Friday, June 3, 2011

Best Blogger Tips
Mjane wa Sisulu A Kusini afariki dunia

Afrika Kusini inaomboleza kifo cha mmoja wa watu walioongoza harakati za kupambana na ubaguzi wa rangi, Albertina Sisulu, aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 92.

Bi Sisulu alikuwa mjane wa Walter Sisulu, rafiki na mshauri wa aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela.

Mwanasiasa mashuhuri wa aina yake, alikuwa mpambanaji katika shirikisho la wanawake wa African National Congress (ANC).

Msemaji wa ANC Brian Sokutu alisema Bi Sisulu alikuwa wakati wote wa maisha yake akiwa katika harakati za kuleta demokrasia nchini Afrika Kusini.

Gazeti la Afrika Kusini la South Africa Times limemnukuu akisema, " Komredi Sisulu ametumia muda wake wote kuitumikia ANC na kuikomboa Afrika Kusini. Tunatoa heshima zetu kwa kiongozi huyu na mama wa harakati hizi."
Endelea kusoma habari hii...................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits