Thursday, June 30, 2011

Slaa afufua upya ufisadi

Best Blogger Tips
Via Raia Mwema

WAKATI wafadhili wakikabidhiwa ripoti inayoonyesha bado Tanzania kuna ufisadi, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, ameibuka na kusema hatorudi nyuma katika mapambano dhidi ya rushwa kutokana na serikali kuwaogopa wala rushwa na mafisadi wakubwa.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na Raia Mwema, jana, Jumanne, Dk. Slaa amesema wakati wote ambao yeye na wenzake katika Upinzani wakipigania hatua kuchukuliwa dhidi ya mafisadi na wala rushwa wakubwa, serikali imekuwa na kigugumizi katika kuchukua hatua; huku ikitumia mbinu za kuwafunga midomo.

Akitoa mfano wa kesi mbalimbali zikiwamo za wizi katika akaunti ya madeni ya nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (EPA) kupitia kampuni ya Kagoda Agricultural Limited na kashfa ya rushwa katika ununuzi wa rada ya kijeshi, Dk. Slaa amesema serikali inawalinda wahusika wakuu.

 “Kampuni kama Kagoda wahusika wanajulikana lakini hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi ya wahusika. Hii si dalili nzuri maana inaashiria kwamba wakubwa wanahusika ama wanawaogopa wahusika. Hatudanganyiki na hatunyamazishwi, tutaendelea kusema na kutaka hatua zichukuliwe,” anasema na kuendelea;

“Kashfa ya rada ni aibu kusikia serikali inadai fedha za rada wakati ilikuwa na kigugumizi wakati Uingereza wakichunguza wahusika wa rada na walishindwa kutoa ushirikiano kwa wachunguzi, lakini sasa eti wanasikia kuna fedha ndio wanazitaka. Kwa nini walikataa kushughulikia wahusika kwa sheria zetu za Tanzania na kuachia Waingereza kila kitu?” alihoji Dk. Slaa.
Endelea kusoma habari hii....................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits