Friday, July 23, 2010

Best Blogger Tips
Mwanamke ajifungua mayai badala ya mtoto

Via Mwananchi 

KATIKA hali isiiyokuwa ya kawaida, Mkazi wa kijiji cha Mwisole wilayani Uyui Mkoa wa Tabora, Kabula Kayungilo (20) amejifungua mayai mawili kama kuku badala ya mtoto.

Tukio hilo ambalo liliwaduwaza wakazi wengi wa Mji wa Tabora huku wengine wakitaka mayai hayo yafanyiwe uchunguzi wa kitalaamu ili kubaini kulikoni, lilitokea jana katika Hospitali ya Misheni ya Ndalla wilayani Nzega.

Mganga mkuu wa hospitali hiyo inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Dk Reuben Nyaruga, alisema tukio hilo lilitokea jana asubuhi wakati mama huyo alipofika kwa ajili ya huduma ya kujifungua mtoto.

Dk Nyaruga alimtaja mkazi huyo kuwa ni Kabula kayungilo (20) ambaye ni mkazi wa kijiji cha Mwisole wilayani Uyui.

Alieleza kuwa msichana huyo alipokewa hospitalini hapo jana asubuhi akidai ni mjamzito anayejisikia uchungu wa kujifungua.
Endelea kusoma habari hii.................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits