Wednesday, June 30, 2010

Best Blogger Tips
Mr II ajitosa ubunge Mbeya Mjini

 SIKU moja baada ya msanii nguli, mwasisi wa muziki wa kizazi kipya ‘Bongo fleva’ hapa nchini, Joseph Mbilinyi ‘Mr II Sugu’ kushikiliwa na polisi kwa mahojiano, jana alitangaza nia ya kuwania ubunge katika Jimbo la Mbeya Mjini sambamba na kufafanua tuhuma zilizomfanya ashikiliwe na chombo hicho cha dola.

Kwa mujibu wa taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa jijini Dar es Salaam jana, Mbilinyi ambaye anajulikana zaidi katika anga la muziki kama Mr II ama Sugu, anatangaza rasmi kugombea ubunge katika Jimbo la Mbeya Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo ().

“Kwa muda mrefu katika maisha yangu ya kimuziki, pamoja na kuimba nyimbo za kuburudisha nimekuwa zaidi mstari wa mbele kuimba nyimbo za kutetea haki za makundi mbalimbali katika jamii na taifa kwa ujumla. Wakati umefika sasa wa kuhamisha jukwaa la mapambano ya kudai haki, kutoka jukwaa la muziki mpaka jukwaa la siasa, kwa dhamira ile ile ya kutumia kipaji changu alichonijalia Mwenyezi Mungu, kuimba na kuhutubia kwa ajili kuleta mabadiliko ya kweli katika taifa letu,” alisema Mr II na kuongeza:

“Nyimbo zangu zimekuwa zikibeba sauti ya watu wasio na sauti, ili zisikike kwa watawala, lakini hata hivyo kwa kipindi chote ambacho nimekuwa nikifanya harakati hizi watunga sheria na wafanya maamuzi ya kisera chini ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameshindwa kuongoza vizuri taifa kuweza kufanya mabadiliko ya kweli, yenye kuhakikisha Watanzania wananufaika na vipaji vyao ambavyo Mwenyezi Mungu amewajalia na taifa linanufaika na rasilimali na maliasili ambazo tumejaliwa kuwa nazo.”

Alisema anatangaza nia ya kugombea ubunge ili kuchangia katika kuongeza nguvu ya chama mbadala katika Bunge la Jamhuri ya Muungano, awe ni sehemu ya sauti mbadala katika kutunga sheria, kuwawakilisha wananchi, kuandaa sera na kuiwajibisha serikali kuweza kutekeleza yale ambayo yeye na wanaharakati wenzake katika sanaa wamekuwa wakiyapigia kelele muda mrefu kupitia muziki na maisha yao.
Endelea kusoma habari hii.................

Saturday, June 26, 2010

Best Blogger Tips
Ghana yafuzu kucheza robo fainali

Gyan Asamoah akiachia mkwaju kutikisa nyavu za Marekani na kuipatia Ghana tiketi ya kucheza robo fainali.

Black Stars imezidi kuibeba Afrika, baada ya timu hiyo ya Afrika Magharibi kufuzu kwa robo fainali ya Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini ilipoitandika Marekani mabao 2-1 katika uwanja wa Royal Bafokeng, mjini Rustenburg.

Mechi hiyo iliingia muda wa ziada baada ya kipindi cha kawaida kumalizika 1-1.

Wakishangiliwa na maelfu ya mashabiki waliofurika uwanja huo, vijana wa Ghana walianza kwa kasi huku wakionyesha mchezo wa hali ya juu na katika dakika ya nne ambapo Kevin-Prince Boateng alipopenya safu ya ulinzi ya Marekani na kuipatia Black Stars bao la kwanza.

Kipindi cha pili kilimalizika Ghana wakiongoza 1-0, na katika kipindi cha pili walilazimika kuimarisha safu ya ulinzi baada ya Marekani kurejea na mwamko mpya, hasa mshambuliaji wao hodari Landon Donovan.

Katika dakika ya 62 Jonathan Mensah alimwangusha Clint Dempsey kwenye eneo la hatari na hapo mwamuzi kutoka Hungary, Viktor Kassai akawapa Marekani penalti, ambayo Landon Donovan aliifunga, na kusawazisha.

Muda wa kawaida ulimalizika kwa matokeo hayo ya 1-1 na kulazimisha mechi kuingia muda wa ziada.

Dakika tatu tu baada ya muda wa ziada kuanza Asamoah Gyan alihimili kumbo la mlinzi wa Marekani, Carlos Bocanegra, na kuifikia pasi ndefu iliyotoka kwa Andre Ayew, na kusukuma mkwaju mkali hadi kwenye nyavu za lango la Marekani.

Sasa Ghana inasubiri kucheza na Uruguay kwenye robo fainali Ijumaa ijayo.

Friday, June 25, 2010

Best Blogger Tips
Remembering Michael Jackson


MusicPlaylistRingtones
Create a playlist at MixPod.com

Tuesday, June 22, 2010

Best Blogger Tips
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa  katika mazungumzo na Rais Mstaafu wa Marekani Bill Clinton Ikulu jijini Dar es Salaam leo mchana.

Sunday, June 20, 2010

Best Blogger Tips
CJ Dippa Dallas America's Got Talent 2010

Best Blogger Tips
Raia wa Australia hawaonekani Afrika

Via BBC

  Wasiwasi unazidi kuongezeka juu ya usalama wa wakurugenzi wa migodi ambao ni raia wa Australia kutokana na ndege yao kutokujulikana ilipo.

Ndege hiyo ilikuwa ikitokea Cameroon kuelekea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Abiria tisa walikuwepo kwenye ndege hiyo, akiwemo mmoja wa matajiri wakubwa wa Australia Ken Talbot.

Kundi hilo lilitoka katika mji mkuu wa Cameroon, Yaounde siku ya Jumamosi kutembelea miradi ya madini ya chuma huko Yangadou, eneo lililo kijijini huko Kongo.

Jeshi la Cameroon linaongoza msako wa ardhini na angani kwenye msitu mkubwa sana.Ndege waliyokuwa wakisafiria lilikodishwa na kampuni ya migodi ya Australia, Sundance Resources.
Endelea kusoma habari hii............

Saturday, June 19, 2010

Best Blogger Tips
Former center Manute Bol dies at age 47

Via NBA.com

Manute Bol, a lithe 7-foot-7 shot-blocker from Sudan who spent 10 seasons in the NBA and was dedicated to humanitarian work in Africa, died Saturday. He was 47.

Bol died at the University of Virginia Hospital in Charlottesville, where he was being treated for severe kidney trouble and a painful skin condition, Tom Prichard, executive director of the group Sudan Sunrise, said in an e-mail.

"Sudan and the world have lost a hero and an example for all of us," Prichard said. "Manute, we'll miss you. Our prayers and best wishes go out to all his family, and all who mourn his loss."

Bol played in the NBA with Washington, Golden State, Philadelphia and Miami, averaging 2.6 points, 4.2 rebounds and 3.3 blocks for his career. He led the league in blocks in 1985-86 with Washington (5.0 per game) and in 1988-89 with Golden State (4.3 a game).

"Manute's impact on this city, our franchise and the game of basketball cannot be put into words," 76ers president and general manager Ed Stefanski said in a statement. "He ... was continually giving of himself through his generosity and humanitarian efforts in order to make the world around him a much better place, for which he will always be remembered."
Access the full story..............
Best Blogger Tips
Kikwete atangaza mikoa, wilaya mpya

Via Mwananchi

RAIS Jakaya Kikwete ametangaza mikoa mitatu , wilaya, tarafa na halmashauri za wilaya mpya ili kuimarisha utawala bora.

Kwa sasa Tanzania bara ina mikoa 26 hivyo kwa tangazo hilo la kusudio la kuanzisha mikoa mipya mitatu itafikia 29.

Hata hivyo, Pinda alidokeza kuwa mazungumzo bado yanaendelea kuhusu uanzishwaji wa mkoa wa Mpanda na mkoa wa Arusha kupewa hadhi ya kuwa Jiji.

Wakati hayo yakiwa yanaelezwa taarifa zinaonyesha kuwa gharama ya kuanzisha mkoa mpya ni kati ya Sh4 mpaka 6 bilioni na kwa wilaya mpya ni Sh1 bilioni.

Gharama hizo zinajumuisha ujenzi wa makao makuu, kulipia gharama za uendeshaji, kuweka miundombinu muhimu pamoja na kuajiri watumishi.
Endelea kusoma habari hii................
Best Blogger Tips
Mwalimu afa akifuata mshahara

Via Majira

WATU wawili wamefariki akiwemo mwalimu wa Shule ya Msingi ya Kivisini baada ya kuangukiwa na mti wakati wakiendesha baiskeli kwenda mjini kuchukua mshahara.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mwanga, Bw. Willy Njau alitoa taarifa hiyo wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani cha kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo.

Mwalimu huyo ni Edmund Mtungo na mkulima Gerald Aloyce ambaye alifariki akipatiwa matibabu katika zahanati ya Kifaru wilayani hapa.

“Wakiwa kwenye baiskeli, bahati mbaya mti ulianguka ghafla na kumgonga mwalimu Mtungo na kufariki papo hapo huku mkulima akijeruhiwa vibaya kichwani na maeneo mengine mwilini, lakini
baadaye naye alikufa akipatiwa matibabu,” alisema.

Miili ya marehemu wote wawili imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya usangi ikisubiri mazishi yao ambayo yatafanyika Kilomeni na Kivisini.

Friday, June 18, 2010

Best Blogger Tips
Lakers vs Celtics

Finals Game 7 Mini-Movie

Thursday, June 17, 2010

Best Blogger Tips
Lakers Mabingwa NBA Finals 2010

Waifunga Celtics 83-79

Derek Fisher, akiwa na mkewe Candace, wakisheherekea ubingwa baada ya kuifunga Boston, Celtics 83-79, huko Staples Center, Los Angeles.

Licha ya Kobe Bryant kutofanikiwa kufunga mara nyingi, aliweza kufunga mara 6 baada ya kujaribu  mara 24 na kufanikiwa kupata point 23, huku Pau Gasol akipata point 16 baada ya kufanikiwa kufunga mara 6 baada ya kujaribu kufunga mara19, waliweza kuibuka washindi baada ya kuifunga Boston, Celtics 83-79, katika mchezo uliochezwa Staples Center, L.A.

Mchezo ulikuwa mkali sana, huku timu zote zikiwa imara katika ulinzi, hali iliyopelekea uhaba wa magoli, kwani ushindi huo wa 83-79 unadhihirisha ni jinsi gani timu zote mbili zilivyokuwa imara katika ulinzi. Ron Artest aliamsha uhai wa Lakers baada ya kurusha mpira na kupata point tatu muhimu katika dakika za mwisho za mchezo huo.

Kobe Bryant ndiye MVP wa mwaka huu, akiwa na wastani wa point 28.6, rebounds 8 na 3.9 assists katika mlolongo wa michuano hiyo. Hii inakuwa ni mara yake ya pili kuchukua taji hilo, mara ya kwanza ilikuwa ni mwaka jana. Pia hii inakuwa ni mara ya 5 kwa Kobe Bryant kuchukua ubingwa huu, mara zote akiwa na Lakers. Bado hajafikia record ya mkongwe Michael Jordan, ambaye alichukua ubingwa huo mara 6, na alikuwa MVP mara 6.

Phil Jackson, anakuwa kocha wa kwanza katika historia ya mchezo huo, kwa kuchukua ubingwa huo mara 11.

Rais wa Marekani, Barack Obama, ambae ni mpenzi mkubwa wa mchezo huo, alitabiri Lakers kuwa mabingwa mwaka huu katika mahojiano yake na TNT.

Celtics, bado wana sifa nzuri katika historia ya mashindano hayo, kwani wameshachukua ubingwa huo mara 17, ukilinganisha na Lakers ambao baada ya kuchukua ubingwa mwaka huu, inakuwa ni mara ya 16, ikiwa nyuma ya Celtics mara 1.
Best Blogger Tips
It's do-or-die time for the Lakers


If they win Game 7 against Boston for second straight title, it significantly improves chances the group will stay long enough to earn more. If they lose, that hope dies and everyone may scatter.

Game Seven. Game Heaven. Game Hell.

The most important three hours in Lakers' history arrive Thursday night on the happy feet of hope beset by the nagging twinges of doom.

"Life or death," said Kobe Bryant, pausing. "But not that extreme."

If the Lakers win, it would be their 16th championship, one short of Boston's record 17 titles. It would be Bryant's fifth ring, one short of Michael Jordan. It would bring the Lakers to within two years of one of the greatest climaxes in sports history, and owner Jerry Buss would never do anything to ruin a Hollywood ending.

Tuesday, June 15, 2010

Best Blogger Tips
Lakers make it one for all

They dominate Celtics from the start and force Game 7 with an 89-67 victory.

The Larry O'Brien trophy was in the building, as was Boston Celtics legend Bill Russell, along with boxes and boxes of T-shirts and hats designating the Celtics as the 2010 NBA champions.

None of them became part of the postgame program.

The Lakers made sure of it, clearly and convincingly, thumping the Celtics, 89-67, and forcing a Game 7, in case it wasn't clear by the time Russell headed for the exit with three minutes left Tuesday at Staples Center.

Kobe Bryant was solid, Pau Gasol was borderline spectacular and there was no way to ignore a resurgent effort from the Lakers' reserves, who were outscoring Boston's backups at one point, 24-0.


So much for the franchise's recent Game 6 wobbles against the Celtics, the Lakers moving past their 39-point loss to them two years ago in a humbling part of their playoff history.

Game 7 is definitely necessary. It'll be Thursday night at Staples Center. Home teams are 13-3 all-time in Game 7 of the Finals.

Bryant found a way to sift through the previous eight months and 104 games by saying of Thursday night: "It's a game we've got to win. It's as simple as that."

He had 26 points and 11 rebounds Tuesday, but it was Gasol who rebounded from a meek 12-point effort in Game 5, coming close to a triple-double Tuesday with 17 points, 13 rebounds and nine assists, the latter a playoff career-high for him.
Access full story...............
Best Blogger Tips
Ivory Coast yatoka sare na Ureno

Ivory Coast imetoka sare 0-0 na Ureno kwenye mechi ya kundi G la Kombe la dunia, katika uwanja wa Nelson Mandela Bay mjini Port Elizabeth.

Ivory Coast iliudhibiti mchezo lakini umaliziaji wa Gervinho na Salomon Kalou ukakosa kuzaa matunda.

Mshambuliaji wa Ivory Coast Didier Drogba aliingia katika kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Salomon Kalou baada ya shirikisho la soka duniani FIFA kumruhusu kufunga kifaa mkononi ili kulinda jeraha lake.

Hata hivyo kuingia kwa Drogba hakukufanikisha safu ya ufungaji, akibanwa na walinzi wa Ureno.

Awali katika mechi shuti la Cristiano Ronaldo liligonga mwamba.

Mechi ya Ivory Coast itakayofuata itakuwa dhidi ya Brazil siku ya Jumapili, kabla ya kumalizia michuano ya makundi dhidi ya Korea Kaskazini tarehe 25.

Mlinzi wa Ivory Coast Kolo Toure aliondoka uwanjani akichechemea baada ya kupata jeraha, na bado haijawa wazi ikiwa ataweza kushiriki michuano itakayofuata.

Refarii Jorge Larrianda aliwaonyesha kadi ya njano Cristiano Ronaldo na Guy Demel kwa kujibizana wakiambiana maneno yasiyokubalika.

Kundi la G linaelezewa na wengi kuwa kundi la 'kifo' , kwani mbali na Ureno na Ivory Coast, linajumuisha mabingwa mara tano wa kombe la dunia Brazil na Korea Kaskazini.
Source: BBC

Sunday, June 13, 2010

Best Blogger Tips

JK kukutana na watoto kesho

Via ippmedia  

Rais Jakaya Kikwete kesho anatarajiwa kukutana na watoto jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine watamuuliza maswali zaidi ya 20 likiwemo kwa nini serikali haijasajili Baraza lao la Watoto lililoanzishwa miaka minane iliyopita.

 Katika mazungumzo hayo watoto pia watamhoji Rais Kikwete juu ya nini kinafanywa na serikali ili kupunguza vitendo vya unyanyasaji dhidi ya watoto, unyonyaji, kuongezeka kwa mimba za utotoni na mikakati ya kuwaondoa mitaani.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi, mtoto Rehema Abbas atakayeongoza watoto kumhoji Rais, alisema katika mahojiano hayo watoto kumi watawawakilisha wenzao wanaokaribia nusu ya watanzania wote kwa sasa. 

 

Friday, June 11, 2010

Best Blogger Tips
Kitukuu wa Nelson Mandela afariki Dunia

 
Kitukuu wa Nelson Mandela, Zenani Mandela amefariki dunia.

Afisi ya uhusiano mwema katika wakfu wa Nelson Mandela imesema kuwa msichana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 13, alifariki katika ajali ya barabarani iliyompata akiwa njiani kutoka sherehe za mkesha wa Kombe la Dunia mjini Soweto.

Duru za polisi zimesema kuwa dereva aliyesababisha ajali hiyo amekamatwa.
Huku hayo yakiarifiwa, mechi ya kwanza kabisa ya Kombe la Dunia kuwahi kufanyika barani Afrika itafanyika Ijumaa jioni kati ya wenyeji Afrika Kusini na Mexico.
Timu 32 zinachuana kuwania kombe hilo baada ya mwezi mmoja na aliyekuwa rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, hatahudhuria sherehe ya ufunguzi.
Source: BBC
Best Blogger Tips
Unasemaje kuhusu hii

Hivi ndivyo jina la yeye mwenyewe Zuma linavyoelezeka
Just
Another
Creator
Of
Babies

and

Zero
Understanding of
Marriage and
Aids


Best Blogger Tips
Wazazi wa Gary Coleman waongea


Visit msnbc.com for breaking news, world news, and ne
Best Blogger Tips
Afrika Kusini yatoka sare 1-1 na Mexico

Wenyeji Bafana Bafana wa Afrika Kusini watoka sare 1-1 na Mexico katika mechi ya ufunguzi ya Kombe la Dunia.

Afrika Kusini wenyeji wa fainali za Kombe la Dunia walianza mashindano hayo Ijumaa kwa kutoka sare 1-1 na Mexico katika mechi ya ufunguzi iliyokuwa na kandanda la kusisimua kabisa baina ya timu hizo mbili. Katika mechi ya pili ya kundi A Ijumaa Ufaransa na Uruguay zilitoka sare 0-0 katika mechi ambapo Uruguay walimaliza mchezo wakiwa wamebakiwa na wachezaji kumi tu baada ya mchezaji wao mmoja kupigwa kadi nyekundu.

Winga wa Afrika Kusini Siphiwe Tshabalala alifunga goli la kwanza katika fainali za mwaka huu katika dakika ya 55 katika uwanja wa Soccer City. Lakini mlinzi wa Mexico Rafael Marquez alipata bao la kusawazisha katika dakika ya 79 ya mchezo.

Thursday, June 10, 2010

Best Blogger Tips
R.I.P Oliver Ngoma

Tuesday, June 8, 2010

Best Blogger Tips
Mwalimu mwingine adaiwa kuoa mwanafunzi wake

SIKU chache baada ya mwalimu mmoja wa shule ya Sekondari ya Byuna wilayani Bariadi mkoani Shinyanga kukamatwa kwa kufunga ndoa na mwanafunzi wake, mwalimu mwingine wa Sekondari ya Nyakabindi wiyalani humo pia amebainika kuoa mwanafunzi wake baada ya kumtia mimba na kuishi naye kama mke.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa timu ya waandishi wa habari ambao waliambatana na maofisa wa Shirika la Utu Mwanamke katika utafiti wa mimba za utotoni wilayani Bariadi, Mwalimu huyo (Jina linahifadhiwa) ambaye ni makamu mkuu wa shule anadaiwa kuwa anaishi na mwanafunzi huyo tangu mwaka 2008 baada ya kupata ujauzito.

Mwalimu huyo anadaiwa kumpatia ujauzito mwanafunzi (Jina linahifadhiwa) ambaye inaelezwa kuwa alikuwa akisoma shule hiyo Nyakabindi, lakini kutokana na kuwa na mahusiano ya siri ya mapenzi na mwalimu wake alipata mimba na hivyo kuamua kumuoa kwa siri ambapo sasa anaishi naye.

Wakizungumza baadhi ya wanafunzi ambao walikuwa wakisoma na mwanafunzi huyo walieleza kuwa wakiwa kidato cha pili mwaka 2008 walikuwa wakisoma na mwanafunzi huyo, lakini aliacha shule katika mazingira ya kutatanisha ambapo baada ya muda walianza kumuona nyumbani kwa mwalimu na akiwa na mtoto.
Endelea kusoma habari hii...............

Monday, June 7, 2010

Best Blogger Tips
Tanzania yanyukwa 5 - 1 na Brazil


Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, ikicheza mbele ya maelfu ya mashabiki wake, ilichapwa magoli 5-1 katika mechi ya kujipima nguvu iliyofanyika Jumatatu jioni katika uwanja wa Taifa jijini Dar Es Salaam.

Mshambuliaji Robinho ndiyo aliwapatia Brazil goli la kwanza, kabla ya kuongeza la pili kwenye mechi ambayo si makosa kusema Taifa Stars walicheza vizuri ingawa tatizo la kawaida limekuwa likijirudia - kukosekana kwa maarifa ya kufunga.

Shambulio la Kaka na mengine mawili kutoka kwa mchezaji wa akiba, Ramires yalikamilisha magoli kwa The Selecao, lakini Stars walionekana kuwachokoza Brazil ambapo katika dakika ya sita Mrisho Ngassa alikosa goli la wazi.

Taifa Stars walipata goli la kufutia machozi kupitia Jabir Aziz, mchezaji wa akiba aliyemalizia kwa kichwa mpira wa kona.

Kocha wa Brazil, Dunga alisisitiza kuwa mechi hiyo haikuwa ya ushindani, bali ilitumika kuandaa kikosi chake kwa Kombe la Dunia.

Mchezaji muhimu aliyekosekana ni mlinda mlango namba moja Julio Cesar aliyejeruhiwa katika mechi ya majaribio dhidi ya Zimbabwe juma lililotangulia, badala yake mlangoni alicheza Heurelho Gomes.
Source: BBC

Sunday, June 6, 2010

Best Blogger Tips
Celtics washinda dhidi ya Lakers


 Ray Allen na Rajon Rondo, wamechangia kwa kiasi kikubwa ushindi wa Celtics dhidi ya Lakers, wameweza kulipiza kisasi kwa kuifunga Lakers kwa points 103-94.

Alikuwa ni Ray Allen aliyeongoza kwa points kwa upande wa Celtics, ametoka na points 32 katika mchezo huo.

Rajon Rondo, aliweza kuwaongoza wenzake kwa ustadi mkubwa na kutoa pasi za uhakika katika kusaidia ushindi huo wa Celtics, alipata points 19, rebounds 12 na 10 assists.
Mchezo wa tatu utakuwa siku ya jumanne ya tarehe 8.

Saturday, June 5, 2010

Best Blogger Tips
Marekani yazuia mali za mfanyabiashara Msumbiji


Wizara ya fedha ya Marekani imezuia mali za mtu anayeshukiwa kuwa mfanya biashara za madawa ya kulevya kutoka Msumbiji baada ya kutajwa kuwa msafirishaji mkuu wa madawa ya kulevya na rais wa Marekani Barack Obama.

Wizara ya fedha ya Marekani imezuia mali za mtu anyeshukiwa kuwa mfanya biashara za madawa ya kulevya kutoka Msumbiji baada ya kutajwa kuwa msafirishaji mkuu wa madawa ya kulevya na rais wa Marekani Barack Obama.

Katika taarifa Jumanne Afisa wa juu wa wizara ya fedha Marekani amesema Mohamed Bashir Suleiman ni muuzaji mkuu wa madawa ya kulevya na kwamba mtandao wake ulichangia kwenye biashara inayokua ya madawa ya kulevya na wizi wa fedha katika eneo kubwa la Afrika.

Biashara tatu za Suleiman zilitajwa kuwa sehemu ya mtandao wake wa usafirishaji Hii ina maana kwamba mali zake zote zilzopo kwenye ardhi ya Marekani hivi sasa zimezuiwa na raia wa Marekani hawaruhusiwi kufanya biashara na makampuni yake matatu.
Source: VOA
Best Blogger Tips
Sumu yauwa watoto mia moja Nigeria


Maafisa wa afya wamesema zaidi ya watoto mia moja wamefariki dunia kutokana na sumu ya madini ya risasi nchini Nigeria katika majuma ya hivi karibuni.

Idadi ya vifo imekuwa ikiongezeka tangu mwezi March, baada ya wakaazi kuanza kuchimba dhahabu kinyume cha sheria katika maeneo yenye madini mengi ya risasi au lead.

Wengi wa waathiriwa ni kutoka maeneo ya vijijini katika jimbo la Zamfara, kaskazini mwa nchi.

Jumla ya kesi 163 kati ya kesi 355 zimesababisha vifo, kulingana na afisa wa afya kutoka Nigeria.

Dr Henry Akpan, afisa katika wizara ya afya, alisema " waathiriwa walikuwa wakichimba dhahabu, lakini maeneo hayo yana kiwango kikubwa cha sumu ya madini ya risasi".

Maafisa wa afya wameweka kambi mbili katika eneo hilo kuwatibu watu wanaosumbuliwa na dalili za sumu hiyo ya madini ya risasi.

Mwandishi wa BBC mjini Kaduna amesema vifo hivyo viligunduliwa wakati wa chanjo ya kila mwaka inayofanyika nchini, baada ya maafisa kutambua kuwa hakuna watoto katika maeneo ya vijijini ya jimbo hilo la kaskazini mwa nchi.

Wanavijiji walisema kuwa watoto walikufa kwa ugonjwa wa malaria, lakini baada ya kundi la madaktari kutoka shirika la kimataifa la Medecins Sans Frontiers kufanya vipimo vya damu wakagundua kuwepo kwa kiwango kikubwa cha sumu hiyo.

Jimbo la Zamfara hivi karibuni liliipatia kandarasi kampuni kutoka Uchina kuchimba dhahabu katika eneo hilo.

Lakini wanavijiji nao walijaribu kujinufaisha kwa kuchimba dhahabu bila ya idhini, jambo ambalo ni kosa nchini Nigeria.

Mwandishi wa BBC anasema huenda wakaazi hao waligonjeka baada ya sumu iliyotokana na mfumo wa kusafisha dhahabu hiyo kuchanganyika na maji.
Source: BBC

Friday, June 4, 2010

Best Blogger Tips
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mwakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Dr. Sipho Moyo Ikulu Dar es Salaam alipokwenda kumuaga baada ya kumaliza muda wa kufanya kazi nchini. (Picha na John Lukuwi).

Best Blogger Tips
Wake na Marafiki wa Kike wa Wachezaji Maarufu wa NBA

NBA Finals, zimeanza jana huko Los Angeles (hilo ni jambo ambalo wapenzi wa Basketball wanalifahamu). Hebu tujaribu kuangalia maisha ya wachezaji ndani na nje ya court.

Ingia hapa na ujaribu kuangalia Wake na Marafiki wa kike wa wachezaji maarufu wa Basketball wakiwa kwenye mitindo mikali ya mavazi katika matukio mbalimbali.
Best Blogger Tips
Joran Van der Sloot Akamatwa


Joran Van der Sloot, ambaye alikuwa mtuhumiwa mkuu wa kupotea kwa Natalee Holloway katika nchi ya Aruba mwaka 2005, amekamatwa nchini Chile kwa tuhuma ya mauaji yaliyotokea Lima, Peru.

Joran Van der Sloot, anatuhumiwa kumuua msichana mwenye umri wa miaka 21, Stephany Flores, ambaye mwili wake uliokuwa umejaa damu ulikutwa hotelini ndani ya chumba ambacho kilihusishwa na Van der Sloot.

Van der Sloot, amekanusha tuhuma hizo, ingawa amekili kwamba alikutana na Flores kwenye Casino ya Lima, msemaji wa polisi amethibitisha.

Bado ni mtuhumiwa mkuu wa kupotea kwa Natalee Hollway, mwanafunzi kutoka Mountain Brook, Alabama, aliyepotea nchini Aruba, akiwa katika mapumziko ya kusherehekea kumaliza shule.

Van der sloot, hakuwahi kushitakiwa kwa kupotea kwa Natalee Hollway, kwa sababu kulikuwa hakuna ushahidi wa kutosha wa kumtia hatiani.

Thursday, June 3, 2010

Best Blogger Tips
Lakers waifunga Celtics , 102-89, kwenye mchezo wa kwanza wa Fainali za NBA


Lakers wameanza vizuri mchezo wao wa kwanza kwa kuifunga Celtics, 102-89, katika mchezo uliofanyika Staples Center, Los Angeles.

Wakicheza kwa kujiamini, Lakers wameonyesha ni jinsi gani ambavyo hawataki kupoteza ubingwa wao waliouchukua mwaka jana.

 Alikuwa ni Kobe Bryant ambaye ndiye aliyewasumbua sana Celtics akitoka na points 30 na 7 rebounds, Paul Gasol (BigMan), alifanya kazi ya ziada akiwa na 14 rebounds, na points 23, huku Mchezaji aliyetoka Houston Rockets, Ron Artest akitoka na points 15 katika ushindi huo dhidi ya Boston Celtics.

Mchezo wa pili utafanyika tena Staples Center, Los Angeles, siku ya jumapili.
Best Blogger Tips
Mandela kuhudhuria Kombe la Dunia

Via BBC

Waziri wa michezo wa Afrika Kusini amesema, aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Nelson Mandela atahudhuria ufunguzi wa sherehe za Kombe la Dunia.

Makhenkesi Stofile amesema Mandela mwenye sifa ya kupinga ubaguzi wa rangi aliomba tiketi kwa ajili ya siku ya ufunguzi na kufunga mashindano hayo.

Awali Mandela alisema alikuwa mdhaifu sana kuhudhuria shindano hilo linaloanza wiki ijayo.

Bw Mandela atakayefikisha umri wa miaka 92 mwezi ujao, alifanya kampeni ya kutaka Kombe la Dunia kufanyika Afrika Kusini.

Bw Stofile amesema, "Mandela ametaka kuhudhuria Kombe la Dunia."

Shirika lake la hisani, Mandela Foundation, halijathibitisha kuhudhuria kwake, wakieleza kuwa ni kutokana na sababu za kiusalama.

Takriban watu 350,000 wanatarajiwa kutembelea Afrika Kusini kwa ajili ya Kombe la Dunia, ambapo inafanyika barani Afrika kwa mara ya kwanza.

Tuesday, June 1, 2010

Best Blogger Tips
R.I.P Gary Coleman

Best Blogger Tips
R.I.P Mayaula Mayoni

Best Blogger Tips
Al and Tipper Gore separate after 40 years


Couple calls it 'a mutual and mutually supportive decision'

Former Vice President Al Gore and his wife, Tipper, are separating after 40 years of marriage. NBC News confirmed the split Tuesday.

According to an e-mail circulated among the couple's friends and obtained by The Associated Press on Tuesday, the Gores said it was "a mutual and mutually supportive decision that we have made together following a process of long and careful consideration."


Gore spokeswoman Kalee Kreider confirmed the statement came from the Gores, but declined to comment further.

Al Gore lost the 2000 presidential election to Republican George W. Bush. He has since campaigned worldwide to draw attention to climate change, which in 2007 led to a Nobel Peace Prize and an Oscar for the documentary "An Inconvenient Truth."
Access the full story...............
Best Blogger Tips
Namibia yashtakiwa kwa kuhasi


Wanawake watatu Namibia wanaishtaki serikali kwa madai ya kuhasiwa bila idhini yao baada ya kupimwa na kuonekana na virusi vya ukimwi.

Wanawake hao wanasema madaktari na wauguzi walitakiwa kuwaelea uzuri kitu gani kilikuwa kikiendelea.

Shirika la utetezi linalowawakilisha, the Legal Assistance Centre LAC, limesema limekusanya ushahidi kutoka kesi 15 za madai ya kuhusika na kuhasiwa baada ya kuonekana na virusi vya HIV katika hospitali tangu mwaka 2008.

Maandamano ya kuwaunga mkono wanawake hao inaendelea huko Windhoek huku kesi ikianza.

Mwandishi wa BBC Frauke Jensen aliyopo kwenye mji mkuu huo, amesema kuna takriban waandamanaji 300.

Wengi wao ni wanawake, wakiwa na kauli mbiu yao " Mwili wangu, fuko langu la uzazi, haki yangu," na wakishika mabango yakisema: " Kwanini umenihasi?"

Pia wana mpango wa kufanya maandamano mengine siku ya Jumatano katika hospitali mbili ambapo inadaiwa shughuli hizo za kuhasi zilipofanyika.
Endelea kusoma habari hii...........

Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits