Monday, May 17, 2010

Best Blogger Tips
Vitisho dhidi ya filamu ya Winnie

Via BBC

Utengenezaji wa filamu kuhusu maisha ya Winnie Madikizela-Mandela inayoigizwa na Jennifer Hudson inatarajiwa kuanza licha ya kuwepo vitisho vya kuchukuliwa hatua za kisheria.

Akizungumza katika tamasha la filamu la Cannes, mtengenezaji wa filamu hiyo Andre Pieterse amesema mawakili wa aliyekuwa mke wa Rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela alimwandikia barua.

Amesema barua hiyo ilikuwa na vitisho vinavyoweza kuzuia utengenezaji huo.

Filamu hiyo, iitwayo Winnie, pia inamhusisha Terrence Howard akiigiza kama Nelson Mandela.

Barua isiyo na madhara

Pieterse amesema barua hiyo pia imesema Bi Madikizela-Mandela "atapenda kuona mswada wa filamu na aidhinishe."

Lakini Pieterse amesema yeye na mkurugenzi Darrell Roodt waliamua filamu hiyo itazingatia utafiti yakinifu bila ya kuwa na ushawishi wowote kutoka wahusika wakuu.

" Ilikuwa barua dhaifu lakini pia ilikuwa na vitisho vya kushtakiwa, jambo linaloweza kuzuia filamu hiyo isitengenezwe."

Amesema: " Iwapo filamu hiyo itamkashifu kwa namna yeyote basi ataweza kuchukua hatua za kisehria."

Utengenezaji huo wa Winnie unatarajiwa kuanza tarehe 31 Mei nchini Afrika Kusini, itakayodumu kwa wiki 10.
Endelea kusoma habari hii kwa undani................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits