Monday, January 9, 2012

Beyonce na Jay-Z wapata mtoto

Best Blogger Tips
 Wanamuziki wenye kipaji cha hali ya juu ambao walifunga ndoa hivi karibuni, Beyonce na mumewe Jay-Z, wamepata mtoto wa kike ambaye wamempa jina la Blue Ivy.

Beyonce mwenye umri wa miaka 30, alijifungua salama mtoto wake kwa njia ya upasuaji siku ya jumamosi. Beyonce alijifungua katika hospitali ya kifahari ya Lenox Hill, jijini Manhattan, huku mume wake Jay-Z, ambaye jina lake halisi ni Shawn Carter, akiwa pembeni yake.

Beyonce alikwenda hospitali siku ya ijumaa na akajiandikisha kwa jina la "Ingrid Jackson," gharama ambayo imelipwa kwenye hospitali hiyo ni $1.3 millioni.

Salamu za pongezi zilianza kumiminika kwenye mtandao wa kijamii wa twitter, zikiwapongeza wawili hao kwa kupata mtoto.

Baadhi ya watu ambao walituma salamu hizo kwa njia ya twitter ni pamoja na Rihanna na pia mdogo wake Beyonce anayeitwa Solange Knowles.


No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits