Sunday, June 5, 2011

Best Blogger Tips
Binti mbaroni kwa 'kubaka kavulana'

Via Majira

MSICHANA mwenye umri wa miaka 16 (jina linahifadhiwa), mkazi wa Kigogo, Luhanga, Dar es Salaam anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za 'kumbaka' mtoto wa
kiume mwenye umri wa miaka mitatu.

Msichana huyo anadaiwa kumbaka mtoto huyo mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo alimuiba nyumbani kwao na kumpeleka kwenye pagale, nyuma ya Shule ya Msingi Kawawa.

Mama mzazi wa mtoto aliyefanyiwa unyama huo, ambaye hakutaka kutajwa jina lake alisema, wakati akifanya usafi ndani ya nyumba yake siku ya tukio saa 4 asubuhi, mtoto wake alikuwa nje akicheza na wenzake.

Alisema alipomaliza ndani alitoka nje kumchukua mwanaye huyo ili ampe kifungua kinywa, lakini hakumwona ndipo, akaanza kumtafuta zaidi ya saa nzima bila mafanikio.

Mama huyo alisema, baada ya kuhangaika kumtafuta mwanaye, akili ilimtuma kuchungulia ndani ya nyumba hiyo inayojengwa na alipofanya hivyo alikuta mwanaye amelaliwa na msichana huyo.

Alisema kuona hivyo alikwenda mbio kuita mama mwingine jirani yake ili ashuhudie kitendo anachofanyiwa mwanaye.

"Nikiwa na jirani yangu tulishuhudia msichana huyo akifanya kitendo hicho kwa mtoto wangu," alisema.

Baada ya kushuhudia yote hayo, walipiga kelele na kumkamata akiwa uchi na kumpeleka Kituo Kidogo cha Polisi Kigogo- Luhanga.

Msichana huyo alishikiliwa kwa muda katika kituo hicho kidogo cha polisi kisha akahamishiwa Kituo cha Urafiki kwa hatua zaidi za kisheria ambapo mtoto aliyebakwa akilipelekwa katika Hospitali ya Amana kupatiwa matibabu.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits