Thursday, April 22, 2010

Best Blogger Tips
Liyumba ainanga serikali

Amtupia mzigo marehemu Balali

ALIYEKUWA Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu, Amatus Liyumba (62), ambaye sasa anakabiliwa na shtaka moja la matumuzi mabaya ya ofisi ya umma, amedai serikali haijui itendalo dhidi ya kesi iliyomfungulia.

Liyumba ameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, izingatie ukweli wakati wa kutoa hukumu dhidi yake Mei 24 badala ya kuwasikiliza watu wasiojua watendalo.

Maneno hayo mawili ‘hawajui watendalo’ yanafanana na yale aliyotumia Yesu Kristo, anayeaminika kuwa ni Mwokozi wa waumini wa Kikristo wakati akieleza kitendo cha Wayahudi waliokuwa wakimsulubisha (Luka 23:34).

Mshtakiwa huyo jana alipanda kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kutoa utetezi wake mbele ya Kiongozi wa Jopo la Mahakimu Wakazi, Edson Mkasimongwa, aliyekuwa akisaidiwa na Lameck Mlacha na Benedict Mwingwa.

Kesi hiyo ambayo imevuta hisia za watu wengi ndani na nje ya jiji la Dar es Salaam ilifikishwa mahakamani hapo Januari 26 mwaka jana ambapo Liyumba alikuwa akikabiliwa na makosa mawili ambayo ni matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia hasara serikali ya sh bilioni 221.

Hata hivyo Aprili 9 mwaka huu, mahakama hiyo ilimfutia shtaka la kuisababishia hasara serikali baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha hasara kwa namba kama ilivyokuwa ikitakiwa.

Liyumba, aliongozwa kutoa ushahidi wake na wakili mahiri wa kujitegemea Majura Magafu aliyekuwa akisaidiwa na Jaji Mstaafu Hillary Mkate, Onesmo Kyauke na Hudson Ndusyepo huku upande wa mashitaka ulikuwa ukiongozwa na mawakili waandamizi Juma Mzarau, Ben Lincoln na Tabu Mzee.
Endelea kusoma habari hii............

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits