Thursday, May 20, 2010

Best Blogger Tips
Karume: Mseto lazima

• Ataka wananchi wajifunze kilichotokea Uingereza

na Mauwa Mohammed, Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Amani Abeid Karume, amesema Wazanzibari wanapaswa kuamka na kujifunza kutoka nje kuhusu mabadiliko ya kisiasa yanayotokea na kuhimiza umoja na mshikamano.

Alisema hakuna hata mtu mmoja aliyetarajia kwamba nchi kama Uingereza ingekubali mabadiliko ya kisiasa kama yanayotokea katika nchi za Bara la Afrika kwa kuunda serikali za umoja.

Rais Karume alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na waalikwa katika hafla ya makabidhiano ya Uwanja wa mpira wa Amani uliokuwa ukifanyiwa matengenezo na Serikali ya Watu wa China mjini Unguja.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na ujumbe wa Chama cha Wananchi (CUF) ulioongozwa na Katibu Mkuu wake, Maalim Seif Sharif Hamad, msaidizi wake, Ismail Jussa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Umma, Salum Bimani, wabunge na wawakilishi wa chama hicho.

“Amkeni ndugu zangu na nyinyi mambo yanabadilika siku hizi mnaona huko Uingereza mambo yamekuwa vingine, kwa hivyo hili si huko tu, kila pahala katika nchi zetu hizi sasa wale wenye ndoto ya kuwa huku hayafiki shauri zao,” aliwaambia waalikwa hao.

Akikumbushia Zanzibar ilipotoka, alisema ilikuwa haina utulivu kama ilivyo sasa, na kwamba hali ya sasa imetokana na maridhiano ya kisiasa yaliyofikiwa kati yake na Maalim Seif Sharif Hamad.

“Mambo mnayaona wenyewe sasa, hali imetulia, hekima na busara zimetawala jazba na ndiyo ukaona maendeleo hivi sasa yanaonekana vizuri na haya yote yamepatikana kwa sababu ya maelewano. Hakuna sababu ya kuendelea kulumbana, hili nalisema wazi kabisa na kwa nia safi, kwa sababu tunataka maendeleo na maendeleo hayaji kama hakuna umoja na mshikamano,” alisisitiza Rais Karume.
Kwa habari zaidi ingia hapa...................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits