Tuesday, August 31, 2010

Best Blogger Tips
Shule iliyokumbwa na mashetani

Via darleo

BAADA ya zaidi ya wanafunzi 26 wa Shule ya Msingi Tumaini kuanguka jana na maruhani leo shule hiyo ilionekana kupwaya baada ya wanafunzi kutofika shuleni wakihofia kukumbwa na masaibu hayo.

Gazeti hili leo asubuhi lilishuhudia shule hiyo ikiwa na idadi ndogo ya walimu na wanafunzi, hali ambayo ilizidi kuifanya shule hiyo kuzizima kutokana na ukimya uliokuwapo.

Imebadinika kuwa baadhi ya wazazi wamelazimika kuwakataza watoto wao kwenda shule kwa kuhofia kukumbwa na balaa hilo.

Akizungumza na gazeti hili leo asubuhi, mwalimu mmoja wa shule hiyo ambaye hakupenda jina lake kuandikwa gazetini kwa madai kuwa si msemaji, alidai kuwa tukio hilo si la kwanza na kwamba kuna uwezekano kukawa na tatizo.

“Kuna taarifa kuwa eneo hili lilikuwa ni la makaburi, hivyo kuna maruerue yanayojitokeza,” alidai mwalimu huyo.
Jana mwalimu mmoja wa shule hiyo, Godfrey Wilbard, wakati akifundisha darasani, ghafla alisikia wmanafunzi mmoja akipiga mayowe akidai kuwa anaona watu walioko uchi na huku wakimwita.
Baada ya muda mwanafunzi huyo alizirai huku akifuatiwa na wanafunzi wenzake wadarasa la saba.

Kutokana na hali hiyo kuendelea idadi ya wanafunzi ilizidi kuongezeka kuanguka jambo lililozua utata kwa wazazi wa wanafunzi hao kulazimika kukimbilia shuleni hapo.

Imedaiwa kuwa wakati wanafunzi hao walikuwa wakizungumza maneno ya yasiyoeleweka ambapo walimu na wazazi walilazimika kuwakimbiza kwenye kanisa la Assembles of God lililopo jirani kwa ajili ya kuombewa.

Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni saa 4.30, bado idadi ya wanafunzi shuleni hapo ilikuwa ndogo na hata waliokuwepo walionekana kuwa na woga.
Best Blogger Tips
Idadi ya raia Kenya yafikia milioni 38


Idadi ya wakazi nchini Kenya imefikia milioni 38.6 (38,610,097), takwimu hizo ni kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka 2009. Kati ya takwimu hizi idadi ya wanaume kwa wanawake imeonekana sawa jinsia zote zikifikia milioni 19.4 wanawake na milioni 19.2 wanaume.

Akitangaza matokeo ya sensa waziri wa mipango ya taifa, Wycliffe Oparanya, hata hivyo amesema matokeo ya wilaya nane yalibatilishwa kutokana na dosari katika kukusanya idadi ya raia wa maeneo hayo.

Wilaya ambazo idadi ya raia haikutolewa ni zile za Kaskazini mwa Kenya ikiwa ni pamoja na Lagdera, Wajir Mashariki, Mandera Kati, Mandera Mashariki, Mandera Magharibi, Turkana Kati na Turkana Kusini.

Bw Oparanya amesema dosari hizo zilipatikana baada ya idadi ya raia kuonekana kuwa juu kuliko nakili za watoto wanaozaliwa na ripoti ya vifo.
Endelea kusoma habari hii....................

Sunday, August 29, 2010

Rais Kikwete akiwa Sumbawanga

Best Blogger Tips
Rais Jakaya akishuka kwenye Helkopta mara baada ya kuwasili Sumbawanga mjini tayari kwa mkutano uliofanyika jana kwenye uwanja wa Mandele mjini humo.

                                           
Umati wa wakazi wa Sumbawanga mjini waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni ili kumsikiliza rais Jakaya Kikwete jana wakati alipohutubia wakazi wa mji mhuo.

Tuesday, August 24, 2010

Best Blogger Tips
Akina mama wakilia kwa uchungu baada ya Mgombea wao wa urais kupitia chama cha mapinduzi CCM. Rais Jakaya Kikwete kuanguka ghafla wakati akihutububia wafuasi wa chama hicho jangwani.(Photo: pwaniraha.com)
Best Blogger Tips
JK ahaha kunusuru mpasuko CCM


MWENYEKITI wa CCM Jakaya Kikwete jana alitumia mkutano wa kampeni kwenye jimbo la Buchosa kujaribu kutuliza wimbi la wanachama wanaohamia vyama vya upinzani kupinga matokeo ya kura za maoni za kupata wagombea ubunge na udiwani, akiwataka waige mfano wake wa uvumilivu.

Alikuwa ameshtushwa na kitendo cha mbunge wa zamani wa Jimbo la Busega, Dk Raphael Chegeni kutoonekana katika msafara ulioenda kumlaki alipowasili na pia kutoonekana kwenye mkutano wa hadhara kwenye jimbo hilo ambalo makada wanne wa CCM wamefungua kesi kumpinga mgombea wa CCM, Dk Charles Tizeba.

Kikwete aliongoza awamu ya kwanza ya kura za maoni za kutafuta mgombea urais wa CCM mwaka 1995, lakini katika amu ya pili aliangushwa na Benjamin Mkapa ambaye baadaye alishinda uchaguzi na kuwa rais wa serikali ya awamu ya tatu.
Endelea kusoma habari hii....................

Thursday, August 19, 2010

Best Blogger Tips
Mwanamume akutwa amefia chumbani Dar

MWANAMUME Omari Disomba, maarufu kwa jina la Kitimutimu (54), ambaye kazi yake ilikuwa ni dereva teksi, amekutwa amekufa chumbani kwake huku maiti yake ikiwa kitandani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Elias Kalinga, amesema tukio hilo limetokea jana saa 12 jioni, Ubungo Kibo.

Amesema mwili wa marehemu huyo umekutwa hauna jeraha lolote na chanzo cha kifo chake bado hakijafahamika.

Kwa mujibu wa Athuman Amri (34), mkazi wa Ukonga Magereza, enzi za uhai wake marehemu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu.

Maiti imehifadhiwa chumba cha maiti Hospitali ya Mwananyamala kwa uchunguzi zaidi na upelelezi unaendelea.

Wakati huo huo, polisi inawashikiliwa wakazi wanane kwa tuhuma za kukutwa na bangi puli 47, miskoto 60 na pombe haramu ya gongo lita 20.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Elias Kalinga, amesema watuhumiwa hao walikamatwa jana saa 3 asubuhi, Magomeni Mapipa, Bonde la Madaba.

Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Scola Mambo (43), Ramadhani Saidi (24), Hawa Adamu (18), JUlieth JOhn (34) na wenzao wanne.
Source: Darleo

Wednesday, August 18, 2010

Best Blogger Tips
Kibao chageukia aliyechukua nafasi ya Bashe Nzega

Via ippmedia

 Wakati msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Isaac Nantanga, akisema kuwa kwa mujibu wa nyaraka zilizoko, mgombea ubunge jimbo la Nzega aliyeenguliwa, Hussein Bashe, ni raia wa Tanzania, aliyepewa nafasi yake na Chama Cha Mapinduzi (CCM), naye ameibua mambo mapya juu ya uraia wake.

Taarifa kutoka jimboni humo zilieleza Dk. Hamis Andrew Kigwangala ambaye alipitishwa na chama hicho uraia wake unadaiwa kuwa na utata.

Kuna taarifa kwamba Dk. Kigwangala jana alihojiwa na maofisa wa Idara ya Uhamiaji katika ofisi za Wilaya ya Nzega wakati akirudisha fomu ya kuwania ubunge kwa msimamizi wa uchaguzi.

Dk. Kigwangala aliteuliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kugombea nafasi hiyo baada ya Bashe aliyekuwa mshindi katika kura za maoni kuenguliwa baada ya kudaiwa kwamba sio raia wa Tanzania.

Habari hizo zilieleza kwamba, Dk. Kigwangala naye uraia wake una utata na kwamba jina alilotumia shuleni (Hamis Andrew) sio la kwake na kuwa mwenyewe yupo wilayani humo, lakini hivi sasa inadaiwa kwamba amefichwa.

Taarifa zaidi zinaeleza kwamba jina lake halisi ni Said Nassor Magaile.

Aidha, inadaiwa kwamba baada ya mgombea huyo kushtukia uraia wake, jana alikimbilia katika Mahakama ya Wilaya kukana jina lake halisi ambalo ni Said Nassor.
Endelea kusoma habari hii.........................

Thursday, August 12, 2010

Best Blogger Tips
Rapper buys $2 million sports car

Birdman Shows Off His $2.1 Million Bugatti

Southern rapper Birdman is showing off the kind of toy a few million dollars can buy: the Bugatti Veyron. The European sports car is not only one of the most expensive things you can buy on four wheels, but it's also the fastest street car on the planet.

Birdman, who goes by his real name, Bryan Williams, when he's doing business as the CEO of Cash Money Records, is making sure everyone knows about his $2.1 million mode of transportation, too. The Dirty South rapper and his crew snapped some shots of the all-red sports car while holding a business card that reads "I am expensive," a statement which would be pretty hard to argue with, given the car's estimated $300,000 annual upkeep costs.


Access the full story..............

Saturday, August 7, 2010

Best Blogger Tips
Dk. Slaa ateka Moshi, Tanga

Leo kunguruma jijini Dar

Via ippmedia

Umati mkubwa wa wakazi wa mji wa Moshi na wilaya za jirani juzi walijitokeza kwa wingi kumlaki mgombea urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk.Willbroad Slaa.

Wananchi hao ambao walijitokeza kwa maandamano ya magari, pikipiki na baiskeli walitembea maeneo mbalimbali ya mji wa Moshi na baadaye majira ya saa tisa alasiri walikwenda kumlaki Dk. Slaa katika uwanja mdogo wa ndege mjini hapa.

Vifijo na nderemo zilizidi pale Dk. Slaa na msafara wake ulipoingia kwenye eneo la mkutano katika viwanja vya Manyema kata ya Bondeni majira ya saa 11:30, huku wananchi wakionyesha ishara ya Chadema na kila aina ya shauku ya kumuona.
Endelea kusoma habari hii......................

Friday, August 6, 2010

Best Blogger Tips
Michaele Salahi Claims Whoopi Goldberg Hit Her?

Michaele Salahi and the other cast members from The Real Housewives of DC were on The View yesterday to promote their show. Michaele started going off with another of those old crows about how they were catty toward each other. They really got off topic. So much, that Whoopi Goldberg
emerged from the back, touched Michaele lightly and asked her if they could get back to the White House. Apparently that made Michaele a bit livid, because after the show, she claimed that Whoopi had hit her.

Or something like that….

Whoopi got wind of the “hitting” lie and confronted Michaele after the show. She proceeded to drop a rambling slew of F-bombs toward the guest, whose husband tried to film on his BlackBerry. Now, their lawyer is claiming that Whoopi defamed and abused Michaele. Go figure. These famewhores will never learn.



Access the full story..................

Thursday, August 5, 2010

Best Blogger Tips
Man accused of Facebook bigamy denies double life

John France claims that Lynn France ‘knew everything I was doing'

In the second part of a tangled he-said, she-said tale of two weddings and a Facebook page, the man accused of bigamy uncovered on the social network claims it’s largely the product of his estranged wife’s imagination.

Tuesday on TODAY, Lynn France said she learned that John France — with whom she had two sons after a gala 2005 wedding — had taken a second bride only when she saw pictures of that second wedding on the Facebook page of John’s new wife, Amanda. Lynn asserts she is still married to John, and that he has spirited away their two toddler sons.

But on Thursday, John France appeared on TODAY with Amanda and an attorney to tell a decidedly different story. He asserted his marriage to Lynn was never valid in the first place, and that Lynn knew what he was up to every step of the way.

“I was not carrying on a double life, no way,” France told Matt Lauer. “I’m no angel, OK? But Lynn knew everything I was doing.”
Access the full story........................

Tuesday, August 3, 2010

Best Blogger Tips
Kikwete aomboleza kifo cha Jidulamabambasi

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi, Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba kutokana na kifo cha Amani Jidulamabambasi kilichotokea juzi.

Jidulamabambasi alikuwa miongoni mwa wanachama wa CCM waliokuwa wamejitokeza kuwania kuteuliwa na kugombea Ubunge Maswa Magharibi.

“Ninakutumia salamu za rambirambi wewe Katibu Mkuu wa CCM na wana– CCM kote nchini kwa kumpoteza mmoja wa makada katika chama chetu”, alisema Kikwete.

Aliongeza, “aidha kupitia kwako, natuma salamu za rambirambi na pole nyingi kwa familia ya marehemu Amani kwa kuondokewa na kiongozi muhimu wa familia yao.”

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Kikwete amemwelezea Amani kuwa miongoni mwa makada jasiri wa CCM wasiokata tamaa katika medani za siasa na mpambanaji hodari aliyekuwa na dhamira ya dhati ya kulitumikia taifa na umma wa Watanzania.
Source: HabariLeo
Best Blogger Tips
9 dead in shooting at Conn. beer distributor


Officials say gunman shot himself as police approached

MANCHESTER, Conn. — An employee who had been asked to resign for stealing went on a shooting rampage Tuesday at a beer distributing company, killing eight people and wounding others before fatally shooting himself, officials said.

The shooting took place at Hartford Distributors Inc., about 10 miles east of Hartford.

The company identified the shooter as Omar Thornton, a 34-year-old warehouse driver.

The driver had worked at the distributor for a couple of years and been called in for a disciplinary hearing, said John Hollis of the Connecticut Teamsters, who was with company officials at the scene of the shooting.

"The union was bringing him in to meet with the company to remedy the problem," Hollis told the Hartford Courant. "He started shooting."

"He wanted to say goodbye and he loved everybody," said Joanne Hannah, whose daughter Kristi had dated Thornton for eight years.
Access the full story.........................

Monday, August 2, 2010

Best Blogger Tips
Alicia Keys afunga ndoa na Swizz Beatz


 Alicia Keys ameolewa na mtayarishaji wa muziki Swizz Beatz, ambaye ana ujauzito wake, katika hafla iliyofanyika kwa faragha mwishoni mwa wiki.

Wapenzi hao walifunga ndoa siku ya Jumamosi katika eneo moja ambalo halikutangazwa hadharani.

Mwakilishi mmoja wa Keys alithibitisha kufanyika kwa sherehe hiyo ya harusi kwa shirika la habari la AP siku ya Jumapili.

Mwanamziki huyo aliyewahi kushindi tuzo za Grammys na Swizz Beatz- ambaye jina lake halisi ni Kasseem Dean- wamekuwa pamoja tangu mwaka 2008.

Keys, mwenye umri wa miaka 29, ameshinda tuzo 12 za Grammys tangu kutoa albamu yake ya kwanza Songs in A Minor mwaka 2001.

Dean, mwenye umri wa miaka 31, ambaye ana watoto wawili kutoka ndoa yake ya mwanzo, ameandika na kutayarisha nyimbo za wasanii zilizovuma sana akiwemo Beyonce na mumewe Jay-Z.

Key aliimba katika sherehe za ufunguzi za Kombe la Dunia mwezi Juni.
Source: BBC

Sunday, August 1, 2010

Best Blogger Tips
 Bushman - Worries and Problems

Best Blogger Tips
Matokeo ya kura za maoni zanzibar, wengi wasema NDIYO kutaka serikali ya mseto


Registered Voters - 407,669
Valid Votes - 266,064
Invalid Votes - 8,309
Total Turn Out - 274,373
Percent Turn Out - 67.00%
Polling Stations Published 1,210 of 1,292
NDIO / YES = 175,476
HAPANA / NO = 90,588
Taarifa nyingine toka mitaani zinasema kuwa majimbo yaliyoshikilia kura ya HAPANA ni Amani, Chaani, Chwaka, Dole, Kwahani, Makunduchi, Muyuni na Uzini.
Best Blogger Tips
Is he the actual father?


Find more videos like this on mytings
Best Blogger Tips
Vituko Vya Uchaguzi - TZ

AONYWA KUJIITA OBAMA
KATIKA jimbo la Bunda, kulikuwa na habari kuwa mgombea Ginche Kisase, ameonywa akitakiwa kuacha kujinadi kwa kutumia jina la Rais Barack Obama wa Marekani, kwa kuwa hawafanani. Onyo hilo lilitolewa na wanachama wa CCM kata za Kunzugu na Mcharo, wakati mgombea huyo akijinadi kuomba kura. Hilo liliibuka baada ya Kisase kusimama kujinadi na kudai anafahamika zaidi kama Obama, jina ambalo alidai amepewa na wananchi. Baada ya kujinadi hivyo, baadhi ya wanachama waliguna, huku wengine wakizomea na kupaza sauti kuashiria kutokubaliana naye. Kwa upande wake, Kisase alisema mtu akitaka kumuita Obama yuko huru na asipotaka anaweza kumuita vingine.

AJINADI KWA KUOGESHA WAZEE
MGOMBEA ubunge, Peter Msuya, aliwavunja mbavu wanachama wa CCM wakati akinadi sera zake, kwa kusema akichaguliwa atajenga kituo cha kuwaosha vikongwe. Msuya anayewania jimbo la Ubungo, alisema kuanzishwa kituo hicho kutaleta ajira kwa vijana, kwani hata Ulaya watu wanafanya kazi hizo na kujipatia fedha na kununua magari ya kifahari na kuahidi kuwa, fedha za mfuko wa jimbo zitatumika kutatua kero jimboni humo. Naye mgombea Alfred Nchimbi, akijinadi alisema anatakiwa kiongozi atakayeleta maendeleo na si kupiga kelele.
Source: Uhuru

Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits