Wednesday, May 25, 2011

Best Blogger Tips
Aliyekuwa mume wa mfanyakazi wa ndani aongea

Aliyekuwa mume wa  mwanamke ambaye ametangazwa na vyombo vya habari kwamba ni mama wa mtoto wa Arnold Schwarzenegger  aliyezaa nje ya ndoa, anasema kwamba anahisi kuzungukwa  na  aliyekuwa Gavana wa Califonia.

Katika mahojiano na jarida la Entertainment Tonight, Rogelio Baena anasema kwamba juma lililopita ndipo alipofahamu kwamba yeye siye baba mzazi wa mtoto huyo. Amesisitiza kwamba ataendelea kumtambua mtoto huyo kama ni wa kwake na si vinginevyo.

Jarida la “The Insider” siku ya jumanne lilionyesha video ya aliyekuwa mke wa Schwarzenegger, Maria Shriver akimsifia mwanamke huyo Mildred Baena katika sherehe ya mmoja wa jamaa zake, kwamba ni mwanamke jasiri na mfanyakazi hodari, huku Schwarzenegger akisikika kusema kwamba mfanyakazi huyo wa nyumbani amefanya kazi “nzuri sana”.

Mildred Baena, ametambuliwa kwamba ni mama mzazi wa mtoto wa Schwarzenegger na jarida la New York Times na  vyombo vingine vya habari.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits