Wednesday, April 21, 2010

Best Blogger Tips
'Nusu ya mawaziri wa Kikwete hawachaguliki'

Utafiti wawataja, waponzwa na kaulimbiu ya 'maisha bora'

Via Tanzania Daima

UTAFITI umeonyesha kuwa zaidi ya nusu ya mawaziri waliotajwa kuwa makamanda katika Serikali ya Awamu ya Nne wanaweza kupoteza nafasi zao za ubunge kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010.

Kwa mujibu wa asasi isiyo ya kiserikali, Nyota, iliyofanya utafiti huo katika kipindi cha miezi sita iliyopita, hali ni tete katika majimbo ya mawaziri hao.

Mawaziri hao wako hatarini kukosa ubunge kutokana na wananchi wengi wa majimbo hayo kukosa imani nao, baada ya kaulimbinu ya ‘maisha bora kwa kila Mtanzania’ kushindwa kuonekana kwa vitendo majimboni mwao.

Taarifa ya awali iliyotolewa na Mratibu wa asasi hiyo, Vincent Kornald Mkisi, ilisema kuwa mazingira ya mawaziri na manaibu hao kupoteza nafasi zao yalianza kuonekana tangu Januari mwaka huu.

Mkisi alitaja majina ya mawaziri walio katika hali mbaya kurudi bungeni kuwa ni pamoja na Profesa Peter Msolla ambaye anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Venance Mwamoto ‘Motto’.

Duru za kisiasa zinasema kuwa Profesa Msolla alitarajia kudra za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuligawa Jimbo la Kilolo na kuwa mawili, hivyo alijipanga kuwania ubunge katika eneo la Ilula ambako anakubalika zaidi kuliko maeneo mengine.
Endelea kusoma habari hii...........

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits