Wednesday, March 30, 2011

Best Blogger Tips
Sadaka ya Babu yafikia mil. 50/-

*Yeye kupata mi. 10/-, kanisa, wasaidizi mi. 20/- kila mmoja
*Kanisa kujenga jengo la huduma la kukaa watu  700 kwa pamoja
*Wanasayansi Kenya wathibitisha dawa yake kutibu maradhi mengi

Via Majira

KANISA la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati limetangaza kiwango cha
fedha ambazo kimekusanywa kutoka kwa wagonjwa wanaokunywa kikombe cha dawa ya Mchungaji Ambilikile Masapila kuwa ni sh milioni 50.

Akitangaza fedha hizo jana, Askofu wa kanisa hilo, Thomas Laizer alisema fedha hizo zimepatikana tangu kuanza kwa tiba hiyo mwishoni mwa mwaka jana, kutokana na mchango wa sh. 500 kwa kila mgonjwa.

Kutokana na mgao wa fedha hizo kama alivyosema Babu ni kuwa yeye anabaki na sh 100 huku sh 200 zikienda kanisani na 200 kwa wasaidizi wake, yeye atapata sh milioni 10. Kanisa sh. milioni 20 na wasaidizi wake sh milioni 20.

Wakati huo huo, Kanisa hilo limekamilisha mipango ya ujenzi wa banda kwa ajili ya tiba ya Mchungaji Ambilikile Masapila ‘Babu’ kijijini Samunge litakalogharimu sh. milioni 100 ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mapendekezo ya mchungaji huyo.

Jengo hilo litakalohudumia watu 700 kwa wakati moja litakua la mviringo na litajengwa karibu kabisa na babu anakotolea tiba hiyo hivi sasa ambapo kutakuwa na viti vya watu zaidi ya 300, eneo la kutolea dawa, kuchemshia dawa hizo na sehemu ya kuhifadhia hiyo dawa.

Askofu Laiser alisema jana kuwa uamuzi huo umekuja wakati ambao idadi kubwa ya watu wanateseka kumfikia mchungaji huo kwa kuwa katika jua kali, na wakati mwingine mvua wakisubiria tiba.
Endelea kusoma habari hii........................



,

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits