Tuesday, February 15, 2011

Best Blogger Tips
Kaka wa Princess Diana atangaza ndoa


Ndoa ya Prince William siyo pekee ambayo inafanyika mwaka huu katika familia yake,  Mjomba wake William anayeitwa Charles Spencer ametangaza  kufunga ndoa na mchumba wake Karen Gordon.

 “Charles Spencer, anayofuraha kubwa kutangaza uchumba wake na Karen Gordon, ambaye ni mzaliwa wa  Canada na pia ni Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Shirika la kimataifa la kuhudumia watoto”, ilisema taarifa hiyo.

Harusi hiyo ambayo itakuwa ni ya kifamilia na marafiki wa jirani, itafanyika tarehe 18 mwezi wa sita mwaka huu kwenye mji wa Althop nchini uingereza, kwenye makazi ya familia ya Spencer.

Spencer, ambaye ni kaka wa marehemu Princess Diana, anakumbukwa kwa maneno aliyozungumza katika mazishi ya Dada yake mwaka 1997, kuhusu familia ya kifalme kutomjali marehemu dada yake.

Hii itakuwa ni ndoa ya tatu kwa Spencer. Ana watoto wanne kutoka kwenye ndoa yake ya kwanza, na watoto wawili kutoka kwenye ndoa yake ya pili.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits