Wednesday, August 8, 2012

NTC yatoa madaraka kwa Congress, Libya

Best Blogger Tips
 Serikali ya mpito nchini Libya imekabidhi madaraka ya kulitawala taifa hilo kwa baraza la Congress lililobuniwa baada ya uchaguzi mkuu wa mwezi uliopita , ikiwa ni hatua muhimu katika kipindi cha mpito katika siasa za taifa hilo.

Mziki wa wa bendi ya jeshi ulichezwa kuwakaribisha wanasiasa na maafisa wa ngazi ya juu katika jeshi waliokuwa wakiwasili tayari kwa sherehe hizo.

Kisha serikali ya mpito nchini Libya ikakabidhi madaraka kwa baraza la Congress ambalo lilibuniwa baada ya uchaguzi wa hivi maajuzi.

Hafla yenyewe ikajawa na taswira ya mwamko mpya katika mji mkuu wa Tripoli.
Hafla hii inaashiria hatua za mpito katika siasa za Libya kutoka utawala wa ki-imla hadi utawala wa kidemokrasia wenye viongozi waliochaguliwa.

Hii haingetokea kama Kanali Muamar Gaddafi angekuwa bado madarakani, wengi wanaamini.
Serikali ya mpito inayovunjwa iliwajumuisha wanamgambo wa upinzani waliomng'oa madarakani na kisha kumuua kanali muamar Gadaffi mwaka mmoja uliopita.

Mustafa Abdel Jalil mwenye kiti wa baraza la kitaifa lililoendesha serikali hiyo ya mpito akihutubu wakati wa sherehe hizo za kukabidhi madaraka, amesema baraza la Congress ndilo pekee lenye haki ya kikatiba kuwaakilisha raia wa Libya.

Waandishi wanasema ingawa kuna utulivu katika mji mkuu, Tripoli, mapigano yanaendelea katika maeneo mengi ya Libya.

Baadhi ya makundi ya wanamgambo yangali yanashikilia madaraka makubwa.
Chanzo: BBC

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits