Saturday, February 26, 2011

Best Blogger Tips
Baraza la usalama kumuwekea vikwazo Gaddafi


Baraza la usalama la Umoja wa mataifa linakutana kuangalia uwezekano wa kuiwekea vikwazo vya kiuchumi  serikali ya Kanali Muammar Gaddafi.

Baraza hilo linategema kuweka vikwazo vya kiuchumi na pia kutaifaisha mali za serikali hiyo.

Pia baraza hilo linapendekeza Kanali Gaddafi kufikishwa katika mahakama ya kimaifa ya makosa jinai  kwa makosa ya kukiuka  haki za binadamu.

Wakati huo huo, Rais Barack Obama wa Marekani, kwa mara ya kwanza amesema, Kiongozi huyo wa Libya anatakiwa kuachia madaraka na kuondoka katika nchi hiyo mara moja.

Ikulu ya Marekani imesema, Rais Obama aliweka msimamo wake wazi  wakati akizungumza na kiongozi wa Ujerumani  Kansela Angela Merkel wakati wa mazungumzo yao kwenye simu siku ya jumamosi jioni.

 “ Rais amesema, kama umefika wakati kiongozi unawaongoza watu wako kwa kutumia nguvu na unyanyasaji, ni kwamba umepotea maana halisi ya utawala na inatakiwa uitendee haki nchi yako kwa kuachia madaraka na kuondoka mara moja,” imesema taarifa hiyo.

Mapema, mmoja wa watoto wa Kanali Gadaffi, anayeitwa Saif al-Islam, alisisitiza kwamba  maisha yanaendelea kama kawaida  kwa robo tatu ya Libya. Taarifa yake inapingana na ya waandamanaji  wanaompinga Gaddafi ambao wanadai wameshikilia asilimia 80 ya nchi hiyo.

Ni vigumu kuthibitisha madai ya pande zote mbili, lakini inaaminika kwamba upande wa upinzani unashikilia mji wa pili wa Benghazi, wakati Kanali Gaddafi bado anashikilia mji mkuu Tripoli, ambao unakisiwa kuwa na watu milioni mbili. Nchi ya Libya inakisiwa kuwa na jumla ya watu milioni sita na laki tano.

Umoja wa Mataifa unakadiria zaidi ya watu 1,000 wamekufa katika uasi huo ambao umeingia siku ya kumi leo hii.
Best Blogger Tips
Hasheem Thabeet


Hasheem Thabeet, alipotakiwa na gazeti moja la Memphis  kuelezea  jinsi ilivyokuwa kwake katika mwaka wake wa kwanza kama mchezaji wa NBA, alitoa jibu la kuvutia , “ Nilikuwa kama nyati aliyeona mwanga wa tochi.”

 Thabeet  akiwa ameshacheza misimu miwili ya NBA, hajaonyesha mchezo wa kuvutia  kama alivyosema kwenye jibu lake.

Inawezeka  ikawa hivyo kwa mtu ambaye bado anajifunza kucheza mchezo huo. Thabeet amekuwa akicheza soka  tangu akiwa mdogo kwenye nchi yake ya Tanzania yenye jumla ya watu takribani milioni 41 iliyopo mashariki ya bara la Afrika.

Thabeet ambaye ametimiza miaka 24 wiki iliyopita, hakuwa akicheza mpira wa kikapu mpaka alipokuwa na miaka 15, muda mfupi baada ya baba yake kufariki. Akiwa mtoto wa kiume kutoka katika moja ya nchi masikini duniani, kuja kwake Marekani ilikuwa ni kwa ajili ya kuisaidia familia yake iwe na maisha bora.

Alituma maombi kwenye vyuo mbalimbali, kwa matumaini kwamba angepata ufadhili wa masomo. Mmoja kati ya walimu wa michezo alimuona katika mashindano, na akaishia katika shule za sekondari za Majimbo ya Califonia na Mississipi kabla ya kwenda katika mji wa Houston kwenye jimbo la Texas, ambapo aliingia katika shule ya sekondari ya Cypress ( Cypress Christian High School).

Thabeet alipofika  shuleni  kwake Cypress Christian mwaka 2005, ilimuwiya vigumu sana katika kujifunza kucheza mpira wa kikapu, licha ya urefu wake wa futi 7-3, alipata shida katika mchezo huo.

Kwa ujumla ilieleweka kwamba Thabeet asingeweza kucheza mchezo huo katika daraja la kwanza.

Hivyo ndivyo kocha msaidizi wa chuo cha Connecticut Andre LaFleur  alivyowaza baada ya kumuona Hasheem kwa mara ya kwanza. Aliyomuona mara ya pili, Thabeet alikuwa amebadilika sana, akionyesha maendeleo mazuri katika mchezo huo, na alipomuona kwa mara ya tatu alikuwa akicheza vizuri zaidi.

Lafleur alikuwa Houston wakati thabeet alipokuwa akipambana na timu ya Blake Griffin katika mashindano ya Kingwood. Lafleur akamjulisha kocha mkuu wa UConn Jim Calhoun kwamba Thabeet anaweza kuwa  namba moja kati ya wachezaji watakaochaguliwa kujiunga na NBA hapo baadaye.

Baadaye mwaka 2009 katika kuwachagua wachezji bora wa kujiunga  na NBA, Hasheem Thabeet alikuwa ni chaguo namba 2 nyuma ya Blake Griffin aliyekuwa namba 1.

Thabeet anaendelea

“Alikuwa anacheza mpira wa kikapu kama vile anacheza soka” Lafleur anasema, “Lakini kitu cha muhimu ni kwamba kila wakati ukimuona alikuwa anakuwa mzuri mzaidi”. “Unafikilia kwamba: kila kitu anachoona hapa ni mara yake ya kwanza, maisha yake aliyokulia ni tofauti na ya wachezaji wa hapo ambao ndoto yao  ni kucheza NBA. Kufanikiwa kwake kufika chuoni kumemfanya ajulikane nyumbani. Ikabidi ajifunze malengo yake mapya, alikuwa hajui kitu.

Sasa hivi ni karibu miaka miwili tangu Hasheem aanze kazi yake katika NBA, watu wengi wanamuona kama vile ambavyo Lafleaur alivyomuona kwa mara ya kwanza, mtu mrefu aliye legelege na asiyeweza kuchangia chochote katika mchezo huo.

Timu ya Rockets, ambayo imewapeleka wachezaji wake Shane Battier na Ish Smith huko Memphis kwa ajili ya kumchukua Thabeet, wana imani kuwa  mchezaji huyo mrefu na mwenye umbo kubwa katika NBA atabadilika na kuwa mzuri zaidi kama ilivyokuwa wakati akianza kujifunza mchezo huo.

“NI wazi kuwa tunahitaji mchezaji wa kati katika timu yetu”, anasema Daryl Morey ambaye ni Meneja Mkuu wa Rockets. “ Hasheem Thabeet ana uwezo wa kuendeleza kipaji chake katika sehemu ya ulinzi na pia kuwa mchezaji mzuri wa kati. Sasa hivi bado hajafikia hapo, kama angekuwa katika hali hiyo sisi tusingekuwa na uwezo wa kumpata.”

Ujasiri na kujiamini

Kujiamini na ujasiri ndivyo vitu vinavyomsaidia, lakini Lafleaur anasema Thabeet ni mtu ambaye anajivunia mafanikio yake. Hali ya kuwa anasakamwa mara kwa mara inamuumiza, lakini hali ya kumchukulia kwamba ameshindwa katika mchezo huo inamuumiza zaidi.

“ Naelewa kwamba kwenye idara ya ulinzi ni mzuri ingawa naweza kufanya vizuri zaidi,” Thabeet alimuandikia barua pepe mwandishi wa Rockets Jonathan Feigen siku ya ijumaa. “ Jambo moja ambalo nimejifunza  ni kwamba wakati wowote unaweza kuwa bora, niko hapa kufanya kazi kwa bidii, kujifunza mfumo wa timu hii ya Rockets na nina furaha kubwa kwa kupata nafasi hii.”
Best Blogger Tips
Posh wa Beckam mjamzito

LONDON, England
WAKATI wadau wa soka na muziki wanasubiri kuona Posh Beckham anajifungua mtoto wa nne, mume wake David ametoboa siri ya moyoni. Akitoa siri hiyo, amesema pamoja na furaha ya kupata mtoto mwingine, ambaye anatarajiwa kuwa wa kwanza mwanamke kwao, mkewe alimliza alipojua ukweli huo.

Anakiri kuwa mkewe ambaye ni mwanamuziki wa zamani wa kundi la Spice Girls na sasa ni mwanamitindo mashuhuri, Victoria, amekuwa mtu mwenye kuficha siri, na mara nyingi amekuwa akimchanganya katika baadhi ya mambo. "Kuna mambo ananificha hadi dakika za mwisho, ananishangaza mno," anasema. Gwiji huyo wa soka alieleza kuwa mkewe anapenda maendeleo ya familia yao na ndio maana hufanya vitu kwa kufikiria kabla ya kumueleza.

Katika maisha yake ya ndoa, anasema hakuna jambo ambalo limeweza kumchanganya hadi sasa, kama suala la mimba hii aliyonayo mkewe maarufu kwa jina la Posh. "Sikuwa nikijua juu ya ujauzito huo, Posh hakunieleza, hadi siku moja ambayo aliamu kunishangaza. "Siku hiyo alinieleza anataka kunipa ofa. Nilimkubalia na tukatoka kwenda kula chakula cha usiku nje kwenye mgahawa.  "Nikiwa sina hili wala lile, tukiendelea kula na kunywa kwa furaha, ndipo alipoamua 'kunitupia bomu'. "Becks, aliita. Nikamuangalia usoni. Kuna kitu nataka nikwambie," alinieleza na nikiwa sina hakika na alilokuwa nalo moyoni, nikamjibu "niambie mpenzi." Huko ndio aliniambia suala la uja uzito,"alisema mchezaji huyo. "Nina mimba!" alitamka huku akiniangalia machoni bila kupepesa. "Nilianza kutokwa na machozi. Si kwamba nilikuwa nalia, bali yalikuwa machozi ya furaha ya kusikia habari hiyo nzuri," alisema Beckham ambaye tayari ni baba wa watoto watatu wa kiume, aliozaa na mkewe huyo. Watoto hao ni  Brooklyn, Romeo na Cruz. "Niliiona hiyo ni habari njema, kwani nilikuwa ninatamani sana kupata mtoto mwingine, matumaini kwamba tutapata mtoto wa kike." Anasema furaha yake hiyo imetokana na ukweli kuwa alijua pia mkewe alikuwa akitaka mtoto mwingine, na niligundua alipokuwa akinieleza habari hizo, hata yeye alikuwa katika furaha.

Furaha yangu anasema, ni kwamba tutaongeza binadamu mwingine katika familia yetu, na anataka kuona familia yake inaongezeka, akitaraji mmoja  wa watoto wake, hasa wa kiume, akirithi kazi yake ya kucheza soka. Hata hivyo, gwiji huyo wa soka anaeleza anapenda kuona familia yake ikitoa wataalamu mbalimbali ambao wataweza kuisaidia nchi yao ya Uingereza, siku zijazo. "England inahitaji wataalamu mbalimbali, hawa watoto Mungu akiwajalia watasoma na kuanza maisha yao huku wakisaidia maendeleo ya nchi hii na ulimwenguni mzima," alisema mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United, ambaye sasa amesajiliwa na timu ya Los Angeles Galaxy ya Marekani. Becks ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 35 na mkewe Victoria akiwa na miaka 36, tayari wameanza kufanya maandalizi ya kumpokea mtoto huyo mpya.

Wanandoa hao wameweza wameshawarifu watoto wao watatu kuwa watarajie kumuona mtoto mchanga kabla ya sikukuu ya Krismasi mwaka huu. David na Victoria wameanza kupokea taarifa za kupongezwa na marafiki zao huku wakimuombea kwa Mwenyezi Mungu, Victoria ajifungue salama. Miongoni mwa watu ambao wametuma ujumbe huo ni pamoja na mwanamuziki maarufu duniani, Kylie Minogue. Hata hivyo, msemaji wa Victoria Beckham, Jo Milloy, ameeleza kuwa mipango mingine kuhusu jambo hilo inaendelea. Lakini baadhi ya vyombo vya habari nchini humo vikiwemo vituo vya luninga, vinahaha kutaka kuingia mkataba na familia hiyo kutangaza wakati mrembo huyo akijifungua.

Vyombo hivyo  vya habari vimekuwa vikijaribu kuteta na watendaji wa wanandoa hao ili waweze kuwashawishi wakubaliane nao, na ikiwezekana waweze kurekodi kipindi cha kuonyesha wakati mwanamuziki huyo wa zamani akijifungua.

Lakini hadi juzi hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na familia hiyo kama itakubali jambo hilo au la.

Thursday, February 24, 2011

Best Blogger Tips
Gaddafi amlaumu Osama

Kiongozi wa Libya Kanali Muammar Gaddafi amekiambia kituo cha televisheni cha taifa kuwa Osama Bin Laden na wafuasi wake, ndio wa kulaumiwa kwa maandamano yanayotikisa nchi yake.

Katika hutuba aliyotoa kupitia simu, mahsusi kwa ajili ya wakazi wa mji wa al-Zawiya, Kanali Gaddafi amesema vijana wanadanganywa kwa kupewa dawa za kulevya na pombe ili washiriki katika "uharibifu na hujuma".

Kanali Ghaddafi anajitahidi kurejesha udhibiti wa mji mkuu Tripoli na maeneo ya magharibi.
Waandamanaji wamekuwa wakipata nguvu katika miji ya mashariki.

Wanasiasa wa upinzani na viongozi wa kikabila wamefanya mkutano muhimu katika mji wa mashariki wa al-Badya, kuonesha umoja dhidi ya Kanali Gaddafi.

Hotuba hiyo ililenga mji wa al-Zawiya uliopo kilomita 50 magharibi mwa mji mkuu, ambapo kumekuwa na ripoti za milio ya risasi mitaani.

Kanali Ghaddafi amesema waandamanaji hawana madai yenye msingi, na walikuwa wakiongozwa na kiongozi wa al-Qaeda.

"Bin Laden.... huyu ndio adui anayewadanganya watu. Msidanganywe na Bin Laden," amesema.

"Ni wazi kuwa sasa jambo hili linaongozwa na al-Qaeda. Vijana wenye silaha, watoto wetu, wanachochewa na watu ambao wanatafutwa na Marekani na nchi za Magharibi.

"Wale wanaochochea ni wachache, na hatuna budi kuwakamata."

Amesema vijana hao waandamanaji "wanafurahia kupiga risasi hasa wakiwa wamelewa".

Amesema Libya sio kama Misri na Tunisia, ambazo zimeshuhudia viongozi wao wakiondolewa madarakani, kwa sababu watu wa Libya wana uwezo wa kubadili maisha yao kwa kupitia kamati.
Source: BBC

Thursday, February 17, 2011

Best Blogger Tips
Watu 20 wauwawa kwenye mlipuko Dar

Hali ya taharuki imetanda mji wa Dar Es Salaam, nchini Tanzania, huku wakaazi wakiamka kuomboleza vifo vya zaidi ya watu kumi na zaidi ya wengine 60 kujeruhiwa kufuatia milipuko iliyotokea kwenye ghala la kuhifadhi silaha za kijeshi, lililo karibu na uwanja wa kimataifa wa ndege.

Wakaazi wa eneo la Gongo la Mboto lililo karibu na ghala hilo wamekesha nje baada ya makaazi yao kubomoka kutokana na mtikisiko wa milipuko hiyo iliyodumu kwa saa kadhaa. Milipuko hiyo ilisikika kwa umbali wa zaidi ya kilomita ishirini kutoka kituo hicho cha kijeshi.

Inaarifiwa kuwa milipuko hiyo ilianza mwendo wa saa mbili usiku.

Msemaji mmoja wa jeshi amesema kuwa kuna watu wengi ambao wamepoteza maisha yao lakini idadi kamili haijajulikana.

Kamanda wa polisi jijini Dar-es-Salaam, Suleiman Kova, ametoa wito kwa raia wa mji kuwa huo watulivu huku maafisa wa ulinzi wakiendelea na mikakati ya kurejesha hali ya uthabiti.

Kova amesema uchunguzi wa awali umebainisha kuwa mlipuko huo ni ajali na wala sio shambulio la kigaidi.
Ni hii mara ya pili kwa milipuko kama hiyo kutoka jijini Dar es Saalam katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.

mwaka wa 2009 zaidi ya watu ishirini waliuawa na wengine 300 kujerihiwa

Tuesday, February 15, 2011

Best Blogger Tips
Kaka wa Princess Diana atangaza ndoa


Ndoa ya Prince William siyo pekee ambayo inafanyika mwaka huu katika familia yake,  Mjomba wake William anayeitwa Charles Spencer ametangaza  kufunga ndoa na mchumba wake Karen Gordon.

 “Charles Spencer, anayofuraha kubwa kutangaza uchumba wake na Karen Gordon, ambaye ni mzaliwa wa  Canada na pia ni Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Shirika la kimataifa la kuhudumia watoto”, ilisema taarifa hiyo.

Harusi hiyo ambayo itakuwa ni ya kifamilia na marafiki wa jirani, itafanyika tarehe 18 mwezi wa sita mwaka huu kwenye mji wa Althop nchini uingereza, kwenye makazi ya familia ya Spencer.

Spencer, ambaye ni kaka wa marehemu Princess Diana, anakumbukwa kwa maneno aliyozungumza katika mazishi ya Dada yake mwaka 1997, kuhusu familia ya kifalme kutomjali marehemu dada yake.

Hii itakuwa ni ndoa ya tatu kwa Spencer. Ana watoto wanne kutoka kwenye ndoa yake ya kwanza, na watoto wawili kutoka kwenye ndoa yake ya pili.

Monday, February 14, 2011

Best Blogger Tips
Ronaldo atundika njumu

Mwanasoka mashuhuri wa Brazil, Ronaldo, ambae aliisaidia nchi yake kunyakua kombe la dunia 1994 na 2002, amethibitisha kuwa anajiuzulu kucheza soka.

Anaacha kandanda akiwa na rekodi ya kufunga mabao mengi zaidi katika fainali za kombe la dunia kushinda mchezaji mwingine yeyote.

Ronaldo atakumbukwa kuwa ni mojawapo wa wachezaji hodari wa kandanda, ambaye aliwavutia mashabiki kila alikocheza kwa mbio zake karibu na lango na umahiri wa kufunga mabao.
Lakini sasa akiwa na umri wa miaka 34, Ronaldo anasema mwili wake haumruhusu tena kuendelea.

Katika miaka ya hivi karibuni amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya magoti ambapo mara tatu yalitishia kumzuia asiweze tena kucheza .

Katika kipindi cha miaka 18 iliyopita Ronaldo amefungia Brazil mabao 62 katika mechi za kimataifa,na kati hayo mabao 15 katika fainali za kombe la dunia, hii ikiwa ni rekodi.

Alionyesha ustadi wake kwa vilabu mashuhuri barani Ulaya, ikiwemo Barcelona, Real Madrid na Inter Milan.

Ametunukiwa tuzo ya FIFA ya kuwa mchezaji bora duniani mara tatu.

Alirejea Brazil akitumaini kukamilisha msimu wa mwisho katika michuano ya klabu.

Lakini maumivu yake na hali ya mwili wake ambayo ilimfanya asiweze kupunguza uzito wa mwili wake hatimaye vilimkatisha tamaa na akaamua asalimu amri.
Source: BBC
Best Blogger Tips
Jeshi la Misri lavunja bunge

Jeshi la Misri limevunja bunge na kusimamisha matumizi ya  katiba, wakikidhi   madai makuu mawili ya waandamanaji  wanaounga demokrasia baada ya siku 18 za ghasia ambazo zilimtoa madarakani Rais Hosni Mubarak.

Utawala wa kijeshi ambao ulichukua udhibiti wakati bwana Mubarak alipojiuzulu Ijumaa, ulitoa taarifa Jumapili ukisema utaongoza kwa muda wa miezi sita au hadi uchaguzi wa Rais na bunge utakapofanyika. Uchaguzi kwa sasa umepangwa kufanyia mwezi Septemba.

Taarifa ilitolewa muda mfupi baada ya Waziri Mkuu wa Misri, Ahmed Shafiq, aliposema kipaumbele cha baraza lake la mawazili linaloungwa mkono na jeshi ni kurejesha usalama na maisha ya kawaida huko Misri. Pia alisema nyadhifa kadhaa katika baraza la mawaziri zinabaki wazi na aliahidi kwamba uteuzi wowote mpya utakuwa unakubalika na jamii.

Mkutano huo na waandishi wa habari ulikuwa mkutano wa kwanza wa Waziri Mkuu tangu bwana Mubarak alipojiuzulu Ijumaa na kukabidhi madaraka kwa jeshi kufuatia  shinikizo la waandamanaji wengi dhidi ya utawala wake wa takribani miaka 30. Bwana Mubarak alimteuwa bwana Shafiq kama Waziri Mkuu Januari 29, siku nne baada ya maandamano kuanza. 
Source: VOA

Friday, February 11, 2011

Best Blogger Tips
Breaking News: Rais Mubarak wa Misri amejiuzuru


Maelfu ya watu wamelipuka kwa furaha baada ya Makamu wa rais wa Misri kutangaza kuwa Rais Hosni Mubarak ameachia ngazi.

Katika tangazo kupitia televisheni ya taifa, makamu wa rais Oma Suleiman amesema Bw Mubarak amekabidhi madaraka kwa jeshi.

Hatua hii imekuja baada ya maelfu ya watu kukusanyika mjini Cairo pamoja na miji mingine mikuu katika siku ya 18 ya maandamano ya kudai Bw Mubarak ajiuzulu.

Waandamanaji walipokea taarifa hizo kwa kushangilia, kupeperusha bendera, kukumbatiana na kupiga honi za magari. "Watu wameuangusha utawala," wamekuwa wakiimba.

"Kwa jina la Mungu mwenye neema, mwenye rehema, raia, katika wakati huu mgumu, Misri inapopitia, Rais Hosni Mubarak ameamua kuachia madaraka kutoka ofisi ya rais ya jamhuri na ametoa jukumu la kuendesha nchi kwa baraza kuu la jeshi," amesema.

"Mungu awasaidie wote,"

Bw Mubarak tayari ameondoka Cairo na yupo katika mji wa Sharm el-Sheikh, ambapo ana makazi mengine huko, maafisa wamesema.

Mjini Cairo, maelfu ya watu wamekusanyika nje ya Ikulu, katika eneo la wazi la Tahrir na katika kituo cha taifa cha televisheni.

Waandamanaji hao walikuwa na hasira kufuatia hotuba ya Bw Mubarak siku ya Alhamisi. Alikuwa akitarajiwa kutangaza kujizulu, lakini hakufanya hivyo na badala yake kupunguza madaraka yake kwa makamu wa rais.
 
Baada ya habari hizo kufika kwa wananchi, ambao wamekuwa wakiaandamana kushinikiza rais kujiuzuru mara moja, furaha kubwa iliibuka, ikiwa ni ushindi mkubwa kwao kwani matakwa yao yametimia.

Mshindi wa tuzo ya Amani ya Nobel Mohammed El Baradei, ambaye alirejea Misri kujiunga na maandamano hayo, alisema, "Hii ni siku kubwa ya maisha yangu"

Thursday, February 10, 2011

Best Blogger Tips
Mubarak agoma kujiuzuru

Rais wa Misri, Hosni Mubarak amesema atasalia madarakani na kukabidhi madaraka yote baada ya uchaguzi wa urais mwezi Septemba.

Matamshi yake katika hotuba kupitia televisheni ya taifa, yamepishana na taarifa za awali kuwa alikuwa akijitayarisha kujiuzulu.

Hasira

Bw Mubarak amesema atakabidhi baadhi ya majukumu kwa makamu wa rais Omar Suleiman, lakini taarifa kamili ya jambo hili haifahamiki vyema.

Maelfu ya waandamanaji katika eneo la wazi la Tahriri wamepokea kwa hasira tangazo lake hilo.

Walikuwa wakipiga kelele za "tumechoka na Mubarak", huku waandamanaji wengine 'wakipeperusha' viatu vyao kwa ghadhabu. Maelfu wameripotiwa kutembea kuelekea katika ikulu ya rais ambayo iko umbali mrefu.

Bw Mubarak alikwisha sema mapema kuwa hatogombea urais mwezi Septemba, na kusema atasalia kusimamia mchakato wa mabadiliko ya katiba.

"Natangaza nia yangu ya kuendelea na kuitetea katiba na kuwalinda wananchi na pia mabadiliko kwa yeyote atakayechaguliwa mwezi Septemba katika uchaguzi huru na wa wazi," amesema Mubarak.

Kutoka Moyoni

Akiwahutubia moja kwa moja waandamanaji "waliopo Tahrir na kwingineko" katika kile alichoita "hotuba kutoka moyoni mwake", bw Mubarak,82, amesema: "Sioni aibu kusikiliza vijana wa nchi yangu na kuchukua hatua."

Ameomba radhi kwa familia za waandamanaji waliokufa katika mapigano na majeshi ya usalama katika wiki za hivi karibuni, na kusema waliohusika na vifo hivyo watachukuliwa hatua.

Bw Mubarak ameongeza kuwa sheria za hali ya dharura nchi humo zitaondolewa pale tu hali itakapokuwa sawa, na kusema atawapuuza "madikteta kutoka nje ya nchi".

Pia ameonekana kutoa wito wa kumalizika kwa maandamano dhidi ya utawala wake wa miaka thelathini, yaliyoanza Januari 25.

"Misri imepitia nyakati ngumu na hatuwezi kuruhusu hali hii kuendelea," amesema. "Hasara kwa uchumi wetu itasababisha hao vijana wanaotaka mabadiliko kuwa wa kwanza kuathirika."

Utengamano

Bw Suleiman, akizungumza baada ya hotuba ya Bw Mubarak, amesema maandamano hayo yamefikisha ujumbe, na mchakato wa mabadiliko ya katiba utaanza.

Ameongeza kuwa Rais Mubarak amemkabidhi madaraka ya kurejesha amani na utengamano nchini MIsri, na kurejesha hali ya kawaida, na kuwataka waandamanaji kurejea nyumbani.

"Vijana wa Misri: rudini nyumbani, rudini kazini, taifa la Misri linawahitaji kupata maendeleo. Msisikilize redio na televisheni, ambazo nia yake ni kuitia doa Misri," alisema.

Mwanaharakati Mustafa Naggar akijibu matamshi ya viongozi hao amesema: "Mitaani wamechoshwa na Mubarak. Iwapo MUbarak ataondoka nchini, atasaidia kumaliza mzozo huu. Akiendelea, atasababisha Wamisri kuingia katika janga.

"Mipango ya kesho inabakia palepale. Tutaandamana kwa mamilioni hadi eneo la Tahrir na maeneo mengine."

Rais wa Marekani Barack Obama amekutana na maafisa wake wa usalama wa taifa katika ikulu ya Marekani, baada ya hotuba ya Rais Mubarak. Serikali ya Marekani katika siku za hivi karibuni, imezidisha wito wake kwa sauti za waandamanaji kusikilizwa.

Kulinda taifa
 
Mapema, katibu mkuu wa chama kinachotawala cha Bw Mubarak - National Democratic Party - Hossam Badrawi alisema, jambo sahihi kwa rais kufanya ni kuondoka madarakani, na kuwa hakuwa akitarajia Bw Mubarak kuwa bado rais siku ya Ijumaa.

Wakati huohuo, jeshi la Misri limetangaza kuwa liko tayari "kulilinda taifa". Shirika la habari la Misri Mena, limeripoti kuwa baraza kuu la jeshi lipo katika hali ya "kulilinda taifa, na matakwa ya watu".

Mazungumzo kati ya serikali na makundi ya upande wa upinzani yamepiga hatua ndogo, huku waandamanaji wakitupilia mbali mipango ya mabadiliko iliyopendekezwa na serikali ya Bw Mubarak.
Source: BBC









 
Best Blogger Tips
Wabunge wa Chadema wamtikisa Pinda bungeni

WABUNGE wa Chadema jana walimtikisa waziri mkuu, Mizengo Pinda katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo wakimtaka kueleza serikali ina tamko gani kuhusu mauaji yaliyotokea Januari 5 mkoani Arusha.Kadhalika kikao cha tatu cha mkutano wa pili wa Bunge la kumi, jana kilishuhudia mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema akiwa mbunge wa kwanza katika bunge la kumi kuwekwa kikaangoni baada ya kupewa siku tano na Spika wa Bunge, Anne Makinda athibitishe madai yake kwamba Waziri Mkuu Pinda aliudanganya umma wa Watanzania wakati akijibu swali kuhusu vurugu za Arusha.

Hoja ya Mbowe
Msumari wa kwanza kwa Pinda, ulipigiliwa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, baada ya kuuliza serikali inatoa tamko gani rasmi kuhusu tukio la mauaji ya watu watatu katika vurugu na maandamano hayo, ikiwa ni pamoja na wahusika akiwamo IGP Said Mwema na Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha kujiuzulu.

Katika swali lake la nyongeza Mbowe alitaka kujua ni lini serikali itaunda tume ya kisheria kuchunguza tukio hilo kwa kupata maelezo kutoka pande zote husika tofauti na sasa ambapo taarifa zilizopo serikalini ni zile zinazotoka upande mmoja wa jeshi la polisi.

Majibu ya Pinda
Hata hivyo, akijibu kombora hilo, Pinda aliinyoshea kidole Chadema akisema kwa mujibu wa maelezo aliyopewa ilivunja makubaliano yake na polisi na kuandamana.

Pinda aliweka bayana kwamba, baada ya hali hiyo kilichotokea ni polisi kujaribu kuzuia maandamano hayo ya wanachama wa Chadema ambao tayari walikuwa wamehamasishwa na viongozi wao kwenda “kuwakomboa” wenzao waliokuwa wameshilikiwa kituo cha polisi mjini Arusha.

"Nakushukuru Mbowe kwa kuuliza swali hilo, serikali hii ni makini, ikiwa jambo limetokea usikimbilie kusema serikali,
serikali..., ni vizuri kuulizaa aliyesababisha...,'' alisema Pinda na kuongeza:

''Mlikiuka makubaliano na polisi, matamshi ya kwenye mkutano
hayakuwa ya chama chenye dhamira ya kujenga amani, mkawataka wafuasi waende kuwakomboa wenzao."

Katika kuondoa wingu na kuweka hadharani kila kitu, Pinda alisema pamoja na juhudi za polisi kuzuia maandamano hayo, lakini yaliendelea hadi mita 50 kutoka kituo cha polisi, nao hawakuwa njia nyingine kwa kuwa hawakujua nini kingewakuta kama waandamanaji wangevamia kituo cha polisi.
Endelea kusoma habari hii....................

Monday, February 7, 2011

Best Blogger Tips
Mubarak na mali zake

Rais wa Misri Hosni Mubarak na familia yake wameripotiwa kuhodhi mali nyingi wakati wakiwa madarakani kwa kipindi cha miongo mitatu.

Kituo cha televisheni cha ABC nchini Marekani katika ripoti yake moja kilidai kuwa utajiri wa familia ya Mubarak unakisiwa kuwa ni dolla billioni 70.

Takwimu hizo zimenukuliwa na vyombo vya habari mbalimbali duniani. Lakini baadhi ya watu wanahisi kuwa taarifa hizo zimeongezwa chumvi.

Ikiwa familia ya Mubarak kweli wana utajiri huo wa dolla billioni 70, basi utakuwa sawasawa na na jumla ya tajiri mkubwa wa Mexico Carlos Slim na billionea wa kampuni ya Microsoft Bill Gates.

Kwa mujibu wa takwimu za mwaka jana za jarida la Forbes, watu hawa wawili ni nambari moja na mbili katika orodha za matajiri wakubwa duniani kila mmoja akiwa na dola billioni 35.

Haielekei kuwa familia ya Mubarak inafikia kiwango hicho. Lakini licha ya hayo bado wanaweza kuwa matajiri wakubwa.

Inaaminiwa wanamiliki nyumba za kifakhari katika maeneo kama Manhattan, Beverley Hills, California na eneo mashuhuri la matajiri la Belgravia jijini London.

Inaarifiwa kwamba familia ya Mubarak ina akiba ya fedha nyingi katika benki za Uingereza na Uswiz
Halikadhalika inasemekana wameelekeza fedha nyingi katika hoteli na sekta ya utalii katika bahari ya Sham.
Ni wazi kabisa Rais Hosni Mubarak amekuwa na fursa nyingi za kujitajirisha katika miaka 30 iliyopita kama mtu mwenye madaraka makubwa.

Wanawe Gamal na Alaa ni wafanyabiashara wakubwa nchini Misri na kabla ya kuzuka maandamano ya hivi majuzi Gamal alitajwa kama Rais mtarajiwa wa siku zijazo.

Kama kawaida taarifa si za uhakika na hazijathibitishwa; lakini si wengi watakaoshangazwa ikiwa familia ya Mubarak itajumuishwa katika fungu moja na familia za Marcos nchini Phillipines na Suharto wa Indonesia kama ni nembo ya ubepari uliokithiri--yaani familia za watawala katika nchi kubwa zinazoendelea ambazo zimefanikiwa kugeuza kuwepo kwao karibu na madaraka kuwa utajiri mkubwa binafsi.
Source: BBC

Friday, February 4, 2011

Best Blogger Tips
Jenerali Ulimwengu na Mchakato wa katiba 2011

Best Blogger Tips
Kasheshe mtaani

Part 1

Thursday, February 3, 2011

Best Blogger Tips
Jennifer Lopez headed to the White House


"American Idol" judge Jennifer Lopez told "Extra's" AJ Calloway she's thrilled to be invited with her husband, Marc Anthony, to watch the Super Bowl with President Barack Obama and the First Family.

"I can't believe it!" Lopez exclaimed at the launch of the Venus Goddess Fund for Education. "I don't know, maybe that's why I don't want to talk about it. I don't even feel like its real!"
What will Lopez bring? "Nothing," she laughed, adding, "I think they're stocked up."

The singer/actress said she doesn't want to go on the record for either team but thinks the Pittsburgh Steelers will win in their game against the Green Bay Packers. "That Roethlisberger, he's a good quarterback!"

Wednesday, February 2, 2011

Best Blogger Tips
Ghasia zachukua sura mpya Misri

Wafuasi wa Rais wa Misri, Hosni Mubarak wamekabiliana na waandamanaji wanaomtaka kiongozi huyo aondoke madarakani katikati mwa mji wa Cairo.

Maelfu ya wafuasi wa Bw Mubarak walimiminika kwenye eneo la Tahrir na kuondoa vizuizi vilivyokuwa vimewekwa na waandamanaji.

Pande hizo mbili zilirushiana maneno kabla ya kuanza kurushiana mawe.

Jeshi ambalo awali lilitoa wito kwa waandamanaji kutawanyika na kurejea katika shughuli zao za kawaida bado halijaingilia kati.

Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinasema maafisa wa polisi waliokuwa wamevalia kiraia walikuwa miongoni mwa baadhi ya wafuasi wa Bw Mubarak waliojitokeza katika eneo la Tahrir.

Mapambano mengine yameripotiwa kwenye mji wa Alexandria.
Source: BBC
Best Blogger Tips
Picture of the Day

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Freeman Mbowe baada ya kukutana nae uso kwa uso katika siku ya maadhimisho ya Sheria nchini leo.

Tuesday, February 1, 2011

Best Blogger Tips
Obama says Egypt's transition 'must begin now'

President Barack Obama warned Tuesday of "difficult days ahead" for Egypt and said the transition following President Hosni Mubarak's earlier announcement that he won't run for re-election in September must begin immediately.

In a brief statement to reporters at the White House, Obama pledged continuing U.S. support for both a longtime ally and the aspirations of protesting Egyptians, whose eight days of growing demonstrations led to Mubarak's dramatic announcement on state television.

"We've borne witness to the beginning of new chapter in the history of a great country and a long-time partner of the United States," Obama said of the Mubarak statement less than three hours earlier.

Noting that he and Mubarak had just spoken by phone, Obama said Mubarak "recognizes that the status quo is not sustainable and a change must take place." Repeating earlier calls for an orderly transition in Egypt from Mubarak's nearly three decades of repressive rule to a fully representative democracy, Obama said the transition "must be meaningful, it must be peaceful and it must begin now."

"Furthermore, the process must include a broad spectrum of Egyptian voices and opposition parties," Obama said."It should lead to elections that are free and fair. And it should result in a government that's not only grounded in democratic principles but is also responsive to the aspirations of the Egyptian people."

Earlier, sources told CNN that a U.S. envoy sent by Obama urged Mubarak to announce he won't run for re-election later this year, a major shift in foreign policy regarding the main Arab ally of the United States and a vital partner in the Middle East peace process because of its 1978 treaty with Israel.
Access the full story...................

Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits