Friday, June 10, 2011

Best Blogger Tips
Tetemeko latikisa Dar

Via Majira

WAKAZI wa jiji la Dar es Salaam jana walikumbwa na taharuki baada ya kutokea kwa tetemeko la ardhi lililodumu kwa sekunde kadhaa.

Tetemeko hilo lililotokea majira ya saa 5:28 asubuhi ambapo kwa mujibu wa wataalamu wa hali ya hewa lilitokea kilometa 52 kusini mashariki mwa jiji hilo.

Baadhi ya watu waliokuwa kwenye majengo marefu waliamua kuzikimbia ofisi zao kwa lengo la kujiokoa licha ya tetemeko hilo kutoleta uharibifu wa mali.

Vikundi vya wananchi vilionekana kujazana katikati ya mitaa mbalimbali nje ya majengo vikijadili tukio hilo.

Abdul Juma, mfanyabiashara aliyepanga katika jengo la PPF, alisema waliamua kutoka katika ofisi hizo kwa hofu kuwa huenda tetemeko hilo lingetokea tena.

“Ndugu yangu maisha ni matamu, mimi sijui nimeshukaje kutoka ghorofa ya tano, nilijawa na hofu baada ya kusikia tetemeko hilo.

Katika jengo la PPF House, askari polisi walionekana kurandaranda huku na huku kwa lengo la kuhakikisha kuna usalama wa raia na mali zao.

Taarifa za mtandao wa Geolojia zilisema kuwa tukio hilo lilikuwa na nguvu ya 4.8 upana kilometa 10.

“Tetemeko hilo limeonekana katika latitudo kusini mwa mstari wa greenwhich limekuwa kwa 7 na mashariki ni longitudo 39,” ilifafanua.

Taarifa hiyo iliyataja maeneo ambayo tetemeko hilo lilipita kuwa ni Zanzibar, Tanga na Nairobi nchini Kenya.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits