Wednesday, December 28, 2011

Korea Kaskazini yafanya maziko ya Kim Jong - Il

Best Blogger Tips
Korea Kaskazini inafanya maziko ya kitaifa ya kiongozi wake Kim Jong-il huku msafara mkubwa wa magari yaliyosindikiza jeneza la kiongozi huyo ukipitia mji mkuu Pyongyang.

Picha cha runinga zimeonyesha maelfu ya wanajeshi wakitoa heshima za mwisho kwa picha ya kiongozi huyo iliyopitia kwenye barabara za mji.

Mridhi wa uwongozi ambaye ni mwanawe wa kiume Kim Jong-Un amezindikisha jeneza la babake lililokuwa juu la gari maalum. Kim Jong-il alifariki dunia Decemba 17 baada ya kupatwa na mshtuko wa moyo akiwa na miaka 69.

Hakuna viongozi wa nje walioalikwa wala waandishi wa habari wa kimataifa. Wadadisi wanasema mazishi ya leo ni sambamba na ya mwasisi wa nchi hiyo Kim IL-Sung mwaka 1994 yalioandamana na gwaride kubwa ya kijeshi.

Kiongozi mtarajiwa Kim Jon-Un ameandamana na mjombake Chang Song-taek anayetarajiwa kuwa na ushawishi mkubwa katika uwongozi mpya pia mkuu wa jeshi Ri Yong-ho, alionekana kando ya jeneza la Kim Jong-Il.

Kabla ya kufariki kiongozi wa Korea Kaskazini alikuwa katika mchakato wa kumtayarisha mwanawe Kim Jong-Un kuchukua hatamu za uwongozi. Kifo chake cha ghafla cha Kim Jong Il kimepelekea hofu ya kuzuka mzozo wa uwongozi katika taifa hilo lenye msingi wa ujamaa.
Chanzo: BBC

Tuesday, December 27, 2011

Hali ya Hewa: Mafuriko makubwa yanakuja Dar

Best Blogger Tips
Eneo la Jangwani likiwa limezingirwa na maji
Yasema alhamisi hadi Jumamosi kuwa siku mbaya zaidi, pia kuyakumba maeneo mengine nchini. 

 MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetoa tahadhari ya kuendelea kunyesha mvua kubwa zaidi katika siku 10 zijazo, huku ikizitaja Alhamisi hadi Jumamosi kuwa ni siku za mafuriko mengine makubwa zaidi katika jiji la Dar es Salaam.

Wakati TMA ikitoa tahadhari hiyo, Shirika la Reli Tanzania (TRL), limesitisha safari za treni ya abiria kwa muda usiojulikana kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma, kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali ya nchi.

Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk Agnes Kijazi alisema jana katika taarifa yake kuwa kutokana na mvua hizo, ni vyema tahadhari zote zikachukuliwa mapema ili kuepuka maafa zaidi.

“Wale wananchi ambao wanaishi mabondeni na waliokumbwa na mafuriko, wahame kutokana na mvua zinazoanza kunyesha Desemba 27 (jana), hadi Desemba 31 mwaka huu, kwani zitaleta madhara makubwa kwa wanaoishi mabondeni na sehemu nyingine mbalimbali,” alisema Dk Kijazi.

Alisema kwamba ukanda wa mvua unatarajia kuimarika maeneo mengi nchini na mvua zinatarajiwa kuanza kwenye ukanda wa pwani, ikiwemo Mkoa wa Dar es Salaam na kuongezeka kuelekea mwaka mpya wa 2012.

Dk Kijazi alisema mifumo ya hali ya hewa inaonyesha kuimarika kwa hali ya joto katika Bahari ya Hindi na kuongezeka kwa msukumo wa hewa yenye unyevunyevu kutoka misitu ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC).

Alisema hali hiyo imesababisha makutano ya upepo katika eneo la Mashariki na Kusini Magharibi mwa nchi, kuanzia leo kuelekea mwaka mpya... “Hali hii inatarajia kusababisha kuanza kwa vipindi vya mvua kubwa katika maeneo mengi hapa nchini.”

Alisema maeneo ya mikoa ya ukanda wa Pwani (Dar es Salaam, Pwani, Mtwara, Lindi na Unguja), yanatarajiwa kuwa na vipindi vya mvua kubwa.

Dk Kijazi aliyataja maeneo mengine kuwa ni ya Nyanda za Juu Kusini Magharibi ambayo ni Mikoa ya Mbeya, Iringa na Rukwa na Kanda ya Kati katika Mikoa ya Dodoma na Singida.

“Kwa upande wa Magharibi mwa nchi, Mikoa ya Kigoma na Tabora na maeneo machache ya Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki katika Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara, yanatarajiwa kuwa na vipindi vya mvua kubwa,” alisema.

Alisema kutokana na viwango vikubwa vya mvua vilivyonyesha, ongezeko kidogo la mvua linatarajia kusababisha mafuriko na uharibifu wa miundombinu, hivyo ni muhimu tahadhari stahili ziendelee kuzingatiwa.

Msimbazi wagoma
Licha ya tahadhari hiyo ya TMA, baadhi ya wakazi waishio katika Bonde la Mto Msimbazi wamedai kuwa hawataondoka katika nyumba zao zilizokumbwa na mafuriko hadi watakapoona maji yamejaa katika mto huo.

Wakizungumza jana kwa nyakati tofauti wakazi hao walisema hawana pa kwenda licha ya kuisikia tahadhari hiyo ya TMA.

“Ningekuwa mpangaji sawa, sasa mimi nimejenga nitakwenda wapi na kwetu ni mikoani huko,” alisema Ramadhani Kimbuyu wakati akifanya ukarabati wa nyumba yake huku akisisitiza kuwa kipimo chao kitakuwa Mto Msimbazi.

Alisema kosa walilofanya awali ni kupuuza licha ya kuona mto huo umejaa jambo ambalo alidai hawatalirudia... “Tukiona yamejaa tu tunahamia juu relini, yakipungua tunarudi.”

Kauli ya RC
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki amesema Serikali itawachukulia hatua kali watakaokaidi amri ilivyotangazwa na Rais Jakaya Kikwete ya kutorejea katika maeneo hatarishi ya mabondeni.

“Tangu mwaka 1979 Serikali ilitoa amri ya watu kuondoka mabondeni lakini wamekuwa wakikaidi na kuendelea kuishi,  kitendo hicho kimechangiwa na uzembe kwa baadhi ya viongozi katika kutekeleza agizo hilo,” alisema.

Sadiki alisema baadhi ya watu wameanza kurejea kwenye mabonde yaliyoathirika na kuwaonya wasirudi na badala yake watafute maeneo mengine kuendesha makazi yao.

Alisema Serikali itawapatia waliojenga mabondeni viwanja na siyo wapangaji. Wakazi hao wametengewa viwanja katika eneo la Mabwe Pande lililoko mpakani na Bagamoyo, Pwani na kwamba mpaka sasa viwanja 700 vimeshapimwa.

“Baada ya kugawa viwanja hivi tutaanza zoezi la kuzibomoa nyumba walizokuwa wanaishi maeneo ya mabondeni ili kutoruhusu watu kurudi tena huko kwani bila kufanya hivyo, hatutafanikisha lengo hilo,” alisema Sadiki.

Treni zatishwa
Kutokana na mvua kubwa zinazonyesha maeneo mbalimbali nchini wa TRL, jana ulitangaza kusitishwa kwa safari za treni ya abiria kutoka Dar es Salaam hadi Kigoma... “Safari hizo zimesitishwa hadi itakapotangwa vinginevyo baadaye,” alisema Meneja Uhusiano wa TRL, Midladjy Maez.

Alisema abiria wote waliokuwa wamepanga kusafiri jana na katika treni zijazo, wanatakiwa kufika na tiketi zao katika ofisi za Stesheni Masta wa kituo husika ili warejeshewe fedha zao.

Walia na huduma mbovu
Waathirika wa mafuriko waliopo katika Kituo cha Hananasifu, Kinondoni Dar es Salaam, wamelalamikia uongozi wa kituo hicho kutoa huduma za chakula na malazi usiku bila umeme.
Wakizungumza kambini hapo jana waathirika hao walisema, uongozi unatoa huduma hizo waathirika kuanzia saa 4:00 hadi saa 6:00 usiku kitendo ambacho kinafanya baadhi yao wapoteze vifaa vyao.Kambi ya Hananasif imeshapoteza magodoro 50, ambayo inaelezwa na wananchi hao kuwa waliohusika ni baadhi ya viongozi waliopewa dhamana ya kuhudumia eneo hilo.

“Hapa kituoni hatuna umeme, lakini utaona viongozi wanakaa  kimya mpaka ifike saa nne ndipo wanaanza kugawa magodoro, wengine wakishirikiana na vibaka usiku  kuhamisha baadhi ya magodoro kupeleka mahali kusikojulikana,” alisema Hamed Shaban.

Habari hii imeandikwa na Boniface Meena, Keneth Goliama na Aidan Mhando, Pamela Chilongola, Joseph Zablon, Ibrahim Yamola.
Chanzo: Mwananchi

Maji ni Dawa kubwa Lakini Hatujui!

Best Blogger Tips
Kheri ya Krismasi mpenzi msomaji, natumaini umekula, umekunywa na umefurahia maisha, sasa ni wakati wa kuutibu mwili wako kama baada ya kula na kunywa kwenye sikukuu hii vimekuletea ‘mgogoro’ tumboni.

Bila shaka kila mtu anafahamu umuhimu wa maji, lakini si watu wote wanafahamu kuwa maji ni dawa pia, licha ya kutumika kwa ajili ya kunywa ili kukata kiu.

Nchini Japan na nchi nyingine nyingi za Bara la Asia, ni jambo la kawaida kwa watu wake kunywa maji kwanza asubuhi kabla ya kula kitu chochote.
Tabia hii ina faida kubwa kwa afya ya binadamu na hata utafiti wa kisayansi uliofanywa, umethibitisha thamani ya maji katika kuponya, kuzuia au kudhibiti magonjwa kadhaa yanayosumbua watu wengi.

Chama Cha Madaktari wa Japan (Japanese Medical Society) kimethibitisha kuwa maji yana uwezo wa kutibu, kwa asilimia 100, magonjwa sugu na maarufu yafuatayo, iwapo mtu atafuata kanuni na taratibu za kunywa maji hayo kama tiba:
Kuumwa kichwa, maumivu ya mwili, mfumo wa moyo, moyo kwenda mbio, kifafa, uzito mkubwa, pumu, kifua kikuu, uti wa mgongo, ugonjwa wa figo, magonjwa ya mkojo, kutapika, vidonda vya tumbo, kuharisha, kisukari, saratani, ukosefu wa choo, matatizo ya macho, tumbo, hedhi, sikio, pua, nk.

JINSI YA KUTUMIA MAJI KAMA TIBA
Ili maji yatumike kama tiba, kunywa kiasi cha lita moja na robo (glasi nne kubwa) za maji safi na salama (yasiwe maji baridi) asubuhi na mapema kabla ya jua kuchomoza na kabla ya kupiga mswaki.

Baada ya kunywa kiasi hicho cha maji, usile wala kunywa kitu kingine hadi baada ya dakika 45 au saa moja. Baada ya muda huo, sasa unaweza kusafisha kinywa na kula mlo wako wa asubuhi kama kawaida.
Aidha, mara baada ya kula mlo wako wa asubuhi, usile wala kunywa kitu chochote hadi baada ya muda wa saa mbili kupita. Hivyo hivyo utafanya baada ya mlo wako wa mchana au jioni.
Kwa wale wagonjwa ambao hawawezi kunywa kiasi cha maji cha lita 1 na robo kwa wakati mmoja, wanaweza kuanza kwa kunywa na kiasi kidogo watakachoweza na kuongeza taratibu hadi kufikia kiwango hicho cha glasi nne kwa siku.
Utaratibu huu wa kunywa maji ulioelezwa hapo juu, una uwezo wa kutibu maradhi yaliyotajwa hapo awali na kwa wale ambao hawana maradhi yoyote, basi wataimarisha afya zao zaidi na kujipa kinga itakayowafanya waishi maisha yenye afya bora zaidi.

UNAWEZA KUPONA BAADA YA MUDA GANI?
Yafuatayo ni baadhi ya magonjwa na idadi ya siku zake za kupona zikiwa kwenye mabano kama ilivyothibitishwa na watafiti:
Shinikizo la damu (High Blood Pressure) (siku 30), vidonda vya tumbo (siku 10), kisukari (siku 30), saratani (siku 180) na kifua kikuu (siku 90).
Kwa mujibu wa watafiti, tiba hii haina madhara yoyote, hata hivyo katika siku za mwanzo utalazimika kukojoa mara kwa mara. Ni bora kila mtu akajiwekea mazoea ya kunywa maji kwa utaratibu huu kila siku katika maisha yake yote ili kujikinga na maradhi mbalimbali.
KUNYWA MAJI ILI UWE NA AFYA NJEMA NA UBAKI MCHANGAMFU SIKU ZOTE!
Chanzo: Global Publishers

Saturday, December 24, 2011

Nawatakia Sikukuu Njema

Best Blogger Tips

Friday, December 23, 2011

Hameni -JK

Best Blogger Tips
Mafuriko Jijini Dar-es-salaam
 RAIS Jakaya Kikwete amewahakikishia waathirika wa mafuriko ya mvua zinazoendelea kunyesha kwa siku tatu mfululizo sasa, kuwa Serikali itawapa msaada wa hali na mali, lakini
lazima wahame mabondeni.

Amesema Serikali ipo tayari kuwatafutia maeneo ya kujenga makazi ya kudumu na kwa dharura iliyopo kuwapa hifadhi ya mahema, vyakula, magodoro, vyoo, maji na huduma ya afya kama ilivyofanyika, lakini haina msamaha juu ya wao kuendelea kuishi mabondeni.

“Wenzetu wa hali ya hewa wanasema mvua hizi zinaendelea, Makamba (Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kabla ya Abbas Kandoro) aliwahamisha kwa helikopta, sasa Sadiki (Said Mecky-Mkuu wa Mkoa wa sasa) naye anawahamisha vivyo hivyo, hivi hali hii tutaiacha ijirudie mpaka lini?.....

“Ni vizuri mjiondoe kwenye maisha ya mashaka, nawahakikishia Serikali yenu ipo nanyi katika hali ngumu hii, lakini ni vizuri muondoke maeneo hayo ya hatari, suala kubwa ni mnahamaje?

Kamati ya Maafa ya Mkoa ihakikishe hilo linatekelezwa kwa ubora na mapema,” alisema Kikwete akizungumza na waathirika hao.

Alizungumza na waathirika walio katika Kambi ya Mchikichini, wilayani Ilala, wapatao 1,900 kwa niaba ya waathirika wengine wa kambi nyingine saba zilizowekwa katika shule za sekondari na msingi kwa hifadhi.

Kabla ya kuzungumza nao, Rais Kikwete alipata nafasi ya kuzunguka kwa helikopta kuona athari za mafuriko hayo katika jiji na pia kutembelea kambi hiyo.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, watu zaidi ya 20 wamepoteza maisha na 4,900 wameathirika kwa kukosa makazi.

Aidha, vifo zaidi havijaripotiwa kwa kuwa bado baadhi ya nyumba zimezingirwa na maji na matope.

Akihutubia hadhara hiyo, Rais alisisitiza watu kuheshimu mikondo ya maji kwa kuwa hakuna mwanadamu anayeweza kuzuia maji, upepo au moto na kutolea mfano kwa Marekani, Australia na nchi zenye teknolojia ya juu, lakini maji huwashinda.

Rais Kikwete aliwaagiza Mipango Miji wafanye kazi ipasavyo kwa kuwa wao ndio wamekuwa vinara wa kugawa maeneo kwa hati halali wakati wakijua wazi ni maeneo hatari kwa maisha ya watu, mabondeni na kwenye mikondo ya maji.

“Maji hayana tajiri wala masikini, nilikuwa napita kwa helikopta nikaona hata kwenye kampuni ile Jangwani (Kajima) ukuta umeenda, Mipango Miji fanyeni kazi vizuri kuepusha yanayoweza kuepukika, mikondo ya maji iachwe nafasi, baadhi ya hawa watu wana hati halali, mmewapa ninyi,” alisema Rais.

Aidha, aliwahakikishia waathirika hao kufuatiliwa kwa karibu suala lao na kuwaahidi kuwa viongozi wakiwemo mameya, wabunge, madiwani na watendaji wahakikishe usiku na mchana watawahudumia mpate makazi maeneo yafaayo.

Awali, akihutubia, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sadiki alisema walioathirika ni 4,900 na vifo vilivyoripotiwa mpaka jana asubuhi ni 20 ambapo miili 18 imetambuliwa na miwili bado ipo Hospitali ya Taifa Muhimbili, aliwataka watu wakatambue miili hiyo.

Katika hotuba yake, Sadiki alisema uongozi wa mkoa kwa kushirikiana na viongozi wa kisiasa wamefikia hitimisho la kuwataka wakazi hao wa mabondeni kuridhia kuhama baada ya kutenga eneo katika Wilaya ya Kinondoni la ekari 2,000 linalotoa viwanja 2,800 ili wakazi hao waanze kujenga makazi mapya.

“Lakini tuna taarifa huko nyuma kwamba kuna waliopewa maeneo Wazo Hill, Yombo Dovya, hawakuhamia huko, wakauza na hata hizi huku wakauza, muda si mrefu shule zitafunguliwa hivyo tutahakikisha mnapata hifadhi ya dharura huko ili tuwapishe wanafunzi huku,” alisema Sadiki.

Kwa mujibu wake, kuna kambi zaidi ya saba jijini Dar es Salaam na vitu mbalimbali vimetolewa na wasamaria wema, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Polisi yakiwemo mahema, vyakula, nguo, dawa na mikeka. Mbunge wa Ubungo, John Mnyika ametoa vitu vyenye thamani ya Sh milioni moja kwa kambi tano.

Gazeti hili lilitembelea katika baadhi ya kambi hizo kwa lengo kujionea hali ilivyo ambapo katika kituo cha Rutihinda, hadi saa 5.45 asubuhi, waathirika 52 waliokuwa wameandikishwa walilalamika kutokuwepo kwa huduma yoyote ikiwemo ya chakula, na magodoro tangu wafike kambini hapo juzi asubuhi.

Akizungumzia suala hilo, msimamizi wa kambi hiyo ambaye pia ni Mtendaji wa Kata ya Kigogo, Kassim Mbezi, alisema iliwalazimu baadhi ya waathirika kuondoka na kujitafutia hifadhi na chakula.

Walikuwa zaidi ya 100 kambini hapo na kubaki hao 52. “Hadi hivi sasa watu waliopo hapa ni 52, awali waliokuwepo wengi lakini wanapokuja na kukuta hali ya kambi ilivyo wanaamua
kuondoka na kurudi katika maeneo waliyotoka na wengine kwenda kujitafutia chakula kwa kuwa wana watoto,” alisema Mbezi.

Alipotafutwa Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuf Mwenda kwa lengo la kuzungumzia tatizo la kambi hiyo, alisema idadi kamili ya waathirika ndiyo kikwazo cha kufikishwa mapema kwa misaada hiyo na hadi kufikia muda huo, tayari walishaipata idadi yao hivyo utaratibu wa kuwafikishia misaada ulikuwa ukiendelea.

Kambi ya Azania iliyopo Manispaa ya Ilala iliyo na waathirika 426, hali ilikuwa ikiendelea vizuri na waathirika wote kupata mahitaji yao muhimu ikiwemo ya vyakula vilivyotolewa na taasisi mbalimbali na wasamaria.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa ya Kata ya Kariakoo, Mathias Muyenjwa, alisema ukiacha kituo hicho vituo vingine vilivyopo katika Kata ya Kariakoo na idadi ya waathirika katika mabano ni Mtambani A (343), Mtambani B (1,340) pamoja na Kariakoo Kaskazini yenye waathirika 302.

Kuhusu hali ya kambi hiyo, Muyenjwa alisema huduma mbalimbali zinaendelea kutolewa kwa waathirika ikiwemo ya afya huku akiitaja misaada iliyotolewa na kuwa ni michele, mikate, maji ya kunywa, juisi, mafuta ya kula, sabuni, mablangeti, mashuka pamoja na nguo za kawaida.

Baadhi ya waliotajwa kufa kutokana na mvua hizo ni Tulihama (65) mkazi wa Ubungo Msewe, Maganga Said (8) mwanafunzi wa Shule ya Msingi Kanjenje Tabora, Gathi Mseti (30) na mwanawe Thomas Rashid (8) wakazi wa Kipunguni, Vian Maxmilian (13) mkazi wa Mburahati, Magreth Makwaya (6), mkazi wa Luhanga, Ibrahim Lusuma(60), mkazi wa Ubungo Msewe.
Chanzo: HabariLeo

Monday, December 12, 2011

Raia wa Afrika Kusini 'auliwa' China

Best Blogger Tips
China imempa adhabu ya kifo mwanamke mmoja raia wa Afrika kusini kwa kufanya biashara haramu ya kusafirisha dawa za kulevya, ikikataa ombi la Rais Jacob Zuma la kumwachia. 

Janice Bronwyn Linden, mwenye umri wa miaka, 38, aliuliwa zaidi ya miaka mitatu baada ya kukamatwa.

Mashirika ya kutetea haki za binadamu tayari yamekuwa yakilaani China mara kwa mara kwa kutekeleza sheria ya hukumu ya kifo, yakisema mfumo wake wa sheria hauna haki.

Serikali ya Afrika Kusini imesema hatua hiyo haitoathiri mahusiano ya karibu ya kidiplomasia na China.

Serikali ya China iliwaruhusu dada zake wawili Bi Linden kukaa naye kwa saa nzima kabla ya kutekeleza hukumu hiyo kwa sindano ya sumu, gazeti binafsi la Afrika Kusini e. News, likimnukuu mwandishi kutoka China.

'Haijashughulikiwa vya kutosha'

Bi Linden alikamatwa Novemba 2008 baada ya kukutwa na kilogramu tatu za methamphetamine alipowasili uwanja wa ndege mjini Guangzhou kusini mwa nchi hiyo.

Aliendelea kutetea nafsi yake, akisema dawa hizo za kulevya zilitumbukizwa kwenye sanduku lake bila yeye kujua.

Hata hivyo, mahakama kuu ya Guangdong na ya rufaa huko Beijing zilikataa rufaa yake.

Msemaji wa idara ya uhusiano wa kimataifa, Clayson Monyela, aliiambia BBC kuwa Bw Zuma aliingilia kati kutaka hukumu hiyo ibadilishwe na apewe kifungo cha maisha.

Bw Monyela alisema, "Tumefanya kila namna kumnusuru hata katika nyanja zote za juu."

Alisema, serikali ya China itakabidhi majivu yake kwa familia yake, kufuatia kuchomwa maiti yake, kulingana na makubaliano yaliyofanywa baina ya mataifa hayo mawili.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa upinzani wa chama cha Democratic Alliance (DA) wa Afrika Kusini, Stevens Mokgalapa, amesema serikali haikufanya vya kutosha kuokoa maisha ya Bi Linden , gazeti binafsi la Afrika kusini Times Lives limeripoti.


Saturday, December 10, 2011

Vitambulisho vya Taifa bure

Best Blogger Tips
KILA Mtanzania atakuwa na kitambulisho cha Taifa kufikia mwaka 2015 ambacho kitatolewa bure na Serikali, na tayari watumishi wa umma wameanza kujaza fomu za utambuzi na usajili na ifikapo Aprili mwakani, watakuwa na vitambulisho hivyo, imefahamika.

Kwa mujibu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), baada ya wafanyakazi wa Serikali, watafuatiwa wanafunzi, wafanyabiashara na hatimaye umma kwa ujumla utafikiwa na kazi hiyo muhimu kwa Taifa.

Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dickson Maimu akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali
vya habari Dar es Salaam jana kuhusu maendeleo ya mradi wa vitambulisho vya Taifa, alisema
ingawa vitatolewa bure, kwa ye yote atakayepoteza atalazimika kuvilipia.

Mradi mzima unatarajiwa kugharimu kiasi cha Sh bilioni 350.

Maimu alisema ni lengo la Serikali kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa na kitambulisho cha
Taifa ifikapo mwaka 2015 na hilo litasaidia kuboresha Daftari la Kudumu la Wapigakura, na hivyo kuipunguzia mzigo mkubwa Serikali katika kuboresha daftari hilo kila wakati wa uchaguzi unapowadia.

“Kwa kuwa zoezi la utambuzi na usajili litafanyika kwenye maeneo yenu nawaomba mtoe
ushirikiano wa kutosha kwa wananchi wote na niwakumbushe kuwa huduma hii ni bure
kwa mujibu wa maagizo ya Baraza la Mawaziri, na hivyo Serikali haitarajii mtendaji yeyote kuomba au kupokea chochote au kuweka tozo.

“Tunawasihi wananchi na wageni, wasikubali kudanganywa au kulipa fedha zozote kwani
kitambulisho ni bure na huduma zote zinazoambatana na zoezi hili ni bure. NIDA haitasita
kuchukua hatua za kisheria kwa ye yote atakayebainika kukiuka uratatibu huu.”

Alisema wameanza na wafanyakazi wa Serikali kwa sababu vitambulisho kwao si tatizo kwa maana ya mfumo walionao una urahisi katika kuwashughulikia, lakini zaidi, itasaidia katika kudhibiti watumishi hewa.

“Hawa kwao kitambulisho kwao kidogo si tatizo, kwani wana mifumo mizuri na hawa tunataka kuwatumia kama majaribio kwa mradi huo. Lakini zaidi, itasaidia katika kudhibiti tatizo la watumishi hewa serikalini,” alisema Maimu na kuongeza kuwa watafuata wanafunzi kwa sababu ya kusaidia katika suala la mikopo ya elimu ya juu na kwa wafanyabiashara ili kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi na kusaidia kuongeza mapato.

“Kutokana na ratiba yetu ya utekelezaji, tutaanza kutoa vitambulisho kwa awamu ya kwanza
mwezi Aprili 26, 2012 wakati wa maadhimisho ya sherehe za Muungano kwa watumishi wa
Serikali ambao tayari usajili umeanza,” alieleza Maimu na kuongeza kuwa katika utekelezaji wa mradi huo, Mamlaka itatoa vitambulisho katika makundi matatu; Watanzania, wageni wakazi na wakimbizi.

“Tutatoa vitambulisho hata kwa mwizi, kwa sababu moja ya faida kuu za mradi huu ni kudhibiti
suala la usalama wetu kwa kila pointi. Ndiyo maana dhana kuu ya mfumo huu inatakiwa ijibu maswali makuu manne; nani ni nani; yuko wapi; anamiliki nini na anafanya nini”alieleza mkurugenzi huyo.

Aliongeza kuwa vitambulisho hivyo katika eneo la usalama, vitasaidia kuimarisha usalama
wa raia na mali zao na kupunguza vitendo vya uhalifu na hasa unaofanywa na raia kutoka
nchi jirani na wafungwa waliomaliza adhabu zao au kuachiwa huru kwa msamaha wa Rais.

“Ni wazi kuwa udhibiti wao umekuwa mgumu kutokana na kushindwa kuwatambua. Pia itasaidia kuweka kumbukumbu za matukio ya uhalifu katika daftari,” alisema Mkurugenzi Mkuu wa NIDA.

Alisema baada ya usajili kukamilika, jukumu kubwa litakalofuatia ni uhakiki wa taarifa za makazi, umri na uraia wa mwombaji aliyesajiliwa ili kupata uhakika wa taarifa zake kwa lengo la kumpatia kitambulisho kinachowiana na kundi lake.

Katika udahili, mwombaji atatakiwa kuthibitisha kama amekuwa akiishi Tanzania kwa kipindi kisichopungua miezi sita; uthibitisho wa umri wa miaka 18 na uthibitisho wa uraia wake.

Aidha, viambatanisho muhimu vitahitajika ambavyo ni cheti cha kuzaliwa; cheti cha ubatizo/falaki; kitambulisho cha Mpigakura; pasipoti ya Tanzania na cheti cha kuhitimu elimu ya msingi.

“Jukumu hili ni la muhimu sana na linatakiwa kufanywa kwa umakini mkubwa bila kuharakishwa kwani uharaka kidogo tu unaweza kabisa kuharibu zoezi zima,” alifafanua
mkurugenzi huyo.

Alisema ili kufanikisha kazi hiyo, wanashirikiana kwa karibu sana na Serikali za Mitaa kwa
lengo la kutambua makazi halali ya mwombaji; Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kwa lengo la kutambua umri wa mwombaji na Idara ya Uhamiaji kutambua na kubaini uraia wa
mwombaji.

Aidha, alisema katika mkutano ujao wa Bunge, wanatarajiwa utapelekwa muswada wa
mabadiliko ya sheria ambayo itakuwa ni lazima kwa kila mtu anayeishi nchini, kuwa na kitambulisho hicho cha kudumu ambacho kadi yake itakuwa ni ya miaka 10.

NIDA imeingia mkataba na mkandarasi wa vitambulisho hivyo, Kampuni ya IRIS Corporation
Berhad ya Malaysia tangu Aprili 21, mwaka huu.

Mshauri mwelekezi wa mradi huo ni Kampuni ya Gotham International Ltd (GIL), na tayari Mamlaka hiyo imepata viwanja katika wilaya zote nchini kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya ofisi za usajili wilayani wakati kituo kikuu cha kuhifadhi takwimu zote za nchi kitakuwa Kibaha, Pwani.

Maimu alisema kulikuwa na uchelewaji wa kutoa fedha kwa mkandarasi kuanza kazi, lakini
tayari Oktoba mwaka huu amekabidhiwa fedha hizo baada ya kuidhinishwa na Bunge na tayari
ameleta mashine kuanza kazi ya mradi huo uliosubiriwa kwa zaidi ya miaka 15 sasa na kugubikwa na maneno mengi katika mchakato wake.
Chanzo: HabariLeo

Wednesday, December 7, 2011

Saadi Gaddafi 'ajaribu kupenya Mexico'

Best Blogger Tips
Saad Gaddafi
Serikali ya Mexico imesema imezuia njama iliyokuwa ifanywe na kundi la wahalifu la kumpenyeza kwa magendo mmoja wa watoto wa aliyekuwa kiongozi wa Libya Kanali Muammar Gaddafi nchini Mexico. 

Saadi Gaddafi amekuwa kwenye kifungo cha nyumbani nchini Niger iliyopo Afrika Magharibi tangu alipoikimbia Libya mwezi Septemba.

Msemaji wa serikali ya Mexico alisema Saadi Gaddafi na baadhi ya wanafamilia wake walizuiwa kutokana na matokeo ya ripoti za kijasusi.

Watu wengi wamekamatwa kutokana na tukio hilo.

Maafisa wa Mexico wamsema jaribio hilo- lililoibuliwa Septemba 6- lilihusisha majina na nyaraka za uongo.

Nyumba salama

Waziri wa mambo ya ndani Alejandro Poire alisema mpango huo unahusisha mtandao wa uhalifu " mkubwa wa kimataifa", lakini ikagundulika mwezi Septemba kabla ya mpango huo kukamilika.

Mtandao huo ulihusisha watu kutoka nchi mbalimbali, ikiwemo Mexico, Denmark na Canada, Bw Poire aliuambia mkutano wa waandishi wa habari huko Mexico.

Alisema, walikuwa wakinunua nyumba zenye salama na kufungua akaunti za benki.

Tarehe 14 Septemba- siku nane baada ya njama hiyo kugundulika- Niger ilisema Saadi Gaddafi, mwenye umri wa miaka 38, aliwasili mjini Niamey.

Iliripotiwa kuwa alisafirishwa kwa ndege ya kijeshi kutoka mji wa Agadez kaskazini mwa nchi hiyo.

Septemba 29, Shirika la polisi la kimataifa, Interpol lilitoa " hati ya kukamatwa" kwa Saadi Gaddafi, wakitaka nchi wanachama imkatae iwapo atatokea kwenye nchi zao.

Wakala wa polisi wa kimataifa wamesema anatakiwa kwa madai ya kutoa vitisho kwa kutumia silaha alipokuwa mkuu wa shirikisho la mpira la Libya.

Saadi Gaddafi, ambaye alikuwa akicheza soka katika ligi kuu ya Italia Serie A, pia amewekewa vikwazo vya kusafiri na mali zake kutiwa tanji chini ya azimio la baraza la usalama la umoja wa mataifa lililopitishwa mapema mwaka huu.
 Chanzo: BBC

Tuesday, December 6, 2011

Jose Chameleone adhihirisha ubilionea

Best Blogger Tips
Jose Chameleone
 HAKUNA ubishi kwamba, unapotaja jina la Jose Chameleone, moja kwa moja akili itakuelekeza kwa msanii anayeporomosha muziki wenye mvuto, uliochanganywa na vionjo vya kiasili kutoka kwa nyota huyo raia wa Uganda.

Amekuwa akikonga nyoyo za mashabiki wa ndani na nje ya Afrika Mashariki kwa takribani miaka 12 sasa.

Bila kutafuna maneno, yafaa kueleza kuwa, ndani ya kipindi hicho Chameleone ambaye jina lake halisi ni Joseph Mayanja, hajachuja.

Na ndiyo maana kila kukicha, nyota ya msanii huyo inazidi kung’ara, hali kadhalika kipato chake kikizidi kuimarika kiasi cha kumfanya mmoja wa vijana wenye uwezo mkubwa kifedha nchini Uganda.

Nyota huyo aliyezaliwa miaka 33 iliyopita ameshavuka katika daraja la umasikini, sasa akiogelea fedha.

Ndiyo, kwa asiyeamini, hebu angalau baadhi ya mambo yanayothibitisha utajiri wa nyota huyo.

Anamiliki jumba la kifahari katika vilima vya Sekuku jijini Kampala, pia ana nyumba huko Arizona, Marekani, achilia ile ya Kigali, Rwanda aliyoinunua hivi karibuni kwa mamilioni ya shilingi.

Ukiachilia mbali gari la kisasa aina ya Cadillac Escalade lililomgharimu zaidi ya Sh milioni 100, Chameleone ambaye ni baba wa watoto watu, pia anamiliki Mercedes Benz, BMW na aina nyingine za magari.

Kwa ujumla, anakadiriwa kuwa na utajiri unaofikia Sh bilioni 1.5 kwa fedha za Tanzania. Na anasema bado anazisaka, kwani bila ya kuwa na tamaa ya kusaka mafanikio zaidi, ndoto huenda zisitimie.

Anayasema hayo akisisitiza kuwa, baada ya nyumba, magari na akaunti nono benki, sasa ana ndoto za kumiliki helikopta yake, baada ya kuwa amekuwa akikodi mara kadhaa ama kwenda katika matamasha au kama alivyofanya wakati anamuoa mkewe Daniela Atim.

Je, ni nini siri ya mafanikio ya nyota huyu kipenzi cha wengi Afrika Mashariki na Kati? Mwenyewe, amekaririwa mara kadhaa akisisitiza kuwa, ni kujituma na kuuchukulia muziki kuwa ni kazi.

“Bila kujituma, hakuna maendeleo. Nimehangaika sana kuyatafuta maendeleo, na hata baada ya kuyapata, sijabweteka. Nafanya kazi usiku na mchana huku nikihakikisha kila shilingi ninayoingiza inazidi kuniinua kimaisha,” anasema nyota huyo mwenye utitiri wa tuzo za ndani na nje ya Uganda.

Ubora wa nyimbo kama Kipepeo, Mama Rhoda, Jamila, Mambo Bado, Mama Mia, Shida za Dunia, Fitina Yako, Haraka Haraka, Ndivyo Sivyo aliomshirikisha Joseph Haule `Profesa Jay’ wa Tanzania, ni baadhi ya kielelezo cha kipaji cha kipekee cha muziki kwa Chameolen, msanii mwenye umbo dogo lakini anayetajwa kuwa mkorofi.

Je, mwenyewe anazungumziaje kuhusu ukorofi? Anasema: “Hata wewe ukiniangalia utaamini kuwa mimi ni mkorofi?

Mara nyingi nasingiziwa ili watu wengine wafanye biashara…” Je, alitokea wapi kimuziki? Ni historia ndefu, lakini kwa kifupi itoshe kusema kwamba, alianzia mwaka 1994 akiwa mchezesha disko katika klabu ya usiku ya Maganjo Mizuri, wakati huo akiwa mwanafunzi wa sekondari jijini Kampala.

Na aliwahi kuajiriwa Rwanda katika klabu ya usiku ya Cadillac mara tu baada ya kuhitimu elimu ya sekondari.

Kwa umahiri wake , mbali ya kumwingizia fedha nyingi, amebahatika pia kuzuru Ulaya, Marekani na hata Mashariki ya Mbali kwa shughuli za kimuziki, achilia heshima ya kutumbuiza wakati wa fainali za Kombe la Dunia zilizofanyika Afrika Kusini mwaka jana.

Katika familia yao, Jose ni mtoto wa nne kati ya saba ambayo ina msichana mmoja. Anakumbuka alisoma Shule ya Msingi Nakasero, Sekondari ya Mengo na Sekondari ya Kiislamu ya Kawempe.

“Ingawa nilifaulu kiasi cha kutakiwa kujiunga chuo kikuu, niliamua kuzama katika muziki. Na sijakata tamaa au kuahirisha, ipo siku nitasoma chuo kikuu na kuitwa msomi,” anasema nyota huyo ambaye wazazi wake walitaka asome na kuwa daktari, lakini akakacha masomo kwa muda.

Hata hivyo anasema kuwa, ingawa aliwaudhi wazazi wake, bado anashukuru kwamba yeye ni daktari wa muziki anayewakuna wengi, ikiwa pamoja na wazazi wake.

“Hatuna uhasama tena kwa sababu kama ni maisha nimeyashika, kwa hivyo nimewafuta machozi wazazi wangu ambao awali waliamini labda ndiyo nilikuwa napotea kimaisha.”

Baadaye alihamishia makazi yake Nairobi, Kenya alikoishi maisha ya kubahatisha, alilazimika kulala studio hadi alipookolewa na Dorotea ambaye jina lake halisi ni Griet Onsia.

Anakumbuka akiwa na Bebe Cool na Redsun alipata fursa ya kutumbuiza katika shindano la kumsaka Mrembo wa Kenya.

Anakiri hapo ndipo milango ya neema ilipoanza kufunguka. Anasema Dorotea, baada ya kuzoeana alimshawishi ahamie nyumbani kwake badala ya kuendelea kulala studio, ushawishi ambao ulimchukua zaidi ya wiki moja kumkubalia.

“Nilipohamia tulikuwa marafiki, lakini mengine yaliibuka tukiwa katika nyumba moja. Mara nyingi kila akitoka, alinikuta nimetulia naandika nyimbo, huku akihoji ni lini nitarekodi. Nilikosa jibu kwa kuwa siku wa na fedha.

“Siku moja akiwa safarini huko Afrika Magharibi aliniachia bahasha yenye dola za Kimarekani 1,000 (karibu Sh milioni 1.8 za Tanzania kwa sasa), akaniambia niingie studio.

“Huo ukawa mwanzo wa kibao Mama Mia na sikuamini kama fedha ile ingebadilisha maisha yangu na kunifikisha hapa nilipo. Mengine yanabaki kuwa historia,” anasema.

Pamoja na utajiri aliovuna kupitia muziki, nyota huyo anasema historia ya kushuhudiwa `Live’ na watu zaidi ya bilioni 9 akitumbuiza wakati wa Kombe la Dunia kwake ni kitu cha kipekee.

“Mtoto wa Afrika tena Afrika Mashariki kupewa heshima ile haikuwa kitu kidogo. Najiona mwenye bahati na ni mastaa wachache wanaweza kuingia katika kundi la bahati hata wangeishi kwa miaka 1000.”

Anasema kutokana na baraka alizopata maishani, ameamua kuanzisha taasisi ya Chameleone ili aweze kuwasaidia wasiojiweza.

“Nikiwa mdogo sikuwa na maisha mazuri, sikutoka katika familia bora, kwa hiyo ninajiona mwenye wajibu wa kuwasaidia wengine wakianzia katika misingi mizuri ya kielimu. “Nimeshanunua eneo kwa ajili ya kujenga kituo.

Nataka jamii siku moja inikumbuke kwamba niliwika na kuitangaza nchi yangu, lakini pia sikuwa mchoyo, bali niliyatumia vyema matunda ya muziki.

Kwa kufanya hivi, naamini ipo siku nitawashawishi wengi kufanya mambo makubwa kwa ajili ya jamii wanayotoka.”

Huyo ndiye Joseph Mayanja ambaye pamoja na misukosuko ya maisha tangu akiwa shule hadi sasa akiwa staa, bado nyota yake inang’ara.

Je, atazidi kupata mafanikio? Bila shaka ni jambo la kusubiri na kuona, hasa ikizingatiwa kuwa, mwenyewe amejijengea falsafa ya kutolewa sifa, bali kazi kwa kwenda mbele.

Pamoja na yote, Chameleone anapaswa mfano wa kuigwa kwa wasanii wengi wa Kitanzania ambao huvuma kwa muda mfupi, lakini wakishazikamata fedha hupotelea kwenye ulimwengu wa anasa na baadaye kujikuta wakiwa `choka mbaya’, tena wakiwa hawana akiba benki wala hawajawekeza.
Chanzo: HabariLeo

Wednesday, November 30, 2011

Wahusika wa kashfa ya BAE TZ kushtakiwa

Best Blogger Tips
Kampuni ya BAE Systems ya Uingereza
 Kundi la wabunge kutoka vyama mbali mbali vya siasa nchini Uingereza limetoa wito wa kufunguliwa mashtaka dhidi ya mtu yeyote aliyehusika katika kashfa ya ufisadi na rushwa kuhusiana na mauzo ya rada yaliyofanywa na kampuni ya vifaa vya ulinzi ya BAE Systems ya Uingereza.

Kampuni ya BAE Systems tayari imekubali kulipa takriban dola millioni 46 kama fidia kwa Tanzania kwa kukosa kuweka kumbukumbu zake za mahesabu kuhusiana na mauzo hayo yenye utata.

Lakini kamati ya maendeleo ya kimataifa ya bunge la Uingereza imeishutumu kampuni hiyo kwa kuchukua muda mrefu kurejesha kiasi cha fedha ilichozidisha katika mauzo ya rada hiyo.

Kiasi kikubwa cha fedha kilichotozwa na kampuni ya BAE system ya Uingereza iliyoiuzia Tanzania rada ya kijeshi kilichochea kufanyika kwa uchunguzi dhidi ya kampuni hiyo.

uchunguzi

Uchunguzi huo ulifanywa na Shirika la Kupambana na Ufisadi la Uingereza, Serious Fraud Office.

Mwaka jana, baada ya BAE kukiri kushindwa kutunza kumbukumbu zake kuhusu mauzo hayo, kampuni hiyo ilikubali kulipa kiasi cha dola milioni 46 kwa Tanzania kama fidia ya mauzo kutokana na ulaghai uliofanyika.

Fedha hizo zilikubalika zitumike kununulia vitabu vya shule na vifaa vingine.

Lakini bunge la Uingereza limesikitishwa kuwa fedha hizo bado hazijalipwa.

BAE systems inasema kwa sasa inawasiliana na shirika la misaada la kimataifa la Uingereza kuona namna fedha hizo zitakavyotumika.

Japokuwa BAE systems haikupatikana na hatia ya rushwa, lakini watu binafsi waliohusika na kashfa hiyo wanaweza kushitakiwa.

Wabunge wa Uingereza wamesema wako tayari kushirikiana na serikali ya Tanzania katika mahakama zake kuendesha mashtaka dhidi ya watu wanaohusika na ulaghai huo.
Chanzo: BBC

Saturday, November 19, 2011

Orodha ya watu matajiri Afrika yatolewa

Best Blogger Tips
Jarida la Forbes limechapisha orodha ya kwanza ya watu matajiri barani Afrika.

Wa kwanza ni mfanyabiashara kutoka Nigeria Aliko Dangote mwenye kumiliki kampuni za saruji ambao utajiri wake unazidi dola za kimarekani bilioni 10.

Nicky Oppenheimer mwenyekiti wa kampuni ya madini ya almasi nchini Afrika Kusini, De Beers ni wa pili.

Orodha hiyo ya Forbes ina majina ya watu 40 matajiri zaidi barani Afrika ambapo utajiri wa hao wote kwa pamoja unafikia zaidi ya dola bilioni 65.


40

Paul Harris

25061
39

Markus Jooste

26050
38

Mohamed Bensalah

27041
36

Cyril Ramaphosa

27559
36

Giovanni Ravazzotti

27568
34

Adrian Gore

28047
34

Strive Masiyiwa

28051
33

Michiel Le Roux

29062
31

Chris Kirubi

30070
31

Jannie Mouton

30064
30

Mohammed Indimi

33063
29

Abdulsamad Rabiu

400NA
28

Hakeem Belo-Osagie

45056
27

Gerrit Thomas (GT) Ferreira

46063
26

Uhuru Kenyatta

50050
25

Raymond Ackerman

54580
24

Oba Otudeko

55067
23

Samih Sawiris

56054
22

Alami Lazraq

57561
21

Theophilus Danjuma

60072
20

Stephen Saad

64047
19

Shafik Gabr

73059
18

Lauritz (Laurie) Dippenaar

75063
17

Jim Ovia

77557
16

Mohamed Al Fayed

1,30078
14

Yasseen Mansour

1,55050
14

Youssef Mansour

1,55066
13

Mohamed Mansour

1,70063
12

Anas Sefrioui

1,75054
11

Othman Benjelloun

2,40079
10

Patrice Motsepe

2,50049
9

Onsi Sawiris

2,60081
8

Christoffel Wiese

2,70070
7

Naguib Sawiris

2,90057
6

Miloud Chaabi

3,00082
5

Mike Adenuga

4,30058
4

Johann Rupert & family

4,70061
3

Nassef Sawiris

4,75050
2

Nicky Oppenheimer & family

6,50066
1

Aliko Dangote

10,10054

Monday, November 14, 2011

Mapigano ya kikabila nchini Libya

Best Blogger Tips
Mapigano Libya
Kumekuwepo na mapambano ya siku kadhaa kati ya makundi yanayokinzana katika mji wa mwambao wa Zawiya nchini Libya ambapo takriban watu 7 waliuawa.

Mwandishi wa BBC Karen Allen akiwa Libya anasema jamii zinazopingana zimekua zikipigania eneo ambalo zamani lilidhibitiwa na wafuasi wa kanali Gaddafi.

Hatahivyo serikali ya mpito imesema kwamba mapigano hayo yalisuluhishwa.

Wachambuzi wanasema mapigano hayo yanazusha masuala kadhaa kuhusu hali ya utulivu baada ya kuondoka kwa Gaddaffi nchini Libya.

Libya bado inakabiliwa na changamoto za kuenea silaha na vikundi vya watu wenye silaha baada ya uasi uliosababisha kuporomoka kwa utawala wa Kanali l Muammar Gaddafi.

Kiongozi wa utawala wa mpito Mustafa Abdul-Jalil alisema baraza la taifa la mpito limewakutanisha wazee kutoka maeneo yanayogombaniwa ya Zawiya na maeneo ya karibu ya makabila ya Warshefana - na kwamba mzozo huo umesuluhishwa mwishoni mwa wiki.

Hatahivyo baadhi ya watu wamearifu kuwa mapigano bado yalikuwa yanaendelea wakati akiongea.
Taarifa zaeleza kuwa mapigano yalianza pale wapiganaji kutoka Warshefana walipoweka kizuizi cha barabarani katika njia panda karibu na Zawiya, na kuwatambia wapiganaji kutoka mjini humo.

Wapiganaji kutoka Zawiya waliwashutumu wale kutoka Warshefana kuwa na ufungamano na utawala wa zamani.
Chanzo: BBC

Wednesday, November 9, 2011

Mke (60) amshitaki mume mwenye miaka 30

Best Blogger Tips
MWANAMKE mwenye umri wa miaka 60, mkazi wa Kibaoni mjini hapa, amewavunja mbavu wasikilizaji wa kesi katika Mahakama ya Mwanzo Ipembe, baada ya kumjibu Hakimu kuwa kijana aliyemfikisha mahakamani hapo si mwanawe bali mumewe.

Katika kesi hiyo, mwanamke huyo Asha Abdallah anamshitaki mumewe, Kiemi Itambu (30), kwa kumwibia Sh 30,000 alizokuwa ameficha chini ya godoro.

Wawili hao wakiwa kizimbani jana, Hakimu Hosea Mkude alimwuliza mke: “Kwa nini wewe bibi unaolewa na kijana ambaye ana umri wa mwanao, huoni aibu?

Asha alijibu: “Mheshimiwa, huyu ni mtoto kwa mama yake aliyemzaa, kwangu ni mume wangu halali ambaye ananitimizia mahitaji yangu yote muhimu.”

Kama vile jibu hilo halikutosha, Asha aliendelea ‘kumpasha’ hakimu: “Kwanza kwa taarifa yako, wako wanawake wengi tu hapa mjini walioolewa na vijana, tena wengine wana vijana wenye umri unaofanana na wa wajukuu zao. Sembuse miye?”

Majibu hayo yalisababisha watu waliojazana kwenye chumba hicho cha Mahakama, washindwe kujizuia na kuangua vicheko.

Ilidaiwa mahakamani hapo, kuwa mshitakiwa Kiemi alitenda kosa hilo Novemba 3, saa mbili asubuhi Kibaoni mjini hapa.

Asha alidai mahakamani hapo kuwa mumewe amekuwa na tabia ya kumwibia Sh 100, 200 na 500, lakini safari hii alivuka mpaka kwa kuiba Sh 30,000 ndiyo maana akaamua kumfikisha mahakamani.

Mshitakiwa alikana mashitaka na yuko nje baada ya kujidhamini mwenyewe kwa ahadi ya kutoa Sh 50,000 hadi Novemba 15 kesi hiyo itakapotajwa.
Chanzo: BBC

Monday, November 7, 2011

Daktari wa Michael Jackson hatiani

Best Blogger Tips
Daktari binafsi wa Michael Jakson, Dk Conrad Murray amekutwa na hatia ya kosa la mauaji bila kukusudia na mahakama moja mjini Los Angeles, Marekani.

 Baraza la wazee wa mahakama - wanaume saba na wanawake watano - walichukua siku mbili kujadili kesi na kufikia hukumu hiyo.

Michael Jackson alifariki Juni 25 mwaka 2009 kutokana na kuzidisha kipimo cha dawa ya usingizi.

Adhabu 

Murray, 58, anaweza kukabiliwa na adhabu kamili ya kwenda gerezani kwa miaka minne na kupoteza leseni yake ya uganga.

 Wanasheria wa Dk Murray walihoji kuwa Michael Jackson alijidunga mwenyewe dawa hiyo wakati daktari wake akiwa nje ya chumba.

Dk Murray alipelekwa rumande baada ya kukutwa na hatia na atasalia huko hadi wakati atakaposomewa adhabu yake, inayotarajiwa kutolewa Novemba 29.

Akielezea uamuzi wake, jaji alisema Dk Murray kwa sasa ni mhalifu aliyekutwa na hatia na kwa kuwa anafahamiana na watu nje ya jimbo la California, inamaanisha hakuna uhakika kuwa daktari huyo ataweza kubakia bila kutoka katika jimbo hilo.

Rumande  

Dk Murray alibaki kimya mahakamani hapo, akijisogeza kidogo katika kiti chake wakati hukumu ikisomwa.

Maafisa wa mahakama walianza kumfunga pingu daktari huyo wakati jaji akikamilisha kusoma hukumu, na baadaye kupelekwa rumande.

Baraza la wazee - lililoundwa na wazungu weupe sita, Mmarekani mweusi mmoja na Wamarekani watano wenye asili ya Hispania - walijadili shauri hilo kuanzia Ijumaa hadi Jumatatu asubuhi.

Nje ya mahakama, mashabiki wa Michael Jackson walikuwa wakishangilia na kuimba "Hatia! Hatia!" muda mfupi kabla ya hukumu kusomwa.

Wakati wa wiki sita za kusikilizwa kwa kesi hiyo, mashahidi 49 na zaidi ya vipande 300 vya ushahidi viliwasilishwa mahakamani hapo.

Michael Jackson ambaye alikuwa kimya katika ulimwengu wa sanaa kwa miaka kadhaa, alikufa mwaka 2009 wakati akijiandaa kufanya mfululizo wa maonesho katika ukumbi wa 02 jijini London.

Kuwa na baba

Katika hoja za mwisho mahakamani siku ya Alhamisi, upande wa mashtaka ulisema Dk Murray alisababisha kifo cha nyota huyo kutokana na uzembe, na hivyo kuwanyima watoto wa Jackson haki ya kuwa na baba.

Upande wa utetezi ulihoji kuwa Jackson alikuwa amejizoesha kutumia dawa, kitu ambacho kilisababisha kifo chake kutokana na kujipa kiwango kikubwa cha dawa ya kulevya huku daktari wake akiwa nje ya chumba katika jumba alilokuwa amekodi nyota huyo mjini Los Angeles.
Chanzo: BBC


Joe Frazier aumwa saratani ya ini

Best Blogger Tips
Joe Frazier
 Bingwa zamani wa ndondi za uzito wa juu duniani Joe Frazier yupo katika nyumba wanayouguzwa wagonjwa mahututi akiwa anaumwa saratani ya ini, meneja wake amesema.

Amesema Frazier - anayejulikana pia kwa jina la Smokin' Joe - aligunduliwa anaumwa saratani wiki kadha zilizopita.

"Nitakuwa muongo iwapo sitawaeleza kwamba hali yake si nzuri," Leslie Wolf alilieleza shirika la habari la Uingereza la Reuters.

Frazier mwenye umri wa miaka 67 alishikilia mkanda wa ubingwa wa dunia miaka kati ya 1970 na 1973. Alikuwa ndiye mtu wa kwanza kumchapa Muhammad Ali mwaka 1971. Baadae akachapwa na Ali katika mapambano mawili yaliyofuatia.

Bw Wolf amesema Frazier aligunduliwa na maradhi ya saratani ya ini mwezi uliopita na kwa sasa anatibiwa katika nyumba maalum inayotunza wagonjwa mahututi huko Philadelphia.

"Joe ni mpiganaji. Joe kamwe hashindwi," meneja huyo alisema, akaongeza madaktari na watu wa karibu wa Frazier "tunafanya kila jitahada".

Frazier alishinda taji la ubingwa wa dunia kwa uzito wa juu mwaka 1970 baada ya kumtwanga Jimmy Ellis mjini New York. Aliendelea kushikilia taji hilo hadi mwaka 1973, ambapo alipigwa na George Foreman.

Lakini mwanamasumbwi huyo huenda anafahamika zaidi kwa mapambano makubwa na Ali, likiwemo lile la kukata na shoka la Phillipines lililopewa jina la Thriller in Manila mwaka 1975.

Friday, November 4, 2011

Ferguson asherehekea miaka 25 Man U

Best Blogger Tips
Sir Alex Ferguson

Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson anasherehekea miaka 25 na timu hiyo.

Ferguson ameeleza miaka hiyo 25 akiwa na mashetani wekundu ni kama hadithi nzuri.

Katika miaka hiyo yote mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 70 ameisaidia Man U kushinda kombe la Premier mara 12, kombe la FA mara tano na Ligi ya mabingwa bara Ulaya mara mbili
.
Licha ya mafanikio hayo, Ferguson amekuwa hapendelei sana kuzungumzia sifa hizo.

Na hata anapoulizwa kuhusu mafanikio yake Man United , Meneja huyo huanza na usemi wake wa kawaida " Sitazungumzia swala hilo".

Lakini mwaka jana akiwa na umri wa miaka 69 alizungumzia kwa muda enzi zake na mafanikio yake tangu alipochukuo uongozi wa Man U Novemba 6 mwaka 1986 kutoka kwa Ron Atkinson.

Kutoka mwaka huo Ferguson amenyakuwa mataji 27 na kushuhudia miamba wengi wakikuza vipaji vyao wakiwa klabu cha Man United.

Kwa wakati huu litakaloangaliwa ni muda gani Fergerson atabakia kuwa kileleni mwa timu hiyo, swali ambalo amenukuliwa akijibu kwa kusema " ataendelea ilimradi afya yake inamruhusu kufanya hivyo"
Chanzo: BBC

Thursday, November 3, 2011

Serikali yakataa ushoga

Best Blogger Tips
TANZANIA imesema ipo tayari kukosa  misaada yote kutoka Serikali ya Uingereza  na kamwe haiwezi kuruhusu sheria inayotambua mashoga na kuhalalisha ndoa za jinsia moja.Msimamo huo mzito wa serikali umekuja siku chache baada ya Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, kutamka kwamba nchi yake ina mpango wa kusitisha misaada yake kwa nchi ambazo sheria na katiba zao, hazitambui mashoga na ndoa za jinsia moja.

Cameron alikaririwa akithibitisha kuwa tayari amewajulisha juu ya suala hilo Wakuu  wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola waliokuwa wakihudhuria mkutano wa Jumuiya hiyo uliomalizika siku nne zilizopita,  mjini Perth , Austaralia ambao pia ulihudhuriwa na Rais Jakaya Kikwete.

Waziri Mkuu huyo kutoka chama cha Conservative ambacho kilishinda uchaguzi Mei mwaka jana, alisema  suala hilo la mashoga na ndoa za jinsi moja ni moja ya mambo yanayoongoza sera ya serikali yake kuhusu misaada kwa mataifa mbalimbali na kwamba tayari imeanza kutekelezwa katika maeneo kadhaa duniani.

Kauli ya Cameron imechukuliwa kama kielelezo cha ukoloni mamboleo ambao Uingereza inajaribu kuupandisha daraja  kwa mataifa yanayoendelea kwa kigezo cha misaada  

Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe,  alisema pamoja na umasikini wake, Tanzania kamwe haitaruhusu upuuzi huo kwa kigezo cha misaada.

“ Tanzania ni nchi maskini lakini hatutakubali kuruhusu upuuzi huo eti kwa sababu ya misaada yake na fedha zao, lakini ushoga si utamaduni wetu, hata sheria zetu zinakataa,” alisema Membe.

Alifafanua kuwa katika kuonesha msimamo wa kutokukubaliana na masharti hayo, Tanzania imeshikilia msimamo thabiti kupinga  upuuzi huo ambapo  Januari mwaka huu,  ilimkataa balozi shoga ambaye aliteuliwa na nchi yake kuja kuiwakilisha hapa  nchini. Hata hivyo Waziri Membe hakutaja jina la balozi huyo wala nchi  anayotoka.

“Niwape siri moja ambayo tuliificha lakini leo ngoja niwaambie, mwanzoni mwa mwaka jana nililetewa barua  kunijulisha ujio wa balozi mmoja anayekuja kuiwakilisha nchi yake, mwanamume mwenye ndoa ya jinsia moja. Nilikwenda kumweleza Rais Jakaya Kikwete kuhusu wasifu wa balozi huyo mtarajiwa naye akajibu kwa maneno matatu, yarabi toba! Mkatae!” 

Waziri Membe alifafanua kuwa serikali ilimkataa balozi huyo kwa kuwa ni kinyume cha utamaduni wetu na sheria za nchi kuwa na watu wenye tabia hizo.

Alisema alimjulisha waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo kwamba balozi huyo haruhusiwi kuja kufanya kazi nchini kwa kuwa ni kinyume na utamaduni wetu.  “ Waliendelea kuniomba kwamba balozi huyo akija hatatoka kwenye makazi yake akiwa na mwenza wake hivyo watu hawatamuona lakini tulimkataa kabisa, wakatuelewa,” alisema Membe.

 Alieleza kuwa  tamko hilo la Waziri Mkuu Cameron linaweza kusababisha hatari ya kuvunjika kwa uhusiano miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola na koloni mama  Uingereza na waziri huyo atabeba lawama hizo

 Akisisitiza msimamo huo wa serikali, Membe,  alisema  Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 kifungu cha tisa, kinatambua ndoa ya jinsia mbili tofauti,  yaani mume na mke.  “ Sheria hizi tunazozitumia hivi sasa tumezirithi kutoka Uingereza ambako leo wanatukuza ndoa za jinsia moja na ushoga,” alisema Membe.

Suala la kile kinachoitwa haki za binadamu kuhusu ushoga ilikuwa moja ya ajenda ambazo viongozi kadhaa walishindwa kuafikiana katika mkutano  Perth .

Hoja ya  kukomesha vizuizi dhidi ya ushoga na ndoa za jinsi moja lilikuwa moja ya mapendekezo yaliyokuwamo katika ripoti ya ndani kuhusu matarajio ya baadaye ya Jumuiya hiyo ya Madola.
  
Itakumbukwa kwamba, Malawi tayari imeathirika na mpango huo wa Uingereza kwa sehemu ya misaada yake kusitishwa kutokana na msimamo wa nchi hiyo kuhusu kile Uingereza na nchi za Magharibi zinazokiita haki za mashoga. Ikumbukwe pia kuwa, mjadala mzito ulioibuka katika Bunge la Uganda mwaka 2009 kuhusu ndoa za jinsi moja ilikuwa sehemu ya utekelezaji wa sera hiyo ya Uingereza na washirika wake.

  Ajenda zingine Mkutano wa Perth   Waziri Membe alisema viongozi wa Jumuiya ya Madola walikubaliana suala la mabadiliko ya tabia nchi kuwa ajenda kuu katika nchi hizo.

Alisema ajenda hiyo sasa inakuwa muhimu kutokana na nchi nyingi wanachama wa jumuiya hiyo kuwa katika tishio kubwa la uharibifu wa mazingira.

Aidha, Membe alisema nchi hizo zimekubaliana kuandaa kanuni na mwongozo ambao utatakiwa kufuatwa na nchi za jumuiya hiyo.

“ Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Jumuiya ya Madola tutakutana Aprili mwakani kuandaa miongozo na kanuni hizo,” alisema Membe.
Source: Mwanachi

Tuesday, October 25, 2011

Gaddafi azikwa kwa siri jangwani

Best Blogger Tips
MISRATA, Libya
MWILI wa aliyekuwa kiongozi wa Libya, Kanali Maummar Gaddafi umezikwa katika sehemu ya siri jana, baada ya kuuawa kwake na wapiganaji waliokuwa wakimpinga wiki iliyopita.

Mmoja wa waopiganaji hao alijitokeza kwa mara ya kwanza jana kupitia mkanda wa video akieleza kwamba yeye ndiye aliyechukua uamuzi wa kufyatua risasi na kumuua Gaddafi, kwa kuwa hakuona haja ya kumshikilia akiwa hai.

Maziko hayo yamefanyika baada ya kuwapo kwa mvutano baina ya wanafamilia wa Kanali Gaddafi na uongozi wa sasa wa Libya ambao ni Baraza la Mpito la Nchi hiyo (NTC) ambalo lilitangaza kuzika mwili huo kwa siri, ili kuficha mahali lilipo kaburi la kiongozi huyo wa Libya kwa miaka 42.

Mwili huo ulichukuliwa na kupelekwa kuzikwa kusikojulikana, baada ya ndugu na watu wake kadhaa wa karibu kuruhusiwa kushiriki katika sala maalum na taratibu zote za Kiislamu.

Mmoja wa wasemaji wa NTC alisema jana kuwa mwili wa Gaddafi, mwanae Mutassim pamoja na mmoja wa wasaidizi wake imezikwa, licha ya kuwapo kwa utata kuhusu pale ilipostahili kuzikwa.

Mvutano uliokuwapo ulitokana na ombi la ndugu wa kabila la Kanali Gaddafi ambao walikuwa wakitaka wapewe mwili wa kiongozi huyo ili wauzike mjini Sirte, alipozaliwa, lakini viongozi wa baraza la kitaifa la mpito walipinga ombi hilo.

Taarifa nyingine zinamnukuu msemaji wa NTC, Ibrahim Beitalmal akisema ndugu wachache wa familia ya Gaddafi walishiriki katika taratibu za ibada ya mazishi ya kiongozi huyo na dua, vilivyofanyika kwa kuzingatia taratibu za dini ya Kiislamu.

Hata hivyo, habari zaidi zinadai kuwa, baada ya sala hiyo, ndugu wa Gaddafi hawakuruhusiwa kuona sehemu ambayo kiongozi huyo amezikwa ambako kunadaiwa kuwa ni katikati ya jangwa.

Baadhi ya watu mjini Misrata wanasema miili ya watu hao watatu iliondolewa usiku kutoka sehemu ilipokiuwa imehifadhiwa katika harakati za kupanga mazishi hayo.

Raia wa Libya wamekuwa wakitembelea eneo hilo la bucha katika mji wa Misrata ambako miili hiyo ilipelekwa na kuhifadhiwa baada ya tangazo la kifo cha kiongozi huyo na baadhi ya walinzi wake, kujionea mwili wake ili kuthibitisha ukweli kuwa ameuawa.

Viongozi wa NTC walikuwa wanahofia kuwa huenda Kanali Gaddafi akizikwa katika sehemu ya wazi, kaburi lake litabadilishwa kuwa pahali patakatifu na wafuasi wake.

Pamoja na hilo, mashirika ya kutetea haki za binadamu yamekuwa yakishinikiza uchunguzi ufanyike kubainisha jinsi alivyouawa Kanali Gaddafi, kwani picha za awali zilionyesha kuwa alikamatwa akiwa hai.

Kiongozi wa NTC, Mustafa Abdul Jalil, ametangaza kuwa uchunguzi utafanyika kuhusu hilo. Hata hivyo, kuna wale wanaohoji ikiwa kweli uchunguzi huo utakuwa wa wazi ikiwa mashirika ya kujitegemea hayakuhusishwa.

Katika video iliyotolewa jana, kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail la Uingereza, kijana mpiganaji anayedai kumuua Kanali Gaddafi baada ya kukamatwa akiwa hai kwenye mtaro wa majitaka, alisema hakuona sababu ya kumuacha aendelee kuwa hai na kumkabidhi kwa uongozi wa NTC.

“Tulimkamata, nilimpiga katika paji la uso. Baadhi ya wapiganaji wenzangu walikuwa wakilazimisha kutaka tumpeleke na kumkabidhi akiwa hai. Niliamua kumpiga risasi mbili. Moja kichwani na nyingine kifuani,” alisema.

Katika kutaka kuthibitisha hilo, kijana huyo alionyesha kipande cha nguo ya Gaddafi kikiwa kimetapakaa damu na pete ya dhahabu ambayo alimvua baada ya kumuua.

Jaji Mkuu Tanzania awania nafasi ya Ocampo

Best Blogger Tips
Jaji Mkuu wa Tanzania Mohamed Chande Othman
 Jaji mkuu wa Tanzania Mohamed Chande Othman ni mmoja kati ya watu wanne muhimu wanaoweza kushika nafasi ya Mwendesha Mashtaka katika Mahakama ya Uhalifu ya Kimataifa iliyoko The Hague, nchini Uholanzi.

Nafasi hiyo ambayo kwa sasa inashikiliwa na Luis Moreno-Ocampo itakuwa wazi hapo mwakani baada ya Bw Ocampo kumaliza kipindi chake cha utumishi wa miaka tisa mwakani.

Kwa mujibu wa shirika la habari la AF, wagombea wengine ni pamoja na Naibu Mwendesha Mashtaka wa sasa Fatou Bensouda wa Gambia, ambaye wengi wanamwona kuwa analeta ushindani mkali.

Anaungwa mkono na Umoja wa Afrika ambao mara nyingi umemkosoa Moreno-Ocampo kwa kufungua uchunguzi wa mataifa ya Afrika pekee.

Katika orodha hiyo pia yupo Andrew Cayley, mwendesha mashtaka mwenza katika mahakama maalum ya Khmer Rouge nchini Cambodia anayetokea Uingereza.

Mwingine ni Robert Petit, ambaye ni mshauri kuhusu uhalifu dhidi ya ubinadamu na uhalifu wa kivita katika Kitengo cha Mahakama nchini Canada.

Kamati ya iliyoundwa na nchi wanachama wa mahakama hayo awali ilikuwa na orodha ya majina 52 ya wagombea walioomba kupendekezwa katika nafasi hiyo ya juu. Kamati hiyo iliwahoji wanane kabla ya kupata wagombea wanne.

Kwa mujibu wa Kamati hiyo ‘
Wote wana uzoefu mkubwa katika kuendesha kesi za kimataifa.

Wasifu wa Wagombea

Jaji Othman ameshika nafasi muhimu mbalimbali za uandamizi katika mfumo wa sheria nchini Tanzania na alikuwa mwendesha mashtaka mkuu katika mahakama maalum ya mauaji ya Rwanda na pia mwendesha mashtaka katika Utawala wa Mpito wa Umoja wa Mataifa katika Timor Mashariki.

Kabla ya kujiunga na mahakama maalum ya Khmer Rouge , Bw Cayley alikuwa mwendesha mashataka mshauri mwandamizi wa ICC, Wakili wa Utetezi katika mahakama maalum za vita vya Sierra Leone na Yugoslavia na pia mwendehsa mashtaka katika mahakama ya Yugoslavia.

Petit alikuwa wakili mwandamizi katika kesi kwenye Mahakama ya Sierra Leone, afisa wa sheria katika mahakama maalum ya Rwanda na mshauri wa sheria kwa ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Kosovo.

Bensouda ni waziri wa zamani wa sheria nchini Gambia ambaye pia aliwahi kufanya kazi kama mshauri mwandamizi wa sheria na wakili katika kesi kwenye Mahakama maalum ya Rwanda.

"Ni orodha nzito kabisa," Alisema Param-Preet Singh, Mshauri Mwandamizi katika kitengo kinachoshughulikia Haki za Binadamu cha Human Rights Watch's International Justice Program.
Chanzo: BBC

Monday, October 24, 2011

Gaddafi dikteta mwenye mafanikio, wosia wake waanikwa

Best Blogger Tips
SIKU chache baada ya  kuuawa kwa kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi, walibya na dunia kwa ujumla imeingia katika mitizamo tofauti kuhusu kiongozi huyo huku wengi wakikumbuka mafanikio aliyoleta kwa taifa hilo tofauti na viongozi wengine waliong’olewa kwa udikteta.Baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikimtangaza na kutafuta namna zote za kujenga picha ya udikteta bila kuangalia upande wa pili wa Libya iliyooachwa  na Gaddafi.

Baadhi ya mambo ambayo yamekuwa yakizungumziwa ni iwapo Libya ya sasa itaweza kuneemeka na kile ambacho ilikuwa ikipata kutoka kwa kiongozi huyo, ambaye  hivi karibuni  aliuawa na wapinzani wake.

Gaddafi, tofauti na viongozi wengine waliowahi kutajwa kuwa madikteta  duniani,  ana mengi ya kukumbukwa na kusifiwa kwayo.Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa na kiuongozi wamekuwa wakieleza kusikitishwa kwao na kutotambua aina ya demokrasia ambayo baadhi ya watu wa Libya wanaililia kwa sasa na iwapo itaboresha au kuharibu kabisa maisha yao.

Hii inawekwa wazi kwamba  pamoja na kwamba Gaddafi ametumia fedha nyingi za Libya katika masuala binafsi,  lakini je, kwa wastani Libya ni maskini? Wapo viongozi waliozitumia nchi zao na kuziharibu kabisa, Gaddafi aliwahi kuifilisi Libya?

Haya ni baadhi ya mambo ambayo Gaddafi  aliyasimamia na kuyatekeleza katika utawala wake wa miaka 42 kwa Libya.Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na tovuti za mawasiliano za Libya na Zimbabwe zimeeleza kuwa nchini Libya hakuna mwananchi aliyewahi kulipa bili ya umeme, umeme ulikuwa bure kwa raia wake wote.

Hakukuwa na riba katika mikopo, benki zote Libya zilikuwa chini ya Serikali,  mikopo ilitolewa kwa wananchi bila riba ya kiasi chochote .
Taarifa hizo zikafafanua kuwa makazi ni haki ya msingi nchini Libya, Gaddafi aliwahi kusisitiza kwamba wazazi wake hawawezi kupata makazi hadi kila raia apate makazi. Baba wa Gaddafi alifariki dunia wakati yeye, mama yake wakiwa wanaishi katika hema.

Wanandoa wote wapya nchini humo walipata Dola 50,000 kwa Serikali kwa ajili ya kununua makazi yao kuwasaidia kuanzisha familia mpya.Elimu na huduma za  kiafya vilitolewa bure. Wakati Gaddafi nachukua nchi  asilimia ya waliokuwa na elimu ilikuwa 25, kwa sasa inafikia  83.
Kwa waliotaka kuwa wakulima, walipewa ardhi bure, nyumba katika shamba lao, vifaa, mbegu na mifugo kwa ajili ya kuanzisha miradi.Iwapo kuna waliokuwa hawawezi kupata huduma za elimu na afya wanazostahili, Serikali iliwalipia kwa ajili ya kuzipata nje ya nchi, hizi hazikuwa bure, walitakiwa kuchangia, walipata Dola2,300 kwa mwezi kwa ajili ya makazi na usafiri.

Kwa waliokuwa wakitaka kununua magari,  Serikali ililipia kwa asilimia 50 ya bei. Bei ya petroli ilikuwa karibu na bure, lita ililipiwa kwa Dola 0.4.
Libya haidaiwi nje, pia ina akiba inayofikia Dola150 bilioni nje ambayo kwa sasa imezuiliwa.Kwa waliomaliza vyuo,  Serikali iliwapatia posho sawa na mshahara wa maofisa hadi watakapopata ajira yenye uhakika. Sehemu ya mauzo ya mafuta ya Libya iliwekwa moja kwa moja kwenye akaunti ya raia wake.

Kila mwanamke aliyejifungua alipata posho ya Dola5000, mikate 40 iliuzwa kwa dola0.15,  asilimia 25 wa Walibya, wana shahada ya chuo kikuu.Kama hiyo haitoshi taarifa hizo zimeeleza kuwa alisimamia mradi mkubwa kabisa wa umwagiliaji, uliopewa jina la Great Man-made River, kuhakikisha maji yanakuwepo kwenye maeneo yote ya nchi yenye jangwa.

Wakati wa vikwazo kwa Serikali yake miaka ya 1980, Libya ilikuwa miongoni mwa nchi tajiri kabisa kwa msingi wa pato la ndani, ikwa na kiwango cha juu cha maisha kuliko Japan. Ilikuwa ni nchi tajiri kuliko zote kabla ya vuguvugu la mapinduzi.
Wastani wa kiwango cha maisha kwa pato la kichwa ni Dola11,314 . Gaddafi amewahi kutumia fedha nyingi kwa ajili ya safari zake na miradi yake, lakini amefanya mabo makubwa ambayo hakuna dikteta aliyewahi kuyafanya kwa watu wake. Alirejesha pato kwa watu wake, aliwajali.

          Wosia wa Gaddafi kabla ya kifo
Katika wosia wake, Kanali Gaddafi aliwaasa wafuasi wanaomuunga mkono kuendelea kupambana.
Alielezea msimamo wake kuwa amechagua kupambana hadi hatua ya mwisho na kufia katika ardhi ya Libya kuliko kuchagua njia nyepesi, ambayo kwa mtizamo wake,  ni kitendo cha kujidhalilisha kisichokuwa na heshima, kukimbilia uhamishoni nje ya nchi yake, ambapo tayari alishapata ahadi nyingi za ulinzi.

Katika lugha ya Kiingereza, waraka wake wa wosia umetafsiriwa ukisomeka: “Hii ni hiyari yangu. Mimi Muammar bin Mohammad bin Abdussalam bin Humayd bin Abu Manyar bin Humayd bin Nayil al Fuhsi Gaddafi, ninaapa kwamba hakuna Mungu mwingine zaidi ya Allah na Muhammad ni Mtume wake, amani iko kwake. Ninaahidi nitakufa nikiwa Muislamu.

 “Iwapo nitauawa, nitapenda kuzikwa kwa mujibu wa taratibu za kiislamu, nikiwa nimevaa mavazi nitakayokuwa nimevaa wakati kifo change kikitokea, bila mwili wangu kuoshwa, katika makaburi ya Sirte, jirani na familia na jamaa zangu.

“Nitapenda kwamba familia yangu, hasa wanawake na watoto, watunzwe vyema baada ya kifo changu. Watu wa Libya wana wajibu wa kulinda wasifu, mafanikio, historia na heshima ya waasisi na mashujaa wake.

“Watu wa Libya hawatakiwi kupuuza kujitapa na lazima wawe  watu huru wa kuthaminiwa. Ninawataka wale wanaoniunga mkono kuendelea kupambana, kuwakabili wote wanaosimama kutoka nje dhidi ya Libya, leo, kesho na siku zote.

 “Hata kama hatutashinda mapema, tutatoa funzo kwa vizazi vyetu vijavyo, kwamba kuchagua kulinda utaifa ni heshima na kuliuza ni uasi mkubwa ambao historia haitausahau milele, pamoja na juhudi za wengine kuwaeleza kinyume cha hayo”.
Endelea kusoma habari hii.....................

Thursday, October 20, 2011

Wasifu wa Kanali Muammar Gaddafi

Best Blogger Tips

Kanali Muammar Gaddafi
Alikuwa mtoto wa wafugaji wa Kibedui, mwenye maisha ya utata, lakini ambaye alitukuzwa sana, huku mataifa ya Magharibi yakimuona mtu wa hatari wakati wote.

Muammar Muhammad Gaddafi aliitawala Libya kwa zaidi ya miaka 40. Hadi mwanzoni mwa Machi 2011, alikuwa akiamini ndani ya moyo wake kwamba watu wake walikuwa wakimpenda na kwamba walikuwa tayari kumlinda hadi kufa kwa ajili yake.

Lakini wakati huo, tayari Gaddafi alikuwa ameshatumia njia za kikatili kuyazima maandamano dhidi yake, maandamano ambayo baadaye yaligeuka vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Kwa mujibu wa taarifa, watu zaidi ya 30,000 waliuawa kwenye vita hivyo. Mara nyingi sana, Gaddafi alitoa matamko makali wakati wa vita hivyo, ila linalojuilikana zaidi ni lile la kuwaita wapinzani wake kuwa ni panya.

Kwa kila hali, yaliyotokea ni mambo ambayo Gaddafi hakuyatarajia asilani. Mtoto huyu wa wafugaji wa Kibedui aliyezaliwa mwaka 1942, alikuja kuibuka kama mkombozi wa Walibya, alipompindua Mfalme Idriss hapo mwaka 1969.

Kuanzia hapo akaanza kujenga kile alichokiona mwenyewe kuwa ni mfumo wa kidemokrasia wa moja kwa moja. Alianzisha kamati za umma zilizoamua juu ya mustakabali wa umma na wa Serikali. Aliuita mfumo wake wa kisiasa na kiuchumi kuwa ni wa kisoshalisti, alioufafanua kwenye kijitabu chake cha Kijani.

Historia yake kiufupi

Alizaliwa mwaka 1942 katika eneo la Jangwa, kwenye mji wa Sirte, katika familia ya baba Mohamed Abdulsalama Abuminiar na mama Aisha Ben Niran. Alijiunga na Jeshi la Libya  mwaka 1965.
Alifanya mapinduzi ya Serikali yasiyo ya umwagaji damu na kumuondoa mfalme Idris katika utawala wake mwaka 1969 na kuwa mtawala wa Libya akiwa na umri wa miaka 27.

Alikuwa maarufu kwa nguo anazopenda kuvaa na walinzi wa kike wenye kubeba silaha, kiongozi huyo wa Libya pia anadhaniwa kuwa na mbinu nzuri za kisiasa kwa kuweza kuirejesha Libya kutokana na kutengwa kidiplomasia duniani.
Baada ya miongo miwili ya kutengwa katika jamii ya kimataifa, mwaka 2003, Tripoli ilikiri kuwa walifanya shambulio la Lockerbie kwa kuiangamiza kwa mabomu ndege ya Pam Am. Umoja wa Mataifa (UN) ulikubali kuondoa vikwazo dhidi ya Libya.

Baada ya miezi kadhaa, Serikali ya Kanali Gaddafi ilisitisha mipango yake ya kuunda silaha za maangamizi na hii ikarejesha ushirikiano na nchi za Magharibi.

Gaddafi ni mtu wa kipekee katika kauli zake, mienendo yake, tabia zake na mikakati yake, kwa mujibu wa Saas Djebbar, mtaalam wa siasa za Libya.
Alipokuwa kijana alivutiwa na kiongozi mzalendo wa Misri, Gamal Abdel Nasser, alipokuwa akishiriki katika maandamano dhidi ya Israel wakati wa mtafaruku wa Suez mwaka 1956.

Alipanga njama ya kupindua utawala wa kifalme alipokuwa mwanafunzi wa kijeshi alipokuwa mafunzoni Uingereza kabla ya kurejea nyumbani Libya. Alipanga mapinduzi ya Septemba 1, 1969 akiwa katika mji wa Benghazi.

Alianza kujenga itikadi zake za kisiasa mwaka 1970 na kuziandika katika kitabu chake cha kijani kibichi.
Alikitumia kitabu chake kuanzisha mfumo wa kisiasa uliojumuisha kanuni za Kiislamu na mfumo ulio tofauti na siasa za ujamaa au ubepari.
Mwaka1977 aliasisi mfumo ujulikanao kama 'Jamahiriya' au 'Taifa la Umma' ambapo raia ndio wanaoendesha uongozi wa nchi yao kupitia 'kamati za umma'.

Mfumo huo wa Gaddafi umevuka mipaka na hauhusishi mambo ya siasa tu, bali pia mambo mengine.
Akiwa safarini ng'ambo, alikuwa akitumia makazi maalum kwenye kambi iliyojengwa na hema yake ya kifahari ya Kibeduwi akiwa amefuatana na walinzi wanawake ambao, inasemekana, huwa hawapotezi umakini kazini kama walinzi wanaume.Hema hiyo pia ilitumiwa kuwalaki wageni wa Libya na Kanali Gaddafi huendesha mikutano na mahojiano yake humo humo akipepea usinga au tawi la mitende.

Rais wa zamani wa Marekani Ronald Reagan alimwita Gaddafi 'mad dog' yaani 'mbwa kichaa' na Marekani ililipiza kisasi dhidi ya Libya kwa madai ya kuhusika na mashambulio ya anga barani Ulaya kwa kuvamia miji ya Tripoli na Benghazi mwaka 1986.Aliposhindwa katika jitihada zake za kuzipatanisha nchi za Uarabuni katika miaka ya 90, Kanali Gaddafi alielekeza nguvu zake barani Afrika na kupendekeza 'Muungano wa Nchi' za bara la Afrika.

Alianza kuvaa mavazi yake binafsi, sare za michezo zilizo na ngao za Bara la Afrika au picha za viongozi kutoka bara hilo.Aliwahi kuvunja na kufuta Wizara za nchi hiyo pamoja na bajeti zao, isipokuwa Wizara chache ikiwemo ya Ulinzi, Fedha na Mambo ya Nje.Licha ya uchumi wa Libya kutoa fursa kwa wawekezaji wa nje, mabadiliko bado yanakwenda taratibu.

Vuguvugu la mageuzi dhidi yake lilipoanza mwanzoni mwa mwaka huu, aliapa kuwafuata wanaompinga nyumba hadi nyumba, mlango kwa mlango, hatua iliyoibua hasira na kuchochea harakati za kijeshi dhidi yake.

Baada ya baadhi ya askari kutangaza kujitoa katika jeshi lake na kuanzisha uasi, aliapa kwamba atapambana hadi tone la mwisho la damu litakapomwagika. Alisisitiza kwamba kamwe hatakimbia kutoka katika ardhi ya Libya, atafia katika ardhi ya mababu zake.

Taarifa zilieleza jana kwamba aliuawa baada ya kukutwa akiwa amejificha katika daraja dogo kwa ajili ya kupitisha maji barabarani (karavati).
Mara baada ya kuuawa, wapiganaji wa Baraza la Mpito waliokuwa katika mapambano dhidi yake walibaini kwamba alikuwa na bastola iliyotengenezwa kwa dhahabu tupu.

Muammar Gaddafi auawa

Best Blogger Tips
Muammar Gaddafi
KIONGOZI wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi  ameuawa. Habari zilizotangazwa na waasi wa majeshi ya serikali walitoa taarifa hiyo muda mfupi baada ya kutangaza kuushikilia mji wa Sirte, alikozaliwa Gaddafi.

Wapiganaji wa waasi walifanikiwa kupiga picha kwa kutumia simu na kusambaza kwa baadhi ya vyombo vya habari. Walidai kuwa  alionekana katika karavati akitambaa  kujaribu kujificha katika kati mwa mji wa Sirte. Hata hivyo walimpiga risasi mguuni.

Mpiganaji wa waasi, Mohammed al Bibi aliwaambia waandishi wa habari kuwa  baada ya kumwona Gaddafi alisikika akiwaambia askari hao: "Usipige risasi, usipige risasi," huku akiwa katika harakati za kujisalimisha. Kumekuwa na habari za utata kwamba  alifariki dunia baada ya maumivu makali ya majeraha miguuni, huku wengine wakisema  bado yu hai.

Waasi hao walidai kuwa alikutwa akiwa na bastola ya dhahabu  huku akiwa amevalia sare ya jeshi rangi ya  khaki. Ofisa mmoja wa  Baraza la Mpito la Taifa,  Abdel Majid  Mlegta alisema Gaddafi alipigwa pia kichwani.

Alisema alipigwa risasi alipokuwa akijaribu kukimbia  huku mpiganaji mwingine akidai kuwa alipigwa risasi tumboni. Gaddafi na familia yake walikuwa mafichoni tangu  Umoja wa Majeshi ya  Kujihami ya nchi za Magharibi, (NATO), na majeshi ya waasi  kuanza kuishambulia Tripoli  katika kati ya Agosti mwaka huu. Tukio hilo limetokea siku moja baada ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Hillary Clinton  kufanya ziara nchini Libya na kusema kuwa ana imani Gaddafi atakamatwa au kuuawa.

WAASI WAMALIZA KAZI SIRTE

MAJESHI ya waasi  Libya yametangaza kumaliza kazi baada ya kufanikiwa kuuteka mji wote wa Sirte, nyumbani alikozaliwa kiongozi wa zamani wa nchi hiyo, Kanali Mummar Gaddafi. Askari hao walisema walifanya mashambulio ya nguvu yaliyodumu kwa muda wa dakika 90 jana asubuhi.

Hata hivyo baadhi ya askari wanaomtii Gaddafi bado wapo katika mji wa Bani Walid, kusini mashariki mwa Tripoli. "Hii ni siku ya mwisho ya mapigano," alisema Luteni Kanali Hussein Abdel Salam wa kikosi cha Misrata. Alisema  katika awamu ya mwisho ya mapambano, waliweza kuwaona askari wa Gaddafi wakiwa wamejificha ndani ya nyumba kadhaa wakiwa na bunduki na silaha nyingine za kivita.

Serikali mpya ya Baraza la Mpito lilisema kuwa litatangaza Libya kuanguka baada ya kuuchukua mji wa Sirte. Wakati huo huo, Uingereza imeitaka Algeria kutoa ushirikiano dhidi ya Libya kuhusu familia ya Gaddafi ambayo imeomba hifadhi nchini humo. Waziri wa Mambo ya Nje wa  Uingereza, William Hague alikuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufanya ziara nchini humo.

Mtoto wa kike wa Gaddafi, Aisha, kaka yake Hannibal na mama yao  Safiya  wamehifadhiwa  nchini Algeria. Katika mkutano huo wa pamoja  na Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria Mourad Medelci,  Hague alisema  Agleria haipaswi kusita iwapo hata mahakama ya uhalifu wa Kimataifa ukiomba lolote ni lazima isikilizwe.

Alisema ni vema Agleria ikafanya kazi kwa karibu na serikali ya mpito ili kuepuka migogoro inayoweza kujitokeza baadaye.

Hata hivyo kwa upande wake, Medelci alisema watu hao wamepewa hifadhi kwa sababu za kibinadamu  na hata serikali ya mpito ya Libya inatambua hilo.

Wednesday, October 19, 2011

Hotuba ya Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa kwa Waandishi wa habari Monduli, Octoba 19, 2011

Best Blogger Tips

NDUGU wana habari nimewaita katika mkutano huu leo kwa sababu moja kubwa, kutoa ufafanuzi kuhusu matukio ambayo yamekuwa yakitokea huku yakinihusisha mimi binafsi kwa namna ambayo sasa yanatishia ustawi na mshikamano wa kimaadili, kihistoria na kikazi miongoni mwa viongozi na baina ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

"Ndugu wana habari, naamini mmekuwa mkifuatilia kwa karibu habari zinazoripotiwa katika baadhi ya vyombo vya habari zinazolihusisha jina langu na harakati kadha wa kadha chafu ambazo hata mimi mwenyewe ninayehusishwa nazo huwa nazisikia na kuzijua baada ya kuwa zimesharipotiwa katika vyombo hivyo vya habari," alisema.

Alisisitiza kwamba uamuzi wake wa kukutana wanahabari haukuwa na nia ya kuzozana na vyombo vya habari wala kwenda kinyume cha utamaduni wa kimaadili wa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unaotaka viongozi kujadili masuala yanayokihusu chama chao ndani ya vikao rasmi vya kimaamuzi, bali kutoa ufafanuzi na angalizo kwa pande zote hizo mbili ambazo zinaguswa na matukio yanayoendelea kutokea.

Moja ya mambo ambayo yameligusa jina langu kwa namna hiyo ni lile linalonihusisha eti na kundi moja la wanasiasa ambao wamekuwa na mikakati ya kumhujumu mwenyekiti wetu wa chama, Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete. Hakuna shaka ni madai ya kipuuzi, kizushi na yenye malengo machafu.
Hawakuishia hapo sasa wamefikia hatua ya kuvitumia vyombo hivyo hivyo vya habari na kufikia hatua ya kudai kwamba nimeanza kuandaa orodha ya kile wanachokiita madhambi ya Rais Kikwete ambayo wanadai nimepanga kuyasoma wakati wa kikao kijacho cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (CCM).

Ninaamini kwa dhati kabisa kwamba, waandishi wa habari wanaofuatilia kwa karibu na kwa umakini mwenendo wa masuala ya kisiasa nchini wanatambua kwamba, watu wanaopenyeza taarifa hizi katika vyombo vya habari wanafanya hivyo kwa malengo ya kufikirika ya kujisafishia njia kisiasa.

Ni jambo lisiloingia akilini kunihusisha na kile kinachoitwa mikakati ya kumhujumu rais au chama ambacho mimi ni kada wake wa muda mrefu, mbunge anayetokana na chama hicho hicho na mtu ninayeiongoza Kamati nyeti ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na zaidi ya yote kiongozi wa ngazi mbalimbali za kisiasa na kiserikali nilizowahi kushikilia.

Kuhusu hili napenda kusema kwa uwazi kwamba, mbali ya ukweli kuwa sijapata kufikiria hata mara moja kuhusu hicho wanachokiiita mabaya au madhambi ya rais, sina na wala siijui hiyo wanayoitaja kuwa ni orodha ya mabaya ya namna yoyote dhidi ya Rais Kikwete.

Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits