Thursday, January 26, 2012

Mheshimiwa Galinoma Amefariki Dunia

Best Blogger Tips
 Aliyekua mbuge wa Jimbo la Kalenga,Iringa miaka ya nyuma.mheshimiwa Galinoma amefariki Dunia leo asubuhi mjini Iringa wakati akiwa garini akipelekwa hospitalini kutoka kijijini kwake Kalenga,ambako alikokuwa anaishi.

Mheshimiwa Galinoma ,alikuwa mtumishi wa serikali mstaafu aliyeshika nafasi mbali mbali katika uhai wake zikiwa Katibu mkuu idara ya ulinzi na jeshi la kujenga taifa,mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa mbuga za wanyama poli,mwenyekiti wa bodi ya mashirika ya Umma(SCOPO),Katibu wa tume ya uchunguzi wa viongozi,pia amewahi kuwa mbunge wa jimbo la Kalenga ,Iringa.

Marehemu Mhe. Galinoma alikuwa anaugua kwa muda mrefu pia aliwahi kuenda India kwa matibabu alikua huko wiki 6, na alipata nafuu kwa kiasi fulani lakini baadae alizidiwa tena.

Marehemu ameacha wajukuu na watoto ,miongoni mwa watoto wa wake ni wanamuziki Innocent na Buti Jiwe aka Henry Galinoma. Taaritibu za mazishi zitatolewa si muda mrefu.

Mungu amlaze mahala pema peponi.

Kwa habari zaidi za msiba wasiliana na Joseph Galinoma kwa namba hii 00255716492048 au Denis Galinoma namba hii 00255784769945
Chanzo: Globu ya Jamii

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits