Thursday, March 31, 2011

Best Blogger Tips
Magufuri apelesha sh1bn Loliondo


WAZIRI wa Ujenzi, Dk John Magufuli, jana aliingia katika Kijijini Samunge kwa mchungaji Ambilikile Masapila na kupata kikombe cha dawa, kisha kutangaza neema ya kujengwa kwa barabara kuu inayoingia kijijini hapo.

Magufuli aliuambia umati wa watu uliokuwa ukisubiri zamu yao kunywa dawa kuwa, Serikali itatumia Sh1.05 bilioni kwa ajili kutengenenza barabara hiyo ili iweze kupitika wakati wote kwa lengo la kuwarahisishia usafiri wanaokwenda kunywa dawa kwa Babu Masapila.

Barabara inayoingia katika kijiji hicho ambacho kimeshuhudia maelfu ya magari yakiingia kila siku tofauti na ilivyokuwa awali, ipo katika hali mbaya kiasi cha baadhi ya maneo kutoruhusu magari kupishana.

Kwa mujibu wa Magufuli, Serikali ilikwishatoa Sh500/-milioni kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kuanzia Mto wa Mbu eneo la Kigongoni, Ngaresero, Samunge hadi kuungana na barabara ya kutoka mkoani Mara.

Dk Magufuli alisema jana ndio aliuagiza uongozi wa Wakala wa Barabara nchini (Tanroads) Makao Makuu kutuma Sh500 milioni ili kuharakisha ujenzi huo.

"Tayari fedha hizo zimeshatumwa Tanroads mkoani Arusha na Meneja wa Mkoa, Kakoko (Deodatus), niko naye hapa hivyo kazi itakwenda haraka ili watu wanaokuja kwa mchungaji kunywa dawa wasiendelee kuteseka," alisema Dk Magufuli huku akishangiliwa na mamia ya watu waliokuwa wakimsikiliza.

Waziri pia huyo alisema kwa mamlaka aliyonayo, atawasiliana na uongozi wa Mfuko wa Barabara ili utume fedha za dharura kiasi cha Sh50 milioni kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorogoro kwa ajili ya kufanya matenegenezo mengine ya barabara, wilayani humo.

Alisema fedha zilizotengwa kwa ajilii ya barabara za nchi nzima kupitia mfuko huo zinafikia Sh286 bilioni katika bajeti ya mwaka 2010/11, na kwamba upo uwezekano mkubwa wa fedha za dharura kupatikana kwa ajili ya matenegenezo ya barabara ya Samunge.
 Endelea kusoma habari hii.....................

Wednesday, March 30, 2011

Best Blogger Tips
Sadaka ya Babu yafikia mil. 50/-

*Yeye kupata mi. 10/-, kanisa, wasaidizi mi. 20/- kila mmoja
*Kanisa kujenga jengo la huduma la kukaa watu  700 kwa pamoja
*Wanasayansi Kenya wathibitisha dawa yake kutibu maradhi mengi

Via Majira

KANISA la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati limetangaza kiwango cha
fedha ambazo kimekusanywa kutoka kwa wagonjwa wanaokunywa kikombe cha dawa ya Mchungaji Ambilikile Masapila kuwa ni sh milioni 50.

Akitangaza fedha hizo jana, Askofu wa kanisa hilo, Thomas Laizer alisema fedha hizo zimepatikana tangu kuanza kwa tiba hiyo mwishoni mwa mwaka jana, kutokana na mchango wa sh. 500 kwa kila mgonjwa.

Kutokana na mgao wa fedha hizo kama alivyosema Babu ni kuwa yeye anabaki na sh 100 huku sh 200 zikienda kanisani na 200 kwa wasaidizi wake, yeye atapata sh milioni 10. Kanisa sh. milioni 20 na wasaidizi wake sh milioni 20.

Wakati huo huo, Kanisa hilo limekamilisha mipango ya ujenzi wa banda kwa ajili ya tiba ya Mchungaji Ambilikile Masapila ‘Babu’ kijijini Samunge litakalogharimu sh. milioni 100 ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mapendekezo ya mchungaji huyo.

Jengo hilo litakalohudumia watu 700 kwa wakati moja litakua la mviringo na litajengwa karibu kabisa na babu anakotolea tiba hiyo hivi sasa ambapo kutakuwa na viti vya watu zaidi ya 300, eneo la kutolea dawa, kuchemshia dawa hizo na sehemu ya kuhifadhia hiyo dawa.

Askofu Laiser alisema jana kuwa uamuzi huo umekuja wakati ambao idadi kubwa ya watu wanateseka kumfikia mchungaji huo kwa kuwa katika jua kali, na wakati mwingine mvua wakisubiria tiba.
Endelea kusoma habari hii........................



,
Best Blogger Tips
Rushwa Loliondo

Via Newhabari

MDUDU rushwa tayari ameingia kwenye utaratibu wa kuruhusu magari yenye watu wanaokwenda kunywa dawa kwa Mchungaji mstaafu Ambilikile Masapila, katika Kijiji cha Samunge, Loliondo mkoani Arusha.


Mamia ya magari yaliyokuwa yamezuiwa juzi katika maeneo ya Meserani, Makuyuni na Mto wa Mbu, yaliruhusiwa kwenda Samunge baada ya madereva kutoa rushwa. Polisi walio kwenye vizuizi ndio watuhumiwa wakuu wa vitendo hivyo.

Kuzuiwa kwa magari hayo hadi Aprili Mosi ilikuwa ni utekelezaji wa ombi la Mchungaji Masapila kwa Serikali la kuzuia magari zaidi kuingia Samunge hadi wale waliopo watakapokuwa wameshapata dawa na kuondoka.

Mamia ya magari juzi yalizuiwa katika vituo vya Mesereni, Makuyuni na Mto wa Mbu wilayani Monduli. Yote yalikuwa na idadi kubwa ya watu.

Baadhi ya watu waliozungumza na MTANZANIA wamesema kuwa magari hayo yalianza kuruhusiwa baada ya wahusika kutoa rushwa.

Vitendo hivyo vilianza muda mfupi baada ya Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, kuondoka katika Kijiji cha Mto wa Mbu.

“Baada ya Makamu wa Rais kupita, polisi na viongozi waliyokuwa wakidhibiti magari walifungua mradi wa kukusanya pesa na kuyaruhusu yote kwenda Loliondo, hawakuwa na wasiwasi katika kukusanya pesa hizo,” alisema mmoja wa watu walioshuhudia tukio hilo.

Jana kwenye vituo vyote vitatu hapakuwapo askari wala magari yaliyozuiwa kwenda Samunge.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye, hakupatikana kuzungumzia suala hilo baada ya simu yake kutopokewa.
Endelea kusoma habari hii...................

Sunday, March 27, 2011

Best Blogger Tips
Adaiwa kumbaka mtoto wa mkewe

Via HabariLeo

POLISI mkoani Tabora wamemkamata mkazi wa Kijiji cha Mtakuja, Amos Gambo kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa kike wa mkewe mwenye umri wa miaka minane.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Liberatus Barlow, alisema, Gambo ambaye alitoweka tangu mwezi uliopita baada ya kudaiwa kufanya kitendo hicho, alitiwa mbaroni jana jioni.

Barlow alisema, mtuhumiwa alikamatwa kijijini hapo baada ya kumpigia simu mkewe (jina limehifadhiwa) akimlalamikia kuwa anakunywa pombe.

Kwa mujibu wa Kamanda Barlow, ndugu waliokuwepo walibaini kwamba mtuhumiwa huyo alipiga simu hiyo akiwa kijijini hapo na si nje ya Kijiji cha Mtakuja, kilichopo Manispaa ya Tabora.

Kamanda alisema, baada ya polisi kupata taarifa hiyo kutoka kwa mama wa mtoto aliyebakwa, walijaribu kumpigia simu na hatimaye kumtia mbaroni na kumfikisha kituoni.

Alisema mtuhumiwa atafikishwa mahakamani mara baada ya mahojiano ya wapelelezi wa kesi hiyo kukamilika.

Mtuhumiwa huyo anadaiwa kutenda kitendo hicho mwezi uliopita baada ya mama wa mtoto huyo kuondoka nyumbani kwenda kulala msibani kwa majirani.

Mama aliporejea alimkuta binti yake akiwa katika hali mbaya na alipomchunguza, alibaini kwamba alikuwa amebakwa .

 

Friday, March 25, 2011

Best Blogger Tips
Msiba Tanzania

Kwa mara nyingine Tanzania imepata pigo kwa upande wa fani ya muziki ambapo wasanii kumi na watatu wa muziki wa taarabu wa bendi ya Five stars Modern Taarabu, wamefariki dunia katika ajali ya barabarani iliyotokea katika kijiji cha Doma, mkoani Morogoro takriban kilomita mia tatu magharibi mwa mji wa Dar es Salaam.

Mwandishi wa BBC kutoka Dar es Salaam, John Sololmbi aliweza kuzungumza na mama mzazi wa marehemu Issa Ali almaarufu Kijoti aitwaye Amina Mahmoud na pia mama yake mdogo marehemu Sophia Said.

Thursday, March 24, 2011

Best Blogger Tips
Historia ya Ghadaffi


Kanali Muammar Gaddafi ni kiongozi aliyekaa madarakani kwa muda mrefu zaidi barani Afrika na katika nchi za Kiarabu.

Ameongoza Libya tangu alipompindua Mfalme Idris I, katika mapinduzi yasiyo ya kumwaga damu, wakati huo akiwa na umri wa miaka 27.

Maarufu kwa nguo anazopenda kuvaa, na walinzi wa kike wenye kubeba silaha, kiongozi huyo wa Libya pia anadhaniwa kuwa na mbinu nzuri za kisiasa, kwa kuweza kuirejesha Libya kutokana na kutengwa kidiplomasia duniani.

Baada ya miongo miwili ya kutengwa katika jamii ya kimataifa, mwaka 2003, Tripoli ilikiri kuwa walifanya shambulio la Lockerbie kwa kuiangamiza kwa mabomu ndege ya Pam Am na hapo Umoja wa Mataifa ukaondoa vikwazo dhidi ya Libya.

Baada ya miezi kadhaa, serikali ya Kanali Gaddafi ilisitisha mipango yake ya kuunda silaha za maangamizi na hii ikarejesha ushirikiano na nchi za magharibi.

Hapo ndipo mabadiliko halisi yalionekana kwa kuwa nchi hizo za magharibi zilibadili mtazamo wao na kuacha kumtenga Gaddafi na kushirikiana naye hata kama alikuwa hatabiriki.

Ni mtu wa kipekee katika kauli zake, mienendo yake, tabia zake na mikakati yake, kwa mujibu wa Saas Djebbar mtaalam wa siasa za Libya.

'Lakini ni mwanasiasa mashuhuri; hakuna shaka lolote kuhusu hilo. Ni mwanasiasa anayeweza kuhimili misukosuko ya kisiasa kwa hali ya juu sana.'
Endelea kusoma habari hii...................

Monday, March 21, 2011

Best Blogger Tips
Rockets Assign Thabeet to Rio Grande Valley Vipers

Houston Rockets center Hasheem Thabeet was assigned to the Rio Grande Valley Vipers, the Rockets’ NBA Development League affiliate, it was announced today. The assignment marks the 48th time in the 2010-11 season an NBA player has been assigned to an NBA D-League affiliate, and it is the second assignment for Thabeet, a second-year pro out of Connecticut.

Thabeet, the No. 2 overall selection in the 2009 NBA Draft, is the 34th NBA player to be assigned to the NBA D-League this season, which is an all-time high. The Memphis Grizzlies, who drafted Thabeet, assigned him to the Dakota Wizards last season, where he averaged 13.8 points, 11.2 rebounds and 3.8 blocks in six games.

Thabeet (7-3, 263) has appeared in 115 career NBA games, averaging 2.3 points and 2.8 rebounds in 10.9 minutes. As a rookie with Memphis last season, Thabeet led the NBA in blocks per 48 minutes with 4.84 (min. 60 games). He also averaged 11.4 points, 8.6 rebounds and 2.8 blocks in five games with Memphis’ 2010 NBA Summer League team. Thabeet has appeared in two games with Houston since joining the Rockets via trade on Feb. 24.

The first Tanzanian-born NBA player, Thabeet played three collegiate seasons at Connecticut, averaging 10.3 points, 8.5 rebounds and 4.17 blocks in 100 games. Thabeet led the Big East in blocks all three seasons, and his 4.17 average ranks 11th in NCAA history. Thabeet was an AP All-America Second Team selection and the Big East Co-Player of the Year in 2008-09. He was also named the Big East Defensive Player of the Year and National Defensive Player of the Year by the National Association of Basketball Coaches in both his sophomore and junior seasons.

Thabeet joins the Vipers for the team’s home game tonight against the Idaho Stampede. Rockets fans can keep track of Thabeet and the Vipers by logging onto NBA.com/dleague to watch every game live, online, for free.

The NBA Development League, founded in 2001, is the NBA’s official minor league. Featuring 16 teams with direct affiliations to NBA franchises, the NBA D-League is a proven developer of talent: 20 percent of players in the NBA at the conclusion of the 2009-10 season boasted NBA D-League experience, and the league continues to develop coaches, referees, and front-office staff for the NBA and its teams. In fostering the league’s connection to the community, its teams, players and staff promote health and wellness, support local needs and interests, and assist in educational development through NBA D-League Cares programs. The NBA D-League also advances the game of basketball as the research and development arm of the NBA. Throughout the league’s 10th season, fans can watch all NBA D-League games on NBA FUTURECAST, the free live Web-streaming initiative found at nba.com/futurecast.
Source: NBA D-League

Sunday, March 20, 2011

Best Blogger Tips
Makazi ya kanali Gaddafi yashambuliwa


Ndege zake za kijeshi, zimeshambulia makaazi ya Kanali Gaddafi mjini Tripoli na kusababisha uharibifu mkubwa kwenye jengo moja.

Viongozi wa muugano wa majeshi hayo wanasema jengo lililoharibiwa lilikuwa linatumika kuamrisha majeshi ya Libya yanayopigana na waasi.

Waandishi wa habari wametembezwa kwenye eneo hilo lakini hakuna taarifa ikiwa maafa yalitokea baada ya shambulizi hilo.

Naibu mkuu wa jeshi la wanamaji wa marekani Bill Gortney anasema mashubulizi hayo hayaja mlenga kanali Gaddafi.

Televisheni ya Libya imeonesha maiti na magari ya kijeshi yaliyoteketea kwenye barabara ya kuelekea mji wa Benghazi, shina la wapinzani wa serikali.

Msemaji wa serikali ameeleza kuwa watu 64 wameuwawa katika mashambulio yaliyofanywa na mataifa ya magharibi, lakini hakuna njia ya kuthibitisha taarifa hiyo.

Awali afisa mkuu wa jeshi la Marekani, , Mike Mullen, alisema ndege kutoka Qatar zinapelekwa huko, kuwa tayari kushiriki katika operesheni dhidi ya Libya, na nchi nyengine piya zimetoa ahadi kusaidia.

Adimeri Mullen alieleza kuwa agizo la Umoja wa Mataifa, la kuzuwia ndege za serikali kuruka katika anga ya Libya, sasa limetekelezwa, na majeshi ya Kanali Gaddafi, katika mji wa Benghazi, unaodhibitiwa na wapinzani, sasa hayawezi kusonga mbele.

Alisema hakuona taarifa, kuwa raia wameuwawa.

Urusi imetoa wito kwa Uingereza, Ufaransa na Marekani, ziache kushambulia maeneo yasiyokuwa ya kijeshi, na kwamba raia wameshambuliwa.

Mkuu wa Jumuiya ya Kiarabu, Amr Moussa, amesema mashambulio yamekwenda mbali, kushinda lile lengo la kulinda tu anga ya Libya, ambavyo ndivo jumuiya yake ilivotaka.
Source: BBC

Saturday, March 19, 2011

Best Blogger Tips
Mataifa yajadili hatua dhidi ya Libya

Mataifa yaliyoahidi kutekeleza azimio la Umoja wa Mataifa, linalokataza ndege kuruka katika anga ya Libya, yanakutana mjini Paris, kujadili hatua ya kuchukua.

Viongozi wa Ufaransa, Ungereza na Marekani, wamejumuika na nchi za Jumuiya ya Kiarabu, pamoja na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon.

Huku ndege za kijeshi zinapelekwa eneo la Mediterranean, Kanali Gaddafi, ameonya Mataifa ya Magharibi, yatajuta, endapo yataingilia kati.

Taarifa yake imesema, azimio la Umoja wa Mataifa, linatoa idhini ya kuingilia kati kijeshi, sio halali.
Mwakilishi wa Ufaransa katika Umoja wa Mataifa, amesema, anatarajia hatua za kijeshi, zitaanza katika saa chache baada ya mkutano huo wa Paris.
Source: BBC

Tuesday, March 15, 2011

Best Blogger Tips
Orijino komedi na Babu wa Loliondo

Best Blogger Tips
Lowasa apata kikombe Loliondo

Via Mwananchi

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa juzi alipata tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwasapile katika Kijiji cha Samunge, Tarafa ya Sale, Loliondo, mkoani Arusha.

Lowassa alifika katika eneo hilo mchana akiwa na viongozi kadhaa wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na Serikali kisha kupata kikombe kimoja chenye dawa kinachotolewa na mchungaji huyo kwa ajili ya tiba.

Tofauti na viongozi wengine, Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM), Jimbo linalopakana na Kijiji cha Samunge, alikwenda huko akiwa na viongozi mbalimbali wakiwamo viongozi wa dini na baadhi ya wapigakura wake.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Lowassa alithibitisha kwenda Loliondo na kuwataja viongozi wa dini alioambatana nao katika msafara wake kuwa ni Askofu Msaidizi wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini, Dk Frederick Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Dayosisi ya Kaskazini Kati (Arusha), Mchungaji John Nangole.

Katika ramani ya utendaji kazi ya KKKT, Jimbo la Masai Kaskazini ndipo kilipo Kijiji cha Samunge ambako ni makazi ya Mchungaji Mwasapile.“Ni kweli, nimekwenda pale na wapigakura wangu pamoja na viongozi wa dini, Msaidizi wa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Dk Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Mchungaji Nangole,” alisema Lowassa na kuuliza: “Kwani hiyo nayo ni habari jamani?”
Baada ya Lowassa kufika katika kijiji hicho akiwa na ujumbe wake, aliongoza moja kwa moja hadi kwa Mchungaji Mwasapile na kuzungumza naye kisha akapata kikombe cha tiba na kuondoka.

Kabla ya Lowassa kwenda kupata tiba, amekuwa akitoa msaada wa nauli kwa wagonjwa mbalimbali wa jimbo lake kwenda kwa mchungaji huyo ambaye dawa yake inadaiwa kutibu magonjwa ya saratani, kisukari, pumu, shinikizo la damu na Ukimwi.Lowassa ni miongoni mwa wanasiasa maarufu nchini ambao wameshafika kwa mchungaji huyo kupata tiba hiyo wakiwamo mawaziri, naibu mawaziri, wabunge, wakuu wa mikoa na wilaya.

Katika jitihada za kudhibiti usalama na kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma kwa mchungaji huyo bila matatizo, Serikali imeimarisha ulinzi kwa kuweka askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), katika kijiji hicho na kusimamia magari. Pia imepeleka wauguzi kusaidia wagonjwa mahututi kabla ya kumfikia mchungaji na imetoa pia jenereta kwa ajili ya kufua umemeKaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Raymond Mushi alisema jana kuwa, sasa walau hali ni nzuri kwani msongamano umepungua.

"Ni kweli sasa hali inaridhisha na jana watu wamekwenda kupata tiba na kurejea makwao mapema hili ndilo serikali inalolitaka. Tunaomba watu wanaopeleka wagonjwa wawe wanauliza kwanza hali ya msongamano," alisema Mushi.Mushi alisema inawezekana watu wanaokwenda katika kijiji hicho kusubiriana katika Mji wa Mto wa Mbu ambako kuna huduma nyingi muhimu kuliko wote kwenda huko kwa wakati mmoja.
Endelea kusoma habari hii.............................

Monday, March 14, 2011

Best Blogger Tips
TOP-PAID U.S GOVERNMENT JOBS 

The 10 highest paid government jobs

Working for the government is often referred to as public service. The term implies sacrifice or taking less than what could be earned in the private sector or in an entrepreneurial position. Many government workers seem overpaid but are probably underpaid when you consider the scope of their responsibilities. Indeed, many in the private sector would not want to stand up to the scrutiny required of a top public service job or to get elected to public office.

The salary of the President of the United States is actually a token sum considering the responsibilities of the office. Still, officials in other public service jobs seem egregiously overpaid. People who hold these jobs are "set for life" after their public service ends because they are in demand for paid speaking gigs, memoirs and consulting roles in private industry.

24/7 Wall Street has gathered data from many public sources to ferret out how much these top government officials earn. Salaries of some jobs are shielded from public scrutiny because of national security reasons. We did not consider the healthcare and retirement packages, security and transportation benefits and more. In some cases, our public service executives have actually taken considerable pay cuts to serve.

One thing also needs to be considered here. Some government salaries are actually shielded under executive order. Some of the shielded pay grades may be well into the hundreds of thousands or even more. Some information, intelligence, and cloak and dagger positions are shielded and above our pay grade when it comes to identifying how much they are.

10. Secretary of State: Hillary Clinton

Annual Base Salary: $186,600
Maximum Job Length: Generally 8 Years
Previous Job: Senator From New York

Job Description: The Secretary of State is appointed by the president to serve as chief diplomatic representative of the U.S. Besides overseeing all State Department operations, including the operations of the U.S. embassies and representation in the UN, Secretary of State Clinton is responsible for the foreign operations of the CIA, the Defense Department, and the Department of Homeland Security. Clinton is also fourth in the chain of succession for presidency.

9. Secretary of Treasury Timothy Geithner

Annual Base Salary: $191,300
Maximum Job Length: Generally 8 years
Previous Job: President of the Federal Reserve Bank of New York

Job Description: Appointed by the President, the Secretary of the Treasury serves as the principal economic advisor for the President. According to the Department of the Treasury: "The Secretary is responsible for formulating and recommending domestic and international financial, economic, and tax policy, participating in the formulation of broad fiscal policies that have general significance for the economy, and managing the public debt." Geithner is a proxy for many other presidential cabinet members, who make the same amount, including Secretary of Homeland Security Janet Napolitano.
Access the full story.........................

Sunday, March 13, 2011

Best Blogger Tips
10,000 wahofiwa kufariki dunia Japan

Juhudi za ukombozi zinaendelea Japan na katika eneo moja lilopigwa na tsunami, inahofiwa watu kama elfu kumi wamekufa.

Wakuu wa Japani wameonya kwamba kunaweza kutokea mripuko mwingine kwenye kinu cha nishati cha nyuklia kaskazini mwa mji wa Tokyo wakijaribu kuzuwia tanuri ndani ya kinu kuripuka.

Wamekiri kuwa miyale ya nyuklia karibu na kinu hicho kilioko Fukushima wakati mmoja ilizidi kiwango kinachofikiriwa kuwa salama baada ya kinu hicho kuharibika katika tetemeko kubwa lilotokea Ijumaa.

Wahandisi wamejaribu na kushindwa kupooza tanuri katika kinu kimoja kwa kutumia maji ya chumvi.

Lakini wanafikiri pipa linalofunika tanuri ni imara na litahimili mripuko kwa hivyo miyale haitovuja.

Jana kulitokea mripuko mkubwa kwenye kinu kimoja cha Fukushima.
Source: BBC

Saturday, March 12, 2011

Best Blogger Tips
Serikali yanywea kwa Mchungaji Loliondo

SERIKALI imebadili msimamo wake wa kusitisha kwa muda huduma ya tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Ambilikile Mwasapile katika Kijiji cha Samunge, Loliondo na badala yake imeunda tume itakayoshirikiana na mchungaji kumwezesha kufanya kazi yake kwa ufanisi zaidi.Juzi, Serikali kupitia kwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Haji Mponda ilimwagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha kusitisha kwa muda utoaji wa huduma hiyo hadi itakapojiridhisha kwamba dawa inakidhi ubora na inatolewa katika mazingira safi.

Hatua hiyo ilipingwa vikali na wananchi, viongozi wa dini na hata Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha,  Raymund Mushi ambaye alisema utekelezaji wake utakuwa mgumu kutokana na hali halisi na mazingira yaliyopo katika eneo hilo kwa sasa.Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi alisema Serikali haina tena mpango wa kuzuia huduma hiyo kwa kuwa inahusisha imani za watu.

“Serikali haina mpango wa kuzuia huduma hiyo na badala yake imeunda kamati itakayofanya kazi kwa kushirikiana na mchungaji huyo ili kuhakikisha jamii inapata huduma hiyo kwa utaratibu unaostahili,” alisema Lukuvi.Alisema kamati hiyo inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambayo imeanza kazi jana imezuia magari yote yanayokwenda kijijini hapo ili kutoa nafasi kwa Mchungaji Mwasapile kuhudumia wagonjwa waliopo hadi idadi yao itakapopungua.

Alisema kazi ya tume kwa sasa itakuwa kuratibu na kupanga idadi inayotakiwa kufika na kutibiwa kwa mchungaji huyo ili kupunguza msongamano na uwezekano wa kutokea kwa matatizo mengine.“Nimeambiwa hadi sasa katika kijiji hicho kuna magari zaidi ya 800 na watu wanakadiriwa kufikia 6,000. Idadi hii ni kubwa na serikali haiwezi kuacha suala hilo likabaki hivi lilivyo. Tumeunda kamati itakayofanya kazi ya kuratibu idadi ya watu watakaotakiwa kufika katika kijiji hicho,” alisema Lukuvi.

Alisema pamoja na kuunda kamati itakayoshirikiana na mchungaji huyo, pia serikali inaandaa utaratibu wa kupeleka gari la kubebea wagonjwa (ambulance) kijijini humo ili kutoa msaada wa haraka kwa watu watakaohitaji huduma hiyo.Alisema sambamba na hilo, serikali itatuma idadi ndogo ya wauguzi ambao watasaidia kutoa huduma kwa watu watakaohitaji ambazo zitakuwa nje ya zile zinazotolewa na Mchungaji Mwasapile.
Waziri huyo aliziomba taasisi nyingine zikiwamo Msalaba Mwekundu kutoa msaada wa mahema kwa watu waliopo katika eneo hilo.

Alisema maofisa wa Serikali waliokwenda katika kijiji hicho kufanya utafiti juu ya dawa hiyo walipata ushirikiano mzuri kutoka kwa mchungaji huyo...
“Maofisa wetu wamekwenda na wamepewa ushirikano mkubwa ukiwamo wa kuonyeshwa namna dawa inavyochimbwa, inavyochemshwa na mti unaotoa dawa hiyo. Sasa kazi wanayofanya ni kutafiti na baada ya hapo watatoa majibu ya kitaalamu kuhusu dawa hiyo.”Alisema baada ya kuondoka kwa wataalamu hao serikali pia imepeleka wengine ambao wanafanya kazi ya kufanya taratibu za kumsajili.

Wananchi wachangia
Wananchi na baadhi ya wamiliki wa kampuni binafsi wameanza kutoa misaada ya mahema na nguvukazi ili kuboresha huduma zinazolalamikiwa kuwa ndizo zinazokwamisha utoaji wa tiba.Magari mawili ya mizigo yakiwa yamesheheni mahema, magodoro, maji ya kunywa, mikate na viti yameonekana katika eneo la barabara kuu ya kuelekea Sonjo katika eneo la Engaruka. Mmoja wa madereva wa magari hayo alisema msaada huo umetolewa na Masista kutoka Parokia ya Kanisa Katoliki, Wilaya ya Karatu.Alisema misaada hiyo itapelekwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro ili uwe mchango wao katika kuboresha huduma za malazi na mlo kwa wagonjwa, hasa kwa wale wa kipato cha chini.

Kauli ya Mchungaji
Mchungaji Mwasapila baada ya kusikia tetesi zilizozagaa jana kwamba serikali ina mpango wa kusitisha huduma zake, aliwaambia waandishi wa habari kuwa suala la kuzuiwa utoaji wa dawa linahitaji muda kwa kuwa linagusa imani ya watu pia."Nitakuwa siwatendei haki hawa maelfu ya watu waliopo hapa labda wakiisha tunaweza kujua la kufanya," alisema Mchungaji Mwasapila na kuongeza kuwa hawezi kuwazuia wagonjwa ambao wanaendelea kufika kwake.

RC Arusha
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Raymond Mushi alisema jana kuwa ofisi yake inawasiliana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kujua ni jinsi gani ya kukabiliana na hali ya Loliondo.Alisema serikali mkoani Arusha inaendelea kuhakikisha hali ya usalama na afya za watu zinakuwa bora kwani tayari vyoo vimechimbwa ili kuzuia magonjwa na pia ulinzi umeimarishwa.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye akizungumza na Mwananchi jana alisema wameongeza askari kulinda usalama katika kijiji hicho lakini imekuwa vigumu kuzuia watu kwenda.
"Sisi tunalinda usalama hatuzuii watu kwenda kwa sasa kwani bado taratibu zinapangwa na sasa hali ni nzuri," alisema Andengenye.Bado mamia ya watu kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi wanaendelea kumiminika katika kijiji hicho kupata dawa. Waliopata huduma hiyo jana ni wagonjwa waliokaa siku tatu katika kijiji hicho.

Viongozi wengine wa dini
Viongozi wa dini na siasa wameendelea kujitokeza kuitaka serikali imruhusu mchungaji huyo aendelee na tiba zake wakati huu ambao bado uchunguzi wa kimaabara unaendelea.Mwenyekiti wa Taasisi ya Kiislamu ya Imam Bukhary, Sheikh Khalifa Khamisi alisema Serikali inaweza ikaendelea kuichunguza dawa hiyo huku mchungaji huyo akiendelea na shughuli zake kwani ameonyesha kuwasaidia watu wengi.“Yule mchungaji ameonyesha nia ya kuwasaidia watu wapone na si kutaka kupata pesa hafanyi mambo yake kwa tamaa hivyo aachwe aendelee na shughuli zake,” alisema Sheikh Khamisi.
Endelea kusoma habari hii...............


 

Friday, March 11, 2011

Best Blogger Tips
Tetemeko kubwa la ardhi Japan

Tetemeko kubwa la ardhi limepiga kaskazini-mashariki mwa Japan, na kuibua mawimbi ya tsunami ambayo yamesababisha hasara kubwa.

Televisheni nchini Japan, imeonesha magari, meli na hata majengo makubwa yakizolewa na mawimbi makubwa ya maji ya bahari baada ya tetemeko lenye ukubwa wa 8.9 kupiga.

Tetemeko hilo pia limesababisha moto katika maeneo mengi ya Japan ikiwemo mji mkuu Tokyo, ambapo imearifiwa watu 15 wamekufa.

Limepiga kiasi cha kilometa 400 kutoka mji mkuu na mawimbi yakaingia umbali wa maili 20 ndani.
Wataalam wa matetemeko wamesema hili ni moja ya tetemeko kubwa kuipiga Japan kwa miaka mingi.

Wakati tetemeko lilipopiga, majengo mjini Tokyo yaliyumba. Mtu kutembea ilikuwa sawa na kuwemo ndani ya meli inayopigwa mawimbi baharini.

Watu walishuka chini kutoka katika ofisi zao na kusalia mitaani wakiwa wanatetemeka.

Moto mkubwa ulizuka katika eneo moja la mji na katika maeneo mengine, watu waliojeruhiwa walitolewa nje ya vituo.

Mara moja serikali ilitoa onyo la tsunami.

Katika mji mkuu Tokyo, usafiri wa umma umesimamishwa, lifti katika majengo mengi zimezimwa na maelfu ya watu wamekusanyika katika bustani za wazi na vituo vya treni.

Onyo la tsunami limetolewa pia katika maeneo yote ya bahari ya Pacific ikiwemo Philippines, Indonesia, Taiwan, Hawaii, na mwambao wa bahari ya Pacific nchini Urusi na kaskazini mwa Amerika Kusini.

Mawimbi makubwa yalipiga katika miji ya Miyagi na Fukushima, na kuharibu vibaya sehemu kubwa ya makazi ya watu eneo la pwani. Shirika la habari la Kyodo limesema mawimbi yaliyofikia urefu wa mita 10 na kupiga bandari ya Sendai huko Miyagi .

Thursday, March 10, 2011

Best Blogger Tips
Askofu abariki tiba ya Loliondo


Via Newhabari

BAADA ya Serikali kupitia Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Haji Mponda, kutangaza kusitisha kwa muda huduma za matibabu yanayotolewa na Mchungaji Ambilikile Mwasapila, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), limepinga hatua yoyote ya kukwamisha huduma hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha jana, Askofu Thomas Laizer wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Kati eneo ambalo pia Mchungaji huyo anaendesha shughuli zake, alisema hatua ya kusitisha huduma hiyo ni kuupinga ukristo.

Kwa sababu hiyo, alisema Kanisa la KKKT halitakubali karama hiyo iliyotolewa na Mungu kupitia mtumishi wake kuhujumiwa.

Badala yake, ameiomba Serikali isaidie kuboresha mazingira ya eneo hilo.

Askofu Laize alisema kujaribu kuizuia kazi hiyo ni kuiingiza jamii katika mfarakano usio na sababu za msingi na huenda ikavuruga jamiii ambayo tayari kupitia huduma hiyo inaonekana kuungana bila kujali taifa, dini kabila wala rangi za watu.

“Si sawa kuzuia huduma ya kiroho kwa kutumia chombo chochote kile bila kuwashirikisha wadau wa kiroho ambao ni sisi viongozi wa dini, na bahati nzuri huduma hii si ya kisayansi kwamba waweza kuichunguza katika maabara,” alisema.

Kuhusu kuitaka Serikali kuingilia kati kusaidia huduma ya Mchungaji Mwasapile, Askofu Laizer alisema kuwa tayari Kanisa la KKKT limeanza mchakato wa kuyaboresha mazingira ya eneo hilo kwa kujenga banda kubwa la watu kupumzikia pamoja na kuchimba mashimo ya vyoo na huduma za maji.

“Tunaomba Serikali ituunge mkono katika hili, tutaanzisha akaunti katika benki ya CRDB, akaunti hiyo kila mtu apitishie mchango wake ili usaidie kuboresha huduma hii muhimu,” alisema.

Aliwashutumu vikali baadhi ya viongozi wa dini hasa wale wa Kikristo wanaopinga huduma ya mchungaji huyo kwa kile alichokiita kuwa ni wivu unaotokana na watu kuyakimbia makanisa ya viongozi hao.

Katika kile kinachonyesha kukerwa na matamshi ya baadhi ya viongozi hao, aliwataka viongozi wa dini, hasa wakristo kusoma na kuuelewa ukristo vizuri badala ya kutoa matamshi yanayoonekana kama wanaotapatapa.
“Wale wanaopinga huduma hii kwanza hawajui theolojia, wanasema mtu ambaye hajaokoka hawezi kutumiwa na Mungu, si kweli. Kwanza hatuokoki, tunaokolewa,” alisema Askofu Laizer.

Aidha aliwatahadharisha waumini wa kikristo na wananchi kuwa makini na viongozi hao aliowaita kuwa ni watu wanaojaribu kumwongoza Mungu kadri ya matakwa yao.

“Hao wanaojiita viongozi wa dini wanaopinga huduma hii wasimshike Mungu pua, kumwendesha na kumpeleleka wanakotaka wao kama farasi, wasifanye monopoly (urasimu) katika kumtumikia Mungu, hilo halipo, yule ni kiumbe dhaifu ambaye Mungu katika mazingira yake ameamua kumtumia yeye na si wao, tumwache afanye kazi yake yeye aliyemteua,” alisema Askofu huyo.

Alitumia fursa hiyo kuwahakikishia wananchi kuwa Mchungaji huyo si mganga wa kienyeji, wala si tapeli kama baadhi ya watu wanavyopotosha, bali ni miongoni mwa watumishi wa KKKT waliostaafu wakiwa waadilifu na ndio wanaoigwa kwa utumishi uliotukuka.

Siku chache baada ya mamia kwa maelfu ya watu kufurika katika Kijiji cha Samunge kupata kikombe cha dawa za mchungaji huyo, wamejitokeza baadhi ya watu kutoa ushuhuda wa kupona.

Wednesday, March 9, 2011

Best Blogger Tips
Serikali yasitisha tiba ya loliondo

Via Mwananchi

WAZIRI wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Haji Mponda amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isdori Shirima kuzuia haraka matibabu ya magonjwa sugu yanayoendeshwa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la KKKT, Ambilikile Mwasapile katika Kijiji cha Samunge, Tarafa Sale, Loliondo.

Dk Mponda alisema hayo jana alipokuwa akijibu swali la waandishi wa habari baada ya kumaliza kuzindua matumizi ya Bajaji kwa ajili ya kusafirishia wagonjwa. Alisema amemwagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha kumzuia mchungaji huyo kuendelea na utoaji wa dawa mpaka serikali itakapojiridhisha na hali ya usalama pamoja na uwezo wa dawa hiyo.

“Kutokana na hali halisi ya usalama wa kiafya kwa sasa katika eneo hilo, kuna hatari ya kuwepo kwa milipuko ya magonjwa kwa kuwa idadi ya watu inazidi kuongezeka,” alisema Dk Mponda.

Hata hivyo, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Raymund Mushi alisema hajapata taarifa yoyote kuhusiana na hatua hiyo ya Wizara ya Afya... "Hadi jioni hii mpaka ninatoka ofisini sijapata taarifa yoyote kuhusiana na uamuzi huo."

Baadhi ya wananchi waliohojiwa kuhusiana na hatua hiyo ya Serikali walisema badala ya kuchukua hatua hiyo, ilipaswa kusimamia mchakato mzima wa utoaji wa dawa hiyo kwa kuhakikisha kwamba inatolewa katika mazingira mazuri na kuhakikisha huduma muhimu za kijamii zinapatikana kijijini hapo ikiwa ni pamoja na kuwabana wamiliki wa magari kupunguza nauli na kukarabati barabara.

Mkazi wa Karatu, Reurent Bortha, alisema anashangazwa na serikali kuibuka sasa wakati mchungaji huyo alianza kutoa dawa hiyo tangu Agosti mwaka jana... "Tunaiomba serikali kusaidia upatikanaji huduma muhimu kama mahema na kukarabati barabara na siyo sasa kuibuka na kusema dawa haijafanyiwa utafiti."

Bortha ambaye amedai kwamba ndugu zake wamepona maradhi mbalimbali kutokana na dawa ya mchungaji huyo, alisema serikali imechelewa kufanya utafiti wa kuthibitisha dawa hiyo kitaalamu na inachopaswa kufanya ni kuweka mazingira bora ya utolewaji wake.

Mwananchi mwingine, Peter Ngoi alisema kama serikali inatilia shaka dawa hiyo, inapaswa kuwafuata watu waliokunywa na kupona na siyo kuhangaika kuipima na kuichunguza... "Hawa watu wa Serikali ni wa ajabu hawajazungumza na sisi wagonjwa wanakaa Dar es Salaam na kutangaza  kusitisha dawa."
Endelea kusoma habari hii...............

Tuesday, March 8, 2011

Best Blogger Tips
NUGGETS: Karl agree to multiyear contract extension


DENVER, March 8, 2011 – The Nuggets and head coach George Karl have agreed to a multiyear contract extension, the team announced today.

Per team policy, terms of the contract were not disclosed.

“I’ve always said Denver is the place I want to end my career,” Karl said. “This puts me one step closer to achieving that goal. Masai Ujiri and Josh Kroenke were very professional throughout these negotiations.

“The Kroenkes have been great throughout this entire process. They’ve been very supportive of me as a coach and during my battle with cancer. I’m excited for the remainder of the season and look forward to making another playoff run.”

Since taking over as Nuggets coach on Jan. 27, 2005, Karl has guided Denver to the playoffs in each of the past six years, including a trip to the 2009 Western Conference finals. The Nuggets also have posted three consecutive 50-win seasons, which marks the most successful three-year stretch in franchise history.

“Extending George’s contract has been one of our top priorities,” Nuggets Vice President of Basketball Operations Masai Ujiri said. “He’s done a tremendous job since arriving in Denver, and particularly with the unique challenges of this season. With George on the bench, we have a bright future and everyone here is focused on finishing the season strong.”

On Dec. 10, Karl became the seventh coach in NBA history to win 1,000 regular-season games, joining Don Nelson (1,335), Lenny Wilkens (1,332), Pat Riley (1,210), Jerry Sloan (1,221), Phil Jackson (1,143) and Larry Brown (1,098).

Now in his 23rd season as an NBA head coach, Karl has taken his teams to the playoffs 19 times, and he has not had a losing season since 1987-88. His 315 victories with the Nuggets rank second in franchise history to Doug Moe (432), while his .613 winning percentage is unmatched.

“George’s record speaks for itself,” Ujiri said. “We’re lucky to have one of the most successful coaches in NBA history to lead our team.”

Overall, Karl has as a career regular-season record of 1,023-698 with Cleveland, Golden State, Seattle, Milwaukee and Denver.
Source: NBA

Saturday, March 5, 2011

Best Blogger Tips
Wapinzani wakabiliana na majeshi ya Libya

Wapinzani nchini Libya wamezuia jaribio la majeshi ya serikali ya kuuchukua tena mji wa Zawiya, kilomita 50 magharibi mwa mji wa Tripoli.

Kufuatia mapigano makali siku ya Jumamosi asubuhi, majeshi ya serikali yalilazimishwa kusogea nje ya mji, ingawa baadhi ya taarifa zinasema wamejipanga upya na huenda wakawa wanapanga mashambulizi mapya.
Idadi ya vifo haiko wazi.

Wakti huohuo, wapinzani wanaompinga Kanali Muammar Gaddafi wamechukua udhibiti wa mji wa bandari wa Lanuf, mashariki mwa Tripoli.

Waangalizi wanasema kwa ujumla ni vigumu kujua nani anadhibiti wapi, wakati mvutano wa kuitawala Libya ukiendelea.

Mjini Tripoli, kuna hali ya kujiamini miongoni mwa wanaoutii utawala, huku udhibiti ukionekana kuongezeka mjini Tripoli na maeneo mengine ya kati, kwa mujibu wa mwandishi wetu aliyepo huko.

Lakini katika maeneo mengine, waandishi wa habari wanasema waandamanaji wana ari kubwa ya kuuondoa utawala wa Kanali Gaddafi.

Taarifa kutoka Zawiya zinasema mji huo umeshambuliwa kutoka upande wa mashariki na magharibi kutoka kwa wanajeshi wa serikali wenye silaha nzito.
Source: BBC

Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits