Sunday, June 19, 2011

Best Blogger Tips
Familia ya Kawawa yagombea nyumba

FAMILIA ya aliyekuwa Waziri Mkuu mstaafu hayati Rashidi Kawawa, imesema itapigania kulinda heshima ya mwanasiasa huyo baada ya kuwapo tishio la nyumba yao iliyopo Kilimani mjini Dodoma inauzwa na kupangishwa na mama yao wa kambo.

Mama huyo, Asina Kawawa, anadai kuwa nyumba hiyo ni mali yake.

Kwa mujibu wa familia hiyo, nyumba hiyo inataka kupangishwa na mama huyo anayedai kwamba alirithishwa na Kawawa, licha ya familia kueleza kutotambua hilo, lakini pia ni makumbusho na moja ya maeneo ya kihistoria ya mwanasiasa huyo aliyepigania Uhuru wa Tanganyika.

Ingawa mama huyo anadaiwa kuwa mbioni kupangisha nyumba hiyo iliyopo kiwanja namba 34 eneo la Uzunguni mjini hapa, lakini ipo hatarini kuuzwa na benki ya CRDB baada ya kutumika kama dhamana ya mkopo wa Sh milioni 350 kwa ajili ya kujenga nyumba nyingine pembeni mwa hiyo, mali ya Asina.

Mmoja wa wanafamilia ya Kawawa, Zainab Kawawa ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), aliwaeleza waandishi wa habari akiwa katika nyumba hiyo, kwamba familia inataka kulinda na kutunza heshima ya Mzee Kawawa, kwa sababu hakuwa mtu wa kukopakopa ovyo.
“Tunataka kulinda heshima ya Mzee Kawawa, tumemweleza mama kuwa tuko tayari kulipa deni hilo, lakini hayuko tayari, kwa sababu anaamini tukilipa deni nyumba hii itakuwa yetu, lakini zaidi ni kwamba tayari kuna notisi ya CRDB ya kuuza nyumba kutokana na deni,” alisema Zainab.
Alisema licha ya kuomba mkopo wa Sh milioni 350, ambao ulikuwa ukitolewa kwa awamu, mama huyo alipewa Sh milioni 74 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa nyumba hiyo ya ghorofa moja nyuma ya nyumba ya Mzee Kawawa, lakini sasa deni hilo limefikia Sh milioni 102.

“Kama familia, tulikaa na kuzungumzia deni hili na kukubaliana kuwa linatuhusu, hivyo baadaye lilisimamishwa na sasa limefikia Sh milioni 102, na tayari CRDB wanataka kuja kuuza nyumba hii kwa sababu ya deni,” alisema Zainab ambaye alizungumza na wanahabari baada ya mkutano kati yake na mama yake na mwanasheria Ngonyani kutoka makao makuu ya CCM.

Alisema kwa mujibu wa maelezo ya mama yao, nyumba hiyo aliyokuwa akiishi Mzee Kawawa kwa muda mrefu, aliinunua kwa ubia mwaka 2007 kutoka serikalini na inadaiwa kuwa ilikuwa na kipengele cha kuwa mmojawapo akifariki dunia, basi anayebaki atairithi. 
Endelea kusoma habari hii.....................

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits