Wednesday, June 22, 2011

Best Blogger Tips
Pinda aacha kutumia Mercedes Benz

Via HabariLeo

KATIKA kile kinachotafsiriwa kuwa ni kuwatega mawaziri na viongozi wa Serikali wanaotumia magari ya kifahari na yenye gharama kubwa, Waziri Mkuu,Mizengo Pinda ameanza kuachana na matumizi ya magari yenye gharama kubwa.

Hatua hiyo inadaiwa kuwa inalenga kuwafanya mawaziri na viongozi wengine wa juu
wa Serikali, kupima, kutafakari na kuchukua hatua juu ya matumizi ya magari
ya gharama kubwa wanayotumia sasa ambayo yamekuwa yakipigiwa kelele na
baadhi ya wabunge na wananchi.

Uchunguzi wa gazeti hili ambao ulithibitishwa pia jana jioni na Katibu Mkuu wa
Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhan Khijjah, ulibaini kuwa Waziri Mkuu,
ameacha kutumia magari ya kifahari aina ya Mercedes Benz na Toyota
Land Cruiser VX na kuanza kutumia Toyota Land Cruiser GX.

Katika mahojiano maalumu na HABARILEO, Khijjah amethibitisha Pinda kuanza
kutumia aina hiyo ya magari katika misafara yake ambayo alisema ni ya gharama ya
chini ikilinganishwa na Benz na VX ambayo gharama yao ni kubwa sana.

“Ni kweli Mheshimiwa Pinda sasa ameamua kutumia magari haya ya GX, hajatangaza
popote juu ya uamuzi wake huu, lakini nahisi ni kama ujumbe kwa viongozi wengine
wa juu wa Serikali wanaotumia magari ya gharama kubwa ili kuwafanya nao wapime
na kuchukua hatua,” amesema Khijjah.

Katibu Mkuu huyo wa Hazina, alisema ipo mikakati kabambe iliyowekwa na Serikali
ili kudhibiti matumizi holela ya fedha za umma, lakini akasema si kila kitu lazima kisemwe bungeni, kwani mambo mengine yanahitaji utekelezaji wa moja kwa
moja.

“Mfano hatua hii ya magari ya msafara wa Waziri Mkuu kuwa ya gharama ya chini
unaonesha dhamira ya dhati ya kuanza kuokoa fedha za umma kwa matumizi yasiyo na sababu. Kama Waziri Mkuu anatumia gari kama hili kuna haja gani kwa kiongozi wa
chini kuagiza gari la thamani zaidi, haiwezekani,” alisema Khijjah.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits