Mwananchi mwaka 2007 akiwa miongoni mwa vijana watano wa kwanza wa kundi la kwanza la programu hiyo.

“Kagashe alitokana na mpango wa kusaka vipaji katika vyuo vya elimu ya juu...mamia ya wahitimu wa vyuo vikuu nakumbuka walijitokeza lakini Beatus Kagashe alikuwa miongoni mwa wanafunzi watano bora, hivyo kujiunga na kozi maalumu huko Nairobi,Kenya,” alisema Machumu.

Kagashe aliajiriwa aliajiriwa na Mwananchi Communications Limited, kampuni inayochapisha magazeti ya The Citizen, Mwananchi na Mwanaspoti mnamo mwaka 2008. Ameacha mjane, Doroster Kagashe na mtoto Emmanuel Mujuni ambaye ana umri wa mwaka mmoja.

Chadema wamlilia
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kimepokea kwa majonzi na masikitiko makubwa, taarifa za kifo cha Kagashe.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mwenezi wa chama hicho, Tumaini Makene imesema: “Kwa wale waliokuwa wakimfahamu marehemu Kagashe, watakubali kuwa alikuwa mmoja wa waandishi makini, waliokuwa wakiamini jamii ya Watanzania inaweza kufanya mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi na kijamii.”

Alisema kwa kutumia vema taaluma yake, akiongozwa na maadili ya tasnia ya habari, alishirikiana na Watanzania wenzake katika kuelimisha, kuhabarisha, kuhamasisha na kuburudisha umma, katika masuala mbalimbali kupitia kalamu yake.

“Tunatoa pole kwa ndugu, jamaa, marafiki na wafanyakazi wenzake na kuwaombea kwa Mungu awape moyo wa subira katika wakati huu mgumu wa majonzi kwa kuondokewa na mpendwa wao,” alisema Makene.
Chanzo: Mwananchi

Sunday, January 22, 2012

Dk. Slaa atinga Ikulu

Best Blogger Tips
 CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), jana kilikutana tena na Rais Jakaya Kikwete katika Ikulu ya Magogoni, Dar es Salaam, kujadili masuala mbalimbali, ukiwamo mchakato wa uanzishaji wa Katiba mpya.

Miongoni mwa wajumbe wa CHADEMA waliokwenda Ikulu ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, ambaye alichuana na Rais Kikwete katika kinyang’anyiro cha urais mwaka 2010, na tangu hapo wawili hao hawajakutana ana kwa ana.

Habari za ndani kutoka Ikulu na CHADEMA zilieleza kuwa Kikwete na Dk. Slaa walikutana katika kikao kilichowashirikisha viongozi wengine wa CHADEMA wakiongozwa na Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe.

Tanzania Daima Jumapili, liliwasiliana na Mbowe kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno (sms) kujua kuhusu safari hiyo, akajibu: “Tunakutana leo in the next 30 minutes (ndani ya dakika 30 zijazo).”

Hata hivyo, Mbowe hakutaja watu walioongozana naye kukutana na Rais Kikwete, ambaye mwishoni awali walikutana naye mwaka jana kuzungumzia upungufu mkubwa kwenye sheria ya uundwaji wa Katiba mpya.

Habari zilizolifikia gazeti hili ni kwamba Rais Kikwete ndiye aliyefanya jitihada za kutaka kukutana na CHADEMA jana, ili kuwaeleza hatua aliyochukua baada ya makubalino yao ya awali.

Tanzania Daima linajua fika kwamba ujumbe wa CHADEMA ulipokutana na rais mwaka jana, ulimwomba asikubali kusaini muswada wa kurekebisha Katiba mpya kuwa sheria, kwa kuwa ulikuwa na upungufu mkubwa.

Hata hivyo, Rais Kikwete alisaini muswada huo kuwa sheria. Watu walio karibu naye wameliambia gazeti hili kuwa alisaini ili kuepusha upinzani mkubwa kutoka kwa wabunge wa CCM ambao walikuwa wamepitisha muswada huo kwa kutekeleza agizo la chama ambacho yeye ni mwenyekiti wake.

Kama asingesaini muswada huo kuwa sheria, ingebidi urejeshwa bungeni kufanyiwa marekebisho kadiri ya mapendekezo ya CHADEMA, lakini wabunge wake wangetafsiri kwamba amewadharau, na wangeweza hata kuleta hoja ya kutokuwa na imani naye, jambo ambalo lingemtikisa zaidi rais ambaye tayari amekuwa anakabiliwa na makundi hasimu ndani ya chama chake.

Habari kutoka kwa watu walio karibu na Ikulu zinasema Rais Kikwete alisema kwamba kutokana na mazingira ya kisiasa yanayomkabili ndani ya chama chake, asingeacha kusaini muswada huo, lakini angehakikisha kwamba sheria hiyo haitumiki hadi baada ya kufanyiwa marekebisho muhimu kwa mujibu wa mapendekezo ya CHADEMA, ambayo Rais Kikwete aliridhika kwamba ni muhimu.

Mbunge mmoja amelidokeza gazeti hili kuwa tayari wamepewa makabrasha yenye marekebisho ya sheria hiyo, na wanatarajia kuyajadili kwenye vikao vya Bunge vinavyotarajiwa kuanza Januari 30, mwaka huu.

Hata hivyo, jitihada za kuwapata viongozi wa Bunge kuzungumzia jambo hilo ziligonga mwamba.
Tanzania Daima Jumapili limedokezwa na baadhi ya wasaidizi wa rais kuwa tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, Rais Kikwete amekuwa akifanya jitihada za kukutana na Dk. Slaa, lakini jitihada zake ziligonga mwamba mara kadhaa kutokana na sababu mbalimbali.

Inadaiwa kwamba hata mwaka jana CHADEMA walipoomba kukutana na rais kujadili suala hilo, alikubali mara moja baada ya kuona jina la Dk. Slaa likiwa miongoni mwa wajumbe waliotarajia kwenda Ikulu. Hata hivyo, Dk. Slaa hakwenda Ikulu, kwani alipata udhuru.

Viongozi hao pia walishindwa ‘kuteta’ katika msiba wa Mbunge wa Viti Maalumu, Regia Mtema (CHADEMA) walipoonana kwenye mazishi Ifakara.

Licha ya mahasimu hao kushiriki mazishi pamoja, bado hawakuonana ana kwa ana, jambo ambalo liliibua hoja kwamba Dk. Slaa alimkwepa Rais Kikwete.

Hoja ya Dk. Slaa kumkwepa Rais Kikwete ilizua mjadala wiki iliyopita, huku mwenyewe akisisitiza kuwa asingependa kutumia msiba wa marehemu Regia kutafuta umaarufu wa kisiasa. Alisisitiza kuwa kutokutana kwake na rais lilikuwa tatizo la kiitifaki.

Awali kabla ya CHADEMA kwenda kuonana na Rais Kikwete mwishoni mwa mwaka jana, wabunge wake walisusia kujadili muswada huo kwa madai kuwa utaratibu wa utungaji wa sheria hiyo haukufuatwa, na kwamba Spika wa Bunge, Anne Makinda, alikuwa amekula njama na CCM kuharibu mchakato wa utungaji wa sheria hiyo, ili kuharibu mchakato na matokeo yake.
Chanzo: Tanzania Daima

Thursday, January 19, 2012

Simanzi nyingine Bunge

Best Blogger Tips
 SIMANZI nyingine imelikumba Bunge la Tanzania, kufuatia kifo cha Mbunge wa Arumeru Mashariki (CCM), Jeremiah Solomon Sumari (60),aliyefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa muda mrefu akipatiwa matibabu.

Kifo cha Sumari kimetokea siku moja tu, tangu kufanyika kwa mazishi ya Mbunge wa Viti Maalum (Chadema),  Regia Mtema aliyefariki dunia kwa ajali ya gari, Jumamosi iliyopita katika eneo la Ruvu mkoani Pwani.

Sumari alianza kuugua kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, hali ambayo ilimfanya aende kampeni katika mazingira magumu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mtoto wa kwanza wa marehemu, Sioi Sumari alisema baba yake alipatwa na mauti katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), alipokuwa amelazwa.

“Baba amefariki saa 8.30 usiku katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu,” alisema Sioi.
Alifafanua kuwa, marehemu anatarajiwa kuzikwa Jumatatu ijayo kijijini kwake katika jimbo la Arumeru Mashariki.
Mtoto  huyo wa marehemu alisema baba yake utaagwa kesho (Jumamosi ) jijini Dar es Salaam, kabla ya kusafirishwa kwenda Arusha.

Ofisi ya Bunge Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alisema ofisi ya Bunge imepokea kwa masikitiko msiba huo kwani umetokea muda mfupi tangu waliporejea kutoka kwenye maziko ya Mtema.Hata hivyo, alisema  kutokana na hali hiyo shughuli za Bunge zitaendelea kama zilivyopangwa na kwamba, zitasimamishwa siku ya kuaga mwili wa marehemu.

“Leo (jana) na kesho tutaendelea na shughuli za bunge kama kawaida, lakini siku ya kuaga tutasitisha shughuli ili kutoa fursa kwa wabunge kushiriki kwenye mazishi ya marehemu Sumari,” alisema Dk Kashililah.   Alisema  kwa sasa wanafanya taratibu za mazishi ya marehemu kwa kushirikiana na familia yake.

Alifafanua kwamba kutokana na hali hiyo, bunge limepata pigo kubwa baada ya kuondokewa na wabunge wawili katika kipindi kimoja, jambo ambalo limesababisha wabunge kushikwa na butwaa.Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema Kamati ya Uongozi ya Bunge itakutana leo kujadili namna ya kuratibu mazishi ya mbunge huyo.

Alisema  kuna uwezekano mbunge huyo akaagwa katika ukumbi wa Karimjee, kama ilivyofanyika kwa mbunge wa Chadema Regia Mtema.

“Tunasikitika sana kwa kuwapoteza wabunge wawili ndani ya muda mfupi,” alisema Ndugai.

Kikwete amlilia
Kwa upande wake, Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Spika wa Bunge, Anne  Makinda  kutokana na kifo cha Sumari.

Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, ilimnukuu Rais Kikwete ikisema; “Nimeshtushwa, nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa za kifo cha Mheshimiwa Jeremia Solomon Sumari….”
“Alikuwa kiongozi aliyewatumikia vema wananchi wa Jimbo lake la Uchaguzi la Arumeru Mashariki na Taifa kwa ujumla katika wadhifa wake wa Waziri kwa umahiri na uhodari mkubwa.”

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Kikwete alisema kutokana na kifo cha Sumari, wananchi wa Arumeru Mashariki wamepoteza kiongozi wa kutegemewa. “Kwa moyo dhati, natuma salamu za rambirambi na pole kwa familia ya marehemu Jeremia Sumari kwa kumpoteza kiongozi na mhimili madhubuti wa familia,” taarifa hiyo ilimnukuu Rais Kikwete.   Alifafanua akisema; “Ninawahakikishia kwamba nipo pamoja nanyi katika kuomboleza msiba huu mkubwa na namuomba Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema aipumzishe roho ya marehemu Jeremia Solomon Sumari mahali pema peponi, Amina.”

 Lowassa amlilia
Mbunge wa Monduli,  Edward Lowassa alisema taifa limepata pigo kubwa kwa kuondokewa na Sumari.
 “Alikuwa mchapakazi sana.., hii imesababisha kuteuliwa kuwa Naibu Waziri katika serikali ya awamu ya nne, kutokana na umahiri wake,” alisema Lowassa.
Lowassa aliongeza kwamba, kutokana na hali hiyo, wananchi wa Arumeru Mashariki wamekosa mwakilishi wa kutetea maslahi yao bungeni.

 Historia yake
Sumari  alizaliwa Machi 2 mwaka 1943, katika kijiji cha Akeri wilayani Arumeru mkoani arusha.
Alipata elimu yake ya msingi katika shule ya Meru Magharibi kati ya mwaka  1950 na 1957. Kati ya mwaka  1958- 1964 alisoma katika shule ya sekondari ya Old Moshi, mkoani Kilimanjaro na baadaye aliendelea na elimu ya juu nchini Uingereza.

Taarifa zinaonyesha kuwa, Sumari alipata elimu ya masoko kwa ngazi ya cheti ACCA, CIS, (Certificatein Marketing and Lincesed Broker lr), nchini Uingereza na baadaye kupata CPA nchini.
Kwa upande wa utumishi wake, mwaka 1996 mpaka 2004 alikuwa Mkurugenzi wa Bodi ya Boko la Disa Dar es Salaam (DSE).
Kisiasa , kuanzia mwaka 2005 mpaka mauti yalipomkuta alikuwa Mbunge wa jimbo hilo la Arumeru Mashariki kwa tiketi ya CCM.

Januari 4 mwaka 2006, aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana na mwaka 2008 mpaka 2010 alipoteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi.
Chanzo: Mwananchi

Wednesday, January 18, 2012

Mvua ‘yamsindikiza’ Mbunge Mtema

Best Blogger Tips
MVUA kubwa iliyoanza kunyesha mchana wakati ibada ya kumwombea marehemu Regia Mtema chini ya Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mahenge mkoani Morogoro Mhashamu Agapiti Ndorobo, ilivuruga kwa kiasi shughuli na utaratibu wa maziko yaliyofanyika mjini hapa jana.

Licha ya mvua hiyo kubwa kunyesha kuanzia saa nane mchana hadi saa 10 jioni mamia ya wananchi wa mjini Ifakara na wageni kutoka mikoa mbalimbali nchini wakiwamo wabunge wakiongozwa na Spika Anne Makinda, walishiriki kikamilifu ibada hiyo hadi mazikoni.

Rais Jakaya Kikwete alihudhuria maziko hayo ambayo yalifanyika kwenye makaburi ya
Mkuya katika barabara ya Kivukoni kuelekea Ulanga, na kabla ya shughuli hiyo, wananchi waliaga mwili wa marehemu kwenye uwanja wa Kiungani mjini Ifakara.

Akizungumza kwa niaba ya Serikali kabla ya ibada hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia, alisema Taifa limepoteza kiongozi shupavu
aliyekuwa akijenga hoja bungeni za kutetea wananchi bila kujali itikadi za vyama, dini au jinsia.

“Amefariki akiwa kiongozi kijana, msomi na nchi ilikuwa ikimhitaji kwa mchango wa mawazo yake na Serikali inatoa pole kwa wabunge, Spika na wananchi wa Kilombero na Morogoro pamoja na familia yake kwa kumpoteza kipenzi chao,” alisema Waziri Ghasia.

Spika Makinda alisema Regia alikuwa mtetezi mkubwa wa wafanyakazi wakiwamo wa kiwanda
cha Sukari cha Kilombero na kuwa kifo chake kimewashitua watu wengi na kukutanisha watu
wengi kutoka pande mbalimbali, wananchi na viongozi wa Serikali, vyama vya siasa, wabunge wa vyama.

Alirudia kauli yake ya juzi Dar es Salaam, akisema Regia alionesha upendo na alikuwa nyota ya
upendo ya uwakilishi wa wananchi na ndiyo maana baada ya kifo chake amekutanisha watu
wengi kwa wakati mmoja Dar es Salaam na Ifakara.

Hivyo aliomba Watanzania, wamuenzi Regia kwa kufuata nyayo zake za upendo wa kila mtu
bila ubaguzi wa dini, jinsia au itikadi na wabunge walimpenda kutokana na ucheshi wake
ulioambatana na kutaniana kwa staha bila kujali rika la mtu.

Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe, alimtaja Regia kuwa kiunganishi cha chama kwa vijana ndani na nje ya chama na alikuwa akitetea hoja alizokuwa akiziamini kuwa za kuleta maendeleo kwa Taifa, wananchi wake na chama chake, hivyo kimempoteza kiongozi muhimu na pengo lake halitazibika hata wakimpata mtu mwingine.

Hata hivyo, aliwahakikishia wananchi wa Kilombero, familia ya marehemu kuwa chama kitakuwa bega kwa bega katika masuala mbalimbali ya kijamii.

"Hatutaangusha wananchi wa Kilombero, wameonesha jinsi walivyokuwa karibu na Mbunge
wao, walivyokuwa wamempenda na hili limetudhihirisha kutokana na umati huu ... kutokana na upendo wake kwa kila mtu ... baada ya kifo chake, leo tumeona jinsi alivyotuunganisha, sisi kama chama, viongozi wa Serikali, wabunge na hili tutalizingatia katika kufanya uamuzi wetu
kwenye vikao," alisema Mbowe.

Hata hivyo, Mwenyekiti huyo wa Taifa pamoja na kuomboleza kifo cha Regia, alitumia fursa hiyo kuwaahidi wananchi wa Kilombero, kuwa chama kitaangalia jinsi ya kuwaondolea machungu ya kumpoteza kipenzi chao katika kumpata mwingine hata kama hataweza kufanana na marehemu kwa vitendo vyake.

Akitoa mahubiri wakati wa ibada ya misa ya kumwombea Regia, Askofu Ndorobo, alimtaja
kuwa mtu wa watu aliyeishi maisha ya kumcha Mungu na pia aliipenda nchi yake, ndiyo maana
alijitoa kutumikia wananchi wake na Taifa.

“Regia aliipenda nchi yake, aliipenda Kilombero na Watanzania wote, hivyo inatupasa tumwombee,” alisema Askofu huyo.

Hata hivyo, alisema pamoja na kuendelea kumhitaji, lakini mapenzi ya Mungu hayawezi
kupingwa na mtu yeyote hivyo ni wajibu wetu siku zote kuishi kwa kumcha Mungu.

Salaamu za Zitto
Akitoa salaamu za Chadema, Naibu Katibu Mkuu, Kabwe Zitto, alisema kuwa Regia nyota iliyozimika lakini kutokana na matendo yake, mwanga wake utaendelea kuangaza katika kuendeleza mapambano ya kuwakomboa Watanzania.

Akinukuu utenzi ulioandikwa mtandaoni na Mwanakijiji aliyesema kuwa alikuwa rafiki mkubwa
wa Regia na kusema kifo cha Regia ni pigo lililowaacha wote waliomfahamu, wakitetemeka,
kumlilia na machozi kuwadondoka.

“Lakini rafiki yako huyo kakuandikia shairi, uende ukisikiliza. Hapa tunalisoma kwa
kubadili sehemu fulani fulani, bila kubadili maudhui wala mtiririko wa mantiki, lakini swali letu kubwa ni je, unaweza kusikiliza?

“Basi sikiliza Regia, ukiweza tughani sote huu utenzi wa rafiki yako, usemao nyota imezimika,”
alisema Zitto.

Spika Anne Makinda alimsifia Regia kwa namna alivyoonesha uhodari katika shughuli zake kuwawakilisha wananchi, huku pia akiwa mcheshi kwa wabunge wenzake.
Chanzo: HabariLeo

Tuesday, January 17, 2012

Michael Jordan thinks only Kobe Bryant deserves comparisons

Best Blogger Tips
Ever since Michael Jordan retired — all three times, really — the NBA has searched for the heir to his throne. Many players have popped up as pretenders to the throne, from Harold Miner to Jerry Stackhouse to Vince Carter. In recent years, people have stopped trying to find a clone and just searched for a similarly dominant great player. If you ever wondered why LeBron James is seen as such a failure, a lot of it has to do with his inability to meet the example set by Jordan.

There are many great players in the NBA these days, most of whom have never been directly compared to Jordan. Nevertheless, His Airness says only one player comes close enough to his greatness to merit the comparison. Not surprisingly, that player is Kobe Bryant. Here's what Roland Lazenby, a great writer currently working on a Jordan book, tweeted on Sunday (via PBT):
Kobe's ultimate competition is MJ. That's why MJ watches him. MJ made people think what he was doing wasn't human. Ditto the Kobester.
I never said Kobe was better than MJ. MJ just told me Kobe's the only one to have done the work, to deserve comparison.
Congratulations, Kobe: Your life's work has meant something. All that time spent aping Jordan's movements and skills has paid off. He acknowledged you. You made it.
Of course, if the notoriously petty Jordan was going to mention anyone, it makes that he'd single out Kobe, and not just because he'd consider the mimicry flattering. Bryant really does work harder than everyone else, and he's been good for long enough (with no signs of slowing down) that he may eventually top Jordan's longevity. They're similarly insane competitors.
The "Next Jordan" idea was always a silly one, but Bryant is certainly the player most like Jordan in all aspects of his game — even if he eventually becomes something less than the greatest player of the post-MJ era, which I'm sure many of you will argue in the comments. That's an accomplishment in itself. Even coming close to the top means something.

Wabunge 100 kumzika Mtema

Best Blogger Tips
 WABUNGE zaidi ya 100 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wanatarajia kushiriki maziko ya marehemu Regia Doto Mtema (32), Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema) yanayotarajia kufanyika leo nyumbani kwao Ifakara, Morogoro.

Pia Rais Jakaya Kikwete ambaye yuko katika ziara ya kikazi mkoani humo, anatarajia kushiriki maziko hayo.

Hayo yalibainika jana wakati wa utoaji heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu katika ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam ulioongozwa na Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliiwakilisha Serikali huku upinzani ukiwakilishwa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe. Viongozi mbalimbali wa Serikali akiwamo Mwanasheria Mkuu Frederick Werema, mawaziri na wabunge walishiriki.

Kati ya wabunge hao 50 waliteuliwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda na watahudumiwa na Serikali wakiwemo wajumbe wote wa Kamati ya Uongozi, wenyeviti wa kamati zote na wajumbe 10 wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu.

Wengine ni wabunge wote wa Mkoa wa Morogoro, wabunge sita waliowakilisha CCM, wanne Chadema, watatu CUF na mmoja mmoja kutoka NCCR-Mageuzi, UDP na TLP.

Wabunge wengine 50 walitokana na vyama vyao, makundi na taasisi mbalimbali wakiongozwa na Makinda, Naibu Spika Job Ndugai na Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Kabwe Zitto .

Akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Serikali, Pinda aliwapa pole Chadema kwa kuondokewa na Mbunge wao mwanamke mwenye uwezo mkubwa.

Alisema atamkumbuka sana kwani kila Alhamisi wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu aliuliza maswali, huku akisisitiza kuwa si rahisi kwa Chadema kuziba pengo hilo la Mbunge aliyekuwa na karama za pekee.

Alisema Rais Kikwete kabla ya kuanza ziara Morogoro alionesha nia ya kushiriki maziko hayo na kama ratiba haitambana atashiriki.

Makinda aliwataka wanawake kumuenzi Regia kwa kuthubutu kugombea nafasi za uongozi bila uoga.

“Regia ametuunganisha Watanzania kwa kutimiza upendo wa asili wa Watanzania, kwani ni nyota iliyomulika Tanzania … kuishi wamoja licha ya tofauti za kisiasa ambazo ni mapambio tu,” alisisitiza.

Makinda alisema Regia aliishi kwa upendo mpaka kwenye nyumba yake ya Mbezi ambako alihifadhi watu wenye shida jambo lililoonesha kuwa alikuwa Mbunge aliyejali matatizo ya watu na ndivyo wabunge wanavyotakiwa kuishi.

“Katika mkutano uliopita wa Bunge ilikuwa kama ananiaga kwani alinitumia karatasi ikisema ‘mama nakupenda … I love you so much’,” alisema Makinda.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, alisema Regia alijiunga na chama hicho mwaka 2001, akiwa chuoni, huku akiamini na kusimamia ukweli kwamba hakuna kazi mwanamume anaweza na mwanamke asiiweze.

Alisema ulemavu wake haukuwa kikwazo katika mapambano ndani ya chama, ujasiri aliouonesha tangu awali alipofanya kazi makao makuu ya chama kwa miezi miwili bila wazazi wake kujua.

Regia alikufa kwa ajali ya gari alilokuwa akiendesha eneo la Ruvu, mkoani Pwani akitokea nyumbani kwake Mbezi-Makabe, Dar es Salaam, kwenda Vigwaza akiwa na watu wengine saba akiwamo mama yake mdogo, Bernadeta Mtema.

Taarifa za polisi wa Pwani zilidai kuwa alilipita lori na ghafla kukutana uso kwa uso na lori lingine na alipojaribu kurudi upande wake, alikosa mwelekeo na kupinduka na kupoteza maisha papo hapo huku wenzake wakijeruhiwa.
Chanzo: HabariLeo

Marehemu Regia Mtegwa aagwa Karimjee , kuzikwa kesho Ifakara

Best Blogger Tips

Monday, January 16, 2012

Akina Professor Jay, Sugu na uongozi wa taifa

Best Blogger Tips
Ahmed Rajab
JUZI nilikuwa nikiangalia mahojiano katika stesheni moja ya televisheni ya lugha ya Kifaransa. Aliyekuwa akihojiwa alikuwa Youssou N’Dour, mwimbaji maarufu wa Senegal aliyetangaza kwenye mahojiano hayo kuwa ataugombea urais wa nchi yake katika uchaguzi utaofanywa Februari 26, mwaka huu.

Katika mahojiano hayo mwimbaji huyo, mwenye umri wa miaka 52, alitamka haya: “Mimi sikusoma lakini nimezingatia yaliyofanywa na waliosoma tangu uhuru nikaingiwa na mori wa kutumia haki yangu na kutoa mchango wangu kwa wananchi wa kawaida. Nimetafakari nikaona nina wajibu wa kuingia katika kinyanganyiro hiki.”

Ingawa mwaka jana Chuo Kikuu cha Yale kilichoko Marekani kilimtunukia shahada ya heshima ya udaktari wa muziki  N’Dour,  kama alivyosema mwenyewe, si mtu aliyesoma. Sana sana amesoma katika shule ya msingi na hakuingia shule ya sekondari.

Alipotimiza umri wa miaka 12 tayari alikuwa akipanda kwenye majukwaa kuwatumbuiza mashabiki wa muziki.  Kabla ya kuwakusanya wanamuziki kadhaa walio na ustadi katika fani hiyo na kuanzisha kundi lake la Étoile de Dakar (Nyota ya Dakar), N’Dour alikuwa mmoja wa wanamuziki wa kundi la Orchestra Baobab na kabla ya hapo Star Band.

Ingawa hakusoma hivyo Youssou N’Dour alitumia kipaji chake kisicho kifani kwa kusoma katika shule ya maisha na kuyafanya maisha yake yawe kivutio. Tangu aanze kujitafutia riziki kwa kuimba ameutumia muziki kuwa ngazi ya kujijenga, sio yeye tu bali pia Waafrika wenzake na taifa lake. Leo hii amefanikiwa kuitangaza Senegal katika ulimwengu wa burudani na kuipatia sifa duniani. 

Ameshirikiana na waimbaji walio wanaharakati maarufu kama Bob Geldof na Bono kusaidia katika kampeni za kupambana na maafa, tangu ya ukame, njaa, magonjwa, umasikini na madeni ya nchi za Magharibi yanayobebwa na nchi zetu.

Pamoja na yote hayo, N’Dour ameanzisha miradi binafsi huko kwao Senegal ya studio ya kisasa ya muziki, steshini ya redio, nyingine ya televisheni na gazeti, akiwaajiri jumla ya vijana wasiopungua 4,000.

Wengi wanajiuliza ni wanamuziki wangapi maarufu barani Afrika  walioweza kufanya alau nusu ya aliyofanya N’Dour. Jibu hakuna.

Kwa muda wa takriban robo karne tangu akiasisi kikundi chake hakuna mwanamuziki wake hata mmoja aliyemuacha mkono. Hili pia ni la kupigiwa mfano. Ni jambo linalodhihirisha  uadilifu wake N’Dour kwa wale anaowaongoza, iwe kimuziki au kibiashara.

Kujitokeza kwake kuwania urais kumeshaanza kuwatia kiwewe wanasiasa wakongwe tangu Rais Abdoulaye Wade, mwenye umri wa miaka 86, hadi baadhi ya wapinzani wake.

Hofu ya Wade, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Kidemokrasia cha Senegal, sio kwamba N’Dour ataweza kushinda moja kwa moja katika duru ya mwanzo, la  hasha. Kinachomtia wahka ni umaarufu wa N’Dour unaoweza kusababisha uchaguzi kuingia duru ya pili. Hiyo ni duru ambayo Wade anaihofia. Anahofia kwamba endapo uchaguzi utaingia duru hiyo na wapinzani wake wakashikana kumuunga mkono mgombea mmoja basi hatoweza kufua dafu.

Nilikutana na Wade kwa mara ya kwanza mwishoni mwishoni mwa mwaka 1999, nilipokuwa nikihariri Jarida la Africa Analysis na miezi kadhaa kabla hajachaguliwa kuwa Rais. Aliletwa ofisini mwangu na Balozi Gaby Sar, aliyekuwa Balozi wa Senegal mjini  London, jambo lililonifanya nimpe heko balozi huyo kwa ustaarabu wake wa kisiasa na Serikali yake kwa uvumilivu wake. Ni nadra kumuona balozi wa kiafrika akimhudumia kiongozi wa upinzani, akimpangia miadi na akifuatana naye na serikali yake isikereke kwa hayo. 

Wakati nilipoonana naye, Wade alikuwa amekwishagombea urais mara nne na mara zote akibwagwa na Rais Abdou Diouf. Nilipokutana naye nilimuonea huruma na sikudhania katu kwamba miezi michache tu baadaye, atatimiza ndoto yake na hatimaye kumshinda Diouf. Nilimuona kuwa ni mtu myenyekevu na haikunipitia kwamba ana ujeuri anaouonyesha sasa.

Wade ni mtu aliyesoma; tena amesoma sana. Kwa hakika ni msomi kwani kuna tofauti kati ya mtu aliyesoma na msomi. Unaweza ukasoma masomo ya juu na kupata mashahada ya juu na usiwe msomi. Na unaweza kuwa msomi bila ya kupata cheti hata kimoja cha masomo.

Wade ana shahada mbili za udaktari — wa sheria na wa uchumi.  Alikuwa akifundisha sheria Ufaransa na nchini Senegal aliwahi kuwa mkuu wa kitivo cha sheria na uchumi katika Chuo Kikuu cha Dakar.
Alipokuwa kiongozi wa upinzani, Wade alikuwa akiukosoa sana  utawala wa chama cha Kisoshalisti wakati wa muasisi wake, Léopold Senghor na baadaye wakati wa uongozi wa Diouf. Nadhani Senghor alimng’amua mapema Wade kwani akimwita ‘sungura’.

Siku hizo Wade alikuwa akipigania sana utaratibu wa rais kutawala mihula miwili tu. Lakini katika kuhakikisha anakuwa tofauti na wengine akataka kipindi kiwe cha miaka saba badala ya mitano kama alivyofanya Paul Kagame, nchini Rwanda. Wade aliyeahidi kuiheshimu Katiba sasa ameivunja ahadi yake na ameibadili Katiba.

Alipoulizwa na mmoja wa wananchi wenzake mbona amekwenda kinyume cha ahadi aliyoitoa alipoingia madarakani alijibu: “Kweli niliyasema hayo wakati ule, lakini sasa nimebadili nia; tatizo likowapi ?”
Tatizo kubwa linalomkabili Wade hivi sasa ni zile shutuma zinazomuandama za utumiaji fedha za umma kwa ubadhirifu, ufisadi, kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari, ukiukwaji wa haki nyingine za kibinadamu na upendeleo wa kuwapa kazi jamaa zake. Mwanawe wa kiume, Karim amemteua kuwa waziri na binti yake, Sindjely amempa kazi ya kuwa msaidizi muhtasi wa Rais. 

Wade anawakebehi wanaosema kuwa yeye ni mzee na huenda asimalize kipindi chake kwa kuhoji kuwa ikiwa babu zake na baba yake waliishi na kufika umri wa miaka 100 ushei, kwa nini naye asifike umri huo.
Hivi sasa gumzo kubwa nchini Senegal ni juu ya uzee wake. Papo hapo kujitokeza kwa Youssou N’Dour kumeanzisha mjadala mwingine kwamba mtu asiye na elimu ya juu hawezi kuwa rais. Suala hili limeanzisha mtindo mpya barani Afrika. Nakumbuka nchini Tanzania, Augustine Mrema alilazimika haraka haraka ajiandikishe chuo kikuu kimoja cha Marekani apate shahada kwa njia ya mtandao ili aweze kugombea urais.

Cha kushangaza ni kuwa raia wa kawaida anaweza kugombea udiwani, ubunge au  hata kuwa waziri bila ya kujali kama ana shahada au elimu ya juu lakini ikija katika kugombea urais anaangushwa. Raia huyo anageuzwa wa daraja la pili na haki yake kukandamizwa.

Hata hivyo, tukitafakari hebu tujiulize hao wanaojiona kuwa ni wasomi au waliosoma pamoja na mashahada waliyonayo wameweza kweli kutimiza matarajio ya raia wa kawaida? Historia inatuonyesha kuwa wengi wao ndio walioharibu zaidi. Wamekosa muelekeo, uadilifu na nia safi ya kulitumikia taifa.

Siku hizi waliosoma wanaingia katika siasa ili wapate madaraka waweze kupora mali ya taifa. Angalia tu mishahara na marupurupu wanayojipa wabunge; yalinganishe hayo na mishahara duni ya watumishi wa kawaida serikalini.  Ndio maana ukaona kwamba leo madaktari, wanahiyari wawe wabunge na mawaziri wakati kuna uhaba wa  madaktari hospitalini. Wahadhiri nao vivyo hivyo wakati kuna uhaba  wa waalimu.
Linalochoma zaidi ni kuwaona wanasayansi wa vipawa vya juu wakizitupilia mbali taaluma zao wakikimbilia kwenye uwanja mchafu wa tope za kisiasa kwani siasa nchini mwetu zimegeuzwa kuwa hivyo. Ndio maana zinanuka.

Lakini si lazima ziwe hivyo. Na ndio maana wanachomoza wanasiasa wapya mithili ya Youssou N’Dour wanaoingia katika siasa kichwa upande kwa lengo la kuzisafisha siasa chafu. Wanaingia katika siasa wakiamini kwamba uongozi ni uwezo na busara na sio lazima kusoma kwingi.

Bila ya shaka hakuna anayetaka kiongozi mbumbumbu. Anayetakiwa ni kiongozi atayeweza kuongoza nchi kwa hekima na uadilifu. Anayetakiwa ni kiongozi imara atayeweza kuamua na kutekeleza uamuzi wake bila ya kuyumbishwa na majambazi wa kisiasa.

Ikiwa waimbaji wa Bongo Flava kama akina Professor Jay (Joseph Haule) na Sugu (Joseph Mbilinyi-Mbunge wa Mbeya Mjini) au hata Bob Junior na Ali Kiba watataka uongozi na wakaonyesha watakuwa na sera safi za kuongoza nchi kwa maadili ya utawala bora kwa nini wananchi wasiwachague? 
Tayari katika uchaguzi uliopita wapiga kura wa Mbeya (Mjini) walimchagua Sugu wa CHADEMA awe mbunge wao akimshinda mwalimu wake wa zamani wa shule, Benson Mpesya aliyekuwa mgombea ubunge mzito kutoka CCM.

Tupime maendeleo yaliyoletwa na vongozi wetu katika sekta za afya, elimu na kilimo. Tuangalie jitihada zao za kukabili njaa na kuondosha umasikini na tusiangalie tu barabara wanazozijenga. Siku hizi imegeuka  nyimbo watu kusema waziri au rais fulani amefanya mengi. ‘Angalia barabara kutoka mahala fulani hadi fulani.’

Sahibu yangu mmoja kutoka Liberia aliwahi kuniambia: “Afrika tunayapima zaidi maendeleo ya mwanasiasa kwa kuangalia kilomita ya barabara aliyojenga, badala ya sekta nyingine.”  Na mara nyingi barabara hizo huzijenga kwao.

Sitoshangaa ikiwa kutapita mizengwe nchini Senegal ya kumzuia Youssou N’Dour asiwe mgombea wa urais. Tayari wanaojiona kuwa ni wasomi wameshaanza kumbeza kuwa hawezi kuzungumza Kifaransa kwa ufasaha, kana kwamba Kifaransa chake ndicho kitakachofanikisha kupatikana elimu bora, matibabu bora na kupambana na umasikini. Lakini wasomi wetu wamezoea;wanaposhindwa kutoa hoja za maana hata kasumba kama hizi huzitumia.
Chanzo: Raia Mwema

Sunday, January 15, 2012

Msiba wa Mh. Regia Mtema

Best Blogger Tips

Mbunge Chadema afariki

Best Blogger Tips
Mh. Regia Estelatus Mtema
 MBUNGE wa Viti Maalumu kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Regia Estelatus  Mtema (32), amefariki dunia baada ya gari alilokuwa akiendesha, kupinduka eneo la Mlandizi, Kibaha mkoani Pwani jana.

Ajali hiyo ilitokea saa 5:30 asubuhi karibu na Sekondari ya Ruvu, wakati mbunge huyo na watu wengine saba, wakisafiri kwa gari aina ya Toyota Landcruiser wakitoka Dar es Salaam kwenda Morogoro.Akielezea mazingira ya ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Ernest Mangu, alisema mbunge huyo alifariki baada ya gari hilo alilokuwa akiendesha mwenyewe, kuacha njia na kupinduka.

Alisema ajali hiyo ilitokea baada ya Mtema kujaribu kulipita gari lililokuwa mbele yake na ghafla aliona gari lingine likija kasi mbele yake,  katika kujaribu kulikwepa, ndipo gari hilo lilipinduka.

"Wakati akiwa hajalipita gari hilo aliliona gari lingine likija mbele kwa kasi , katika kulikwepa wasigongane uso kwa uso, alitoa gari lake barabarani na kusababisha kupinduka,’’ alisema Mangu.

Alisema watu wengine saba  waliokuwa kwenye gari hilo walijeruhiwa, wawili kati yao  hali zao zilikuwa mbaya,  walipelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) Dar es Salaam kwa matibabu zaidi, huku wengine watano, wakiwahishwa Hospitali Teule ya Tumbi Kibaha.

Aliwataja majeruhi waliolazwa Tumbi kuwa ni Lawrence Mtokambali (58), Benadetha Mtema (50), Peter Madesa (50) na Rogers Abdallah(18).

Chadema yatoa tamko
Chadema kilisema kuwa Mtema alikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama hicho na Waziri Kivuli wa Kazi na  alikuwa mchapa kazi hodari katika majukumu mbalimbali yakiwepo ya kijamii na kisiasa.

Taarifa hiyo iliyotolewa na Chadema jana na kusainiwa na Katibu Mwenezi wa chama hicho, John Mnyika ilieleza kuwa viongozi wakuu wa chama hicho wakiongozwa na Mwenyekiti wao Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Dk Willibroad Slaa, wajumbe wa Kamati Kuu, Wakurugenzi wa chama hicho makao makuu na wabunge, wameshtushwa na kifo hicho na kuungana na familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

Chadema kimesema taarifa zaidi kuhusu taratibu za maziko, itatolewa mara baada ya kukamilisha majadiliano kati familia ya marehemu, chama na Ofisi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kufuatia kifo hicho, mkutano wa Chadema uliokuwa umepangwa kufanyika jana Mjini Kibaha umehirishwa hadi itakapotangazwa wakati mwingine.

Elimu yake
Mtema alizaliwa Aprili 21, 1980. Alisoma elimu ya msingi kati ya mwaka 1989 na 1995. Alijiunga na Shule ya Sekondari Forodhani, Dar es Salaam mwaka 1996 hadi  1999 na kuhitimu kidato cha nne.
Aliendelea kidato cha tano 2002 na sita kati ya mwaka 2000 na 2002 katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Machame, mkoani Kilimanjaro.

Mwaka 2003 hadi 2006 alisoma Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na kupata Shahada ya Maarifa ya nyumbani na Lishe. Baada ya kuhitimu shahada yake, marehemu Mtema alifanya kazi katika taasisi mbalimbali kabla ya kujiunga na Chadema na kuteuliwa kuwa Ofisa Mwandamizi katika Kurugenzi ya Vijana ya chama hicho.

Baadaye aliteuliwa kuwa Ofisa Mwandamizi katika Kurugenzi ya Mafunzo ya chama hicho, nafasi ambayo aliishikilia hadi mwaka 2010 alipoteuliwa kuwa Mbunge wa Viti Maalum.

JK amtumia rambirambi Mbowe
Wakati huo huo, Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kufuatia kifo cha mbunge huyo.

Katika salamu hizo, Rais ameelezea kusikitishwa kwake na taarifa za kifo cha mbunge huyo na kueleza kwamba, marehemu Mtema  amepoteza maisha akiwa kijana na kwamba pigo hilo si kwa Chadema pekee bali kwa taifa zima.

“Nimepokea kwa masikitiko na huzuni nyingi habari za kifo cha Mheshimiwa Mtema katika ajali ya gari. Siyo kwamba ajali hii imechukua maisha ya kijana bali imelinyang’anya taifa mbunge hodari, na kwa hakika, kifo chake siyo tu ni pigo kwa chama chako bali ni pigo kwa sote na kwa taifa letu kwa jumla.

"Nakutumia wewe binafsi, chama chako na wanachama wake salamu za dhati ya moyo wangu kuomboleza kifo na msiba huu mkubwa," alisema Rais Kikwete kupitia taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu.

Aliongeza: “Napenda ujue kuwa niko nanyi katika msiba huu. Napenda vilevile uniwasilishie salamu zangu za rambirambi za dhati kabisa kwa wana-familia, ndugu na jamaa wa marehemu Mheshimiwa Mtema.

Taarifa hiyo imemwomba Mbowe kufikisha salamu za Rais Kikwete kwa familia ya mbunge huyo na kuijulisha kuwa amepokea habari hizo kwa huzuni kubwa. "Wajulishe kuwa nawaombea kwa Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, awajalie uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu kwa sababu yote ni mapenzi yake.

Wananchi wamlilia
Katika kuonyesha kuguswa na kifo hicho mamia ya watu wanaotumia mtandao wa kijamii maarufu kwa jina la ‘Facebook’  walielezea kusikitishwa na kifo hicho huku wakitoa maoni mbalimbali.

Miongoni mwa maelezo yao ni juu ya maneno aliyowahi kuyazungumza mbunge huyo kijana, ukiwamo ujumbe alioandika katika mtandao huo akiwataka wananchi wamweleze kero zao ili azifikishe katika mkutano ujao wa Bunge.

Ujumbe huo aliouandika Januari 10 mwaka huu na kuungwa mkono na watu 159 ulisomeka hivi;

“Wapenzi, habari zenu kama una kero yoyote unayoona inafaa ikasemewe bungeni au nje ya Bunge na Wabunge na Viongozi wa Chadema basi tupia hapa kero yako. Angalizo; isiwe kero binafsi..., karibuni sana pamoja tunaweza”.

Mtema anakuwa mbunge wa pili wa chama hicho kufariki dunia kwa ajali ya gari, Julai 27, 2008 Mbunge mwingine wa chama hicho Jimbo la  Tarime, Chacha Wangwe alikufa katika ajali ya gari eneo la Pandambili mkoani Dodoma.

Taarifa ya Chadema ilieleza kwamba mipango ya mazishi ya marehemu inapangwa  nyumbani kwa baba yake, Tabata Dar es Salaam.
Chanzo: Mwananchi

Monday, January 9, 2012

Dallas Mavericks Ndani Ya White House

Best Blogger Tips

Beyonce na Jay-Z wapata mtoto

Best Blogger Tips
 Wanamuziki wenye kipaji cha hali ya juu ambao walifunga ndoa hivi karibuni, Beyonce na mumewe Jay-Z, wamepata mtoto wa kike ambaye wamempa jina la Blue Ivy.

Beyonce mwenye umri wa miaka 30, alijifungua salama mtoto wake kwa njia ya upasuaji siku ya jumamosi. Beyonce alijifungua katika hospitali ya kifahari ya Lenox Hill, jijini Manhattan, huku mume wake Jay-Z, ambaye jina lake halisi ni Shawn Carter, akiwa pembeni yake.

Beyonce alikwenda hospitali siku ya ijumaa na akajiandikisha kwa jina la "Ingrid Jackson," gharama ambayo imelipwa kwenye hospitali hiyo ni $1.3 millioni.

Salamu za pongezi zilianza kumiminika kwenye mtandao wa kijamii wa twitter, zikiwapongeza wawili hao kwa kupata mtoto.

Baadhi ya watu ambao walituma salamu hizo kwa njia ya twitter ni pamoja na Rihanna na pia mdogo wake Beyonce anayeitwa Solange Knowles.


Sunday, January 8, 2012

Wagonjwa Muhimbili walia adha ya mgomo

Best Blogger Tips
BAADHI ya wagonjwa na madaktari katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), wamesimulia adha wanazopata kutokana na kufukuzwa kwa madaktari wanafunzi waliokuwa wamegoma na wameiomba Serikali ifanye kila linalowesekana kunusuru hali hiyo.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, walisema mgomo huo umefanya hali katika hospitali hiyo  kuwa mbaya, kiasi cha baadhi ya wagonjwa kupoteza maisha kwa kukosa huduma.

Mmoja wa wagonjwa hao Godliver Alfonsi aliyetokea mkoani Kigoma alisema ana wiki moja tangu afike hospitalini hapo lakini hajaweza kuonana na daktari.

"Tangu nije leo (jana) tu ndio nawaona madaktari wakipita, lakini kwangu hawakupita kwa kuwa muda ni mdogo na wameniahidi kuwa watakuja kwangu kesho (leo)," alisema.

Mama wa mtoto Fatma Iddi katika wodi ya jengo la watoto, Hidaya Idrisa alisema madaktari hawaonekani wodini hapo kama ilivyokuwa awali.

Alisema kabla ya mgomo madaktari walikuwa wakikaa katika moja ya vyumba vya wodi hiyo, hivyo ilikuwa rahisi kuwapata kunapotokea tatizo.

“Madaktari hapa walikuwa hawaondoki kila wakati wapo na wakati wowote ukiwa na shida unapata msaada lakini hivi sasa chumba chao kitupu, hawapo” alisema Hidaya.

Hali katika wodi ya Kibasila pia ni mbaya na muuguzi wa zamu katika moja ya wodi za jengo hilo alisema; "Inawachukua muda wagonjwa kuonana na daktari kutokana na uchache wa madaktari."

“Mfano daktari ambaye yupo sasa aliingia kazini jana (juzi) mpaka sasa ninavyoongea hajaondoka maana yuko peke yake,” alisema muuguzi huyo.

Mgonjwa mwingine hospitalini hapo ambaye hakutaka kutajwa gazetini alisema: “Tangu asubuhi sijaonana na daktari sasa ni mchana (saa 12.30) na sina tumaini la kupata huduma”.

“Kama ningekuwa mahututi pengine hata wewe mwandishi usingenikuta, tungekuwa tunaongea mengine hapa,” alisema mgonjwa huyo.

Mmoja kati ya wanafunzi (jina limehifadhiwa), ambaye yupo katika mafunzo kwa vitendo tatu mwezi Desemba mwaka jana hosipitalini hapo, anasema hali si nzuri na kwamba ikiendelea hivyo huenda idadi ya vifo ikaongezeka.

“Idadi ya vifo vya sasa huwezi kuvihusisha na mgomo moja kwa moja lakini sina shaka kabisa kuwa vipo ambavyo vinachangiwa na hali hii,”alisema daktari huyo mwanafunzi.

Alisema kwa sasa madaktari bingwa hawana wasaidizi hali ambayo inawafanya wafanye kazi muda mrefu na kushindwa kuwafikia baadhi ya wagonjwa.

“Madaktari wanachoka, hata sisi wachache ambao tunasaidiana nao tunakuwa katika wakati mgumu” alisema na kuongeza kuwa hali hiyo inawafanya wawazungukie wagonjwa hadi saa nane mchana badala ya muda wa kawaida wa saa mbili asubuhi.

Madaktari
Katibu wa Chama cha Madakitari Tanzania (MAT) Dk. Rodrick Kabangila alisema tabia ya Serikali kuingiza siasa katika taaluma inaathiri huduma kwa umma.

Alisema kila jambo hivi sasa linachukuliwa kisiasa kwa kupiga porojo badala ya utekelezaji na kwamba sasa siasa zimeingia katika taaluma ya udaktari na uuguzi.

Kabangila alisema serikali inatumia mamilioni ya shilingi kuwatibu viongozi nje ya nchi lakini inashindwa kutumia pesa hizo kuwalipa madaktari stahili zao na kununua vifaa tiba vya kisasa.

Alisema Tanzania inaongoza kwa kupeleka wagonjwa nchini India, sifa ambayo alisema si nzuri na kwamba hatari zaidi viongozi serikalini wanajivunia hali hiyo.

Katibu huyo alisema wamekaa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na viongozi wengine wa serikali na wamewataadharisha juu ya mwenendo huo.

Kabangila alisema chama cha madaktari kitafanya mkutano wake mkuu Jumamosi ijayo, ambao pamoja na mambo mengine utajadili masuala ambayo yamejitokeza katika mgomo huo na kufikiria hatua zaidi za kuchukua.

Alisema wanaishangaa wizara ambayo baada ya kulipa posho za madaktari wanafunzi wamewaita wahusika wizarani na kwamba hatua hiyo ni kukwepa hoja ya msingi.

Kauli ya Serikali
Madaktari hao 229 walianza mgomo Jumanne wiki iliyopira, wakiishinikiza Serikali iwalipe posho zao za Desemba mwaka jana ambazo ni zaidi ya Sh179 milioni.

Kwa mujibu wa madaktari hao, uamuzi huo ulifikiwa baada ya wizara kushindwa kuwalipa posho zao kwa wakati hali iliyowafanya waishi kwa tabu.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda, alikiri hali hiyo na kusema kuwa imesababishwa na ukata ulioikumba wizara hivyo kushindwa kuwalipa madaktari hao kwa wakati.

Dk Mponda alisema kwa kawaida posho hizo hulipwa tarehe 22 ya kila mwezi na kwamba kiasi cha fedha ambacho hulipwa ni Sh900 milioni kwa madaktari wanafunzi nchi nzima.

Pamoja na maelezo hayo, serikali iliwapa barua za kujieleza madaktari wote waliokuwa wamegoma licha ya kwamba baadhi yao walishaanza kurejea kazini baada ya kuwa wamelipwa posho hizo.
Chanzo: Mwananchi

Thursday, January 5, 2012

Lebron James amvisha pete mama watoto

Best Blogger Tips
Mchezaji mahili wa mpira wa kikapu wa timu ya Miami Heat,Lebron James, amesheherekea sikukuu ya mwaka mpya na ile ya kuzaliwa kwake kwa kumvalisha pete mchumba wake.

James alimvisha pete mchumba wake wa muda mrefu Savannah Brinson, mama wa watoto zake wawili katika hoteli ya South Beach iliyopo jijini Miami

Wawili hao wamekuwa pamoja kwa muda mrefu tangu  James akiwa shuleni  huko Akron, katika jimbo la Ohio.

Wiki iliyopita aliyekuwa mchezaji hodari wa mpira wa kikapu na mmiliki wa timu ya Challote, Michael Jordan, alimvisha pete mchumba wake Yvette Prieto.

Tunapenda kutoa pongezi kwa ndugu hawa kwa jambo hili muhimu walilolifanya.

Wednesday, January 4, 2012

Hamad Rashid ang'olewa CUF

Best Blogger Tips
Hamad Rashid
 HATIMAYE Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed na wenzake watatu wamefukuzwa uanachama wa CUF kuanzia jana. Hatua hiyo ilichukuliwa na zaidi ya robo tatu ya wajumbe wa Baraza Kuu la chama hicho katika kikao chake kilichofanyika hapa.

Uamuzi huo umekata mzizi wa fitina wa hatma ya Hamad na washirika wake hao kisiasa ndani ya chama hicho, baada ya kuibuka mvutano wa muda mrefu kati yake na uongozi wa juu.

Mvutano huo uliochomoza zaidi baada ya Hamad kutangaza kuwania nafasi ya Katibu Mkuu inayoshikiliwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad.

Hata hivyo, hatua hiyo imepingwa na Hamad ambaye ameiita kuwa ni ya kihuni kwani imekiuka amri ya Mahakama iliyotangaza kusitishwa kwa kikao kilichochukua uamuzi huo.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), Julius Mtatiro alithibitisha kuvuliwa uanachama kwa Hamad na kuwataja wengine walioondolewa pia kuwa ni Mjumbe wa Baraza Kuu (Tanga), Doyo Hassan Doyo, Mjumbe wa Baraza Kuu (Pemba), Shoka Khamis Juma, Mjumbe wa Baraza Kuu Unguja, Juma Saanane na Mjumbe wa Baraza Kuu (Mbeya), Yassin Mrotwa.

“Kwa mujibu wa katiba ya chama, wasioridhika na uamuzi huo wanaweza kukata rufaa kwenye mkutano mkuu wa taifa,” alisema.

Naibu Katibu Mkuu CUF Zanzibar, Ismail Jussa akizungumza jana jioni na Idhaa ya Kiswahili ya Redio Ujerumani (DW), alisema haoni kama hatua hiyo ya kuwafukuza wanachama hao akiwamo Hamad ambaye aliwahi kuwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni kunaweza kuhatarisha mustakabali wa chama hicho.

“Ni kweli Hamad ametoa mchangao mkubwa ndani ya chama. Lakini wakati mwingine unapima faida na hasara sasa hivi Hamad alikuwa anaelekea kuvuruga chama,” alisema Jussa

Hamad: Ni uamuzi wa kihuni


Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kikao hicho, Hamad alisema anashangazwa na kiongozi wa nchi (Maalim Seif), kushindwa kuheshimu amri ya Mahakama na kuendelea na kikao ambacho ilikuwa imeamuru kisitishwe.

“Kiongozi wa nchi anakaidi uamuzi wa mahakama... uamuzi huu mimi nauita ni uamuzi wa kihuni, nimekwenda kwenye kikao naulizwa maswali ambayo wao wamejipanga na mashahidi wao mimi sijajipanga, sina shahidi nawaambia wanipe maswali ili nipate muda wa kuyajibu na kuandaa mashahidi kama wao hawataki, sasa demokrasia ipo wapi hapo?” alisema Hamad.

Hamad alisema hati ya kusimamishwa kwa kikao hicho ilifika ukumbini hapo saa 6:10 mchana, lakini wajumbe wa kikao hicho walionekana kuipuuza na kuendelea nacho na hati iliyopelekwa makao makuu ya Dar es Salaam saa 2:00 jana ilikatiliwa kupokewa akidai kwamba ni kwa agizo kutoka kwa viongozi wakuu.

Alisema hati ya mahakama inaonyesha kwamba wanatakiwa kwenda mahakamani Februari 14, mwaka huu na kusema kwamba uamuzi wa kuaminika utatolewa huko kwani katika chama hicho wanachama wengine wanaonekana hawana nguvu kama katibu mkuu.

Alisema wanachama wote wa CUF wanapaswa kufurahi kwani hajaumizwa na uamuzi kwa kuwa viongozi wake wamekuwa wakionekana kuhubiri haki sawa huku wakienda tofauti na msimamo wa chama.

“Maalim Seif kila siku anaonekana anahubiri haki sawa kumbe hana lolote, anakandamiza tu watu kwa kuharibu chama na kutoa maamuzi kibabe. Mimi sipo tayari kuburuzwa, wakitaka tuelewane haki wanayoihubiri iwe inatendeka kweli,” alisema Hamad.

Kwa upande wake, Shoka Khamis ambaye alikuwa Mbunge wa Micheweni, Kaskazini Pemba katika Bunge la Tisa, alisema kwa mujibu wa katiba ya CUF hamjui aliyemtuhumu kwani haiwezekani mtu asomewe shtaka bila kujua anayemtuhumu.

“Nimejifundisha mengi sana CUF mazuri na mabaya, lakini leo kwa sababu wamenifukuza ngoja niseme mabaya, CUF sisi ni CCM B kama wanavyosema wenzetu. Chama kina sifa mbaya ya kufukuza watu, lakini anayefukuza wenzake, Seif Sharif Hamad yeye anajiona kama mungu hafanyi makosa,” alisema Shoka.

Alisema hawapo tayari kujiunga na chama chochote cha siasa kama maneno yanavyosambazwa kuwa watahamia Chadema. Alisema watafufua Chama Cha Wananchi (CCW) ambacho kiliungana n Kamahuru na kuipata CUF.

“Tuna mpango wa kuanzisha chama kingine kwani CUF kwa sasa kimeshakuwa chama cha mtu ambaye ni Seif na siyo cha wananchi kama kinavyojulikana katika siasa za nchi hii,” alisema Shoka.

Hamad na hujuma

Desemba 27, mwaka jana Hamad aligoma kuhojiwa na Kamati ya Maadili na Nidhamu, akitoa sababu tano huku akiibua tuhuma nzito za kunasa waraka wa mawasiliano uliotumwa kwa barua pepe na Maalim Seif kwenda kwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba ukionyesha mpango wa kumshughulikia.

Sababu ya pili, alisema baadhi ya walioteuliwa katika kamati hiyo ya Nidhamu na Maadili walikwisha mtuhumu hadharani na kumtia hatiani hivyo, kikao hicho kisingeweza kumtendea  haki.

Alitaja sababu nyingine ya kukataa kuhojiwa kuwa ni kutoelezwa tuhuma zake hasa vifungu vya Katiba alivyodaiwa kuvikiuka.

Pia alitaka apewe hadidu za rejea za kikao kilichounda Kamati ya Nidhamu na Maadili kwa sababu haipo kikatiba, hakuna chombo kama hicho. Aligoma pia kuhudhuria kikao hicho kwa kuwa tayari alibaini njama za kumshughulikia zilizosukwa na Maalim Seif na Lipumba.

Hamad Rashid alijikuta kwenye mgogoro huo baada ya kutangaza dhamira yake hiyo ya kugombea nafasi ya katibu mkuu mwaka 2014.

Kuanzia hapo akajikuta ameingia kwenye mgogoro na chama hicho kiasi cha kunusurika kushambuliwa na watu wasiojulikana wakati akigawa misaada katika matawi ya chama hicho, Kata ya Manzese.
Chanzo: Mwananchi

Sheria mpya Saudi Arabia

Best Blogger Tips
Mwanamke wa Kisaudi
Sheria mpya inayowapiga marufuku wanaume kuuza nguo za ndani za wanawake kama vile chupi na sidiria inaanza kutekelezwa hii leo nchini Saudi Arabia.

Wanaharakati wa kike katika Ufalme huo wa kiislamu wanatumai kuwa agizo hilo lililotolewa na mfalme Abdulla mwaka wa 2006, utamaliza mfadhaiko ulipo wakati wanawake wanauziwa nguo zao za wasaidizi wanaume madukani.

Ajira kwa wanawake

Hatua hiyo itawapa fursa adimu zaidi ya wanawake 40,000 kuchukua nafasi za kazi zitakazoaachwa wazi.
Maafisa wa kidini wasiopendelea mabadiliko wamepinga vikali hatua hiyo ya wanawake kufanya kazi nje ya nyumba zao.

Serikali imepanga kupeleka waangalizi katika vituo vya biashara kote nchini kuhakikisha kwamba wasaidizi wanawake madukani hawabughudhiwi na maafisa wa polisi wa kidini.
Chanzo: BBC

 


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits