Saturday, March 19, 2011

Best Blogger Tips
Mataifa yajadili hatua dhidi ya Libya

Mataifa yaliyoahidi kutekeleza azimio la Umoja wa Mataifa, linalokataza ndege kuruka katika anga ya Libya, yanakutana mjini Paris, kujadili hatua ya kuchukua.

Viongozi wa Ufaransa, Ungereza na Marekani, wamejumuika na nchi za Jumuiya ya Kiarabu, pamoja na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon.

Huku ndege za kijeshi zinapelekwa eneo la Mediterranean, Kanali Gaddafi, ameonya Mataifa ya Magharibi, yatajuta, endapo yataingilia kati.

Taarifa yake imesema, azimio la Umoja wa Mataifa, linatoa idhini ya kuingilia kati kijeshi, sio halali.
Mwakilishi wa Ufaransa katika Umoja wa Mataifa, amesema, anatarajia hatua za kijeshi, zitaanza katika saa chache baada ya mkutano huo wa Paris.
Source: BBC

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits