Saturday, May 21, 2011

Best Blogger Tips
Mamia wamzika Sheikh Yahya


Via Tanzania Daima

MAELFU ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, wakiongozwa na viongozi wa serikali, dini, vyama vya siasa na makundi ya jamii jana walijitokeza kwenye mazishi ya mnajimu mashuhuri nchini na Afrika Mashariki ya Kati, Sheikh Yahya Hussein aliyefariki dunia juzi.
Sheikh Yahya Hussein (87), aliyefariki dunia juzi majira ya saa nne asubuhi, muda mfupi baada ya kufikishwa katika Hospitali ya Mtakatifu Ukombozi, Kinondoni baada ya kuugua ghafla alizikwa katika makaburi ya Tambaza.
Rais Jakaya Kikwete, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, Mufti, Sheikh Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Shaaban bin Simba, Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), la Ubungo Kibangu, Anthony Lusekelo, ni miongoni mwa viongozi waliokuwapo kwenye mazishi hayo yaliyowafanya wakazi wa jiji hilo kuacha shughuli zao kwa muda ili kushiriki.

Baadhi ya viongozi waliokuwapo nyumbani kwa marehemu Sheikh Yahya, Mwembe Chai eneo la Magomeni, walisema kuwa kifo chake ni pigo kubwa kwa Watanzania na hasa Jumuiya ya Waislamu kwa kuwa alikuwa mstari wa mbele kupigania haki za Waislamu.

Mchungaji Lusekelo, alisema kuwa kifo cha Sheikh Yahya ni pigo kubwa kwa Waislamu na hata watu wa dini nyingine kutokana na kuwa msuluhishi mkubwa ilipotokea kuna kutokuelewana kwa viongozi wa dini hizo au makundi mengine ya kijamii.

“Siku tatu nyuma niliota Sheikh Yahya amepandishwa daraja kubwa la uongozi… lakini siku iliyofuata nikasikia taarifa za kifo chake, nilimheshimu na kumpenda kutokana na hekima na busara zake wakati wa uhai wake na hata ulikuwa ukija kwa ajili ya kuomba ushauri hakusita kufanya hivyo kwa wakati.

“Yapo aliyoyafanya na kuwa mchango mkubwa wa nchi yetu, lakini kutokana na aliyoyafanya Mungu amuweke mahali panapostahili, tupo pamoja katika kuomboleza msiba wa Sheikh Yahya na subira ni jambo jema kwa wafiwa,” alisema
Endelea kusoma habari hii..................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits