Wednesday, March 21, 2012

Muamba azungumza na Coyle kwa ufupi

Best Blogger Tips
Meneja wa Bolton Owen Coyle amesema alizungumza "kwa ufupi" na Fabrice Muamba kwa mara ya kwanza tangu kiungo huyo alipopoteza fahamu kutokana na matatizo ya moyo.

Mchezaji huyo amelazwa katika hospitali ya London Chest baada ya kuanguka na kupoteza fahamu wakati Bolton walipokuwa wakicheza dhidi ya Tottenham katika robo fainali ya kuwania Kombe la FA siku ya Jumamosi.

"Bado ana safari ndefu kupona kabisa lakini kusema ukweli maendeleo yake yanatia moyo," alisema Coyle.
"Kwa hali tuliyokuwa nayo siku ya Jumamosi usiku, kwa hapa tulipofikia kamwe sikutarajia hali ya kutia moyo kama hii."

Muamba alipata usingizi "mzuri" usiku wa Jumatatu katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum, taarifa ya pamoja ya klabu ya Bolton na hospitali ilieleza siku ya Jumanne.

Waganga wamesema wanaendelea kumuangalia kwa karibu kujua maendeleo yake.

Siku ya Jumatatu ilielezwa bado alikuwa akiumwa sana lakini kwa sasa hali hiyo imetengemaa baada ya mchezaji huyo wa zamani wa kikosi cha vijana cha England chini ya umri wa miaka 21 kuanza "kupumua bila ya msaada wa mashine".
Source: BBC

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits