Thursday, May 20, 2010

Best Blogger Tips
Wanaume wapendanao wafungwa Malawi


 Jaji mmoja nchini Malawi amewahukumu kifungo cha miaka 14 jela ikiambatana na kufanya kazi ngumu kwa wanaume wawili wanaofanya mapenzi ya jinsia moja kwa kosa la kufanya vitendo kinyume cha maumbile na vitendo vya aibu.

Jaji huyo amesema anataka "kuulinda" umma.

Steven Monjeza, 26, na Tiwonge Chimbalanga, 20, walikuwa gerezani tangu walipokamatwa Desemba 2009 baada ya kufanya sherehe ya uchumba.

Kukamatwa kwao kulipingwa na nchi za kimataifa na kusababisha mjadala mkubwa juu ya mapenzi ya jinsia moja nchini Malawi.
Kwa habari zaidi ingia hapa...................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits