Monday, May 24, 2010

Best Blogger Tips
Mnigeria Dangote akanusha hisa Arsenal


Mfanyabiashara raia wa Nigeria Aliko Dangote amekanusha kwamba ana mipango ya kununua asilimia 15 ya hisa za klabu ya Ligi Kuu ya England ya Arsenal.

Awali kulikuwa na uvumi anakusudia kujiingiza katika mchakato wa hisa za Lady Nina Bracewell-Smith zenye thamani ya paundi milioni 100.

Katika taarifa yake, Dangote amethibitisha, "alihusishwa katika mazungumzo juu ya kuwekeza siku zilizopita".

Lakini akaongeza: "Kimsingi ninachoweza kusema kwa wakati huu sina nia ya kuwekeza katika klabu hiyo na sitaomba hisa."

Dangote, ambaye ni Rais na mtendaji mkuu wa kampuni ya Dangote Group, anaheshimika kuwa Mwafrika tajiri zaidi, huku gazeti la Forbes nchini Marekani likikadiria miaka miwili iliyopita alikuwa na utajiri wa dola bilioni 3.3 sawa na paundi bilioni 2.3.

Utajiri wake unatokana na himaya kubwa ya biashara aliyojijengea tangu mwaka 1977 na sasa anamiliki kampuni kubwa ya sukari nchini Nigeria, kiwanda cha saruji na cha nguo.

Hivi karibuni aliliambia gazeti moja la Nigeria amekuwa mpenzi wa Arsenal kwa muda mrefu na akaongeza: "Ilikuwa mwaka 1980 wakati nilipofanya urafiki na Bw David Dein, makamu mwenyekiti wa zamani wa bodi ya Arsenal."
Endelea kusoma habari hii..............

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits