Thursday, September 22, 2011

Michael Sata ashinda uchaguzi Zambia

Best Blogger Tips
Mshindi wa uchaguzi wa Zambia Michael Sata
Kiongozi wa chama cha Patriotic Front, Micheal Sata ametangazwa kwa mshindi wa uchaguzi wa urais nchini Zambia

Bw Sata alipata asilimia 43 ya kura zilizopigwa na kumshinda Rais Rupiah Banda wa chama tawala cha MMD ambacho kimekuwa mamlakani kwa muda wa miaka 20.

Tangazo hilo lilitolewa na Jaji Mkuu wa Zambia Ernest Sakala.

Awali watu wawili waliuawa kufuatia ghasia katika maeneo ambayo ni ngome ya upinzani.

Mkuu wa Polisi wa jimbo hilo maafuru kwa uzalishaji Shaba ameliambia shirika la habari la Reuters watu wamejitokeza katika barabara za mji wa Kitwe na Ndola wakivurumisha mawe.

Mwandishi wa BBC anasema ghadhabu hizi zimechochewa na agizo la serikali kupiga marufuku vyombo vya habari kutangaza matokeo bila ya idhini ya tume ya uchaguzi ya nchi hiyo.

Mwandishi wa BBC Mutuna Chanda akiwa Lusaka kilomita 300 kusini mwa Kitwe, anasema huko Kitwe, waandamanaji waliteketeza soko moja usiku na Polisi wameweka vizuwizi katika mji wa Wusaikile.

Rais Banda alimshinda Bw Sata kwa kura 35,000 katika uchaguzi wa mwaka 2008, matokeo yaliozusha ghasia kutoka upande wa upinzani katika ngome zao za mijini.

Tangu uchaguzi wa mwaka 2008, watu wengine milioni moja wamejiandikisha kuwa wapiga kura,wengi wao vijana wasio na ajira.
Chanzo: BBC

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits