Thursday, January 5, 2012

Lebron James amvisha pete mama watoto

Best Blogger Tips
Mchezaji mahili wa mpira wa kikapu wa timu ya Miami Heat,Lebron James, amesheherekea sikukuu ya mwaka mpya na ile ya kuzaliwa kwake kwa kumvalisha pete mchumba wake.

James alimvisha pete mchumba wake wa muda mrefu Savannah Brinson, mama wa watoto zake wawili katika hoteli ya South Beach iliyopo jijini Miami

Wawili hao wamekuwa pamoja kwa muda mrefu tangu  James akiwa shuleni  huko Akron, katika jimbo la Ohio.

Wiki iliyopita aliyekuwa mchezaji hodari wa mpira wa kikapu na mmiliki wa timu ya Challote, Michael Jordan, alimvisha pete mchumba wake Yvette Prieto.

Tunapenda kutoa pongezi kwa ndugu hawa kwa jambo hili muhimu walilolifanya.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits