Saturday, June 11, 2011

Best Blogger Tips
Marekani yathibitisha kifo cha Fazul

Via BBC

Waziri wa mashauri ya nje wa Marekani Bi Hillary Clinton, amesema kifo cha Fazul Abdullah Mohammed, aliyeshukiwa kuwa mkuu wa Al Qaeda Afrika Mashariki, "ni pigo kubwa" kwa kundi hilo na washirika wake.

Jumamosi serikali ya Marekani imethibitisha kifo cha Fazul Abdullah Mohammed, katika tukio la kufyatuliana risasi na vikosi vya Somalia mjini Mogadishu.

"Kifo cha Harun Fazul ni pigo kubwa kwa Al Qaeda, washirika wake wa siasa kali, na shughuli zake Afrika Mashariki," Clinton aliwaeleza waandishi wa habari akiwa mjini Dar es Salaam, Tanzania.

"Ni mwisho unaostahili kwa gaidi aliyewaletea wengi kifo na huzuni watu wasiokuwa na hatia Nairobi, Dar es Salaam na kwingineko; Watanzania, Wakenya, Wasomali na wafanyakazi wetu wa ubalozi".

Awali afisa mmoja wa cheo cha juu katika serikali ya Marekani alithibitisha kifo cha kiongozi huyo wa Al Qaeda Afrika Mashariki, na kuipongeza serikali ya muda nchini Somalia.

Kiongozi huyo wa Al Qaeda katika kanda ya Afrika ya Mashariki Fazul Abdullah Mohammed, alishukiwa kuhusika na shambulio dhidi ya balozi za Marekani katika Kenya na Tanzania mnamo mwaka 1998.

Fazul Abdullah amekuwa mtu anayetafutwa sana barani Afrika baada ya zaidi ya watu 220 kuuawa na zaidi ya 5000 kujeruhiwa katika mashambuliio ya mwaka 1998.

FBI iliahidi dola milioni 5 kwa kichwa chake.
Endelea kusoma habari hii......................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits