Wednesday, January 4, 2012

Sheria mpya Saudi Arabia

Best Blogger Tips
Mwanamke wa Kisaudi
Sheria mpya inayowapiga marufuku wanaume kuuza nguo za ndani za wanawake kama vile chupi na sidiria inaanza kutekelezwa hii leo nchini Saudi Arabia.

Wanaharakati wa kike katika Ufalme huo wa kiislamu wanatumai kuwa agizo hilo lililotolewa na mfalme Abdulla mwaka wa 2006, utamaliza mfadhaiko ulipo wakati wanawake wanauziwa nguo zao za wasaidizi wanaume madukani.

Ajira kwa wanawake

Hatua hiyo itawapa fursa adimu zaidi ya wanawake 40,000 kuchukua nafasi za kazi zitakazoaachwa wazi.
Maafisa wa kidini wasiopendelea mabadiliko wamepinga vikali hatua hiyo ya wanawake kufanya kazi nje ya nyumba zao.

Serikali imepanga kupeleka waangalizi katika vituo vya biashara kote nchini kuhakikisha kwamba wasaidizi wanawake madukani hawabughudhiwi na maafisa wa polisi wa kidini.
Chanzo: BBC

 

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits