Friday, September 24, 2010

Best Blogger Tips

The Richest People In America

See the 2010 Forbes 400 Rich List
 
America's super rich are getting poorer. For only the fifth time since 1982, the collective net worth of The Forbes 400, our annual tally of the nation's richest people, has declined, falling $300 billion in the past 12 months from $1.57 trillion to $1.27 trillion.

Faltering capital markets and real estate prices, along with divorce and fraud, pushed the fortunes of 314 members down and drove 32 plutocrats off the rankings.
Access the full story................
Best Blogger Tips

Wednesday, September 22, 2010

Best Blogger Tips

Couple admits using five disabled Tanzanian children to beg for alms

Via Nation

A couple has admitted bringing disabled children from Tanzania into the country and using them to earn money by begging in city streets.

Mr Jisena Kulwa Dutu, a Tanzanian, and his Kenyan wife Josephine Mueni appeared before Makadara principal magistrate Terry Ngugi.

Accompanying the couple were the five paralysed children. A bag containing money in various denominations was also exhibited in court.

“Your honour police have brought before this court these unusual exhibits - distraught paralysed children and a bag containing the alms they had collected from good Samaritans. I wish to produce them before this court,” prosecutor Esther Ngure said.

Ms Ngure added that the cash in the bag amounted to Sh13,000.
Access the full story........................

Tuesday, September 21, 2010

Best Blogger Tips
Hili ni Kanisa la RC lililopo Mshindo, Mkoani Iringa. Ukiwa sehemu yoyote ya mji wa Iringa unaweza kuliona Kanisa hili.
Picha hii na nyingine nyingi pamoja na habari zinazohusu Mkoa wa Iringa utazipata kwenye blog ya Francis Godwin, Mzee wa Matukio.

Monday, September 20, 2010

Best Blogger Tips
CCM yamwangukia Bashe

CHAMA cha Mapinduzi (CCM), kimegeuka kuwa kigeugeu baada ya kumwangukia aliyekuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) na Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC), Hussein Bashe, kikimtaka akasaidie kukipigia kampeni katika jimbo la Nzega mkoani Tabora.

Habari za kuaminika zilizopatikana kutoka Nzega na Dar es Salaam jana, zinasema CCM imeteua zaidi ya makada 20 katika jimbo hilo, kwa ajili ya kukinadi chama hicho ambacho kinaonekana kupata wakati mgumu.

Bashe ambaye alitangazwa na CCM hivi karibuni na kuvuliwa nyadhifa zote na Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), kisha kutangazwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa chama hicho, Kapteni John Chiligati, kuwa si raia, kunaibua maswali mengi kama uamuzi huo, ulikuwa sahihi.

Bashe ambaye alishinda kura za maoni kwenye jimbo la Nzega, lililokuwa likishikiliwa na Lucas Selelii, (CCM) na ushindi wake kupewa Dk. Hamisi Kigwangala ambaye amepitishwa rasmi kupeperusha bendera ya chama katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Akitangaza uamuzi huo, baada ya kumalizika kwa kikao cha NEC cha mchujo wa wagombea ubunge na Baraza la Wawakilishi, Chiligati, alisema CCM imeamua kumtimua Bashe uanachama na kumuengua kuwania ubunge katika jimbo la Nzega, baada ya kubaini kuwa ni raia wa Somalia.
Endelea kusoma habari hii.............

Thursday, September 16, 2010

Best Blogger Tips
Prosper Riddim

Sunday, September 12, 2010

Best Blogger Tips
Miss Tanzania 2010

Vodacom Miss Tanzania Geneviva Mpangala akiwa na washindi wenzie mara baada ya kutangazwa mshindi kwenye shindano hilo lililofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam usiku huu kulia ni mshindi wa tatu Consolata Msofe na kushoto ni mshindi wa pili Groly Mwanga, Geneviva ataiwakilisha nchi katika shindano kubwa la Dunia Miss World litakalofanyika mwishoni mwa mwaka huu.

Thursday, September 9, 2010

Best Blogger Tips
Eid Mubarak

May the Guidence and Blessings of Allah Be with You and Your family

Friday, September 3, 2010

Best Blogger Tips
Dk.Slaa amtega Makamba

Via ippmedia

.Amtaka atoboe kilichomfukuzisha ualimu
.Vinginevyo atayaanika yote aliyoyatenda
.Kingunge naye atumbukia hoja ya ndoa

Mgombea wa Urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibroad Slaa, amesema Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba, hana ubavu wa kuhoji masuala ya uadilifu wa ndoa.

Alisema badala yake, Makamba anapaswa kuuelezea umma sababu zilizomfanya afukuzwe katika kazi ya ualimu akiwa Mkuu wa shule ya msingi.

Dk. Slaa alivunja ukimya jana alipokuwa akihutubia mkutano wa kampeni katika uwanja wa Kwaraha mjini Babati.

Dk. Slaa alisema ndoa yake kamwe haijamshinda na kwamba hakuna mwenye uwezo wa kumchagulia mke na kwamba kufunga ndoa ni makubaliano ya watu wawili.

Alitumia fursa hiyo kumtambulisha mke wake, Josephine na kuhoji, “kipi bora kuwa na mke mmoja hadharani au kuwa na nyumba ndogo nyingi?”

Pia alivunja ukimya na kuamua kujibu tuhuma mbalimbali zinazoelekezwa kwake na wapinzani wake wa kisiasa hasa masuala ya Ukatoliki, kuacha upadre na maisha yake ya ndoa.

Aidha, Dk. Slaa alieleza kusikitishwa kwake na kitendo cha polisi kusimamisha magari ya msafara wake juzi, na kuwataka kutenda haki na kusimamia kile walichokubaliana katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu.
Endelea kusoma habari hii..............................

Thursday, September 2, 2010

Best Blogger Tips
Slaa amvaa mke wa Kikwete

Via Mwananchi

KAMPENI za uchaguzi mkuu zimezidi kunoga baada ya mgombea urais wa Chadema, Dk Slaa kumgeukia mke wa Rais Jakaya Kikwete akieleza kuwa anatumia vibaya rasilimali za nchi kumpigia kampeni mumewe huku akimtaka katibu mkuu wa CCM, Yusuph Makamba aeleze kisa cha kufukuzwa ualimu mkuu wa shule ya msingi.

Kwa muda mrefu Salma Kikwete, mke wa Rais Kikwete na ambaye pia ni mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (Wama), amekuwa katika ziara kwenye mikoa mbalimbali, jambo ambalo limekuwa likitafsiriwa kuwa anafanya ziara za kampeni kwa ajili ya mumewe. Kwa sasa yuko mkoani Manyara.

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni, Dk Slaa ambaye ameripotiwa kuwa na makombora 20 kwa ajili ya kuimaliza CCM, alisema kitendo cha mke huyo wa rais kumpigia kampeni kwa kutumia rasilimali za umma ni ufisadi.

“Mke wa rais si rais," alisema Dk Slaa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Kwara ulio Babati Mjini.

"Mama Salma anatembea na askari wa serikali; magari ya serikali na wakuu wa mikoa na wilaya. Anatumia fedha za Ikulu kwa sababu walinzi wake wanalipwa na Ikulu. Huu ni ufisadi.”
Endelea kusoma habari hii......................

Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits