Thursday, October 14, 2010

Best Blogger Tips
Ndoto za Nyerere zimewekwa kando


WASOMI, wanasiasa na viongozi wa dini wamesema ndoto za Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere zimemezwa na watu wachache wenye uchu wa madaraka na wasiojali wala kuitakia mema Tanzania.

Wakitoa maoni yao jana kwa nyakati kuhusiana na maadhimisho ya miaka 11 tangu Mwalimu Nyerere alipofariki dunia inayofanyika leo, wanazuoni na viongozi hao waliwataka Watanzania mwaka huu kumwenzi muasisi huyo taifa kwa kutowachagua watu wabaya na kuwahimiza wagombea wa nafasi mbalimbali kuheshimu matokeo ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Okotba 31.

Walisema maadili ya uongozi yaliyoachwa na Nyerere yamesahauliwa na viongozo hivyo kuna haja kwa taifa kurejesha maadili hayo ili kuinusuru nchi.
Mwalimu Nyerere alifariki dunia kwa ugonjwa wa saratani ya damu Oktoba 14, 1999 katika Hospitali ya Mtakatifu Thomas nchini Uingereza alikoenda kutibiwa.

''Moja ya mambo ya msingi ambayo tunapaswa kumuenzi Mwalimu Nyerere, ni kuheshimu maamuzi ya wananchi katika kuchagua mgombea wa urais, ubunge na udiwani. Kuchakachua matokeo, itakuwa ni jambo la hatari,'' alisema aliyewahi kuwa Waziri katika Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Arcado Ntagazwa.

Ntagazwa alisema kuheshimu maamuzi ya wananchi ni sehemu ya kumuenzi Mwalimu Nyerere katika kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu.
Endelea kusoma habari hii..............

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits