Monday, November 7, 2011

Joe Frazier aumwa saratani ya ini

Best Blogger Tips
Joe Frazier
 Bingwa zamani wa ndondi za uzito wa juu duniani Joe Frazier yupo katika nyumba wanayouguzwa wagonjwa mahututi akiwa anaumwa saratani ya ini, meneja wake amesema.

Amesema Frazier - anayejulikana pia kwa jina la Smokin' Joe - aligunduliwa anaumwa saratani wiki kadha zilizopita.

"Nitakuwa muongo iwapo sitawaeleza kwamba hali yake si nzuri," Leslie Wolf alilieleza shirika la habari la Uingereza la Reuters.

Frazier mwenye umri wa miaka 67 alishikilia mkanda wa ubingwa wa dunia miaka kati ya 1970 na 1973. Alikuwa ndiye mtu wa kwanza kumchapa Muhammad Ali mwaka 1971. Baadae akachapwa na Ali katika mapambano mawili yaliyofuatia.

Bw Wolf amesema Frazier aligunduliwa na maradhi ya saratani ya ini mwezi uliopita na kwa sasa anatibiwa katika nyumba maalum inayotunza wagonjwa mahututi huko Philadelphia.

"Joe ni mpiganaji. Joe kamwe hashindwi," meneja huyo alisema, akaongeza madaktari na watu wa karibu wa Frazier "tunafanya kila jitahada".

Frazier alishinda taji la ubingwa wa dunia kwa uzito wa juu mwaka 1970 baada ya kumtwanga Jimmy Ellis mjini New York. Aliendelea kushikilia taji hilo hadi mwaka 1973, ambapo alipigwa na George Foreman.

Lakini mwanamasumbwi huyo huenda anafahamika zaidi kwa mapambano makubwa na Ali, likiwemo lile la kukata na shoka la Phillipines lililopewa jina la Thriller in Manila mwaka 1975.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits