Monday, September 12, 2011

Miss Universe 2011 ni Leila Lopes Kutoka Angola

Best Blogger Tips
Miss Universe 2011 Leila Lopes
Miss Angola Leila Lopes amevishwa taji la Miss Universe 2011 katika mchuano uliofanyika siku ya jumanne katika jiji la Sao Paulo nchini Brazil.

Lopez, alikuwa katika la watu watano walioweza kufika katika fainali za mashindano hayo. Wengine walikuwa ni kutoka China, Brazil, Philippines, Ukraine na Panama.

Nchi zilizoingia katika kumi bora ni Australia, Costa Rica, France, Ukraine, Portugal, Panama, Philippines, Angola, China na Brazil.

Lopez ameweza kuwashinda washiriki wengine 88 kutoka nchi mbambali duniani zilizoshiriki mashindano hayo ikiwamo Tanzania.

Mashindano hayo yalikuwa ni ya 60 kufanyika tangu yaanzishwe 1952.




No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits