Tuesday, May 24, 2011

Best Blogger Tips
Tiba ya Babu Samunge: Mwingine adai kupona ukimwi

Via Mwananchi

MKAZI wa Kijiji cha Galapo, Babati, mkoani Manyara, Abdalah Ally (38), aliyekuwa mgonjwa wa Ukimwi, amedai kupona ugonjwa huo na kinga zake za mwili (CD4) kuongezeka baada ya kunywa dawa ya Mchungaji, Ambilikile Mwasapila.Ally anakuwa mtu wa pili kujitangaza kupona Ukimwi baada ya kunywa kikombe cha dawa hiyo, baada ya Wilia John Lengume wa Samunge aliyekuwa wa kwanza kutangaza kupona ugonjwa huo baada ya kupata dawa hiyo.

Akizungumza jana kijijini hapa, Ally alisema kwamba amekuwa akitumia Dawa za Kupunguza Makali ya Ukimwi (ARV), tangu mwaka 2009 kabla ya kupata kikombe cha Babu, Januari 5, mwaka huu.

Akiwa na vyeti vya vilivyoonyesha kwamba alikuwa na maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU), Ally alisema kuwa Aprili 22, 2009 alipimwa na kukutwa na maambukizi hayo wakati huo akiwa mfungwa katika Gereza la Babati.

Alisema alipima afya yake Februari 25, mwaka huu wilayani Babati na katikia Kituo cha Msalaba Mwekundu na kukutwa hana tena VVU. Alipima tena katika Hospitali ya Wilaya ya Babati ambako pia alikutwa kinga yake ya mwili ni ya kutosha na hana tena VVU ndipo alipoamua kuacha kutumia ARV.

Alidai kwamba hata baadhi ya maofisa wa afya waliokuwa wakisimamia matibabu yake wilayani Babati walishangazwa na kupona kwake kwa tiba ya Mchungaji Mwasapila na hilo liliwafanya nao kufunga safari kuja Samunge Aprili 28, mwaka huu kupata kikombe.

"Ninavyo vyeti vinavyothibitisha kuwa sina tena Ukimwi na mwezi huu pia natarajia kupima kuona afya yangu ipo vipi," alisema Ally.
Endelea kusoma habari hii.....................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits