Monday, May 30, 2011

Best Blogger Tips
America's Best Affordable Places, 2011 

As the old saying goes, you get what you pay for. Unfortunately in real estate, value is a trade-off. Someone in Manhattan is willing to pay $2,200 per month to rent a studio apartment so as to be near jobs and cultural amenities, sacrificing square footage. For someone in Las Vegas, where housing is inexpensive—the city's median home value is about $115,000, according to real estate site Zillow.com—and the labor market is tough, the reverse is true. What if you could have both proximity to work and quality of life at an affordable cost?

While this may sound too good to be true, it's the status quo in some places.

In an exclusive ranking for Businessweek.com, Bloomberg Rankings analyzed government-gathered data on more than 3,000 counties across the U.S. to select the best affordable place in each state. We then scored each county by state. Next we tallied the top-ranked county in each state to arrive at a national ranking. Factors that were most heavily weighted include housing cost, crime, unemployment, and educational attainment in the county, in addition to such other metrics as family income, poverty, commute time, air quality, diversity, and share of families with children.

The Midwest made out well in the ranking. No. 1 on Bloomberg's list: North Dakota's Cass County, home to Fargo and West Fargo. Other areas with high scores include Brown County, S.D., Cleveland County, Okla. (in the West South Central region), Story County, Iowa, and Olmsted County, Minn.
Coastal states with high unemployment such as California, Florida, and Rhode Island ranked lower, as did states with a generally high cost of living, such as Hawaii.
Access the full story................

Friday, May 27, 2011

Best Blogger Tips
Hospitali kubwa ya moyo kujengwa Mlimani City

Via HabariLeo

HOSPITALI kubwa ya moyo itaanza kujengwa eneo la Mlimani City Dar es Salaam wakati wowote kuanzia sasa na kukamilika ndani ya miezi 30 ijayo, ili kutoa huduma ya upasuaji na tiba ya moyo.

Ujenzi huo utafanywa na Shirika la Hifadhi ya Jamii Nchini (NSSF) kwa ushirikiano na Hospitali ya Apollo za India, chini ya usimamizi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ya Tanzania.

Mkataba wa ujenzi huo ulisainiwa Ikulu Dar es Salaam jana mbele ya Rais Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu wa India, Dk. Manmohan Singh na umelenga kuimarisha uwezo wa Tanzania kukabili magonjwa ya moyo, saratani na figo yanayohitaji utaalamu zaidi.

Akizungumza baada ya kusainiwa kwa mkataba huo, Rais Kikwete alisema hayo ni matunda ya ujio wa Dk. Singh nchini.

Rais alisema, ujenzi wa hospitali hiyo utaokoa mabilioni ya fedha za Serikali yanayotumika kupeleka wagonjwa wa moyo nchini India kwa ajili ya upasuaji na tiba nyingine pamoja na gharama za mafunzo ya madaktari.

Madaktari hao wamekuwa wakitumwa kupata utaalamu zaidi katika Hospitali ya Apollo nchini India lakini Rais Kikwete alisema fedha hizo za mafunzo zitaokolewa kwa kuwa wanachokifuata huko kitapatikana nchini.

Rais Kikwete alitoa mfano wa mwaka jana amabo Serikali ilitumia Sh. bilioni 11 kupeleka wagonjwa wake India kwa ajili ya matibabu ya ugonjwa wa moyo wakati gharama hizo zingeweza kupungua zaidi kama huduma hiyo ingepatikana nchini.

“Kwa kuanzia, tutahakikisha hospitali hiyo mpya inakuwa na wataalamu bora wa kutosha wa kutibu ugonjwa wa moyo ndipo tuendelee na ule wa saratani na figo. Wenzetu wa Apollo wamekubali kuja kutumegea utaalamu kwa kutoa mafunzo hapa hapa nchini hospitali hiyo itakapo anza kazi miaka miwili na nusu ijayo.

“Hatutakuwa na sababu ya kuhamishia wagonjwa wetu wa moyo India tena kwa sababu mkataba tulio saini unaeleza wazi kuwa hospitali hiyo itatoa huduma kama tunayoifuata katika nchi hiyo. Vifaa vya tiba na wataalamu watakao wapa ujuzi wataalamu wa nchini pia watatoka India kwa makubaliano ya ushirikiano,” alisema Rais Kikwete.

Kwa mujibu wa Kikwete, baada ya kusainiwa kwa mkataba huo wagonjwa wanaotakiwa kuhudhuria kliniki za moyo nchini humo kila baada ya miezi mitatu, hawatafanya hivyo kwa sababu madakitari wao watakuja nchini mara kwa mara kuwaona.

“Utaratibu huu upo kwenye makubaliano yetu na utatuondolea gharama tunazozipata sasa. Madaktari wa India wataanza kuwafuata wagonjwa wao nchini. Huu ni ushirikiano wenye faida,” alisema.

Akizungumzia uwezo wa madaktari wanaopata mafunzo kutoka kwa wataalamu wa India, Rais Kikwete alisema umedhihirika pale walipofanikisha operesheni 155 za moyo nchini.

Alisema, madaktari na wauguzi 29 wa magonjwa ya moyo na mengine yanayoambatana na ugojwa huo walipata mafunzo India na kufaulu kwa kiwango kizuri cha kuendesha huduma hiyo kwa upana zaidi nchini.

Mbali na hilo, Rais alimweleza Dk. Sigh kuwa uwekezaji wa nchi yake Tanzania ni Sh. bilioni 1.3 tu, kiasi alichosema kuwa ni kidogo sana ikilinganishwa na uzuri wa uhusiano wa nchi hizo mbili.

Alisema anaamini baada ya kusainiwa kwa mkataba huo kuhusu ukataji kodi, uwekezaji utaimarika maradufu kwa sababu kampuni iliyowekeza katika nchi hizo mbili itawajibika kulipa kodi kwenye nchi moja pekee.

Dk. Singh alimuhakikishia Rais Kikwete kuwa atafanya ushawishi wa kutosha kuuimarisha wawekezaji kuwekeza nchini.

Mbali makubaliano ya ushirikiano katika uwekezaji na ulinzi, Dk. Singh alimhakikishai Rais Kikwete kuwa nchi yake itaiwezesha Tanzania kupata ujuzi wa teknolojia mbalimbali na biashara ili iwe kitovu cha maendeleo katika Afrika Mashariki kwa kuwa ni mshirika wake wa karibu katika masuala ya kiuchumi.

Dk. Singh anayerejea nchini kwake leo alizindua mradi wa Kituo cha Ubora katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano cha Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) ulioanzishwa kwa ushirikiano wa nchi hizo mbili.

Thursday, May 26, 2011

Best Blogger Tips
Wabunge, Waziri watunishiana misuli

Via Newhabari

WAZIRI wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Gaudensia Kabaka jana alivutana vikali na wabunge wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii waliokuwa wanataka kutembelea Kiwanda cha Vyombo vya Nyumbani cha Jambo Plastiki kilichoko Dar es Salaam.


Wakati wajumbe wa Kamati hiyo wakiwa wamekwisha kujiandaa kwenda katika kiwanda hicho jana, ghafla Waziri Kabaka aliwaeleza kuwa ziara hiyo imeahirishwa hadi wakati mwingine.

Kabaka alitoa sababu za kutaka kuahirisha ziara hiyo kuwa ni mgogoro wa wafanyakazi na mwajiri kiwandani hapo ambao upo mahakamani hivyo ziara hiyo itakuwa ni kuingilia uhuru wa mahakama.

Baada ya kutolewa taarifa hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Jenista Mhagama alikuja juu na kumweleza Kabaka kuwa kamwe kamati yake haiwezi kuahirisha ziara hiyo bila kutolewa sababu za kuridhisha. Alisema kitendo alichokifanya Waziri kinadhalilisha kamati yake.

“Mheshimiwa Waziri kitendo ulichokifanya unaingiza mgogoro mkubwa katika kamati ya Bunge… kwa mazingira ya sasa Watanzania hawana mahali popote pa kutolea shida zao zaidi ya bunge na hii inadhihirika wazi wataalamu wako hawakukushauri vizuri,” alisema Mbunge huyo wa Peramiho kwa tiketi ya CCM na kuongeza:
“Basi kama ni hivyo, Mheshimiwa Waziri mimi nakupisha uwe mwenyekiti wa kamati ya Bunge maana naona hutaki kutuelewa.”

Kuona hivyo, Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde alikwenda mbali zaidi kwa kusema kwa uzoefu uliopo nchini unaonyesha kuwa ziara hiyo tayari imekwicha kuchakachuliwa na wahusika kwa manufaa wanayoyajua wao.

Alisisitiza kwamba kama ziara itaahirishwa basi yeye hatakuwamo kwenye orodha hiyo.

Naye Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Chadema) alisema kama kamati haitaki kwenda kwenye kiwanda hicho yeye atapanga ziara yake kama mbunge wa Chadema na kwenda kusikiliza na kukagua mazingira kiwandani hapo.
Endelea kusoma habari hii.......................

Wednesday, May 25, 2011

Best Blogger Tips
Nato yaishambulia Libya usiku kucha

Takriban milipuko mikubwa mitano imeitikisa Tripoli usiku kucha, wakati harakati za majeshi ya umoja wa nchi za kujihami za Ulaya Nato zikiendelea kwenye mji mkuu wa Libya.

Kwa usiku wa pili, mashambulio ya anga yalilenga ngome ya Bab al-Aziziya ya Kanali Muammar Gaddafi.

Nato inatekeleza azimio la umoja wa mataifa la kulinda raia wa Libya, kufuatia maandamano dhidi ya uongozi wa Kanali Gaddafi.

Lakini Urusi, ambayo haikuunga mkono azimio hilo, imesema uvamizi huo ni ukiukwaji wa umoja huo.

Mwandishi wa BBC Andrew North mjini Tripoli alisema mashambulio ya Jumanne usiku si makubwa kama yaliyofanyika Jumatatu usiku, lakini bado yalitikisa majengo eneo kubwa.

Moshi ulionekana kutanda kwenye mji huo.

Nato ilisema ngome hiyo ya Bab al-Aziziya imekuwa ikitumika kama kituo cha majeshi na magari ya kijeshi yaliyotumika kushambulia raia.

Lakini serikali ya Libya imesema Nato inajaribu kumwuua Kanali Gaddafi na mashambulio ya usiku yanawatisha raia wa Tripoli.
Source: BBC
Best Blogger Tips
Aliyekuwa mume wa mfanyakazi wa ndani aongea

Aliyekuwa mume wa  mwanamke ambaye ametangazwa na vyombo vya habari kwamba ni mama wa mtoto wa Arnold Schwarzenegger  aliyezaa nje ya ndoa, anasema kwamba anahisi kuzungukwa  na  aliyekuwa Gavana wa Califonia.

Katika mahojiano na jarida la Entertainment Tonight, Rogelio Baena anasema kwamba juma lililopita ndipo alipofahamu kwamba yeye siye baba mzazi wa mtoto huyo. Amesisitiza kwamba ataendelea kumtambua mtoto huyo kama ni wa kwake na si vinginevyo.

Jarida la “The Insider” siku ya jumanne lilionyesha video ya aliyekuwa mke wa Schwarzenegger, Maria Shriver akimsifia mwanamke huyo Mildred Baena katika sherehe ya mmoja wa jamaa zake, kwamba ni mwanamke jasiri na mfanyakazi hodari, huku Schwarzenegger akisikika kusema kwamba mfanyakazi huyo wa nyumbani amefanya kazi “nzuri sana”.

Mildred Baena, ametambuliwa kwamba ni mama mzazi wa mtoto wa Schwarzenegger na jarida la New York Times na  vyombo vingine vya habari.

Tuesday, May 24, 2011

Best Blogger Tips
Tiba ya Babu Samunge: Mwingine adai kupona ukimwi

Via Mwananchi

MKAZI wa Kijiji cha Galapo, Babati, mkoani Manyara, Abdalah Ally (38), aliyekuwa mgonjwa wa Ukimwi, amedai kupona ugonjwa huo na kinga zake za mwili (CD4) kuongezeka baada ya kunywa dawa ya Mchungaji, Ambilikile Mwasapila.Ally anakuwa mtu wa pili kujitangaza kupona Ukimwi baada ya kunywa kikombe cha dawa hiyo, baada ya Wilia John Lengume wa Samunge aliyekuwa wa kwanza kutangaza kupona ugonjwa huo baada ya kupata dawa hiyo.

Akizungumza jana kijijini hapa, Ally alisema kwamba amekuwa akitumia Dawa za Kupunguza Makali ya Ukimwi (ARV), tangu mwaka 2009 kabla ya kupata kikombe cha Babu, Januari 5, mwaka huu.

Akiwa na vyeti vya vilivyoonyesha kwamba alikuwa na maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU), Ally alisema kuwa Aprili 22, 2009 alipimwa na kukutwa na maambukizi hayo wakati huo akiwa mfungwa katika Gereza la Babati.

Alisema alipima afya yake Februari 25, mwaka huu wilayani Babati na katikia Kituo cha Msalaba Mwekundu na kukutwa hana tena VVU. Alipima tena katika Hospitali ya Wilaya ya Babati ambako pia alikutwa kinga yake ya mwili ni ya kutosha na hana tena VVU ndipo alipoamua kuacha kutumia ARV.

Alidai kwamba hata baadhi ya maofisa wa afya waliokuwa wakisimamia matibabu yake wilayani Babati walishangazwa na kupona kwake kwa tiba ya Mchungaji Mwasapila na hilo liliwafanya nao kufunga safari kuja Samunge Aprili 28, mwaka huu kupata kikombe.

"Ninavyo vyeti vinavyothibitisha kuwa sina tena Ukimwi na mwezi huu pia natarajia kupima kuona afya yangu ipo vipi," alisema Ally.
Endelea kusoma habari hii.....................
Best Blogger Tips
Mfugale bosi mpya TANROADS

WAZIRI wa Ujenzi John Magufuli amemteua, Patrick Mfugale, kuwa mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Ephraim Mrema.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyopatikana Dar es Salaam jana kisha kutiwa saini na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Herbert Mrango, kabla ya uteuzi huo Mfugale alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa uteuzi huo ni kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia Mei 20 mwaka huu. Mfugale amewahi kushika nafasi mbalimbali serikalini ikiwemo kusimamia ujenzi wa barabara na daraja la Mkapa.

Katika taarifa yake, katibu mkuu alieleza kuwa injinia huyo ana shahada ya uhandisi (BSc Civil Engeneering) kutoka Chuo Kikuu cha Roorkee nchini India na shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Loughborough, Uingereza.

Kabla ya uteuzi wake, alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Barabara nafasi aliyoenguliwa na Rais, siku chache kabla ya kuingia TANROADS. Desemba Mosi mwaka jana, Mfugale aliteuliwa kukaimu nafasi ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa TANROADS.

Sunday, May 22, 2011

Best Blogger Tips
Mali: Mabadiliko ya kura kombe la Dunia

Via BBC 

Rais wa Shirikisho la Soka la Mali Hammadoun Kolado Cisse ametaka mabadiliko yafanyike ya mfumo wa upigaji kura kutafuta nchi itakayoandaa Kombe la Dunia.

Pia amesema bado hajaamua nani atampigia kura katika uchaguzi unaokuja wa Rais wa Fifa.
Kauli hiyo ameitoa licha ya Shirikisho la Soka barani Afrika kueleza litamuunga mkono Rais wa sasa wa Fifa Sepp Blatter na sio mpinzani wake pekee Mohamed Bin Hammam.

"Kwa wakati huu siwezi kuzungumzia mgombea gani tutakayemuunga mkono," alisema Cisse.
Katika mkutano uliofanyika mjini Cairo siku ya Jumatatu, Shirikisho la Soka barani Afrika, lilisema kamati yake kuu imekuwa na kura ya siri na imepitisha muswda wa kumuunga mkono Blatter katika uchaguzi wa Fifa.

"Kamati kuu inaweza kutoa mapendekezo, lakini chama au shirikisho la soka la nchi huamua kivyake nani wa kumpigia kura," Cisse alifafanua.

"Hawapaswi kufuata mapendekezo ya kamati na baadhi ya nchi zinamuunga mkono Blatter na nyingine bin Hammam.

"Tunataka mabadiliko ya kweli ndani ya Fifa - namna tunavyofanya kazi, jinsi usimamizi wa fedha ulivyo - lakini siwezi kusema iwapo hicho ndio kigezo cha kubadilisha Rais."

Cisse anataka Mkutano Mkuu wa Fifa kuliko wajumbe 24 wa kamati ya utendaji kutoa uamuzi wa mwisho ni nchi gani ya kuandaa Kombe la Dunia.

Mchakato huo umezongwa na tuhuma za rushwa.

"Iwapo kila nchi itaweza kupiga kura kwa nchi itakayoandaa Kombe la Dunia, hiyo itasaidia sana kupunguza tuhuma za rushwa kwa sababu huwezi kuhonga vyama na mashirikisho 203 ya soka."

Cisse ameongeza kundi la nchi za Afrika litashauri mabadiliko haya kabla ya uchaguzi haujafanyika tarehe 1 mwezi wa Juni, lakini akakataa kusema iwapo nchi nyingine zitaunga mkono.

Pia amesema angefurahi mfumo wa wajumbe wa Kamati Kuu ya Fifa nao ungeangaliwa na kuwa na wajumbe zaidi ya wanne wa sasa kutoka nchi za Afrika.

Saturday, May 21, 2011

Best Blogger Tips
Mamia wamzika Sheikh Yahya


Via Tanzania Daima

MAELFU ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, wakiongozwa na viongozi wa serikali, dini, vyama vya siasa na makundi ya jamii jana walijitokeza kwenye mazishi ya mnajimu mashuhuri nchini na Afrika Mashariki ya Kati, Sheikh Yahya Hussein aliyefariki dunia juzi.
Sheikh Yahya Hussein (87), aliyefariki dunia juzi majira ya saa nne asubuhi, muda mfupi baada ya kufikishwa katika Hospitali ya Mtakatifu Ukombozi, Kinondoni baada ya kuugua ghafla alizikwa katika makaburi ya Tambaza.
Rais Jakaya Kikwete, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, Mufti, Sheikh Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Shaaban bin Simba, Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), la Ubungo Kibangu, Anthony Lusekelo, ni miongoni mwa viongozi waliokuwapo kwenye mazishi hayo yaliyowafanya wakazi wa jiji hilo kuacha shughuli zao kwa muda ili kushiriki.

Baadhi ya viongozi waliokuwapo nyumbani kwa marehemu Sheikh Yahya, Mwembe Chai eneo la Magomeni, walisema kuwa kifo chake ni pigo kubwa kwa Watanzania na hasa Jumuiya ya Waislamu kwa kuwa alikuwa mstari wa mbele kupigania haki za Waislamu.

Mchungaji Lusekelo, alisema kuwa kifo cha Sheikh Yahya ni pigo kubwa kwa Waislamu na hata watu wa dini nyingine kutokana na kuwa msuluhishi mkubwa ilipotokea kuna kutokuelewana kwa viongozi wa dini hizo au makundi mengine ya kijamii.

“Siku tatu nyuma niliota Sheikh Yahya amepandishwa daraja kubwa la uongozi… lakini siku iliyofuata nikasikia taarifa za kifo chake, nilimheshimu na kumpenda kutokana na hekima na busara zake wakati wa uhai wake na hata ulikuwa ukija kwa ajili ya kuomba ushauri hakusita kufanya hivyo kwa wakati.

“Yapo aliyoyafanya na kuwa mchango mkubwa wa nchi yetu, lakini kutokana na aliyoyafanya Mungu amuweke mahali panapostahili, tupo pamoja katika kuomboleza msiba wa Sheikh Yahya na subira ni jambo jema kwa wafiwa,” alisema
Endelea kusoma habari hii..................

Friday, May 20, 2011

Best Blogger Tips
Sheikh Yahya Hussein afariki dunia

MTABIRI maarufu ndani na nje ya Tanzania, Sheikh Yahya Hussein leo asubuhi amefariki kutokana na tatizo la ugonjwa wa moyo baada ya  kukimbizwa Hospitali ya Ukombozi, Kinondoni, jijini Dar es Salaam leo asubuhi na  ilipotimu saa tatu asubuhi alikataka roho akiwa hospitalini hapo. Kwa mujibu wa mtoto mkubwa wa marehemu aitwaye Hassan, baba yake atazikwa kesho saa saba mchana kwenye makaburi ya Tambaza jijini Dar es Salaam.

Sheikh Yahya ambaye wakati wa uhai wake alipata umaarufu mkubwa kutokana na kutabiri matukio makubwa katika maeneo mbalimbali duniani, alizaliwa wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani, mashariki mwa Tanzania mwaka 1932.

Alipata elimu yake ya awali katika shule ya Al Hassanain jijini Dar es Salaam, kabla ya kwenda visiwani Zanzibar ambako aliendelea na masomo katika chuo cha Muslim Academy.

Baada ya kuhitimu alikwenda nchini Misri alikopata elimu ya juu zaidi katika masuala ya dini ya Kiislam katika chuo kikuu cha Al Azhar kilichoko jijini Cairo.

Sheikh Yahya Hussein baadae alirejea nchini Tanzania mwanzoni mwa miaka ya sitini na kuanza shughuli zake za utabiri wa elimu ya nyota akiwa mtabiri wa mwanzo kabisa kueneza shughuli za utabiri wa nyota katika magazeti mbalimbali ya ukanda wa Afrika Mashariki.

Mnajimu huyo, amewahi kuendesha shughuli zake katika nchi za Afrika Mashariki na maeneo mengine duniani.

Pamoja na elimu yake ya unajimu, vile vile Sheikh Yahya Hussein alikuwa kiongozi wa dini ambaye pia alijihusisha na uchambuzi wa masuala ya siasa kupitia utabiri hususan wakati wa uchaguzi, ingawa hakushiriki kikamilifu katika kuwania nyadhifa zozote za kisiasa.

Pia alivuma sana katika kutabiri matokeo ya mechi kubwa za soka katika michuano ya Gossage na hata timu za Simba na Yanga za Tanzania bila kusahau vifo vya watu mashuhuri kama wanasiasa na wasanii pamoja na matukio makubwa duniani.

Marehemu Yahya Hussein ameacha mjane na watoto wapatao ishirini.

Thursday, May 19, 2011

Best Blogger Tips
Mkuu wa IFM Ajiuzuru kutoka wadhifa wake

Via BBC

Mkuu wa shirika la fedha duniani, Dominique Strauss Kahn amejiuzulu.

Taarifa hiyo ya kujiuzulu kwa Strauss Kahn imechapishwa katika wavuti wa shirika hilo.
Anasema amejiuzulu ili atumie muda uliobakia kujitea katika kesi inayomkabili ya kujaribu kumbaka mwanamke mmoja mjini New York.

Strauss Kahn ametuma taarifa yake kwa bodi ya shirika hilo. Amesema kuwa anakanusha mashtaka yote dhidi yake na amesikitishwa na kisa hicho kilichomkabili.

Shirika hilo limesema kuwa litatangaza hivi karibuni utaratibu wa kumteua mkurugenzi mpya. Kwa sasa John Lipsky ataendelea kuwa kaimu Mkurugenzi mkuu wa IMF.

Awali waziri wa fedha wa Marekani amesema kuwa mkuu wa shirika la fedha duniani (IMF), Dominique Strauss-Kahn, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya kujaribu kumbaka mhudumu wa hoteli, hawezi tena kuendesha shughuli za shirika hilo.

Timothy Geithner ametoa wito kwa IMF kumteua rasmi kaimu mkuu wa shirika hilo.
Bwana Strauss-Kahn anazuiliwa katika jela moja mjini New York baada ya kukamatwa hapo jumamosi kwa kosa la kujaribu kumbaka mhudumu wa hoteli moja.

Strauss-kahn ambaye amezuiliwa katika gereza la wafungwa sugu la Rikers Islands mjini New York yupo chini ya ulinzi mkali kuchunga asijiue. Hii ni baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu.

Wakili wa mwanamke huyo kutoka Guinea, Afrika Magharibi, anayemtuhumu Strauss-Kahn, amesema mteja wake amepata mshutuko ambao sio wakawaida.

Wakili huyo ameongeza kuwa kwa sasa yupo mafichoni na kwamba anajihisi ''Yuko pekee duniani''.

Strauss-Kahn, mwenye umri wa miaka 62, anakabiliwa na mashtaka saba dhidi yake na iwapo atapatikana na hatia, atahukumiwa kifungo cha hadi miaka 25 jela.
Best Blogger Tips
CCM Arusha kwachafuka

 HALI si shwari chama tawala mkoani Arusha mara baada ya gari la Katibu wa CCM hapa, Mary Chatanda kunusurika kuchomwa moto na baadhi ya wanachama wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM).Wanachama wa umoja huo kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Arusha waliandamana katika Jengo la Makao Makuu ya CCM Mkoa wa Arusha, wakishinikiza Chatanda pamoja na Mjumbe wa Baraza la Vijana mkoani Arusha, Mrisho Gambo "wajivue gamba".

Hali hiyo ilijitokeza jana katika jengo la makao makuu ya chama hicho wakati Kikao cha Kamati ya Siasa Mkoa kikiendelea ambapo, hali iliyosababisha dereva wa gari la katibu huyo wa CCM kulitoa nje ya jengo hilo na kisha kulikimbiza mahali kusikojulikana.

Vijana hao walikuwa wameshika mabango yenye ujumbe mbalimbali huku wakipaza sauti zilizokuwa zikimtaka Chatanda kuondoka katika nafasi yake ya uongozi kwa madai kwamba amekuwa akikivuruga CCM mkoani Arusha.

Wakizungumza na waandishi wa habari, wanachama hao kutoka wilaya za Monduli, Longido, Arusha, Arumeru, Karatu na Ngorongoro walisema pamoja na wao kutoa malalamiko mbalimbali juu ya Chatanda na Gambo, lakini uongozi wa CCM taifa umekuwa ukiwakumbatia viongozi hao na kudai sasa wamechoka.

Walisema malaliko yao kuwa Chatanda amekuwa akikivuruga chama chao ikiwa ni pamoja na kusababisha kukosa ushindi wa Jimbo la Arusha Mjini lililoenda kwa Chadema huku wakisema kwamba ikiwa atakataa kung'oka watajua cha kufanya.

“Hatumtaki Chatanda na hatumtaki Mrisho Gambo hawa watu kwanza ni wasaliti, lakini pia wamechangia sisi kushindwa kuchukua jimbo hili kwani walikuwa wanaiunga mkono Chadema tunataka waondoke mara moja hadi kieleweke,” ilisikika sauti ya mmoja wa vijana hao.

Miongoni mwa jumbe ambazo zilikuwa zimeandikwa kwenye mambango hayo ni "Chatanda umehujumu uchaguzi kwa siasa zako za makundi zilizojaa chuki, ubinafsi na ubabe usio na manufaa kwa Chama Cha Mapinduzi", "Chatanda kwa siasa zako za ubabe umetuchonganisha na viongozi wa dini”, na nyingine kadha wa kadha.

Hali hiyo ilisababisha Mwenyekiti wa UVCCM mkoani Arusha, James Ole Millya aliyekuwa kwenye kikao cha kamati ya siasa kutoka nje na kwenda ukumbini kuwatuliza wanachama hao, lakini juhudi zake ziligonga mwamba.

Akizungumza na wanachama hao, Milya aliwataka wapunguze jazba na kusema kuwa yeye ni mjumbe ametumwa kusikiliza madai yao hivyo wampatie na kisha taufikisha ujumbe huo.

“Jamani ninawaomba mtulie sidhani kama mtafanya fujo ninaomba mnipatie ujumbe mnitume niufikishe jamani nami nitaufikisha tulieni jamani,” alisema Milya

Hata hivyo, ushawishi wa Milya haukuzaa matunda na kuamua kurudi kikaoni kwani wanachama hao waliendelea kupaza sauti zao kwa wakidai kuwa wanamtaka katibu huyo aondolewe mkoani Arusha kwa kuwa amekuwa akiingilia uamuzi wa umoja wao na kuendelea kumkubatia Gambo.

“Mheshimiwa tunakipenda sana chama chetu na tunakuheshimu sana, tunaomba Chatanda aondoke la sivyo tutachoma gari lake, tukikutana nalo tutamondoa kwa nguvu,” alisema kwa jazba mmoja wa vijana hao.
Endelea kusoma habari hii......................

Sunday, May 15, 2011

Best Blogger Tips
Mkuu wa IMF ameshtakiwa New York


Polisi mjini New York wamemshtaki mkuu wa Shirika la Fedha Duniani, IMF, Dominique Strauss-Kahn, kwa kujaribu kumbaka mtu na kumzuwia.

Mashtaka hayo yanahusu msichana mfanyakazi wa hoteli chumbani alimokuwa akikaa Bwana Strauss-Kahn.

Wakili wake amesema atakanusha mashtaka hayo.

Bwana Strauss-Kahn, alikamatwa ndani ya ndege kabla ya kuondoka kuelekea Ulaya.

Dominique Strauss-Kahn, mkuu wa IMF, hivi sasa yuko kati-kati ya juhudi za kuziokoa nchi za Umoja wa Ulaya zenye matatizo ya fedha.

Mwaka wa 2008, alichunguzwa na bodi ya IMF, kuhusu uhusiano wake na mwanamke aliyekuwa piya mfanyakazi wa IMF.

Hakutolewa kazini, lakini iliamuliwa kuwa alionesha "ukosefu mkubwa wa busara".

Anakanusha tuhuma kuhusu tukio lilotokea jana mjini New York, lakini ni wazi kuwa tukio hilo litamuandama, na linaweza kuathiri imani ya watu juu yake katika majadiliano yoyote atayofanya.
Alikuwa yuko njiani kwenda Ujerumani, kukutana na Kansela Merkel.

Mada ya mazungumzo haikufichuliwa, lakini inajulikana kuwa hali ya uchumi wa Ugiriki imekuwa kwenye mawazo ya duru za kifedha.
Source: BBC

Monday, May 9, 2011

Best Blogger Tips
Waziri amfungia umeme mchungaji Mwasapila

Via Mwananchi

WAZIRI wa  Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, William Lukuvi, amebadili sura ya makazi ya Mchungaji  mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kulutheri  Tanzania(KKKT),  Ambikile Mwasapila kwa kumfungia umeme unaotumia mionzi ya jua.

Umeme huo, ulifungwa jana na kampuni ya  Ensol(t) Limited na hivyo kufanya makazi ya mchungaji huyo kuwa na umeme wa uhakika na hivyo kuboresha tiba yake kwa kuchemsha.

Kwa mujibu wa mafundi wa Kampuni ya Ensol, gharama za kufungwa kwa umeme huo ni zaidi ya Sh4  milioni  na fedha hizo zimetolewa na Lukuvi.

Waziri Lukuvi ambaye ni mmoja wa mawaziri wa kwanza kufika Samunge na kupata kikombe cha tiba, pia ndiye
alisaidia  kupunguza msongamano wa magari baada ya kuanzisha utaratibu wa kuingia Samunge kwa vibali.

Akizungumza na Mwananchi jana kwa niaba ya mchungaji Mwasapila, msaidizi wake, Fredrick Nsajile alisema, mchungaji ameshukuru sana kwa msaada huo wa Lukuvi.

"Mchungaji Mwasapila anashukuru kwa msaada huu mkubwa ambao utasaidia kuwapo kwa umeme wa ukakika na kwa wakati wote na hivyo kurahisisha  kazi ya kuchesha dawa,"alisema Nsajile.

Nsajile pia alitoa shukrani kwa msaada wa waziri wa nchi ofisi ya Makamu wa Rais, Dk Terezya Huvisa na serikali Mkoa wa Arusha, wa kumalizika kuezeka mabati nyumba mpya ya mchungaji Mwasapila.

"Tunatoa shukrani kwa wote wanaoendelea kutusaidia ili kuboreshwa huduma hapa Samunge, wapo wengi na mchungaji anawaombea maisha mema,"alisema Nsajile.

Saturday, May 7, 2011

Best Blogger Tips
Samunge wazuia helikopta kutua

Via Mwananchi

WAKAZI wa Kijiji cha Samunge jana walizuia helikopta zinazofika hapo kupeleka wagonjwa kupata tiba ya magonjwa sugu kutoka kwa Mchungaji Ambilikile Mwasapila kutua na kuwafukuza wakusanya ushuru wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro.

Kitendo hicho ni mwendelezo wa mvutano wa mapato yanayotokana na ushuru unaotozwa kwa helikopta, ndege na magari. Wakazi hao wanapinga halmashauri kukusanya ushuru wa Sh5,000 kwa kila magari na 150,000 kwa helikopta bila ya kupewa mgawo.

Kutokana na hali hiyo, jana Halmashauri ya Ngorongoro ililazimika kuomba msaada wa polisi na askari zaidi ya 20 walipelekwa kuwasimamia maofisa wa halmashauri kukusanya ushuru huo na kulinda uwanja wa ndege. Pia polisi  walimkamata Diwani wa Samunge, Jackson Sandea na kumhoji akidaiwa kuchochea mgogoro huo.

Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Ngorongoro, Dominick Lusasi amekuwa akisisitiza kuwa uamuzi wa kukusanya ushuru huo, ambao awali ulikuwa ukikusanywa na kijiji hicho, unatokana na kikao cha wakuu wa mikoa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi.

Halmashauri ya Ngorongoro ilianza kukusanya ushuru huo tangu April 6, mwaka huu na kila siku wastani wa  magari 800 yanapata huduma Samunge huku helikopta zikitua wastani wa sita.
Wiki iliyopita Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali aliagiza wakusanya ushuru wa kijiji kushirikiana na wale wa halmashauri lakini juzi wakusanya ushuru wa kijiji walisema hawakushirikishwa ipasavyo na fedha zote zinaendelea kupelekwa halmashauri na hakuna anayewalipa.

Kutokana na hali hiyo, wananchi hao juzi jioni waliitisha mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa Nane Nane kijijini hapo na kukubaliana kumwondoa  mkusanya ushuru wa halmashauri, Felix Jackson na kuyaruhusu magari kwenda kupata tiba bila kulipa ushuru kutokana na ofisa huyo kuwanyima kitabu.

Pia walitangaza kuanza kukusanya wenyewe fedha kuanzia jana huku, wakidhibiti uwanja wa helikopta na kukusanya wao wapato.Wakizungumza katika kikao hicho wanakijiji, David Richard na Tito Garaa walisema kitendo cha halmashauri kuchukua mapato yote na kuwaachia uchafu hakikubaliki.

"Mbona Kijiji cha Soitsambu wameanzisha ushuru wa Sh500 kwa magari kutoka Kenya na halmashauri haijakataza? Kwa nini mapato yetu sisi wang'ang'anie?" alisema Garaa.Akizungumzia kukamatwa kwake, Sandea alisema alitakiwa kutoa maelezo kuhusu mgogoro huo… “Sijui kosa langu ila wananiambia twende kuhojiwa."Sandea aliwahi kupeleka hoja kwenye Baraza la Madiwani akiomba Kijiji cha Samunge kipewe ruhusa ya kukusanya mapato ya ushuru.

Wananchi waandamana hadi kwa Babu

Wanakijiji jana waliandamana hadi kwa Mchungaji Mwasapila wakitaka kumweleza kwamba watavuruga utaratibu huo wa kutoa tiba kutokana na tatizo hilo la mapato. Hata hivyo, walishindwa kuzungumza naye kwani alikuwa akiendelea na kazi ya kugawa dawa. Walizungumza na Msaidizi wake, Fredrick Nisajile ambaye aliwaambia kwamba Mchungaji hahusiki na mgogoro huo wa mapato hivyo ni vyema suala hilo likafanyiwa kazi na halmashauri na serikali."Nimewaomba watulie kwani Mchungaji hahusiki mambo ya ushuru wa magari na helikopta yeye anatoa tiba," alisema Nsajile.

Wednesday, May 4, 2011

Best Blogger Tips
LA Lakers vs. Dallas

Via The Miami Herald

The Mavericks came to Staples Center this week having never beaten the Los Angeles Lakers in a road playoff game. Now they'll head back to Dallas with a 2-0 lead in their Western Conference semifinal series.

Dirk Nowitzki scored 24 points, as the Mavericks upended the Lakers, 93-81, putting a damper on a possible three-peat for Kobe Bryant and Co.

Coming off a 96-94 comeback win on Monday, the Mavs pulled another surprise on the Lakers Wednesday. J.J. Barea came off the bench to score eight of his 12 points in the final quarter. Shawn Marion contributed 14 points and nine rebounds in the win.

This is the first time the Lakers have lost the first two games of a playoff series at home since 1977 when Portland beat them in the Western Conference finals. The Blazers won the title that year.

Bryant scored 23, but the Lakers missed their first 15 three-point tries and ended 2-of-20 from beyond the arc. Andrew Bynum tallied 18 points and 13 rebounds, while Pau Gasol totaled 13 and 10 boards.

A frustrated Ron Artest, who had 11 points, was ejected in the game's final minute after clothes-lining Barea with a hit to the head.

Game 3 of the best-of-seven set is Friday in Dallas.
Best Blogger Tips
Picha ya Osama haichapishwi

Via BBC

Rais Barack Obama ameamua kuwa picha za Osama Bin Laden, aliyeuwawa siku ya jumatatu, zisichapishwe.

Maafisa wa Marekani wamekuwa wakijadili iwapo wachapishe picha za mwili wa Bin Laden kukabili habari za uongo kuwa hakuuawa.

Lakini Bw Obama anaamini kuwa picha hizo huenda zikazua hisia kali akisema, '' sisi hatutaki kuonyesha picha hizi kama kikombe cha kujivunia cha kumwonyesha kila mtu."

Kiongozi huyo wa al- Qaeda alipigwa risasi katika uvamizi jumatatu iliyopita na vikozi maalum vya Marekani, Kaskazini mwa Pakistan.

Mwandishi wa BBC mjini Washington amesema kuwa rais Obama ameamua wazi kuwa kutoa picha hizo hazina thamani yeyote kwani huenda ikatishia maisha ya raia.

Bw Obama amefichua uamuzi huo wakati wa mahojiano na kituo cha televisheni cha CBS.
Uamuzi huo ulifikiwa wakati maafisa wa Marekani walianza kuchunguza habari kwenye kompyuta, simu za rununu na vifaa vingine vya kuhifadhi habari ambavyo vilipatikana wakati wa uvamizi huo katika eneo la Abbottabad, ambapo Bin Laden alikuwa amejificha.

Mwanasheria mkuu wa Marekani Eric Holder amesema serikali hiyo inatarajia kuongeza majina mengine kwenye orodha ya magaidi wanaotakikana na Marekani, kufuatia habari walizopata katika nyumba ya Bin Laden.

Laini mbili za simu na euro 500 ($745; £450) zilipatikana zime shonelewa kwenye nguo ya Bin Laden, kana kwamba angehitajika kutoroka kwa haraka.

Wakosoaji wameelezea wasiwasi wao kuhusu uhalali wa oparesheni hiyo, baada ya Marekani kubadilisha maelezo kuhusiana na kuuwawa wa Bin Laden akiwa ajajihami kwa silaha.

Sunday, May 1, 2011

Best Blogger Tips
Osama Bin Laden auwawa

Via BBC

Rais Barack Obama ametangaza kwamba wanajeshi wa Marekani wamemuua kiongozi wa mtandao wa Al Qaeda Osama BIn Laden. Obama amesema kundi la wanajeshi wachache wa Marekani walifanya operesheni iliyomlenga BinLaden katika eneo moja nchini Pakistan ambapo pia wamechukua maiti yake.

Wanajeshi wa Marekani wamekuwa wakimsaka Osama Bin Laden tangu kabla ya Mashambulizi ya Marekani ya Septemba 11, 2001 katika jengo la World Trade Centre na makao makuu ya kijeshi nchini humo, Petangon, na kuwaua zaidi ya watu 3,000.

Wasifu wa Osama Bin Laden

Osama bin Laden alizawa mwaka wa 1957, katika familia ya kitajiri nchini Saudi Arabia. Ana zaidi ya mandugu na dada 50. Babake Osama alimiliki kampuni kubwa ya ujenzi. Katika baadhi ya picha zake za utotoni, Osama ameonyeshwa akiwa na mavazi ya kifahari na ghali, akiwa likizoni katika miji mbali mbali barani Uropa.

Hata hivyo mwanzoni mwa miaka ya themaninialiyupia mgongo maisha haya ya starehe na kitajiri, ana kujiunga na vugu vugu la kupigania haki dhidi ya utawala wa kisovieti baada ya majeshi yake kuishambulia Afghanistan.

Na hapo akipigana pamoja na waarabu wenzake, ndipo alizindua kundi la kigaidi la Al qaeda. Mnamo mwaka wa 1998, alitangaza fatwa yaani vita vikali vya kidini dhidi ya Marekani. Kufuatia ghadhabu aliyokuwa nayo na Marekani, kwa kuweka majeshi yake katika ardhi ya kiislamu, katika nchi mbali mbali mashariki ya kati.

Alioa mke wake wa kwanza akiwa na miaka 17, na baadaye akawaoa ya wake wengine wanne. Osama Bin Laden naaminiwa kuwa na watoto 17.




Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits