Thursday, June 30, 2011

Aibiwa gari baada ya kuleweshwa

Best Blogger Tips
Via habariLeo

DEREVA teksi Minaji Omary (39), ameibiwa gari baada ya abiria aliyempakia
kumnywesha soda inayodhaniwa kuwa na dawa za kulevya.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Adolfina Chialo alisema, tukio hilo limetokea jana saa 6 usiku kwenye baa ya Uhuru, mjini Morogoro.

Gari iliyoibwa ni yenye namba za usajili T321 BCU aina ya Toyota Corola ambayo dereva wake, baada ya kunywa soda hiyo alipoteza fahamu.

Kamanda Chialo alisema, alfajiri dereva huyo alipoamka hakuiona gari wala
abiria huyo na ndipo alipofika katika Kituo Kikuu cha Polisi na kutoa taarifa hizo. Polisi wanaendelea na uchunguzi.

Katika hatua nyingine, Kamanda Chialo alisema, mkazi wa Kihonda, Amina Maulid amefariki dunia baada ya kunywa vidonge ambavyo havifahamiki. Chanzo cha kujiua hakijajulikana.

Mtoto wa mwanamke huyo ambaye polisi haikutaja jina lake, ndiye aliyetoa taarifa Polisi kuwa mama yake alifariki dunia Juni 28 mwaka huu saa 5:30 usiku eneo la Kihonda, mjini Morogoro.

Alisema, baada ya polisi kufika nyumbani kwao, walikuta dawa za aina mbalimbali kwenye meza ndani ya chumba alichokuwa amelala mwanamke huyo.

Polisi inaendelea na uchunguzi wakati mwili ukiwa umehifadhiwa katika hospitali ya mkoa.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits