Thursday, May 20, 2010

Best Blogger Tips
Campbell huenda akaitwa mahakamani


Via BBC

Waendesha mashtaka wa uhalifu wa kivita huko Hague wamesema mlimbwende Naomi Campbell anatakiwa kufika mahakamani kutoa ushahidi katika kesi ya Rais wa zamani wa Libya Charles Taylor.

Wanasema Bi Campbell "aligaiwa almasi ambayo haikuchongwa" na Bw Taylor mwaka 1997 katika nyumba ya Nelson Mandela Afrika Kusini.

Bw Taylor anatuhumiwa kutumia "almasi zinazotoka kwenye nchi zenye migogoro ya kivita" iliyochochea uasi Sierra Leone iliyosababisha vifo vya maelfu ya watu.

Awali Bi Campbell alikataa kutoa ushahidi kwa waendesha mashtaka.

Taarifa iliyokusanywa na upande wa mashtaka kutoka mahakama maalum ya Sierra Leone imesema, " Taarifa ya Bi Campbell ni muhimu kwa vile kuna ushahidi kuwa Bi Campbell alipewa almasi ambazo hazikuchongwa na mtuhumiwa (Taylor) Septemba 1997."
Endelea kusoma habari hii....................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits