Tuesday, May 24, 2011

Best Blogger Tips
Mfugale bosi mpya TANROADS

WAZIRI wa Ujenzi John Magufuli amemteua, Patrick Mfugale, kuwa mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Ephraim Mrema.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyopatikana Dar es Salaam jana kisha kutiwa saini na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Herbert Mrango, kabla ya uteuzi huo Mfugale alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa uteuzi huo ni kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia Mei 20 mwaka huu. Mfugale amewahi kushika nafasi mbalimbali serikalini ikiwemo kusimamia ujenzi wa barabara na daraja la Mkapa.

Katika taarifa yake, katibu mkuu alieleza kuwa injinia huyo ana shahada ya uhandisi (BSc Civil Engeneering) kutoka Chuo Kikuu cha Roorkee nchini India na shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Loughborough, Uingereza.

Kabla ya uteuzi wake, alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Barabara nafasi aliyoenguliwa na Rais, siku chache kabla ya kuingia TANROADS. Desemba Mosi mwaka jana, Mfugale aliteuliwa kukaimu nafasi ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa TANROADS.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits