Thursday, February 23, 2012

Wakristu watakiwa kujitakasa

Best Blogger Tips
WAKRISTO nchini wameonywa kuacha mzaha na Mungu kwa kujitokeza kwa wingi katika siku maalumu tu za Jumatano ya Majivu na Ijumaa Kuu ili kubusu msalaba kwani
kufanya hivyo ni kupoteza maana ya kipindi hicho cha toba.

Wametakiwa kujitokeza siku zote katika Misa na kuwa na muda binafsi wa kufanya toba, kufunga na kusaidia wahitaji ili kuleta maana ya kweli ya Kwaresima na Ukristo.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Eusebius Nzigirwa alisema hayojana
alipokuwa akihubiri katika Misa ya Jumatano ya Majivu kwenye Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, Dar es Salaam.

“Kuna msemo wa Kiswahili unasema mtu amekuja bila kitu duniani na ataondoka bila kitu,
mimi nasema si kweli, tumekuja bila kitu lakini tutaondoka na mizigo ya matendo yetu yawe
mema au mabaya, hilo lazima tujue, tusifunge kujiandaa kwa Pasaka bali kifo chema,” alisema Nzigirwa.

Kutokana na ukweli huo, aliwataka waumini kutofanya mzaha katika kipindi pekee cha
Kwaresima cha siku 40 akiwakumbusha wengine kuwa huenda ikawa Kwaresima ya mwisho katika maisha yao.

Kwa upande wake Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Mhashamu Method Kilaini
amewataka Wakristo kote nchini hasa Wakatoliki kujitenga na starehe kwa kujinyima ili kuwasaidia wahitaji.

Akizungumza na gazeti hili jana kwa simu, alisema Kwaresima ni kipindi pekee cha kujiweka karibu na Mungu kwa kuwasaidia yatima, wajane na wasiojiweza huku akiwataka
wanandoa, kuongeza ukaribu na upendo kwa familia.

Jumatano ya Majivu ni mwanzo wa kipindi cha Kwaresima cha siku 40 ambapo Wakristo kote duniani hupakwa majivu usoni na kukumbushwa kuwa binadamu ni mavumbi namavumbiniatarudiiliaishimaisha mema.
Chanzo: HabariLeo

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits