Thursday, June 30, 2011

Urusi: Wafaransa wamekiuka maadili Libya

Best Blogger Tips
Via BBC

Waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov amelaani hatua ya Ufaransa kuwapa silaha waasi wanaopinga utawala wa kanali Muammar Gaddafi.

Bw Lavrov anasema hatua hiyo ikiwa imedhibitshwa ni kosa kubwa kwani imekiuka azimio 1970 la umoja wa mataifa ambalo linazuia silaha kuingizwa nchini humo na pande zote husika kwenye mzozo huo.

Wanajeshi wa Ufaransa walikiri kuwaangushia silaha wapiganaji wa kabila la Berber wanaoishi kwenye maeneo ya milima kusini mwa mji mkuu wa Tripoli.

Umoja wa Afrika pia umelaani uaamuzi wa Ufaransa wa kuimarisha nguvu za kijeshi za waasi hao.

Mwenyekiti wa tume ya Umoja huo Jean Ping amesema kitendo hicho kinaweka eneo zima hatarini.

Waziri wa mambo ya nje wa urusi amepanga kukutana na mwenzake kutoka Ufaransa Alain Juppe mjini Moscow kudhibitisha suala hilo tete.

Serikali ya urusi ilisusia kupigia kura mswada uliowasilishwa kwenye baraza la usalama la umoja wa mataifa kuruhusu harakati za kijeshi nchini Libya.

Mzozo unaoendelea mjini Libya ndio umepewa kipa umbele katika mkutano wa viongozi wa Afrika unaoendelea nchini Equatorial Guinea.

Bw Ping amesema kuna uwezekano mkubwa vita vya wenyewe kwa wenyewe vikazuka nchini humo sawa na hali iliyoko nchini Somalia.

Mwenyekiti wa tume hiyo ya Umoja wa Afrika amefahamisha BBC kuwa mpango wa amani uliyobuniwa mnamo mwezi March bado unazingatiwa.

Mpango huo unataka pande zote zisitishe mapigano ili mazungumzo ya amani yaweze kuanza.
Habari kwamba Ufaransa imedondosha silaha nchini Libya zilijitokeza kupitia gazeti la Ufaransa, Le Figaro la jumatano.

Gazeti hilo lilisema kuwa Ufaransa, nchi inayoongoza operesheni ya NATO nchini Libya haikufahamisha nchi wanachama wenzake kuhusu operesheni hio.

Uwamuzi huo ulifikiwa baada ya mkutano uliofanyika mwezi April kati ya Rais Nicolas Sarkozy na Mkuu wa vikosi vya waasi wa Libya Gen Abdelfatah Younis.

Slaa afufua upya ufisadi

Best Blogger Tips
Via Raia Mwema

WAKATI wafadhili wakikabidhiwa ripoti inayoonyesha bado Tanzania kuna ufisadi, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, ameibuka na kusema hatorudi nyuma katika mapambano dhidi ya rushwa kutokana na serikali kuwaogopa wala rushwa na mafisadi wakubwa.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na Raia Mwema, jana, Jumanne, Dk. Slaa amesema wakati wote ambao yeye na wenzake katika Upinzani wakipigania hatua kuchukuliwa dhidi ya mafisadi na wala rushwa wakubwa, serikali imekuwa na kigugumizi katika kuchukua hatua; huku ikitumia mbinu za kuwafunga midomo.

Akitoa mfano wa kesi mbalimbali zikiwamo za wizi katika akaunti ya madeni ya nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (EPA) kupitia kampuni ya Kagoda Agricultural Limited na kashfa ya rushwa katika ununuzi wa rada ya kijeshi, Dk. Slaa amesema serikali inawalinda wahusika wakuu.

 “Kampuni kama Kagoda wahusika wanajulikana lakini hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi ya wahusika. Hii si dalili nzuri maana inaashiria kwamba wakubwa wanahusika ama wanawaogopa wahusika. Hatudanganyiki na hatunyamazishwi, tutaendelea kusema na kutaka hatua zichukuliwe,” anasema na kuendelea;

“Kashfa ya rada ni aibu kusikia serikali inadai fedha za rada wakati ilikuwa na kigugumizi wakati Uingereza wakichunguza wahusika wa rada na walishindwa kutoa ushirikiano kwa wachunguzi, lakini sasa eti wanasikia kuna fedha ndio wanazitaka. Kwa nini walikataa kushughulikia wahusika kwa sheria zetu za Tanzania na kuachia Waingereza kila kitu?” alihoji Dk. Slaa.
Endelea kusoma habari hii....................

Aibiwa gari baada ya kuleweshwa

Best Blogger Tips
Via habariLeo

DEREVA teksi Minaji Omary (39), ameibiwa gari baada ya abiria aliyempakia
kumnywesha soda inayodhaniwa kuwa na dawa za kulevya.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Adolfina Chialo alisema, tukio hilo limetokea jana saa 6 usiku kwenye baa ya Uhuru, mjini Morogoro.

Gari iliyoibwa ni yenye namba za usajili T321 BCU aina ya Toyota Corola ambayo dereva wake, baada ya kunywa soda hiyo alipoteza fahamu.

Kamanda Chialo alisema, alfajiri dereva huyo alipoamka hakuiona gari wala
abiria huyo na ndipo alipofika katika Kituo Kikuu cha Polisi na kutoa taarifa hizo. Polisi wanaendelea na uchunguzi.

Katika hatua nyingine, Kamanda Chialo alisema, mkazi wa Kihonda, Amina Maulid amefariki dunia baada ya kunywa vidonge ambavyo havifahamiki. Chanzo cha kujiua hakijajulikana.

Mtoto wa mwanamke huyo ambaye polisi haikutaja jina lake, ndiye aliyetoa taarifa Polisi kuwa mama yake alifariki dunia Juni 28 mwaka huu saa 5:30 usiku eneo la Kihonda, mjini Morogoro.

Alisema, baada ya polisi kufika nyumbani kwao, walikuta dawa za aina mbalimbali kwenye meza ndani ya chumba alichokuwa amelala mwanamke huyo.

Polisi inaendelea na uchunguzi wakati mwili ukiwa umehifadhiwa katika hospitali ya mkoa.

Posho kumfukuza Shibuda Chadema

Best Blogger Tips
Via Mwananchi

KITENDO cha Mbunge wa Maswa Mashariki, John Shibuda kupingana na sera ya chama chake kuhusu suala la posho za vikao (sitting allowance), kimeichefua Chadema ambayo imemuita msaliti ikisema, "adhabu yake ni kufukuzwa.

"Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe aliliambia Mwananchi mjini Dodoma jana kuwa, alikerwa na kauli iliyotolewa na Shibuda ya kwenda kinyume na msimamo kambi hiyo kupinga posho za vikao kwa wabunge na wafanyakazi wengine wa umma.

Mbowe alisema kwamba kwa kauli yake ya juzi ya kuunga mkono posho ilidhihirisha kwamba mbunge huyo ni msaliti wa kambi hiyo, hivyo sheria zitafuata mkondo wake.

"Kutokana na tukio la jana (juzi) bungeni, Shibuda kutusaliti katika suala la posho za vikao, taratibu za kisheria zitafuata mkondo wake kwani utovu wa nidhamu haukubaliki katika kambi yetu, hata katika chama chetu,"alisema Mbowe na kuongeza:

"Suala la posho si la mtu binafsi, lipo kwenye Ilani ya Uchaguzi wa 2010 ya chama chetu na kama kuna kiongozi hafahamu hili basi hakustahili kugombea ubunge kwa sababu naamini Ilani ya Uchaguzi, Shibuda anayo."

"Posho zilijadiliwa na kupitishwa katika vikao maalumu vya chama, kwa hiyo kama Katiba yetu ya chama inavyotuongoza, Shibuda alitakiwa kulipinga katika vikao hivyo sio kutoka nje ya kikao na kuanza kupingana na maamuzi yake,"alisema Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema.


Akinukuu kifungu katika Katiba ya chama chake kinachoeleza maadili ya viongozi, Mbowe alisema, "Kiongozi anatakiwa kutii na kutimiza maagizo anayopewa na viongozi wa ngazi ya juu au vikao halali na kama hakubaliani na maagizo hayo aeleze hivyo kwa kupitia taratibu na ngazi zilizowekwa kwenye kanuni."

Kauli ya Zitto
Kwa upande wake, Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe, aliliambia gazeti hili jana kuwa mbunge kupingana na sera ya chama chake, ni kutokiamini chama hicho.

"Maana yake hakiamini chama, hivyo hafai kuendelea kuwa mwanachama na mbunge wa chama hicho,"alisema Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema.

Aliendelea, "Hapa kuna mambo mawili; masuala ya kisera na masuala ya utaratibu. Mbunge anayepingana na taratibu adhabu yake ni kumwita na kumpa onyo, lakini mbunge anayepingana na sera, huyo hakiamini chama na dhabu yake ni kufukuzwa."

Kwa mujibu wa Zitto, suala la kupinga posho kwa Chadema ni sera kwa kuwa limo kwenye Ilani yake ya Uchaguzi ya mwaka 2010.

"Hili (suala la posho), lipo kisera. Kwenye Ilani yetu ya uchaguzi tulisema, tutapunguza mishahara ya wabunge na posho zao. Sasa kama mbunge anachaguliwa kwa sera hiyo halafu anaipinga haradhani, huyo hakiamini chama na chama hakipaswi kumwamini."

Aliendelea,"Sasa, adhabu ya juu kabisa ya mbunge asiyekiamini chama, ni kufukuzwa. Huu ni usaliti. Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni na mwenyekiti wa chama ameshalitolea tamko suala hilo halafu mbunge anakuja kumpinga hadharani maana yake nini,?" alihoji.

Tundu Lissu je?
Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake jana, Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu alisema kitendo cha Shibuda kupingana na sera ya chama chake, "ni uasi usiovumilika".

"Sasa nikiwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni nadhani ninahitaji kukaa naye. Nitamwita anieleze kulikoni. Aseme kulikoni ameamua kukiasi chama na upinzani kwa ujumla?"

Aliendelea, "Lakini kwa bahati mbaya sana, adhabu kubwa inayoweza kutolewa na kambi ya upinzani ni kumtenga na kambi. Lakini kwa mtu kama Shibuda ambaye tayari anaijua adhabu hiyo na kuitafuta kwa makusudi, inaonekana haitamtosha."

"Kwa sababu hiyo basi, kambi ya upinzani itaenda mbali zaidi baada ya kumtenga. Tutakiandikia chama barua kukijulisha usaliti huo wa mbunge wake halafu chenyewe kina taratibu zake za kinidhamu."
Endelea kusoma habari hii...........................

Wednesday, June 29, 2011

Mwanamke wa kwanza kuongoza IMF

Best Blogger Tips
Via BBC

Waziri wa Fedha wa Ufaransa Christine Lagarde ameteuliwa kuwa mkurugenzi mkuu wa shirika la fedha duniani IMF.

Kufuatia uteuzi huo Ufaransa itakuwa imeshikilia kiti hicho kwa miaka 26 kati ya miaka 33 iliyopita.

Christine Lagarde mwenye umri wa miaka 55, alikuwa mwanamke wa kwanza kuteuliwa waziri wa fedha katika muugano wa nchi saba zilizostawi maarufu kama G-7.

Lagade anatarajiwa kujiuzulu kutoka serikali ya Ufaransa ili kuandikisha historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwahi kuongoza shirika la fedha duniani IMF.

Uteuzi wake umefuatia kujiuzulu wa mfaransa mwenzake Dominique Strauss Kahn, baada ya kukabiliwa na kashfa ya ubakaji.

Sio wengi walioshangazwa na uteuzi wa wakili huyo wa zamani ambaye ana sifa nzuri kote duniani.
Amekuwa msuluhishi wa matatizo mengi ya kiuchumi yanayokumba mataifa kadhaa barani ulaya katika miaka ya hivi karibuni.

Kabla ya kuteuliwa kwake alikuwa ameungwa mkono na China na India na hivyo kuteuliwa kwake kama mkurugenzi mkuu wa shirika hilo la fedha duniani ilikuwa jambo lililotarajiwa.

Kuna maelewano ambayo hayajanakiliwa kuwa raia wa mataifa ya bara ulaya pekee ndio wanaopaswa kuteuliwa kuhudumu kama mkurugenzi mkuu wa IMF huku raia wa marekani wakipewa nafasi za kuongoza benki kuu ya dunia.

Mataifa yaliostawi yanataka kupewa nafasi kuu katika siasa za dunia, lakini huu ni wakati mgumu kwa mataifa ya ulaya huku mzozo wa kiuchumi wa Ugiriki ukitishia kuathiri mataifa mengine katika kanda hiyo.

Muungano wa ulaya na IMF zimeishurutisha serikali ya Ugiriki kupunguza matumizi yake ili kuendelea kupata msaada kutoka kwao.

Lagarde amekuwa katika mstari wa mbele kujaribu kutatua matatizo hayo ya nchi wanachama wa EU.

Tuesday, June 28, 2011

Hawara amuua mwenye mume

Best Blogger Tips
Via HabariLeo

MWANAMKE mkazi wa Ronsoti mjini Tarime mkoani Mara, Debora James (30), anatuhumiwa kumuua mwenzake, Teresia Nago, kwa kumchoma kisu katika mauaji yanayohusisha kugombea mwanamume.

Kwa mujibu wa Polisi, Teresia aliuawa jana saa 4.30 asubuhi Bomani mjini Tarime, baada ya kuchomwa visu viwili tumboni na kifuani na mgomvi wake huyo.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rorya/Tarime, Sebastian Zakaria, alisema Debora alikuwa akituhumiwa kuwa na uhusiano na mume wa Teresia, John Nago ambaye ni mtumishi wa Idara ya Ujenzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Kaimu Kamanda alisema, wanawake hao wawili walikuwa na ugomvi wa muda mrefu na vurugu wakigombea mwanamume huyo.

Alisema, jana Teresia na Debora walikwenda kusuluhishwa na mzee wa Kanisa ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja eneo la Bomani.

Lakini wakiwa Bomani, kulitokea vurugu na Debora ambaye alikuwa na kisu alimshambulia Teresia kwa kumchoma kisu kifuani karibu na moyo na tumboni na kusababisha kifo chake papo hapo, baada ya kutokwa damu nyingi naye akajichoma visu sehemu mbalimbali za mwili wake kwa lengo la kujimaliza.

Kamanda Zakaria alisema Debora amelazwa katika hospitali ya wilaya mjini hapa chini ya ulinzi wa Polisi baada ya kujijeruhi.

Monday, June 27, 2011

Best Blogger Tips
Libya yapuuza hati dhidi ya Gaddafi

Via BBC

Waziri wa sheria nchini Libya Mohammed al Qamoodi amesema hati za mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita za kutaka Kanali Muammar Gaddafi akamatwe zimelenga kuficha uhalifu wa Nato.

Akizungumuza mjini Tripoli, Bw Qamoodi amesema operesheni za Nato zinazoendelea nchini humo ni uhalifu wa kivita dhidi ya raia wa Libya lakini ICC imezifungia jicho.

Waziri huyo ameongeza kuwa wanajeshi wa Nato sasa wamepata kisingizio cha kumuua kiongozi wao Kanali Gaddafi.

Hata hivyo ametangaza kuwa Libya imepata fursa ya kufungulia Nato mashtaka ya uhalifu wanaoendeleza nchini Libya.

Mahakama hiyo imemtuhumu Gaddafi kwa uhalifu dhidi ya binadamu na kuamuru mashambulio kwa raia baada ya machafuko dhidi yake kuanza kati kati ya mwezi Februari.

Mahakama hiyo iliyopo the Hague pia imetoa hati ya kukamatwa kwa mtoto wake wa kiume Saif al-Islam na mkuu wa idara ya ujasusi Abdullah al-Sanussi.

Hatua hio imeendelea kuzua hisia tofauti.

Mwenyekiti wa kamati ya bunge ya mashauri ya nchi za kigeni nchini Urusi, Konstatin Kosachev amesema kuwa uamuzi wa jaji hao sasa utavuruga juhudi za kutafuta suluhu ya mzozo huo.

Bw Kosachev amesema nia kuu ya jumuiya ya kimtaifa ni kuwa Kanali Gaddafi ajiuzulu na atoke nchini humo lakini sasa hilo huenda lisifanyike.

Badala yake, Kosachev amesema huenda kiongozi huyo atafanya kila juhudi kushinda vita hivyo na hii sio habari njema kwa Libya.

Lakini kwa upande wao, wapinzani wamekaribisha uamuzi huo.

Msemaji wao Ibrahim Dabbashi amesema sasa jukumu lipo kwa washirika wa Gaddafi kuelewa kuwa wanafanya kazi na mhalifu na wamshauri aondoke madarakani.

Maelfu ya watu wanaaminiwa kufariki dunia kwenye ghasia hizo.

Saturday, June 25, 2011

Best Blogger Tips
Katiba mpya 2014

Via Tanzania Daima

SERIKALI imetangaza rasmi kuwa Katiba mpya itazinduliwa Aprili 26 mwaka 2014, siku ambayo itakuwa ni maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Kauli hiyo ilitolewa jana mjini Dodoma na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipokuwa akifungua Semina Elekezi kwa wakuu wa mikoa na wa wilaya kuhusu mchakato wa Katiba Mpya.

Semina hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya St. Gasper, Pinda alisema mchakato wa uundwaji wa katiba hiyo umeshaanza ambapo wananchi wamepewa fursa ya kutoa maoni yao.

Alisema matarajio ya serikali ni kuwa mpaka ifikapo mwaka 2014 mchakato wa Katiba mpya utakuwa umekamilika na Aprili 26 Katiba mpya itazinduliwa.

“Ni matarajio ya serikali kuwa Katiba mpya itakuwa imekamilika na kuzinduliwa ifikapo Aprili 26, 2014 katika maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,” alisema.

Pinda alisema kama mambo yote yatakwenda kama yalivyopangwa, Muswada wa Sheria kuhusu Mapitio ya Marekebisho ya Katiba utawasilisha bungeni mwishoni mwa Mkutano wa Nne wa Bunge unaoendelea hivi sasa.

Alisema iwapo muswada huo hautawasilishwa katika mkutano wa nne basi utawasilishwa mwanzoni mwa mkutano wa tano unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Waziri Mkuu, aliwataka wakuu wa mikoa na wa wilaya kutoa ushirikiano kwa Tume ya Kuratibu na Kukusanya Maoni itakayoundwa ili kuwezesha mikutano ya hadhara ya kukusanya maoni kufanyika kama ilivyokusudiwa kwa kuhamasisha wananchi kuhudhuria na kutoa maoni yao.“Suala hili ni kubwa na la kitaifa, ni vyema viongozi wasiingize siasa na wajiepushe kuwashawishi wananchi katika kutoa maoni yao, bali wawaache watoe maoni kwa uhuru au pasipo shinikizo lolote,” alisema.

Waziri Mkuu alisisitiza kuwa hatua ya sasa si ya kutunga Katiba Mpya bali ni kuunda Tume ya Kuratibu na Kukusanya Maoni ya Wananchi kuelekea kutungwa kwa Katiba Mpya.

Mchakato huo wa kuelekea uundwaji wa Katiba Mpya, umekwishaanza na katika hatua ya awali, serikali imeandaa rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Marekebisho ya Katiba (The Constitutional Review Act) ya mwaka 2011.

Hata hivyo mchakato huo ulipata upinzani mkali kutoka kwa wadau mbalimbali wakipinga vipengele kadhaa vilivyomo kwenye muswada huo uliopelekwa bungeni kwa hati ya dharura katika Mkutano wa Tatu wa Bunge uliofanyika Aprili mwaka huu.

Miongoni mwa mambo yaliyolalamikiwa na wadau ni kuwa muswada huo uliandikwa kwa lugha ya Kiingereza ambayo ni watu wachache wanaoizungumza na kuielewa.

Wadau walipinga pia vituo vya kutolea maoni kuwa vitatu, ambavyo ni Zanzibar, Dar es Salaam na Zanzibar.

Hata hivyo serikali ililazimika kuuondoa muswada huo katika mkutano wa tatu wa Bunge na kuahidi kuwa utaandikwa kwa lugha ya Kiswahili na kuufanyia marekebisho kulingana na maoni ya wadau.

Wednesday, June 22, 2011

Best Blogger Tips
Pinda aacha kutumia Mercedes Benz

Via HabariLeo

KATIKA kile kinachotafsiriwa kuwa ni kuwatega mawaziri na viongozi wa Serikali wanaotumia magari ya kifahari na yenye gharama kubwa, Waziri Mkuu,Mizengo Pinda ameanza kuachana na matumizi ya magari yenye gharama kubwa.

Hatua hiyo inadaiwa kuwa inalenga kuwafanya mawaziri na viongozi wengine wa juu
wa Serikali, kupima, kutafakari na kuchukua hatua juu ya matumizi ya magari
ya gharama kubwa wanayotumia sasa ambayo yamekuwa yakipigiwa kelele na
baadhi ya wabunge na wananchi.

Uchunguzi wa gazeti hili ambao ulithibitishwa pia jana jioni na Katibu Mkuu wa
Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhan Khijjah, ulibaini kuwa Waziri Mkuu,
ameacha kutumia magari ya kifahari aina ya Mercedes Benz na Toyota
Land Cruiser VX na kuanza kutumia Toyota Land Cruiser GX.

Katika mahojiano maalumu na HABARILEO, Khijjah amethibitisha Pinda kuanza
kutumia aina hiyo ya magari katika misafara yake ambayo alisema ni ya gharama ya
chini ikilinganishwa na Benz na VX ambayo gharama yao ni kubwa sana.

“Ni kweli Mheshimiwa Pinda sasa ameamua kutumia magari haya ya GX, hajatangaza
popote juu ya uamuzi wake huu, lakini nahisi ni kama ujumbe kwa viongozi wengine
wa juu wa Serikali wanaotumia magari ya gharama kubwa ili kuwafanya nao wapime
na kuchukua hatua,” amesema Khijjah.

Katibu Mkuu huyo wa Hazina, alisema ipo mikakati kabambe iliyowekwa na Serikali
ili kudhibiti matumizi holela ya fedha za umma, lakini akasema si kila kitu lazima kisemwe bungeni, kwani mambo mengine yanahitaji utekelezaji wa moja kwa
moja.

“Mfano hatua hii ya magari ya msafara wa Waziri Mkuu kuwa ya gharama ya chini
unaonesha dhamira ya dhati ya kuanza kuokoa fedha za umma kwa matumizi yasiyo na sababu. Kama Waziri Mkuu anatumia gari kama hili kuna haja gani kwa kiongozi wa
chini kuagiza gari la thamani zaidi, haiwezekani,” alisema Khijjah.

Tuesday, June 21, 2011

Best Blogger Tips
Michelle Obama akutana na Nelson Mandela


Michelle Obama mke wa Rais wa Marekani amekutana na kiongozi wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake katika nchi mbili za kusini mwa Africa.

Wakfu wa Mandela umesema kuwa Bi Michelle Obama, mama yake na binti zake wawili wamemtembelea Bw. Mandela na kuzungumza nae kwa muda mfupi.

Mwandishi wa BBC Karen Allen ambaye yuko Johannesburg anasema kuwa shujah huyo wa ukombozi dhidi ya ubaguzi wa rangi mwenye umri wa miaka 92 anaonekana hafifu na ni nadra yeye kuwapokea wageni.

Ziara hii ya Michelle Obama inanuiwa kupigia debe umuhimu wa vijana uwongozini.

Ziara hii ni ya pili rasmi ambayo Michelle Obama amefanya peke yake tangu mumewe achukuwe hatamu za uwongozi mwaka 2009.Anatarajiwa kukutana na kiongozi wa sasa wa Afrika Kusini Jacob Zuma kabla ya kuelekea Bostwana.

Bi Michelle Obama pia anatarajiwa kuyatembelea makumbusho ya enzi za utawala wa ubaguzi wa rangi na mji wa mabanda wa Soweto ambao ulikuwa katikati ya harakati za kukabiliana na utawala wa wazungu waliochache katika enzi hizo za ubaguzi wa rangi.

Ziara hii pia itajumuisha kutembelea kisiwa cha Robin ambako Bw. Mandela alihudumu 18 kati ya miaka 27 aliyokuwa gerezani.

Bi Obama alikaribishwa Afrika Kusini jumanne jioni baada ya kutua katika uwanja wa ndege wa kijeshi mjini Pretoria ambako binti zake wawili Malia na Sasha walipewa blanketi kubwa zilizokuwa na rangi ya bendera ya Afrika Kusini kujikinga baridi.

Jumatano Michelle atakutana na viongozi vijana wa kike atakapotoa hotuba yake.
Source: BBC

Sunday, June 19, 2011

Best Blogger Tips
Familia ya Kawawa yagombea nyumba

FAMILIA ya aliyekuwa Waziri Mkuu mstaafu hayati Rashidi Kawawa, imesema itapigania kulinda heshima ya mwanasiasa huyo baada ya kuwapo tishio la nyumba yao iliyopo Kilimani mjini Dodoma inauzwa na kupangishwa na mama yao wa kambo.

Mama huyo, Asina Kawawa, anadai kuwa nyumba hiyo ni mali yake.

Kwa mujibu wa familia hiyo, nyumba hiyo inataka kupangishwa na mama huyo anayedai kwamba alirithishwa na Kawawa, licha ya familia kueleza kutotambua hilo, lakini pia ni makumbusho na moja ya maeneo ya kihistoria ya mwanasiasa huyo aliyepigania Uhuru wa Tanganyika.

Ingawa mama huyo anadaiwa kuwa mbioni kupangisha nyumba hiyo iliyopo kiwanja namba 34 eneo la Uzunguni mjini hapa, lakini ipo hatarini kuuzwa na benki ya CRDB baada ya kutumika kama dhamana ya mkopo wa Sh milioni 350 kwa ajili ya kujenga nyumba nyingine pembeni mwa hiyo, mali ya Asina.

Mmoja wa wanafamilia ya Kawawa, Zainab Kawawa ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), aliwaeleza waandishi wa habari akiwa katika nyumba hiyo, kwamba familia inataka kulinda na kutunza heshima ya Mzee Kawawa, kwa sababu hakuwa mtu wa kukopakopa ovyo.
“Tunataka kulinda heshima ya Mzee Kawawa, tumemweleza mama kuwa tuko tayari kulipa deni hilo, lakini hayuko tayari, kwa sababu anaamini tukilipa deni nyumba hii itakuwa yetu, lakini zaidi ni kwamba tayari kuna notisi ya CRDB ya kuuza nyumba kutokana na deni,” alisema Zainab.
Alisema licha ya kuomba mkopo wa Sh milioni 350, ambao ulikuwa ukitolewa kwa awamu, mama huyo alipewa Sh milioni 74 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa nyumba hiyo ya ghorofa moja nyuma ya nyumba ya Mzee Kawawa, lakini sasa deni hilo limefikia Sh milioni 102.

“Kama familia, tulikaa na kuzungumzia deni hili na kukubaliana kuwa linatuhusu, hivyo baadaye lilisimamishwa na sasa limefikia Sh milioni 102, na tayari CRDB wanataka kuja kuuza nyumba hii kwa sababu ya deni,” alisema Zainab ambaye alizungumza na wanahabari baada ya mkutano kati yake na mama yake na mwanasheria Ngonyani kutoka makao makuu ya CCM.

Alisema kwa mujibu wa maelezo ya mama yao, nyumba hiyo aliyokuwa akiishi Mzee Kawawa kwa muda mrefu, aliinunua kwa ubia mwaka 2007 kutoka serikalini na inadaiwa kuwa ilikuwa na kipengele cha kuwa mmojawapo akifariki dunia, basi anayebaki atairithi. 
Endelea kusoma habari hii.....................

Thursday, June 16, 2011

Best Blogger Tips
Zawahir sasa ni mkuu wa Al-Qaeda


Ayman al-Zawahiri, ambaye kwa muda mrefu mno amekuwa msaidizi wa Osama Bin Laden katika kuiongoza Al-Qaeda, na akishikilia nafasi ya pili katika kutoa amri, sasa ataliongoza kundi hilo.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa katika wavuti ya kundi hilo.

Bin Laden aliuawa nchini Pakistan alipopigwa risasi na kikosi maalum kutoka nchini Marekani mwezi Mei.
Kundi la Al-Qaeda limeonya kwamba litaendelea na vita vyake dhidi ya Marekani na Israel chini ya uongozi wa Zawahiri.

Wadadisi wa masuala ya Al-Qaeda wanaelezea kwamba Zawahiri, mwenye umri wa miaka 59, na aliyezaliwa nchini Misri, ni mtu mwerevu sana, lakini hana uwezo wa kuwavutia wafuasi wengi kama alivyofanya Osama.

Baadhi ya wadadisi wanasema yeye ndiye aliyepanga na kuendesha shughuli nyingi zilizohusiana na shambulio la Marekani la 9/11.

Kwa muda wa miaka mingi, msaidizi wa Bin Laden, ambaye atakayefanikiwa kumpata atapokea dola milioni 25 (pauni milioni 15), alitazamiwa kurithi madaraka hayo.

Taarifa iliyotangaza madaraka hayo ilichapishwa katika wavuti ya Al-Qaeda, na kusemekana imetolewa na uongozi wa juu unaotoa amri katika kundi hilo.

"Sheikh Dk Ayman al-Awahiri, Mungu amsaidie, katika kuendelea na uongozi wa kundi", taarifa ilielezea.
Endelea kusoma habari hii..............

Monday, June 13, 2011

Best Blogger Tips
Mavs know Dirk is the primary reason they won an NBA title

Dirk Nowitzki had taken 12 shots, missed 11. He was -- for a shooter, for a scorer, for a leader -- having a nightmarish offensive game.

And since he and his Dallas Mavericks had mentally framed Game 6 as their Game 7, with a championship on the line not across 72 hours but right now, right then, Nowitzki could not have picked a worse time to suffer through a horrible, potentially crushing half of basketball.

OK, OK, Dallas actually was in front at that point, 53-51. So it wasn't a worst-case scenario, just a bad-case scenario. Especially if Nowitzki's just-off-the-mark shots kept missing, if the Miami Heat found their rhythm or (yikes) both.

His pal, Steve Nash, had Tweeted in the afternoon that he sensed a "monster" game from Nowitzki, and he wasn't far off. His many misfires were scaring small children.

"It was weird," Nowitzki said. "I had so many good looks. I can't even explain it. I had some threes, top of the key. I had a wide-open three in the corner. I had some pull-ups. I had some one-leg fadeaways that I normally make.

"The team always told me, 'Stay with it. Stay with it. You're too good of a shooter, too good of a player to keep missing.' "

Ya think?

Nowitzki isn't LeBron James, a player versatile enough or self-conscious enough -- you be the judge -- to turn away from his duties as a scorer. He did what shooters do and kept shooting.

He drained a 17-footer 12 seconds after halftime. He hit a pull-up bank shot on the break minutes later. He splashed a 3-pointer that made it 71-65 with 5:08 left in the third.
 Access the full story..................

Saturday, June 11, 2011

Best Blogger Tips
Marekani yathibitisha kifo cha Fazul

Via BBC

Waziri wa mashauri ya nje wa Marekani Bi Hillary Clinton, amesema kifo cha Fazul Abdullah Mohammed, aliyeshukiwa kuwa mkuu wa Al Qaeda Afrika Mashariki, "ni pigo kubwa" kwa kundi hilo na washirika wake.

Jumamosi serikali ya Marekani imethibitisha kifo cha Fazul Abdullah Mohammed, katika tukio la kufyatuliana risasi na vikosi vya Somalia mjini Mogadishu.

"Kifo cha Harun Fazul ni pigo kubwa kwa Al Qaeda, washirika wake wa siasa kali, na shughuli zake Afrika Mashariki," Clinton aliwaeleza waandishi wa habari akiwa mjini Dar es Salaam, Tanzania.

"Ni mwisho unaostahili kwa gaidi aliyewaletea wengi kifo na huzuni watu wasiokuwa na hatia Nairobi, Dar es Salaam na kwingineko; Watanzania, Wakenya, Wasomali na wafanyakazi wetu wa ubalozi".

Awali afisa mmoja wa cheo cha juu katika serikali ya Marekani alithibitisha kifo cha kiongozi huyo wa Al Qaeda Afrika Mashariki, na kuipongeza serikali ya muda nchini Somalia.

Kiongozi huyo wa Al Qaeda katika kanda ya Afrika ya Mashariki Fazul Abdullah Mohammed, alishukiwa kuhusika na shambulio dhidi ya balozi za Marekani katika Kenya na Tanzania mnamo mwaka 1998.

Fazul Abdullah amekuwa mtu anayetafutwa sana barani Afrika baada ya zaidi ya watu 220 kuuawa na zaidi ya 5000 kujeruhiwa katika mashambuliio ya mwaka 1998.

FBI iliahidi dola milioni 5 kwa kichwa chake.
Endelea kusoma habari hii......................

Friday, June 10, 2011

Best Blogger Tips
Tetemeko latikisa Dar

Via Majira

WAKAZI wa jiji la Dar es Salaam jana walikumbwa na taharuki baada ya kutokea kwa tetemeko la ardhi lililodumu kwa sekunde kadhaa.

Tetemeko hilo lililotokea majira ya saa 5:28 asubuhi ambapo kwa mujibu wa wataalamu wa hali ya hewa lilitokea kilometa 52 kusini mashariki mwa jiji hilo.

Baadhi ya watu waliokuwa kwenye majengo marefu waliamua kuzikimbia ofisi zao kwa lengo la kujiokoa licha ya tetemeko hilo kutoleta uharibifu wa mali.

Vikundi vya wananchi vilionekana kujazana katikati ya mitaa mbalimbali nje ya majengo vikijadili tukio hilo.

Abdul Juma, mfanyabiashara aliyepanga katika jengo la PPF, alisema waliamua kutoka katika ofisi hizo kwa hofu kuwa huenda tetemeko hilo lingetokea tena.

“Ndugu yangu maisha ni matamu, mimi sijui nimeshukaje kutoka ghorofa ya tano, nilijawa na hofu baada ya kusikia tetemeko hilo.

Katika jengo la PPF House, askari polisi walionekana kurandaranda huku na huku kwa lengo la kuhakikisha kuna usalama wa raia na mali zao.

Taarifa za mtandao wa Geolojia zilisema kuwa tukio hilo lilikuwa na nguvu ya 4.8 upana kilometa 10.

“Tetemeko hilo limeonekana katika latitudo kusini mwa mstari wa greenwhich limekuwa kwa 7 na mashariki ni longitudo 39,” ilifafanua.

Taarifa hiyo iliyataja maeneo ambayo tetemeko hilo lilipita kuwa ni Zanzibar, Tanga na Nairobi nchini Kenya.

Tuesday, June 7, 2011

Best Blogger Tips
Rais Saleh wa Yemen 'aliumia' sana

Rais wa Yemen, Ali Abdullah Saleh, alijeruhiwa zaidi katika shambulio la makombora katika boma lake juma lililopita kuliko ilivyodhaniwa, maafisa wa Serikali wameambia vyombo vya Habari vya Marekani.

Maafisa wa Serikali waliambia shirika la Habari la AP kuwa Bwana Saleh alichomeka asilimia 40 ya mwili wake na anavuja damu katika fuvu lake kutokana na shambulio hilo la Ijumaa.

Rais anaendelea kupata matibabu nchini Saudi Arabia baada ya kushambuliwa katika Ikulu yake katika Mji Mkuu wa Yemen, Sanaa.

Afisa wa cheo cha juu Serikalini aliambia BBC kuwa hawatasema lolote kuhusiana na afya ya Rais Saleh.

"Sisi si madaktari. Na kama Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani, Bi Hillary Clinton alivyosema jana, sisi tuko hapa na Sanaa na tunafanya kila juhudi kuhakikisha kuwa tunaleta mabadiliko kwa utaratibu, amani na bila ghasia, kama inavyosema Katiba ya Yemen," afisa huyo alisema.
Endelea kusoma habari hii....................

Sunday, June 5, 2011

Best Blogger Tips
Binti mbaroni kwa 'kubaka kavulana'

Via Majira

MSICHANA mwenye umri wa miaka 16 (jina linahifadhiwa), mkazi wa Kigogo, Luhanga, Dar es Salaam anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za 'kumbaka' mtoto wa
kiume mwenye umri wa miaka mitatu.

Msichana huyo anadaiwa kumbaka mtoto huyo mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo alimuiba nyumbani kwao na kumpeleka kwenye pagale, nyuma ya Shule ya Msingi Kawawa.

Mama mzazi wa mtoto aliyefanyiwa unyama huo, ambaye hakutaka kutajwa jina lake alisema, wakati akifanya usafi ndani ya nyumba yake siku ya tukio saa 4 asubuhi, mtoto wake alikuwa nje akicheza na wenzake.

Alisema alipomaliza ndani alitoka nje kumchukua mwanaye huyo ili ampe kifungua kinywa, lakini hakumwona ndipo, akaanza kumtafuta zaidi ya saa nzima bila mafanikio.

Mama huyo alisema, baada ya kuhangaika kumtafuta mwanaye, akili ilimtuma kuchungulia ndani ya nyumba hiyo inayojengwa na alipofanya hivyo alikuta mwanaye amelaliwa na msichana huyo.

Alisema kuona hivyo alikwenda mbio kuita mama mwingine jirani yake ili ashuhudie kitendo anachofanyiwa mwanaye.

"Nikiwa na jirani yangu tulishuhudia msichana huyo akifanya kitendo hicho kwa mtoto wangu," alisema.

Baada ya kushuhudia yote hayo, walipiga kelele na kumkamata akiwa uchi na kumpeleka Kituo Kidogo cha Polisi Kigogo- Luhanga.

Msichana huyo alishikiliwa kwa muda katika kituo hicho kidogo cha polisi kisha akahamishiwa Kituo cha Urafiki kwa hatua zaidi za kisheria ambapo mtoto aliyebakwa akilipelekwa katika Hospitali ya Amana kupatiwa matibabu.
Best Blogger Tips
UKIMWI uliginduliwa mwaka 1981

Mwaka wa 1981, daktari mmoja wa California Marekani aliona vijana wa kiume watano, walioshiriki katika mapenzi ya jinsia moja, wakiwa na ugonjwa usiokuwa wa kawaida.

Walikuwa na homa ya pneumonia na saratani ya ngozi.

Dakta Gottlieb hakujua kuwa ripoti zake, ndio zitakuwa historia ya kwanza kuandikwa juu ya ugonjwa ambao baadae utakuja kuwa janga kubwa la AIDS, au UKIMWI.

Virusi vya HIV viligundulikana miaka miwili baada ya ugunduzi huo wa Dakta Gottlieb.

Tena damu ikaweza kupimwa kama ina virusi vya HIV, na baadae zikapatikana dawa kadha za kudhibiti ugonjwa huo.

Umoja wa Mataifa unakisia kuwa tangu mwaka wa 1981, UKIMWI umeuwa watu milioni 30, na idadi kama hiyo hivi sasa wanaishi na virusi vya HIV.

Lakini juma lilopita, umoja huo uliripoti kuwa idadi ya watu wanaoambukizwa inapungua katika nchi kadha, lakini mamilioni ya wagonjwa bado hawapati dawa wanazohitaji.

Matabibu wanasema virusi vya HIV sasa wanavifahamu sawasawa, na wagonjwa wanaofululiza kula dawa kwa wakati, wanaweza kuishi karibu maisha ya kawaida.
Source: BBC

Saturday, June 4, 2011

Best Blogger Tips
NY-born twin friars die on same day at age 92

BUFFALO, N.Y. – Identical twins Julian and Adrian Riester were born seconds apart 92 years ago. They died hours apart this week. The Buffalo-born brothers were also brothers in the Roman Catholic Order of Friars Minor. Professed friars for 65 years, they spent much of that time working together at St. Bonaventure University, doing carpentry work, gardening and driving visitors to and from the airport and around town.

"It was fun to see them, just quiet, gentle souls," Yvonne Peace, who worked at the St. Bonaventure Friary for nearly 21 years, said Friday.

They died Wednesday at St. Anthony Hospital in St. Petersburg, Fla., Brother Julian in the morning and Brother Adrian in the evening.

Both died of heart failure, said Father James Toal, guardian of St. Anthony Friary in St. Petersburg, where the inseparable twins lived since moving from western New York in 2008.

"It really is almost a poetic ending to the remarkable story of their lives," St. Bonaventure spokesman Tom Missel said. "Stunning when you hear it, but hardly surprising given that they did almost everything together."

Julian and Adrian Riester were born Jerome and Irving on March 27, 1919, to a couple who already had five daughters. They took the names of saints upon their ordination in the Catholic church.
"Dad was a doctor and he said a prayer for a boy," Adrian once said, according to St. Bonaventure. "The Lord fooled him and sent two."

After attending St. Joseph's Collegiate Institute, the brothers were turned away by the military because of their eyesight, the university said. One had a bad left eye, the other a bad right eye.

Eventually they joined the friars of Holy Name Province in New York City. They received separate assignments before reuniting at the seminary at St. Bonaventure from 1951 to 1956. After serving parishes in Buffalo for 17 years, they returned to St. Bonaventure in 1973 and spent the next 35 years there.

They had separate rooms in the friary but one telephone extension that rang into both, Peace recalled. It was usually the more talkative Adrian who answered, though Julian possessed a quiet authority. They never said who was born first.

"Brother Julian was like the big brother. Brother Adrian would defer to him," Peace said. "They picked up one of our friars at the airport one time and the friar said, `Can I take you to dinner?'
"Brother Adrian looked at Brother Julian and said, `We aren't going to dinner?' `No, we'll go home,'" Peace said. "So that was it. No discussion, no contradicting. `No, we aren't going today.'"

Funeral services are scheduled for Monday at St. Mary Our Lady of Grace Church in St. Petersburg. Afterward, the brothers' bodies will be flown to Buffalo and buried Wednesday at St. Bonaventure Cemetery, across the street from the university.
Source: Associate Press

Friday, June 3, 2011

Best Blogger Tips
Mjane wa Sisulu A Kusini afariki dunia

Afrika Kusini inaomboleza kifo cha mmoja wa watu walioongoza harakati za kupambana na ubaguzi wa rangi, Albertina Sisulu, aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 92.

Bi Sisulu alikuwa mjane wa Walter Sisulu, rafiki na mshauri wa aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela.

Mwanasiasa mashuhuri wa aina yake, alikuwa mpambanaji katika shirikisho la wanawake wa African National Congress (ANC).

Msemaji wa ANC Brian Sokutu alisema Bi Sisulu alikuwa wakati wote wa maisha yake akiwa katika harakati za kuleta demokrasia nchini Afrika Kusini.

Gazeti la Afrika Kusini la South Africa Times limemnukuu akisema, " Komredi Sisulu ametumia muda wake wote kuitumikia ANC na kuikomboa Afrika Kusini. Tunatoa heshima zetu kwa kiongozi huyu na mama wa harakati hizi."
Endelea kusoma habari hii...................

Thursday, June 2, 2011

Best Blogger Tips
Hillary Clinton kutembelea Afrika

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Hillary Clinton, atasafiri wiki ijayo kuelekea nchi tatu barani Afrika, kuzungumzia biashara, maendeleo  na masuala ya usalama wa kieneo.

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani inasema Clinton atatembelea Zambia, Tanzania na Ethiopia, kisha ataelekea Umoja wa falme za  kiarabu, ambapo atalenga mgogoro wa Libya.

Clinton amepangiwa kuhudhuria mkutano wa biashara nchini Zambia, utakaofanyika Ijumaa ya Juni 10 na kukutana na Rais wa Zambia, Rupiah Banda. Akiwa nchini Tanzania, wizara ya mambo ya nchi za nje ya Marekani inasema Clinton, ataelezea mafanikio ya nchi mbili  ikiwa ni pamoja na program kadhaa zilizopo huko.

Clinton anatarajiwa kutembelea Umoja wa Afrika wakati akiwa Ethiopia na kukutana na mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, Jean Ping. Wakati wa safari yake, Clinton pia atakutana na Waziri Mkuu wa Ethiopia,  Meles Zenawi na Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete.
Source: VOANews

Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits