Monday, April 25, 2011

Best Blogger Tips
Asakwa na polisi kwa kumlawiti mwanafunzi

Via Majira

POLISI jijini Mwanza wanamsaka mwanamume mmoja akidaiwa kumwingilia kinyume cha maumbile mwanafunzi wa kike wa Shule ya Msingi Mahina katika Wilaya ya
Nyamagana Jijini Mwanza.

Tukio hilo lilitokea Aprili 20 mwaka huu majira ya saa 12:00 katika eneo la Gedeli Mahina ambapo mtu huyo alimwingilia mwanafunzi huyo na kumsababishia maumivu makali sehemu hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Bw. Nonosius Komba alisema mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 11 alilawitiwa na mtu mmoja asiyemfahamu jina bali anamtambua kwa sura ambaye ni wa kabila la Kimasai.

Alisema mara baada ya kufanya kitendo hicho, mtuhumiwa huyo alitokomea kusikojulikana ambapo jeshi la polisi linaendelea kumsaka ikiwa ni pamoja na kufanya uchunguzi wa tukio hilo.

No comments:


Copyright 2011 Mambo ya Leo Blog. All Rights Reserved.
 

yasmin lawsuits